A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Tuesday, April 23, 2019

Udhamini wa NBC wang’arisha shindano la Shika Ndinga jijini Dodoma

Meneja wa Benki ya NBC Kanda ya Kati, James Ndimbo, akikabidhi zawadi ya pikipiki kwa mkazi wa Dodoma, Twaha Saleh aliyojishindia katika kampeni ya Shika Ndinga inayodhaminiwa na benki hiyo na kuandaliwa na kituo cha redio cha EFM. hafla hiyo ilifanyika jijini Dodoma hivi karibuni. 
Washiriki wa Shindano a Shika Ndinga Upande wanaume wakichuana ili kumpata mshindi wa shindano hil lililodhaminiwa na Benki ya NBC na kufanyika mjini Dodoma hivi karibuni. Twaha Saleh alishinda na kuzawadiwa zawadi ya pikipiki.
Washiriki wa Shindano a Shika Ndinga Upande wanawake wakichuana ili kumpata mshindi wa shindano hil lililodhaminiwa na Benki ya NBC na kufanyika mjini Dodoma hivi karibuni. Sarah Ntenga  alishinda na kuzawadiwa zawadi ya pikipiki.
Baadhi ya wakazi wa Dodoma waliohudhuria katika shindano la Shika Ndinga wakimsiliza mfanyakazi wa NBC kitengo cha mauzo akiwaeleza kuhusu huduma za kibenki zitolewazo na benki hiyo na jinsi wanavyoweza kufungua akaunti ya Fasta ya NBC kwa gharama za kuanzia shs 5000 na kupewa kadi ya ATM aina ya Visa papo hapo.
Meneja wa Benki ya NBC Kanda ya Kati, James Ndimbo, akikabidhi zawadi ya pikipiki kwa mkazi wa Dodoma, Sarah Ntenga aliyojishindia katika kampeni ya Shika Ndinga inayodhaminiwa na benki hiyo. hafla hiyo ikifanyika jijini Dodoma hivi karibuni.
Meneja wa Benki ya NBC Kanda ya Kati, James Ndimbo, akiungumza na umati wa watu uliojitokeza katika shindano la Shika Ndinga linalodhaminiwa na benki hiyo mjini Dodoma hivi karibuni.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive