A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Thursday, June 30, 2022

VODACOM TANZANIA YAKABIDHI VIFAA KWA SHULE YA WASICHANA

 


Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa kampuni ya Vodacom Tanzania Plc, Vivienne Penessis(wan ne kushoto) akikabidhi baadhi ya vitabu kwa Mkuu wa shule ya sekondari ya watoto yatima ya Bethsaida iliyoko Mpiji Magoe jijini Dar es Salaam, Hollness Moshi (kushoto) ikiwa ni sehemu ya msaada uliotolewa na wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom kwa shule hiyo, wafanyakazi hao wametoa viti 100, meza 100, vifaa vya kuzalisha umeme jua (solar power) 20 na vitabu 388. Kulia ni Mkurugenzi wa Udhibiti wa Hatari na Utii wa sheria, Agapinus Tax na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo.


Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa kampuni ya Vodacom Tanzania Plc, Vivienne Penessis akizungumza wakati wa Hafla ya kukabidhi misaada ya vifaa mbalimbali vya Elimu katika shule ya sekondari ya watoto yatima ya Bethsaida iliyoko Mpiji Magoe jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya msaada uliotolewa na wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom kwa shule hiyo, wafanyakazi hao wametoa viti 100, meza 100, vifaa vya kuzalisha umeme jua (solar power) 20 na vitabu 388.


Mkurugenzi wa Udhibiti wa Hatari na Utii wa sheria wa kampuni yaVodacom Agapinus Tax akizungumza wakati wa Hafla ya kukabidhi misaada ya vifaa mbalimbali vya Elimu katika shule ya sekondari ya watoto yatima ya Bethsaida iliyoko Mpiji Magoe jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya msaada uliotolewa na wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom kwa shule hiyo, wafanyakazi hao wametoa viti 100, meza 100, vifaa vya kuzalisha umeme jua (solar power) 20 na vitabu 388.


Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Vodacom Tanzania Plc, Vivienne Penessis(wa tano kushoto), akikata utepe wakati wa Hafla yakukabidhi misaada ya vifaa mbalimbali vya Elimu katika Shule ya sekondari ya watoto yatima ya Bethsaida iliyoko Mpiji Magoe jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya msaada uliotolewa na wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom kwa shule hiyo, wafanyakazi hao wametoa viti 100, meza 100, vifaa vya kuzalisha umeme jua (solar power) 20 na vitabu 388. Wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Udhibiti wa Hatari na Utii wa sheria wa kampuni yaVodacom Agapinus Tax, uongozi wa shule pamoja na maofisa wengine wa Vodacom.


Mkurugenzi wa Udhibiti wa Hatari na Utii wa sheria wa kampuni yaVodacom Agapinus Tax akisalimiana na Mkuu wa shule ya sekondari ya watoto yatima ya Bethsaida iliyoko Mpiji Magoe jijini Dar es Salaam, Hollness Moshi wakati walipo kwenda kutoa msaada katika shule hiyo.


Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wakitoa burudani ya ngoma za asili wakati wa kampuni ya Vodacom walipokwenda shuleni hapo kwa ajili ya kutoa misaada ya vifaa mbalimbali


Mkurugenzi wa Udhibiti wa Hatari na Utii wa sheria wa kampuni yaVodacom Agapinus Tax akikabidhi baadhi ya vitabu kwa wanafunzi shule ya sekondari ya watoto yatima ya Bethsaida iliyoko Mpiji Magoe jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya msaada uliotolewa na wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom kwa shule hiyo, wafanyakazi hao wametoa viti 100, meza 100, vifaa vya kuzalisha umeme jua (solar power) 20 na vitabu 388.


Vodacom Tanzania Yakabidhi Vifaa kwa Shule ya WasichanaVodacom Tanzania Foundation leo imekabidhi vifaa na samani kwa Shule ya Wasichana ya Bethsaida mjini Dar es Salaam ambavyo kampuni ilishinda katika mashindano ya makampuni ya Vodacom duniani.


Akiongea wakati wa makabidhiano, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Vodacom Tanzania, Vivienne Penessis alisema, “Elimu ni msingi pekee ambao unampatia mtu kianzio cha kujenga miasha bora.


Hii ni kweli zaidi kwa Watoto yatima ambao tegemeo lao ni elimu pekee.”Shule ya Wasichana ya Bethsaida ilichaguliwa kupokea msaada huu kwa kuwa ni moja ya shule chache zinazotoa elimu ya sekondari kwa Watoto yatima wa kike nchini.


Mkurugenzi wa Vodacom pamoja na wafanyakazi wengine wa kampuni waliikabidhi shule hiyo viti 100, vitabu Zaidi ya 300 pamoja na vifaa 20 vya kuzalisha umeme wa jua. Bi penessis alielezea Imani yake kuwa msaada huo utatumika ipasavyo kwani kampuni ya Vodacom ilijiridhisha juu ya utaalam na moyo wa kujitoa wa wafanyakazi wa shule ya Bethsaida.


Msaada huu unaendana na malengo ya Vodacom Tanzania kuongeza ujumuishwaji katika elimu. Hivi karibuni, kampuni ya Vodacom ilizindua mpango wa kupanua wigo wa mfumo wa E-Fahamu kufikia nchi nzima. E-Fahamu ni huduma inayotoa mawaidha ya elimu yenye viwango vya kimataifa na vyenye kukidhi miongozo ya serikali juu ya elimu.


Kuhusu Vodacom Tanzania FoundationThe Vodacom Tanzania Foundation ni sehemu ya kampuni ya Vodacom Tanzania PLC yenye mamlaka ya kutoa huduma za kijamii zikiwa zinawalenga zaidi wanwake na vijana. Foundation inajumuisha utoaji wa hisani na kutumia uwezo utakanao na teknolojia kuleta suluhisho kwa mahitaji ya kijamii.Ikishirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali, Vodacom Tanzania Foundationimesaidia zaidi ya miradi 120 hadi sasa ikiwa imewekeza zaidi ya Shilingi bilioni 15 kuboresha Maisha ya watanzania.Kwa maelezo zaidi, tafadhali tembelea: https://vodacom.co.tz/en/vodacom_foundation_aboutus/?SID=1u5nsmti8ahqks35k9tds71652
Share:

Wednesday, June 29, 2022

MAAJABU YA BIDHAA ZA LG SMART HOME , UOKOA NISHATI NA MUDA

 Na Mwandishi Wetu

• Faida kuu za vifaa Vya Nyumbani vya LG ni pamoja na kutoa urahisi na uharaka wa kutumia vifaa kama TV na friji, utendakazi ulioboreshwa kupitia teknolojia ya Upelelezi wa Artificial Intelligence (AI) kwa washer na kuokoa nishati kwa viyoyozi.

• Teknolojia mpya iliyobuniwa na Kampuni ya LG inayosifiwa kwa kusaidia kuhifadhi nishati na maji, kuwa rafiki wa mazingira huku ikitumika kwa urahisi, hivyo basi kukuza malengo muhimu ya maendeleo endelevu.

DAR ES SALAAM, TANZANIA, 29 JUNI 2022… Watanzania sasa wanaweza kuishi maisha rahisi, ya vitendo na rahisi zaidi wakiwa na Bidhaa za LG zilizoletwa hivi Karibuni, vifaa mahiri vya nyumbani vinavyolenga kukidhi mahitaji mengi, na kazi za kila siku zenye changamoto.

Bidhaa kama Majokofu, Microwave, televisheni na mashine za kufulia nguo, vifaa mahiri vya nyumbani vitakavyoweka muonekano wa kidijitali nyumba za Watanzania , kwa maana kwamba vifaa hivi kutoka kampuni ya LG havitoi kelele za aina yeyote wakati wa matumizi na kuifanya nyumba kuwa shwari na tulivu huku shughuli nyingine zikiendelea.

Akizungumzia ubunifu wa bidhaa bora za nyumbani za hivi karibuni, Mkurugenzi Mtendaji wa LG Electronics Afrika Mashariki, Sa Nyoung Kim alisema, "hatua ya kuweka vyumba vya kuishi, jikoni na vyumba vingine vyovyote katika nyumba za Watanzania kuwa za kidijitali imechochewa na dhamira yetu ya kuweka vipaumbele kwa urahisi na faraja kwa ajili ya wateja wetu. Ili sisi sote kufikia hili, lazima kuwe na usambazaji wa kutosha wa vifaa vya nyumbani ”.

Kulingana na uchunguzi wa hivi majuzi wa LG ThinQ Smart Home Report, 17.3% ya watumiaji waliohojiwa walichagua uokoaji wa nishati kama manufaa makubwa zaidi ya nyumbani. Faida nyingine kuu zilizotajwa katika utafiti huo ni pamoja na urahisi na usalama wa kutumia kwa TV na friji na utendakazi bora kupitia teknolojia ya Artificial Intelligence (AI) kwa washer na kuokoa nishati kwa viyoyozi.

Miongoni mwa vifaa muhimu vya nyumbani vilivyoletwa na LG nchini ni pamoja na Televisheni za Smart OLED zinazoendeshwa na teknolojia ya hali ya juu ya akili ya bandia ambayo hufanya nyumba kuwa nzuri na rahisi. Televisheni zimeunda vichakataji vya AI ambavyo huchanganua yaliyomo kwenye skrini ili kuyarekebisha kwa sauti, picha na video bora zaidi kulingana na mazingira ya mtumiaji .

Kando na hilo, TV zina kipengele cha akili cha utambuzi wa sauti ambacho huwezesha watumiaji kuzidhibiti kwa amri rahisi. Pia hutoa dashibodi ya nyumbani inayoonyesha hali ya vifaa vingine mahiri vya nyumbani na kuwaarifu watumiaji kuhusu hali yoyote ambayo watumiaji wanapaswa kufahamu, kama vile mlango wa friji kuwa wazi na muda uliosalia wa kuisha kwa mzunguko wa kuosha.
Ili kusaidia katika ufuaji, LG imehifadhi mashine mahiri za kufulia kama vile Mashine ya Kuosha ya Vivace na mashine nyinginezo (Ai DD™️/DD) mashine nyingine za kufulia za AI DD™️ / DD ambazo hutambua aina ya kitambaa cha watumiaji na kupendekeza kozi bora zaidi ya kufulia.


Pia hutatua masuala madogo haraka kabla hayajaongezeka.
Kwa watumiaji wanaotaka kuweka vyakula na matunda vikiwa vipya kwa muda mrefu, LG imethibitisha kundi la Friji mahiri zilizoundwa kuunganishwa kwenye simu janja ya mtumiaji ili kudhibiti halijoto ya friji, kudhibiti Express Freeze, na kupokea uchunguzi wowote wa friji na chakula cha mtumiaji, taarifa za tarehe ya kumalizika muda wake. Hii inajumuisha LG Net 426(L) | Fridge Slim French Door, pamoja na InstaView Door-In-Door™️ ambayo kwa simu mahiri inayooana iliyounganishwa kwenye programu ya LG SmartThinQ™️, watumiaji wanaweza kurekebisha mipangilio ya halijoto wakiwa mbali ili friji iwe tayari kuchukua mkondo mkubwa wa ununuzi.
Vipengele vingine bora ni pamoja na mlango wa kisasa wa Ufaransa wenye chaguo bunifu za kuhifadhi kama vile Rafu inayokunjwa ambayo inaweza kujikunja yenyewe kwa ajili ya kuhifadhi vitu virefu zaidi na Mfumo wa Barafu wa Slim SpacePlus™️ ambao umejengwa ndani ya mlango wa friji ili watumiaji waweze kutumia rafu nzima ya juu.
Kulingana na Sa Nyoung Kim, teknolojia hii ya hivi punde ya msingi inayoangazia programu mpya na za kijanja husaidia kaya kuhifadhi nishati, na maji na ni rafiki wa mazingira huku ikitumika kwa urahisi, hivyo basi kukuza malengo muhimu ya maendeleo endelevu.

 

Share:

Friday, June 17, 2022

TANZANIA COMMERCIAL BANKI YATANGAZA KUPATA FAIDA YA BILIONI 19.7

Mwenyekiti wabodiya Tanzania Commercial Bank Dkt. Edmund Mndolwa (katikati), akizungumza na wanahabari wakati akitangaza kupata faida ya shilingi Bilioni 19.7 kwa mwaka ulioishia Desemba 31 2021 hatua inayo tajwa kuwa yamafanikio na kuimarika kwa benki hiyo ambayo ni muunganiko wa iliyokuwa benki ya TPB na TIB Corparate.
Afisa MtendajiMkuuwa Tanzania Commercial Bank TCB, Sabasaba Moshingi akizungumza wakati wa hafla ya kutangaza faida ya shilingi Bilioni 19.7 kwa mwaka ulioishia Desemba 31 2021 hatua inayotajwa kuwa ya mafanikio na kuimarika kwa benki hiyo ambayo ni muunganiko wa iliyokuwa benki ya TPB na TIB Corparate.
Mwenyekitiwabodiya Tanzania Commercial Bank Dkt. Edmund Mndolwa (katikati), akizungumza na wanahabari wakati akitangaza kupatafaida ya shilingi Bilioni 19.7 iliyopata benki hiyo wa pilikulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Commercial Bank TCB, Sabasaba Moshingi pamoja na maafisa wengine wa benki hiyo.

Tanzania Commercial Bank TCB imetangaza kupata faida ya shilingi Bilioni 19.7 kwa mwakaulioishiaDesemba 31 2021 hatua inayotajwa kuwa ya mafanikio na kuimarika kwa benki hiyo ambayo ni muunganiko wa iliyokuwa benki ya TPB na TIB Corparate.

Mwenyekitiwabodiya Tanzania Commercial Bank Dkt. Edmund Mndolwa ametoa taarifahiyo katika mkutano wa mwaka wa wanahisa wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar esSalaam nakusema kuwa faida hiyo ni kabla ya kodi.

Faida iliyopatikana mwaka 2021 inatajwa na uongozi wa benki kuwa ni kubwa kufuatia ile ya mwaka 2020 ambayo haijawahi kufikiwa tangu kuanzishwa kwa Benki ya TCB takriban miaka 95 iliyopita.

Amepongeza uongozi pamoja na wafanyakazi wa Tanzania Commercial Bank kwakuchangia mafanikio hayo licha ya changamoto zamdororo wauchumi uliosababishwa na wimbi la ugonjwawa UVOKO-19 ambao pia umeathiri uchumi wamataifa mengi duniani.

Kwaupande wake Afisa Mtendaji Mkuuwa Tanzania Commercial Bank TCB, Sabasaba Moshingi amesema kufuatia mafanikio hayo, wanahisa wamekubaliana kutoa gawio la hisa na kuelekeza kwenye kuimarisha mtaji wa Benki.

Mafanikio hayo pia wamewezesha amana za wateja kuongezeka hadi kufikia shilingi trilioni 1.18 mwaka 2021 kutoka shilingi trilioni 1.04 huku mikoponayo ikiongezeka hadi kufikia shilingi bilioni 718.6 kutoka bilioni 617.81

Tanzania Commercial Bank TCB imekuwa ikifanya kazi na wafanyabiashara kuanzia mfanyabiashara mdogo, wakati na mkubwa nakuhakikisha kila mwananchi anapata huduma kutoka benki ya TCB kila kona ya Tanzania na mipaka yake.

Share:

BENKI YA ABSA TANZANIA YAJA NA MIKAKATI KUWANUFAISHA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA KATI KIUCHUMI

   
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Kennedy Nyoni (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Abdi Mohamed (Kulia), Mkurugenzi wa Biashara wa Absa, Mervin Saprapasen na Mkurugenzi wa Uwezeshaji na Ushiriki wa Watanzania kwenye Miradi ya Kimkakati wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi (NEEC), Neema Mwakatobe wakibonyeza kitufe kuzindua kampeni ya uboreshaji wa huduma za kibenki kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati (SME) wa Benki ya Absa, uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Kennedy Nyoni (wa pili kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Abdi Mohamed (Kulia), Mkurugenzi wa Biashara wa benki hiyo, Mervin Saprapasen na Mkurugenzi wa Uwezeshaji na Ushiriki wa Watanzania kwenye Miradi ya Kimkakati wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi (NEEC), Neema Mwakatobe wakimsikiliza Meneja Huduma za Jamii wa Absa, Hellen Siria wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uboreshaji wa huduma za kibenki kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati (SME) uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkuu wa Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Ndabu Lillian Swere (kushoto) akizungumza na Mkurugenzi wa Biashara wa benki hiyo, Mervin Saprapasen (katikati) na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), Frank Nyabundege wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uboreshaji wa huduma za kibenki kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati (SME) uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Kennedy Nyoni (katikati) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Abdi Mohamed (Kulia) na Mkurugenzi wa Biashara wa benki hiyo, Mervin Saprapasen wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uboreshaji wa huduma za kibenki kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati (SME) uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Kennedy Nyoni akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uboreshaji wa huduma za kibenki kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati (SME) wa Benki ya Absa Tanzania.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Pass Leasing, Killo Lussewa akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uboreshaji wa huduma za kibenki kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati (SME) wa Benki ya Absa Tanzania uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya maofisa wa benki ya Absa wakishiriki uzinduzi wa kampeni ya uboreshaji wa huduma za kibenki kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati (SME) wa benki hiyo pamoja na waalikwa wengine jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Kennedy Nyoni akipiga picha ya kumbukumbu na Wakurugenzi pamoja na baadhi ya wakuu wa idara za Benki ya Absa baada ya uzinduzi wa kampeni ya uboreshaji wa huduma za kibenki kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati (SME) wa Benki ya Absa Tanzania uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Share:

Thursday, June 16, 2022

SERIKALI YATOA VITAMBULISHO VYA BIMA YA AFYA KWA WAZEE 937,266 NCHINI

Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk. Doroth Gwajima, akizungumza leo Juni 15/2022 wakati wa maadhimisho ya kupinga ukatili kwa wazee yaliyofanyika kitaifa katika Kijiji cha Kisharita Wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mwanaidi Ali Khamis, akizungumza kwenye maadhimisho hayo.
Katibu Mkuu Wizara  wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk. Zainabu Chaula akizungumza kwenye hafla hiyo.

 Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Wazee Taifa, Lameck Sendo, akizungumza kwenye maadhimisho hayo.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk. Doroth Gwajima, akisalimiana na Wazee mara baada ya kuwasili kwenye maadhimisho hayo.

Wananchi wa Kijiji cha Kisharita wakiserebuka katika sherehe hiyo.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kisharita wakiwa kwenye maadhimisho hayo.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Iramba, Pius Sangoma akizugumza kwenye maadhimisho hayo.

Mwenyekiti wa Machifu Mkoa wa Singida, Mugheni Sengi akizungumza kwenye maadhimisho hayo.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk. Doroth Gwajima, akitoa kwa Neema Msengi ambaye ni mmoja wa ndugu wa Wazee watatu waliouawa kikatili katika Kijiji cha Kisharita Wilaya ya Iramba mkoani Singida.

Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye maadhimisho hayo.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk. Doroth Gwajima, akizungumza na vijana wa SMAUJATA.

Afisa Mradi wa Sight Savers, Mradi wa Boresha Maisha, Edwin Barongo akizungumzia kuhusu shughuli mbalimbali zikiwemo za kuwapa huduma wazee.

Programu Meneja wa Shirika la HelpAge Tanzania, Joseph Mbasha, akizungumza kwenye maadhimisho hayo.


Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda akizungumza kwenye maadhimisho hayo.
Shabani Muhali kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa akizungumza kwenye maadhimisho hayo.

Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri wa Wazee Manispaa ya Singida, Juma Mudida, alihoji kwanini watuhumiwa wa mauaji ya wazee wa Kijiji cha Kisharita hawajapatikana hadi leo.

Wazee wakiwa katika maadhimisho hayo.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Iramba, Pius Sangoma  akiserebuka na Wanafunzi wa Shule ya Msingi, Kisharita.
Mwenyekiti wa Machifu Mkoa wa Singida Chifu Mughenyi Sengi (kushoto) na Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Wazee Manispaa ya Singida, Juma Mudida wakiserebuka na wanafunzi wa Shule ya Msingi Kishirita.
Wananchi wa Kijiji cha Kishirita wakiwa kwenye maadhimisho hayo.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Iramba, Ashery Samwel aakizungumza kwenye maadhimisho hayo.
Share:

LAUNCH AFRICA DISRUPTS THE MARKET TO BECOME PAN-AFRICA’S MOST ACTIVE EARLY-STAGE VC FUND

  
From left to right: Co-founder Janade du Plessis (in white sneakers); Margaret O’Connor(Chairperson of the Launch Africa Board) and co-founder Zach George.
  • Launched in July 2020, Launch Africa Ventures(‘Launch Africa”) has disrupted the market to become the most active early-stage Pan-African venture capital (“VC”) fund.
  • At the end of March 2022, its inaugural fund, Launch Africa Ventures Fund 1 (“Fund1”),closed at US$36.3 million, with investments from 238 retail and institutional investors in 40 countries.
  • Following the successful closure, Fund 1 announced its 100th investment at the end of May 2022, with $24 million invested in 108 early-stage tech and tech-enabled companies across 20 African countries.
In what most would describe as an audacious move, Launch Africa was established in July 2020, at the height of Covid-19, and had its first close in September 2020. The pandemic created a landscape that encouraged innovation and technological adoption at a speed once thought impossible, triggering business opportunities for African start-ups across technology industry verticals.

As a result, companies in the Launch Africa portfolio saw accelerated revenue growth and network effects during this period with the adoption of digital financial services, open banking, telemedicine, remote learning, data analytics, artificial intelligence (AI), digital identity management, and e-commerce across Africa.

Within 20monthsofits first close, the Pan-African VC fund has become widely known as a disruptor of the model for early-stage tech investments on the African continent. This was achieved by leveraging extensive ecosystem partnerships and trust networks with founders across Africa and investors around the globe.

Launch Africa’s partners believe that they have a critical role to play in developing and equipping tomorrow’s leaders today. With a focus on investing in the next generation of African technology start-ups, most of Launch Africa’s portfolio founders and their employees are 35 years of age and younger.

In addition to a focus on investing in the next generation of African tech leaders, diversity and inclusion are central to the Launch Africa investment ethos. To date, Fund 1 has invested in 91% African and 20% female co-founders.

Launch Africa is the brainchild of Zachariah (“Zach”) George and Janade du Plessis, both venture capital pioneers.

Zach completed his studies at the world-renowned Indian Institute of TechnologyMadras (I.I.T Madras) and graduate school at Stanford University whereafter he became a Wall Street bulge-bracket investment banker. He proceeded to become co-founder ofthe Barclays RiseGrowth Accelerator programmeand Startupbootcamp Afritech, two of the most significant accelerator programs on the African continent.

Part of the Barclays Accelerator, Rise offersan intensive start-upprogramme, designed to capture, shape and scale the next generation of innovative fintech businesses, whileStartupbootcamp Afritech is a Pan-African accelerator program that invests and grows innovative and scalable startups across Africa. Zach is also one of the most prominent Angel investors in African technology ventures.

Janade, a University of Cape Town (UCT) and Harvard Business School graduate, was the former Chief Investment Officer of the African Development Bank as well as the Head of Venture Capital at one of South Africa’s leading banks. He founded Abrazo Capital, a unique investment partner and capital management firm focused on disruptive social impact across Africa, underpinning hispassion for entrepreneurship and uplifting communities.

The two partners are joined on the Launch Africa Board bychairperson Margaret O’Connor – formerly a successful tech entrepreneur with a Silicon Valley exit, who later helped launch MasterCard across several key geographies in Asia. This was followed by a lengthy stint at the Center for Disruptive Technologies (CDT),a network born out of a collaboration between members of the of Singularity University's Global Studies Program and the Singularity Institute of Africa. As partner in CDT, Margaret kick-started CDT's Adventure Capitalist Network, connecting corporate venture capital, angel investors and early-stage VCs to emerging technology start-ups.

The 14-member Launch Africa team is actively supported by more than 30 global advisors, many of whom are leading C-suite executives at large global institutions, bolstering the skill set of Launch Africa’s portfolio founders with regional, product and sector expertise.

We assist the African founders of early-stage tech and tech-enabled companies to focus on what the continent needs right now—the rapid growth of businesses solving real-world problems combined with the creation of high-value jobs in sustainable ventures. We are proud to have helped many founders close their Seed funding rounds in 4-6 weeks, notably faster than the 4-6 months it typically takes for early-stage founders to close rounds in Africa,” saysZach.

LaunchAfrica also facilitates co-investment by its Limited Partners (LPs) through sharing due diligence, waiving fees and absorbing charges for LPs in the Seed and Pre-Series A investmentsled by the fund. To date, LaunchAfrica LPs have co-invested in excess of $14m in LaunchAfrica portfolio companies.

The LaunchAfrica team works with founders and expert advisors to fast-track exitopportunitiesfor investors.” Janade says. “Providing our exit strategy during these challenging times instills investor confidence and brings significant benefits to the African tech ecosystem.

CommerzVentures,a leading German fintech-focused Venture Capital firm, is one of the lead institutional investors in LaunchAfrica Ventures Fund 1. As a sector specialist, CommerzVentures offers a comprehensive network of partners, decision-makers and investors within Fintech and financial services across the European Union, as well as actionable intelligence and advisory.

We are pleased to partner with LaunchAfrica Ventures to invest in some of the most exciting fintech investment opportunities in Africa,” says CommerzVentures Managing Partner, Patrick Meisberger. “LaunchAfrica provides a diversification of risk, returns, and impact byoffering access to early-stage, post-revenue companies across multiple market verticals and geographic regions.

Adapting the lean start-up methodology to early-stage investing, the fund created due diligence systems that captured investment insights from expert advisors and ecosystem partners across Africa to supplement the team’s extensive experience, growing value in tech and tech enabled companies across the continent.

LaunchAfrica Fund 1’s portfolio currently includes 38% Fintech, 16% e-Commerce and Marketplaces, 13% Health-Tech, 12% Logistics and Mobility, 11% Data Analytics/A.I. and 7% Ed-Tech.

Launch Africa is domiciled in Mauritius and administered by the Apex Group – one of the world’s leading fund administrators with over $2 trillion in assets under administration.
Share:

SEKONDARI BUNDA YAITAKA DIT KUHAMASISHA MASOMO YA SAYANSI

 

Na Mwandishi Wetu, Mara

MKUU wa shule ya Sekondari Bunda iliyopo Wilaya ya Bunda mkoani Mara, Charles Somba, ameitaka Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) kuwa na muendelezo wa programu ya uhamasishaji kuhusu mtoto wa kike kupenda masomo ya Sayansi.

Somba ameyasema hayo alipokuwa anafungua programu ya kuwahamasisha mabinti iliyoratibiwa na kuongozwa na wataalam kutoka DIT iliyofanyika shuleni hapo ikihusisha shule nne za sekondari za Wilaya hiyo ambazo ni shule ya Sekondari Sazila, Rubana na Nyendo Sekondari pamoja na Bunda.

"Naipongeza Taasisi hii, hiki mnachokifanya ni kitu kizuri, maana wakati mwingine tunafundisha hawa lakini wasipoona kwa uhalisia kama ambavyo mmekuja hawaweki bidii ila sasa hata ninyi mabinti mmeona wamama wanasayansi hawa hapa kazi kwenu mjitahidi," alisema.

Aidha, Somba aliiomba DIT kupanua wigo ili kuhakikisha watoto wa kike wanahamasika hata ikiwezekana wanapoingia kidato cha kwanza ili waweze kuwajengea uelewa mapema na hii isiwe Bunda pekee, ikiwezekana fanyeni kila mkoa hata nchi nzima.

Mratibu wa program ya uhamasishaji Dk. Triphonia Ngailo alisema, kwa sasa idadi ya watoto wa kike wanaohitimu masomo ya Sayansi bado ipo chini ambapo takwimu zinaonesha wanawake wanasayansi ni 21% wakati wanaume ni asilimia 79% hivyo DIT kupitia ufadhili wa Mradi wa EASTRIP wakaanzisha programu hiyo ili wawape moyo kuwa inawezekana kwa pamoja wawatie moyo na wapambane kuhakikisha idadi inaongezeka kwa kuwa Serikali inawajali na imeweka mazingira wezeshi ili kuwapatieni ninyi elimu ili muweze kunufaika na fursa zilizopo kwenye masomo ya sayansi.

Naye Mwalimu Samora Laizer wa Bunda Sekondari amefurahishwa na program hiyo kwa kuwa inaleta uhalisia wa kile kinachofundishwa.

"Hili ni jambo jema maana wakati mwingine ukifundishwa tu bila kuona uhalisia inapoteza nguvu ila kama walivyosikia leo itawaongezea nguvu" alisema Laizer

Aidha, Mwalimu Fibe Musa wa Rubana Sekondari ameishauri Taasisi kujipanga zaidi kwa kuwa jambo hilo zuri na linawasaidia zaidi hasa wanafunzi wakishahitimu masomo wanakuwa na mwanga wa kuchagua fani wanazozipenda.
Share:

Sunday, June 12, 2022

BENKI YA NBC YAPONGEZWA KWA HUDUMA BORA ZANZIBAR

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mh. Hemed Suleiman Abdulla (kulia) na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Zubeir Ali Maulid wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC, Theobald Sabi (kushoto) walipokutana Zanzibar. Pamoja na mambo mengi, Mh. Abdulla ameipongeza Benki hiyo kwa kuendelea kutoa huduma bora za kifedha kwa wananchi wa Zanzibar na Tanzania bara na Taifa kwa ujumla hapa nchini.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, MH. Hemed Suleiman Abdulla pamoja na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Zubeir Ali Maulid wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi na Maofisa wengine kutoka benki hiyo.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla ameipongeza Benki ya NBC kwa kuendelea kutoa huduma bora za kifedha kwa wananchi wa Zanzibar na taifa kwa ujumla.

Mheshimiwa Abdulla aliyasema hayo wakati akizungumza na viongozi kutoka Benki ya Taifa ya Biashara NBC alipokutana nao katika ofisi ya Spika mjini Unguja, mara baada ya viongozi hao kuhudhuria kikao cha Baraza la Wawakilishi wakiwa ni wageni wa Spika wa Zanzibar, Mheshimiwa Zubeir Ali Maulid.

“Nawapongeza sana NBC kwa kuendelea kuwa mdau muhimu hapa Zanzibar na pia Tanzania bara kwa uwezeshaji wa kiuchumi kwa watu wa Zanzibar.

Endeleeni kuongeza wigo wa kutoa huduma kwa kuongeza matawi na mawakala ili muweze kuwafikia wananchi wengi zaidi.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inawaahidi kutoa ushirikiano na kuendelea kuweka mazingira bora ya kufanyia biashara” alisema.

Kwa upande wake Spika wa Zanzibar, Mheshimiwa Zubeir Ali Maulid aliishukuru Benki ya NBC kwa kuendelea kuwa mdau mkubwa wa maendeleo akitolea mfano misaada mbalimbali kwa jamii ambayo benki hiyo imekuwa ikitoa kila mwaka.

Spika Zubeir alipongeza pia udhamini wa Benki ya Taifa ya Biashara NBC katika ligi ya mpira wa miguu nchini, NBC Premier League kuwa ni wenye tija kwa taifa kwa kutoa vipato na kuibua vipaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi alimshukuru Makamu wa Pili wa Rais wa Jamhuri ya Mapinduzi ya Zanzibar Mheshimiwa Abdulla na Spika wa Zanzibar Mheshimiwa Zubeir Ali Maulid kwa mkutano huo wenye lengo la kuboresha mahusiano ya pande zote ili kuhakikisha wanaunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuru ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan hasa katika kukuza uchumi wa nchi yetu.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive