A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Showing posts with label LOCAL. Show all posts
Showing posts with label LOCAL. Show all posts

Monday, April 13, 2026

BENKI YA ABSA TANZANIA YAKABIDHI WODI YA WAZAZI ILIYOKARABATIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA TEMEKE

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya (kushoto), na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke, Dk. Mfaume Kibwana (Katikati), wakifungua pazia kuashiria makabidhiano rasmi ya Wodi ya Wazazi, iliyofanyiwa ukarabati na Benki ya Absa. Hafla hiyo ilifanyika hospitalini hapo, Temeke, Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo, Bw. Aron Luhanga.

Benki ya Absa Bank Tanzania leo imekabidhi rasmi wodi iliyokarabatiwa ya Wazazi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke, ikiwa ni sehemu ya mpango wa kijamii unaoongozwa na wafanyakazi wa benki hiyo, wenye lengo la kuboresha mazingira ya huduma kwa kina mama, watoto pamoja na wahudumu wa afya.

Ukarabati huo umetekelezwa kupitia mpango wa Absa unaojulikana kama “Adopt a Ward”, ambao unaendeshwa na wafanyakazi wenyewe kwa kubaini mahitaji ya jamii, kukusanya rasilimali na kushirikiana na benki katika kuleta mabadiliko chanya yenye tija kwa jamii.

Kazi za ukarabati zilizofanyika katika wodi hiyo ni pamoja na akarabati wa paa na dari, uwekaji wa vigae kwenye kuta za vyoo, ukarabati wa madirisha, kazi za nje za mabomba maalumu ya plastiki (PVC), ukarabati wa mifumo ya umeme, kazi za mabomba ya maji, ufungaji wa milango ya alumini, ufungaji wa viti vya vyoo na sinki pamoja na uchoraji wa majengo.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya, alisema kuwa mpango huo unaonyesha imani ya muda mrefu ya benki kwamba jamii huimarika pale taasisi na watu binafsi wanapowekeza pamoja katika suluhisho za vitendo zinazoboresha maisha.

Katika Absa, tunaamini kuwa ‘Stori yako ina Thamani’, na leo tunakumbushwa kuwa hadithi za kina mama, watoto, familia na wahudumu wa afya zina umuhimu mkubwa. Ukarabati huu ni utekelezaji wa dhana yetu ya ‘Kuwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, Hatua Moja baada ya nyingine’. Pia unaonyesha utamaduni tunaoujenga Absa, ambapo watu wetu wanachukua jukumu la kubaini mahitaji ya jamii, kuhamasisha msaada na kushirikiana na benki kuleta mabadiliko endelevu.

Aliongeza kuwa mradi huo unaakisi ajenda pana ya uwajibikaji wa kijamii na uendelevu ya Absa, kwa kusaidia kuboresha mazingira ya huduma kwa heshima na ustahiki kwa wanawake na watoto, sambamba na kuimarisha mchango wa benki katika ustawi wa jamii.

Huu ni mfano halisi wa namna Absa inavyokuwa nguvu chanya katika jamii. Kwa kuboresha wodi ya Mama na Mtoto, tunawaunga mkono wahudumu wa afya wanaohudumia jamii kila siku, na pia kuboresha uzoefu wa huduma kwa kina mama na watoto. Tunaamini uwekezaji wa pamoja wa aina hii ni muhimu katika kujenga jamii imara na yenye afya.

Mpango huo uliwakutanisha wafanyakazi wa Absa kutoka idara mbalimbali, ukiakisi utamaduni wa ndani wa taasisi hiyo unaowahamasisha wafanyakazi kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo ya jamii, huku benki ikiongeza nguvu katika jitihada zao ili kuongeza athari chanya.

Mfumo huu wa utoaji unaoongozwa na wafanyakazi pamoja na msaada wa taasisi, umeendelea kuwa sehemu ya mkakati mpana wa Benki ya Absa Tanzania katika uwajibikaji kwa jamii, unaojikita katika ushirikiano, ujumuishi na uundaji wa thamani ya muda mrefu kwa jamii.

Hatua hiyo ya makabidhiano pia inaendana na lengo la Absa ya “Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, Hatua Moja baada ya nyingine” pamoja na ahadi yake ya chapa ya “Stori yako ina Thamani”, ambayo ni msingi wa namna benki hiyo inavyotoa thamani kwa wateja, jamii na wadau wake.

Kupitia uboreshaji wa mazingira katika sekta muhimu ya afya, Benkiy a Absa Tanzania inalenga kuchangia katika kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto, huku ikiimarisha umuhimu wa ushirikiano wa pamoja katika kutatua changamoto za jamii.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya (katikati), akikata utepe kuashiria makabidhiano rasmi ya Wodi ya Wazazi ya Hosptali ya Rufaa ya Mkoa Temeke, iliyofanyiwa ukarabati na Benki ya Absa. Hafla hiyo, ilifanyika hospitalini hapo, Temeke, Dar es Salaam leo. Kulia ni na Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Mfaume Kibwana na kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga.
Mkuu wa Udhibiti ya Udhibiti Ubora wa, Bw. Hosptali ya Rufaa ya Mkoa Temeke, Dk. Selemani Kivoja, akisalimiana na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya (kushoto), huku Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Mfaume Kibwana (kushoto), akiangalia, katika hafla ambayo beni hiyo ilikabidhi jengo la wodi ya wazazi lililokarabatiwa na benki hiyo, katika hafla hiyo ilifanyika hospitalini hapo, Temeke, Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Absa Tanzania wakiongozwa na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu, Bw. Patrick Foya, pamoja na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke, wakipiga picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa hafla ya makabidhiano ya Wodi ya Wazazi iliyofanyiwa ukarabati na benki hiyo.
Share:

Wednesday, March 18, 2026

MBUNGE WA SEGEREA AWAKUMBUKA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU WAKUSIKIA BUGURUNI.

Mbunge wa Jimbo la Segerea, Agnesta Lambert (CHAUMA), ameendeleza juhudi zake za kuimarisha ustawi wa makundi maalum kwa kuwafikia watoto wenye ulemavu wa kusikia katika Shule ya Msingi ya Viziwi Buguruni, jijini Dar es Salaam ambapo amekabidhi msaada wa vyakula pamoja na mahitaji mengine muhimu, kwa lengo la kuwawezesha watoto hao kusherehekea kwa heshima na furaha sikukuu za Idd el-Fitr na Pasaka.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mbunge huyo ameeleza kuwa anahisi kuwajibika kusimamia masuala ya kijamii, hususan yanayohusu watoto wenye mahitaji maalum na kusisitiza kuwa uwekezaji katika ustawi na elimu ya watoto hao ni msingi muhimu wa kujenga jamii jumuishi na yenye usawa wa fursa.

‎Amebaini changamoto kubwa inayoikabili shule hiyo, ni upungufu wa mabweni kwa wanafunzi hao na kuahidi kufikisha suala hilo bungeni na kuongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka kipaumbele katika sekta ya elimu, na hivyo ana imani kuwa changamoto zilizopo zitapatiwa ufumbuzi.

Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule hiyo ameeleza kuwa uhaba wa mabweni unawaweka watoto hao katika hatari, ikiwemo uwezekano wa kupata ajali kutokana na mazingira yasiyo rafiki kwa hali yao.


‎Wanafunzi hao wakatoa wito kwa jamii na wadau mbalimbali kuendelea kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum, wakisisitiza umuhimu wa mshikamano wa kijamii katika kujenga mustakabali bora kwa wote.

Share:

Tuesday, March 3, 2026

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR AWASHAURI VIONGOZI KUJENGA UTAMADUNI WA KUWASAIDIA WANANCHI

  

Mwakilishi wa Jimbo la Kiwani ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amewashauri viongozi kujenga utamaduni wa kuwasaidia wananchi hasa katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani ili kuweka uwiano sawa wa mahitaji.

Ametoa wito huo mara baada ya zoezi la kuwagawa Iftar kwa wananchi wa jimbo la kiwani shehia ya kendwa yenye nyumba zaidi ya 1156 hafla iliyofanyika kwenye uwanja wa mpira wa Mauuwani Jimbo la Kiwani.

Amesema ataendeleza utamaduni wake wa kugawa Iftari kwa wananchi wote hasa wenye mahitaji Maalum ili kupunguza ukali wa maisha na kupata chakula katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Amefahamisha kuwa mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni Maalum kwa waumini wa Dini ya kiislamu kufanya matendo mema yanayompendeza Mwenyezi Mungu,hivyo ni vyema kwa kila mwenye uwezo kutoa na kuwapa wahitaji ili kupata fadhila zilizomo ndani ya mwezi huu.

Aidha, Mhe. Hemed amesema anatarajia kuzifikia shehia zote saba ( 7 ) zilizomo ndani ya Jimbo hilo na kuzipatia Iftari jambo ambalo litaongezea umoja na mshikamano kwa wannachi wa jimbo hilo.

Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewaomba wafanya biashara kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu wakiweo Masikini, Wajane, Mayatima na watu wasiojiweza hasa katika mwezi mtukufu wa ramadhani ili kuzidi kuzitakada biashara zao na kupata fadhila zilizomo ndani ya mwezi wa ramadhani.

Kwa upande wake mfanya biashara SAID NASSIR NASOR ( BOBAR ) ameishukuru serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kwa kuendelea kumpatia ushirikiano ambapo kwa mwezi huu wa ramadhani amepatiwa usafiri wa kusafirisha bidhaa mbali mbali ambazo atawakabidhi wananchi wa kisiwani Pemba wakiwemo waannchi wa jimbo la kiwani.

Amesema kuwa lengo lake ni kuwafikia wananchi mbali mbali wasio na uwezo kwa Unguja na Pemba ili kila mwananchi apate sadaka itakayowasaidia kwa Iftari lakini pia aweze kupata fadhila hapa duniani na kesho akhera.

Nao wananchi waliopatiwa sadaka hizo wamemshukuru mwakilishi wao kwa kuendelea kuwatumikia kwa moyo wa upendo, huruma na usawa kwa wananchi wote jimboni humo jambo ambalo linawapa faraja na imani kubwa juu yake.

Wamesema hawana shaka na utendaji kazi wa Mhe. Hemed na matumaini yao makubwa ni kuzidi kuwaletea maendeleo jimbo humo kama vile alivyoanza kuzitekeleza ahadi mbali mbali alizoziahidi wakati akiomba ridhaa ya kuwa mwakilishi wa Jimbo la Kiwani.

Share:

Tuesday, December 9, 2025

INNOVATION HUBS NETWORK STAKEHOLDERS RECOGNIZED FOR OUTSTANDING CONTRIBUTION

The Chairperson of the Board of the Tanzania Hubs Network (THN), Dr. Irene Shubi Isinika, speaking at the ceremony to commend pioneering innovation stakeholders held alongside the THN Annual General Meeting in Dar es Salaam recently. Since its establishment in 2020, THN has been at the forefront of building an innovation ecosystem by empowering innovation hubs to support innovators and entrepreneurs in driving social and economic development.
The Chairperson of the Board of the Tanzania Hubs Network (THN), Dr. Irene Shubi Isinika (right), presenting an honorary award to the Project Manager of the Funguo Program run by the United Nations Development Programme (UNDP), Mr. Joseph Manirakiza, in recognition of his contribution to innovation development in the country. This took place during the ceremony to commend innovation stakeholders held alongside the THN Annual General Meeting in Dar es Salaam recently.
Senior Lecturer at the College of Information and Communication Technologies of the University of Dar es Salaam and Innovation Coordinator through the university’s innovation hub (UDICTI), Dr. Moses Ismail (left), receiving an award presented by the Tanzania Hubs Network (THN) from the Country Director of the Westerwelle Tanzania Foundation, Mr. Isaack Shalo, at a ceremony organized by THN in Dar es Salaam to recognize pioneering stakeholders who have contributed to the advancement of innovation in the country.

By Peter Mgongo, Dar es Salaam

In recognizing the contribution of stakeholders who have supported the growth of innovation in the country, the Tanzania Hubs Network (THN) organized an official ceremony to commend pioneering innovation stakeholders, alongside the network’s annual general meeting.

Speaking at the ceremony in Dar es Salaam yesterday, the Executive Director of the network, Mr. Kiko Kiwanga, said the network, which was established in 2020, connects more than 62 hubs across Mainland Tanzania and Zanzibar, bringing together innovation hubs from universities, organizations, governmental bodies, and private centers.

Today is a very special day for our ecosystem because since we began, this is our first annual meeting, which started this morning with the guest of honor being the Director of the ICT Commission, Dr. Nkundwe Mwasaga. We are now doing something unique within our ecosystem to recognize stakeholders who have made significant contributions in advancing innovation and strengthening these hubs.

The contributions of these stakeholders have always been acknowledged, but today, for the first time, we are holding this event to recognize the pioneering stakeholders who have put great effort into ensuring that young innovators and startup entrepreneurs grow and receive support within our ecosystem,” said Mr. Kiwanga.

Speaking about the THN Network, the director said that since its establishment, it has been at the forefront of building an innovation ecosystem by empowering innovation hubs to support innovators and entrepreneurs to drive social and economic development.

We call upon the government to increase investment in supporting youth through this network, enabling them to achieve their innovation goals and establish companies with great potential to create jobs and solve various societal challenges. These hubs have done tremendous work in preparing young people, many come in without any ideas at all, and they are supported until they develop concrete concepts.

Speaking at the event, one of the stakeholders who received an award, Dr. Moses Ismail, a Senior Lecturer at the College of Information and Communication Technologies of the University of Dar es Salaam and Innovation Coordinator through the university’s innovation hub (UDICTI), said that although the university engages in teaching, research, community service, and consultancy, with innovation and entrepreneurship taught to first-year students for many years, in 2010 the college established the UDICTI innovation hub with the aim of providing practical innovation training.

The hub provides a dedicated workspace, specialized training in developing innovative products, and linkages to innovation stakeholders who can support the work they undertake.

Innovation is a crucial tool for the development of a country and its people because it enhances the value of local innovative products. Many of us rely heavily on imported products, yet locally we have various innovative products that help our students become major contributors to the production of these products, which eventually grow into companies and help increase employment, especially at a time when we want our university graduates to be key drivers of job creation rather than job seekers,” said Dr. Ismail.

Meanwhile, the Chief Executive Officer of the Business Registrations and Licensing Agency (BRELA), Mr. Godfrey Nyaisa, speaking at the event, urged innovators, especially those running startups to register their businesses with BRELA so they can benefit from various guidelines that will enable them to operate efficiently. He also challenged the THN Network to involve government authorities in their day-to-day operations.

With a vision of strengthening collaboration, providing resources, and promoting knowledge exchange among its members, THN also collaborates with the Information and Communication Technologies Commission (ICTC) to strengthen the innovation environment and promote the establishment of innovation hubs in various regions.

Share:

Sunday, August 31, 2025

DK.MWINYI:CCM ITAFANYA KAMPENI ZA KISTAARABU KWA SERA ZENYE TIJA KWA WANANCHI

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ambaye pia ni Mgombea Mteule wa Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo katika Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na kuahidi kuwa CCM itafanya kampeni za kistaarabu zitakazozingatia Utamaduni, Silka na Desturi za Wazanzibari.

Dkt. Mwinyi amechukua fomu hiyo katika Afisi za Tume ya Uchaguzi leo, tarehe 30 Agosti 2025, asubuhi, na hatimaye msafara wake ukaelekea Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui kupitia Barabara ya Miembeni, Kariakoo, Rahaleo na Michenzani, akisindikizwa na mamia ya wanachama wa chama hicho waliokuwa wamejipanga pembezoni mwa barabara.

Aidha, Dkt. Mwinyi amezuru Kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Hayati Abeid Amani Karume, na kisha kuzungumza na Wazee wa Chama Cha Mapinduzi afisini hapo.

Akizungumza na mamia ya wanachama wa CCM katika Uwanja wa Mao Tse Tung, Mgombea Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesisitiza kuwa CCM itafanya kampeni zitakazoepuka chuki, mifarakano na ubaguzi miongoni mwa wananchi, na badala yake kufanya kampeni zitakazowaunganisha Wazanzibari kwa kuzingatia maslahi yao ya kijamii na kiuchumi.

Ameeleza kuwa katika kampeni hizo, CCM itaonesha mafanikio yaliyopatikana katika awamu ya kwanza ya Uongozi wa Awamu ya Nane pamoja na utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2025–2030, ambayo itawasilishwa kwa wananchi wakati wa kampeni.

Aidha, ametoa wito kwa wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla kuungana na kuwapigia kura wagombea wote walioteuliwa na chama hicho katika nafasi zote kuanzia Urais, Ubunge, Uwakilishi na Udiwani ili kuhakikisha CCM inaendelea kushika dola.

Halikadhalika, Dkt. Mwinyi amewahakikishia wananchi kuwa CCM itaendelea kudumisha hali ya utulivu na amani iliyopo nchini wakati wa kampeni, uchaguzi na baada ya uchaguzi.
Share:

Wednesday, August 13, 2025

AGRA, Sahara Accelerator kunufaisha vijana wengi kupitia kilimo

Na Mwandishi Wetu

Kilimotech Accelerator kupitia Youth Entrepreneurship for the Future of Food and Agriculture (YEFFA) inayodhaminiwa na shirika la AGRA Tanzania na kutelekelezwa na Sahara Accelerator inatarajia kunufaisha vijana wapatao 265,000 wanaojihusisha na masuala ya kilimo.

Akizungumza wakati wakijadili na vijana kuhusu fursa hiyo jijini Dar es Salaam, Adam Mbyallu wa Sahara Accelerator alisema fursa hiyo itatoa kiasi cha dola milioni 20 kwa bunifu za kilimo zinazojumisha mnyororo wa thamani kwa mazao manne ambayo ni mbogamboga na matunda, alizeti, mpunga na mahindi.

"Tuna hakikisha namna gani tunaweza kusaidia upatikanaji wa vifaa vya kilimo kupitia teknolojia za kidigitali tunasaidia vijana wenye bunifu mbalimbali zinzojibu changamoto za upatikanaji wa vifaa za kilimo," alieleza Mbyallu.

Alisema kupitia bunifu hizo watawapatia vijana hao mafunzo,mentorship na kuwaunganisha wa wadau mbalimbali na kusaidia kwenda shambani kwenye kilimo na kujiuza.
Alifafanua kuwa bunifu wanazotafuta zitajibu changamoto za kilimo kama vifaa,mafundi,masoko,udhibiti wa mazao,uharibifu wa mazao baada ya mavuno changamoto ambazo wadau wa kilimo walisema zipo.

"Maeneo hayo yote kama vinavifaa vya kilimo vingesaidia sana vijana kujiajiri kwenye kilimo kama watajiajiri tunaangalia jinsi ya kuwawezesha kupitia teknolojia ya kidijitali," aliongeza.

Mbyallu alisema ili kufanikisha upatikanaji wa bunifu hizo wamefungua dirisha la usajili wa bunifu kwa muda wa miezi miwili ambapo itafungwa Agosti 18, 2025 na zitachujwa kuangalia kama bunifu hizo zinakidhi vigezo na baada ya hapo watawaunga mkono.

"Tutawaunga mkono Kwa mafunzo,mentorship,changamoto na kuwaunganisha na wadau watakaowasaidia bunifu zao kwenda soko kama wadau wanaouza zana za kilimo,mafundi wa zana za kilimo,wanaotengeneza zana za kilimo,taasisi za fedha na wadau wengine," alisisitiza.
Aliongeza: "Bunifu zitakwenda kwenye mazao manne yamegawiwa katika kanda kuna miradi kulingana na mazao ya eneo mfano Morogoro wanajikita na mbogamboga na alizeti ,Mbeya wana mbogamboga na mpunga, Njombe mbogamboga na mahindi, Singida ni alizeti kila kanda imepewa aina ya zao… tunakwenda kote."
Share:

Friday, June 13, 2025

UWT TANGA YAKUNWA NA UCHAPAKAZI WA MBUNGE UMMY MWALIMU

Na - Mwandishi Wetu, TANGA

Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) imempongeza Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini, Ummy Mwalimu, kwa uchapakazi na uwajibikaji wake wa kuwaletea wananchi maendeleo na namna anavyoilea Jumuiya hiyo muhimu kwa uhai wa Chama.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo wilaya ya Tanga, Bi. Moza Seif, katika Baraza lake la Kikanuni lililokaa Juni 12, 2025 katika Ukumbi wa CCM wilaya ya Tanga ambapo pamoja na mambo mengine, Baraza hilo lilikuwa na ajenda ya kusoma Utekelezaji wa Ilani kwa Madiwani wa Viti Maalum wa Jiji la Tanga.

Bi. Moza amempongeza Mbunge Ummy Mwalimu ambaye amekuwa bega kwa bega na Jumuiya hiyo katika kusukuma gurudumu la maendeleo ndani ya Jiji la Tanga. Katika kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazofanywa na Mbunge huyo, uongozi wa UWT Tanga ulimpatia Mbunge Ummy Mwalimu Zawadi mbalimbali za Pongezi ambazo zilipokelewa na Bi. Mwanahawa Mwalimu kwa niaba ya Mbunge.

Sambamba na hilo, Madiwani wa Viti Maalum wa Jiji la Tanga walisoma Utekelezaji wa Ilani ambapo kazi nyingi na miradi mingi ya maendeleo imefanyika katika kipindi cha uongozi wao. Aidha, wanachama wameaswa kuwa wamoja kuelekea Uchaguzi Mkuu Mwezi Oktoba, 2025 kwa kuepuka fitna, majungu na makundi.

Katika hatua nyingine, Baraza hilo lilihudhuriwa viongozi mbalimbali wa Chama wakiwemo Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga, Meja Mstaafu Hamisi Bakari Mkoba ambaye alikuwa Mgeni Rasmi pamoja na Katibu wa CCM wilaya ya Tanga, Jamal Khimji.
Share:

Friday, April 18, 2025

WATU 12,000 WAHOFIWA KUUGUA UGONJWA WA HIMOFILIA NCHINI

Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (katikati), akika utepe kuashiria uzinduzi wa kliniki ya himofilia, sambamba na maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani katika hafla iliyofanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, Visiwani Zanzibar, jana. Pamoja naye ni wawakilishi kutoka Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Taasisi ya himofilia ya novo nordisk, Wizara za afya kutoka Tanzania na Zanzibar, Hospitali ya Taifa Muhimbili, Chama cha Himofilia Duniani na wadau wengine.

Na mwandishi wetu, Zanzibar.

TAKWIMU zinaonyesha kati ya watu elfu sita hadi elfu 12, wanahofiwa kuugua ugonjwa wa himofilia nchini huku idadi ya watu waliogundulika kuwa na ugonjwa huo hadi sasa wakiwa ni 451 pekee.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui katika hafla ya maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani iliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, Visiwani humo jana.

Hafla hiyo iliandaliwa na Chama cha Himofilia Tanzania (HST), kwa uwezeshaji kutoka Taasisi ya himofilia ya novo nordisk na Chama cha Himofilia Duniani kwa ushirikiano kutoka Serikali ya Tanzania na ya Zanzibar, wizara za afya kutoka pande zote mbili, Hospitali ya Taifa Muhimbili na wadau wengine.

Mheshimiwa waziri alisema takwimu za kidunia zinaonesha mtu mmoja kati ya 10 anapatikana na ugonjwa huo, hii ikimanisha kuwa Tanzania yenye watu takribani milioni 61 inaweza kuwa na wagonjwa elfu 6 hadi elfu 12, huku ikielezwa 97% ya watu wenye ugonjwa huu duniani kote hawajagundulika, ambapo kwa upande wa Tanzania waliogundulika mpaka sasa ni 451 tu.

Kama tunavyofahamu himofilia ni ugonjwa wa damu kukosa uwezo wa kuganda unaosababishwa na ukosefu wa kiwango cha chembechembe za protini zinazotakiwa kugandisha damu hivyo kusababisha damu kuvuja kwa mda mrefu pindi mtu anavyopata jeraha hivyo kuhatarisha maisha yake."

Maisha ya watu wenye matatizo haya yanahitaji uangalizi mkubwa na tahadhari kubwa ili kuzuia uvujaji wa damu, ulemavu na vifo hivyo kuwepo na hitaji la kubaini aina ya himofilia na kupata matibabu ya kuchomwa sindano yenye chembechembe za protini zinazokosekana mwilini ili kusaidia kuzalisha damu”, alisema Waziri Mazrui.

Alisema Mwaka 2020 Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ikishirikiana na Taasisi ya himofilia ya Novo Nordisk ilianzisha mradi wa kuongeza kasi ya upatikanaji wa huduma kwa watu wenye magonjwa ya damu lengo kuu ikiwa ni kuunga mkono serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya afya katika kupunguza madhara ya vifo vinavyotokana na magonjwa yasiyo ambukiza ikiwemo himofilia na selimundu.

Pamoja na hayo alisema, lengo kubwa la mradi huu ni kuwezesha upatikanaji wa vipimo vya wagonjwa wa damu, seli mundu, na himofilia katika hospitali za rufaa nchini sambamba na kuanzisha kliniki za magonjwa hayo, kuwezesha mafunzo na upatikanaji wataalamu wa afya waliobobea kwenye hospitali hizo pamoja na upatikanaji wa miundo mbinu sahihi, vipimo na dawa ili wagonjwa wahudumiwe mahali popote nchini bila kulazimika kufika Muhimbili.

Katika maadhimisho haya leo nina furaha kubwa kuwaambia kuwa mradi huu katika kipindi cha uhai wake kuanzia kipindi cha kwanza hadi kipindi cha pili tayari umefanikisha kukamilisha ukarabati wa kliniki za himofilia katika hospitali 13 zikiwemo hospitali za Muhimbili, KCMC, mbeya na Bugando."

Tunawashukuru pia wafadhili wetu kwa msaada wa dawa zenye thamani ya shs milioni 500, kwa kweli mmetusaidia sana na vifaa nyenye gharama kubwa, chini ya uongozi wa maraisi wetu, Samia Suluhu Hassan na Hussein Ali Mwinyi, tunaendelea kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kila mtanzania anapata matibabu kwa usahihi na kwa wakati, hivyo juhudi zenu hizi zinatufanya twende sambamba na juhudi za viongozi wetu hawa”, aliongeza waziri huyo.

Akizungumzia zaidi kuhusu himofilia, Mwenyekiti wa Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Dk. Stella Rwezaura alisema, asilimia 70 ya wagonjwa wa himofilia wanarithi na inabebwa katika kinasaba cha kike, kwani mwanamke ana ‘x’ mbili na mwanaume ana ‘xy’, hivyo endapo mwanamke ana ‘x’ yenye vinasaba vya himofilia, asilimia 50 ya watoto wake wa kiume watakuwa na tatizo hilo hivyo kufanya asilimia 99 ya wagonjwa wa himofilia kuwa wanaume.

Tunaposherehea Siku ya Himofilia Duniani, sambamba na Kauli Mbiu ya Mwaka 2025 isemayo, ‘Wanawake na Wasichana pia wanakumbwa na tatizo la kuvuja damu, licha ya himofilia kuwapata zaidi wanaume, tuwaite wanawake waje kupima, waweze kutambulika mapema hivyo kupata matibabu sahihi."

Lengo la mradi huu ni kuwatambua wagonjwa wengi zaidi na kupata huduma kwani wapo wengi wenye tatizo hili na hii ilitokana na changamoto ya uhaba wa vifaa, mashine na vitendanishi vya kutambua ugonjwa huu, hivyo kwa msaada wa wafadhili, vyama vya wagonjwa pamoja na serikali yetu sikivu ya Tanzania, ikiongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan pamoja Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi, wizara yake ya afya na wadau wengine, huduma hizi sasa zinafika karibu kwa wananchi kwa usahihi zaidi”, aliongeza Dk. Stella.

Naye mmoja wa wagonjwa wa Himofilia ambaye pia anauguza watoto wawili wenye ugonjwa huo, Regina Shirima alisema anakabiliwa na changamoto kubwa ya hali duni ya kiuchumi baada ya kutumia muda wake mwingi katika kuhudumia watoto hivyo kutokuwa na muda kabisa wa kujishughulisha na kazi za kujitafutia kipato.

changamoto nyingine ni kwa watoto wenyewe hawapati muda wa kusoma, kucheza na wenzao ama kuwa na furaha kwani muda mwingi wanakuwa wagonjwa, lakini ni ukweli kuwa wanawake ndio wanabeba vinasaba vya himofilia, lawama nyingi zinakuja kwetu kwa kuzaa watoto wenye changamoto hii, hivyo unajikuta familia imekuacha”. Akiongeza kuwa kuna wakati kulikuwa na changamoo ya upatikanaji wa dawa ukizingatia kuwa mgonjwa wa himofilia akikosa dawa tu anaweza uhai wake unakuwa hatarini.

Natoa wito kwa jamii kuwa gonjwa hili la himofilia lipo na mama sio anayesababisha mtoto kuzaliwa na ugonjwa huu, kwani huwezi kupata mtoto bila ya baba”, aliongeza Bi. Regina kwa mshangao.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Dk. Lawrence Museru alisema HST imekuwa sauti ya wenye ugonjwa wa himofilia katika kuangalia changamoto wanazopitia katika kutafuta tiba, moja ya changaoto ni utambuzi wa ugonjwa huu katika jamii.

Wagojwa wamekuja kutambulika baada ya kupoteza maisha ama kupata ulemavu wa kudumu kwasababu ugonjwa huo haukutambulika hivyo tunaokoa sauti yao kuona jamii na watoa huduma za afya wanatambua ugonjwa huo na wagonjwa wanapata tiba sahihi."

Tiba sahihi ni ghali sana na serikali haiwezi peke yake, hivyo lazima uwepo ushirikiano kutoka kwa sisi chama ambacho kina wataalamu na wadau wengine ili kuusemea ugonjwa huu, na tunaimani uwepo wako mheshimiwa waziri unafanya ugonjwa huu usemeke katika vyombo vya maaumuzi”, alisema Prof. Museru.

Akimkaribisha Mheshimiwa Waziri, Mkurugenzi wa Tiba na Elimu ya Afya Zanzibar, Dk. Marijani Msafiri alisema katika kipindi cha miaka minne, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar chini ya uongozi wa Dr. Hussein Ali Mwinyi imefanya mapinduzi makubwa katika kuboresha huduma za afya, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa hospitali 10 za wilaya na hospitali moja kubwa ya kisasa ya mkoa ya Lumumba.

Ndani ya hospitali hizi sasa tumeimarisha miundombinu na huduma, serikali yetu ya awamu na nane pia imeamua kufanya kazi na sekta binafsi ili kutoa huduma bora kwa wagonjwa wote ikiwa ni pamoja na wagonjwa wa himofilia, zikiwemo huduma za maabara, utoaji wa dawa na uendeshaji wa hospitali”, alisema Dk. Msafiri.
Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (katikati), akiagana na Mwenyekiti wa Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Dk. Stella Rwezaura, mara baada ya maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani iliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, Visiwani Zanzibar jana. Mstari wa chini ni baadhi ya watoto wanaougua ugonjwa wa himofilia.
Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Prof. Lawrence Museru (katikati), akiongoza maandamano kuadhimisha Siku ya Himofilia Duniani, Visiwani Zanzibar jana. Maadhimisho hayo yalifanyika pamoja na uzinduzi wa kliniki ya Himofilia katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, visiwani humo.
Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (kushoto), akipokea cheti cha shukurani, kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Dk. Stella Rwezaura, mara baada ya maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani, pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika hafla iliyofanyika kwenye Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, Visiwani Zanzibar, jana.
Mkazi wa Zanzibar, Baba mwenye watoto wawili wanaougua himofilia, Suleiman Ali Seif, akishiriki matembezi akiwa na watoto wake wenye ugonjwa huo, Murshin Ali (kulia), na Sahir Ali, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani, mjini Zanzibar jana. Maadhimisho hayo yaliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, yaliandaliwa na Chama cha Himofilia Tanzania (HST), kwa uwezeshaji kutoka Taasisi ya himofilia ya novo nordisk na Chama cha Himofilia Duniani. Himofilia ni ugonjwa wa damu kukosa uwezo wa kuganda unaosababishwa na ukosefu wa kiwango cha chembechembe za protini zinazotakiwa kugandisha damu hivyo kusababisha damu kuvuja kwa mda mrefu pindi mtu anavyopata jeraha hivyo kuhatarisha maisha yake.
Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (kushoto), akisalimiana na Mwenykiti wa Bodi ya Chama cha Himofilia Tanzania, Prof. Lawrence Museru, wakati akipokea maandamano, yaliyokuwa sehemu ya shamrashamra za maadhinisho ya Siku ya Homifilia Duniani, sambamba na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, mjini Zanzibar, jana.
Mmoja wa wadau wa himofilia, akipokea cheti cha shukurani, mara baada ya kukamilika kwa hafla ya maadhimisho Siku ya Homifilia Duniani, sambamba na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, mjini Zanzibar, jana.
Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (katikati), akiwa na wawakilishi kutoka Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Taasisi ya himofilia ya novo nordisk, Wizara za afya kutoka Tanzania na Zanzibar, Hospitali ya Taifa Muhimbili, Chama cha Himofilia Duniani na wadau wengine katika hafla ya maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani iliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, Visiwani Zanzibar jana.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive