A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Showing posts with label LOCAL. Show all posts
Showing posts with label LOCAL. Show all posts

Friday, June 13, 2025

UWT TANGA YAKUNWA NA UCHAPAKAZI WA MBUNGE UMMY MWALIMU

Na - Mwandishi Wetu, TANGA

Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) imempongeza Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini, Ummy Mwalimu, kwa uchapakazi na uwajibikaji wake wa kuwaletea wananchi maendeleo na namna anavyoilea Jumuiya hiyo muhimu kwa uhai wa Chama.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo wilaya ya Tanga, Bi. Moza Seif, katika Baraza lake la Kikanuni lililokaa Juni 12, 2025 katika Ukumbi wa CCM wilaya ya Tanga ambapo pamoja na mambo mengine, Baraza hilo lilikuwa na ajenda ya kusoma Utekelezaji wa Ilani kwa Madiwani wa Viti Maalum wa Jiji la Tanga.

Bi. Moza amempongeza Mbunge Ummy Mwalimu ambaye amekuwa bega kwa bega na Jumuiya hiyo katika kusukuma gurudumu la maendeleo ndani ya Jiji la Tanga. Katika kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazofanywa na Mbunge huyo, uongozi wa UWT Tanga ulimpatia Mbunge Ummy Mwalimu Zawadi mbalimbali za Pongezi ambazo zilipokelewa na Bi. Mwanahawa Mwalimu kwa niaba ya Mbunge.

Sambamba na hilo, Madiwani wa Viti Maalum wa Jiji la Tanga walisoma Utekelezaji wa Ilani ambapo kazi nyingi na miradi mingi ya maendeleo imefanyika katika kipindi cha uongozi wao. Aidha, wanachama wameaswa kuwa wamoja kuelekea Uchaguzi Mkuu Mwezi Oktoba, 2025 kwa kuepuka fitna, majungu na makundi.

Katika hatua nyingine, Baraza hilo lilihudhuriwa viongozi mbalimbali wa Chama wakiwemo Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga, Meja Mstaafu Hamisi Bakari Mkoba ambaye alikuwa Mgeni Rasmi pamoja na Katibu wa CCM wilaya ya Tanga, Jamal Khimji.
Share:

Friday, April 18, 2025

WATU 12,000 WAHOFIWA KUUGUA UGONJWA WA HIMOFILIA NCHINI

Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (katikati), akika utepe kuashiria uzinduzi wa kliniki ya himofilia, sambamba na maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani katika hafla iliyofanyika katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, Visiwani Zanzibar, jana. Pamoja naye ni wawakilishi kutoka Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Taasisi ya himofilia ya novo nordisk, Wizara za afya kutoka Tanzania na Zanzibar, Hospitali ya Taifa Muhimbili, Chama cha Himofilia Duniani na wadau wengine.

Na mwandishi wetu, Zanzibar.

TAKWIMU zinaonyesha kati ya watu elfu sita hadi elfu 12, wanahofiwa kuugua ugonjwa wa himofilia nchini huku idadi ya watu waliogundulika kuwa na ugonjwa huo hadi sasa wakiwa ni 451 pekee.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui katika hafla ya maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani iliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, Visiwani humo jana.

Hafla hiyo iliandaliwa na Chama cha Himofilia Tanzania (HST), kwa uwezeshaji kutoka Taasisi ya himofilia ya novo nordisk na Chama cha Himofilia Duniani kwa ushirikiano kutoka Serikali ya Tanzania na ya Zanzibar, wizara za afya kutoka pande zote mbili, Hospitali ya Taifa Muhimbili na wadau wengine.

Mheshimiwa waziri alisema takwimu za kidunia zinaonesha mtu mmoja kati ya 10 anapatikana na ugonjwa huo, hii ikimanisha kuwa Tanzania yenye watu takribani milioni 61 inaweza kuwa na wagonjwa elfu 6 hadi elfu 12, huku ikielezwa 97% ya watu wenye ugonjwa huu duniani kote hawajagundulika, ambapo kwa upande wa Tanzania waliogundulika mpaka sasa ni 451 tu.

Kama tunavyofahamu himofilia ni ugonjwa wa damu kukosa uwezo wa kuganda unaosababishwa na ukosefu wa kiwango cha chembechembe za protini zinazotakiwa kugandisha damu hivyo kusababisha damu kuvuja kwa mda mrefu pindi mtu anavyopata jeraha hivyo kuhatarisha maisha yake."

Maisha ya watu wenye matatizo haya yanahitaji uangalizi mkubwa na tahadhari kubwa ili kuzuia uvujaji wa damu, ulemavu na vifo hivyo kuwepo na hitaji la kubaini aina ya himofilia na kupata matibabu ya kuchomwa sindano yenye chembechembe za protini zinazokosekana mwilini ili kusaidia kuzalisha damu”, alisema Waziri Mazrui.

Alisema Mwaka 2020 Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ikishirikiana na Taasisi ya himofilia ya Novo Nordisk ilianzisha mradi wa kuongeza kasi ya upatikanaji wa huduma kwa watu wenye magonjwa ya damu lengo kuu ikiwa ni kuunga mkono serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya afya katika kupunguza madhara ya vifo vinavyotokana na magonjwa yasiyo ambukiza ikiwemo himofilia na selimundu.

Pamoja na hayo alisema, lengo kubwa la mradi huu ni kuwezesha upatikanaji wa vipimo vya wagonjwa wa damu, seli mundu, na himofilia katika hospitali za rufaa nchini sambamba na kuanzisha kliniki za magonjwa hayo, kuwezesha mafunzo na upatikanaji wataalamu wa afya waliobobea kwenye hospitali hizo pamoja na upatikanaji wa miundo mbinu sahihi, vipimo na dawa ili wagonjwa wahudumiwe mahali popote nchini bila kulazimika kufika Muhimbili.

Katika maadhimisho haya leo nina furaha kubwa kuwaambia kuwa mradi huu katika kipindi cha uhai wake kuanzia kipindi cha kwanza hadi kipindi cha pili tayari umefanikisha kukamilisha ukarabati wa kliniki za himofilia katika hospitali 13 zikiwemo hospitali za Muhimbili, KCMC, mbeya na Bugando."

Tunawashukuru pia wafadhili wetu kwa msaada wa dawa zenye thamani ya shs milioni 500, kwa kweli mmetusaidia sana na vifaa nyenye gharama kubwa, chini ya uongozi wa maraisi wetu, Samia Suluhu Hassan na Hussein Ali Mwinyi, tunaendelea kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kila mtanzania anapata matibabu kwa usahihi na kwa wakati, hivyo juhudi zenu hizi zinatufanya twende sambamba na juhudi za viongozi wetu hawa”, aliongeza waziri huyo.

Akizungumzia zaidi kuhusu himofilia, Mwenyekiti wa Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Dk. Stella Rwezaura alisema, asilimia 70 ya wagonjwa wa himofilia wanarithi na inabebwa katika kinasaba cha kike, kwani mwanamke ana ‘x’ mbili na mwanaume ana ‘xy’, hivyo endapo mwanamke ana ‘x’ yenye vinasaba vya himofilia, asilimia 50 ya watoto wake wa kiume watakuwa na tatizo hilo hivyo kufanya asilimia 99 ya wagonjwa wa himofilia kuwa wanaume.

Tunaposherehea Siku ya Himofilia Duniani, sambamba na Kauli Mbiu ya Mwaka 2025 isemayo, ‘Wanawake na Wasichana pia wanakumbwa na tatizo la kuvuja damu, licha ya himofilia kuwapata zaidi wanaume, tuwaite wanawake waje kupima, waweze kutambulika mapema hivyo kupata matibabu sahihi."

Lengo la mradi huu ni kuwatambua wagonjwa wengi zaidi na kupata huduma kwani wapo wengi wenye tatizo hili na hii ilitokana na changamoto ya uhaba wa vifaa, mashine na vitendanishi vya kutambua ugonjwa huu, hivyo kwa msaada wa wafadhili, vyama vya wagonjwa pamoja na serikali yetu sikivu ya Tanzania, ikiongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan pamoja Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi, wizara yake ya afya na wadau wengine, huduma hizi sasa zinafika karibu kwa wananchi kwa usahihi zaidi”, aliongeza Dk. Stella.

Naye mmoja wa wagonjwa wa Himofilia ambaye pia anauguza watoto wawili wenye ugonjwa huo, Regina Shirima alisema anakabiliwa na changamoto kubwa ya hali duni ya kiuchumi baada ya kutumia muda wake mwingi katika kuhudumia watoto hivyo kutokuwa na muda kabisa wa kujishughulisha na kazi za kujitafutia kipato.

changamoto nyingine ni kwa watoto wenyewe hawapati muda wa kusoma, kucheza na wenzao ama kuwa na furaha kwani muda mwingi wanakuwa wagonjwa, lakini ni ukweli kuwa wanawake ndio wanabeba vinasaba vya himofilia, lawama nyingi zinakuja kwetu kwa kuzaa watoto wenye changamoto hii, hivyo unajikuta familia imekuacha”. Akiongeza kuwa kuna wakati kulikuwa na changamoo ya upatikanaji wa dawa ukizingatia kuwa mgonjwa wa himofilia akikosa dawa tu anaweza uhai wake unakuwa hatarini.

Natoa wito kwa jamii kuwa gonjwa hili la himofilia lipo na mama sio anayesababisha mtoto kuzaliwa na ugonjwa huu, kwani huwezi kupata mtoto bila ya baba”, aliongeza Bi. Regina kwa mshangao.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Dk. Lawrence Museru alisema HST imekuwa sauti ya wenye ugonjwa wa himofilia katika kuangalia changamoto wanazopitia katika kutafuta tiba, moja ya changaoto ni utambuzi wa ugonjwa huu katika jamii.

Wagojwa wamekuja kutambulika baada ya kupoteza maisha ama kupata ulemavu wa kudumu kwasababu ugonjwa huo haukutambulika hivyo tunaokoa sauti yao kuona jamii na watoa huduma za afya wanatambua ugonjwa huo na wagonjwa wanapata tiba sahihi."

Tiba sahihi ni ghali sana na serikali haiwezi peke yake, hivyo lazima uwepo ushirikiano kutoka kwa sisi chama ambacho kina wataalamu na wadau wengine ili kuusemea ugonjwa huu, na tunaimani uwepo wako mheshimiwa waziri unafanya ugonjwa huu usemeke katika vyombo vya maaumuzi”, alisema Prof. Museru.

Akimkaribisha Mheshimiwa Waziri, Mkurugenzi wa Tiba na Elimu ya Afya Zanzibar, Dk. Marijani Msafiri alisema katika kipindi cha miaka minne, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar chini ya uongozi wa Dr. Hussein Ali Mwinyi imefanya mapinduzi makubwa katika kuboresha huduma za afya, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa hospitali 10 za wilaya na hospitali moja kubwa ya kisasa ya mkoa ya Lumumba.

Ndani ya hospitali hizi sasa tumeimarisha miundombinu na huduma, serikali yetu ya awamu na nane pia imeamua kufanya kazi na sekta binafsi ili kutoa huduma bora kwa wagonjwa wote ikiwa ni pamoja na wagonjwa wa himofilia, zikiwemo huduma za maabara, utoaji wa dawa na uendeshaji wa hospitali”, alisema Dk. Msafiri.
Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (katikati), akiagana na Mwenyekiti wa Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Dk. Stella Rwezaura, mara baada ya maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani iliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, Visiwani Zanzibar jana. Mstari wa chini ni baadhi ya watoto wanaougua ugonjwa wa himofilia.
Mwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Prof. Lawrence Museru (katikati), akiongoza maandamano kuadhimisha Siku ya Himofilia Duniani, Visiwani Zanzibar jana. Maadhimisho hayo yalifanyika pamoja na uzinduzi wa kliniki ya Himofilia katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, visiwani humo.
Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (kushoto), akipokea cheti cha shukurani, kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Dk. Stella Rwezaura, mara baada ya maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani, pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika hafla iliyofanyika kwenye Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, Visiwani Zanzibar, jana.
Mkazi wa Zanzibar, Baba mwenye watoto wawili wanaougua himofilia, Suleiman Ali Seif, akishiriki matembezi akiwa na watoto wake wenye ugonjwa huo, Murshin Ali (kulia), na Sahir Ali, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani, mjini Zanzibar jana. Maadhimisho hayo yaliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, yaliandaliwa na Chama cha Himofilia Tanzania (HST), kwa uwezeshaji kutoka Taasisi ya himofilia ya novo nordisk na Chama cha Himofilia Duniani. Himofilia ni ugonjwa wa damu kukosa uwezo wa kuganda unaosababishwa na ukosefu wa kiwango cha chembechembe za protini zinazotakiwa kugandisha damu hivyo kusababisha damu kuvuja kwa mda mrefu pindi mtu anavyopata jeraha hivyo kuhatarisha maisha yake.
Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (kushoto), akisalimiana na Mwenykiti wa Bodi ya Chama cha Himofilia Tanzania, Prof. Lawrence Museru, wakati akipokea maandamano, yaliyokuwa sehemu ya shamrashamra za maadhinisho ya Siku ya Homifilia Duniani, sambamba na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, mjini Zanzibar, jana.
Mmoja wa wadau wa himofilia, akipokea cheti cha shukurani, mara baada ya kukamilika kwa hafla ya maadhimisho Siku ya Homifilia Duniani, sambamba na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, mjini Zanzibar, jana.
Waziri wa Afya wa Zanzibar, Mhe. Nassor Ahmed Mazrui (katikati), akiwa na wawakilishi kutoka Chama cha Himofilia Tanzania (HST), Taasisi ya himofilia ya novo nordisk, Wizara za afya kutoka Tanzania na Zanzibar, Hospitali ya Taifa Muhimbili, Chama cha Himofilia Duniani na wadau wengine katika hafla ya maadhimisho ya Siku ya Himofilia Duniani iliyofanyika pamoja na uzinduzi wa Kliniki ya Himofilia, katika Hospitali ya Wilaya ya Ijitimai, Visiwani Zanzibar jana.
Share:

Wednesday, March 19, 2025

Benki ya Absa Tanzania na World Vision Tanzania Washirikiana Kuboresha Upatikanaji wa Maji katika Kijiji cha Kwedizinga

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa pili kushoto) na Mkurugenzi wa Miradi wa Shirika la World Vision Tanzania, Bi. Nesserian Mollel, wakisaini hati ya makubaliano jijini Dar es Salaam leo kwa ajili ya ushirikiano kwenye Mradi wa Maji katika Kijiji cha Kwedizinga, Wilaya ya Handeni mkoani Tanga. Benki ya Absa imetoa mchango wa TZS milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa kisima katika kijiji hicho kitakachowanufaisha wakazi zaidi ya 3,000, ambapo watoto wanawakilisha 55% ya idadi ya wakazi wa kijiji hicho.

Absa Bank Tanzania imetangaza ushirikiano wa kimkakati na Shirika la World Vision Tanzania ili kuboresha upatikanaji wa maji safi, usafi wa mazingira na watu katika kijiji cha Kwedizinga, Wilaya ya Handeni, Mkoa wa Tanga. Mpango huu unaonyesha dhamira ya Absa ya kuwawezesha jamii na kuwa chachu ya maendeleo chanya.

Kijiji cha Kwedizinga, ambacho kina vijiji vidogo saba na idadi ya watu takriban 4,000, kimekuwa kikikabiliwa na changamoto za kupata maji safi na salama. Hivi sasa, wakazi wanategemea mabwawa na mito ya msimu, hali inayosababisha ongezeko la magonjwa yanayotokana na maji na kuweka mzigo mkubwa kwa wanawake na watoto ambao mara nyingi husafiri zaidi ya kilomita 2 kila siku kutafuta maji.

Mradi huu unalenga kushughulikia changamoto hizi kupitia hatua kuu zifuatazo:

Uchunguzi wa Kihidrolojia na Uchimbaji wa Visima: Kufanya uchunguzi wa kina wa maji chini ya ardhi ili kubaini eneo linalofaa zaidi kwa ajili ya kisima chenye mavuno mengi, ikifuatiwa na uchimbaji hadi kina cha mita 180.

Mfumo wa Kusukuma Maji kwa Nguvu za Jua: Kufunga mfumo rafiki wa mazingira wa kusukuma maji kwa kutumia nishati ya jua ili kusafirisha maji kutoka kisimani hadi kwenye tanki la kuhifadhi lililoinuliwa.

Uhifadhi na Usambazaji wa Maji: Kujenga tanki la kuhifadhi maji lenye ujazo wa lita 50,000 na kuanzisha mtandao wa usambazaji maji wenye vituo vingi vya ukusanyaji, kuhakikisha kwamba vijiji vidogo vyote saba vinapata maji safi ndani ya mita 400, sambamba na viwango vya sera ya maji ya Tanzania.

Ushirikishwaji wa Jamii na Mafunzo: Kuunda na kutoa mafunzo kwa kamati ya watumiaji wa maji ili kusimamia mfumo wa usambazaji maji, kukuza mbinu endelevu, na kufanya uhamasishaji wa jamii kuhusu usafi wa mazingira na usafi binafsi.

Mpango huu unalingana na Malengo kadhaa ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa, ikiwemo SDG 3 (Afya Bora na Ustawi), SDG 4 (Elimu Bora), na SDG 6 (Maji Safi na Usafi wa Mazingira). Pia unaunga mkono Awamu ya 3 ya Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Maji ya Tanzania (2022/2025), ambao unalenga kuwaunganisha mamilioni ya watu na vyanzo vipya na vilivyoboreshwa vya maji.

Absa Bank Tanzania imejitolea TZS 50,000,000 kuwezesha mradi huu, ikionyesha dhamira ya benki ya kuiwezesha Afrika ya Kesho, pamojaz, hatua moja baada ya nyingine.

Akizungumza katika hafla ya utiaji saini, Bw. Obedi Laiser, Mkurugenzi Mtendaji wa Absa Bank Tanzania, alisisitiza dhamira ya benki ya kuwa chachu ya maendeleo chanya katika jamii wanazofanya kazi: "Katika Absa, tunaamini kwamba kila story ina umuhimu. Ushirikiano huu ni ushahidi wa lengo letu la kuiwezesha Afrika ya Kesho, pamoja, hatua moja baada ya nyingine. Kwa kutoa upatikanaji endelevu wa maji safi katika kijiji cha Kwedizinga, hatuboreshi tu afya na usafi wa mazingira, bali pia tunashughulikia masuala ya utofauti na ujumuishaji, fursa za kielimu, na kuwezesha ukuaji wa kiuchumi."

Bi. Nesserian Mollel, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa World Vision Tanzania, pia alitoa maoni kuhusu ushirikiano huo: "World Vision imejitolea kufanya kazi na jamii kuleta maendeleo. Ushirikiano huu na Absa Bank Tanzania unaonyesha dhamira yetu ya kukuza mabadiliko ya kibinadamu. Pamoja, tunahakikisha kwamba watoto na familia katika kijiji cha Kwedizinga wanapata moja ya mahitaji ya msingi ya maisha - maji safi."

Mradi unatarajiwa kunufaisha moja kwa moja wakazi wote 3,890 wa kijiji cha Kwedizinga na kuwanufaisha kwa namna tofauti watu wengine 596 kutoka vijiji jirani, hatua muhimu kuelekea kuboresha afya, elimu, na matokeo ya kiuchumi katika eneo hilo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa tatu kushoto) akibadilishana hati ya makubaliano ya ushirikiano na Mkurugenzi wa Miradi wa Shirika la World Vision Tanzania, Bi. Nesserian Mollel, jijini Dar es Salaam leo, ambapo kupitia makubaliano hayo Benki ya Absa imetoa mchango wa TZS milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa kisima cha maji kitakachowanufaisha wakazi zaidi ya 3,000 wa Kijiji cha Kwedizinga, Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga ambapo watoto wanawakilisha 55% ya idadi ya wakazi wa kijiji hicho.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (katikati), Mkurugenzi wa Wateja wa Makampuni wa Absa Tanzania, Bi. Nellyana Mmanyi na Mkurugenzi wa Miradi wa Shirika la World Vision Tanzania, Bi. Nesserian Mollel wakifurahi jijini Dar es Salaam leo, muda mfupi mara baada ya kusaini hati ya makubaliano, kwa ajili ya ushirikiano katika Mradi wa Maji kwenye Kijiji cha Kwedizinga, Wilaya ya Handeni mkoani Tanga.
Share:

Wednesday, March 12, 2025

"Stori za Afya za Wanawake wa Tanzania zina thamani kwetu", Absa Bank

Baadhi ya Wafanyakazi Wanawake wa Benki ya Absa Tanzania kupitua umoja wao uitwao ‘Red Skirts’ wakiwa katika picha ya pamoja na madaktari pamoja na wagonjwa katika Hospitali ya CCBRT, baada ya kukabidhi msaada wa vifaa tiba kwa ajili ya wagonjwa wa fistula kama sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, hospitalini hapo mwishoni mwa wiki.
Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya Absa wakibeba msaada wa vifaa vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti), kab;la hawajavikabidhi katika Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.

Meneja Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Anna Chacha (wa saba kushoto) akikabidhi msaada wa vifaa tiba na vifaa muhimu vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti) katika Hospitali ya Muhimbili kwa Mkuu wa Kitengo cha Watoto Wachanga, Dk. Martha Mkony, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Lilian Swere (kulia) akikabidhi msaada wa vifaa tiba kwa Mkuu wa Ubora na Huduma kwa Wateja wa Hospitali ya CCBRT, Bi. Emelda Lwena, kwa ajili ya wagonjwa wa fistula, kwenye jengo la mama na mtoto la hospitali hiyo, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

WATOTO wanaozaliwa na changamoto mbalimbali katika Hospitali ya Muhimbili, sasa wanaweza kupata ahueni zaidi mara baada ya wafanyakazi wanawake wa Benki ya Absa Tanzania, kukabidhi msaada wa vifaa tiba na vifaa muhimu vya kusaidia watoto hao wanazaliwa kabla ya kufika wakati wa kujifungua.

Akizungumza wakati akipokea vifaa hivyo, Mkuu wa Kitengo cha Watoto Wachanga katika hospitali hiyo, Dk. Martha Mkony alitoa shukrani kwa wafanyakzi hao ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Wanwake Duniani alisema msaada huo umekuja kwa wakati muafaka kwani utasaidia sana watoto wanaozaliwa kila siku katika hospitali hiyo.

Nipende kuwashukuru sana wanawake wa Benki ya Absa kwenye kundi lao wanalojiita ‘Red Skirts’ kwa tendo hili la kijamii, na tunajua hii ni mwanzo wa mahusiano marefu kati ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha watoto wachanga pamoja na Benki ya Absa na tunaahidi kushikiriana kwa pamoja katika kuwahudumia watoto wachanga”, alisema Dr. Marha.

Akizumgumza wakati akibidhi vifaa hivyo, Meneja katika Kitengo cha Rasilimali Watu wa Benki ya Absa, Bi. Martha Chacha alisema, kwa kuthamini mchango wa wanawake katika maendeleo ya Taifa, pamoja na changamoto mbalimbali zinazowakabili, wanawake wa Benki ya Absa Tanzania, kupitia umoja wao wa ‘Red Skirt’ walikwenda kutoa misaada kwa wagonjwa wa fistula katika Hospitali ya CCBRT pamoja na kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Muhimbili.

Kwa niaba ya wanawake wenzangu tupo mahali hapa tukiwakisha benki yetu kutoa misaada hii, Benki ya Absa inajali Story za Wanawake wa Tanzania, Story za mafanikio ya kiafya na kiuchumi kwa wanawake zina umuhimu sana kwetu”, aliongeza Bi. Anna
Share:

Friday, January 24, 2025

FEZA BOYS YANG'ARA UFAULU WA KIDATO CHANNE WAPATA ALAMA A,,

SHULE Sekondari Feza Boys imejivunia uwekezaji iliyofanya katika kumuandaa mwanafunzi kuwa bora baada ya kufaulisha wanafunzi wote kwa kupata daraja la kwanza katika mtihani wa Taifa wa kidato cha nne ulifanyika mwaka 2024, huku zaidi ya asilimia 65 wakipata division 1.7.

Hayo ameyasema Makamu Mkuu wa Shule ya FEZA Boys, Shabani Mbonde wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 23,2025 katika shule hiyo iliyopo Kunduchi Dar es Salaam mara baada ya Baraza la Mitihani kutangaza matokeo ya kidato cha nne.

Mbone ameleeza kuwa matokeo hayo hajatokea tu kirahisi bali ni uwekezaji na mazingira ya shule yanayomtengeza mwanafunzi kuwa bora na walimu wa kutosha ambapo kila mwalimu ana wastani ya kufundisha wanafunzi 10.

" FEZA SHOOLS haitoi mwanafunzi bora katika A tu, bali katika nyanja zote.Sisi katika elimu hatumjengi mwanafunzi kupata A tu lakini pia katika kukabiliana na hali zote katika maisha kulingana na wakati uliopo.

"Hii yote inatokana na jitihada mbalimbali za wanafunzi wenyewe na walimu. Mwanafunzi wetu anakuwa ni kama ametoka kwenye mashine au kiwanda kilichomjenga katika kupambana na changamoto mbalimbali katika mtihani na maisha.Tunajivunia wanafunzi wetu na walimu wetu," amesema Makamu Mkuu huyo.

Aidha Mbonde amesema kama sekta binafsi wanashukuru serikali kwa kusisitiza suala la elimu na wanaiunga mkono Serikali katika kuhakikisha elimu inakuwa bora.

Naye Mkuu wa taaluma msaidizi wa kidato cha tatu na nne, Abdallah Juma ameeleza mbinu wanazotumia kuwafundisha wanafunzi hao kuwa ni progamu mbalimbali walizonazo shuleni hapo.

" Sio kwamba sisi vijana wote tunaowachukua ni wale 'cream' tu bali wanakuja hata wenye uwezo mdogo tunawatengeneza na wanakiwa sawa na wenzao na wanafaulu kwa pamoja.

" Matokeo haya yamepatikana kwa njia tofauti, pande zote tatu zina mchango yaani wazazi, walimu na wanafunzi, pia tuna programu mbalimbali za masomo kuanzia asubuhi, jioni na hata usiku, pia wanapata muda wa kucheza", amesema.

Kwa upande mmoja wa wanafunzi wa FEZA BOYS waliofanya vizuri kwa kupata division one 1.7, Moses Francis, amesema anamshukuru Mungu kwani mafanikio hayo hayakuja kirahisi ya kupata A masomo yote 10 ila mazingira ya shule yamechangia ikiwamo kusoma kwa bidii kama mwanafunzi.

Amefafanua kuwa kutokana na ratiba za shule zilivyopangiliwa wanapata muda wa kutosha wa kupumzika lakini kuna kipindi kigumu unatakiwa kusoma sana ili kufaulu mtihani.

"Hii haipatikani kirahisi, mtu kufaulu lazima kuwe na motisha kuanzia kwa mwanafunzi wenyewe na mzingira mazuri ya kujifunzia pamoja na kumtanguliza Mungu.Kila wiki tunafanya mazoezi ya masomo kwa kufanya test," amesema Moses.

Katika matokeo ya kidato cha nne yaliyotangazwa leo na Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), ufaulu umeongezeka ambapo jumla ya watahiniwa wa shule 477,262 kati ya 516,695 wenye matokeo sawa na asilimia 92.32 wamefaulu kwa kupata madaraja ya I,II,III,IV.

Makamu mkuu wa shule ya sekondari ya Feza Boys ,Shabani Mbonde akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutangazwa matokeo ya kidato cha nne na shule hiyo kupata ufaulu wa alama A kwa wanafunzi waoote kwenye atokeo ya kidato cha nne.Kulia ni mmoja ya mwanafunzi aliyepata ufaulu wa A. Mosses Mwaijande na Kushoto ni Mtaalumu Abdalla Juma
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Feza Boys wakishangilia kwa kumbeba mwanafunzi mwenzao,Allan Masaka aliyefanya viziuri katika matokeo ya kidato cha nne kwa kupata ufaulu wa alama A.7 jumla ya wanafuzi woote katika shule hiyo wamepata ufaulu wa alama A .Na,mpiga picha maalumu
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Feza Boys wakishangilia kwa kumbeba mwanafunzi mwenzao,Moses Mwaijande aliyefanya viziuri katika matokeo ya kidato cha nne kwa kupata ufaulu wa alama A.7 jumla ya wanafuzi woote katika shule hiyo wamepata ufaulu wa alama A
Share:

Wednesday, September 11, 2024

TUME YA SAYANSI YA TEKNOLOJIA YAANZISHA MFUMO KUWASAIDIA WASICHANA NA WANAWAKE KIDIJITALI

KATIKA kuwasaidia Wasichana na Wanawake kumudu maisha na kuisaidia jamii Tume ya Sayansi na Teknolojia ( Costech), imezindua Program mbili kwa ajili ya kuwajengea uwezo kidijitali.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 10, 2025 jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Costech, Dkt. Amos Nungu amesema kuwa Program hizo ni kwa ajili ya wasichana ambao hawakumaliza masomo yao na Wanawake wenye mawazo au biashara zinazohusiana na Teknolojia.


Lengo ni kuwapa ujuzi na taaluma ya kiteknolojia ili waweze kuja na biashara ambazo zinaweza zikasaidia waweze kumudu maisha yao, na wasaidie jamii.


Dkt. Nungu amesema Program ya kwanza inajulikana kama 'Future Femtech' inayowasaidia wanawake wenye kampuni changa au mawazo machanga ya kiteknolojia.


Amesema Program ya pili ijulikanayo kama 'Kuzatech' inaangalia mabinti ambao walikuwa shule lakini kwa namna moja au nyingine wakashindwa kuendelea na masomo hivyo wamewapa fursa ya kupata mafunzo kidijitali.


"Sasa hizi Program mbili tunazifanya kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo,"amesema.


Nungu amesema Kuzatech wataunganika na Future Femtech ambao baadhi yao ni wahitimu wa vyuo vikuu wenye mawazo ya biashara ambapo wadogo wanapata fursa ya kuungana na hawa wakubwa ili waweze kupata mafunzo yatakayowasaidia kuwa nankitu cha kufanya.


Kwa upande wake Meneja Usimamizi na Uhaulishaji Teknolojia Costech, Dkt. Erasto Mlyuka amesema Program hiyo ya Future Femtech inawalenga wasichana ambao wamekuwa ni waanzilishi wa kampuni changa.


Amesema hupewa msaada wa kitaalam kwa maana ya mafunzo elekezi ya kujengewa uwezo pia kupewa fedha za kuwawezesha kufanya biashara zao.


Amesema program hizo zitatengeneza ajira kwa wanawake ili na wenyewe wapate nafasi ya kuchangia kwenye pato la nchi kwa kuwa na kipato halali.


Mbunifu kutoka Arusha, ambaye ni mnufaika wa Future Femtech, Pamela Chogo amesema mafunzo aliyoyapata ni chachu kubwa kwenye ubunifu wa biashara.


Amesema Program hizo ni muhimu kwa sababu zinasaidia kupata elimu ya ujasiriamali.
Share:

Monday, August 5, 2024

USAID Technical Adviser visits beneficiaries of USAID Afya Yangu Southern and USAID Kizazi Hodari Southern projects.

The United States Agency for International Development (USAID) Technical Adviser Sarah Dastur pictured with some pupils of the JJ Mungai Primary in Iringa who are beneficiaries of the USAID Kizazi Hodari (Brave Generation) Southern Zone Project when she made a visit to inspect the project beneficiaries over the weekend.

Iringa Monday 5 August 2024 - The United States Agency for International Development (USAID) Technical Adviser Sarah Dastur conducted a joint visit to the USAID Afya Yangu (My Health) Southern and USAID Kizazi Hodari (Brave Generation) Southern Zone projects in Iringa. This visit involved representatives from USAID Tanzania and Washington. The visit assessed and supported ongoing Orphans and Vulnerable and Children (OVC) and pediatric HIV/TB activities, showcasing collaborative efforts between the projects to improve health outcomes in the region. The two projects are both implemented by Deloitte Consulting Limited aiming at improving the health status of the thriving youth, children and communities.

The USAID Technical Adviser Sarah Dastur visited JJ Mungai Primary School within Iringa Municipal, Isakalilo center which cares for children living with HIV and Tosamaganga hospital which has been provided care and counselling for people living with HIV.

During the visit, beneficiaries of the projects commented USAID for coming up with the projects that helped Tanzanians especially low-income earners saying that the projects has brought back smiles to them.

One of the project beneficiaries, Omary Juma (not his real name) who has been diagnosed with HIV and burdened by financial hardships said the project has really helped to bring back his smile. ‘My health has well improved through this project comprehensive support which includes health monitoring and education about reproductive health and HIV/Aids’, said Juma.

He added, ‘The project has helped me a lot. I learned most things from my community care workers and that has changed my life. I now have hopes with my life and I can now accomplish my dreams. I feel happy and courageous.

Speaking after visiting the beneficiaries, the USAID Technical Adviser Sarah Dastur said ‘Our commitments are aligned with the Government of Tanzania strategic priorities which involves close collaboration with Ministry of Health, Ministry of Community Development, Gender, Women and Special Groups and the President’s Office-Regional Administration and Local Government (PO-RALG)’.
Dr Stella Mtera (left) who is the CTC in charge of Tosamaganga Hospital in Iringa, listens to the United States Agency for International Development (USAID) Technical Adviser Sarah Dastur when she made a visit to inspect beneficiaries of the USAID Afya Yangu (My Health) Southern Project over the weekend.
Share:

Friday, August 2, 2024

UINGEREZA KUENDELEA KUFADHILI MIRADI YA UKIMWI NCHINI

Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. David Concar, akikabidhi cheti kwa mmoja wa washiriki wenye umri mdogo wa Kampeni ya kupanda mlima kilimanjaro ya GGM Kili Challenge, Regina Enos Baraka (kulia), mara baada ya kumaliza zoezi la kupanda na kushuka mlima huo, mjini Moshi, Kilimanjaro, hivi karibuni. Kampeni hiyo ya kila mwaka ina lengo la kusaidia miradi inayojikita katika kutokomeza VVU na Ukimwi imendaliwa na Kampuni ya Dhahabu ya Geita Gold Mining kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) ambapo jumla ya wapanda mlima 48 na waendesha baisketi 23 walishiriki. Regina anaishi katika Kituo cha Moyo wa Huruma cha Geita kilichoanzishwa kwa msaada kutoka Mfuko wa Kili Challenge.

Balozi wa Uingereza nchini, Mhe. David Concar amesema nchi yake itaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya Tanzania katika kupambana na ugonjwa wa Ukimwi Ili kutimiza malengo ya Kimataifa ya muda wa kati na mrefu ili kuona hakuna maambukizi mapya, unyanyapaa na vifo vinavyohusiana na VVU .

Balozi Concar aliyasema hayo wakati wa mapokezi ya wapanda mlima Kilimanjaro 71 walikuwa wakishiriki Kampeni ya kila mwaka ya GGM Kili Challenge mjini Moshi, Kilimanjaro, inayoandaliwa na Kampuni ya Dhahabu ya Geita Gold Mining kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Kupambana na Ukimwi (TACAIDS)

Njia kuu ambayo Uingereza inafanya ni kuwa mmoja wachangiaji wakubwa wa Mfuko wa Kimataifa wa kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria, kwa miaka mitatu kutoka 2024 hadi 2026, Uingereza itatoa pauni bilioni 1 kwa mfuko huo, ambao kwa jumla utatoa dola milioni 602 kwa Tanzania."

Nitoe pongezi kwa AngloGold Ashanti na Bodi ya Wadhamini ya Geita Gold Mining Limited Kilimanjaro Challenge dhidi ya HIV/AIDS pamoja na TACAIDS kwa kuifanya Kili Challenge kuwa tukio la kila mwaka la kupendeza likileta ujumbe wa nguvu kwa wanaoishi na VVU”, alisema.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mwakilishi ukutoka Geita Gold Mining, Mhandisi Nzuamkende alisema kampeni hiyo inayofanyika Kwa mwaka wa 22, inalenga kukusanya fedha kuchangia jitihada za Serikali ya Tanzania kufikia malengo ya sifuri tatu ( Maambukizi mapya Sifuri, Unyanyapaa Sifuri na vifo vinavyohusiana na UKIMWI Sifuri).

Tunapokusanyika hapa ili kusherehekea mafanikio yenu, ninatoa shukrani zangu za dhati kwa kila mmoja wenu kwa kukabiliana na hofu zenu, na kushinda mojawapo ya milima mirefu zaidi na yenye changamoto duniani."

Juhudi zenu, kwenye miteremko ya Mlima Kilimanjaro na kwenye njia tambarare za baiskeli, hazijadhihirisha tu nguvu ya uamuzi na umoja lakini pia zimeleta athari kubwa katika dhamira yetu ya pamoja ya kupambana na VVU na UKIMWI, mmetuonyesha kwamba hakuna changamoto isiyoweza kuzuilika tunapokutana kwa sababu moja na kwa hilo, nawapongeza nyote”, alisema.

Aidha aliwashukuru wafadhili na washiriki wote kutokana na michango yao inayoendelea kufanikisha Kampeni hiyo hadi kuufanya Mfuko wa Kili Challenge Against HIV/AIDS Trust kuwa mfuko wa kimataifa, unaohusisha wapanda mlima na waendesha baiskeli kutoka mabara yote na zaidi ya nchi 20.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TACAIDS, Dk. Jerome Kamwela alisema Tanzania inafanya vizuri kueleka malengo ya kimataifa ya muda mrefu na wa kati ambayo ni kufikia 95 tatu kufikia mwaka 2025 ambazo kama tawimu za karibuni zinavyoonesha kuwa kuna watu milioni 1.7 wanaishi na VVU, hivyo 95 ya kwanza ni kuona watu hao wanatambuliwa na kujua hali zao ambapo sasa imefika asilimia 83, huku 95 ya pili ni wale wanaoishi na VVU watumie dawa za kufubaza makali ya ukimwi (ARV) ambapo Tanzania imevuka lengo kwa kufikisha asilimia 98 na 95 ya tatu wale wanaotumia ARV asilimia 95 wawe wamefubaza virusi, utafiti wa mwisho unaonyesha maambukizi mapya yakipungua.

Nao baadhi ya washiriki wenye umri mdogo waliopanda Mlima Kilimanjaro, Regina Baraka na Baraka Erasto, kutoka kituo cha Moyo wa Huruma cha mkoani Geita, kilichoanzishwa kupitia mfuko wa Kili Challenge walielezwa kufurahishwa kwa uzoefu walioupata Kwa mara ya kwanza wakipanda mlimani hivyo kutoa hamasa Kwa vijana wadogo wenye umri kama wao kujitokeza kushiriki katika Kampeni hiyo Ili kuweza kuleta mabadiliko kwa wenye VVU.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. David Concar, akikabidhi cheti kwa mmoja wa washiriki wenye umri mdogo wa Kampeni ya kupanda mlima kilimanjaro ya GGM Kili Challenge, Baraka Erasto (kulia), mara baada ya kumaliza zoezi la kupanda na kushuka mlima huo, mjini Moshi, Kilimanjaro, hivi karibuni. Kampeni hiyo ya kila mwaka ina lengo la kusaidia miradi inayojikita katika kutokomeza VVU na Ukimwi imendaliwa na Kampuni ya Dhahabu ya Geita Gold Mining kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) ambapo jumla ya wapanda mlima 48 na waendesha baisketi 23 walishiriki. anaishi katika Kituo cha Moyo wa Huruma cha Geita kilichoanzishwa kwa msaada kutoka Mfuko wa Kili Challenge.
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. David Concar, akihutubia katika hafla ya kuwapokea wapanda mlima Kilimanjaro waliokuwa wakishiriki kampeni ya kila mwaka ya GGM Kili Challenge yenye lengo la kusaidia miradi inayojikita katika kutokomeza VVU na Ukimwi. Kampeni hiyo imendaliwa na Kampuni ya Dhahabu ya Geita Gold Mining kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) ambapo jumla ya wapanda mlima 48 na waendesha baisketi 23 walishiriki zoezi hilo lilioanza Julai 19 kufikia tamati yake mjini humo hivi karibuni.
Share:

Saturday, July 20, 2024

MADEREVA BODABODA TANGA WASHUKURU JESHI LA POLISI KWA KUTOA ELIMU KUHUSU USALAMA BARABARANI.

Na Mwandishi Wetu,Tanga

KAMANDA wa Polisi , Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Tanga ACP Bernard Zacharia amewataka madereva bodaboda katika Mkoa huo kuwa  mfano wa kuigwa na mabalozi wazuri wa kutii bila shuruti sheria za salama barabarani ili kuhakikisha wanakuwa salama wao na abiria zao.
Akizungumza na madereva bodaboda 204 waliohitimu mafunzo ya elimu ya usalama barabarani wilayani Tanga ,Kamanda Zacharia amesisitiza Jeshi la  Polisi linawahimiza watii sheria bila shuruti huku akiwashukuru Ubalozi wa Uswiss na Amend kwa ushirikiano wao na Jeshi la polisi kwa kuwaangalia vijana kwa ukaribu na kuwapatia mafunzo hayo.

"Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani tunafahamu kuwa bodaboda wamekua sehemu kubwa ya urahisishaji kwa abiria na mali zao,hivyo mafunzo waliyoyapata madereva bodaboda hao wa Wilaya ya Tanga na maeneo mengine ya mkoa huo yatawasaidia wao na abiria wao kuwa salama.

Amesema kwa Wilaya ya Tanga madereva bodaboda maarufu maofisa usafirishaji 204 wamehitimu mafunzo ya msasa ya usalama barabarani na kusisitiza waliopatiwa mafunzo wahakikishie wanakuwa.mabalozi kwa madereva wengine.Pia amesema anafahamu Kuna madereva bodaboda wengi waliofikiwa na mafunzo hayo katika Mkoa wa Tanga.

"Tunatarajia bodaboda Mkoa wa Tanga mtakua mfano wa kuigwa na mtakuwa mabalozi wazuri.Jeshi la Polisi linawahimiza kutii sheria bila shuruti na tunawashukuru Ubalozi wa Uswiss na Amend kwa ushirikiano huu na Jeshi la polisi kwa kuwaangalia vijana kwa ukaribu huu."

Kwa upande wake Mratibu wa Shirika la Amend Ramadhan Nyanza amesema wanaishukuru Serikali inayoongozwa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kushirikiana kwa karibu na mashirika yasio ya kiserikali kuzifikia jamii. 

"Katika kipindi cha mwaka mmoja kwa ufadhili wa Ubalozi wa Uswiss nchini ,- Shirika la Amend kwa kushirikiana na wadau mbalimbali tumefanikiwa kutoa mafunzo kwa vijana zaidi ya 900 kwa mkoa wa na Tanga na Dodoma."
Share:

Sunday, June 16, 2024

WAZIRI WA AFYA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA KIDO BALOZI WA KAMPENI YA HOLELA-HOLELA ITAKUKOSTI

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu akipokea Zawadi kutoka kwa KIDO ambaye ni balozi wa kampeini ya Holela-Holela itakukosti mara baada ya kukutana na kufanya mazungumzo leo Jijini Dodoma. Kampeni ya Holela-Holela Itakukosti inazingatia udhibiti kuhusu usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA) na magonjwa ya kipaumbele ya zuonotiki (magonjwa ambayo yanaweza kuambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa wanadamu) na inaratibiwa na ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Wizara ya Mazingira, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, na Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID). Kampeni ya Holela-Holea Itakukosti inasisitiza mbinu kamilifu ya “Afya Moja" kushughulikia tatizo la UVIDA na magonjwa ya zuonotiki. Holela-Holela ilizinduliwa mwishoni mwa mwezi uliopita ikiwa ni ushirikiano ya Ofisi ya Waziri Mkuu Wizara ya Afya, Wizara ya Mazingira, Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID).

Dodoma Jumamosi 15 Juni 2024

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu leo amekutana na kufanyia mazungumzo na KIDO ambaye ni balozi wa kampeni ya Holela-Holela itakukosti. Kampeni ya Holela-Holela itakukosti inasisitiza mbinu kamilifu ya "Afya Moja" kushughulikia tatizo la UVIDA na magonjwa ya zuonotiki na ilizinduliwa Jijini Dar es Salaam mwishoni mwa mwezi uliopita kwa uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana Wizara ya Afya, Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Wizara ya Mazingira huku ikifadhaliwa na Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) kupitia mradi wa Breakthrough ACTION.

Akizungumza leo Jijini Dodoma baada ya kufanyia mazungumzo na balozi KIDO, Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alisisitiza juu ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA) na magonjwa ya kipaumbele ya zuonotiki (magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu) ambayo kampeini ya Holela-Holela Itakukosti imelenga. ‘Naomba nichukue fursa hii nitoe wito kwa jamii kuwa Mtanzania anaweza kufanya mambo machache tu kukabiliana na UVIDA, kama vile kupata na kufuata ushauri wa mtaalamu wa afya kabla ya kutumia dawa, kutumia dozi ya dawa kikamilifu kama unavyoshauriwa na mtaalam wa afya, kufuata maelekezo ya mtaalam wa mifugo/kilimo juu ya matumizi sahihi ya dawa kwa mifugo/mimea, na kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni na usafi wa mazingiria kwa ujumla’.

Waziri Ummy aliongeza, ‘Suala la UVIDA ni tatizo kubwa sana, na athari zake ni kama vile ugonjwa kujirudia rudia na kuchukua muda mrefu kupona, kuenea na kusambaa kwa vimelea sugu vya magonjwa dhidi ya dawa, ulemavu na hata kifo. Mbali na hapo kuna athari za kiuchumi kama vile kutumia gharama kubwa kwenye matibabu, hivyo kupungua kwa pato binafsi, la familia na taifa’.

Waziri Ummy alisema kuwa Serikali inafanya jitihada kabambe za kukabiliana na UVIDA, ikiwemo kuzindua kampeni ya “Holela Holela itakukosti”, inayolenga kuongeza uelewa juu ya UVIDA na kuleta mabadiliko chanya ya tabia ili kukabiliana na UVIDA katika jamii. Pamoja na kampeni hiyo upo mpango kazi wa mapambano ya UVIDA (NAP AMR 2023-2028), na kamati ya Taifa ya Mapambano ya UVIDA (AMR MCC) inayofanya kazi chini ya mwamvuli wa Afya moja. Vilevile kuna miongozo mbalimbali ya Kisekta inayosaidia katika mapamabano ya UVIDA

Kwa Upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa USAID nchini Tanzania Alex Klaits alisisitiza umuhimu wa juhudi za pamoja, akisema, "Kampeni inaonyesha jukumu muhimu la ushirikiano katika kuleta athari chanya na kuhakikisha uendelevu wa muda mrefu, ikiwaleta pamoja wadau wa Afya moja kutoka sekta mbalimbali kupambana na UVIDA na magonjwa ya zuonotiki.
Share:

Thursday, May 30, 2024

WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI TANGA WAFURAHIA KUJENGEWA VIVUKO VYA WAENDA KWA MIGUU.

  


Na Mwandishi Wetu,Tanga

KATIKA jitihada za kupunguza ajali za barabarani kwa wanafunzi jijini Tanga ,Shirika la Amend kwa kushirikiana na Ubalozi wa Uswis wamefanikiwa kuweka miundombinu salama barabarani yenye lengo la kuhakikisha wanafunzi wanavuka salama katika safari ya kwenda na kurudi shuleni.

Miundombinu hiyo salama ya barabara imefanyika katika Shule ya Msingi Makorora pamoja na Shule ya Msingi Azimio kwa kuwekewa vivuko vya Pundamilia, njia za watembea kwa miguu pamaja na alama muhimu za usalama barabarani.

Akizungumza kuhusu mradi huo wa miundombinu salama ya barabara, Mkurugenzi wa Shirika la Amend Tanzania Simon Kalolo amefafanua mradi huo umehusisha ujenzi wa njia za watembea kwa miguu, vivuko 4 vya pundamilia, matuta saba ya kupunguza mwendo kasi, alama 15 za barabarani, na michoro 16 ya usalama barabarani.

Pia wametoa elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi 1,694 na walimu wa shule za msingi Makorora na Azimio ndani ya mwezi tano, 2024 Tanga na Tanzania kwa ujumla.

Kalolo amesema mpango wa kuboresha miundombinu salama ya watembea kwa miguu ni sehemu ya mradi wa mwaka mmoja unaoitwa "Usalama wa Pikipiki kwa Vijana Tanzania".

Amesisitiza mradi huo unaungwa mkono na Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania na una bajeti ya Sh. 424,983,396 huku akifafanua tangu Septemba 2023, shughuli nyingine za mradi zimejumuisha mafunzo ya waendesha pikipiki 300 jijini Tanga, waendesha pikipiki 253 Dodoma.

Pia kampeni a uhamasishaji kuhusu masuala ya usalama wa pikipiki, na kuanzishwa kwa 'Kanuni za Maadili' kwa madereva, Waendesha pikipiki 200 zaidi watapewa mafunzo jijini Tanga ifikapo Juni 2024 na tathmini ya athari za shughuli hizo zote inafanywa hivi sasa.

“Ajali za barabarani ndiyo chanzo kikuu cha vifo vya watoto na vijana wenye umri kati ya miaka 5 na 29 duniani kote nchini Tanzania na kuna zaidi ya majeruhi 330,000 wa ajali za barabarani kwa mwaka ambayo ni ya juu kuliko wastani katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara”amesema.

Amesema mradi huo wa kuokoa maisha unaonesha ajali za barabarani zinaweza kuzuilika kazi hiyo iliyoungwa mkono na Fondation Botnar na sasa Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania, itaendelea kupunguza ajali za barabarani na kuokoa maisha.

Ameongeza kupitia Mpango Kazi wao wa Usafiri Salama na Endelevu kwa Jiji la Tanga, wanalenga kuhakikisha kila mtoto wa Tanga anakuwa na safari salama ya kwenda na kurudi shuleni.

“Hakuna sababu ya kuchelewa kuchukua hatua hili linahitaji kuwa kipaumbele cha juu kwa watunga sera wetu na Tanga ina uwezo wa kuongoza nchi na bara letu katika kukabiliana na chanzo hiki kikibwa cha vifo kwa vijana,”alisema

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Wilaya ya Tanga Dalmia Mikaya aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Tanga James Kaji , amepongeza kutekelezwa kwa mradi huo wa miundombinu ya barabara katika Shule hiyo Makorora na Azimio na matamio yao ni kuona mradi wa usalama barabarani unakwenda katika shule zote za Tanga.

Pia amewaomba wazazi na walezi kuhakikisha wanawalinda wanafunzi dhidi ya vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia.Tunafahamu suala la usalama barabarani ni muhimu lakini tuweke nguvu kusimamia usalama dhidi ya ukatili wanaofanyiwa katika jamii zetu.”

Kwa upande wake Mwakilishi wa Ubalozi wa Uswisi Rashid Mbaramula ambaye anashughulikia Miradi amesema nchi Uswis inahistoria kubwa wa kimahusiano na Tanzania na Jiji la Tanga ni miongoni mwao huku akifafanua kuanzia mwaka 1960 Uswis imekuwa mdau mkubwa wa maendeleo na imekuwa ilishiriki kikamilifu katika kufanikisha Miradi ya maendeleo.

Amesema kupitia mradi huo madereva bodaboda zaidi ya 550 wamepatiwa mafunzo ya usalama barabarani na kufanikiwa kwa mradi huo kunatokana na ushirikiano wa wadau mbalimbali huku akiwapongeza Amend kwa kazi kubwa wanayofanya ya kutoa elimu ya usalama barabarani.

Awali Inspekta wa Jeshi la Polisi Rajab Mhumbi aliyemwakilisha Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Tanga amesema vivuko vya barabarani ambavyo vimewekwa na Amend ni vema vikalindwa na kila mmoja wetau na si jukumu la wanafunzi na walimu peke yao.



Share:

Saturday, November 25, 2023

SERIKALI YAZINDUA MPANGO WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI, MAGONJWA YA NGONO NA HOMA YA INI

 

Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalim akizungumza wakati wa Uzinduzi wa mpango wa taifa wa kudhibiti ukimwi, magonjwa ya ngono na homa ya ini uliozinduliwa leo.

Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani Nchini Tanzania, Bw. Sagoe Moses akizungumza wakati wa Uzinduzi wa mpango wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi magonjwa ya ngono na homa ya ini uliozinduliwa leo na Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalim ambae ndio alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.

Mratibu Mwandamizi Ofisi ya Uratibu wa PEPFAR Ubalozi wa Marekani Nchini Dk. Hiltruda Chrisant Temba akizungumza wakati wa Uzinduzi wa mpango wa taifa wa kudhibiti ukimwi, magonjwa ya ngono na homa ya ini uliozinduliwa Leo na Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalim ambae ndio alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.

Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalim pamoja na viongozi mbalimbali wakiserikali na wadau wa sekta ya afya wakikata utepe kuashiria Uzinduzi rasmi wa mpango wa taifa wa kudhibiti ukimwi, magonjwa ya ngono na homa ya ini uliozinduliwa leo jijini Dar es Salaam.



Serikali imedhamiria kutokomeza maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa mama mjamzito kwenda kwa mtoto pamoja na kuzuia maambukizi mapya ya ukimwi kwa kundi la vijana kuanzia umri wa miaka 15 hadi 24 kutokana na takwimu kuonyesha kuwa kundi hilo la vijana ndilo linaloathirika zaidi na maambukizi hayo.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa mpango wa Taifa wa kudhibiti ukimwi, magonjwa ya ngono na Homa ya ini jijini Dar es salaam Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema licha ya hatua kubwa ambayo serikali na wadau wa masuala ya afya iliyopigwa katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa ukimwi ikiwemo kupungua kwa maambukizi lakini bado makundi hayo yanahitaji nguvu zaidi katika kuyasaidia dhidi ya ugonjwa huo.

Katika hatua nyingine Waziri Ummy amebainisha kuwa bado kuna ongezeko kubwa la maambukizi ya magonjwa ya ngono na Homa ya Ini nchini hivyo serikali inakuja na mpango mkakati wa wa kuhakikisha kutokomeza maambukizi hayo.

Waziri ameeleza kuwa serikali ya awamu ya sita imeboresha huduma za afya kuanzia ngazi ya taifa hadi msingi kwa kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya karibu zaidi na maeneo yao

“Serikali kupitia Wizara ya Afya wadau wa sekta na wataalamu wengine tayari wamefanyia kazi hoja zote zilizoibuliwa na bunge na semina zimefanyika kwa makundi mbalimbali ndani ya jamii kuhusu umuhimu wa bima za Afya kwa wote”.

“Kwa sasa nchi yetu iko mbali katika utoaji wa huduma, kuna vifaa vya kisasa vya uchunguzi wa magonjwa, huduma nyingi za kibingwa zinapatikana hapa hapa nchini lakini pia huduma za Afya zimesogezwa sana kwa wananchi hivyo kama serikali tuko tayari kutekeleza na kuhakikisha kuwa tunaendelea kuboresha huduma za afya kote nchini”.

Nayo baadhi ya mashirika ya kimataifa ambayo ni Shirika la La afya la Kimataifa WHO pamoja na Shirika la misaada la Marekani UNAIDS yaliyohudhuria uzinduzi huo kupitia kwa wawakilishi wao wamesifu juhudi za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dk Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muuungano waTanzania katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa ukimwi na kusema wataendelea kuunga mkono juhudi hizo
Share:

Friday, November 17, 2023

Shirika la USAID laipongeza serikali ya Tanzania mafanikio katika miradi ya elimu na afya nchini

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart (kushoto), akikabidhi mipira kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Njia Panda, Bi. Tatu Mohamedi (kulia), wakati wawakilishi wa USAID, Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR) pamoja na mashirika yanayosimamia miradi inayotoa huduma kwa wagonjwa wa VVU inayofadhiliwa na mfuko huo, wakitembelea shule hiyo kuangalia maendeleo ya miradi ya USAID Kizazi Hodari Kusini, inayotekelezwa na Shirika la Deloitte shuleni hapo, Iringa, jana. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Mradi wa Kizazi Hodari, Bi. Dorothy Matoyo, Mkurugenzi Msaidizi wa USAID kitengo cha afya nchini, Bi. Anna Hofmann na Kaimu Ofisa Elimu Msingi wa Manispaa ya Iringa, Samweli Mtovagakye. Ziara hiyo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 20 ya Mfuko wa PEPFAR.
Mkurugenzi wa Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini, Bi. Dorothy Matoyo, akitoa maelezo kuhusu mafanikio ya mradi huo unaoendeshwa na Shirika la Deloitte, wakati wawakilishi wa USAID, PEPFAR, pamoja na mashirika yanayosimamia miradi inayotoa huduma kwa wagonjwa wa VVU inayofadhiliwa na PEPFAR, wakitembelea shule ya msingi Njia Panda, kuangalia maendeleo ya afua mbili za wanafunzi wasichana ya Dreams na wavulana ya ‘coaching boys into men' (CBIM) shuleni hapo, Iringa, jana.
Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Bwana Craig Hart (katikati), akiangalia michoro inayotumika kufundishia afua za Dreams na CBIM kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Njia Panda shuleni hapo jana. Afua hizo zinahusu elimu ya uzazi, maambukizi ya VVU, tabia njema na stadi za maisha ikiwemo elimu ya kifedha. Miradi hiyo imechangia ufaulu wa shule hiyo kwa mwaka 2022, darasa la saba ufaulu ukiwa ni 97% huku darasa la nne ukiwa ni 93%.
Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Bwana Craig Hart, akisalimiana na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Njia Panda mjini Iringa, alipokwenda pamoja na ujumbe wake kukagua miradi ya USAID Kizazi Hodari Kusini inayofadhiliwa na Mfuko wa PEPFAR.
Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Bwana Craig Hart (kulia), akiagana na Mkurugenzi wa Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kusini, Bi. Dorothy Matoyo (wa pili kushoto), mara baada ya kutembelea Shule ya Msingi Njia Panda kuangalia maendeleo ya inayosimamiwa Shirika la Deloitte kupitia mradi wa Kizazi Hodari Kusini, chini ya ufadhili wa Mfuko wa PEPFAR.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart (katikati), pamoja na Mkurugenzi Msaidizi wa USAID kitengo cha afya nchini, Bi. Anna Hofmann (wa pili kushoto), wakipiga picha ya kumbukumbu na baadhi ya mabinti wanaohudumiwa na mradi wa EpiC unaosimamiwa na Shirika la FHI360 kwa ufadhili wa Mfuko wa PEPFAR, wakati wawakilishi wa USAID na PEPFAR nchini wakifanya ziara mkoani Iringa kuangalia maendeleo ya miradi inayofadhiliwa na mfuko huo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 20 ya Mfuko wa PEPFAR. Katikati ni Mkurugenzi Msaidizi wa USAID.
Mkurugenzi wa Shirika la FHI360, Bwana Bernard Ogwang, linalosimamia mradi wa EpiC, akitoa maelezo kuhusu mafanikio ya mradi huyo katika kutoa huduma kwa wenye VVU.
Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Bwana Craig Hart (katikati kulia), akiangalia ubunifu wa kazi za mikono za mmoja wa mabinti wenye VVU wanaohudumiwa na mradi wa EpiC chini ya usimamizi wa Shirika la FHI360 mjini Iringa wakati wa ziara ya wawakilishi wa USAID, PEPFAR, mashirika yanayosimamia miradi ya USAID pamoja na waandishi wa habari kuangalia maendeleo ya miradi hiyo mkoani humo.

Na Zuhura Rashidi, Iringa

SHIRIKA la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), limeipongeza Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, chini ya Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada kubwa zinazofanyika katika kuboresha maendeleo ya miradi ya afya na elimu nchini.

Pongezi hizo zilitolewa na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la USAID, Bwana Craig Hatz, katika Shule ya Msingi Njia Panda Mkoani Iringa wakati akihitimisha ziara ya siku tatu ya wawakilishi wa shirika hilo na wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR), pamoja na mashirika yanayosimamia utekelezaji wa miradi ya ukimwi inayofadhiliwa na PEPFAR.

Akihitimisha ziara hiyo ambayo pamoja na mambo mengine ilienda pamoja na maadhimisho ya miaka 20 ya Mfuko wa PEPFAR, Bwana Hart alisema jitihada zinazofanywa na serikali kwa kushirikiana na USAID, PEPFAR, zimechangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya miradi yote inayofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia USAID kwa zaidi ya miaka 60 iliyopita.

Serikali ya Marekani kwa zaidi ya miaka 20 imewekeza zaidi ya USD Bilioni 6 nchini Tanzania, kuhakikisha tunashirikiana pamoja na serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, sekta binafsi, wazazi na familia kukabiliana na HIV/AIDS."

Dola bilioni 6 inaweza kuonekana nyingi, Mwaka 2000 hadi 2019 umri wa kuishi kwa mtanzania uliongezeka kwa miaka 15, ikimaanisha sasa watanzania wote wameongeza umri wao wa kuishi kwa miaka 15 zaidi, wadau wote hawa wameungana kwa ajili yako, mpo katika mazingiza bora, mnapata elimu pamoja na elimu bora ya afya, muhimu sana kwa Tanzania ya kesho, maisha yako na maisha yetu ya baadae”, alisema.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini, Bi. Dorothy Matoyo alisema wao kama Deloitte wanayo furaha kupata uwezo wa kuchangia katika maendeleo ya kizazi chenye furaha na kinachojiamini na ndipo jina lao lilipotokea.

Kizazi tunachokiangalia sasa tunatumaini baada ya miaka 10 ama 20 ijayo kitakuwa kizazi salama chenye kujiamini, chenye upendo, kujua jinsi ya kujilinda na VVU, unyanyapaa na ukatili wa kijinsia."

Deloitte kupitia mradi wa Kizazi Hodari Kanda ya Kusini, ni wajibu wetu kuhakikisha tunawasaidia watoto yatima pamoja na wanaoishi katika mazingira magumu katika kuwaunganisha katika vituo watakavyoweza kupata usaidizi”, alisema Bi Dorothy.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Njia Panda, Bi. Tatu Mohamedi alisema alisema shuleni hapo chini ya uratibu wa Mradi wa Kizazi Hodari Kusini, wanajishughulisha na afua mbili za ‘Dreams’ kwa wanafunzi wa kike na ‘Coaching Boys Into Men’ (CBIM) ambapo jumla ya watoto wa kike 235 na wa kiume 204 wamenufaika na mpango wa mafunzo katika afua zote mbali.

Afua hizi zinalenga kuwasadia watoto kujitambua, kujithamini na kujiheshimu hivyo watoto hawa wamepata mafunzo kuhusu ugonjwa wa ukimwi, afya ya uzazi, ukatili wa kijinsia na kuondokana na unyanyapaa kwa wale wenye virusi."

Miradi hii imeleta mafanikio makubwa hata kwa wanafunzi wetu kitaaluma, kupitia USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini wamesaidia vifaa vya shule kama madaftari na kalamu kwa watoto wa kike 235 kwa lengo la kuwasaidia watoto hao kufanya vizuri katika mitihani yao”, alisema mwalimu huyo.

Mkurugenzi wa Shirika la FHI360, Bwana Bernard Ogwang alisema shirika lao linalosimamia mradi wa EpiC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR, limechangia kwa kiasi kikubwa kuboresha maisha ya vijana wa kike na wa kiume wanaoishi katika mazingira hatarishi ya kupata Virusi vya ukimwi.

Katika mikoa 11 tunayohudumia, tuna idadi ya vijana wa kike na wa kiume 225 wanaopata huduma kamili ya kinga na tiba ya VVU, lakini pia vijana hawa hujishughulisha katika shughuli za kiuchumi ili waweze kuboresha maisha yao”, alisema.

Baadhi ya mabinti wenye VVU wanaopata huduma kupitia mradi wa EpiC wakitoa ushuhuda ni jinsi gani miradi ya Mfuko wa PEPFAR imeboresha maisha yao mara baada ya kugundua hali zao na kujiunga katika vituo vya huduma na tiba walisema moja ya changamoto zinazochangia kutojitokeza kwa watu wengi kupima virusi vya ukimwi ni unyanyapaa unaotokana na imani, mila potofu na kukosa elimu sahihi juu ya ugonjwa wa ukimwi.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive