A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Showing posts with label LOCAL. Show all posts
Showing posts with label LOCAL. Show all posts

Saturday, November 25, 2023

SERIKALI YAZINDUA MPANGO WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI, MAGONJWA YA NGONO NA HOMA YA INI

 

Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalim akizungumza wakati wa Uzinduzi wa mpango wa taifa wa kudhibiti ukimwi, magonjwa ya ngono na homa ya ini uliozinduliwa leo.

Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani Nchini Tanzania, Bw. Sagoe Moses akizungumza wakati wa Uzinduzi wa mpango wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi magonjwa ya ngono na homa ya ini uliozinduliwa leo na Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalim ambae ndio alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.

Mratibu Mwandamizi Ofisi ya Uratibu wa PEPFAR Ubalozi wa Marekani Nchini Dk. Hiltruda Chrisant Temba akizungumza wakati wa Uzinduzi wa mpango wa taifa wa kudhibiti ukimwi, magonjwa ya ngono na homa ya ini uliozinduliwa Leo na Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalim ambae ndio alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.

Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalim pamoja na viongozi mbalimbali wakiserikali na wadau wa sekta ya afya wakikata utepe kuashiria Uzinduzi rasmi wa mpango wa taifa wa kudhibiti ukimwi, magonjwa ya ngono na homa ya ini uliozinduliwa leo jijini Dar es Salaam.



Serikali imedhamiria kutokomeza maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa mama mjamzito kwenda kwa mtoto pamoja na kuzuia maambukizi mapya ya ukimwi kwa kundi la vijana kuanzia umri wa miaka 15 hadi 24 kutokana na takwimu kuonyesha kuwa kundi hilo la vijana ndilo linaloathirika zaidi na maambukizi hayo.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa mpango wa Taifa wa kudhibiti ukimwi, magonjwa ya ngono na Homa ya ini jijini Dar es salaam Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema licha ya hatua kubwa ambayo serikali na wadau wa masuala ya afya iliyopigwa katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa ukimwi ikiwemo kupungua kwa maambukizi lakini bado makundi hayo yanahitaji nguvu zaidi katika kuyasaidia dhidi ya ugonjwa huo.

Katika hatua nyingine Waziri Ummy amebainisha kuwa bado kuna ongezeko kubwa la maambukizi ya magonjwa ya ngono na Homa ya Ini nchini hivyo serikali inakuja na mpango mkakati wa wa kuhakikisha kutokomeza maambukizi hayo.

Waziri ameeleza kuwa serikali ya awamu ya sita imeboresha huduma za afya kuanzia ngazi ya taifa hadi msingi kwa kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya karibu zaidi na maeneo yao

“Serikali kupitia Wizara ya Afya wadau wa sekta na wataalamu wengine tayari wamefanyia kazi hoja zote zilizoibuliwa na bunge na semina zimefanyika kwa makundi mbalimbali ndani ya jamii kuhusu umuhimu wa bima za Afya kwa wote”.

“Kwa sasa nchi yetu iko mbali katika utoaji wa huduma, kuna vifaa vya kisasa vya uchunguzi wa magonjwa, huduma nyingi za kibingwa zinapatikana hapa hapa nchini lakini pia huduma za Afya zimesogezwa sana kwa wananchi hivyo kama serikali tuko tayari kutekeleza na kuhakikisha kuwa tunaendelea kuboresha huduma za afya kote nchini”.

Nayo baadhi ya mashirika ya kimataifa ambayo ni Shirika la La afya la Kimataifa WHO pamoja na Shirika la misaada la Marekani UNAIDS yaliyohudhuria uzinduzi huo kupitia kwa wawakilishi wao wamesifu juhudi za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dk Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muuungano waTanzania katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa ukimwi na kusema wataendelea kuunga mkono juhudi hizo
Share:

Friday, November 17, 2023

Shirika la USAID laipongeza serikali ya Tanzania mafanikio katika miradi ya elimu na afya nchini

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart (kushoto), akikabidhi mipira kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Njia Panda, Bi. Tatu Mohamedi (kulia), wakati wawakilishi wa USAID, Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR) pamoja na mashirika yanayosimamia miradi inayotoa huduma kwa wagonjwa wa VVU inayofadhiliwa na mfuko huo, wakitembelea shule hiyo kuangalia maendeleo ya miradi ya USAID Kizazi Hodari Kusini, inayotekelezwa na Shirika la Deloitte shuleni hapo, Iringa, jana. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Mradi wa Kizazi Hodari, Bi. Dorothy Matoyo, Mkurugenzi Msaidizi wa USAID kitengo cha afya nchini, Bi. Anna Hofmann na Kaimu Ofisa Elimu Msingi wa Manispaa ya Iringa, Samweli Mtovagakye. Ziara hiyo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 20 ya Mfuko wa PEPFAR.
Mkurugenzi wa Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini, Bi. Dorothy Matoyo, akitoa maelezo kuhusu mafanikio ya mradi huo unaoendeshwa na Shirika la Deloitte, wakati wawakilishi wa USAID, PEPFAR, pamoja na mashirika yanayosimamia miradi inayotoa huduma kwa wagonjwa wa VVU inayofadhiliwa na PEPFAR, wakitembelea shule ya msingi Njia Panda, kuangalia maendeleo ya afua mbili za wanafunzi wasichana ya Dreams na wavulana ya ‘coaching boys into men' (CBIM) shuleni hapo, Iringa, jana.
Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Bwana Craig Hart (katikati), akiangalia michoro inayotumika kufundishia afua za Dreams na CBIM kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Njia Panda shuleni hapo jana. Afua hizo zinahusu elimu ya uzazi, maambukizi ya VVU, tabia njema na stadi za maisha ikiwemo elimu ya kifedha. Miradi hiyo imechangia ufaulu wa shule hiyo kwa mwaka 2022, darasa la saba ufaulu ukiwa ni 97% huku darasa la nne ukiwa ni 93%.
Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Bwana Craig Hart, akisalimiana na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Njia Panda mjini Iringa, alipokwenda pamoja na ujumbe wake kukagua miradi ya USAID Kizazi Hodari Kusini inayofadhiliwa na Mfuko wa PEPFAR.
Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Bwana Craig Hart (kulia), akiagana na Mkurugenzi wa Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kusini, Bi. Dorothy Matoyo (wa pili kushoto), mara baada ya kutembelea Shule ya Msingi Njia Panda kuangalia maendeleo ya inayosimamiwa Shirika la Deloitte kupitia mradi wa Kizazi Hodari Kusini, chini ya ufadhili wa Mfuko wa PEPFAR.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart (katikati), pamoja na Mkurugenzi Msaidizi wa USAID kitengo cha afya nchini, Bi. Anna Hofmann (wa pili kushoto), wakipiga picha ya kumbukumbu na baadhi ya mabinti wanaohudumiwa na mradi wa EpiC unaosimamiwa na Shirika la FHI360 kwa ufadhili wa Mfuko wa PEPFAR, wakati wawakilishi wa USAID na PEPFAR nchini wakifanya ziara mkoani Iringa kuangalia maendeleo ya miradi inayofadhiliwa na mfuko huo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 20 ya Mfuko wa PEPFAR. Katikati ni Mkurugenzi Msaidizi wa USAID.
Mkurugenzi wa Shirika la FHI360, Bwana Bernard Ogwang, linalosimamia mradi wa EpiC, akitoa maelezo kuhusu mafanikio ya mradi huyo katika kutoa huduma kwa wenye VVU.
Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Bwana Craig Hart (katikati kulia), akiangalia ubunifu wa kazi za mikono za mmoja wa mabinti wenye VVU wanaohudumiwa na mradi wa EpiC chini ya usimamizi wa Shirika la FHI360 mjini Iringa wakati wa ziara ya wawakilishi wa USAID, PEPFAR, mashirika yanayosimamia miradi ya USAID pamoja na waandishi wa habari kuangalia maendeleo ya miradi hiyo mkoani humo.

Na Zuhura Rashidi, Iringa

SHIRIKA la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), limeipongeza Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, chini ya Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada kubwa zinazofanyika katika kuboresha maendeleo ya miradi ya afya na elimu nchini.

Pongezi hizo zilitolewa na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la USAID, Bwana Craig Hatz, katika Shule ya Msingi Njia Panda Mkoani Iringa wakati akihitimisha ziara ya siku tatu ya wawakilishi wa shirika hilo na wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR), pamoja na mashirika yanayosimamia utekelezaji wa miradi ya ukimwi inayofadhiliwa na PEPFAR.

Akihitimisha ziara hiyo ambayo pamoja na mambo mengine ilienda pamoja na maadhimisho ya miaka 20 ya Mfuko wa PEPFAR, Bwana Hart alisema jitihada zinazofanywa na serikali kwa kushirikiana na USAID, PEPFAR, zimechangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya miradi yote inayofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia USAID kwa zaidi ya miaka 60 iliyopita.

Serikali ya Marekani kwa zaidi ya miaka 20 imewekeza zaidi ya USD Bilioni 6 nchini Tanzania, kuhakikisha tunashirikiana pamoja na serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, sekta binafsi, wazazi na familia kukabiliana na HIV/AIDS."

Dola bilioni 6 inaweza kuonekana nyingi, Mwaka 2000 hadi 2019 umri wa kuishi kwa mtanzania uliongezeka kwa miaka 15, ikimaanisha sasa watanzania wote wameongeza umri wao wa kuishi kwa miaka 15 zaidi, wadau wote hawa wameungana kwa ajili yako, mpo katika mazingiza bora, mnapata elimu pamoja na elimu bora ya afya, muhimu sana kwa Tanzania ya kesho, maisha yako na maisha yetu ya baadae”, alisema.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini, Bi. Dorothy Matoyo alisema wao kama Deloitte wanayo furaha kupata uwezo wa kuchangia katika maendeleo ya kizazi chenye furaha na kinachojiamini na ndipo jina lao lilipotokea.

Kizazi tunachokiangalia sasa tunatumaini baada ya miaka 10 ama 20 ijayo kitakuwa kizazi salama chenye kujiamini, chenye upendo, kujua jinsi ya kujilinda na VVU, unyanyapaa na ukatili wa kijinsia."

Deloitte kupitia mradi wa Kizazi Hodari Kanda ya Kusini, ni wajibu wetu kuhakikisha tunawasaidia watoto yatima pamoja na wanaoishi katika mazingira magumu katika kuwaunganisha katika vituo watakavyoweza kupata usaidizi”, alisema Bi Dorothy.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Njia Panda, Bi. Tatu Mohamedi alisema alisema shuleni hapo chini ya uratibu wa Mradi wa Kizazi Hodari Kusini, wanajishughulisha na afua mbili za ‘Dreams’ kwa wanafunzi wa kike na ‘Coaching Boys Into Men’ (CBIM) ambapo jumla ya watoto wa kike 235 na wa kiume 204 wamenufaika na mpango wa mafunzo katika afua zote mbali.

Afua hizi zinalenga kuwasadia watoto kujitambua, kujithamini na kujiheshimu hivyo watoto hawa wamepata mafunzo kuhusu ugonjwa wa ukimwi, afya ya uzazi, ukatili wa kijinsia na kuondokana na unyanyapaa kwa wale wenye virusi."

Miradi hii imeleta mafanikio makubwa hata kwa wanafunzi wetu kitaaluma, kupitia USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini wamesaidia vifaa vya shule kama madaftari na kalamu kwa watoto wa kike 235 kwa lengo la kuwasaidia watoto hao kufanya vizuri katika mitihani yao”, alisema mwalimu huyo.

Mkurugenzi wa Shirika la FHI360, Bwana Bernard Ogwang alisema shirika lao linalosimamia mradi wa EpiC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR, limechangia kwa kiasi kikubwa kuboresha maisha ya vijana wa kike na wa kiume wanaoishi katika mazingira hatarishi ya kupata Virusi vya ukimwi.

Katika mikoa 11 tunayohudumia, tuna idadi ya vijana wa kike na wa kiume 225 wanaopata huduma kamili ya kinga na tiba ya VVU, lakini pia vijana hawa hujishughulisha katika shughuli za kiuchumi ili waweze kuboresha maisha yao”, alisema.

Baadhi ya mabinti wenye VVU wanaopata huduma kupitia mradi wa EpiC wakitoa ushuhuda ni jinsi gani miradi ya Mfuko wa PEPFAR imeboresha maisha yao mara baada ya kugundua hali zao na kujiunga katika vituo vya huduma na tiba walisema moja ya changamoto zinazochangia kutojitokeza kwa watu wengi kupima virusi vya ukimwi ni unyanyapaa unaotokana na imani, mila potofu na kukosa elimu sahihi juu ya ugonjwa wa ukimwi.
Share:

Thursday, November 16, 2023

ROTARY TANZANIA KUENDESHA KAMBI YA MATIBABU BURE KWA WAKAZI WAA BUNJU.

 

Rais wa Rotary Club upande wa Oystarbay jijini Dar es Salaam Abdulrahman Hussein (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari wakati wakitangaza fursa ya kutoa huduma ya afya na matibabu bure kwa wakazi wa Bunju ikiwa ni muendelezo wa Rotary kusaidia jamii hasa katika sekta ya afya hii imekuwa ni utaratibu wa Rotary kujitolea kuhakikisha wanasaidia watu ambao wanamatatizo mbalimbali ya kiafya na kukosa uwezo wakujitibu. Hafla hiyo hiyo imefanyika leo masaki jijini humo wengime pichani ni Mwenyekiti wa Rotary Tanzania Diamond Carvalho pampja na Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi Bi Mehreen Khatri.


Mwenyekiti wa Rotary Tanzania Diamond Carvalho (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari wakati wakitangaza fursa ya kutoa huduma ya afya na matibabu bure kwa wakazi wa Bunju ikiwa ni muendelezo wa Rotary kusaidia jamii hasa katika sekta ya afya hii imekuwa ni utaratibu wa Rotary kujitolea kuhakikisha wanasaidia watu ambao wanamatatizo mbalimbali ya kiafya na kukosa uwezo wakujitibu. Hafla hiyo hiyo imefanyika leo masaki jijini humo wengine pichani ni Rais wa Rotary Club upande wa Oystarbay jijini Dar es Salaam Abdulrahman Hussein pamoja na Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi Bi Mehreen Khatri.


Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi Bi Mehreen Khatri(kushoto), akizungumza na waandishi wa habari wakati wakitangaza fursa ya kutoa huduma ya afya na matibabu bure kwa wakazi wa Bunju ikiwa ni muendelezo wa Rotary kusaidia jamii hasa katika sekta ya afya hii imekuwa ni utaratibu wa Rotary kujitolea kuhakikisha wanasaidia watu ambao wanamatatizo mbalimbali ya kiafya na kukosa uwezo wakujitibu. Hafla hiyo hiyo imefanyika leo masaki jijini humo wengime pichani ni Mwenyekiti wa Rotary Tanzania Diamond Carvalho pamoja na Rais wa Rotary Club upande wa Oystarbay jijini Dar es Salaam Abdulrahman Hussein



Mamia ya wakazi wa Bunju na maeneo ya Jirani wametakiwa kujitokeza kwa wingi siku ya Jumamosi Novemba 18 2023 katika viwanja vya shule ya msingi bunju kupima afya zao katika kambi maalum ya afya itakayoendeshwa na Rotary Tanzania.


Rotary ikishirikiana na wadau mbalimbali wa afya na wafadhili, wataendesha huduma hiyo siku nzima ya Jumamosi Novemba 18, ili kuwawezesha wakazi wengi wa Bunju, maeneo ya Jirani na Dar es Salaam kwa ujumla kupata mud awa Kwenda kupima afya zao na kupata ushauri wa kitaalamu bure bila malipo yoyote.


Hayo yameelezwa na Diamond Carvalho, Mwenyekiti wa Rotary Tanzania wakati akizungumza na waandishi wa habari masaki jijini Dar es Salaam alipokuwa akielezea kuhusu maandalizi ya kambi hiyo ya siku moja itakayofanyika Bunju jijini Dar es Salaam.


Inakadiriwa kuwa kuna wanafunzi 3500 na watu wazima 1500 watakaoshiriki, na kila mmoja wao atapata huduma muhimu kama vile vipimo, na elimu ya afya na kinga, uchunguzi wa macho, uchunguzi wa saratani mbali mbali, ukaguzi wa meno, elimu ya hedhi salama, na fursa ya kupata chanjo, dawa na rufaa za wataalamu kama itahitajika.


Kwa moyo wa kujitolea, madaktari takribani 100 wakiwemo madaktari wa kawaida 50 na wataalamu wengine 50 wa meno, Macho, Ngozi, Watoto, na huduma nyingine wameahidi kutoa msaada wao kwa kutoa huduma hizi muhimu wakishirikiana na timu kubwa ya wahudumu takribani 500 inaunga mkono juhudi hizi, na ushirikiano huu unasisitiza umuhimu wa upendo na umoja katika kukabiliana na mahitaji ya afya ya jamii.


Diamond Carvalho, , ameeleza, kuwa “Rotary Tanzania, kwa kushirikiana hasa na Klabu ya Rotary ya Oysterbay, imekuwa ikiandaa kambi za matibabu kwa ushirikiano na Klabu ya Rotaract ya Kairiuki tangu mwaka 2012, lengo likiwa kutoa huduma za afya msingi kwa jamii ya Dar es Salaam. Kampeni ya afya ya leo inaadhimisha hatua muhimu sana, ikiwa imeongezeka mara tatu ukubwa wa kambi za matibabu zilizofanywa hapo awali na klabu yetu.


“Tunapenda kuwashukuru sana Vilabu vya Rotary na Rotaract washirika wetu, vilevile washirika muhimu – Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Awamu ya Sita Ikiongozwa na Raisi Doctor Mama Samia Suluhu Hassan, Wizara ya Afya, Bill & Melinda Gates Foundation, Guaranty Trust Bank, Pepsi, SGA Security, Jollie Pads, Agha Khan Health Service, Manufaa Media, Bakhressa Group ,Chemi Cotex, Hitech Sai Hospitals, Afya Intelligence na Management and Development for Health (MDH).” Amesema Calvalho


Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi Mehreen Khatri amesema maandalizi yote yamekamilika na amewashauri wakazi wa Dar es Salaam kutumia fursa hii adhimu kuja na kupima afya zao Pamoja na kupata ushauri na elimu ya afya. “tunashukuru maandalizi yote yamekamilika. Hii ni kutokana na ushiriki mkuwa wa wanachama wa Rotary Tanzania Pamoja wafadhili wetu. Tunaamini watu wengi watajitokeza kupima afya zao siku hiyo” alisema Mehreen.


Naye Abdulrahman Hussein Rais wa Rotary Club ya Osterbay Dar es Salaam amesema Jumla ya wakazi 5000 kutoka Bunju na maeneo ya jirani watapata huduma za afya na elimu bila malipo wakati wa tukio la siku ya Afya ya Rotary inayofanywa kwa ushirikiano na Vilabu vya Rotaract vya Kairuki, Muhimbili, KIUT, Alpha, na Kwanza
Share:

Takwimu sahihi nyenzo muhimu mapambano dhidi ya Ukimwi

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la maendeleo ya kimataifa (USAID) Bw. Craig Hart (katikati) akiangalia, wakati mmoja wa wenye VVU akijisajili katika mfumo wa alama za vidole mara baada ya mkurugenzi huyo kukabidhi msaada wa kifaa hicho kwa hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa. Mfumo huo unasaidia kupata takwimu sahihi za wenye VVU, jambo ambalo ni muhimu katika kufanikisha utoaji wa huduma bora. Hafla hiyo iliyofanyika mkoani humo jana inakwenda sambamba na maadhimisho ya miaka 20 ya Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani (PEPFAR) unaofadhili miradi ya kupabana na Ukimwi inayosimamiwa na (USAID)
Mkurugenzi wa mradi wa USAID Afya yangu kanda ya Kusini unaoendeshwa na Shirika la Deloitte, Dk Marina Njekela, akielezea utendaji na mafanikio ya mradi huo katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU katika hafla hiyo Mjini Iringa jana.
Mwakilishi wa mabinti wanaoishi na Virusi Vya Ukimwi Tanzania, Lucy Michael Mpwage, aliyezaliwa na maambukizi ya ugonjwa huo akitoa ushuhuda pamoja na changamoto za unyanyapaa alizokumbana nazo katika vipindi tofauti vya maisha yake na jinsi huduma za miradi ya USAID inayoendeshwa na Shirika la Deloitte ilivyookoa maisha yake. Ilikua ni wakati wawakilishi wa mfuko PEPFAR, USAID, mashirika yanayosimamia utoaji wa huduma kwa wenye VVU pamoja na waandishi wa wabari wakitembelea Hosptali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa jana, kuangalia mafanikio ya miradi hiyo .
Baadhi ya wanawake waliowezeshwa na Mradi wa Hebu tuyajenge unaoendeshwa na Shirika la NACOPHA wakishangilia wakati wa ziara ya wawakilishi wa PEPFAR, USAID wakitembelea katika ofisi za shirika hilo mjini Iringa jana.

Na Zuhura Rashidi, Iringa.

UWEPO wa takwimu sahihi za wenye VVU unachangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya mipango mikakati katika uratibu wa miradi ya kupambana na ukimwi imeelezwa mkoani Iringa jana.

Hayo yalisemwa na Maganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa, Dk. Mohamedi Mang’ula wakati wa ziara ya wawakilishi wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa kukabiliana na ukimwi (PEPFAR), pamoja na Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) hospitalini hapo ili kuangalia huduma mbalimbali za utoaji tiba kwa wenye VVU zinazofadhiliwa na mfuko huo kupitia USAID.

Dk Mang’ula alisema hayo muda mfupi baada ya kukabidhiwa msaada wa kifaa cha kufanyia usajili wa wenye VVU kwa kutumia mfumo wa alama za vidole kilichokabidhiwa na Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Bwana Craig Hart akishukuru ufadhili wa USAID uliochangia uboreshaji wa huduma za afya kwa wenye VVU hospitalini hapo.

Tunaipongeza Kampuni ya Deloitte inayoendesha miradi hii inayofadhili na Mfuko wa PEPFAR katika mkoa wetu kwani imeweza kutusaidia kupata mafanikio makubwa katika kufikia malengo ya 95;95;95 katika kutambua wenye VVU, waliotambuliwa kuanza kupata tiba na suala la kufubaza virusi vya ukimwi”, alisema.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Mradi wa USAID Afya Yangu Kusini, Dk. Marina Njelekela alisema wamekuwa na safari ndefu ila yenye mafanikio lukuki katika kutekeleza miradi inayofadhiliwa na PEPFAR kwa kupitia USAID.

Alisema misaada inayotolewa na PEPFAR kupitia Shirika la USAID imesainia kuokoa maisha ya watanzania wengi katika kipindi hiki cha miaka 20 huku kukishuhudiwa uimarikaji mkubwa wa huduma kwa wenye VVU katika vituo mbalimbali nchini.

USAID Afya Yangu Kusini tunasharehekea miaka 20 kwa kuboresha miradi ya PEPFAR USAID, tukipitia hatua mbalimbali za kimaendeleo moja ikiwa ni kuwajengea uwezo watoa huduma za afya katika vituo mbalimbali."

Tumeboresha ubora wa utoaji huduma bora za VVU na Kifua Kikuu katika ngazi ya jamii, mwaka 2004 tukiwa na vituo vya kutolewa huduma 33 lakini kwa msaada wa PEPFAR kwa hadi mwaka 2023 tumeweza kufikisha vituo 676."

Deloitte pamoja na washirika wake wa kiufundi wa MDH na T-marc tunajivunia sana kusimamia miradi inayofadhiliwa na PEPFAR, mwaka 2004 aina ya wagonjwa tulioanza nao kwa sasa imebadilika kabisa, sasa wapo na furaha na matumaini, wamewezeshwa, hawajisikii unyanyapaa”, alisema Dk. Marina.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Baraa la Taifa la Watu Wanaoishi na UVVU Tanzania (NACOPHA), Bwana Deogratius Rutwatwa wanaoendesha mradi wa ‘Hebu Tuyajenge’ alisema moja ya mikakati ya malengo ya mradi huo ni kuhakikisha pamoja na mambo mengine watu wenye maambukizi ya VVU wanatambua hali zao.

Ofisa mtendaji huyo alizungumzia suala la unyanyapaa kuwa moja ya changamoto inayosababisha watu wengi wenye VVU kushindwa kujitokeza kupata huduma za upimaji na kuunganishwa kwenye vituo vya tiba.

Baadhi ya huduma tunazozitoa ni pamoja na elimu kwa wenye VVU kuhusu namna bora ya kujzuia maambukizi mapya, kutambua wenza na watoto wenye VVU hivyo kuwaunganisha kwenye huduma za upimaji na kutoa usaidizi juu ya matumizi sahihi ya dawa za ARV’s."

Kwa namna ya kipekee niupongeze Mfuko wa PEPFAR kupitia USAID kipindi hiki unapotimiza miaka 20 kwa mafanikio na jitihada zake katika kupambana na janga la ugonjwa wa ukimwi hapa Tanzania”, alisema.
Share:

Wednesday, November 15, 2023

Serikali yaupongeza Mfuko wa PEPFAR ukitimiza miaka 20 ya kurudisha matumaini ya wenye VVU nchini

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bi. Halima Dendego, akipokea cheti cha shukurani kwa kutambua mchango wake katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi na unyanyapaa kwa wenye VVU katika Mkoa wa Iringa, kutoka kwa Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart, wakati wa ziara ya waandishi wa habari mkoani humo leo ikiwa ni sehemu ya matukio kuadhimisha miaka 20 ya Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR). Ziara hiyo, ililenga kuangalia mafanikio ya miradi inayohudumia wenye VVU na kusimamiwa na mashirika ya Deloitte, Nacopha na FHI360.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa mradi wa USAID Afya Yangu Kanda ya Kusini Dk. Marina Njelekela, kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa leo. Wa kwanza kushoto ni muwakilishi wa PEPFAR nchini, Bi. Jessica Greene na Mkurugenzi Msaidizi wa USAID kitengo cha afya nchini, Bi. Anna Hofmann.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini, Bi. Dorothy Matoyo (kulia) kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa leo. Wa kwanza kushoto ni mwakilishi wa PEPFAR nchini, Bi. Jessica Greene na Mkurugenzi Msaidizi USAID kitengo cha afya nchini, Bi. Anna Hofmann.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la maendeleo ya Kimataifa USAID Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa mradi wa Rise project, Maende Makokha, kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa leo. Kushoto ni mwakilishi wa PEPFAR nchini, Jessica Greene na Mkurugenzi Msaidizi USAID Kitengo cha Afya nchini, Bi. Anna Hofmann.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana. Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa Shirika la FHI360, Bwana Bernard Ogwang, kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa leo
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart, akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi wa Shirika wa Nacopha, Bwana Deogratius Rutatwa, kwa kutambua mchango wa shirika hilo, likiwa ni moja ya Mashirika yanayofadhiliwa na Shirika la USAID katika kutoa huduma bora kwa wenye VVU. Hii ni sehemu ya matukio ya kuadhimisha miaka 20 ya mfuko wa PEPFAR Mkoani Iringa.
Mratibu wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR) nchini, Bi. Jessica Greene akizungumza katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bw Craig Hart (katikati), akipozi kwa picha ya kumbukumbu mjini Iringa leo, na baadhi ya wawakilishi kutoka mfuko wa PEPFAR, USAID na Mashirika yanayoratibu miradi ya Ukimwi inayofadhiliwa na PEPFAR kwa usimamizi wa USAID.

*Zaidi ya Dola za Kimarekani Bilioni 6 zatumika

*Mwaka 2022 pekee ikitumia Dola 450 milioni kupambana na maambukizi ya ukimwi nchini

Na Zuhura Rashidi, Iringa

SERIKALI ya Tanzania imeupongeza Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR), kwa jitihada zake katika kuleta matumaini mapya katika mikoa iliyoelemewa na mzigo mkubwa wa maambukizi ya ugonjwa wa HIV na Kifua Kikuu.

Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bi. Halima Dendegu wakati wa ziara ya wawakilishi wa mfuko wa PEPFAR, Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), mashirika yanayotekeleza miradi ya ukimwi pamoja na waandishi wa habari mkoani humo wakitembelea miradi na vituo vinavyotoa huduma za ukimwi ikiwa ni sehemu ya matukio kuadhimisha miaka 20 tokea kuanzishwa kwa mfuko huo.

Mkuu wa Mkoa huyo alisema Iringa ni mmoja wa mikoa iliyoathiriwa sana na maambuki ya VVU lakini kwa msaada wa PEPFAR chini ya Shirika la USAID imewawezesha kuwa na vituo vya huduma na tiba (CTC) 261 kutoka vinane vilivyokuwepo awali, huku 136 vikiendeshwa na USAID vilivyosaidia kuleta mabadiliko chanya katika utoaji elimu na huduma bora kwa kutumia vifaa vilivyoboreshwa na wahudumu wa afya wenye elimu na ujuzi katika utoaji wa huduma bora za afya.

Tafadhali pokeeni pongezi za dhati kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassani, tunashukuru sana kwa misaada tunayoipokea kwani tunatarajia kushuka kwa maambukizi mapya kwa magonjwa ya ukimwi, kifua kikuu huku tukiendelea kupunguza unyanyapaa kwa wenye VVU."

Awali akizungumza mafanikio miradi ya PEPFAR inayosimamiwa na USAID, Mkurugenzi Mkazi wa shirika hilo nchini, Bwana Craig Hart alisema tokea mwaka 2003 serikali ya Marekali imetoa zaidi ya Dola za Kimarekani Bilioni 6 ikiwa ni pamoja na Dola 450 Milioni kwa mwaka 2022 pekee katika kupambana na ugonjwa wa Ukimwi chini Tanzania.

Mwaka 2003 ni watanzania 1000 tu waliokuwa wakipokea dawa za kupunguza makali ya VVU (ARV), leo wakati tukiadhimisha miaka 20 ya PEPFAR zaidi ya watanzania milioni 1.5 wananufaika na mpango huu wa tiba wa kuokoa maisha yao ikiwa ni asilimia 98 ya watu wanaoishi ya VVU."

Misaada yetu kwa watu wa Tanzania ni uwekezaji wa baadae, kwani kufikia mwaka 2050 robo ya watu wote duniani wataishi Afrika, nchini Tanzania theluthi mbili ya idadi ya watu wakiwa ni vijana chini ya umri wa miaka 25, hivyo kufanya uwekezaji katika kizazi kijacho kuwa ni jambo muhimu mno na lisiloepukika”, anasema Bwana Hart.

Naye Mratibu wa Mfuko wa PEPFAR nchini Bi. Jessica Greene alimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa kugusia maeneo manne ambayo mfuko huo umekuwa ukiyapa kipaumbele akiyataja kama; tiba, utoaji huduma bora, vituo vya afya na dawa za kupunguza makali ya VVU.

Tumeungana na Serikali ya Tanzania katika kuhakikisha vipaumbele hivi vinafanikiwa na tutandelea kuhakikisha watu wenye VVU wanapata huduma boza za matunzo na tiba”, alisema Bi. Jessica.

Baadhi ya miradi inayofadhiliwa na PEPFAR chini ya usimamizi wa USAID ni USAID Afya Yangu Kanda ya Kusini unaolenga utoaji huduma jumuishi za matunzo, matibabu na kuzuia maambukizi ya VVU na kifua kikuu na kuboresha mazingira wezeshi ya utoaji wa huduma bora za afya katika mikoa sita ya kusini mwa Tanzania, huku mradi wa USAID Kizazi Hodari Kusini unaoangalia utoaji wa huduma jumuishi za watoto yatima na wanaoishi katika mazingira hatarishi pamoja na walezi wao ili kuboresha afya, ustawi na ulinzi wa watoto yatima pamoja na vijana katika mikoa 11, miradi hii ikiendesha na Shirika la Deloitte.

Mradi mwingine ni ‘Epic’ unaotekelezwa na Shirika la FHI360 uKjjikita katika kufikia na kuendeleza udhibiti wa janga la VVU huku ukijihusisha katika kutoa msaada wa kitaalamu na huduma za moja kwa moja katika kuondoa vikwazo kufikia malengo ya 95-95-95 ukilenga makundi maalumu wakiwemo wasichana, wamama vijana, wanaume na wanawake walio katika hatari ya kupata maambukizi ya VVU.

Aidha mradi wa ‘Hebu Tuyajenge’ ukishirikisha watu wanaoishi na VVU, unalenga katika kuongeza matumizi ya huduma za upimaji VVU, tiba na uzazi wa mpango mongoni mwa vijana balehe na wenye VVU ukitekelezwa na Baraza la Taifa la Watu wanaoishi na VVU Tanzania (NACOPHA).
Share:

Thursday, October 26, 2023

AZAKI WAJENGEWA UWEZO WA MATUMIZI SAHIHI YA TEKNOLOJIA

Wadau mbalimbali wanaoshiriki katika wiki ya AZAKI inayoendelea Jijini Arusha wamejengewa uwezo wa matumizi sahihi ya teknolojia katika ustahimilivu wa fedha ili kuziwezesha Asasi zao kujisimamia kiuchimi.

Akizungumza katika mdahalo uliofanyika Jijini humo, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya FCS TRUST ambayo ni Kampuni tanzu ya Foundation For Civil Society (FCS) Arthur Mtafya amesema muda umefika kwa AZAKI kuwekeza miundombinu itakayosaidia kufanikisha mstakabali wa kukuza ustahimilivu wa fedha, na kuondokana na utegemezi wa wahisani wa nje.
Akizungumzia majukumu ya FCS TRUST, Mtafya ameeleza kuwa taasisi hiyo ilianziashwa kwa lengo la kutoa ushauri wa kitaalam kwenye maendeleo ya AZAKI na uwekezaji, kwaajili ya kutengeneza faida na kuchangia kwenye ustahimilivu wa taasisi mama ya Foundation For Civil Society.

Aidha, ametoa ushauri elekezi na mafunzo kwa AZAKI, ambapo taasisi hiyo pia imefanya uwekezaji kwenye maeneo mawili ambayo ni Soko la Mitaji na kwenye majengo.
"Kwa sasa tuna mikakati ya miradi miwili ambapo tuna jengo ambalo tunatarajia kulipangisha ili tupate faida, pia tumewekeza kwenye soko la mitaji na tayari tumeshaanza kupata faida kidogo ambayo baada ya muda tunaamini tunaweza kupata mtaji utakaowezesha kufanya uwekezaji kwenye maeneo mengine mbalimbali kwa ajili ya kupata fedha itakayochangia kuimarisha ustahimilivu wa kifedha wa taasisi mama". amesema Mtafya.
Pia, amefafanua kuwa moja ya eneo ambalo taasisi hiyo inalifanyiakazi ni kuzijengea uwezo AZAKI, na kwamba kwenye mdahalo huo wamepata fursa ya kuwasilisha kile ambacho wanafanya katika matumizi ya teknolojia inayosaidia ustahimilivu wa fedha.

"FCS Trust tuna uzoefu wa kutengeneza mifumo ndani ya hizi taasisi ambayo inaweza kurahisisha mambo yao mengi ya ndani lakini pia namna ya kuwasiliana na taasisi za nje".ameongeza Mtafya
Share:

Monday, October 23, 2023

SERIKALI YAOMBWA KUTOFAUTISHA KAZI ZA CSO's NA NGO's

Serikali imeombwa kutofautisha kazi zinazofanywa na Asasi za Kiraia (CSO's), na Asasi zisizo za kiserikali (NGO's) ili kila Mhimili uweze kufanya shuguli zake kwa ufanisi.

Ombi hilo limetolewa na Rais wa foundation for civil society (FCS) Dkt. Stigmata Tenga alipokuwa akifunga rasmi Wiki ya Asasi za Kiraia (AZAKI), iliyofanyika kwa juma moja kuanzia Octoba 23 hadi 27, 2023 Katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano AICC Jijini Arusha.
Amesema kuwa Asasi za Kiraia zitaendelea kuboresha mahusiano mazuri yalipipo kati yao na Asasi zisizo za Kiserikali kwa kuwa wadau wote hao wana jukumu la kuhakikisha wanafanya kazi zao kwaajili ya kuimarisha maendeleo ya Jamii na Taifa kwa ujumla.

"Asasi za Kiraia tutaboresha mahusiano yetu na Asasi zisizo za Kiserikali kwani nchi hii ni yetu, tunaifahamu, na sauti tunazoleta Serikalini ni sauti za wananchi wa nchi hii" amesema Dkt. Tenga.

Ameiomba Serikali kuendeleza ushirikiano na kuwasaidia, kwani wana ajenda nyingi ambazo wanashindwa kuzifanyia kazi kutokana na ushindani uliopo baina ya Asasi hizo.
Katika hatua nyingine, Dkt. Tenga ametangaza kusogezwa muda wa kufanyika Wiki ya AZAKI Kutoka mwezi Octoba kama ilivyo sasa, ambapo kwa mwaka wa 2024, Wiki hiyo itafanyika tarehe 26 hadi 30 mwezi Agosti.

"Tumefanya tathimini ya faida ambayo wana AZAKI wanaipata kwa kushiriki katika makongamano mbalimbali kwa mwaka, na umuhumu wa hayo matamasha yote kupitia kamati tendaji, tunatoa mapendekezo ya kufanya Wiki ya Asasi za Kiraia mwakani, iwe tarehe 26 hadi 30, mwezi Agosti" amesema Dkt. Tenga.

Wiki ya AZAKI 2023 iliyoanza Octoba 23 imehitimishwa rasmi leo Octoba 27, 2023 Jijini Arusha, ambayo imewaleta pamoja Asasi za Kiraia (AZAKI) kutoka Tanzania nzima kwa lengo la kujadili na kuboresha ushirikiano wa kimkakati.
Kauli mbiu ya Wiki ya AZAKI 2023, ni 'Teknologia na Jamii, Tulipotoka, tuilipo sasa na tunapoelekea, kuangazia fursa na changamoto zinazotokana na ulimwengu wa teknolojia unaoendelea'
Share:

Tuesday, October 10, 2023

USAID Afya Yangu Southern and USAID Kizazi Hodari Bring new hope for HIV and Tuberculosis Patients

USAID Afya Yangu Southern Project Chief of Party, Dr. Marina Njelekela (right), USAID Kizazi Hodari Southern Chief of Party, Ms. Doroth Matoyo (left), and Deloitte Tanzania Consulting Partner, Ms. Zahra Nensi, attending the 10th Tanzania Health Summit in Dar es Salaam at the weekend.

By Our Correspondent, Dar es Salaam.

The five-year projects of USAID Afya Yangu Southern ya Kusini and USAID Kizazi Hodari Southern, managed by Deloitte under the sponsorship of the United States President's Emergency Plan for AIDS Relief (PEPFAR), through the coordination of the United States Agency for International Development (USAID), have achieved significant success in assisting the Government of Tanzania in addressing the challenges of HIV and tuberculosis in the southern regions heavily burdened by the effects of these diseases.

Dr. Marina Njelekela, the Chief of Party of the USAID Afya Yangu Southern project, speaking at the 10th Tanzania Health Summit in Dar es Salaam over the weekend, stated that the $102 million project aims to support the delivery of quality HIV and Tuberculosis (TB) services, including prevention, care, TB treatment, and HIV antiretroviral therapy in six southern regions of Tanzania.

"The project supports approximately 1,409 health facilities in the regions of Iringa, Lindi, Morogoro, Mtwara, Njombe, and Ruvuma in providing services and testing for both communicable and non-communicable diseases, for the year 22/23, 1.1 million people were tested for HIV/AIDS, with 48,000 of them testing positive for the virus," Dr. Marina Njelekela explained.

On the other hand, the Chief of Party of the USAID Kizazi Hodari Southern, Ms. Doroth Matoyo, said that the five-year, $28.5 million project aims to assist orphaned and vulnerable children living in high-risk environments who, in one way or another, have been affected by HIV, It has reached more than 86,965 beneficiaries, including 56,527 women and 30,438 men, in 11 regions of mainland Tanzania and Zanzibar.

"The project has been highly successful in providing HIV services as well as services that improve nutrition, health, education, prevention, mental health, and life skills," said Ms. Doroth.

On his party Mr. Carlton Jones, the Director Advisory of Deloitte Tanzania, emphasized the importance of Tanzanians adhering to best health practices, as despite various efforts, the rate of infection remains unsatisfactory, he noted that the current perception of HIV as a common disease within the community leads to the disregard of health professionals' advice.

Earlier, the Deloitte Tanzania Director of Results Management, Dr. Moses Ringo, emphases the significance of using HIV antiretroviral drugs, highlighting that it is crucial in the fight against the disease. “When a person uses medication to suppress the virus to below 50 copies in their blood, the likelihood of transmitting it to others decreases,” said Dr. Ringo.

Both projects, each spanning five years, began with the USAID Afya Yangu Southern Project on November 9, 2021, and the USAID Kizazi Hodari Southern Project on March 24, 2022, serving the regions of Iringa, Njombe, Ruvuma, Lindi, Mtwara, Rukwa, Katavi, Songwe, Pwani, Morogoro, and Mjini Magharibi in Zanzibar.
Share:

Thursday, September 14, 2023

TANZANIA BLOGGERS EAGER TO COLLABORATE WITH USA IN MEDIA TRAINING

The Tanzania Bloggers Network (TBN), today held an informal gathering and luncheon with Ms. Jeanne Clark and Kalisha Holmes, US Embassy's Public Affairs Officer and Press and Information Officer respectively, at the Serena Hotel in Dar es Salaam.

During the meeting, senior TBN members who attended discussed a number of issues with the officers, including the current and future plans of the association.

"We shared our vision of developing the association further to enhance the promotion of the valuable work carried out by our members since its inception in early 2015", TBN founding member Josephat Lukaza said.

"We were thrilled to learn of the American Embassy's keen interest in the work of online journalists and their commitment to collaborating with TBN", said John Bukuku, another veteran blogger.
The TBN members expressed gratitude to the US Embassy for expressing interest in providing training opportunities to enhance professionalism and adhere to the ethical standards of journalism, saying that the move was truly encouraging.

"We believe that such collaborations will play a pivotal role in uplifting the standards of online journalism in Tanzania".

"Your dedication to fostering a supportive and empowering environment for bloggers and online journalists is inspiring. We are confident that this partnership will contribute significantly to the growth and development of our association, as well as the broader media landscape in Tanzania", pioneering blogger Issa Michuzi said.

Michuzi added: "We are excited about the potential for future collaborations and the positive impact they will have on our members and the Tanzanian blogging community as a whole".
Share:

Tuesday, June 20, 2023

Benki ya Absa yajitosa kuokoa maisha ya Watoto Njiti

  
Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete (kulia), akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser katika hafla ya makabidhiano wa msaada wa vifaa vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti) wakiwa hospitalini. Benki ya Absa imetoa ufadhili wa kiasi cha shs milioni 30 kwa taasisi ya Doris Mollel Kwa ajili hiyo. Kushoto ni Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Doris Mollel.
Rais Mstaafu wa awamu ya nne, mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akizunguza katika hafla ya makabidhiano wa msaada wa vifaa vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti) wakiwa hospitalini. Benki ya Absa imetoa ufadhili wa kiasi cha shs milioni 30 kwa taasisi ya Doris Mollel kwa ajili hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser(katikati), akizungumza katika hafla ya makabidhiano wa msaada wa vifaa vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti) wakiwa hospitalini. Benki ya Absa imetoa ufadhili wa kiasi cha shs milioni 30 kwa taasisi ya Doris Mollel Kwa ajili hiyo. Kushoto kwake ni Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais Mstaafu wa awamu ya nne, mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati), akikata utepe kuzindua hafla ya makabidhiano ya msaada wa vifaa vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti) wakiwa hospitalini. Benki ya Absa imetoa ufadhili wa kiasi cha shs milioni 30 kwa taasisi ya Doris Mollel kwa ajili hiyo.
Mkurugenzi wa taasisi ya Doris Mollel Foundation, Doris Mollel akitoa shukurani Kwa mgeni rasmi, benki ya Absa na wote wakiofanikisha upatikanaji wa vifaa hivyo vitakavyosaidia kuokoa maisha ya watoto nyiti wakiwa hospitalini.
Share:

Monday, May 8, 2023

Kampeni ya Upandaji miti yapamba moto katika Kijiji cha Green Village Estate Bunju Mabwepande

Naibu Kamishna na Mkurugenzi wa Uzalishaji Mbegu Bora za Miti na Vipando wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), SACC Caroline Malundo (katikati), akiwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Green Village Estate, Bwana Reeves Ngalemwa (kulia kwake), wakati akiwasili kijijini hapo akimwakilisha Kamishna wa Uhifadhi wa TFS, CC Prof. Dos Santos Silayo, kuhitimisha kilele cha kampeni ya upandaji miti 1000 iliyokuwa na malengo ya kuhamasisha wakazi wa Green Village na maeneo jirani umuhimu wa utunzaji wa mazingira kwa njia ya upandaji miti. Mti hiyo 1000 ilipatikana kwa ufadhili wa TFS Ofisi ya Kinondoni. Kushoto kabisa ni mwakilishi kutoka Shirika la Watumishi Housing Investment (WHI), Bwana Valentine Arra wamiliki wa kijiji hicho.
Naibu Kamishna na Mkurugenzi wa Uzalishaji Mbegu Bora za Miti na Vipando wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), SACC Caroline Malundo (katikati), akielezea namna bora ya upandaji miti alipoenda kuhitimisha kilele cha kampeni ya upandaji miti 1000 iliyokuwa na malengo ya kuhamasisha wakazi wa Green Village na maeneo jirani umuhimu wa utunzaji wa mazingira kwa njia ya upandaji miti.
Naibu Kamishna na Mkurugenzi wa Uzalishaji Mbegu Bora za Miti na Vipando wa Wakala wa Huduma za Misitu nchini (TFS), SACC Caroline Malundo, akipanda miti kuhitimisha kilele cha kampeni ya upandaji miti 1000 iliyokuwa na malengo ya kuhamasisha wakazi wa Green Village na maeneo jirani umuhimu wa utunzaji wa mazingira kwa njia ya upandaji miti. Mti hiyo 1000 ilipatikana kwa ufadhili wa TFS Ofisi ya Kinondoni. Naibu Kamishna alimwakilisha Kamishna wa Uhifadhi wa TFS, CC Prof. Dos Santos Silayo.
Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kipolisi ya Mabwepande Colle Mohamed Senkondo, akipanda mti katika hafla ya kuhitimisha kampeni ya upandaji miti 1000 katika Kijiji cha Green Village Estate, Bunju Mabwepande, Kinondoni, Dar es Salaam hivi karibuni.
Kiongozi wa kiroho wa Kanisa la KKKT Mabwepande, Anna Mbaga, naye alipata heshima ya kupanda mti wa kumbukumbu katika hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Green Village Estate, Bwana Reeves Ngalemwa akizungumza katika hafla hiyo pamoja na mambo mengine alitoa taarifa ya maendeleo ya kijiji pamoja mkakati endelevu wa kampeni ya utunzaji wa mazingira kijijini hapo. Alisema tuzo licha ya tuzo iliyozinduliwa kushindanisha wanakijiji ili kumpata mtunza mazingira bora lakini mipango imo mbioni ya kuwa na tuzo yenye wigo mpana wa washiriki wake itakayowashirikisha watu kutoka nje ya kijiji.
Naibu Kamishna na Mkurugenzi wa Uzalishaji Mbegu Bora za Miti na Vipando wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), SACC Caroline Malundo akihutubia kwa niaba ya Kamishna wa Uhifadhi wa TFS, CC Prof. Dos Santos Silayo katika hafla hiyo kuhitimisha kampeni ya upandaji miti 1000 iliyopatikana kwa uwezeshaji wa TFS. Katika hotuba yake, Naibu Kamishna alitoa hamasa kwa watanzania kuona umuhimu wa kupanda miti kwani takwimu zinaonyesha kuna uharibifu wa misitu wa takribani hekta 412,000 kwa mwaka huu unaosababishwa na shughuli za kibinadamu.
Naibu Kamishna na Mkurugenzi wa Uzalishaji Mbegu Bora za Miti na Vipando wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), SACC Caroline Malundo (wa pili kulia), akipokea Tuzo ya Mazingira ya Green Village Estate Mazingira Award 2023 kwa niaba ya Kamishna wa Uhifadhi wa TFS, CC Prof. Dos Santos Silayo kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mazingira, Afya na Miundombinu ya kijiji hicho, Dk. Rehema Simba (wa tatu kushoto), wakati akizindua rasmi tuzo hiyo itakayotolewa kila mwaka. Mshindi wa tuzo hiyo atakapatikana kutokana na vigezo vilivyowekwa na kamati hiyo. Lengo ikiwa ni kuhamasisha wanakijiji na wakazi wa maeneo ya jirani umuhimu wa kutunza mazingira kwa njia ya kupanda miti.
Katibu wa Kamati ya Mazingira, Afya na Miundombinu wa Green Village Estate, Bwana Andrew Tarimo (kulia), akimkaribisha Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kipolisi ya Mabwepande, OCD Colle Mohammed Senkondo, ambapo yeye pamoja na Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Mabwepande, ASP Goodluck Lema (wa pili kushoto), wakiwa baadhi ya wageni maalumu walioalikwa katika hafla hiyo. Wengine kutoka kushoto ni, Bi. Tumaini Masako, mjumbe wa kamati ya mazingira, Mwenyekiti wa Kijiji, Bwana Reeves Ngalemwa na Mjumbe wa Kamati ya Burudani, Bwana Swalehe Kweka (wa pili kulia).
Ni shangwe tu….Mwenyekiti wa Green Village Estate, Bwana Reeves Ngalemwa (kulia), Katibu wa Kijiji, Bwana Pantaleo Shoki (kushoto), wakimlaki Naibu Kamishna na Mkurugenzi wa Uzalishaji Mbegu Bora za Miti na Vipando wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), SACC Caroline Malundo mara baada ya kuwasili kuhitimisha kilele cha kampeni ya upandaji miti 1000 zoezi lililoratibiwa kwa ufanisi na Kamati ya Mazingira, Afya na Miundombinu ya kijiji hicho. Wa pili kulia ni Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kipolisi ya Mabwepande, OCD Colle Mohammed Senkondo.
Timu ya ushindi! Wanakamati wa Kamati ya Mazingira, Afya na Mazingira chini ya uenyekiti wa Dk. Rehema Simba wakipiga picha ya kumbukumbu na mgeni rasmi, viongozi wa Green Vilage pamoja na baadhi ya wageni maalumu walioalikwa katika hafla hiyo.
Baadhi ya wakazi wa Green Village Estate pamoja na mwakilishi kutoka Watumishi Housing wakipozi mbele ya wapiga picha pamoja na mgeni rasmi na wageni wengine waalikwa mara baada ya kumalizika kwa tukio hilo.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive