A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Wednesday, December 27, 2023

BAYPORT YANOGESHA ROMBO MARATHON

Naibu Waziri Mkuu, Dk. Doto Biteko akikabidhi cheti cha shukurani kwa Meneja Rasilimali Watu wa Taasisi ya Kifedha ya Bayport, Bi. Evalyn Hall (kulia), kutambua mchango wa kampuni hiyo kama mdhamini mkuu wa mbio za Rombo Marathon 2023 zilizotimua vumbi lake mjini Rombo mkoani Kilimanjaro jana. Kulia kwa Naibu waziri mkuu ni Waziri wa Elimu na Mbunge wa Rombo, Prof. Adolf Mkenda na kushoto kwake ni Waziri Biteko ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bwana Nurdin Babu.
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Taasisi ya Kifedha ya Bayport, Bwana Nderingo Materu (wa pili kushoto), Mkuu wa Mauzo wa kampuni hiyo, Bwana Lugano Kasambala (kushoto kwake), pamoja na wakimbiaji wengine, wakishiriki mbio za Rombo Marathon mjini Rombo, Kilimanjaro jana. Mbio hizo zilizodhaminiwa na Bayport, zina lengo la kuhamasisha vivutio vya utalii mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bwana Nurdin Babu (kulia), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi ya Kifedha ya Bayport, wakishiriki mbio za Rombo Marathon mjini Romb, Kilimanjaro jana. Mbio hizo zilizodhaminiwa na Bayport, zina lengo la kuhamasisha vivutio vya utalii mkoani humo.

Na mwandishi wetu, Rombo, Kilimanjaro

TAASISI ya Kifedha ya Bayport imenogesha na kufanikisha mbio za Rombo Marathon 2023 zilizofanyika mjini Rombo, Kilimanjaro jana, zikiwa na lengo la kuhamasisha vivutio vya utalii wilayani humo.

Ikiwa ni mwaka wa pili sasa Rombo Marathon imefanyika ikihudhuriwa na viongozi wa kiserikali, wageni, na watu mashuhuri huku mgeni rasmi akiwa Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe, Dk. Doto Biteko.

Akizungumza wakati wa mbio hizo, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Bayport, Bwana Nderingo Materu alisema Bayport ilikubali kuwa mdhamini Rombo Marathon ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali pamoja na muasisi wa mbio hizo, Waziri wa Elimu na Mbunge wa Rombo, Prof. Adolf Mkenda katika kukuza utalii pamoja na suala zima la uhifadhi wa mazingira.

Kama mnavyofahamu sisi Bayport tumekuwa namba moja katika suala la utunzaji wa mazingira kwa njia ya upandaji miti, leo hii tumeamua kudhamini Rombo Marathon na tutaendelea kuunga mkono juhudi zozote nchini zenye lengo la kukuza utalii na kuhifadhi mazingira."

Lakini pia kama inavyofahamika umuhimu wa kufanya mazoezi ya mwili kwa ajili ya ubora wa afya za wafanyakazi na familia zetu, tunaamini mbio hizi zitaleta hamasa pia kwa watanzania kutilia mkazo umuhimu wa kufanya mazoezi ili kujiepusha na magonjwa yasiyo ya kuambukiza,” alisema Bwana Materu.
Katika hotuba yake, Naibu Waziri Mkuu, Mhe, Dk. Biteko alitoa pongezi kwa waandaaji na wadhamini wa mbio za Rombo Marathon akisema zimekuwa na mafanikio makubwa lakini kikubwa ikiwa ni kujifunza utamaduni wa wana Rombo pamoja ya vivutio vya utalii vinavyopatikana katika wilaya na mkoa huo.

Natoa pongezi nyingi kwa muasisi wa Rombo Marathon, Waziri wa Elimu na Mbunge wa Rombo, Prof. Mkenda, natoa pongezi kwa serikali ya Mkoa wa Kilimanjaro, Wilaya ya Rombo bila kuwasahau wadhamini wote waliojitolea rasilimali zao kufanikisha tukio hili."

Serikali chini ya Rais, Mhe, Dk. Samia Suluhu Hassan itaendelea kuunga mkono juhudi yoyote inayofanywa yenye lengo la kuwaletea maendeleo watu wa Rombo na kwa watanzania kwa ujumla,” alisema Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu.

Naye Waziri wa Elimu, Mbunge wa Rombo na muasisi wa mbio hizo, Prof. Adolf Mkenda alitoa shukurani zake kwa Mhe. Naibu Waziri Mkuu, Dk. Biteko kwa kukubali kuwa mgeni rasmi pamoja na wadhamini wa mbio hizo Taasisi ya Kifedha ya Bayport kwa kufanikisha tukio hilo muhimu kwa maendeleo ya watu wa Rombo na wananchi wa Kilimanjaro.

Namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu kwa kuungana na wana Rombo katika kushiriki tukio hili, natoa pia shukrani kwa wadhamini wote waliowezesha kufanya tukio hili kuwa lenye ubora ikiwemo Taasisi ya Bayport Financial Services,” alisema Prof. Mkenda.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bwana Nurdin Babu, alichukua nafasi hiyo kuwakaribisha wageni wote wanaotoka ndani na nje ya Tanzania kwenda kuangalia vivutio vya utalii mkoani humo akisema Kilimanjaro ipo salama na wapo tayari kuwapokea na kuwahudumia.
Mbio za Rombo Marathon zinazofanyika kwa mwaka wa pili sasa zimeshirikisha mbio za Km 21, Km 10 na mbio za kujifurahisa za kilomita 5.
Share:

Thursday, December 21, 2023

Filamu za kibongo zote kali kuonekana kupitia Airtel TV

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Dk. Kiagho Kilonzo (katikati), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati Kampuni ya Airtel Tanzania ikitambulisha filamu za kitanzania zaidi ya 100 ambazo wapenzi wa filamu wanaweza kuziangalia kupitia Airtel TV inayopatikana ndani ya aplikesheni ya Airtel App. Kati ya filamu hizo zimo za washindi na washiriki wa Tuzo za Filamu Tanzania zilizofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kulia ni Meneja Bidhaa wa Airtel App, Bwana James Gua na kushoto ni msanii nguli wa vichekesho nchini na Balozi wa Airtel Money, Lucas Lazaro Mhuville ‘Joti’.
Meneja Bidhaa wa Airtel App, Bwana James Gua (kulia), akionyesha baadhi ya filamu za kitanzania zinazoonyeshwa katika Airtel TV, wakati Airtel Tanzania ikitambulisha filamu za kibongo zaidi ya 100 ambazo wapenzi wa filamu wanaweza kuziangalia kupitia Airtel TV inayopatikana ndani ya aplikesheni ya Airtel App. Kati ya filamu hizo zimo za washindi na washiriki wa Tuzo za Filamu Tanzania zilizofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Katikati ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Dk. Kiagho Kilonzo na msanii nguli wa vichekesho nchini na Balozi wa Airtel Money, Lucas Lazaro Mhuville ‘Joti’.
Msanii nguli wa vichekesho na Balozi wa Airtel Money, Lucas Lazaro Mhuville ‘Joti’ (kushoto0, akizungumza katika hafla hiyo huku akitoa hamasa kwa wasanii wenzake kupeleka kazi zao Airtel TV na pia kupakua Airtel App kwani Airtel imekuja kivingine katika kuwapa watanzania burudani za filamu za kibongo na kutoa fursa za kiuchumi kwa wasanii. Kushoto kwake ni Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Dk. Kiagho Kilonzo na Meneja Bidhaa wa Airtel App, Bwana James Gua.

*Ni fursa kwa wasanii pia kujiongezea kipato

WAPENZI wa filamu za kibongo, wana kila sababu ya kufurahia msimu huu wa sikukuu za mwisho wa mwaka, mara baada ya Kampuni ya Simu za Mkononi ya Airtel Tanzania, kupitia Aplikesheni yake ya (Airtel App), kuweka filamu zaidi ya 100 katika Airtel TV inayopatikana katika App hiyo inayowawezesha watanzania kuangalia filamu hizo kwa urahisi na kwa unafuu mahali popote walipo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo katika hafla ya kutambulisha filamu hizo ambayo pia ilihudhuriwa na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Dk. Kiagho Kilonzo, Meneja Bidhaa wa Airtel App, Bwana James Gua alisema filamu hizi 100 nzuri kwani kati yake zimo za washindi na washiriki wa Tuzo za Filamu Tanzania 2023 zilizofanyika jijini humo hivi karibuni.

Tunayo furaha kubwa kuwajulisha wapenzi wa burudani za filamu za kitanzania kuwa sasa Kampuni ya Airtel kupitia Airtel App tumeweka filamu kali zaidi ya 100 za washiriki na washindi wa mwaka huu wa Tuzo za Filamu nchini pamoja na aina nyingine za burudani hivyo ni wakati mzuri kwa wazazi na familia kuwa na wakati mzuri wa kufurahia katika kipindi hiki cha sikukuu za mwisho wa mwaka."

Airtel App ni rahisi kuipakua na kuanza kupata huduma mbalimbali zikiwemo huduma mbalimbali za Airtel Money kama vile kutuma na kutoa pesa kwa wakala, kufanya malipo ya huduma mbalimbali na sasa kwa kupitia Airtel TV inayopatikana ndani ya app hiyo tumewaletea burudani ya aina yake ya filamu za kitanzania zenye ubora ili kukonga nyoyo za wateja wetu wenye kiu ya kuangalia filamu za kikwetu”, alisema Bwana Gau.

Naye Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Dk. Kiagho Kilonzo aliishukuru Kampuni ya Airtel kwa udhamini wake katika tuzo za filamu za mwaka huu zikishindanisha filamu kutoka Tanzania na nje ya Tanzania katika nchi za Afrika Mashariki akisema umechangia kwa kiasi kikubwa katika kufanikisha tuzo hizo kufanyika katika viwango vyenye ubora wa kimataifa.

Kwa niaba ya Bodi ya Filamu Tanzania ningependa kuchukua fursa hii kuishukuru kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania kwa kuthamini maendeleo ya tasnia ya filamu nchini na kwa maendeleo ya wasanii wetu kwani kati ya filamu 565 zilizopokelewa mwaka huu, filamu 535 zilitoka nchini na 30 tu ndio zilitoka nje ya nchi."

Natoa wito kwa wasanii wote nchini kuleta filamu zenu zenye vigezo na zilizopata kibali kutoka katika Bodi ya Filamu Tanzania ili ziweze kupakiwa katika Airtel App ziweze kutazamwa na kuwapa burudani wapenda filamu za kitanzania nchini lakini pia zitumike kama fursa ya kujiongezea kipato kwenu wasanii”, alisema katibu mtendaji huyo.

Naye mmoja ya wasanii nguli wa vichekesho nchini na Balozi wa Airtel Money, Lucas Lazaro Mhuville ‘Joti’ ambaye katika tuzo za mwaka huu alijinyakulia tuzo kwa miaka mitatu mfululizo ya Filamu Bora ya Uchekeshaji alitoa hamasa kwa wasanii kupeleka kazi zao Airtel TV na pia kupakua Airtel App kwani Airtel imekuja kivingine katika kuwapa watanzania burudani za filamu za kibongo na kutoa fursa za kiuchumi kwa wasanii.
Share:

Friday, December 8, 2023

Waziri Nape azipongeza Airtel, Jubilee Insurance na Axieva kuanzisha Afya Bima

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (katikati), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu huduma mpya ya Afya Bima inayotolewa na Airtel Money kwa ushirikiano na makampuni ya Jubilee Insurance na Axieva. Waziri Nape alisema Afya Bima itasaidia kuokoa maisha ya watanzania wengi kiafya na kiuchumi. Wengine ni viongozi kutoka makampuni hayo.
Mkurugenzi wa Airtel Money, Bwana Charles Rugambwa (kulia), akizungumza katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam leo kuhusu huduma ya Afya Bima inayopatikana kwa wateja wote wa Airtel Money wenye simu janja na za kawaida.. Kulia kwake ni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye na Mkurugenzi Mtendaji wa Jubilee Insurance, Dk. Harold Adamson.
Mkurugenzi Mkuu wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Bi. Beatrice Singano (kushoto), akizungumzia faida mbalimbali watakazozipata wateja wa Airtel Money kwa kujiunga na huduma mpya ya Afya Bima wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Axieva, Davrav Dhingra, akizungumza katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam leo. Kulia kwakwe ni Mkurugenzi wa Airtel Money, Bwana Charles Rugambwa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye.

*Asema itaokoa maisha ya watanzania na kuwapunguzia umasikini.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Technolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye amezipongeza kampuni ya Airtel Tanzania kwa ushirikiano wake na kampuni za Jubilee Insurance pamoja na Axieva kwa kuanzisha huduma Afya Bima, akisema huduma hiyo imekuja wakati muafaka katika kipindi hiki ambacho Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan akisaini muswada wa Bima ya Afya kwa Wote ili kuwapa fursa watanzania wengi zaidi kunufaika na mpango huo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, wakati akitambulishwa rasmi huduma hiyo, Waziri Nape alisema, huduma ya Afya Bima itakayotolewa Airtel kwa kushirikiana na Jubilee Insurance pamoja na Axieva itaenda kuokoa maisha na uchumi wa watanzania wengi ambao hawakuwa katika mfumo wa bima ya afya hivyo kulazimika kutumia pesa taslimu na wakati mwingine kulazimika kuuza rasilimali zao ili kujitibu wao ama wategemezi wao.

Nichukue nafasi hii kuzipongeza Airtel Tanzania, Jubilee Insurance pamoja Axieva kwani huduma hii inapatikana kirahisi kwa njia ya kidigitali kupitia Airtel Money hivyo kuwafanya watanzania wengi zaidi kujiunga mahali popote walipo bila usumbufu."

Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan imefanya uwekezaji mkubwa katika kuongeza miundo mbinu mingi ya kutoa huduma za afya, ujenzi wa zahanati katika ngazi ya vijiji, vituo vya afya katika ngazi ya kata, hospital za halmashauri, hospital za rufaa za mikoa, hospital za Kanda pamoja na hospital za kitaifa hivyo ujio wa Afya Bima utasaidia watanzania wengi kuweza kunufaika na huduma bora za afya zitolewazo katika hospitali za umma”, alisema Waziri Nape.

Waziri Nape aliongeza kuwa uwekezaji wa Serikali katika kutengeneza miundombinu ya afya hautakuwa na maana kama wananchi watakuwa wanapata huduma hizo kwa kusuasua na ndiyo maana Serikali ya Awamu ya Sita ikaamua kusukuma ajenda ya Bima ya afya kwa wote.

Jambo kubwa ni kwamba Bima hii, imewalenga watanzani wote hasa ambao hawana uwezo wa kuweza kujigharamia matibabu pindi wakipata shida ya kuumwa kama madereva bodaboda na Mama ntilie kwa hiyo jambo hili ni suluhisho kubwa kwao kupata huduma za afya huku Maisha yao yakiendelea”, Alisema Waziri Nape.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Airtel Money, Bwana Charles Rugambwa alisema huduma ya Afya Bima ni moja ya mikakati ya Airtel katika kuwaletea watanzania huduma bora za kiubunifu na rahisi kujiunga kwa njia ya kidigitali ambapo wateja wote wa Airtel Money wanaweza kujiunga kwa kutumia simu janja na ya kawaida.

Kwa kuwa huduma ya Afya Bima ni kwa ajili ya watu wote na hiki ni kipindi cha msimu wa sikukuu za kuelekea mwaka mpya, natoa wito kwa wateja wa Airtel Money kuwapa zawadi wapendwa wao kwa kuwalipia vifurushi ya Afya Bima, hii ni zawadi ya ukweli."

Ni rahisi kujiunga, mteja wa anachotakiwa kufanya ni kuingia katika menu ya Airtel Money kisha anaingia namba 6, Huduma za kifedha, kisha 2, Bima, kisha 2 tena, Afya Bima, kisha kuthibitisha na baadae kuchagua aina ya vifurushi ukitakacho”, alisema Bwana Rugambwa.

Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bima ya Jubilee, Dk. Harold Adamson amesema kuwa wamefarijika kuwapata wadau ambao wameshirikiana nao katika kuongeza thamani ya tehama na kuhudumia moja kwa moja kwenye Maisha ya watanzania wote.

Sisi kama Jubilee tumefarijika kuweza kupata wadau wenzetu ili kuanzisha huduma na bidhaa hii mpya kwa watanzania hasa wanaotumia mtandao wa airtel, bidhaa hii ya afya bima inaunga mkono juhudi za Mhe. Rais za kuhakikisha watanzania wote wanafikiwa na bima ya afya”, Alisema Dkt. Adamson.

Akitaja baadhi ya manufaa na Afya Bima, Dk. Adamson alisema, Afya Bima inakuja na bima za afya aina tatu ambazo ni Afya Poa, Afya Supa na Afya Dhahabu ambapo mteja ataweza kuchagua vifurushi tofauti kulingana na uhitaji wake.

Bima ya Afya Poa inalenga kurudisha mapato yaliyopotea wakati mgonjwa alipolazwa ambapo mgonjwa anapokuwa amelazwa atakuwa anarudishiwa gharama kati ya Tzs 20,000 mpaka Tzs 50, 000, vile vile, Afya Poa inatoa faida ya bima ya gharama za mazishi ya mpaka Tzs 1 milioni moja, ajali, ulemavu au kifo faida ya mpaka Tzs 500,000 na vifurushi vyake gharama yake kati ya Tzs 6,000, Tzs 7,000 mpaka Tzs 35, 0000 kulingana na uhitahitaji wake.

Kwa upande Afya Supa na Afya Dhahabu zinatoa faida kwa mteja kupata huduma za matibabu bila malipo, Afya Supa inampa mteja kupata gharama ya matibabu ya hadi Tzs 5 milioni na hii ni pamoja na mteja aliyelazwa au kupata matibabu ya bila kulazwa. Bima hii ina kufurushi cha kulipia kati ya Tzs 15,000 mpaka Tzs 45,000 kwa mwaka kulingana na mahitaji ya mteja, lakini pia Afya Supa inakuja na faida ya uzazi ya gharama ya hadi Tzs 2 milioni”, alisema.

Awali Mkurugenzi Mkuu wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania, Bi. Beatrice Singano amesema kuwa kampuni hiyo inatekeleza maelekezo yaliyotolewa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ya kuhakikisha watoa huduma kupitia Tehama wanatumia ujuzi huo kuwasaidia wananchi wa aina zote na kuipa thamani sekta hiyo.

Alisema kuwa Huduma na Bidhaa mpya ya Afya Bima itakwenda kwa watanzania wapatao milioni 17.5 wanaotumia mtandao huo kuweza kupata matibabu kwa bei nafuu katika vituo zaidi ya 600 nchini na kuwawezesha wananchi kuwa na unafuu wakati wa shida ya kuumwa na kusimama kufanya kazi.

Mteja anayejiunga na Afya Bima ataweza kupata huduma ya matibabu kulingana na hospitali ambazo Wizara ya Afya Imesajili ambazo ni Hospitali za Umma, hospitali za kibinafsi na za Misheni kulingana na orodha iliyotolewa.
Share:

Wednesday, December 6, 2023

Benki ya Absa Tanzania yazindua mfumo wa malipo ya kadi za benki kupitia simu za mkononi

Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Lilian Swere (wa nne kutoka kushoto, mstari wa mbele), Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo, Bwana Aron Luhanga (kushoto kwake), wakipozi kwa picha mbele ya waandishi wa habari wakati wa uzinduzi rasmi mfumo wa malipo ya kadi za benki kupitia simu za mkononi ‘Absa Tanzania Mobi Tap’ jijini Dar es Salaam leo.
Meneja Mauzo na Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Frank Mboya (kushoto), akionyesha jinsi mfumo wa malipo ya kadi za benki kupitia simu za mkononi unavyofanya kazi kwa waandishi wa habari, katika hafla ya uzinduzi rasmi wa mfumo huo, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto kwake ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano, Bwana Aron Luhanga, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Lilian Swere na Meneja Bidhaa na Kadi, Bi. Elfrida Mruma.
Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Aron Luhanga (katikati) akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa mfumo wa malipo ya kadi za benki kupitia simu za mkononi 'Absa Mobi Tap' katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka kushoto ni; Meneja Mauzo na Biashara, Bwana Frank Mboya, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Lilian Swere na Meneja Bidhaa na Kadi, Bi. Elfrida Mruma.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Lilian Swere (katikati) akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa mfumo wa malipo ya kadi za benki kupitia simu za mkononi 'Absa Mobi Tap' katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka kushoto ni; Meneja Mauzo na Biashara, Bwana Frank Mboya, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano, Bwana Aron Luhanga na Meneja Bidhaa na Kadi, Bi. Elfrida Mruma.

Absa MobiTap inawezesha wauzaji kupokea malipo ya kadi za benki kutoka kwa wateja kwa kutumia simu janja kama mashine ya kuchanjia kadi.

Benki ya Absa Tanzania imezindua Absa Mobi Tap – ambayo ni suluhisho la kwanza la aina yake nchini Tanzania ambalo linawawezesha wafanyabiashara wadogo wadogo na wa kati (SMMEs) kutumia simu zao kwa ajili ya kuchakata miamala ya kadi za benki na kuondoa hitaji la mashine za kuchanjia kadi, yaani POS.

Absa MobiTap inatarajiwa kuharakisha mchakato wa ulipiaji wa bidhaa kwa wanunuzi na wauzaji kwa kutumia simu janja kama mashine ya kuchanjia kadi. Wateja wanaweza tu kugusa kadi zao za benki kwenye simu ya muuzaji ya Android au kompyuta kibao ili kufanya malipo.

Kwa upande wa wafanyabiashara, wanachohitaji kufanya ni kupakua programu ya Absa Mobi Tap kutoka Play Store kwenye simu zao janja. Baada ya hapo wataweka taarifa zao na kuunganishwa na kuwa tayari kupokea malipo ya kadi za benki. Ili kuchakata malipo, mfanyabiashara ataingiza kiasi cha manunuzi kwenye program ya Absa MobiTap, kisha mteja atagusisha kadi yake nyuma ya simu hiyo na kuingiza PIN yake ikiwa inahitajika na kukamilisha malipo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Ndabu Swere, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi, alisema kuanzishwa kwa Absa Mobi Tap ni ushahidi wa mkakati wa benki hiyo kuendelea kujikita katika kujenga kampuni ya kisasa ya kidijitali ambayo inaenda na nyakati na mahitaji ya wateja.

Kama benki inayoongozwa kidijitali, tumejitolea kuongoza njia katika uvumbuzi wa kidijitali na tutaendelea kuzindua suluhisho nyingi za kidigitali za ubunifu wa hali ya juu ambazo zinakidhi mahitaji ya wateja wetu ya sasa na ya baadae, na kuhakikisha kuwa bidhaa zetu zimeundwa kushughulikia changamoto ambazo wateja wetu wanakabiliwa nazo.

Absa MobiTap ni suluhisho la kwanza la aina yake hapa nchini na tunajivunia kuwa benki ya kwanza kuwaletea Watanzania suluhisho la malipo ya kidigitali la ubunifu huu wa kipekee.

Tunaamini suluhisho hili litaleta mapinduzi katika namna ambayo wafanyabiashara wadogo wadogo na wa kati nchini yanavyoendesha biashara zao, kwani itaondoa vizuizi na kupanua chaguzi katika upatikanaji wa huduma za malipo ya kidijitali.

Biashara nyingi ndogo ndogo hazikuweza kupata mashine za POS kwa sababu ya uwekezaji mzito unaohitajika kwaajili ya hizo mashine. Lakini Absa MobiTap amekuja kuleta ufumbuzi kwenye hili.

Sasa hata dereva wa Uber/Bolt anaweza kupokea malipo ya kadi kupitia simu yake ya mkononi ambayo ni njia salama, ya haraka, na rahisi kwa wote – wanunuzi na wauzaji. Dhama hii ya kuwezesha wafanyabiashara wa aina zote inaenda sambamba na kusudi letu la ‘Kuwezesha Afrika ya kesho, pamoja, …hatua moja baada ya nyingine’.

Kwa upande wake, Aron Luhanga, Mkuu wa Kitengo Mawasiliano, Masoko na Mahusiano, alisema suluhisho hili la Absa MobiTap ni moja ya mengi ambayo benki itaendelea kutoa katika ufumbuzi wa malipo ya kidijitali wakati Absa inaendelea kuimarisha nafasi yake kama kinara katika nyanja hiyo hapa nchini.

Alisema, “MobiTap inaruhusu wauzaji kutumia teknolojia ambayo tayari wanayo – simu janja, karibuni kila mfanyabiashara siku hizi ana simu janja. Hata hivyo, mtej wetu akiwa hana simu janja, na anahitaji kujiunga na Absa MobiTap, tutampatia simu bure ili kumfanikisha.

Kwa mujibu wa Aron, suluhisho hili kimsingi linalenga wafanyabiashara wadogo na wa kati (SMEs), hasa wale ambao hapo awali walitegemea malipo kwa fedha taslimu au uhamishaji wa kielektroniki (EFT). Wafanyabiashara mbalimbali, kama vile madereva wa Uber/Bolt, migahawa, saluni, maduka ya vifaa, wakulima, wote wanaweza kutumia fursa hii ya uvumbuzi kuwasaidia kuendesha biashara zao kwa ufanisi zaidi.

Katika hotuba yake ya kuhitimisha, Ndabu, alitoa wito kwa wafanyabiashara wote – wafanyabiashara wa ukubwa wote (wadogo na wa kati) kutumia fursa ya Absa MobiTap kuwezesha biashara zao kupokea malipo ya kadi za benki kwa njia ya haraka, rahisi, na salama zaidi, ili kuwezesha kukuza jamii ya kidijitali, isiyotembea na pesa taslimu kwa faida ya wote.
Share:

Thursday, November 30, 2023

MKAZI WA KINONDONI MANYANYA AJISHINDIA PIKIPIKI KUPITIA DROO YA Y9 MICROFINANCE

 

Meneja Masoko wa Taasisis ya Kifedha ya Y9 microfinance Bi Sophia Mang’enya (kulia), akikabidhi zawadi ya pikipiki kwa mshindi wa droo ya nane Bw.Anold Jacob ambae aliibuka mshindi  wakati wakuchezesha droo hiyo wiki iliyopita ikiwa nimuendelezo wa Taasisi hiyo kutoa zawadi kila wiki kwa wateja wake wa Pakua APP ya Y9 na ukope na ulipe kwa wakati ili kuingia kwenye droo na ushine zawadi ya simu janja na pikipiki. hafla ya makabidhiano hayo yamefanyika nyumbani kwa kina  Anold kinondoni manyanya jijini Dar es Salaam. Na baada ya wiki mbili itachezeshwa droo kubwa ambapo mshindi atajinyakulia Gari mpya kabisa Toyota Ist.

Meneja Masoko wa Taasisi ya Kifedha ya Y9 microfinance Bi Sophia Mang’enya (kulia), akizungumza wakati wa hafla yakukabidhi zawadi ya pikipiki kwa mshindi wa droo ya saba Anold Jacob ambae aliibuka mshindi  wakati wakuchezesha droo hiyo wiki iliyopita ikiwa nimuendelezo wa Taasisi hiyo kutoa zawadi kila wiki kwa wateja wake wa Pakua APP ya Y9 na ukope na ulipe kwa wakati ili kuingia kwenye droo na ushinde zawadi ya simu janja na pikipiki hafla ya makabidhiano hayo yamefanyika nyumbani kwa kina  Anold kinondoni manyanya jijini Dar es Salaam na baada ya wiki mbili itachezeshwa droo kubwa ambapo mshindi atajinyakulia Gari mpya Toyota Ist.

Mshindi wa pikipiki wa wa Pakua APP ya Y9 Microfinance ushinde Bw. Anold Jacob akionesha ufunguo wa pikipiki mara baada ya kukabidhiwa na Meneja Masoko wa Taasisis ya Kifedha ya Y9 microfinance Bi Sophia Mangenya wakati wa hafla yakukabidhi zawadi ya pikipiki kwa mshindi wa droo ya nane . Na baada ya wiki mbili itachezeshwa droo kubwa ambapo mshindi atajinyakulia Gari mpya Toyota Ist.

Mshindi wa pikipiki wa wa Pakua APP ya Y9 Microfinance ushinde Bw. Anold Jacob akionesha plate namba na kadi ya pikipiki mara baada ya kukabidhiwa na Meneja Masoko wa Taasisis ya Kifedha ya Y9 microfinance Bi Sophia Mangenya wakati wa hafla yakukabidhi zawadi ya pikipiki kwa mshindi wa droo ya nane . Na baada ya wiki mbili itachezeshwa droo kubwa ambapo mshindi atajinyakulia Gari mpya Toyota Ist
Share:

Wednesday, November 29, 2023

Sabasaba Moshingi, kuipeleka DCB kwenye kilele cha mafanikio

Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Benki ya Biashara ya DCB, Bwana Sabasaba Moshingi (katikati), akizunguza mara baada ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo, Bi. Zawadia Nanyaro (kushoto kwake), kumtambulisha rasmi jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka kushoto ni Katibu wa Benki, Bi. Regina Mduma, Mkurugenzi wa Biashara, Bi. Lilian Mtali na Ofisa Fedha Mkuu, Bwana Deusdedit Mulindwa.

Benki ya Biashara ya DCB, moja kati ya benki kongwe inayoongoza katika mabenki yenye ukubwa wa kati, imemtambulisha Mkurugenzi Mtendaji wake mpya katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Akizungumza, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro alimtambulisha Bwana Sabasaba Moshingi, kuchukua nafasi hiyo adhimu ya kushika usukukani wa kuongoza benki hiyo akisema, licha ya mchakato kuchukua muda mrefu lakini kama benki pamoja na wanahisa wake wanayo furaha kwa kumtapata mtu anayekidhi vigezo walivyohitaji.

Benki yetu, wateja wetu pamoja na wanahisa wake walihitaji mtu sahihi atakayesukuma mbele vyema gurudumu la maendeleo la DCB, kwa weledi, umakini na uhakika zaidi, atakayeweza kuitoa DCB mahali ilipo na kuipeleka mbele zaidi kimafanikio, na baada ya kupitia hatua na taratibu kadhaa Bodi na Menejimenti ya DCB zina kila sababu ya kutembea vifua mbele kwa kumpata mtu sahihi ambaye kutokana na ukongwe wake katika tasnia za kibenki na taasisi za fedha tuna imani matarajio yetu yametimia."

Bwana Moshingi ni Mtaalamu mbobevu katika masuala ya benki kwa zaidi ya miaka 12, Bwana. Moshingi, analeta pamoja naye hazina kubwa ya uzoefu katika tasnia za kibenki za Kitaifa na Kimataifa akiwa na rekodi thabiti katika Uendeshaji wa Benki, Biashara za Fedha, Huduma za Kibenki kwa Wateja Binafsi, Masuala ya Mikopo na mengineyo."

Bwana Moshingi ana Shahada ya Uzamili ya Utawala wa Biashara katika Fedha kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, amethibitishwa na Taasisi ya Mabenki Tanzania na kabla ya uteuzi wake wa sasa, Bw. Moshingi alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TCB akishika pia nafasi mbalimbali za uongozi katika benki za, Standard Chartered, Stanbic na KCB."

Ni matumaini ya benki yetu, wateja wetu na wanahisa wetu kuwa ujio wa Bwana Moshingi umekuja kwa wakati sahihi na kutokana na historia iliyotukuka ya mafanikio aliyoyapata katika taasisi alizowahi kufanya kazi, tunaiona benki yetu ikizidi kupanda kila siku kuelekea katika kilele cha mafanikio”, alisema Bi Zawadia.

Akizungumzia kuhusu maendeleo ya benki, Bi Zawadia alisema DCB inazidi kupiga hatua siku hadi siku ikizidi kuendeleza jukumu mama la kuanzishwa kwake tokea miaka 21 iliyopita likiwa ni kutoa huduma bora za kifedha ikijikita zaidi katika kusaidia miradi endelevu ya kupunguza umasikini na kuendeleza jamii kwa kutoa huduma na bidhaa zenye ubunifu kwa wateja.

Alisema Benki ya DCB kwa miaka 21 imepiga hatua mbalimbali za kimaendeleo ikikuza mtaji wake kutoka kiasi cha shs Bilioni 1.7 ilipoanzishwa hadi kufikia kiasi cha shs Bilioni 27.5 kwa sasa, maendeleo hayo yalichangia mabadiliko mbalimbali katika benki ikiwa ni pamoja na kutoka kuwa Benki ya Kijamii hadi kuwa Benki kamili ya Biashara.

Benki yetu imeendelea kunyanyua wajasiriamali wengi wadogo kiuchumi ambao hawakuwa na namna ya kupata mitaji huku DCB ikiwa mstari wa mbele katika kutoa mikopo ikiwemo mikopo ya vikundi kwa wajasiriamali wadogo, mikopo ya biashara kwa wafanyabiashara wa kati na wakubwa."

Benki yetu imeendelea kupata faida mwaka hadi mwaka, kwa mwaka jana benki ilipata faida baada ya kodi ya shs 747 milioni, faida iliyochangiwa na mapato yasiyotokana riba ya shs 10.3 bilioni ambayo ni mafanikio ya asilimia 111 ya malengo tuliyojiwekea kwa mwaka 2022, huku mapato yatokanayo na riba yakifika shs 28.6 bilioni ikiwa ni asilimia 86 ya malengo tuliyojiwekea."

Akizungumza zaidi Bi Zawadia alisema “mali za benki zimekuwa hadi kufikia shs 227 bilioni hadi kufikia Septemba mwaka huu, kutoka shs 132 bilioni kwa mwaka 2018. Tukijivunia ukuaji huu ulioitoa benki yetu kutoka kwenye kundi la benki ndogo za biashara hadi kufikia benki za ukubwa wa kati nchini. Haya ni mafanikio makubwa ambayo ni matumaini yetu Mkurugenzi Mtendaji wetu mpya Bwana Sabasaba Moshingi ataendelea kushika usukani wa DCB kwa ustadi mkubwa kwa ukuaji zaidi wa benki yetu."

Benki ya DCB itaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dk Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha wananchi wengi zaidi wa maeneo ambayo hakuna matawi ya benki wanafikia na huduma za kifedha, ikienda sambamba na vipaumbele vya benki yetu kuhakikisha huduma zetu bora za kibenki zinapatikana nchi nzima na hii inatikana na uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanyika katika huduma zetu za kibenki kwa njia za kidigitali, hususan DCB Wakala na DCB Kidigitali inayowawezesha wateja kupata huduma mbalimbali za kibenki mahali walipo ikiwa ni pamoja na kufungua akaunti."

Huduma mbalimbali za kibenki zinapatikana kwa njia ya kidigitali mfano DCB Pesa ambayo mteja anaweza kufanya malipo na manunuzi kama vile, kuweka akiba au kutoa pesa, kulipa bili ya maji au umeme, kulipia ving’amuzi na pia kufanya malipo malipo ya serikali."

Aidha Mwenyekiti huyo wa Bodi alitaja baadhi ya huduma na akaunti zinazoendesha na benki hiyo kama kaunti ya elimu ya DCB Skonga, Wahi Akaunti kwa wenye mahitaji ya kutimiza malengo kwa njia ya kuwekeza kidogo kidogo, Akaunti za Mshahara & mikopo ya nusu mshahara, akaunti ya Wastaafu, Mikopo ya Nyumba, Lamba Kwanza na nyinginezo nyingi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji mpya wa benki hiyo, Bwana Sabasaba Moshingi alitoa shukurani zake kwa Bodi ya Wakurugenzi na Wanahisa wa benki hiyo kwa kuwa na imani naye akiahidi kutumia uzoefu wake wa miaka 21 alioupata katika kutumikia taasisi mbalimbali za fedha kuiinua DCB kutoka mahali ilipo na kuipeleka mbali zaidi.

Alisema anajua matarajio ya wateja wa DCB, wanahisa wao, Bodi, wafanyakazi, wateja pamoja na wadau, ni matumaini yake kuwa kwa kutumia uzoefu alionao pamoja na ushirikiano wa wadau wote wataweza kutimiza matarajio makuu ikiwa ni kutoa huduma bora za kifedha zinazolingana na mahitaji ya wateja na kutoa huduma bora zenye kiwango cha kimataifa.

Nikiwa na uzoefu wa miaka mingi katika maeneo ya biashara za kifedha, mikopo na wateja binafsi, ni matumaini yangu kuwa kwa pamoja tutaendeleleza azma hii kwa kutoa suluhu nyingi zaidi za mitaji kwa wafanyabiasha wadogo na wakati na pia kuliangalia kwa jicho la pembeni uboreshaji wa huduma za kifedha kwa njia za kidigitali ili zilingane na mahitaji ya watanzania lakini pia ziwe na ubora wa kimataifa."

Nina imani kwa ushirikiano wa pamoja hakuna kitakachoshindikana, maendeleo niliyoyapata katika taasisi nilikotoka, yanawezekana na hapa pia, tukae tayari kwa biashara."

Ndugu Mwenyekiti wa Bodi na Waandishi wa Habari, Kwa kuwa leo sio siku yangu, ni siku ya Mwenyekiti wetu, ni siku tu ya kutambulishwa kwangu, ningeomba niishie hapa ili panapo majaliwa ya Mungu basi tutawaita tena ili tuweze kuzungumza pamoja kuhusu maendeleo ya benki yetu ukizingatia kuwa wengi kati yenu tunafahamiana vizuri tokea huko nyuma”, alisema Bwana Moshingi.
Share:

Saturday, November 25, 2023

SERIKALI YAZINDUA MPANGO WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI, MAGONJWA YA NGONO NA HOMA YA INI

 

Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalim akizungumza wakati wa Uzinduzi wa mpango wa taifa wa kudhibiti ukimwi, magonjwa ya ngono na homa ya ini uliozinduliwa leo.

Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani Nchini Tanzania, Bw. Sagoe Moses akizungumza wakati wa Uzinduzi wa mpango wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi magonjwa ya ngono na homa ya ini uliozinduliwa leo na Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalim ambae ndio alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.

Mratibu Mwandamizi Ofisi ya Uratibu wa PEPFAR Ubalozi wa Marekani Nchini Dk. Hiltruda Chrisant Temba akizungumza wakati wa Uzinduzi wa mpango wa taifa wa kudhibiti ukimwi, magonjwa ya ngono na homa ya ini uliozinduliwa Leo na Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalim ambae ndio alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.

Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalim pamoja na viongozi mbalimbali wakiserikali na wadau wa sekta ya afya wakikata utepe kuashiria Uzinduzi rasmi wa mpango wa taifa wa kudhibiti ukimwi, magonjwa ya ngono na homa ya ini uliozinduliwa leo jijini Dar es Salaam.



Serikali imedhamiria kutokomeza maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa mama mjamzito kwenda kwa mtoto pamoja na kuzuia maambukizi mapya ya ukimwi kwa kundi la vijana kuanzia umri wa miaka 15 hadi 24 kutokana na takwimu kuonyesha kuwa kundi hilo la vijana ndilo linaloathirika zaidi na maambukizi hayo.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa mpango wa Taifa wa kudhibiti ukimwi, magonjwa ya ngono na Homa ya ini jijini Dar es salaam Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema licha ya hatua kubwa ambayo serikali na wadau wa masuala ya afya iliyopigwa katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa ukimwi ikiwemo kupungua kwa maambukizi lakini bado makundi hayo yanahitaji nguvu zaidi katika kuyasaidia dhidi ya ugonjwa huo.

Katika hatua nyingine Waziri Ummy amebainisha kuwa bado kuna ongezeko kubwa la maambukizi ya magonjwa ya ngono na Homa ya Ini nchini hivyo serikali inakuja na mpango mkakati wa wa kuhakikisha kutokomeza maambukizi hayo.

Waziri ameeleza kuwa serikali ya awamu ya sita imeboresha huduma za afya kuanzia ngazi ya taifa hadi msingi kwa kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za afya karibu zaidi na maeneo yao

“Serikali kupitia Wizara ya Afya wadau wa sekta na wataalamu wengine tayari wamefanyia kazi hoja zote zilizoibuliwa na bunge na semina zimefanyika kwa makundi mbalimbali ndani ya jamii kuhusu umuhimu wa bima za Afya kwa wote”.

“Kwa sasa nchi yetu iko mbali katika utoaji wa huduma, kuna vifaa vya kisasa vya uchunguzi wa magonjwa, huduma nyingi za kibingwa zinapatikana hapa hapa nchini lakini pia huduma za Afya zimesogezwa sana kwa wananchi hivyo kama serikali tuko tayari kutekeleza na kuhakikisha kuwa tunaendelea kuboresha huduma za afya kote nchini”.

Nayo baadhi ya mashirika ya kimataifa ambayo ni Shirika la La afya la Kimataifa WHO pamoja na Shirika la misaada la Marekani UNAIDS yaliyohudhuria uzinduzi huo kupitia kwa wawakilishi wao wamesifu juhudi za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dk Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muuungano waTanzania katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa ukimwi na kusema wataendelea kuunga mkono juhudi hizo
Share:

Friday, November 24, 2023

MTEJA WA Y9 MICROFINANCE AJISHINDIA PIKIPIKI KWA MKOPO WA BUKU MBILI

 

_L5A2403

Mkurugenzi wa Mauzo na Usambazaji wa Taasisi ya Kifedha Y9 Microfinance Fredrick Mtui (katikati) akizungumza na mshindi wa pikipiki droo ya saba kwa njia ya simu Anorld Jacob na Jekapo ambaye amejishindia simu janja wote ni wakazi wa Dar es Salaam ikiwa ni muendelezo wa Y9 kutoa zawadi kila wiki Kwa wateja wake. Hafla ya kuchezesha droo hiyo imefanyika leo jijini Dar es salaam, Wengine pichani ni Meneja Masoko ya Taasisi hiyo Bi. Sophia Mang'enya pamoja na mshindi wa pikipiki Wa droo ya sita Bw Baraka Bazarae (kushoto).

_L5A2489Meneja Masoko ya taasisi Bi Sophia Mang'enya akimkabidhi zawadi ya pikipiki mmoja kati ya washindi wa droo ya sita Baraka Bazarae katika hafla ya uchezeshwaji wa droo ya saba iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.

_L5A2481Mshindi wa pikipiki Droo ya sita ya Y9 Microfinance Baraka Bazarae Katikati akizungumza wakati wa hafla ya kuchezesha droo ya saba iliyofanyika leo jijini Dar es salaam, Wengine pichani Mkurugenzi wa mauzo na usambazaji wa taasisi ya kifedha Y9 microfinance Fredrick Mtui (kulia) na Mkaguzi kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha nchini Salim Buguvi (kushoto).

_L5A2495Meneja Masoko ya Taasisi ya Kifedha ya Y9 Microfinance Bi Sophia Mang'enya (kulia), akimkabidhi zawadi ya pikipiki kwa mshindi wa droo ya sita Baraka Bazarae ambae aliibuka kidedea wakati wakuchezesha droo ya sita wiki iliyopita makabidhiano hayo yalifanyika wakati wa yakuchezesha droo kwaajili ya kutafuta washindi wa droo ya Saba. Kushoto ni Mkaguzi kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha nchini Salim Buguvi (kushoto).



Washindi wa Droo ya saba ya Y9 Microfinance wapatikana mshindi wa pikipiki ni Anorld Jacob na mshindi wa simu Jekapo wote wakiwa ni wakazi wa Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kuchezesha droo hiyo Mkurugenzi wa mauzo na usambazaji taasisi ya kifedha Y9 microfinance Fredrick Mtui ameeleza kuwa huu ni muendelezo wa Y9 microfinance kuchezesha droo kila wiki na kupata washindi wawili.

Alisema "Matamanio makubwa ya Y9 microfinance ilikuwa ni kuhakikisha kuwa kila mteja wa Y9 microfinance anapata nafasi ya kushiriki na kushinda katika droo inayochezeshwa kila wiki.

Alitoa wito kwa watanzania kujiunga na Y9 microfinance ili kupata huduma za kifedha kwa urahisi pia kujiweka katika nafasi nzuri za ushindi.

Alieleza kuwa sasa tunakwenda ukingoni Kwenye uchezeshaji wa droo hizi tuliahid Kwa watanzania kuwa tutatoa pikipiki 8 na simu 8 hivyo hadii sasa washindi Saba wa pikipiki na wasimu janja wameshapatikana.

Aliongezea kwa kusema "Hadi sasa tumeshatoa zawadi ya pikipiki sita na simu sita na mshindi wa Saba pikipiki na simu wameshapatikana hivyo tumesalia na droo Moja yakutoa zawadi ya pikipiki na simu ili kumamilisha Ile ahadi tuliyotoa".

Mtui amewakumbusha watanzania kuwa "sasa tunakwenda mwisho wakuchezesha droo zetu hivyo niwasihi nduguzangu wakati wako ni sasa tumia App ya Y9 Microfinance ili upate mkopo Kwa njia rahisi pia kujishindia zawadi mbalimbali".

"Baada ya droo yetu ya nane kukamilika tutakwenda kuchezesha droo kubwa ambapo mchindi ataondoka na ndinga mpya kabisa Toyota Ist hii sio ya kukosa endelea kupakuwa app yetu kopa na ushinde".

Alieleza namna ya kushiriki ni rahisi hakikisha umepakua app ya Y9 microfinance kisha kujisajili na kuanza kukopa na moja kwa moja utaingia kwenye droo hii baada ya marejesho.

Kwa upande wake Mkaguzi kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha nchini Salim Buguvi ameeleza "kama bodi ya michezo ya kubahatisha nchini tumeridhishwa na namna ya uchezeshwaji wa droo hii na uhalali katika upatikanaji wa washindi”.
Share:

Thursday, November 23, 2023

Airtel, itel washirikiana kuzindua simu janja mpya na ya kisasa aina ya A70

Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu ya Mkononi ya Airtel Tanzania, Bwana Jackson Mmbando, akizungumza wakati wa uzinduzi wa simu mpya aina ya Itel A70 AWESOME ya kampuni Itel kwa ushirikiano na Airtel katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu ya Mkononi ya Airtel Tanzania, Bwana Jackson Mmbando (kushoto) Meneja Bidhaa wa Kampuni ya Itel, Bwana Thomas Wang (wa pili kulia), pamoja na wengine kutoka kampuni hizo, wakipozi wa picha ya 'selfie' katika hafla ya uzinduzi wa simu mpya aina ya Itel A70 AWESOME ya kampuni Itel kwa ushirikiano na Airtel katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.

• Wateja wa Airtel kuunganishwa na GB 75 kwa miezi kumi na 12 wakinunua simu ya Airtel katika maduka ya Airtel na itel popote nchini
• Ni toleo maalum kwa ajili ya msimu huu wa sikukuu

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania na kampuni ya kutengeneza simu ya itel leo kwa pamoja wameshirikiana wamezindua simu mpya ya itel A70 iliyoambatanishwa na ofa ya bando ya intaneti yenye kifurushi cha BURE cha GB 75 ambacho kinadumu kwa muda wa miezi kumi na mbili.

Ushirikiano wa Airtel na itel unawahakikishia Watanzania uwezo wa kupata simu za kisasa za smartphone zenye ubora wa juu kwa gharama nafuu zaidi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, wakati wa uzinduzi wa simu hiyo ya kisasa kabisa yenye ofa kabambe, Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano alisema “Tunajivunia ushirikiano wa Airtel na itel kwa kuzindua simu mpya na ya kisasa ya A70".

Wenzetu wa itel wanalenga kuhudumia wateja wa kipato cha kati na cha chini kwa bidhaa zenye ubora na unafuu, hivyo basi Airtel ikiwa moja ya makampuni yanayotoa huduma za smartphone za kisasa na uhakika, tukaona tuwafikishie ofa hii kabambe watanzania wote ili kuwawezesha kuendana na ulimwengu wa kidigitali kwa kutumia mtandao wetu ulio bora na ulioenea kote nchini na simu ya itel.

Simu ya A70 itakuwa inapatikana kwenye maduka yote ya Airtel na itel kote nchini ikiwa na ofa ya kifurushi cha bando ya intaneti ya 75GB kwa muda wa miezi kumi na mbili.

Kwa upande wake, Meneja wa Chapa wa itel kutoka itel Mobile Bw, Thomas Wang, alisema kuwa ni furaha kubwa sana kushirikiana na Airtel kuzindua simu mpya ya kisasa ya itel A70 ambayo ni Smartphone ambayo ni toleo la kisasa na inapatikana kwa bei nafuu kabisa Tanzania nzima.

Simu ya A70 ni nyepesi sana na inatoa suluhisho bora kwa watumiaji wa huduma za kidigitali kwa uhakika na haraka kabisa itapatikana kwa gharama nafuu,

Aliongeza kuwa simu ya itel A70 ina uwezo wa 128GG ROM + 8GB RAM, 6,6” na ukubwa wa kioo wa 13MP super HDR CAM. Hivi vyote kwa pamoja vinampa mtumiaji kufarahi matumizi ya simu hii pamoja na kumpa Uhuru wa mawasiliano.

‘Sababu kubwa ya ushirikiano baina ya Airtel na itel ni kuwapa Watanzania kuwa na uwezo wa kutumia smartphone za kisasa zenye ubunifu wa hali ya juu kwa gharama nafuu pamoja na kufurahi kifurushi cha intaneti cha 75GB kutoka Airtel kwa mwaka mzima.
Share:

Friday, November 17, 2023

Shirika la USAID laipongeza serikali ya Tanzania mafanikio katika miradi ya elimu na afya nchini

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart (kushoto), akikabidhi mipira kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Njia Panda, Bi. Tatu Mohamedi (kulia), wakati wawakilishi wa USAID, Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR) pamoja na mashirika yanayosimamia miradi inayotoa huduma kwa wagonjwa wa VVU inayofadhiliwa na mfuko huo, wakitembelea shule hiyo kuangalia maendeleo ya miradi ya USAID Kizazi Hodari Kusini, inayotekelezwa na Shirika la Deloitte shuleni hapo, Iringa, jana. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Mradi wa Kizazi Hodari, Bi. Dorothy Matoyo, Mkurugenzi Msaidizi wa USAID kitengo cha afya nchini, Bi. Anna Hofmann na Kaimu Ofisa Elimu Msingi wa Manispaa ya Iringa, Samweli Mtovagakye. Ziara hiyo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 20 ya Mfuko wa PEPFAR.
Mkurugenzi wa Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini, Bi. Dorothy Matoyo, akitoa maelezo kuhusu mafanikio ya mradi huo unaoendeshwa na Shirika la Deloitte, wakati wawakilishi wa USAID, PEPFAR, pamoja na mashirika yanayosimamia miradi inayotoa huduma kwa wagonjwa wa VVU inayofadhiliwa na PEPFAR, wakitembelea shule ya msingi Njia Panda, kuangalia maendeleo ya afua mbili za wanafunzi wasichana ya Dreams na wavulana ya ‘coaching boys into men' (CBIM) shuleni hapo, Iringa, jana.
Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Bwana Craig Hart (katikati), akiangalia michoro inayotumika kufundishia afua za Dreams na CBIM kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Njia Panda shuleni hapo jana. Afua hizo zinahusu elimu ya uzazi, maambukizi ya VVU, tabia njema na stadi za maisha ikiwemo elimu ya kifedha. Miradi hiyo imechangia ufaulu wa shule hiyo kwa mwaka 2022, darasa la saba ufaulu ukiwa ni 97% huku darasa la nne ukiwa ni 93%.
Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Bwana Craig Hart, akisalimiana na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Njia Panda mjini Iringa, alipokwenda pamoja na ujumbe wake kukagua miradi ya USAID Kizazi Hodari Kusini inayofadhiliwa na Mfuko wa PEPFAR.
Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Bwana Craig Hart (kulia), akiagana na Mkurugenzi wa Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kusini, Bi. Dorothy Matoyo (wa pili kushoto), mara baada ya kutembelea Shule ya Msingi Njia Panda kuangalia maendeleo ya inayosimamiwa Shirika la Deloitte kupitia mradi wa Kizazi Hodari Kusini, chini ya ufadhili wa Mfuko wa PEPFAR.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), Bwana Craig Hart (katikati), pamoja na Mkurugenzi Msaidizi wa USAID kitengo cha afya nchini, Bi. Anna Hofmann (wa pili kushoto), wakipiga picha ya kumbukumbu na baadhi ya mabinti wanaohudumiwa na mradi wa EpiC unaosimamiwa na Shirika la FHI360 kwa ufadhili wa Mfuko wa PEPFAR, wakati wawakilishi wa USAID na PEPFAR nchini wakifanya ziara mkoani Iringa kuangalia maendeleo ya miradi inayofadhiliwa na mfuko huo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 20 ya Mfuko wa PEPFAR. Katikati ni Mkurugenzi Msaidizi wa USAID.
Mkurugenzi wa Shirika la FHI360, Bwana Bernard Ogwang, linalosimamia mradi wa EpiC, akitoa maelezo kuhusu mafanikio ya mradi huyo katika kutoa huduma kwa wenye VVU.
Mkurugenzi Mkazi wa USAID, Bwana Craig Hart (katikati kulia), akiangalia ubunifu wa kazi za mikono za mmoja wa mabinti wenye VVU wanaohudumiwa na mradi wa EpiC chini ya usimamizi wa Shirika la FHI360 mjini Iringa wakati wa ziara ya wawakilishi wa USAID, PEPFAR, mashirika yanayosimamia miradi ya USAID pamoja na waandishi wa habari kuangalia maendeleo ya miradi hiyo mkoani humo.

Na Zuhura Rashidi, Iringa

SHIRIKA la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), limeipongeza Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, chini ya Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada kubwa zinazofanyika katika kuboresha maendeleo ya miradi ya afya na elimu nchini.

Pongezi hizo zilitolewa na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la USAID, Bwana Craig Hatz, katika Shule ya Msingi Njia Panda Mkoani Iringa wakati akihitimisha ziara ya siku tatu ya wawakilishi wa shirika hilo na wa Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR), pamoja na mashirika yanayosimamia utekelezaji wa miradi ya ukimwi inayofadhiliwa na PEPFAR.

Akihitimisha ziara hiyo ambayo pamoja na mambo mengine ilienda pamoja na maadhimisho ya miaka 20 ya Mfuko wa PEPFAR, Bwana Hart alisema jitihada zinazofanywa na serikali kwa kushirikiana na USAID, PEPFAR, zimechangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya miradi yote inayofadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia USAID kwa zaidi ya miaka 60 iliyopita.

Serikali ya Marekani kwa zaidi ya miaka 20 imewekeza zaidi ya USD Bilioni 6 nchini Tanzania, kuhakikisha tunashirikiana pamoja na serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, sekta binafsi, wazazi na familia kukabiliana na HIV/AIDS."

Dola bilioni 6 inaweza kuonekana nyingi, Mwaka 2000 hadi 2019 umri wa kuishi kwa mtanzania uliongezeka kwa miaka 15, ikimaanisha sasa watanzania wote wameongeza umri wao wa kuishi kwa miaka 15 zaidi, wadau wote hawa wameungana kwa ajili yako, mpo katika mazingiza bora, mnapata elimu pamoja na elimu bora ya afya, muhimu sana kwa Tanzania ya kesho, maisha yako na maisha yetu ya baadae”, alisema.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Mradi wa USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini, Bi. Dorothy Matoyo alisema wao kama Deloitte wanayo furaha kupata uwezo wa kuchangia katika maendeleo ya kizazi chenye furaha na kinachojiamini na ndipo jina lao lilipotokea.

Kizazi tunachokiangalia sasa tunatumaini baada ya miaka 10 ama 20 ijayo kitakuwa kizazi salama chenye kujiamini, chenye upendo, kujua jinsi ya kujilinda na VVU, unyanyapaa na ukatili wa kijinsia."

Deloitte kupitia mradi wa Kizazi Hodari Kanda ya Kusini, ni wajibu wetu kuhakikisha tunawasaidia watoto yatima pamoja na wanaoishi katika mazingira magumu katika kuwaunganisha katika vituo watakavyoweza kupata usaidizi”, alisema Bi Dorothy.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Njia Panda, Bi. Tatu Mohamedi alisema alisema shuleni hapo chini ya uratibu wa Mradi wa Kizazi Hodari Kusini, wanajishughulisha na afua mbili za ‘Dreams’ kwa wanafunzi wa kike na ‘Coaching Boys Into Men’ (CBIM) ambapo jumla ya watoto wa kike 235 na wa kiume 204 wamenufaika na mpango wa mafunzo katika afua zote mbali.

Afua hizi zinalenga kuwasadia watoto kujitambua, kujithamini na kujiheshimu hivyo watoto hawa wamepata mafunzo kuhusu ugonjwa wa ukimwi, afya ya uzazi, ukatili wa kijinsia na kuondokana na unyanyapaa kwa wale wenye virusi."

Miradi hii imeleta mafanikio makubwa hata kwa wanafunzi wetu kitaaluma, kupitia USAID Kizazi Hodari Kanda ya Kusini wamesaidia vifaa vya shule kama madaftari na kalamu kwa watoto wa kike 235 kwa lengo la kuwasaidia watoto hao kufanya vizuri katika mitihani yao”, alisema mwalimu huyo.

Mkurugenzi wa Shirika la FHI360, Bwana Bernard Ogwang alisema shirika lao linalosimamia mradi wa EpiC kwa ufadhili wa USAID na PEPFAR, limechangia kwa kiasi kikubwa kuboresha maisha ya vijana wa kike na wa kiume wanaoishi katika mazingira hatarishi ya kupata Virusi vya ukimwi.

Katika mikoa 11 tunayohudumia, tuna idadi ya vijana wa kike na wa kiume 225 wanaopata huduma kamili ya kinga na tiba ya VVU, lakini pia vijana hawa hujishughulisha katika shughuli za kiuchumi ili waweze kuboresha maisha yao”, alisema.

Baadhi ya mabinti wenye VVU wanaopata huduma kupitia mradi wa EpiC wakitoa ushuhuda ni jinsi gani miradi ya Mfuko wa PEPFAR imeboresha maisha yao mara baada ya kugundua hali zao na kujiunga katika vituo vya huduma na tiba walisema moja ya changamoto zinazochangia kutojitokeza kwa watu wengi kupima virusi vya ukimwi ni unyanyapaa unaotokana na imani, mila potofu na kukosa elimu sahihi juu ya ugonjwa wa ukimwi.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive