A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Saturday, March 28, 2020

HALMASHAURI YA UBUNGO NA TARURA WAJENGA DARAJA LA KISASA MTO GIDE KIMARA.


Diwani wa Kata ya Kimara Paschal Manota, akizungumza  na waandishi wa habari pamoja na wananchi wa kata hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa daraja katika mto Gide uliopo kimara ambapo Daraja hilo litagharimu takribani Shilingi za kitanzania milioni 321 ambapo katika hizo milioni 200 zimetoka kwenye mfuko wa Halmashauri ya Ubungo na hizo nyengine zimetolewa na Wakala wa Barabara za Mijini na VIjijini (TARURA)
Mkurugenzi wa Kampuni ya Ujenzi , Mpeha 2000 Ltd Never Black, akizungumza  na waandishi wa habari pamoja na wananchi wa kata ya kimara wakati alipokabidhiwa eneo kwaajili ya Ujenzi wa daraja katika mto Gide uliopo kimara ambapo Daraja hilo litagharimu takribani Shilingi za kitanzania milioni 321 ambapo katika hizo milioni 200 zimetoka kwenye mfuko wa Halmashauri ya Ubungo na hizo nyengine zimetolewa na Wakala za Barabara wa Mijini na VIjijini (TARURA)
 Msimamizi wa Mradi kutoka Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Manispaa ya Ubungo  Mhandisi Denis Charles akizungumza  na waandishi wa habari pamoja na wananchi wa kata ya kimara wakati alipokabidhiwa eneo kwaajili ya Ujenzi wa daraja katika mto Gide uliopo kimara ambapo Daraja hilo litagharimu takribani Shilingi za kitanzania milioni 321 ambapo katika hizo milioni 200 zimetoka kwenye mfuko wa Halmashauri ya Ubungo na hizo nyengine zimetolewa na Wakala za Barabara wa Mijini na VIjijini (TARURA)
Mkazi wa kata hiyo Mwajuma Mungila, akitoa neno la shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh John Magufuli pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, kwa kuwatatulia kero iliyodumu kwa muda mrefu zaidi ya miaka kumi.
Jinsi wakazi wa Kimara wanavyopita kwasasa
Wanahabari wakiwajibika wakati wa hafla hiyo Picha zote na Brian Peter

 Sasa Ujenzi wa daraja la mto Gide kuanza kujengwa jumatatu baada ya wakazi wa kata hiyo kupata shida ya kutumia njia hiyo kwa muda wa miaka kumi
Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es Salaam, Mkandarasi anaetarajia kujenga daraja hilo Never black amezibitisha  kuwa wanatarajia kuanza ujenzi huwo rasmi siku ya Jumatatu Tarehe 30 mwezi huu.
“Tunatarajia kuanza ujenzi haraka iwezekanavyo na tumepewa muda wa miezi mitatu yaani siku 90 lakini tunatarajia kufanya kazi kwa muda wa miezi miwili kama mvua itasimama kunyesha au haitonyesha  kwa wingi.
“Daraja litakuwa na urefu wa mita kumi na moja na litakuwa la njia mbili ambalo lita ghalimu kiasi cha shilingi za kitanzania milioni 321Daraja hilo litaweza kupitisha magari ya uzito wa tani kumi pamoja na njia ya watembea kwa miguu” anasema Black.
Kwa upande wa Diwani wa Kimara Baruti, Paschal Manota, anasema Halmashauri imetoa sh milioni 200, na Wakala wa barabara, TARURA imetoa milioni 100 kwaajili ya mchango wa ujenzi wa daraja hilo la mto Gide.
“Mkandarasi anatakiwa atoe kazi kwa wananchi wa eneo la baruti na makoka asipewe mtu wa kutoka mbali na eneo hili la ujenzi wa daraja ili lijenge kwa wakati.



Share:

Sunday, March 22, 2020

Nabii SUGUYE atia SAINI leso za WAUMINI

Nabii Nicolaus Suguye akisaini moja ya Kitambaa cha muumini wa Kanisa hilo

Na Mwandishi wetu,

KATIKA jambo lililowashangaza wengi, ndani ya Kanisa la WRM lillopo Kivule Matembele ya Pili, Ukonga, jijini Dar es Salaam, Kiongozi na Msimamizi Mkuu wa huduma hiyo, Nabii Nicolaus Suguye ameendesha Ibada ya kutia saini vitambaa vya maelfu ya waumini wa kanisa hilo.

Neno saini limetoholewa kutoka katika neno la kiingereza ‘sign’ ili lifanane na muundo wa Kiswahili na liwe ni neno kamili la Kiswahili na kutumika kama kitenzi na wakati mwengine kama nomino.

Nabii Suguye akionesha dhamiri ya dhati kuhakikisha kila aliyehudhuria Ibada hiyo anamsainia kitambaa chake.

Saini (kitenzi) ni kutoa idhini ili kitendo Fulani kitendeke au kipatikane. Matumizi yaliyozoeleka na kukubaliwa na wengi ni kutoa idhini au kuthibitisha kupatikana kwa kitu au jambo Fulani na mara nyinine ni kwa kuandika jina lako.

Tunatumia neno hili tunapotaka kuweka saini mahali fulani. Ni sahihi kusema kuweka saini na wala siyo kutia saini. Kutia lina maana ya kufanya kitu kiwemo ndani ya kitu kwa mfano nitilie chai badala ya kusema niwekee chai. Kuweka kitu maana yake ni kukitua kitu kama vile kuweka kitabu mezani au kuweka silaha chini.

Msururu wa Waumini ukisubiria kusainiwa Leso zao na Nabii Suguye

Neno sahihi (nomino) lina maana ya kuthibitisha au kuidhinisha kwa jambo kutendeka au kupatikana.

Awali nabii Suguye aliwafundisha maelfu ya waumini wa kanisa hilo umuhimu wa kuthibitishwa na Mungu, “Unapothibitishwa ni rahisi kwako kuomba lolote kwa Yule aliyekuthibitisha na akalifanya”

Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.” Nabii alinukuu kutoka kwenye maandiko ya Biblia Injili ya Yohana 14:14

“Ninaposaini Leso ya kila mtu aliye hudhulia mahali hapa hii ni Saini ya USHINDI, ninapoisaini mahali hapa imesainiwa mbinguni na kupitishwa kuwa MSHINDI” alisema Nabii Suguye.

Nabii Suguye akiwahubiria maelfu ya waumini waliohudhuria Ibada hiyo

Akifundisha katika Ibada hiyo alisema kupitia tendo hilo la Imani iwe ni fahari kwao kujua kuwa, kuna umuhimu wa kujitakasa na kuwa katika mstari ule Neno la Mungu linatufundisha ili tupate kuthibitishwa nakuwa na hakika ya kupokea yale yote tuyaombayo kwa Mungu.

“Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.” Waebrania 11:1



“Kupitia saini hii nakutabiria ukafanikiwe katika kila kitu utakachokwenda kukifanya kwaajili ya Utukufu wa Mungu, katika Jina la Yesu Kristo.” Alisema Nabii Suguye wakati wa Ibada hiyo.
Share:

Sunday, March 15, 2020

Washindi wa Ongeza Mshahara Wako na Absa Tanzania wapatikana

Mkuu wa Bidhaa kwa Wateja Rejareja wa Benki ya Absa Tanzania, Heristraton Genesis (wa pili kushoto), akichukua tiketi, ili kumpata mmoja wa washindi wa droo ya kwanza ya promosheni ya akaunti ya mshahara ya benki hiyo iliyopewa jina la ‘Ongeza Mshahara wako’ jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Ili kushinda mteja mpya hutakiwa kufungua akaunti ya mshahara ama kwa mteja wa zamani kupitisha mshahara wake benki katika mwezi ulio ndani ya kipindi cha promosheni ili kujishindia kiasi cha fedha hadi asilimia 100 ya mshahara uliowekwa. Wengine kutoka kushoto ni, Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Rasuli Masudi, Mkuu wa Mtandao wa Matawi wa Absa, John Beja na Meneja Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, Beda Biswalo.
Mkuu wa Mtandao wa Matawi wa Benki ya Absa Tanzania, John Beda (wa pili kulia), akisoma jina la mmoja wa washindi wa droo ya kwanza ya promosheni ya akaunti ya mshahara ya benki hiyo iliyopewa jina la ‘Ongeza Mshahara wako’ jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Ili kushinda mteja mpya hutakiwa kufungua akaunti ya mshahara ama kwa mteja wa zamani kupitisha mshahara wake benki katika mwezi ulio ndani ya kipindi cha promosheni ili kujishindia kiasi cha fedha hadi asilimia 100 ya mshahara uliowekwa. Wengine kutoka kushoto ni, Mkuu wa Bidhaa kwa Wateja Rejareja, Heristraton Genesis, Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Rasuli Masudi, na Meneja Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, Beda Biswalo.
Mkuu wa Bidhaa kwa Wateja Rejareja wa Benki ya Absa Tanzania, Heristraton Genesis (wa pili kushoto), akisoma jina la moja wa washindi wa droo ya kwanza ya promosheni ya akaunti ya mshahara ya benki hiyo iliyopewa jina la ‘Ongeza Mshahara wako’ jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Ili kushinda mteja mpya hutakiwa kufungua akaunti ya mshahara ama kwa mteja wa zamani kupitisha mshahara wake benki katika mwezi ulio ndani ya kipindi cha promosheni ili kujishindia kiasi cha fedha hadi asilimia 100 ya mshahara uliowekwa. Wengine kutoka kushoto ni, Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Rasuli Masudi, Mkuu wa Mtandao wa Matawi wa Absa, John Beja na Meneja Msoko na Mawasiliano wa beni hiyo, Beda Biswalo.
Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Beda Biswalo (kulia), akichanganya tiketi  ili kumpata mmoja wa washindi wa droo ya kwanza ya promosheni ya akaunti ya mshahara ya benki hiyo iliyopewa jina la ‘Ongeza Mshahara wako’ jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Ili kushinda mteja mpya hutakiwa kufungua akaunti ya mshahara ama kwa mteja wa zamani kupitisha mshahara wake benki katika mwezi ulio ndani ya kipindi cha promosheni ili kujishindia kiasi cha fedha hadi asilimia 100 ya mshahara uliowekwa. Wengine kutoka kushoto ni, Mkuu wa Bidhaa kwa Wateja Rejareja, Heristraton Genesis, Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Rasuli Masudi, Mkuu wa Mtandao wa Matawi wa Absa, John Beja.
Meneja Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Beda Biswalo (wa pili kulia), akisoma jina la mmoja wa washindi wa droo ya kwanza ya promosheni ya akaunti ya mshahara ya benki hiyo iliyopewa jina la ‘Ongeza Mshahara wako’ jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Ili kushinda mteja mpya hutakiwa kufungua akaunti ya mshahara ama kwa mteja wa zamani kupitisha mshahara wake benki katika mwezi ulio ndani ya kipindi cha promosheni ili kujishindia kiasi cha fedha hadi asilimia 100 ya mshahara uliowekwa. Wengine kutoka kushoto ni, Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Rasuli Masudi, Mkuu wa Bidhaa kwa Wateja Rejareja, Heristraton Genesis na Mkuu wa Mtandao wa Matawi wa Absa, John Beja.
Share:

Friday, March 13, 2020

Wafanyakazi wanawake wa Jubilee Insurance na Jubilee Life insurance waadhimisha Siku ya Wanawake kwa kutoa misaada Hospitali ya Mwananyamala

Muuguzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala, Rose Musa (wa tatu kushoto), akipokea msaada wa vitu mbalimbali vikiwemo sabuni, mashuka na mataulo ya kike vilivyotolewa na wafanyakazi wa Kampuni ya Bima ya Jubilee Insurance na Jubilee Life Insurance kwa kusaidia wanawake waliolazwa katika wodi ya wazazi ya hospitali hiyo ikiwa ni sehemu ya matukio kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani. Hafla hiyo ilifanyika hospitalini hapo, Mwananyamala, Dar es Salaam jana. 
Wafanyakazi wanawake wa Kampuni ya Bima ya Jubilee na Jubilee Life pamoja na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala wakionyesha ishara maalumu ya kauli mbiu ya Siku ya Wanawake Duniani 2020 isemayo ‘Wanawake katika Mshikamano Tutaendelea Mapambano’ wapolitembelea hospitalini hapo kutoa msaada  wa vitu mbalimbali vikiwemo sabuni, mashuka na mataulo ya kike kusaidia wanawake waliolazwa katika wodi ya wazazi ya hospitali hiyo ikiwa ni sehemu ya matukio yao kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani. Hafla hiyo ilifanyika hospitalini hapo, Mwananyamala, Dar es Salaam jana.
Ofisa Rasilimali Watu wa Kampuni ya Jubilee Insurance, Grace Tupa (kushoto), na mwenzake kutoka Jubilee Life Insurance, Doreen Offen Martin (kulia), wakikabidhi msaada wa shuka na vitu vingine kwa mmoja wa wazazi aliyejifungua katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwananyamala, Tatu Hashim wakati wafanyakazi wanawake wa kampuni hiyo wakitembelea hospitalini hapo kutoa msaada  wa vitu mbalimbali vikiwemo sabuni, mashuka na mataulo ya kike kusaidia wanawake waliolazwa katika wodi hiyo hospitali hapo ikiwa ni sehemu ya matukio yao kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani. Hafla hiyo ilifanyika hospitalini hapo, Mwananyamala, Dar es Salaam jana.
Ofisa Utumishi na Utawala wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala, Mansour Anchi (kushoto), akizungumza wakati wafanyakazi wanawake wa Kampuni ya Bima ya Jubilee Insurance na Jubilee Life Insurance wapolitembelea hospitalini hapo kutoa msaada  wa vitu mbalimbali vikiwemo sabuni, mashuka na mataulo ya kike kusaidia wanawake waliolazwa katika wodi ya wazazi ya hospitali hiyo ikiwa ni sehemu ya matukio yao kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani. Hafla hiyo ilifanyika hospitalini hapo, Mwananyamala, Dar es Salaam jana.
Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Bima ya Jubilee Insurance, Angela Tungaraza (kushoto), na Ofisa Mawasiliano wa kampuni hiyo, Baraka Mosha (kulia), wakikabidhi msaada wa shuka na vitu vingine kwa mmoja wa wazazi aliyejifungua katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwananyamala, Tatu Hashim wakati wafanyakazi wa kampuni hiyo wakitembelea hospitalini hapo kutoa msaada wa vitu mbalimbali vikiwemo sabuni, mashuka na mataulo ya kike kusaidia wanawake waliolazwa katika wodi hiyo hospitali hapo ikiwa ni sehemu ya matukio yao kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani. Hafla hiyo ilifanyika hospitalini hapo, Mwananyamala, Dar es Salaam jana.
Share:

Monday, March 9, 2020

SCANIA READY TO INTRODUCE CNG BUSES IN TANZANIA

Managing Director of Scania Tanzania Ltd, Lars Eklund, officially announces the company’s plan to unveil new edition of Scania buses that use natural gas, which transport analysts tout as more suitable for Tanzania, especially in the Bus Rapid Transit system. The event took place today at the company’s head office at Vingunguti, Dar es Salaam.
Managing Director of Scania Tanzania Ltd, Lars Eklund, speaks during the company’s executive briefing on its scheduled launch of new class of Scania buses that employ natural gas, which transport analysts tout as suitable for Tanzania, especially in the Bus Rapid Transit system. The event took place today at the company’s head office at Vingunguti, Dar es Salaam.  To his left is Scania Tanzania Ltd Marketing Manager, Eliavera Timoth.
Marketing Manager of Scania Tanzania Ltd, Eliavera Timoth (right) speaks during the company’s announcement that it will launch in the market new version of Scania buses that run on natural gas, considered as more suitable for Tanzania, especially in the Bus Rapid Transport system. The event took place at the company’s head office at Vingunguti, Dar es Salaam. To his right is Scania Tanzania Ltd Managing Director, Lars Eklund.

By Scania Reporter;

Scania Tanzania Ltd has made an announcement today about its CNG (Compressed Natural Gas) buses and why they would be ideal for the Tanzanian market and especially for BRT city buses. This product is just one part of the company’s commitment to ensure that they lead the shift of the transport industry to a sustainable future. Scania believe that it is time for Tanzania to adopt this and other solutions to improve the lifestyle of the people, both economically and environmentally.

Tanzania has huge reserves of Natural Gas and needs thousands of city buses for the BRT systems which Scania can deliver. Scania has since managed to deliver the CNG gas buses for quite a while and have delivered in delivered in different parts of the world like South America, Europe and Australia among others. The CNG driven buses come equipped with a “green” Euro 6 compliant engine that reduces the CO2 up to 20%, the same engine can also run on locally produced biogas to reach a CO2 reduction of as much as 90%. It is paramount to reduce CO2 as it is the main contributor to the global warming issues. Buses fitted with these engines produces less particles and lower emissions in the air and is very efficient in terms of fuel consumption and can achieve lower operational costs that benefit the passengers in terms of low ticket prices, income for the government to sell local Natural Gas and an advantage for the operators too to cut their operational costs. A “win win win” solution.

Dar es salaam is expanding quite rapidly with an ever-increasing population and it is important to not only think of how this will affect the movement in the city but also to consider how this will happen in a way that is safe for the environment and the citizens.

Speaking during the announcement at their head office, located in Vingunguti along Julius Nyerere Road, the Managing Director of Scania Tanzania, Lars Eklund said, as Tanzania is working towards becoming more industrialized, it is important that efficiency becomes key and that the environment is not forgotten along the process. ‘We believe that Tanzania needs to adopt world tested technologies and move at the same pace with other developed countries’, he added. ‘Tanzania is very rich in natural gas and it is important to use this local energy to the country´s advantage, the country will gain tremendously as it will save on the amount of oil that is imported’ and can instead sell the local gas to local operators, said Mr Eklund.

Further, he also explained “that it is a very poor technical solution and expensive to try convert a current diesel engine to a gas engine. He mentioned that there has been talks in the media to do so for the current BRT buses, technical and economically it does not make sense. The diesel engine is designed to run in a “diesel cycle” while a gas and petrol engine runs according to the Otto principle with a spark plug ignition. All Scania CNG engines run according to the Otto principle and are thus efficient and reliable. It therefor very important that the plans for the CNG infrastructure expansion get real and dates are firm so suppliers and operators can dare to invest in proper CNG gas products to be used on the streets as soon as possible. Hopefully already for the next BRT phase in Dar es Salaam.”

As part of its efforts to promote after sales services, Scania Tanzania is seeking cooperation with Education  institutions to offer scholarship to students that are pursuing studies related to CNG. This will increase the number of technicians and professionals in that field and thus increase support to customers that operate the buses. The Marketing Manager, Eliavera Timoth explained that not only is this part of their commitment to improve service but also a way of giving back to the community and making sure that they make an impact in the market.

About Scania Tanzania

Scania Tanzania Ltd, operates as a subsidiary of Scania CV AB with its HQ in Sweden. The company is the exclusive importer and distributor of Scania products in the country with an extensive network for services supporting its customers. The Dar es Salaam-headquartered firm has dealerships in Arusha, Mwanza, Mbeya and Parts outlets in several other locations and is annually investing in growth and improvements in its network and customer services.

The company entered the market in 1973 when Scania CV AB delivered 200 tipper trucks to the Chinese who were constructing the Tanzania-Zambia Railway line (TAZARA).
Share:

Sunday, March 8, 2020

Absa Bank Tanzania sponsors celebrated local golfer

Absa Bank Tanzania Managing Director, Abdi Mohamed hands over a box contains some golf sports gears and travelling documents to Tanzania renowned golf player, Victor Mbunda (left), on his mission as Tanzania’s flag-bearer in the coming Kenya Open Golf Championship to be staged at Karen Country Club in Nairobi, Kenya on date to be disclosed soon. Mbunda participation is full sponsored by Absa Tanzania. Right is ABT Head of Marketing and Corporate Relations, Aron Luhanga and others from second left are veteran golfers, Martin Warioba and Marian Mugo. A brief occasion was held in Dar es Salaaam during the weekend.

By Staff Reporter

ABSA Bank Tanzania said it has fully sponsored local golf celebrity, Victor Mbunda,  on his mission as Tanzania’s flag-bearer in the coming Kenya Open Championship.

Speaking in Dar es Salaam yesterday, Absa Bank Tanzania Managing Director, Abdi Mohamed, said the bank was happy with Mbunda’s ambition, giving rise to the decision to support him.

“We always aim to bring possibilities into life and, knowing that Mbunda is the current number one golfer in Tanzania, it is our willingness to be part of his success story by facilitating him into this tournament,” said Mohamed.

He said the bank was always proud to be associated with sports so as to inspire Tanzanian youth, as Mbunda does, into showing they were capable to brush shoulders with world-class sportsmen.

Kenya Open is an annual golf tournament founded in 1967. It has been an event on Europe-based Challenge Tour schedule since 1991, before being affix onto the European Tour in 2019.

The tourney’s past champions include Seve Ballesteros, Ian Woosnam, Ken Brown, Christy O’Connor Jr and Trevor Immelman.

“Mbunda is a symbol of ambitions. We, Absa Bank Tanzania respect the ambitions of our customers as well as those of our nation at large. As a way of putting in action the noble aim of our ‘Africanacity’ maxim, we feel obliged to give Mbunda support, and we believe he won’t let us down,” said Mohamed.

Earlier, Absa Tanzania Head of Marketing and Corporate Relations Aron Luhanga, said Mbunda would be fully sponsored.

“We provide a return ticket to Nairobi, allowances as well as golf gears,” he said.

Luhanga urged Tanzanians to play down the misguided notion that golf was reserved for the affluent, saying it was like any other sports and was open to people from all walks of life, whether driven by the urge to keep fit or are out to make money.

Mbunda, flanked by veteran golfers Martin Warioba and Marian Mugo, thanked Absa Bank Tanzania for giving him a helping hand, and promised not to let them down.

“I am willing to be brand ambassador for Absa Bank Tanzania in the tourney as well as in other future golf   contests. You have showed the way,” he said.

The four-day regional classic is scheduled to take off at the Karen Country Club in Nairobi, Kenya on date to be disclosed soon.
Share:

Mwanamke ni kiungo katika uhifadhi wa mazingira

Catherine Kahuka (kushoto) na Gloria Wangeleja (kulia), wawakilishi kutoka taasisi ya PLPDF kupitia Shirika la Uhifadhi Mazingira Daniani (WWF), ofisi ya Tanzania wakipanda mtiti.

Na Asha Mwakyonde

SHIRIKA la Uhifadhi wa Mazingira  Duniani (WWF), ofisi ya Dar es Salaam Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Vodacom Tanzania imepanda miti mia moja na kuwatembelea akina mama waliojifungua katika Hospitali ya Taifa Muhimbili - Mloganzila  ikiwa ni kuelekea maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani ambayo hufanyika Machi 8, kila mwaka.

Upandaji miti huo ulienda sambamba na uchangiaji damu na utoaji zawadi kwa watoto waliozaliwa hospitalini hapo  ikiwa ni kujumuika pamoja na akina mama hao katika siku hiyo ya wanawake duniani.

Akizungumza jijini Dar es Salaam hospitalini hapo mara baada ya kufanya shughuli hizo Meneja Mawasiliano wa WWF, Joan Tanisa amesema kuwa shirika la uhifadhi mazingira kupanda  miti ni moja kati ya kazi zao za msingi.

Joan amesema mazingira yakiwa mazuri mama mwenye mzigo wa mkubwa wa kuilea familia yake  anaweza kupata nafuu na kwamba miti inapopandwa na kustawi vizuri  kutakuwa na upatikanaji wa maji ya kutosha  na mama huyo hatapata shida ya kutembea umbali mrefu kutafuta maji.

Amesema kuwa mwanamke ni kiungo katika suala la uhifadhi wa mazingira kwani shughuli nyingi anazozifanya zinahusiana na mazingira na kwamba ana nafasi ya kubwa ya kuelimisha familia yake juu ya uhifadhi huo.

"Kwa wanawake wenzetu wa vijijini wabaolima, wanaokwenda kutafuta kuni na ndio wanaohudumia familia hivyo ndio mwalimu wa kwanza wa kuweza kutoa elimu ya uhifadhi mazingira,"amesema Joan.

Ameongeza  kuwa wamepanda miti maeneo mbalimbali  hapa nchini hivyo wameona wafanye kitu gani ambacho kitangusa  mwanamke moja kwa moja katika yale ambayo anayafanya  kila siku.

Naye Meneja Ruzuku na Mawasiliano wa Taasisi ya Vodacom Sandra Oswadi amesema taasisi hiyo ni ya kujitolea kwa jamii  na kwamba wamejumuika na akina mama hao waliojifungua  kwa kupanda miti na kutoa zawadi kwa watoto.

"Siku hii tumekuja kupanda miti ambayo imetokana na mkakati wetu wa miaka mitatu wa kutunza mazingira. Kwa mwaka wa kwanza tumedhamiria kupanda miti 70,000 ambao unaishia mwishoni mwa mwezi huu,"amessema.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Uunguzi na Ukunga kutoka hospitali ya Nuhimbili - Mloganzila Redemptha Matindi  ametoa shukrani kwa WWF na taasisi ya Vodacom  kwa kupanda miti na kuungana na wanawake waliojifungua na kulazwa hospitalini hapo.
Share:

Friday, March 6, 2020

UMOJA WA WANAWAKE KITUNDA WAFANYA ZIARA KUTEMBELEA WENYE UHITAJI MAALUM

Afisa Maendeleo kata ya Kitunda, Sosina Soka (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule pamoja na Wanachama wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda akikabidhi msaada wa taulo za wasichana kwa wasichana waliopo katika kituo cha Kulea watoto yatima pamoja na wanaoishi katika mazingira magumu cha Camp Caleb katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kwa kata ya Kitunda yatafanyika tarehe 7 machi katika viwanja vya shule ya msingi Kerezange.
Baadhi ya Wanachama wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakikabidhi msaada wa godoro, unga na sukari kwa Mmoja wa wakazi wa kata hiyo mwenye mazingira magumu kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yatakayofanyika tarehe 8 machi. Umoja huo umefanya hafla ya kuwatembelea watu wenye uhitaji mbalimbali pamoja na kutembelea kituo cha watoto yatima cha Camp Caleb kilichopo mtaa wa Kipera kata ya Kitunda.  Matembezi hayo yamefanyika jijini Dar es Salaan jana.

Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakiongozana kwa pamoja wakiwa na misaada yao kueleka kwa watu wenye uhitaji katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani. Ni miongoni wa mwa mila na desturi za umoja huo kusaidia wenye uhitaji maalum. Matembezi hayo yamefanyika jijini Dar es Salaan jana.

Baadhi ya Wanawake wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakisalimiana na Mmoja wa wakazi wa Kitunda, Bibi Tausi Ramadhani baada ya kuwasili mahali alipohifadhiwa kwaajili ya kumkabidhi msaada katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani.
Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakikabidhi msaada wao kwa Bibi Tausi Ramadhani katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kwa kata ya Kitunda yanafanyika tarehe 7 machi katika viwanja vya shule ya msingi Kerezange.

Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakikabidhi msaada wao kwa Mwakilishi wa Bibi anayeishi katika mazingira Magumu Bibi Salum katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kwa kata ya Kitunda yanafanyika tarehe 7 machi katika viwanja vya shule ya msingi Kerezange.
Mwanachama wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda akizungumza jambo na watoto yatima pamoja na wanaishi katika mazingira magumu baada ya kuwasili katika kituo cha Kulea watoto hao cha Camp Caleb kilichopo katika mtaa wa Kipera kata ya Kitunda kwa ajili ya kutoa msaada katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kwa kata ya Kitunda yatafanyika tarehe 7 machi katika viwanja vya shule ya msingi Kerezange.
Baadhi ya Wanachama wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakiimba nyimbo za kukataa unyanyasaji wa kijinsia baada ya kuwasili katika kituo cha Kulea watoto yatima pamoja na wanaoishi katika mazingira magumu cha Camp Caleb kilichopo katika mtaa wa Kipera kata ya Kitunda kwa ajili ya kukabidhi msaada katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.
Afisa Maendeleo kata ya Kitunda, Sosina Soka akigawa biskuti kwa watoto wanaolelewa katika kituo hicho.
Wanachama wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakiwa katika picha ya pamoja na watoto wanaolelewa katika kituo cha Kulea watoto yatima pamoja na wanaoishi katika mazingira magumu cha Camp Caleb katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kwa kata ya Kitunda yatafanyika tarehe 7 machi katika viwanja vya shule ya msingi Kerezange.
Afisa Maendeleo kata ya Kitunda, Sosina Soka (wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Taasis ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), pamoja na Wanachama wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda msaada wa chandarua kwa watoto waliopo katika kituo cha Kulea watoto yatima pamoja na wanaoishi katika mazingira magumu cha Camp Caleb katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kwa kata ya Kitunda yatafanyika tarehe 7 machi katika viwanja vya shule ya msingi Kerezange.

HABARI KATIKA PICHA













Heri ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive