A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Wednesday, April 24, 2024

Benki ya Absa yaendeleza udhamini wake Absa Dar City Marathon

Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Aron Luhanga (wa pili kushoto) akionyesha fulana zitakazovaliwa siku ya mbio za Absa Dar City Marathon wakati wa hafla ya uzinduzi wa mbio hizo jijini Dar es Salaam jana, zinazotarajiwa kufanyika Mei 5 mwaka huu, jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Ofisa Masoko wa Hill Water, Sylvia Shoo, Mkuu wa Kitengo cha Habari wa Klabu ya The Runners, waandaaji wa Absa Dar City Marathon, Godfrey Mwangungulu, Meneja wa Bima Kibenki wa Alliance Life Assurance, Juma Patrice na Meneja Bima Binafsi, Jumanne Muruga.

BENKI ya Absa Tanzania imeendeleza udhamini wake kwa mwaka wa nne mfululizo katika mbio za Absa Dar City Marathon , ikilenga kuifanya Tanzania kuwa Taifa lenye watu wenye afya njema.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mbio za Absa Dar City Marathon 2024, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, Bwana Aron Luhanga alisema afya njema ni mtaji namba moja katika maendeleo ya Taifa la Tanzania na wanaokimbia wanajenga Afya.

Alisema lengo lingine kuu la Absa Dar City Marathon ni mapato yatayakayopatikana katika mbio hizo kuelekezwa katika shughuli za kijamii Kwa kununua vifaa vitakavyosaidia wodi ya wanawake katika hospitali ya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Pamoja na hayo kama kauli mbiu ya mbio hizi isemayo ‘Kata Mtaa, Ujue Jiji’ sisi kama Absa Bank, tukiwa na Matawi ya kibenki hapa jijini, tunajisikia fahari kusapoti mbio hizi zenye lengo pia la kutangaza vivutio vya utalii vilivyomo katika jiji letu."

Kauli yetu ya Absa inasema ‘Story Yako ina Thamani’ hivyo tunaamini kuwa ukienda kukimbia unaandika Story Yako, ukienda kusaidia jamii, unaandika Story Yako, nasi kama Absa, Story Yako Ina thamani sana kwetu”, alisema Bwana Luhanga.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa The Runners Club, Bwana Godfrey Mwangungulu alisema mbio za mwaka huu zinazofanyika chini ya udhamini mkubwa wa Benki ya Absa Tanzania zitashirikisha mbio za Kilomita, 21, 10 na Kilomita tano.

Absa Dar City Marathon ya mwaka huu inayotarajiwa kufanyika Mei 5 mwaka huu ikianzia katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, ni zaidi ya mbio, ni zaidi ya sherehe, ni kilele cha sherehe za mbio zote zinazoendelea kufanyika hapa nchini."

Tumefanya mbio hizi kwa miaka mitatu mfululizo, mwaka huu tunataka kuzifanya Kwa mafanikio zaidi, tunatarajia zaidi ya wakimbiaji 3000 kushiriki, tunawashukuru sana wadhamini wetu wakuu, Benki ya Absa pamoja na wadhamini wengine”, alisema Bwana Mwangungulu.

Mbali na Benki ya Absa kama mdhamini mkuu, wadhamini wengine ni Kampuni ya Alliance Life Assurance, Hill Water, Kilimanjaro Milk na Kampuni ya Garda Security.
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Aron Luhanga (wa tatu kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Mawasilino wa The Runners Club, Bwana Godfrey Mwangungulu (kushoto kwa Aron), pamoja na wawakilishi wa wadhamini wengine, wakionyesha fulana na vitu vingine vitakavyotumika wakati wa mbio za Absa Dar City Marathon, jijini Dar es Salaam Mei 5 mwaka huu, zikianzia katika Viwanja vya Mnazi Mmoja. Hafla hiyo ilifanyika jijini humo jana.
Share:

Saturday, April 20, 2024

ORYX GAS TANZANIA NA DORIS MOLLEL FOUNDATION WATOA MSAADA WA MITUNGI YA GAS YA KUPIKIA KWA WAUGUZI HOSPITALI YA MWANANYAMALA


Na Mwandishi Wetu 

JUHUDI za serikali kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia zimezidi kuungwa mkono baada ya Kampuni ya Gesi ya Oryx Tanzania kuingia mkataba na Taasisi ya Doris Mollel, kuwapatia mitungi na majiko ya gesi wauguzi kutoka mikoa 10 nchini.

Akizungumza wakati wa hafla ya kutia saini makubaliano hayo leo Aprili 19, 2024 katika Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala, Kinondoni Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Oryx, Benoite Araman amesema lengo la hatua hiyo ni kutanua matumizi ya nishati ya kupikia katika jamii.

Araman amesema matarajio ya Kampuni hiyo ni kuhakikisha kila Mtanzania anatumia nishati safi ya kupikia.

“Kunahitajika elimu ya kuhakikisha watu wanaokolewa dhidi ya matumizi ya nishati isiyofaa, tunatarajia kutoa majiko mengi zaidi na hadi sasa tumeshatoa majiko 32,000,” amesema.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel Foundation, Doris Mollel amesema lengo la kulifikia kundi la wauguzi anya ni kuhakikisha wanawaepusha na athari za matumizi ya nishati chafu ambayo ina madhara kwa jamii.

Doris, ameeleza ugawaji wa majiko hayo utawagusa wauguzi katika mikoa 10.

“Tunatambua nafasi ya wauguzi wa afya, wamekuwa na mchango mkubwa kwenye jamii, tunaona makundi mengine yakipewa majiko sisi tunaona ni muhimu tuwape wauguzi,” ameeleza.

Amebainisha kuwa, majiko hayo yatakabidhiwa kwa wauguzi walio katika mazingira magumu kuwaepusha na matumizi ya nishati yenye madhara 

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mwananyamala, Zavery Benela amesema matumizi ya nishati chafu ni moja ya sababu ya magonjwa mengi ya mfumo wa hewa kwa binadamu.

Ameeleza kati ya wagonjwa 500 wa nje wanaopokelewa katika hospitali hiyo, zaidi ya nusu wanasumbuliwa na magonjwa ya mfumo wa hewa.

“Haya ndiyo magonjwa namba moja kwa wagonjwa wengi kwenye hospitali yetu, tumekuwa tukiwapokea na ukiuliza namna anavyoishi utakuta anatumia nishati isiyofaa kupikia,” ameeleza.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel akisaini hati ya makubaliano ya ushirikiano na Kampuni ya Oryx Gas kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Kampuni ya gesi ya oryx Araman Benoite akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini na Taasisi ya Doris Mollel kushirikiana kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.






Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel (katikati) akizungumza katika hafla ya utiaji saini ya makubalinao na Kampuni ya Oryx Gas kushirikiana kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo
Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala mkoani Dar es Salaam Dk.Zavery Benela akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini na Taasisi ya Doris Mollel kushirikiana kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Kampuni ya gesi ya oryx Araman Benoite na Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel wakionesha mkataba waliosaini kwaajili ya kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Kampuni ya gesi ya oryx Araman Benoite na Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel wakimkabidhi mtungi wa kupikia wa gesi ya Oryx mmoja wa wauguzi katika hospitali ya rufaa ya Mwananyamala Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya utiaji saini makubalino kati ya kampuni ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Kampuni ya gesi ya oryx Araman Benoite akitoa elimu ya matumizi sahihi ya mtungi wa kupikia wa gesi ya Oryx kwa wauguzi wa hospitali ya rufaa ya Mwananyamala katika hafla ya utiaji saini kati ya kampuni ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Baadhi ya wauguzi wa hospitali ya rufaa ya Mwananyamala wakifuatilia hafla ya utiaji saini kati ya kampuni ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel akisaini hati ya makubaliano ya ushirikiano na Kampuni ya Oryx Gas kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Kampuni ya gesi ya oryx Araman Benoite akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini na Taasisi ya Doris Mollel kushirikiana kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.






Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel (katikati) akizungumza katika hafla ya utiaji saini ya makubalinao na Kampuni ya Oryx Gas kushirikiana kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo
Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Mwananyamala mkoani Dar es Salaam Dk.Zavery Benela akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini na Taasisi ya Doris Mollel kushirikiana kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Kampuni ya gesi ya oryx Araman Benoite na Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel wakionesha mkataba waliosaini kwaajili ya kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Kampuni ya gesi ya oryx Araman Benoite na Mkurugenzi wa Taasisi ya Doris Mollel , Doris Mollel wakimkabidhi mtungi wa kupikia wa gesi ya Oryx mmoja wa wauguzi katika hospitali ya rufaa ya Mwananyamala Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya utiaji saini makubalino kati ya kampuni ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Mkurugenzi wa Kampuni ya gesi ya oryx Araman Benoite akitoa elimu ya matumizi sahihi ya mtungi wa kupikia wa gesi ya Oryx kwa wauguzi wa hospitali ya rufaa ya Mwananyamala katika hafla ya utiaji saini kati ya kampuni ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Baadhi ya wauguzi wa hospitali ya rufaa ya Mwananyamala wakifuatilia hafla ya utiaji saini kati ya kampuni ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation kuwezesha nishati safi ya kupikia kwa wauguzi na madaktari 1000 kutoka mikoa 10 nchini watakabidhi mitungi ya kupikia ya Oryx Gas lengo likiwa kuliwezesha kundi hilo la sekta ya afya kuondokana na matumizi ya kuni na mkaa. Hafla hiyo imefanyika leo Aprili 19, 2024.
Share:

Sunday, April 14, 2024

ASASI YAUNGANA NA ORXY GAS TANZANIA KUSAIDIA WAATHIRIKA WA MAFURIKO RUFIJI

   

Mbunge wa Jimbo la Rufiji mkoani Pwani ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa (kulia), akipokea Moja ya msaada wa vitu mbalimbali vilivyotolewa na Kampuni ya Oryx pamoja na Asas kwaajili ya kusaidia waathirika wa mafuriko yaliyotokea wilayani Rufiji mkoani Pwani kutoka Kwa Meneja Mauzo wa Kampuni ya Oryx Shabani Fundi hafla ya makabidhiano hayo yamefanyika Leo.
Mbunge wa Jimbo la Rufiji mkoani Pwani ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa (katikati), akipokea Moja ya msaada wa vitu mbalimbali vilivyotolewa na Kampuni ya Oryx pamoja na Asas kwaajili ya kusaidia waathirika wa mafuriko yaliyotokea wilayani Rufiji mkoani Pwani kutoka Kwa Meneja Mauzo wa Kampuni ya Oryx Shabani Fundi, hafla ya makabidhiano hayo yamefanyika Leo. Kulia ni Meneja Uendeshaji wa Kampuni ya Asas Abdul Ally.

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Oryx Gas Kwa kushirikiana na Kampuni ya ASAS wamekabidhi msaada wa vyakula pamoja na mitungi ya gesi ya oryx kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa mafuriko yaliyotokea wilayani Rufiji mkoani Pwani.

Msaada huo umekabidhiwa leo Aprili 13,2024 jijini Dar es Salaam kwa Mbunge wa Jimbo la Rufiji mkoani Pwani ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa.

Akizungumza wakati akipokea msaada huo Waziri Mchengerwa amesema kwa niaba ya wananchi  wanaushukuru kwa kupatiwa msaada huo unaokwenda kusaidia wananchi waliopatwa na mafuriko na kwa sasa wamehifadhiwa kambini kutokana na kukosa makazi pamoja na vyakula.

"Tunaashuhudia kuwepo kwa muamko wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan ambaye yeye ni mfariji namba moja katika Taifa letu alioutoa kwa siku ya jana alipokuwa kule Arusha lakini taarifa ambazo amekuwa akizitoa kuwataka Watanzania kuwa wamoja na kusaidia wale ambao wana nafasi basi wajitolee kwa ajili ya wenzao,"amesema.

Ameongeza kuwa hivyo leo wanashuhudia shehena ya vyakula ambavyo vimetolewa na ASAS pamoja na Kampuni ya Oryx Gas ambapo Oryx wametoa mitungi pamoja na majiko ambayo wananchi wa Rufiji hasa walioko makambini watakwenda kutumia.

Pia Oryx kwa kushirikiana na ASAS wametoa vyakula ambavyo vitakwenda kutolewa kwa wananchi wote walioko makambini ambao wanahifadhiwa na wanahudumiwa na Serikali kwa wakati huu huku akitumia nafasi hiyo kumshukuru Rais Samia kwani tayari amekwisha elekeza  utolewaji wa shehena ya vyakula 

Ametaja vyakula hivyo ni  mchele  Maharage, unga pamoja naa vyakula  vingine ambavyo Rais Dk Samia ameelekeza kwenda Rufiji kwa ajili ya kusaidia wananchi waliokumbwa na mafuriko kwa mwaka huu.

"Niendelee kuwasihi Watanzania wote katika maeneo yao wale wenye nafasi wanaona wanataka kutoa kwa ajili ya ndugu zao tunawakaribisha Rufiji.Nitume nafasi hii kuwashukuru na kuwaomba tuendelee kushikamana katika kipindi hiki kugumu, tuendelee kuwa wamoja na kwamba mafuriko hayo hayakuanza mwaka huu yamekuwepo tangu enzi wa baba wa Taifa."

Awali kabla ya kukabidhi msaada huo, Meneja Mauzo wa Oryx Gas Shaban Fundi  amesema kwa niaba ya  Oryx Energies wanatoa pole kwa waathirika wote wa mafuriko yaliyotokea nchini hususan watu wa Rufiji.

"Kampuni ya Oryx Gas ikishirikiana na wadau wenzetu ASAS tumeamua tuwashike mkono wenzetu wa Rufiji kwa kuwapa msaada wa vyakula na mitungi ya gas ili kusaidia watu waliopo katika makambi ya kutolea misaada ya kibinaadam.

"Tumetoa mchele, unga wa sembe, mafuta ya kupikia yenye thamani ya zaidi ya milioni 52. Zaidi tumetoa mitungi mikunwa 100 na majiko 100, pia tumetoa mitungi midogo 100 yenye thamani ya zaidi ya mili 25.Tunampa pole muheshimiwa Waziri Mchengerwa, Wananchi wa Rufiji na Serikali kwa ujumla,"amesema Fundi.
Share:

Thursday, April 4, 2024

KAMPUNI ya Gesi ya Oryx Tanzania imeahidi kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kulinda afya za watanzania.

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani Meja Edward Gowele(wa tatu kushoto) akimkabadhi mtungi wa gesi ya Oryx Furaha Mawikia wakati wa hafla ya kukabidhi mitungi ya gesi na majiko yake 400 kwa wanawake wa vijiji vya Mwalusembe ,Kinene,Kitomondo na Kisele wilayani Mkuranga. Wengine pichani ni Balozi wa Heshima Shelisheli nchini Tanzania Maryvyonne Pool(watatu  kulia) Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Oryx Janeth Mutashobya (wa kwanza kulia), Katibu Tawala Wilaya ya Mkuranga Omary Mwanga.
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Meja Edward Gowele(kulia) pamoja na  Balozi wa Heshima wa Shelisheli nchini Tanzania Maryvyonne wakiangalia vyakula vya asili ya kitanzania ugali,wali na mboga ambazo vimepikwa kwa kutumia jiko la gesi ya Oryx wakati wa hafla ya kukabidhi mitungi ya gesi 400 yakiwa na
majiko yake kwa wanawake wa Kata ya Mwalusembe wilayani humo.
Baadhi ya wanawake wa Kata ya Mwalusembe wilayani Mkuranga mkoani Pwani wakiendelea kupika chakula kwa kutumia jiko la Oryx wakati wa hafla ya kukabidhi mitungi ya gesi ya Oryx kwa wanawake wa vijiji vya kata ya Mwalusembe wilayani Mkuranga.

Na Mwandishi Wetu, Mkuranga

Hayo yameelezwa na Meneja Usalama Afya na Mazingira wa Oryx Energies Tanzania, Janet Mutashobya, alipomwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo Benoite Araman wakati wa hafla ya kugawa mitungi 400 ya gesi na majiko yake kwa akinamama wa Kata ya Mwalusembe wilayani Mkuranga mkoani Pwani.

Ugawaji wa mitungi hiyo umefanyika kwa ushirikiano wa Balozi wa Heshima wa Shelisheli nchini Tanzania Maryvyonne Pool ambaye pia ni Mwanzilishi wa taasisi ya African Reflections Foundation ambayo imekuwa ikijihusisha na kusaidia jamii katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo

"Kupika kwa gesi ya Oryx ni kulinda mazingira kwa kuacha kukata miti. Pia ni kulinda afya ya wanawake kwa kuwaepusha kuvuta moshi na mvuke unaoathiri mapafu na afya yao unaotokana na kuni na mkaa," amesema.

Ameongeza kupika kwa kutumia nishati safi kunafungua fursa kwa wanawake kutumia muda mwingi kujishughulisha na shughuli za uzalishaji wa kiuchumi.

"Kwa kuanawake wanatumia muda mchache kupika hivyo wanapata nafasi kufanya shughuli nyingine za maendeleo na kuepuka kugombana na wenza wao kwa kuchelewesha chakula. Kwa kutumia gesi ya Oryx, Watoto wanakua na muda mwingi zaidi kusoma na sio kwenda kutafuta kuni,"amesema Mutashobya.

Aidha amesema kwa  miaka mingi Oryx Gas imekuwa kampuni kiongozi katika kukuza matumizi ya Gesi nchini Tanzania na Kuanzia Julai  mwaka 2021 wamekuwa mstari wa mbele kutekeleza maelekezo ya Serikali waliyopokea toka kwa Rais Dk.Samia Suluhu Hassan ifikapo mwaka 2023 asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia.

Amesema kupitia mipango hiyo Oryx Gas inataka kutokomeza matumizi ya nishati chafu ya kuni na mkaa ambayo si tu mbaya kwa afya zetu bali pia ni hatari kwa mazingira yao  na pia Oryx Gas inatekeleza juhudi za kueneza matumizi ya nishati safi kwa Watanzania wengi ipasavyo ambayo ni ndoto kubwa ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake Balozi Pool amesema  uamuzi wa kushirikiana na Oryx kutoa mitungi hiyo kwa wanawake wa vijiji vya kata vya Mwalusembe, unatokana na kutambua na kuunga mkono jitihada za Rais Samia za kuhamasisha nishati safi ya kupikia.

“Hii kwangu si mara ya kwanza kwani mwaka 2022 nilinunua mitungi ya gesi na kugawa kwa wanawake wa Mkuranga kwa sababu mimi ni balozi wa heshima hapa Mkuranga. Ndio maana nimekuwa nikishiriki katika miradi ya maendeleo ukiwemo wa kilimo cha kisasa cha umwagiliaji,” amefafanua.

Ameeleza taasisi yake imekuwa ikiwasidia wanawake na vijana kulima, huku akibainisha kuwa hatua hiyo ya kusaidia wanawake hao kupata nishati safi ya kupikia imetokana na kutambua mchango wa Rais Dk. Samia baada ya kuwa champion wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi.

"Kulifanyika mkutano wa mazingira wa kimataifa Dubai ambapo Rais Samia alichaguliwa kuwa champion wa kuhamasisha nishati safi ya kupikia , hivyo ni vema kumuunga mkono Rais Samia katika ajenda hiyo.

“Katika ule mkutano nilikaa meza moja na Rais (Dk.Samia) pamoja na Bilionea wa Marekani Bill Gate ambapo Rais Samia alichaguliwa kuwa champion wa Afrika katika kuhamasisha nishati safi, hivyo anastahili pongezi na nimeahidi kuunga mkono na kumsaidia kadri nitakavyoweza,”amesema Balozi Pool.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Rufiji ambaye pia anakaimu nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Meja Edward Giwele, amesema umefika wakati wa kumuunga mkono kwa vitendo Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Amesema kufanya hivyo kutasaidia kuokoa mazingira na kutanua fursa za kiuchumi hususan kwa wanawake wa wilaya hiyo nan a maeneo mengine nchini.

"Tumegawa mitungi ya gesi 400 kwa wanawake wa kijiji cha Kinene katika kata ya Mwalusembe ndani ya wilaya Mkuranga ikiwa sehemu ya mwendelezo wa jitihada za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha tunatumia nishati safi au nishati mbadala na kuachana na matumizi ya kuni na mkaa."

Amewapongeza Oryx na Balozi Pool Afrika Reflections Foundation kwa kushirikiana na kuhakikisha wanagwa mitungi hiyo kwa akinamama tena wa hali ya chini kabisa katika kijiji hiki cha Kinene.

Awali KatibuTawala Wilaya ya Mkuranga Omar Mwanga, amesema Wilaya  hiyo ni miongoni mwa wahanga wa uharibifu wa mazingira kwani misitu mingi ya asili imekatwa mkaa kwa matumizi mbalimbali ikiwemo kuwivisha chakula.

"Miti inakatwa kwa ajili ya kuchoma mkaa katika maeneo yetu, misitu ya vijiji ambayo imehifadhiwa na mingine ya asili imekuwa ikiathirika na wananchi kufanya shughuli za kijamii hasa zaidi ya hizi shughuli za ukataji mkaa, kwa hiyo na sisi tunaendelea kuhamasisha kama wanavyofanya Kampuni ya Gesi ya Oryx Tanzania.
Share:

MKANDALASI MKUU WA UJENZI WA RELI YA UMEME KAMPUNI YA YAPI MERKEZI YAWAKUMBUKA WATOTO MWEZI HUU WA RAMADHANI





Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KAMPUNI ya Yapi Merkezi, ambayo ni Mkandarasi Mkuu wa Reli ya umeme (SGR), imetoa msaada kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha Mama Mwana kilichopo Vingunguti jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu yao ya kujitolea kwa Jamii. Mchango huo umelenga kutoa mahitaji muhimu kwa watoto wanaoishi katika kituo hicho kwa wakati wa sikukuu zijazo za Eid El fitir.

Kampuni hio imetoa msaada wa bidhaa mbalimbali ikiwemo chakula, vifaa vya usafi, mafriji , nguo za Eid ikiwa ni sehemu moja ya kuwapa faraja watoto hao katika kipindi hiki cha sikukuu.

Bi Amisa Juma, Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano Yapi Merkezi, alitoa shukrani zake za dhati kwa kupata fursa ya kusaidia Kituo cha Watoto Yatima cha Mama Mwana. Alisema, "Yapi Merkezi ina nia ya dhati ya kuleta matokeo chanya katika jamii tunazofanyia kazi. Tunapokaribia msimu wa sikukuu ya Eid, ni jukumu na Furaha kwetu kutoa msaada kwa Kituo cha watoto yatima cha Mama Mwana na kuleta tabasamu kwenye nyuso za hawa watoto wanaostahili."

Bi Juma aliongeza zaidi, "Mchango wetu unaakisi tunu kuu za Yapi Merkezi nazo ni ukarimu, na uwajibikaji wa kijamii.

Tunatumai kupitia mchango huu, tunaweza kuwapa faraja na furaha watoto wa kituo cha Mama Mwana, huku tukiendelea kuwakumbusha kuwa wana haki ya kuthaminiwa na kutunzwa, pamoja na kuhimiza zaidi Makampuni mengine ya kiserikali na kibinafsi kuendelea kufariji Jamii hizi.

Hafla ya kukabidhi msaada huo, iliyoambatana na furaha na shukrani, ilihudhuriwa na wawakilishi kutoka Menejimenti na wafanyakazi wa kampuni ya Yapi Merkezi wakiongozwa na Bw. Levent Doruck, kama Afisa Mkuu wa Fedha wa kampuni iyo, ambaye aliwasilisha dhamira ya dhati ya kampuni hiyo ya kuendelea kusaidia juhudi zinazoendelea za kuboresha mazingira ya watoto yatima au wanaoishi katika hali ngumu.

Mlezi mkuu wa kituo cha Mama Mwana Bi Saada Omar, alitoa shukran zake za dhati na kupongeza kampuni ya Yapi Merkezi kwa moyo na ukarimu wao , huku akiendelea kusisitiza faida na umuhimu wa michango hiyo kwa ustawi wa Watoto hao.

Yapi Merkezi imeahidi kuendelea kukuza ushirikiano na kituo cha Watoto Yatima cha Mama Mwana, ikisisitiza dhamira yake ya uwajibikaji wa kampuni kwa jamii na mipango ya maendeleo ya jamii
Share:

Benki ya Absa kuendelea kuwezesha hadithi za watoto kielimu

Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Lilian Swere akizungumza katika hafla ambayo benki hiyo pia ilikabidhi msaada wa vifaa vya shule kwa watoto yatima wanaolelewa wa vituo vya Tuyata Orphanage Centre na Watoto Wetu Tanzania vilivyopo chini ya Taasisi ya Adonai El Roi Foundation jijini Dar es Salaam jana.

Na mwandishi wetu, Dar es Salaam.

Benki ya Absa Tanzania imesema itaendelea kuweka kipaumbele katika kufanikisha ndoto za kielimu za watoto wa kitanzania katika kuboresha huduma za kibenki zinazohusu watoto, hususan akaunti yake maalumu ya watoto ya Absa Child Savings Account.

Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla waliyowaandalia watoto wenye uhitaji kutoka katika vituo vya watoto yatima vilivyo chini ya Taasisi ya Adonai El Roi, Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya Absa, Bi. Ndabu Lilian Swere alisema hayo yanaenda kupitia lengo kuu la Benki Absa ambalo ni kuiwezesha Afrika na Tanzania ya Kesho Pamoja hatua Moja baadae ya nyingine kiuchumi sambamba na ahadi mpya ya Chapa yake isemayo ‘Story Yako ni ya Thamani’.

Watoto wana ndoto nyingi katika maisha yao, wapo wanaotamani kuwa madaktari, wanasheria, viongozi wa makampuni, viongozi wa kisiasa, tunathamini Story za watoto wetu, Absa tupo hapa kuwasapoti ili waweze kikamilisha ndoto za story zao.

Absa inatoa Huduma za kibenki kwa makundi mbalimbali, ni kwa kutumia huduma hizi pia tunawezesha hadithi za wazazi ama walezi wa watoto hawa nao pia kuweza kikamilisha hadithi zao mbalimbali za kiuchumi.

Hii si mara ya kwanza kwa Absa kufanya shughuli za kujitolea kusaidia jamii, hivi karibuni tulisaidia watoto wanaozaliwa kabla ya siku zao, hawa pia tutaangalia ni namna gani nyingine bora zaidi ya kuwasaidia”, aliongeza Bi Ndabu.

Akizungumza kuhusu akaunti ya watoto ya benki hiyo, Mkuu wa Mkakati na Bidhaa za Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Heristraton Genesis alisema akaunti hiyo haina makato ya mwezi na anaweza kupokea riba hata mara mbili endapo hatatoa pesa zaidi ya mara moja katika kipindi cha miezi mitatu.

katika kuonyesha Benki ya Absa imejipanga vizuri katika kuziwezesha ndoto za watoto, tunatoa riba mara mbili katika kile kiasi kilichokaa ndani ya miezi mitatu Ili kuwarejeshea watoto waweze kukamilisha story za ndoto zao za kielimu.

Ni rahisi kufungua akaunti hii, mahitaji ni kitambulisho cha taifa cha mzazi ama mlezi, cheti cha kuzaliwa cha mtoto ama utambulisho wowote kutoka shule anakosoma mtoto, na akaunti inaweza kuendeshwa kwa kutumia huduma zetu za kidigitali bila kuhitajika kufika katika matawi ya benki”, alisema Bwana Genesis.

Naye Mwanzilishi wa asasi ya Adonai El Roi inayolea vituo mbalimbali vya watoto nchini, Bi. Ngole Melaisho alisema lengo lao kubwa la shirika lao lisilo la kiserikali pamoja na mambo mengine ni kutokomeza umasikini katika vituo hivi.

Taasisi yetu Ina malengo ya kuwafuatilia watoto hawa kwa umakini waweze kuendeleza ndoto zao kwa kupitia kukuza vipaji vilivyo ndani yao.

Nipende kuhamasisha watanzania waendelee kusaidia vituo hivi na pia kuongeza upendo kwa watoto hawa waweze kukamilisha malengo yao”, aliongeza Bi. Ngole.
Mkuu wa Mikakati na Bidhaa za Wateja Binafsi wa Benki ya Absa, Bwana Heristraton Genesis akizungumza katika hafla ambayo benki hiyo pia ilikabidhi msaada wa vifaa vya shule kwa watoto yatima wanaolelewa wa vituo vya Tuyata Orphanage Centre na Watoto Wetu Tanzania vilivyopo chini ya Taasisi ya Adonai El Roi Foundation jijini Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Lilian Swere (wa pili kulia) akikabidhi begi lenye vifaa vya shule kwa mmoja wa watoto wanaolelewa katika Kituo cha Watoto Wetu Tanzania, Johnson Helman katika hafla iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Mikakati na Bidhaa za Wateja Binafsi, Bwana Heristraton Genesis (kulia) na Meneja Kitengo cha Kadi wa benki hiyo, Elfrida Mruma wakishirikiana kutengeneza keki na watoto yatima wa vituo vya Tuyata Orphanage Centre na Watoto Wetu Tanzania vilivyopo chini ya Taasisi ya Adonai El Roi Foundation katika hafla ambayo benki hiyo pia ilikabidhi msaada wa vifaa vya shule kwa watoto hao jijini Dar es Salaam jana
Meneja Msaidizi wa Hoteli ya Johari Rotana, Ahmed Said (kulia) akikabidhi begi lenye vifaa vya shule kwa mmoja wa watoto wanaolelewa katika Kituo cha Watoto Wetu Tanzania, Abigael Maliki katika hafla iliyoandaliwa na Benki ya Absa kwa kushirikiana na hoteli hiyo kwa watoto wa vituo vya Watoto Wetu na Tuyata vilivyo chini ya Taasisi ya Adonai El ROI, jijini Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Kitengo cha Bima wa Benki ya Absa Tanzania, Sandeep Chavda (kushoto), Mkuu wa Mikakati na Bidhaa za Wateja Binafsi, Bwana Heristraton Genesis, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Maalum, Thereza Majinge na Meneja Kitengo cha Kadi wa benki hiyo, Elfrida Mruma wakipiga picha ya pamoja na watoto wa watoto yatima wa vituo vya Tuyata Orphanage Centre na Watoto Wetu Tanzania vilivyopo chini ya Taasisi ya Adonai El Roi Foundation baada ya kukabidhi msaada wa vifaa vya shule katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Share:

Friday, March 29, 2024

KAMPUNI YA MAFUTA YA PUMA TANZANIA WAYAKUMBUKA WATEJA WAKE

KAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha watanzania na wadau mbalimbali katika futari iliyoandaliwa na Kampuni hiyo huku ikitumia nafasi hiyo kuwaomba Watanzania kuendelea kutumia bidhaa zinazotoka Kampuni hiyo 
Hafla ya futari iliyoandaliwa na Kampuni hiyo ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wake Fatma Abdallah imefanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa wadau mbalimbali wakiwemo wakuu wa taasisi za umma na binafsi pamoja na wateja wa kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Mgeni rasmi katika Iftar hiyo alikuwa Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Walid aliyewakilishwa na Sheikh wa Wilaya ya Temeke ...

Akizungumza wakati wa Iftar hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni hiyo Dk Selemani Majige ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa ni vema kila Mtanzania kwa nafasi yake kuendelea kuliombea Taifa sambamba na kumuunga mkono Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.
"Tunafahamu kwa sasa tunaendelea na Mfungo wa Ramadhan pamoja na Kwaresima hivyo wakati tukiendelea na Mfungo ni vema tukaliombea Taifa letu lakini wakati huo huo kudumisha Umoja,amani na mshikamano,"amesema Dk Majige.

Amesisitiza kuendelea kudumisha amani katika nchini Kunafanya uchumi Wetu kuendelea kuimarika  na biashara zetu ziendelee vizuri."Kulinda amani ni jambo kubwa kwani kama hakuna amani basi hata biashara haziwezi kufanyika vizuri.

"Hivyo kupitia mwezi mtukufu wa Ramadhan ni vema kuendelea kumuomba Mungu na kuendelea kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ili aendelee kutuongoza na kudumisha amani katika taifa letu."
Pia amewaomba Watanzania kuendelea kutumia mafuta  ya Puma Energy Tanzania pamoja na bidhaa zake zote huku akifafanua mafuta ya Kampuni hiyo yana ubora na viwango vya hali ya juu.

"Tunawaomba muendelee kutumia mafuta ya Puma  ili tuongeze faida na tukiongeza faida Serikali inapata gawio na inapotoa gawio zinapatikana fedha ambazo zinakwenda kuhudumia jamii katika maeneo mbalimbali,"
Kwa upande wake Sheikh wa Wilaya ya Temeke Sheikh Zailai Hassan Mkoyogole aliyemwakilishwa  Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Omar  aliyekuwa mgeni rasmi, amesema kipindi hiki cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan jambo kubwa ni kuzidisha wema kwa maana wanadamu ni wakosaji mbele za Mwenyezi Mungu.

"Binadamu anamkosea Mwenyezi Mungu kwa vitu vingi hivyo sasa ameleta Mwezi mtukufu wa Ramadhan ili kutubu kwa yale yote ambayo ameyafanya.Hivyo kinachotakiwa katika mwezi huu ni kufanya yale yaliyomema na kurejea  kwake,"
Pia amesema Mwenyezi Mungu anapenda kuombwa ,hivyo ametoa wito kwa watu wote kurejea kwa Muumba  na kuomba msamaha.

Awali Mkurugenzi Mkuu wa Puma Energy Tanzania Fatma Abdallah  amewashukuru wadau  kwakuitikia wito  katika futari hiyo huku akitumia nafasi hiyo kuwaomba Watanzania kuwaunga mkono kwa kununua bidhaa za mafuta ya Kampuni hiyo.

Aidha amesema  kama Puma Energy Tanzania wataendelea kuunga mkono juhudi za Serikali hasa katika utekelezaji matumizi ya  nishati safi ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa lengo la  kuendelea kutunza mazingira .

"Puma  Energy Tanzania tunatambua mwelekeo wa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na hasa kwenye suala la nishati safi hivyo tutaendelea kua mstari wa mbele kutoa elimu kwa lengo la kuhakikisha   mazingira yanalindwa na matumizi ya nishati  safi kwa watanzania yanakuwa kipaumbele."

Wakati huo huo Mkurugenzi Mkuu UDA- RT  Waziri Kindamba aliyeshiriki futari hiyo amewapongeza kwa kuandaa futari hiyo ni kuwaalika wateja wao ambao wanatumia bidhaa zao ikiwemo vilainishi na mafuta.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive