A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Wednesday, June 21, 2023

Mheshimiwa Spika akutana na Uongozi wa juu wa Benki ya Absa Tanzania na kufanya mazungumzo

  
Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson (kulia) akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser, wakati yeye na ujumbe wake ukimtembelea ofisini kwake, bungeni, Dodoma Jana.
Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson (kushoto) kuzungumza na na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser, wakati yeye na ujumbe wake ukimtembelea ofisini kwake, bungeni, Dodoma Jana.
Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson (wa tatu kushoto) akipiga picha ya kumbukumbu pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser (kulia kwake), wakati yeye na ujumbe wake ukimtembelea ofisini kwake, bungeni, Dodoma Jana.
Share:

Airtel Afrika yaitaja Tanzania Miongoni mwa nchi Tatu kuwashwa Masafa ya Teknolojia ya Mawasiliano ya kasi ya 5G

  
  • Airtel Tanzania miongoni mwa himaya tatu za Airtel zitakazohamia teknolojia ya 5G hivi karibuni
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Airtel Africa, kampuni inayoongoza katika kutoa huduma za mawasiliano na za kuhamisha pesa kwa kutumia simu za mkononi, ikiwa imejikita katika nchi 14 barani Afrika, leo hii nchini Nigeria imezindua mchakato wa kuhamia masafa ya mtandao wa 5G ili kutoa huduma za kisasa na kasi Zaidi kwa wateja wake wote huku ikibainisha Tanzania itafuta kuwashwa kwa teknolojia hiyo ya mawasiliano ya kisasa ya 5G.

Uzinduzi wa masafa hayo ya mtandao wa 5G utafanyika awali katika nchi tatu ikianza Nigeria, ikifuatiwa na Tanzania na Zambia, huku mipango ikiwa inaandaliwa ya kusambaza maeneo yaliyobaki kwenye soko zima.

Kwa kutumia 5G, wateja sasa wanaweza kufurahia kuangalia video zikiwa ngáavu zaidi ya ilivyo sasa, kufurafia kutazama michezo mtandaoni, kurusha matukio mubashara Pamoja na kufurahia kasi zaidi wakiwa popote. Kutokana na kwamba wigo wa mawasiliano utapanuka zaidi kutokana na teknolojia ya kisasa ya 5G pia shughuli za biashara zitaimarika hasa zile zinazotumia mtandao kutoa huduma zake, pamoja na kufanikisha mikutano ya mbali mubashara kupitia mtandao.

Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Airtel Afrika Group, Segun Ogunsanya alisema: “Kupitia mtandao wa 5G, tunawapa wateja wetu fursa ya kuishi kidijitali kwa kufurahia maajabu yanayoweza kufanywa na mtandao huu wa teknolojia ya mawasiliano ya kisasa ya 5G. Kwa kukamilisha hili kwa nchi zetu hizi tatu Ikiwemo Tanzania tunadhihirisha tunadhihirisha dhamira yetu tuliyojiwekea ya kuwekeza katika teknolojia ya mtandaoni ya kisasa zaidi ili kufungua wigo mpana na kutoa fursa kwa watumiaji kufanya makubwa, tunawezesha kuiunganisha dunia kidijitali pamoja na wateja wetu kukamilisha maono waliyonayo.

Mtandao wa 5G utajikita zaidi katika maeneo maalum, mfano maeneo ya makazi yenye msongamano mkubwa wa watu na yale yenye huduma kama maduka, hospitali, maeneo ya kati ya mji na maeneo makuu ya kibiashara na mjini. Wakiwa katika maeneo haya mahsusi ya 5G ambayo yatatambulika rasmi na kuwekewa alama, wateja wanaweza kufurahia mtandao kwa kasi ya mara kumi zaidi ya kawaida, na kurusha picha za video za ubora wa hali juu mubashara bila ya kukatika katika. Mtandao wa 5G unaweza kuunganishwa tu kupitia vifaa vinavyoendana nao.
Share:

Tuesday, June 20, 2023

Benki ya Absa yajitosa kuokoa maisha ya Watoto Njiti

  
Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete (kulia), akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser katika hafla ya makabidhiano wa msaada wa vifaa vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti) wakiwa hospitalini. Benki ya Absa imetoa ufadhili wa kiasi cha shs milioni 30 kwa taasisi ya Doris Mollel Kwa ajili hiyo. Kushoto ni Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Doris Mollel.
Rais Mstaafu wa awamu ya nne, mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akizunguza katika hafla ya makabidhiano wa msaada wa vifaa vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti) wakiwa hospitalini. Benki ya Absa imetoa ufadhili wa kiasi cha shs milioni 30 kwa taasisi ya Doris Mollel kwa ajili hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Obedi Laiser(katikati), akizungumza katika hafla ya makabidhiano wa msaada wa vifaa vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti) wakiwa hospitalini. Benki ya Absa imetoa ufadhili wa kiasi cha shs milioni 30 kwa taasisi ya Doris Mollel Kwa ajili hiyo. Kushoto kwake ni Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais Mstaafu wa awamu ya nne, mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati), akikata utepe kuzindua hafla ya makabidhiano ya msaada wa vifaa vitakavyosaidia huduma za watoto wanaozaliwa kabla ya muda (Njiti) wakiwa hospitalini. Benki ya Absa imetoa ufadhili wa kiasi cha shs milioni 30 kwa taasisi ya Doris Mollel kwa ajili hiyo.
Mkurugenzi wa taasisi ya Doris Mollel Foundation, Doris Mollel akitoa shukurani Kwa mgeni rasmi, benki ya Absa na wote wakiofanikisha upatikanaji wa vifaa hivyo vitakavyosaidia kuokoa maisha ya watoto nyiti wakiwa hospitalini.
Share:

Sunday, June 18, 2023

Benki ya DCB yazidi kujiimarisha kimtaji na kuendelea kupata faida

   
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Alexander Sanga (wa tatu kushoto) akiwa na baadhi ya wajumbe wa bodi ya benki hiyo wakati wa Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo 2023 jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni Mwanasheria wa benki hiyo, Alex Mgongolwa, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, Isidori Msaki na wajumbe wengine; Dk. Amina Baamary, Cliff Maregeli na David Shambwe.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Alexander Sanga akifungua Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo jijini Dar es Salaam jana
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Isidori Msaki akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo jijini Dar es Salaam jana
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Dk. Amina Baamary (kulia) akizungumza na baadhi ya wanahisa na wajumbe wengine wa bodi hiyo, baada ya kumaliza Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo jijini Dar es Salaam Jana.
Sehemu ya wanahisa wa Benki ya DCB wakihudhuria Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo, jijini Dar es Salaam jana.

Na Mwandishi Wetu,

BENKI ya Biashara ya DCB imeendelea kujivunia kuongezeka kwa mtaji wake huku ikijiendesha kwa faida inayoongezeka kila mwaka licha ya changamoto kadhaa za kiuchumi, wanahisa wa benki hiyo wameelezwa jijini Dar es Salaam jana

Akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Wanahisa wa DCB, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo, Bi. Zawadia Nanyaro alisema benki yao ipo imara kimtaji unaofikia kiasi cha shs 28.5 bilioni unaovuka vigezo vya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) vya shs 15 bilioni vilivyowekwa kwa benki za biashara.

Benki yetu ilipata faida baada ya kodi ya shs 747 milioni kwa mwaka 2022, faida iliyochangiwa na mapato yasiyotokana riba ya shs 10.3 bilioni ambayo ni mafanikio ya asilimia 111 ya malengo tuliyojiwekea kwa mwaka 2022, huku mapato yatokanayo na riba yakifika shs 28.6 bilioni ikiwa ni asilimia 86 ya malengo tuliyojiwekea".

Mazingira ya uendeshaji wa taasisi za fedha kwa mwaka 2022 yaliendelea kuwa tulivu huku thamani ya shilingi ya kitanzania ikiendelea kuimarika dhidi ya mataifa mengine, uchumi ukikua tena baada ya janga la Uviko-19, mfumuko wa bei ukiendelea kuwa chini kwa mwaka mzima, mafanikio katika sekta ya utalii na kufunguliwa kwa milango ya biashara kumechagiza kwa DCB kuendelea kufanya vizuri sokoni”,

Akizungumzia utendaji wa benki, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa wa benki hiyo Bw. Isidori Msaki alisema DCB imekuwa makini katika kusimamia mikakati yake ya muda mrefu jambo linaloleta matokeo chanya ikiwemo kukua kwa mali za benki.

Mwaka 2022 mali za benki zimekuwa hadi kufikia shs 211 bilioni kutoka shs 192 bilioni kwa mkwa 2021, ukuaji ulioitoa benki yetu kutoka kwenye kundi la benki ndogo za biashara hadi kufikia benki za kati nchini."

DCB imeendelea kulinda thamani ya wanahisa wake kwa kukuza mapato yasiyotokana na riba kutoka asilimia 30 ya mapato yote mwaka 2021 hadi kufikia asilimia 49 kwa mwaka 2022 ongezeko lililotokana na kuimarika kwa mifumo ya kidigitali inayochangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la miamala kwa zaidi ya asilimia 135”, alisema Bwana Msaki.

Akizungumzia baadhi ya vipaumbele vya benki hadi ifikapo mwaka 2025 kwa wanahisa waliofurika katika ukumbi wa JK Nyerere International Conference Centre jijini humo mkurugenzi huyo alisema ni kuhakikisha huduma za benki hiyo zinapatikana nchi nzima na hiyo inawezekana kwa kupitia hatua mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa ikiwa ni pamoja na kuimarisha huduma zake kwa njia za kidigitali.

Tumeanzisha vituo vidogo vya huduma katika maeneo ya kimkakati, huduma za mawakala zaidi ya 700 nchini kote pamoja na mtandao wa matawi saba ndani na nje ya mkoa wa Dar es Salaam".

Benki yetu inalenga kuongeza wigo wa kutoa mikopo kwa njia za kidigitali kwa kiwango kikubwa ifikapo mwaka 2025, mwaka 2022 tulitoa mikopo isiyopungua shs 1.2 bilioni, mikopo hii ni salama zaidi kwa sababu inalipwa ndani ya kipindi cha mwezi mmoja” , aliongeza mkurugenzi huyo.

Aidha mkurugenzi huyo alisema DCB inaendelea na mkakati wake wa kuhakikisha inapata faida mwaka hadi mwaka ili kufikia thamani ya hisa ya asilimia 18.9 na kuendelea kupunguza uwiano wa mikopo chechefu hadi kufikia chini ya asilimia 5 na pia kuongeza idadi ya wateja.

Aliwaomba wanahisa hao kuzidi kuwekeza ndani ya benki yao na kuzidi kuiamini menejimenti na bodi kwani uwekezaji wao umeleta faida kubwa kwa maisha ya watoto wa watanzania kwani umewawezesha kutoa msaada wa madawati kwa shule zenye uhitaji mkubwa jambo linalowapa amani watoto hao kusoma katika mazingira bora.

Ni kwa uwekezaji wenu wanahisa wetu uliotuwezesha pia kutoa elimu ya ujasiriamali kwa watanzania, elimu hii ni muhimu katika maendeleo ya biashara na maisha yao, tutaendelea kuimarisha ufanisi wa utendaji kazi wetu ili kuendelea kuleta matokeo chanya”, alisema.

Pamoja na kupata faida ya baada ya kodi ya sh 747 milioni 2022, na kwa kuzingatia sheria ya Benki Kuu, Bodi ya Wakurugenzi ya DCB imependekeza faida iliyopatikana ikaongeze fedha za wanahisa badala ya kutoa gawio.
Share:

Friday, June 2, 2023

USHIRIKIANO WA KIBIASHARA WA BENKI YA TBC NA ALAT WAANZA KWA KISHINDO

Uhusiano wa kufanya kazi kwa karibu kati ya Benki ya Biashara Tanzania (TCB) na Jumuiya ya Tawala za Serikali za Mitaa (ALAT Taifa) umeanza kwa kishindo kiuwezeshaji na ahadi za kushirikiana kibiashara ili kuisaidia serikali kulijenga taifa na kuwahudumia vyema wananchi.

Wiki hii, taasisi hizo mbili zimesema zimejipanga vizuri kuunganisha nguvu zao kutimiza azma hiyo na ziko tayari kuhakikisha zinafanya kila linalowezekana kusaidia kuboresha maisha ya Watanzania na kuchangia maendeleo ya kiuchumi nchini.

Na kwa mara ya kwanza, TCB imeshiriki mkutano mkuu wa mwaka wa ALAT ambao mara hii umefanyika kwa siku mbili jijini Arusha kuanzia Jumatatu. Mbali na ushiriki huo, benki hiyo pia ilikuwa mmoja wa wadhamini wake kwa ufadhili wa TZS 100 milioni.

Benki ya TCB ilitumia fursa hiyo kujinadi si tu kwa washiriki zaidi ya 500 wa mkutano huo lakini pia hata kwa wajumbe wa ALAT na viongozi wa wanachama wa jumuiya hiyo ambao ni halmashauri zote 184 nchini.

Wakitoa maoni yao kuhuss ushirikiano huo, wana ALAT walisema hilo ni jambo ambalo jema na wako tayari kufanya kazi kwa karibu na TCB kwani kufanya hivyo si tu ni jambo la kimaendeleo kwa taifa lakini pia la kizalendo.

“Kwa namna ya kipekee niwashukuru TCB kwa uhusiano huu na tunawahakikishia mchango mkubwa wa kibiashara kutoka kwetu kama taasisi pamoja na wanachama wetu wote kwa ujumla,” Meya wa Mwanza, Bw Sima Constantine ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa ALAT Taifa alisema.

Hiyo ilikuwa ni kwenye hafla iliyoandaliwa na TCB kama sehemu ya udhamini wake wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa 37 wa ALAT uliofanyika katika ukumbi wa AICC na kufunguliwa rasmi Jumatatu na Makamu wa Rais, Dkt Philip Mpango.

Wajumbe wa mkutano huo, akiwemo Bi Halima Mchoma, diwani kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu, Mtwara, alisema kufanya kazi na TCB ni kusaidia kuiwezesha serikali hasa kimapato.

Wengine, kama Bw Bahati Heneriko, mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa ya Kagera, walisema kufanya biashara na TCB pia kuna tija kimaslahi ya taifa kwa sababu ndiyo benki pekee inayomilikiwa kwa kiasi kikubwa na serikali.

“Kwa jinsi muundo wa umiliki wake ulivyo, hii ndiyo benki yetu Watanzania wote ambayo kila mtu anapaswa kuiunga mkono izidi kushamiri na kuchangia kikamilifu maendeleo yetu,” Mwenyekiti wa Hamashauri ya Wilaya ya Kibondo, Bw Habili Charles Maseke, aliliambia gazeti hili.

“TCB ni benki ya taifa na ya kizalendo kutokana na serikali kumiliki asilimia 83 ya hisa zake. Kwa hilo, tuipe ushirikiano stahiki,” kiongozi huyo kutoka Kigoma aliongeza na kuichagiza TCB kujitanua zaidi kwa kupeleka huduma zake katika maeneo ambayo haipo kwa sasa kama Kibondo.

Awali kwenye wasilisho lake siku ya Jumatatu, Afisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Bw Sabasaba Moshingi, alisema wao ndiyo wenye mtandao wa tatu mpana wa matawi ambayo ni 82 nchi nzima yanayosaidiwa na ATMs 86 na zaidi ya mawakala 5000 kulihudumia taifa.


Mbali na serikali, Bw Moshingi alisema wamiliki wengine wa TCB ni Shirika la Posta lenye hisa asilimia nane, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (3%), Posta na Simu Saccos (3%), PSSSF (2%) na Mfuko wa Fidia ya Wafanyakazi (WCF) (1%).

Lililomvutia zaidi kiongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini A ya Zanzibar, Bw Mchano Fadhil Babra, ni pale CEO Moshingi aliposema siku si nyingi TCB itafikisha miaka 100. Sasa hivi benki hiyo ina uzoefu wa kuwepo sokoni kwa miaka 97 ikichangia ujenzi wa taifa kupitia huduma mbalimbali hususani zile za mikopo kwa makundi maalumu.

“Tuko vizuri hasa katika makusanyo ya fedha na kuyakopesha makundi maalumu kama yale ya akina mama na vijana ambayo hadi sasa tumeyapatia mikopo yenye thamani ya zaidi ya TZS bilioni 60,” Bw Moshingi alisema wakati akieleza faida ambazo halmashauri zitapata kwa kufanya kazi na TCB.

Aidha, alibainisha kuwa benki hiyo pia ina sifa ya kuanzisha huduma mbalimbali nchini kama zile za benki wakala na benki mtandaoni ambazo zimekuwa na mchango mkubwa katika ajenda ya taifa ya ujumuishaji kifedha.

Nyingine kuybwa ni ile ya kuwakopesha wastaafu.


Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Tanzania Commercial Bank Tawi la Arusha-Meru
Selestine Mteta alipotembelea banda la benki hiyo wakati wa mkutano mkuu wa 37 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania - ALAT unaofanyika jijini Arusha. Benki ya TCB ilikuwa ni mmoja wa wadhamini wa mkutano huo.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive