Tanzania – 18 Juni 2025 – Akiba Commercial Bank Plc (ACB) iliandaa mkutano Maalum wa Wateja jijini Mbeya lililowakutanisha zaidi ya wateja 150 kutoka sekta mbalimbali, kwa lengo la kuimarisha mahusiano na kuwataarifu wateja kuhusu maendeleo ya Benki pamoja na fursa mbali mbali za kuwainua wateja kiuchumi.
Showing posts with label BUSINESS. Show all posts
Showing posts with label BUSINESS. Show all posts
Thursday, June 19, 2025
AKIBA COMMERCIAL BANK PLC YAANDAA JUKWAA LA WATEJA MKOANI MBEYA ZAIDI YA WATEJA 150 WASHIRIKI.
Jukwaa hili lililenga kutoa taarifa kuhusu maendeleo ya hivi karibuni ya benki, hususan katika huduma za kidijitali na maboresho ya uzoefu wa wateja. Aidha, lilitumika kama jukwaa la kutoa elimu ya kifedha kwa wateja ili kuwasaidia kufanya maamuzi sahihi ya kifedha. Wateja walishiriki kikamilifu kwa kutoa maoni, mrejesho na mapendekezo kuhusu huduma za benki.
Benki ilitumia fursa hiyo kusikiliza, kujifunza na pia kutoa shukrani kwa wateja wake kwa uaminifu na ushirikiano wao wa muda mrefu. Akizungumza katika tukio hilo, Bi. Wezi Mwazani, Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya Akiba, alitoa pongezi kwa mwitikio mkubwa na kusema: "Mwonekano wa ushiriki huu mkubwa unatupa faraja kuwa wateja wetu wanatuamini na wamechagua Akiba kama Benki yao pendwa. Hatuchukulii jambo hili kuwa la kawaida, na tunaendelea kujitolea kuwahudumia kwa ubora siku zote.
" Bw. Ntupa, Kiongozi wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Soko la Mbeya, alipongeza juhudi za Benki kwa kuandaa jukwaa lenye maana kubwa, hasa kwa kuweka kipaumbele kwenye elimu ya kifedha. "Majukwaa kama haya ni muhimu kwa maendeleo ya biashara, yanatoa maarifa kwa wateja wetu na kuimarisha uhusiano wa kuaminiana kati ya benki na jamii ya wafanyabiashara," alisema Bw. Mtupa. Akihitimisha tukio hilo,
Afisa Biashara Mkuu wa Akiba Commercial Bank Plc Bi. Wezi Mwazani akifungua mkutano wa wateja ulioandaliwa na benki hiyo mkoani mbeya.
Bw. Humphrey Nyandidi, Meneja wa Tawi la Mbeya, alishukuru wateja kwa ushirikiano wao na kuahidi kuendelea kuwahudumia kwa bidii na kujituma. "Tunathamini sana uaminifu wenu, na tunaahidi kuendelea kuwahudumia kwa ari na moyo wa dhati ili kutimiza matarajio yenu na hata kuvuka kiwango hicho," alisema. Jukwaa hili la wateja ni sehemu ya mkakati mpana wa Benki ya Akiba wa kuimarisha mahusiano na wateja wake kupitia majukwaa ya majadiliano na mirejesho kutoka kwa wateja. Benki inaendelea kujikita katika kutoa huduma shirikishi za kifedha pamoja na elimu ya fedha.
Friday, June 13, 2025
AKIBA COMMERCIAL PLC YASHIRIKIANA NA TIA KUPANDA MITI 1,500 KATIKA KAMPENI YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA

Dar es Salaam, 13 Juni 2025: Akiba Commercial Plc imeonyesha dhamira yake endelevu ya kutunza mazingira kupitia zoezi la kupanda miti kwa ushirikiano na Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) katika kampasi ya Kurasini, Dar es Salaam. Miti 1,500 imepandwa kama sehemu ya mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) unaolenga kukuza utunzaji wa mazingira na kuimarisha ustawi wa jamii. Zoezi hilo liliongoza na Afisa Biashara Mkuu wa Benki hiyo Bi. Wezi Mwazani (Picha ya kwanza) kwa kushirikiana na wafanya kazi wengine pamoja na wanafunzi wa TIA.
Akizungumza kwa niaba ya benki katika tukio hilo, Bwana Emmanuel Mseti, Meneja Mwandamizi wa Kitengo cha Wateja Binafsi, alitoa shukrani za dhati kwa uongozi, wafanyakazi na wanafunzi wa TIA kwa mapokezi na ushirikiano mzuri uliowezesha mafanikio ya shughuli hiyo ya kimazingira. Alibainisha kuwa zoezi hili si ishara tu bali ni kitendo kinachoonyesha imani ya Benki kwamba kulinda mazingira ni jukumu la pamoja.

“Shughuli hii ni mfano halisi wa imani yetu kuwa kulinda mazingira ni jukumu la kila mmoja wetu. Jukumu letu halikomi tu kwenye kupanda miti peke yake bali, tunaendelea kuhimiza huduma rafiki kwa mazingira kupitia huduma zetu za kidijitali kama ACB Mobile, Internet Banking na Akiba Wakala, ambazo si tu huongeza urahisi na ufanisi, bali pia hupunguza matumizi ya karatasi na kuunga mkono utunzaji wa mazingira,” alisema Bwana Mseti.

Benki pia ilibainisha juhudi zake nyingine za utunzaji wa mazingira ikiwemo jukumu endelevu la kutunza na kuboresha Viunga vya Independence Square jijini Dodoma. Katika tukio hilo, Bwana Mseti aliwahimiza wanafunzi wa TIA kuchukua jukumu la kulinda miti iliyopandwa na kuhakikisha inakua vizuri kwa faida ya vizazi vijavyo.
Pia aliwahakikishia kuwa Benki itaendelea kushirikiana na TIA katika kampeni za mazingira katika kampasi zake nyingine pindi itakapohitajika.
Kwa mtazamo wa Uwajibikaji kwa Jamii, Akiba Commercial inaamini kuwa kwao kurudisha kwa jamii si chaguo bali ni wajibu.
Kupitia sekta za afya, elimu, uwezeshaji wa kiuchumi, na utunzaji wa mazingira, Benki imejitolea katika maendeleo jumuishi na endelevu yanayonufaisha jamii inayoihudumia.
Ili kupata taarifa zaidi kuhusu ushiriki wetu katika maswala ya kijamii na huduma za kibenki kwa ujumla, tafadhali skani QR yetu hapa chini.

Thursday, June 12, 2025
Mkurugenzi wa Benki ya DCB, Sabasaba Moshingi aongoza wafanyakazi wa benki hiyo kujitolea damu wakiadhimisha Siku ya Wachangia damu Duniani

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Hospitali ya Aga Khan, Bw. Sisawo Konteh (Kulia) akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Bw.Sabasaba Moshingi, wakati yeye na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo walipofika hospitalini hapo kujitolea damu kuadhimisha Siku ya Wachangiaji Damu Duniani, jijini Dar es Salaam Leo.
BENKI ya Biashara ya DCB imesema itaendelea kufanya jitihada tofauti katika kusaidia afya za watanzania wenye uhitaji wa kupata damu kutokana na kukabiliwa na changamoto mbalimbali imeelezwa jijini Dar es Salaam leo.
Akizungumza katika zoezi la kujitolea damu kama sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wachangia Damu Duniani, jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Bw. Sabasaba Moshingi alisema yeye pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake wameamua kujitolea damu kwani licha ya benki yao kujishughulisha na utoaji wa huduma za kifedha lakini pia wanabeba jukumu la kuhakikisha watu wanaohitaji damu salama mahospitalini wanazipata bila kuwa na haja ya kusubiria ndugu waje kujitolea.
“Leo tupo hapa pamoja na washirika wenzetu hospitali ya Aga Khan kwa lengo la kuchangia damu, tutaendelea kushiriki matukio mengine kama haya na mengineyo yenye lengo la kusaidia kuokoa maisha ya watanzania wenzetu wenye uhitaji wa damu na mahitaji mengine ya kibidamu”, alisema Bw. Moshingi.
Akizungumza katika hafla hiyo Mkuu wa Kitengo cha Maabara katika Hosptali ya Aga Khan, Dk. Caroline Ngimba alitoa hamasa kwa watanzania wote nchini kuwa na moyo na utamaduni wa kujitolea damu bila kusubiri siku rasmi za kitaifa ama kimataifa bali liwe ni jambo endelevu kwani uhitaji wa damu upo kila siku mahospitalini.
“Uzuri ukichangia damu kama afya inaruhusu kila baada ya miezi mitatu unaweza kuchangia tena, tungeomba tabia hii iwe endelevu kwani hakuna kiwanda cha kutengeneza damu, damu inayopewa mwanadamu inatoka kwa mwanadamu”, alisema Dk. Caroline.
Naye mtaalamu wa utoaji damu kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama, Peter Chami alitoa shukurani kwa Benki ya DCB, huku akizitaka taasisi nyingine kuiga mfano wa benki hiyo ili kuokoa maisha ya watanzania wenye shida ya damu kwani mahitaji ya damu ni makubwa sana.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Bw.Sabasaba Moshingi, akifanyiwa uchunguzi wa afya yake kabla hajajitolea damu katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam leo, alipongoza baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo kujitolea damu, kuadhimisha Siku ya Wachangiaji Damu Duniani. Picha nyingine zikionesha matukio mbalimbali katika hafla hiyo.

Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya DCB, Bw. Deogratius Thadei, akijitolea damu katika hafla ya maadhimisho ya Siku ya Wachangiaji Damu Duniani, katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam leo, ambako yeye pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake walishiriki. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Maabara, Dk. Caroline Ngimba na kulia ni Mtaalamu wa mishipa Kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama, Bw. Peter Chami.


Baadhi ya wakurugenzi wa Benki ya DCB, waliojitolea damu pamoja na baadhi ya wafanyakazi wengine wa benki hiyo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wachangia damu Duniani katika Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam, leo.
.jpg)

Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya DCB, wakishiriki zoezi la uchangiaji damu Ili kusaidia wenye uhitaji ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wachangia damu Duniani, jijini Dar es Salaam leo.


Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya DCB, wakijitolea damu kusaidia wenye uhitaji ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wachangia damu Duniani, jijini Dar es Salaam leo.
Wednesday, June 11, 2025
AIRTEL TANZANIA YASHIKA NAFASI YA PILI KWA GAWIO LA BIL. 73.9. KWA SERIKALI
Dar es Salaam: Airtel Tanzania imeibuka nafasi ya pili katika mashirika yaliyotoa gawio kubwa kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwaka wa fedha 2024/25, na kuwasilisha hundi ya Shilingi bilioni 73.9 kwenye hafla ya siku ya Gawio iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Hafla hiyo iliandaliwa Ofisi ya Msajili wa Hazin na kuhudhuriwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Utoaji wa Gawio na Mchango huo sio tu inadhihirisha ufanisi na kukuaji kwa Airtel kibiashra bali unaonyesha jinsi Airtel ilivyojidhatiti kuendelea kuwa mdau muhimu wa maendeleo ya taifa kupitia ushirikiano wa kimkakati baina ya sekta ya umma na sekta binafsi.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan alitoa shukrani kwa mashirika ya sekta binafsi kwa kuchangia kiasi cha trilioni 1.28 kwa mwaka huu. Pia alisisitiza kuwa Serikali inaendelea kuweka mazingira bora ili kuendelea kuchochea uwekezaji na kuongeza kasi ya ukuaji kiuchumi.
Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu hassan ameeleza kuwa siku ya hiyo inadhihirisha muelekeo wa serikali katika uendeshaji wa mashirika ya umma huku akiyataka yaweze kuzalisha na kujiendesha yenyewe.
“Nawapongeza wote ambao mmeweza kuchangia. Siku hii inatoa fursa kwa wananchi kuona namna mashirika mbalimbali yanawajibika kwao. Niyatake mashirika na taasisi kuongeza ubunifu kwa lengo la kuongeza ufanisi katika utendaji na kutatua changamoto zinazowakabili,” alisema Dkt Samia.
Pia Mheshimiwa Rais Dkt. Samia alitoa rai kwa mashirika ambayo yanamilikiwa na serikali kwa hisa yahakikishe yanatumia kikamilifu mifumo ya TEHAMA ili kuongeza ufanisi na tija na uwazi katika utendaji.
Tangu mwaka 2019, Airtel Tanzania Plc pamoja na Airtel Money Tanzania Ltd zimechangia jumla ya zaidi ya shilingi bilioni 280 kwa serikali. Kupitia umiliki wa serikali kwa asilimia 49, kampuni hii imebaki kuwa mfano wa namna ushirikiano na sekta binafsi unaweza kuleta manufaa ya muda mrefu.
Akizungumza baada ya makabidhiano hayo, Mwenyekiti wa Bodi ya Airtel Tanzania, Eliudi Sanga, alibainisha kuwa kujituma kwa Airtel kuna mchango mkubwa katika kuchochea mabadiliko ya kiuchumi na kijamii.
“Airtel Tanzania inajivunia kuwa mshirika wa kuaminika katika safari ya maendeleo ya taifa. Uwekezaji wetu unaendana na vipaumbele vya kitaifa vya Serikali kwa kupanua miundombinu ya kidijitali kwa kuchangia upatikanaji uliojumuishi na wezeshi wa uchumi wa kidijitali,” alisema Sanga.
Kwa upande wake, Charles Kamoto, Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, alisisitiza juu ya malengo ya kampuni kuwezesha ukuaji jumuishi na uwezeshwaji wa kidijitali.
“Mchango wa gawio letu ni kielelezo cha msimamo wetu katika kuchagiza kwenye maendeleo endelevu ya Tanzania. Hii inaakisi namna sera ya serikali inavyoendana na ubunifu wa sekta binafsi katika kuleta maendeleo jumuishi na kuelekea katika uchumi wa kidigitali,” alisema Kamoto.
Kamoto alihitimisha kwa kusema kuwa Airtel inajivunia kuiunga mkono serikali kupitia uwekezaji wake kupitia upanuzi wa mtandao, unafuu wa vifaa vya mawasiliano na majukwaa ya kidijitali nchini Tanzania.
Tuesday, June 10, 2025
TOP TANZANIAN BRANDS RECEIVE GLOBAL RECOGNITION FOLLOWING CONSUMER SURVEY
Superbrands East Africa CEO, Jawad Jaffer speaking to journalists and guests attending the event.
Superbrands East Africa CEO Jawad Jaffer (R) pictured in Dar es Salaam yesterday presenting to The Guardian Limited deputy general manager Jackson Paulo a Superbrands Award for 2024-2025 won by The Guardian newspaper.
Dar es Salaam, June 9th, 2025: Superbrands, the world’s largest independent arbiter of branding, hosted an intimate yet impactful event on 9th June in Dar es Salaam, celebrating 13 leading Tanzanian brands that have earned the prestigious Superbrands status for 2025. Attended by key members of the press and Directors from the honored brands, the event marked a milestone in Tanzania’s branding landscape.
Each awarded brand underwent a rigorous selection process involving consumer voting by Tanzanians from all over the country. Superbrands recognition is awarded only to those that demonstrate exceptional scores in brand quality, reliability, and distinction. These parameters are used by Superbrands globally.
Superbrands partnered with IPSOS Tanzania for this research, an international research firm they have partnered with in several other regions. Participants for this research were scientifically sampled to ensure a representative mix of age, gender, location, and socio-economic status, with a specific focus on the urban population. Just over 1100 brands across 67 distinct categories were shortlisted.
IPSOS Regional Director of Behavior Change and Growth - PA, the company that conducted the research, Doreen Bangapi, she said the goal of recognizing these institutions is to increase the efficiency of fulfilling their responsibilities and to have their value recognized in the country.
“Today we are here to name the top 10 Institutions that have been granted Super Brand status due to their performance during the year 2024-25,” said Doreen.
The following Tanzanian brands Abood Bus, ASAS, Azam, GSM, Kilimanjaro Water, NIC, Petrogroup, Red Gold, Super Doll, Tanfoam Tanzania, The Guardian, ITV and Whitedent have been awarded Superbrands Status for the year 2024 to 2025.
"What's different this year is that Tanzanian Premier League football clubs were included in the process, with Simba Club taking first place among football teams in Tanzania and second among all institutions, while Yanga team took second place among football clubs and third among all institutions in the country, with Colgate taking first place." Said Doreen.
Earlier, Superbrand East Africa CEO, Jawad Jaffer, said that for the Institute to have a chance to be included and become a Superbrand, it is necessary to ensure that it meets the criteria of quality, reliable and differentiated products above all.
"If you can ensure that your product has sustainable quality, is appreciated by consumers and is distinctive in the market, we as Superbrand will certainly invite you to participate in the process of becoming a Superbrand in the country and even worldwide," said Jawad.
The survey is conducted annually by various institutions in the country with the aim of encouraging effective work to bring about positive results, by interviewing users of the companies' products at the family and individual levels, where online users are also involved in finding winners.
As more brands are identified to have scored exceptionally well in the consumer research, Superbrands will be continuing to recognize more top Tanzanian brands as the strongest in the region.





Superbrands East Africa CEO, Jawad Jaffer handling over Superbrands Awards to some institutions who won and attending the event.
For more information please contact:
Abdi Juma
Superbrands East Africa
Who is Superbrands?
Superbrands is the world's largest independent arbiter of branding, and has been in operation since 1994 globally, and has been present in East Africa since 2007. It is headquartered in London, UK.
Superbrands currently identifies and pays tribute to exceptional brands in 90 countries globally, through it’s publications and granting use of the “Superbrands Status” to qualifying brands.
The Superbrands Seal and Status are recognized as a symbol of quality, reliability, distinction and excellence.
Who is IPSOS?
IPSOS is a multinational market research and consulting firm headquartered in Paris, France. They are considered a global leader in their field, working with both nationals and multinational brands to provide precise and insightful research.
Benki ya Absa Tanzania Yathibitisha Uwazi na Dhamira ya Ukuaji Katika Mkutano na Gavana wa BoT

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba (katikati), akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa tatu kutoka kushoto), wakati wa ziara yao katika ofisi ya gavana jijini Dar es Salaam jana. Ujumbe huo ulifanya mazungumzo ya kina na gavana, ukimpa taarifa kuhusu masuala muhimu yakiwemo utendaji wa kifedha wa benki hiyo, sera za faragha na ulinzi wa taarifa, mipango ya ukuaji na upanuzi, maendeleo ya udhibiti, na maeneo mengine muhimu ya kipaumbele kama Utawala wa Mazingira, Jamii na Uongozi (ESG) pamoja na huduma za kijamii, ikionesha dhamira thabiti ya taasisi hiyo ya kifedha kwa uwazi, ulinganifu wa udhibiti na ukuaji endelevu. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria na Udhibiti wa Benki ya Absa, Bw. Alistides Kashasira na Afisa Mkuu wa Uendeshaji, Bw. Oscar Mwamfwagasi. Kulia ni baadhi ya maafisa kutoka Benki Kuu.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa tatu kutoka kushoto), akizungumza na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba (kulia), wakimtembelea gavana ofisi kwake, jijini Dar es Salaam jana. Ujumbe huo ulifanya mazungumzo ya kina na gavana, ukimjulisha kuhusu masuala muhimu yakiwemo utendaji wa kifedha wa benki hiyo, sera za faragha na ulinzi wa taarifa, mipango ya ukuaji na upanuzi, maendeleo ya udhibiti, na maeneo mengine muhimu ya kipaumbele kama Utawala wa Mazingira, Jamii na Uongozi (ESG) pamoja na huduma za kijamii, yakionesha dhamira ya benki hiyo katika uwazi, kuzingatia kanuni na ukuaji endelevu. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria na Udhibiti wa Absa, Bw. Alistides Kashasira na Afisa Mkuu wa Uendeshaji, Bw. Oscar Mwamfwagasi.

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba (kulia), akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), pamoja na ujumbe wake, mara baada ya kikao kilichofanyika katika ofisi ya gavana jijini Dar es Salaam jana. Ujumbe huo ulifanya mazungumzo ya kina na gavana, ukimpa taarifa juu ya masuala muhimu yakiwemo utendaji wa kifedha wa benki, sera za faragha na ulinzi wa taarifa, mipango ya ukuaji na upanuzi, maendeleo ya udhibiti, pamoja na maeneo mengine muhimu kama Utawala wa Mazingira, Jamii na Uongozi (ESG) na huduma za kijamii, yakionesha dhamira thabiti ya benki hiyo kwa uwazi, ulinganifu wa udhibiti na maendeleo endelevu.

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba (wa nne kutoka kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa tatu kutoka kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya maafisa waandamizi kutoka Benki ya Absa na Benki Kuu jijini Dar es Salaam jana, wakati wa ziara ya ujumbe wa Absa katika ofisi ya gavana. Kupitia mazungumzo ya wazi na ushirikiano na benki kuu, Benki ya Absa inaendelea kulinganisha malengo yake na vipaumbele vya kitaifa na kuchangia kikamilifu katika mustakabali wa kifedha wa nchi.
SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA LATEKELEZA MABADILIKO MAKUBWA, LATOA GAWIO LA TZS BILIONI 5.5 KWA SERIKALI
Dar es Salaam, Juni 10, 2025: Katika hafla ya kihistoria iliyofanyika leo katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limepata heshima ya kutajwa miongoni mwa taasisi tatu bora zilizofanya maboresho ya haraka na ya kuigwa katika utoaji wa gawio kwa Serikali. Hii ni baada ya Shirika hilo kuongeza gawio lake kutoka Shilingi Bilioni 1 mwaka uliopita hadi kufikia Shilingi Bilioni 5.5 kwa mwaka huu wa fedha.
Akizungumza katika hafla hiyo, Msajili wa Hazina, Ndg. Nehemia Kyando Mchechu, alilitaja Shirika la Nyumba la Taifa kama mfano bora wa taasisi zilizopokea kwa vitendo maelekezo ya Mheshimiwa Rais ya kuongeza tija, ufanisi na uzalishaji wa mapato kwa taasisi za umma.
“Kundi la tatu ni la mashirika yaliyoongeza mchango wake kwa kasi zaidi… la kwanza katika kundi hili ni Shirika la Nyumba la Taifa, ambao wametoka katika kiwango cha shilingi bilioni 1 hadi bilioni 5.5. Wameonesha mabadiliko makubwa na ya kuigwa,” alisema Mchechu.
Tuzo ya mfano wa hundi ya gawio hilo ilikabidhiwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kuwasilishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NHC, Dkt. Sophia Kongela, pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Ndg. Hamad Abdallah.
Shirika la Nyumba la Taifa limekuwa mstari wa mbele katika kutekeleza majukumu yake ya msingi kwa ufanisi mkubwa, likijikita katika ujenzi wa miradi ya kimkakati inayochochea uchumi wa taifa, kuongeza ajira, na kuhakikisha Watanzania wanapata makazi bora na ya bei nafuu.
Hafla hiyo ya upokeaji wa gawio na michango kutoka kwa taasisi na mashirika ya umma, ambayo mwaka huu yalifikia takriban 256, imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, wakiwemo Mawaziri, Wakuu wa Taasisi, Wenyeviti wa Bodi pamoja na Wakurugenzi Wakuu.
Katika salamu zake, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliwapongeza viongozi na taasisi zote zilizowasilisha gawio, akisisitiza kuwa fedha hizo zitachangia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na huduma za kijamii kwa wananchi.
NHC inaendelea kuonesha dhamira ya dhati ya kujitegemea kifedha huku ikitekeleza majukumu yake kwa weledi, uwazi na ufanisi. Mabadiliko haya makubwa ni ishara ya uongozi makini, mipango madhubuti, na matumizi bora ya rasilimali za umma kwa manufaa ya taifa.
Sunday, May 25, 2025
Akiba Commercial Bank Yakutana na Wateja wa Mwanza: Zaidi yaWateja 250 Wahudhuria Mkutano wa Mahusiano
Mkurugenzi Mtendaji wa Akiba Commercial Bank Plc, Bw. Silvest Arumasi (katikati), akizungumza na wateja wa Benki hiyo mkoa wa Mwanza wakati wa hafla ya kukuza na kuimarisha mahusiano na wateja hao pamoja na kupokea mrejesho kwa ajili ya kufanya maboresho ya bidhaa pamoja na viwango vya huduma. wengine pichani kutoka kushoto ni Afisa Biashara Mkuu wa ACB, Bi. Wezi Mwazani pamoja na mwakilishi wa wafanya Biashara wa soko kuu la Mwanza.
Meneja wa Akiba Commercial Bank Tawi la Mwanza Bw.Emmanuel Makula akitambulisha timu yake ya ushindi ya Tawi hilo Wakati wa hafla ya kukuza na kuimarisha mahusiano na wateja wa benki hiyo mkoa wa mwanza.
Benki ya Akiba imeendelea kuonyesha dhamira yake ya kuwa karibu na wateja kwa kuandaa mkutano maalum na wateja wa Mwanza uliofanyika tarehe 22 Mei 2025 katika ukumbi wa Gold Crest Hotel.
Tukio hili lilivutia zaidi ya wateja 250, ikiwa ni ishara ya hamasa kubwa na utayari wa jamii ya Kanda ya Ziwa kunufaika na huduma Benki hiyo.
Katika mkutano huo wa ana kwa ana, wateja walipata nafasi ya kuzungumza moja kwa moja na viongozi waandamizi wa benki, kutoa maoni yao kuhusu huduma, kueleza changamoto wanazokutana nazo katika shughuli za kifedha, pamoja na kujifunza kuhusu huduma na bidhaa mpya za benki.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Akiba, Bw. Silvest Arumasi, alipata nafasi ya kuzungumza na wateja na kueleza kuwa mkutano huu ni sehemu ya mikakati ya Benki katika kuimarisha mawasiliano na wateja wake. Alisema:
“Benki ya Akiba inaamini katika kusikiliza wateja wake. Lengo letu ni kuelewa vizuri zaidi mahitaji yao halisi ili tuweze kutoa huduma zinazogusa maisha yao kwa namna chanya, hasa katika mazingira yao ya kila siku.”
Bw. Arumasi aliongeza kuwa benki inaendelea kuweka mkazo katika kutoa msaada kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati kwa kuwapa jukwaa la kuzungumza moja kwa moja na wataalamu wa kifedha na kupata ushauri wa kibiashara wenye manufaa ya moja kwa moja.
Afisa Mkuu wa Biashara, Bi. Wezi Mwanzani, alieleza kuwa mwitikio mkubwa wa wateja wa Mwanza ni ushahidi wa Imani ya Wakazi wa Mwanza kwa Benki ya Akiba pamoja na uhitaji mahitaji mkubwa wa huduma za kifedha. Alisema
“Tunashukuru kwa mwitikio mzuri kutoka kwa wateja wa Mwanza. Kama benki, tutaendelea kutoa huduma bunifu na zinazolenga kumsaidia mteja katika uhalisia wa biashara zake. Mwanza ni sehemu muhimu ya mpango wetu wa kuhakikisha huduma zetu zinawafikia watu wote.”
Bi. Wezi alisisitiza kuwa dhamira ya benki ni kuijenga jamii jumuishi kifedha, kwa kuhakikisha watu wote wanapata nafasi sawa ya kutumia huduma za kifedha kama njia ya kujikwamua kiuchumi.
Mbali na majadiliano, tukio hili pia liliambatana na utoaji wa elimu ya kifedha. Wateja walielimishwa kuhusu usimamizi wa fedha binafsi na za biashara, matumizi salama ya huduma za kidijitali kama benki mtandao na miamala kwa njia ya simu, pamoja na mbinu bora za kukuza biashara kwa njia endelevu.
Sunday, April 13, 2025
AKIBA COMMERCIAL BANK PLC YATOA ELIMU YA KIFEDHA KWA WATEJA WAKE KARIAKOO
Mkurugenzi Mtendaji wa Akiba Commercial Bank Plc, Silvest Arumasi (kushoto), akiwa Kwenye kikao na wateja na wajasiriamali (SMEs) kutoka Kariakoo, katikati ya kitovu cha biashara Afrika Mashariki, ili kujadili changamoto zao na kushirikiana mawazo kuhusu masuluhisho yanayoweza kukuza biashara zao hafla hiyo imefanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya hiyo Bi Wesi Olivia.
Mkurugenzi Mtendaji wa Akiba Commercial Bank Plc, Silvest Arumasi (katikati), akiwabkatika picha ya pamoja wateja na wajasiriamali (SMEs) kutoka Kariakoo, katikati ya kitovu cha biashara Afrika Mashariki, ili kujadili changamoto zao na kushirikiana mawazo kuhusu masuluhisho yanayoweza kukuza biashara zao
Mnamo tarehe 12/04/2025 Benki ya Akiba ilifanya kikao na wateja wake na wajasiriamali (SMEs) kutoka Kariakoo, katikati ya kitovu cha biashara Afrika Mashariki, ili kujadili changamoto zao na kushirikiana mawazo kuhusu masuluhisho yanayoweza kukuza biashara zao. Hii ni sehemu ya juhudi zetu za kuwa karibu na wateja na kutekeleza dhamira yetu ya kuwawezesha wajasiriamali na kuimarisha elimu ya fedha, alisema Bi. Dora Saria Mkuu wa Kitengo cha masoko na Mawasiliano wa Benki hiyo.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Bwana Silvest Arumasi, alielezea furaha yake kwa kushirikiana moja kwa moja na wateja, akisema, "katika Benki yetu , tunaamini kwamba mafanikio ya wateja wetu ni mafanikio yetu. Tunajivunia sana kushirikiana na wajasiriamali wote nchini katika kusaidia kukuza biashara zao kupitia elimu ya fedha, mikopo, na huduma za kidijitali."
Akizungumza katika tukio hilo, Bi. Wezi Olivia Mwazani, Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya Akiba, alisisitiza umuhimu wa kujenga uhusiano ya kudumu na wateja kwa kutoa huduma za kifedha zinazolingana na mahitaji yao.
"Tunafurahi kuwa na fursa ya kuzungumza na wateja wetu moja kwa moja, kuelewa changamoto zao na kutoa masuluhisho ya kifedha ambayo yatasaidia katika mafanikio yao ya muda mrefu."
Wateja waliokuwepo waliotoa shukrani zao kwa juhudi hizo, wakielezea jinsi fursa ya kushirikiana na Benki hiyo ilivyo muhimu kwa ukuaji wa biashara zao. Wengi walielezea kuwa mpango huu wa elimu ya fedha na huduma za kidijitali utawawezesha kufanya biashara zao kwa ufanisi zaidi.
Bw. Silvest Arumasi, Mkurugenzi Mtendaji wa ACB aliwashukuru wateja kwa uaminifu wao na ushirikiano wa muda mrefu, akiongeza, "Tunapenda kuwashukuru wateja wetu wa Kariakoo na maeneo mengine kwa ushirikiano wao ikiwa ni pamoja na kutuchagua na kutuamini. Pamoja, tutaendelea kuleta mabadiliko katika sekta ya SMEs na kusaidia katika maendeleo endelevu ya kiuchumi."
Benki ya Akiba inaendelea kutoa huduma za kibenki zinazolenga mahitaji ya wateja na kusaidia ukuaji wa biashara za watu binafsi, SMEs pamoja na makampuni makubwa na taasisi mbalimbali kupitia huduma zinazokidhi mahitaji yao na matumizi ya teknolojia ya kidijitali.
Friday, April 11, 2025
WADAU ZAIDI YA 500 KUSHIRIKI WIKI YA AZAKI 2025 MWEZI JULAI ARUSHA


Kuelekea katika wiki hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa FCS Justice Rutenge amewahimiza wananchi kupaza sauti zao kwa kutoa maoni yatakayopelekea kupata dira bora kwa maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.
Rutenge amesema hayo Dar es Saalam wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Asasi za Kiraia (AZAKI) 2025, ambapo zaidi ya washiriki 500 wanatarajiwa kushiriki na kutoa wito kwa watanzania kushiriki kwa wingi.
“Wiki ya Azaki imefanyika kwa miaka sita mfululizo na sasa ni mwaka wa Saba lengo likiwa kuwaleta pamoja wadau wa sekta ya Azaki kufanya mijadala mbalimbali ya maendeleo kwa mustakabali wa nchi yetu Tanzania,"
“Kila mwaka tuna utaratibu wa kuangazia mambo mbalimbali na kuweka sawa Mahudhui ya wiki ya Azaki na mwaka huu tutaangazia mchakato mzima wa dira ya Taifa."
“Watanzania wengi wanatambua kuwa mwaka huu tumeshiriki kwa kina kwenye mchakato wa kutengeneza dira yetu ya maendeleo ya mwaka 2050 ambayo ni fursa inayokujaga mara chache mara moja kwa miongo miwili au miwili na nusu."

Kwa upande wake Mkurugenzi mkazi, CBM International ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati za Asasi za Kiraia Nesia Mahenge amesema wiki hiyo inalenga kutatua changamoto ambazo zipo katika azaki za kiraia na kuona ni namna gani zinatatuliwa.
“Azaki kutoka nchi za Tanzania bara, Zanzibar wanaangalia ni namna gani kila mwaka ndani ya wiki moja tunakutana na kutathimini kazi za mashirika yasio ya kiserikali kuangalia maendeleo ambayo tumeyaleta katika nchi yetu."
“Kwa mwaka huu itakuwa tofauti tulizoea kufanya mwezi wa kumi mkoani Dodoma lakini kwa sasa ni Arusha kutokana na mapendekezo ya jamii hatutafanya mkoa mmoja."
“Tujumuike kuangalia jinsi ya kupanga mikakati na kutenga fedha za kuleta maendeleo kwenye jamii na pia mataifa mengine kuangalia maendeleo yetu na kuyapeleka kwenye nchi zao."


Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkurugenzi Mkaazi wa Trademark Africa Elibariki Shami, amesema kuwa FCS imeonesha jitihada kubwa katika kuimarisha utetezi wa AZAKi kwa kuhakikisha haki za walaji zinapatikana na kuongeza uelewa katika ulinzi wa watumiaji.
“FCS inalenga kuhakikisha kuwa ifikapo 2026, AZAKi zinashiriki kikamilifu katika mipango ya ulinzi wa watumiaji na kuwepo kwa ongezeko la uelewa wa jamii juu ya ulinzi wa walaji” amesema.
Ameongeza kuwa kushiriki wa moja kwa moja wa FCS katika kushughulikia masuala ya kijamii, sambamba na utaalamu wa utetezi na kujitolea, unawakilisha maslahi ya raia na walaji, nakwamba AZAKi huziba pengo kati ya sera na hatua za msingi za kuhakikisha ulinzi thabiti wa walaji unakuwepo.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Association NGoS Adamsoni Nsimba amesema wamefurahi kujumuika katika uzinduzi wa wiki za Azaki itakayomsaidia na kumlinda mlaji na kujenga uwezo kwa jamii na kumpa mlaji haki tofauti na mfanya biashara kuchagiza sera na sheria.


Friday, March 28, 2025
AKIBA COMMERCIAL BANK YAWAKUMBUKA WATOTO WENYE UHITAJI DAR ES SALAAM.
Akiba Commercial Bank Plc Yapeleka Tabasamu Kituo cha Kulea Watoto- Chakuwama Sinza Dar es Salaam, 28/03/2025 – Katika kuendelea kujitoa kwa jamii, Akiba Commercial Bank Plc imetoa msaada kituo cha kulea Watoto cha Chakuwama, ikilenga kuboresha ustawi wa watoto na kuleta tabasamu kwenye nyuso zao.
Msaada huu, ambao unajumuisha mahitaji muhimu, unaonesha dhamira ya Benki hiyo ya kusaidia wenye uhitaji na kujenga matumaini kwa mustakabali mwema.
Akizungumza wakati wa makabidhiano, Bi. Dora Saria, Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Akiba Commercial Bank, alieleza kuwa Benki hiyo inaamini katika kuunga mkono jamii na kuleta mabadiliko chanya ya kudumu.
"Akiba Commercial Bank, tunaamini katika nguvu ya mshikamano katika kubadili maisha. Msaada huu ni hatua muhimu ya kuhakikisha ustawi wa watoto hawa na kuleta matumaini kwa wenye uhitaji kwa maisha bora yajayo," alisema Bi. Saria.
Kwa upande wake, Bw. Hassan Tabu, mwakilishi wa Kituo cha Chakuwama, aliishukuru Akiba Commercial Bank kwa ukarimu wake, akibainisha kuwa msaada huo utakuwa na mchango mkubwa katika kuboresha maisha ya watoto hao.
"Tunaishukuru sana Akiba Commercial Bank kwa kusimama nasi. Msaada huu utasaidia kwa kiasi kikubwa kukidhi mahitaji ya watoto na kuwapatia sababu ya kutabasamu," alisema.
Kupitia juhudi hizi, Akiba Commercial Bank Plc inathibitisha tena dhamira yake ya kuwajibika kwa jamii kwa vitendo, ikilenga kuleta mabadiliko chanya na ya kudumu kwa jamii inayoihudumia.
Friday, March 21, 2025
Taasisi za Ulinzi wa Mlaji zimetakiwa kushirikiana na FCC
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Suleimani Jafo, amezitaka taasisi zote za serikali zinazohusika na ulinzi wa mlaji kufanya kazi kwa pamoja ili kuhakikisha haki za watumiaji zinalindwa.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam katika maadhimisho ya Siku ya Haki za Watumiaji Duniani, Dkt. Jafo amesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya mamlaka mbalimbali za udhibiti ili kuhakikisha bidhaa na huduma zinazopatikana zinakidhi viwango vya ubora na zinauzwa kwa bei nafuu.
Dkt. Jafo amezihimiza taasisi kama Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Shirika la Vipimo (WMA), Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na taasisi nyingine muhimu kushirikiana kwa karibu ili kuimarisha ulinzi wa walaji.
“Haki za watumiaji ni nguzo muhimu kwa ustawi wa uchumi wetu. Serikali ina jukumu la kuhakikisha kuwa watumiaji wanalindwa dhidi ya unyonyaji, hasa katika mazingira ya mabadiliko ya soko la kimataifa,” alisema Dkt. Jafo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), William Erio, amesema kuwa FCC inaendelea kuchukua hatua madhubuti kulinda maslahi ya watumiaji na kuimarisha ushindani wa haki katika soko.
“Tunajivunia juhudi za kimataifa zinazolenga kulinda haki za walaji, na hapa Tanzania, tunahakikisha soko letu linakuwa la haki, uwazi na lenye ushindani wa kweli,” alisema Erio.
Aidha, alibainisha kuwa FCC imepata cheti cha Shirika la Uthibitisho la Kimataifa (ICO), hatua inayothibitisha jitihada za tume hiyo katika kupata utambuzi wa kimataifa na kujenga imani katika soko la Tanzania.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI), Leodegar Tenga, amepongeza FCC kwa juhudi zake katika kuimarisha ushindani mzuri kwenye sekta ya viwanda.
“Ni muhimu kwa viwanda vyetu kuendelea kuboresha bidhaa na huduma zao ili kukidhi matarajio ya watumiaji. Ushindani wa haki unaleta mazingira mazuri kwa biashara kukua huku tukihakikisha haki za watumiaji zinalindwa,” alisema Tenga.
Maadhimisho haya ya Siku ya Haki za Watumiaji Duniani yamekuwa jukwaa muhimu la kutathmini maendeleo yaliyofikiwa katika kulinda walaji na kutoa wito wa ushirikiano madhubuti kati ya serikali, wadau wa sekta binafsi na mashirika ya watumiaji ili kuimarisha mazingira ya soko la Tanzania.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Suleimani Jafo, akizugumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Haki za Watumiaji Duniani.
Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani FCC Dkt. Aggrey Kalimwage Mlimuka.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), William Erio
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Suleimani Jafo,akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (F. CC), William Erio.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI), Leodegar Tenga.