A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Showing posts with label BUSINESS. Show all posts
Showing posts with label BUSINESS. Show all posts

Sunday, February 8, 2026

Portwest Deepens East African Footprint with Apparel Manufacturing Investment in TanzaniaDar es Salaam, Tanzania

The Deputy Minister for Industry and Trade, Hon. Denis Londo (center), cuts the ribbon to mark the official opening of Afriport’s occupational safety garments manufacturing factory located in Ubungo, Dar es Salaam. Second from the right is the company’s Chief Executive Officer, Mr. Henry Huge, together with other company officials and government representatives.
Portwest, the world’s fastest-growing manufacturer and distributor of workwear, safety wear and personal protective equipment (PPE), has strengthened its presence in East Africa with the operationalization of a new apparel manufacturing facility in Dar es Salaam, Tanzania—positioning the country as a strategic hub within the company’s global supply chain.

The investment has received strong support from the Government of Tanzania, which reiterated its commitment to creating a conducive environment for local and foreign investors.

Speaking during the official visit to the facility, Assistant Minister for Industry and Trade, Hon. Denis Londo, said the Government will continue to implement investor-friendly policies and legal frameworks to attract industrial investments.

The Government of the United Republic of Tanzania, through the Ministry of Industry and Trade, will continue to put in place enabling policies, laws and regulations to attract investors and support the establishment of industries in the country,” said Hon. Londo.

Investments such as this apparel manufacturing facility demonstrate growing confidence in Tanzania’s industrial environment and our commitment to building a strong manufacturing base that creates jobs and adds value locally.

Founded in 1904 in Ireland and still owned and managed by the Hughes family, Portwest operates in more than 150 countries and employs over 5,500 people globally. The company is internationally recognised for innovation in occupational safety solutions, producing flame-resistant and high-visibility clothing, safety footwear, PPE accessories and fall-protection equipment.

The Dar es Salaam facility is currently employing 200 workers, with existing infrastructure capable of scaling up to 1,000 direct jobs. The investment is expected to contribute significantly to skills development, technology transfer and value addition, in line with Tanzania’s industrialisation agenda and the objectives of the East African Community (EAC).

Meanwhile, Human Resources Manager of the facility, Ms. Anna Lucas, revealed that the company has invested more than USD 8.8 million in the project.

This investment reflects our long-term commitment to Tanzania. Beyond production, we are creating sustainable employment opportunities for Tanzanian youth and contributing to skills development within the local workforce,” she said.

Some employees also noted that the factory has played a vital role in addressing youth unemployment by providing stable jobs and professional training opportunities.
Share:

Wednesday, February 4, 2026

BENKI YA ABSA TANZANIA YAKABIDHI ZAWADI YA FEDHA TZS MILIONI 48, IKIHITIMISHA KAMPENI YA “UJANJA NI KUSWIPE NA KADI YA ABSA”

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akikabidhi mfano wa hundi ya shs 30,000,000 kwa mshindi wa droo kubwa ya kampeni ya ‘Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa’ Bi.Nasreen Karim Abdallah (wa pili kushoto), katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Katika kampeni hiyo ya miezi mitatu iliyokuwa na lengo la kuhamasisha wateja wa benki hiyo na watanzania kutumia huduma za kibenki kwa njia za kidigitali, zawadi zenye jumla ya shs 120,000,000 zilitolewa. Kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Swere na kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga.

Benki ya Absa Tanzania imekabidhi zawadi kwa washindi wa kampeni yake ya “Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa”, ikihitimisha kampeni yake ya miezi mitatu iliyokuwa na lengo la kuhamasisha wateja na watanzania kutumia huduma za kibenki kwa njia za kidigitali katika kufanya miamala mbalimbali ya kifedha.

Katika hafla hiyo, mteja wa benki hiyo, Bi. Nasreen Karim Abdallah alikabidhiwa mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 30, baada ya kuibuka mshindi wa droo kubwa iliyofanyika januari 21 mwaka huu, huku washindi wengine wa kila mwezi akiwemo Bw. Abdulrazak Ali Seif aliyepata TZS milioni 10, Bi. Aysha Mbarak Meghji aliyepata TZS milioni 5, na Bw. Gibbons Samuel Katule aliyepata TZS milioni 3 na wote kwa pamoja wakithibisha fedha hizo kuingizwa katika akaunti zao.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser alisema, kampeni hiyo ililenga katika kuwazawadia wateja wao kwa kuendelea kutumia huduma za kibenki zilizo salama, rahisi na za kisasa; “Zaidi ya zawadi, tunajivunia mabadiliko chanya tuliyoyaona kuelekea matumizi ya miamala isiyo ya fedha taslimu, ambayo huokoa muda, hupunguza hatari na kuchangia ujumuishi wa kifedha, hafla ya leo inaashiria mafanikio ya kampeni ambayo yamebadilisha maisha ya watu wengi.

Dhamira yetu iko wazi, Kuiwezesha Afrika ya kesho, pamoja, hatua moja baada ya nyingine. Kila kampeni, kila ubunifu na kila zawadi tunayotoa inaongozwa na imani yetu kwamba Stori yako ina thamani”, alisema Bw. Laiser.

Kampeni hiyo ilionesha ongezeko kubwa la matumizi ya kadi na huduma za kidijitali, ikithibitisha mwelekeo unaokua wa wateja kupendelea huduma za kibenki zinazopatikana muda wowote na mahali popote, huku zikisaidia kupunguza foleni ndefu katika matawi na kuongeza kasi, usalama na urahisi wa huduma.

Akizungumzia mafanikio ya kampeni hiyo, Bi. Ndabu Swere alisema; Kampeni ya “Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa” inaonesha jinsi miamala midogo ya kila siku inavyoweza kuwa na nguvu kubwa. Wateja waliitikia vyema, wakidumu katika kufanya miamala kwa njia za kidijitali, na kwa upande wetu tuliweza kuwazawadia uaminifu wao kwa njia yenye maana.

Kwa upande wake, mshindi wa zawadi kubwa, Bi. Nasreen Karim Abdallah, aliishukuru Benki ya Absa kwa zawadi hiyo, akisema ushindi huo ni hatua muhimu katika maisha yake. Alibainisha pia urahisi wa kushiriki kampeni hiyo kwa kutumia tu kadi katika miamala ya kila siku.

Kilichonivutia zaidi ni urahisi wa kushiriki, ni kutumia tu kadi yangu kwenye matumizi ya kawaida. Zawadi hii haithibitishi tu umuhimu wa huduma za kidijitali katika maisha yetu ya kila siku, bali pia ni ya kubadilisha maisha,” alisema.

Benki ya Absa Tanzania imethibitisha dhamira yake ya kuendelea kubuni bidhaa na kampeni zinazowaletea wateja thamani zaidi, ikikumbusha kuwa mwaka 2024 benki hiyo ilitoa zawadi ya magari matatu na mwaka 2025 imetoa TZS milioni 120 kama zawadi za fedha taslimu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akizungumza katika hafla ambayo benki hiyo ilikabidhi mfano wa hundi ya shs 30,000,000 kwa mshindi wa droo kubwa ya kampeni ya ‘Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa’ Bi.Nasreen Karim Abdallah (kushoto), jijini Dar es Salaam jana. Katika kampeni ya miezi mitatu iliyokuwa na lengo la kuhamasisha wateja wa benki hiyo na watanzania kutumia huduma za kibenki kwa njia za kidigitali, zawadi zenye jumla ya shs 120,000,000 zilitolewa. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Swere na kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akikabidhi mfano wa hundi ya shs 3,000,000 kwa mmoja wa washindi wa droo ya kila mwezi ya kampeni ya ‘Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa’ Bw. Gibbons Samuel Katule (wa pili kushoto), katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Katika kampeni hiyo ya miezi mitatu iliyokuwa na lengo la kuhamasisha wateja wa benki hiyo na watanzania kutumia huduma za kibenki kwa njia za kidigitali, zawadi zenye jumla ya shs 120,000,000 zilitolewa. Kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Swere na kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akikabidhi mfano wa hundi ya shs 3,000,000 kwa mmoja wa washindi wa droo ya kila mwezi ya kampeni ya ‘Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa’ Bw. Gibbons Samuel Katule (wa pili kushoto), katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Katika kampeni hiyo ya miezi mitatu iliyokuwa na lengo la kuhamasisha wateja wa benki hiyo na watanzania kutumia huduma za kibenki kwa njia za kidigitali, zawadi zenye jumla ya shs 120,000,000 zilitolewa. Kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Swere na kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga.
Mshindi wa droo kubwa ya kampeni ya ‘Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa’, Bi. Nasreen Karim Abdallah (kushoto), akizungumza baada ya kukabidhiwa zawadi yake ya shs 30,000,000 jijini Dar es Salaam jana. Kampeni hiyo ya miezi mitatu iliyokuwa na lengo la kuhamasisha wateja wa benki hiyo na watanzania kutumia huduma za kibenki kwa njia za kidigitali, zawadi zenye jumla ya shs 120,000,000 zilitolewa. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Wateja Binafsi, Bi. Ndabu Swere, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser na Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga.
Share:

UNDP YAWAPATIA WANAFUNZI WAJASIRIAMALI 20, SH. 70 MIL. KUPITIA YOUTH IGNITE FELLOWSHIP

Dkt. Harun Makandi, Mkurugenzi Msaidizi wa Sayansi na Teknolojia kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (wa tatu kushoto), akimkabidhi Bi. Herriet Nairumbe, Mwanzilishi wa Niches Food Products yenye makao yake Arusha na mshindi wa nafasi ya kwanza wa Youth Ignite Student Founders Fellowship – Msimu wa Pili, mfano wa hundi. Wanaoshuhudia tukio hilo upande wa kushoto ni John Rutere, Naibu Mwakilishi Mkazi wa UNDP Tanzania, na Bi. Shakila Mshana, Mwanzilishi Mwenza na Mkurugenzi Mtendaji wa StartHub Africa. Upande wa kulia kabisa ni Bi. Sanna-Liisa Taivalmaa, Mkuu wa Ushirikiano katika Ubalozi wa Finland, na Joseph Manirakiza, Meneja wa Programu ya FUNGUO, UNDP Tanzania.
John Rutere, Naibu Mwakilishi Mkazi wa UNDP Tanzania, akitoa pongezi wakati wa hafla ya kukabidhi vyeti kwa mmoja wa washindi wakuu wa Youth Ignite Student Founders Fellowship – Msimu wa Pili, iliyofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wanaoshuhudia tukio hilo upande wa kulia ni Dkt. Harun Makandi, Mkurugenzi Msaidizi wa Sayansi na Teknolojia kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, pamoja na Joseph Manirakiza, Meneja wa Programu ya FUNGUO, UNDP Tanzania.

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) nchini Tanzania limewapatia wanafunzi wajasiriamali 20 kutoka vyuo vikuu mbalimbali zawadi za fedha taslimu zenye thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 70, kufuatia shindano la uwasilishaji wa mawazo bunifu ya biashara lililoandaliwa chini ya Awamu ya Pili ya programu ya Youth Ignite Student Founders Fellowship.

Programu hiyo inatekelezwa kupitia Programu ya FUNGUO ya UNDP Tanzania, kwa ufadhili wa pamoja wa Serikali ya Uingereza kupitia Ofisi ya Mambo ya Nje, Jumuiya ya Madola na Maendeleo (FCDO), Umoja wa Ulaya (EU), pamoja na Serikali ya Finland.
Kukuza Ubunifu na Ujasiriamali wa Vijana

Hafla hiyo iliwakutanisha wanafunzi 30 kutoka taasisi mbalimbali za elimu ya juu nchini, waliowasilisha mawazo yao ya biashara mbele ya jopo la majaji. Mawazo hayo yalilenga kutoa suluhisho bunifu kwa changamoto za kijamii na kiuchumi, hatua inayoonesha ukuaji wa ubunifu na ujasiriamali miongoni mwa vijana wa Kitanzania.

Mbali na tuzo za fedha, washiriki wa programu walipatiwa msaada wa kitaalamu ikiwemo mafunzo ya maendeleo ya biashara, ushauri elekezi (mentorship), pamoja na maandalizi ya kuwafanya wawe tayari kuvutia wawekezaji.
Serikali Yapongeza Ushirikiano

Mgeni rasmi wa hafla hiyo, Dkt. Harun Makandi, Mkurugenzi Msaidizi wa Sayansi na Teknolojia kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, alisema programu hiyo inaendana kikamilifu na ajenda ya Serikali ya kukuza utafiti wenye tija kibiashara, ubunifu na ujasiriamali miongoni mwa vijana.

Mpango huu unaunga mkono jitihada za serikali za kulea kizazi kipya cha wabunifu na wazalishaji wa ajira kutoka taasisi zetu za elimu ya juu. Unaakisi mwelekeo wa Tanzania wa kuunganisha sayansi, teknolojia na ujasiriamali katika maendeleo ya taifa,” alisema Dkt. Makandi.

UNDP: Vijana ni Msingi wa Dira 2050

Akizungumza katika hotuba kuu, John Rutere, Naibu Mwakilishi Mkazi wa UNDP Tanzania, alibainisha kuwa programu hiyo ni sehemu ya mkakati mpana wa kusaidia utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050, inayolenga kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kipato cha kati cha juu ifikapo mwaka 2050.

Kufikia uchumi wa thamani ya Dola za Marekani trilioni moja kunahitaji uwekezaji wa makusudi kwa vijana na biashara zao. Youth Ignite Student Founders Fellowship ni mfano halisi wa miradi inayowawezesha vijana kwa ujuzi, mitandao ya wawekezaji na mitaji muhimu kwa ukuaji wa biashara zenye athari kubwa kiuchumi,” alisema Rutere.
Washirika wa Maendeleo Wasisitiza Ajira Jumuishi

Kwa upande wake, Bw. Euan Davidson, Kiongozi wa Timu ya Miradi Endelevu kutoka FCDO, alisisitiza umuhimu wa kuwekeza katika biashara zinazoongozwa na vijana kama njia ya kuchochea ukuaji wa uchumi jumuishi.

Westerwelle Foundation Tanzania na StartHub Africa walitoa mchango wao kwa kutoa mafunzo ya vitendo katika uandaaji wa mipango ya biashara na uwasilishaji wa mawazo (pitching), ili kuwaandaa washiriki kuvutia wawekezaji.

Naye Bi. Sanna-Liisa Taivalmaa, Mkuu wa Ushirikiano kutoka Ubalozi wa Finland, alithibitisha dhamira ya Finland kuendelea kuunga mkono mifumo ya ubunifu na ujasiriamali wa vijana nchini Tanzania.

Washindi Wapata Shilingi Milioni 6 Kila Mmoja

Miongoni mwa washindi waliofanya vizuri zaidi, kila mmoja alipokea Shilingi milioni 6 kwa ajili ya kukuza biashara zao.

Herriet Nairumbe, Mwanzilishi wa Niches Food Products kutoka Arusha, inayojishughulisha na uongezaji thamani wa pilipili na matunda, alisema fedha hizo zitasaidia kuongeza uzalishaji na kupanua masoko.

Fedha hizi zitanunua mashine zitakazoongeza tija na kutuwezesha kufikia masoko mapya ya mikoa mingine,” alisema Herriet, akiongeza kuwa programu hiyo imewasaidia kuimarisha ujuzi wa uhasibu, upangaji wa bei, ujenzi wa timu na huduma kwa wateja.

Mshindi mwingine, Irene George Ngatibigwa, Mwanzilishi Mwenza wa Eco Mushroom, alisema ufadhili huo utasaidia kuongeza uwezo wa uzalishaji wa bidhaa za uyoga na kuajiri vijana zaidi.

Kupitia mafunzo ya Youth Ignite, nimejifunza masoko, uwasilishaji kwa wawekezaji na ujenzi wa mitandao ya kibiashara. Ujuzi huu ni msingi wa ukuaji wa biashara yetu,” alisema Irene.

Kujenga Biashara za Kesho

Kupitia mafunzo, ushauri elekezi na msaada wa kifedha, Youth Ignite Student Founders Fellowship inaendelea kujenga kizazi cha wajasiriamali vijana wenye biashara zenye uwezo wa kukua na kuchangia katika mabadiliko ya kiuchumi ya Tanzania.

Washindi wa awamu hii wanawakilisha sekta mbalimbali zikiwemo teknolojia, kilimo-biashara, mabadiliko ya tabianchi, uzalishaji viwandani na ubunifu wa kijamii — ishara ya upana na ubora wa mawazo bunifu yanayotoka katika taasisi za elimu ya juu nchini.

Kupitia Programu ya FUNGUO, UNDP na washirika wake wanaendelea kuondoa vikwazo katika mfumo wa ubunifu nchini kwa kuwezesha upatikanaji wa ufadhili, ujuzi na mitandao, ili biashara changa ziweze kukua, kustawi na kuleta athari chanya endelevu kwa uchumi wa taifa.
Dkt. Harun Makandi, Mkurugenzi Msaidizi wa Sayansi na Teknolojia kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (wa pili kushoto), akimkabidhi mfano wa hundi mshindi wa nafasi ya pili wa Youth Ignite Student Founders Fellowship – Msimu wa Pili, iliyofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wanaoshuhudia tukio hilo upande wa kushoto ni John Rutere, Naibu Mwakilishi Mkazi wa UNDP Tanzania, huku upande wa kulia kabisa wakiwa Bi. Sanna-Liisa Taivalmaa, Mkuu wa Ushirikiano katika Ubalozi wa Finland, pamoja na Joseph Manirakiza, Meneja wa Programu ya FUNGUO, UNDP Tanzania.
Share:

Monday, February 2, 2026

Absa Bank Tanzania and World Bank Deepen Strategic Collaboration

 

Absa Bank Tanzania Managing Director, Mr. Obedi Laiser this week met with Mr. Nathan Belete, World Bank Division Director for Malawi, Tanzania, Zambia and Zimbabwe, for a strategic business engagement in  Dar es Salaam. The engagement focused on strengthening collaboration between the two institutions. News in pictures follows;
Share:

Monday, January 26, 2026

APeF Yazindua Mfuko wa Ziada Kupanua wigo wa uwekaji Akiba, Uwekezaji na Ulinzi

  

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana, (CMSA), CPA Nicodemus Mkama, akikabidhi waraka wa ofa kwa Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Africa Pension Fund (APeF), Dkt. Hamisi Kibola (wa tatu kushoto), kuashiria uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund, jijini Dar es Salaam leo. Wa pili kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa APeF, Bw. Mfaume Kimario, pamoja na wadau wengine wa Mfuko wa Ziada; kuanzia kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Alliance Life, Bw. Byford Mutikwasa, Bi. Tupokigwe Mwalwisi kutoka NBC na Bw. Lusungu.

DAR ES SALAAM, 26 Januari 2026. Africa Pension Fund Limited (APeF) leo imezindua rasmi Mfuko wa Ziada, ambao ni mfuko wa kwanza wa uwekezaji wa pamoja katika soko la fedha nchini Tanzania unaojumuisha mafao ya bima ya maisha, hatua inayoweka alama muhimu katika kupanua upatikanaji wa suluhisho za uwekezaji zilizo chini ya udhibiti. Hafla ya uzinduzi imefanyika katika Hoteli ya KingJada, Morocco Square, jijini Dar es Salaam. Kipindi cha awali cha uuzaji wa vipande kupitia mfuko huu kinaanza leo tarehe 26 Januari hadi 25 Februari 2026.

Hafla ya uzinduzi huo ilihudhuriwa na mgeni rasmi, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), CPA Nicodemus Mkama, ikihudhuriwa pia na wawakilishi kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), mifuko ya hifadhi ya jamii, wasimamizi wa mifuko, madalali, taasisi za kibenki na bima, pamoja na wanahabari.

Mfuko wa Ziada umebuniwa kuwasaidia wawekezaji kuweka akiba na kukuza fedha zao kupitia uwekezaji wenye nidhamu katika soko la fedha, ukiwa na faida ya ziada ya ulinzi wa bima ya maisha kwa wawekezaji binafsi wanaokidhi vigezo. Mfuko huu umerahisishwa kiutendaji, kwa kuwawezesha wawekezaji kuanza kwa urahisi, kuongeza uwekezaji wakati wowote, na kupata fedha zao ndani ya siku tatu za kazi.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa APeF, Bw. Mfaume Kimario, alisema, Ziada imeundwa kwa wawekezaji wanaotaka njia rahisi na za kuaminika za kukuza fedha zao bila kupoteza uwezo wa kupata fedha zao pindi zinapohitajika. Huu ni mfuko imara katika soko la fedha unaopatikana kwa urahisi, wenye ulinzi wa bima ya maisha kwa wawekezaji wanaokidhi vigezo ukianzia na thamani halisi ya uwekezaji (vipande), ya chini kabisa ya shilingi 250,000. Bima hiyo hutoa kinga sawa na asilimia 50 ya thamani halisi ya uwekezaji (vipande) hadi kiwango cha juu cha thamani kilichohakikishwa cha shilingi milioni 100, na kiwango cha juu cha malipo ya bima cha shilingi milioni 50.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti na Bodi ya Wakurugenzi, Dkt. Hamisi Kibola, Mjumbe wa Bodi ya APeF, aliipongeza CMSA kwa hatua zilizofikiwa katika kuendeleza masoko ya mitaji nchini Tanzania na kwa kukuza ukuaji na uhai unaoonekana sokoni kwa sasa. Alibainisha kuwa kiwango cha uwekaji akiba nchini Tanzania bado kiko chini ya asilimia 3, na akatoa wito wa kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya wasimamizi na wadau wa sekta ya fedha ili kujenga utamaduni imara wa kujiwekea akiba unaojengwa juu ya taaluma, uaminifu, elimu ya fedha na upatikanaji rahisi wa huduma. Aliongeza kuwa ndiyo sababu APeF ilianzishwa, ubunifu ukiwa kama msingi wake, ili kuongeza wigo kwa vitendo njia za uwekaji akiba na uwekezaji kupitia mifuko ya uwekezaji wa pamoja, mipango binafsi ya pensheni inayounganisha suluhisho za bima na masoko ya mitaji.

Mfuko wa Ziada umeandaliwa kwa ushirikiano na taasisi washirika muhimu, ambapo Alliance Life Assurance Limited ni mtoa bima, Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ni Mtunza Dhamana na Mdhamini. Wawekezaji wanaweza kupata huduma za Mfuko wa Ziada kupitia benki wakusanyaji zikiwemo CRDB Bank, NMB Bank, Exim Bank, Azania Bank, COOP Bank, NBC na Mwanga Hakika Bank, pamoja na kupitia mawakala walioidhinishwa na DSE na majukwaa ya kidijitali ya APeF.

Tunaalika Watanzania kufanya suala la kuweka akiba kuwa utamaduni wao kupitia Ziada. Unapoweka akiba kwa uthabiti, unaimarisha familia yako, kuinua jamii yako, na kuunga mkono maendeleo ya taifa. Ziada inakupa mahali rahisi pa kuanzia, kukua hatua kwa hatua, na kulinda kile kilicho muhimu zaidi,” aliongeza Ofisa Mtendaji Mkuu wa APef, Bw. Kimario.

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), CPA. Nicodemus Mkama alisema kuidhinishwa kwa mfuko wa ziada kunaendelea kuleta chachu zaidi katika maendeleo ya uwekezaji kwenye mifuko hiyo na kuifanya idadi ya mifuko hiyo ya uwekezaji wa pamoja kufikia 26.

Kuhusu APeF

Africa Pension Fund Limited (APeF) ni msimamizi wa mifuko aliyeidhinishwa, anayetoa huduma za usimamizi wa mifuko, mifuko ya uwekezaji wa pamoja, suluhisho za pensheni binafsi, usimamizi wa mali, na ushauri wa kifedha. APeF imejizatiti kuimarisha usalama wa kifedha kupitia suluhisho za uwekezaji bunifu, zenye uwazi na zinazozingatia misingi bora ya suluhisho za uwekezaji.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Africa Pension Fund (APeF), Bw. Mfaume Kimario, akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund, jijini Dar es Salaam leo.
Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Africa Pension Fund (APeF), Dkt. Hamisi Kibola akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund, jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wadau wakihudhuria hafla ya uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund unaoendeshwa na Africa Pension Fund (APeF).
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Africa Pension Fund (APeF), Bw. Mfaume Kimario (kushoto) akizungumza na baadhi ya wadau wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund wakati wa hafla ya uzinduzi wa mfuko huo, jijini Dar es Salaam leo.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana, (CMSA), CPA Nicodemus Mkama (katikati), Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Africa Pension Fund (APeF), Dkt. Hamisi Kibola (wa nne kushoto) na Ofisa Mtendaji Mkuu wa APeF, Bw. Mfaume Kimario (wa nne kulia) wakipiga picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa taasisi hiyo baada uzinduzi rasmi wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja wa Ziada Fund, jijini Dar es Salaam leo.
Share:

Wednesday, January 21, 2026

ABSA BANK TANZANIA YAFUNGA KAMPENI YA 'UJANJA NI KUSWIPE NA KADI YA ABSA' KWA DROO YA MWISHO NA KUTANGAZWA KWA MSHINDI WA ZAWADI KUU

Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki yaAbsaTanzania, Bw. Aron Luhanga (kushoto), akifanya droo ya mwisho ya kampeni ya benki ya miezi mitatu ya 'Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa', jijini Dar es Salaam jana. Mteja wa benki hiyo, Bi. Nasreen Karim Abdallah, alijinyakulia zawadi kuu ya Tsh 30,000,000. Kampeni hiyo ililenga kuwahamasisha wateja kuongeza matumizi ya kadi za debit na credit za Absa pamoja na huduma za kibenki kwa njia za kidigitali za benki hiyo.

Benki ya Absa Tanzania imehitimisha rasmi kampeni yake ya 'Ujanja ni Kuswipe na Kadi ya Absa' iliyodumu Kwa miezi mitatu baada ya kufanyika kwa droo ya tatu na ya mwisho katika hafla Iliyofanyika jijini Dar es Salaam, jana.

Droo ya mwisho imehitimisha kampeni ya miezi mitatu iliyolenga kuwazawadia wateja kwa kufanya miamala na huduma za kibenki kwa njia za kidijitali ikiwa ni pamoja na matumizi ya kadi, huku ikithibitisha dhamira ya Absa ya kuhimiza miamala salama, rahisi na isiyotumia fedha taslimu.

Katika hafla hiyo, Absa ilifanya droo ya mwisho ya kila mwezi na kutoa jumla ya shilingi milioni 18 za Kitanzania (TZS 18 milioni) kwa wateja watatu walioibuka washindi kutokana na ushiriki wao katika mwezi wa mwisho wa kampeni.

Washindi hao ni Bw. Abdulrazak Ali Seif (TZS 10 milioni), Bi. Aysha Mbarak Meghji (TZS 5 milioni), na Bw. Gibbons Samuel Katule (TZS 3 milioni). Droo hiyo ilifanyika kwa kuzingatia Masharti na Vigezo vya kampeni na mbele ya mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, ili kuhakikisha uwazi na haki katika mchakato wa uchaguzi wa washindi.

Katika tukio lililosubiriwa kwa hamu zaidi wakati wa kilele cha kampeni hiyo, Bi. Nasreen Karim Abdallah aliibuka Mshindi wa Zawadi Kuu, akiondoka na shilingi milioni 30 za Kitanzania (TZS 30 milioni). Ushindi huo umetokana na matumizi yake ya mara kwa mara ya huduma za benki za kidijitali na kadi za Absa katika kipindi chote cha kampeni, na unaonesha jinsi miamala ya kila siku inaweza kuleta mabadiliko makubwa katika maisha.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga, alisisitiza mchango mkubwa wa wateja katika mafanikio ya kampeni hiyo:

Kampeni hii imekuwa na Manufaa mkubwa kwa wateja wetu tangu mwanzo. Tumehamasishwa kuona jinsi wengi wao wakichangamkia njia rahisi, salama na zisizotumia fedha taslimu katika kufanya miamala. Play Your Cards Right imeonesha kuwa pale wateja wanapochagua benki ya kidijitali, kila mtu hunufaika, kuanzia urahisi wa huduma hadi kuimarika kwa ujumuishaji wa kifedha.

"Tunawashukuru kwa dhati wateja wetu kwa kuendelea kuiamini Absa na kuwa sehemu ya safari hii.

Kwa upande wake, Mkuu wa Usimamizi wa Taarifa na Uchambuzi wa Takwimu (MI & Analytics), Bw. Denis Kessy, alieleza athari pana ya kampeni hiyo:

Absa tunaamini kuwa kila mteja ana Stori yenye thamani. Kampeni hii imetupa fursa ya kusherehekea Stori hizo, kubwa na ndogo, kwa kuwazawadia wateja wetu kwa kutumia tu huduma zetu za benki.

Tunapohitimisha kampeni hii leo, tunajivunia si mshindi wa zawadi kuu pekee, bali kila mteja aliyeshiriki.

Aliendelea kusisitiza ukubwa wa mafanikio ya kampeni hiyo kwa kusema:

Kupitia kampeni hii, Absa iliwazawadia washindi 72 wa kila wiki, washindi tisa wa kila mwezi na mshindi mmoja wa Zawadi Kuu, kwa jumla ya shilingi milioni 120 za Kitanzania (TZS 120 milioni) zilizorejeshwa kwa wateja wetu.

Huu ni uthibitisho dhahiri kuwa kuchagua Absa kunalipa.

Kampeni ya Play Your Cards Right ilikuwa kampeni ya zawadi kwa wateja iliyodumu kwa miezi mitatu kuanzia Oktoba hadi Desemba 2025, ikiwa na lengo la kuhamasisha matumizi ya malipo ya kidijitali na yasiyotumia fedha taslimu. Wateja walipata nafasi ya kushiriki katika droo za kila wiki na kila mwezi kwa kutumia kadi zao za debit au credit za Absa kupitia malipo ya kuswipe, kutap (tap) au ununuzi mtandaoni.

Kwa kukamilika kwa droo ya mwisho, kampeni ya Play Your Cards Right imefikia tamati rasmi. Washindi waliotangazwa katika droo ya mwisho watatambuliwa rasmi katika hafla maalum ya kukabidhi zawadi itakayofanyika mwezi Februari, na hivyo kuhitimisha kampeni hii kwa namna ya kukumbukwa, ikiwa ni uthibitisho wa dhamira ya Absa ya kuwaweka wateja katikati ya kila zawadi na kila hatua ya safari yake.
Mmoja wa washindi wa kila mwezi wa kampeni ya miezi mitatu ya benki ya Absa Tanzania iitwayo 'Ujanja ni Kuswipe na Benki ya Absa' Bw. George Kivaria, akichukua tiketi ya bahati nasibu ili kumpata mshindi wa droo Kuu wakati wa droo ya mwisho iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Mteja wa benki hiyo, Bi. Nasreen Karim Abdallah, alishinda zawadi kuu ya Tsh 30,000,000. Kampeni hiyo ililenga kuwahamasisha wateja kuongeza matumizi ya kadi za debit na credit za Absa pamoja na pamoja na huduma za kibenki kwa njia za kidigitali za benki hiyo. Kushoto ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga.
Mkuu wa Usimamizi wa Taarifa na Uchambuzi wa Takwimu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Dennis Kessy (wa tatu kushoto), akikabidhi hundi ya mfano ya Tsh 500,000/- kwa Bw. George Kivaria (wa pili kushoto), mmoja wa washindi wa kampeni ya miezi mitatu ya benki hiyo iitwayo 'Ujanja ni Kuswipe na Benki ya Absa' wakati wa hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kampeni hiyo ililenga kuwahamasisha wateja kuongeza matumizi ya kadi za debit na credit za Absa pamoja na huduma za kibenki kwa njia za kidigitali za benki hiyo.
Mkuu wa Usimamizi wa Taarifa na Uchambuzi wa Takwimu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Dennis Kessy, akikabidhi hundi ya mfano ya Tsh 500,000/- kwa Bw. Mohammed Zulfikar Hemani (kushoto), mmoja wa washindi wa kampeni ya miezi mitatu ya benki hiyo iitwayo 'Ujanja ni Kuswipe na Benki ya Absa', wakati wa hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga.
Share:

Monday, December 15, 2025

BENKI YA ABSA YAIPONGEZA BLACK SWAN KWA USHINDI WA BARA AFRIKA, YATHIBITISHA DHAMIRA YA KUKUZA SAFARI YA UBUNIFU WA TEKNOLOJIA YA KIFEDHA (FINTECH) TANZANIA

Benki ya Absa Tanzania imeipongeza Black Swan kwa kuibuka mshindi wa jumla wa Absa–MEST Africa Challenge 2025, shindano la ubunifu linalojumuisha nchi mbalimbali barani Afrika na linaloendeshwa kwa ushirikiano na Meltwater Entrepreneurial School of Technology (MEST Africa). Black Swan pia ilikuwa miongoni mwa washindi watatu bora wa Absa Wazo Challenge Tanzania 2025.

Ushindi huo wa ngazi ya bara, uliopatikana kupitia kampuni ya Black Swan iliyosajiliwa nchini Mauritius, ni hatua muhimu kwa teknolojia ya fedha (fintech), ambayo safari yake ilianza kutambulika ndani ya nchi kupitia Wazo Challenge Tanzania ya Absa Bank Tanzania. Mafanikio hayo yanaonesha nafasi ya Absa kama kichocheo cha ubunifu, kutoka uthibitisho wa ndani hadi ukuaji wa kiwango cha bara.

Shindano la Absa–MEST Africa Challenge liliwakutanisha kampuni bunifu zinazojihusisha na teknolojia za kifedha zenye uwezo mkubwa kutoka katika nchi mbalimbali ambako Absa inafanya kazi. Black Swan ilijitofautisha kwa suluhisho lake la upimaji mbadala wa uaminifu wa mikopo linalotumia Akili Bandia (AI), linalolenga kupanua upatikanaji wa huduma za kifedha kwa watu na biashara ndogo na za kati (SMEs) ambazo hazijahudumiwa vya kutosha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kulia) akishikana mikono na Mkurugenzi wa Huduma Jumuishi za Fedha wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Kennedy Komba jijini Dar es Salaam hivi karibuni, wakati wa hafla ya uzinduzi wa mpango wa Wazo Challenge Tanzania, unaolenga kuimarisha ubunifu na ujasiriamali katika sekta ya Teknolojia ya Fedha (FinTech) na biashara changa (startup) nchini Tanzania. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja na Huduma za Kidigitali, Bw. Samuel Mkuyu. (Picha; Maktaba)

Akizungumza kuhusu mafanikio hayo, Sam Mkuyu, Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja na Huduma za Kidigitali wa Benki ya Absa Tanzania, Samuel Mkuyu, alisema: “Ushindi wa Black Swan ni uthibitisho madhubuti wa sababu za kuwepo kwa majukwaa kama Wazo Challenge Tanzania. Ubunifu haukui ukiwa peke yake, unahitaji upatikanaji wa utaalamu, matumizi halisi, na taasisi zilizo tayari kushirikiana. Kupitia Wazo Challenge Tanzania, tunaunda kwa makusudi mazingira yanayowezesha fintech kujaribu mawazo, kuimarisha mifumo yao ya kiteknolojia, na kujenga suluhisho zinazoweza kukua, salama, na zinazoendana na mustakabali wa sekta ya benki. Kuona ubunifu uliojikita Tanzania ukishinda katika ngazi ya bara ni matokeo hasa tuliyolenga kuyawezesha.

Wazo Challenge Tanzania, iliyoanzishwa na Benki ya Absa Tanzania kwa ushirikiano na Hindsight Ventures, ilibuniwa kusaidia teknolojia za kifedha na wabunifu wanaoendeleza suluhisho zinazolingana na kaulimbiu ya “Bank of the Future.” Tangu kuanzishwa kwake, mpango huu umejenga imani miongoni mwa wabunifu wa ndani, ukionesha kuwa kampuni zinzojishughulisha na teknolojia za kifedha za Tanzania zinaweza kushindana na kushinda katika majukwaa makubwa barani Afrika.

Zaidi ya Tanzania, Absa Group inaendelea kuchangia kwa kiwango kikubwa ukuaji wa fintech barani Afrika kupitia mipango kama MEST Africa Challenge, inayounganisha kampuni changa na mitaji, ushirikiano wa kibiashara wa kiwango cha taasisi, pamoja na fursa za kuvuka mipaka ya nchi.
Baadhi ya washiriki wa Wazo Challenge Tanzania 2025, wakiwa katika hafla ya makabidhiano ya zawadi kwa washindi, jijini Dar es Salaam hivi karibuni. (Picha; Absa Bank Tanzania)

Akizungumza kuhusu dhamira pana ya Absa na umuhimu wa kusimulia hadithi za ubunifu, Aron Luhanga, Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, alisema:

Safari ya Black Swan inaakisi kikamilifu ahadi ya chapa yetu isemayo ‘Stori yako ina thamani’. Kutoka katika mfumo wa ubunifu wa Tanzania hadi kutambulika katika ngazi ya bara, hii ni stori ya imani, ushirikiano na uwezekano. Katika Absa, dhamira yetu iko wazi, Kuiwezesha Afrika ya Kesho, pamoja, hatua moja baada ya nyingine. Stori za fintech kama Black Swan zinatuhamasisha kuendelea kuunga mkono ubunifu na kusimama bega kwa bega na wajasiriamali wanaounda mustakabali wa Afrika.

Absa Bank Tanzania pia imetangaza kuwa maandalizi ya toleo lijalo la Wazo Challenge Tanzania yanaendelea, likitarajiwa kufanyika mwaka 2026, likiwa na msisitizo mkubwa zaidi kwenye suluhisho za teknoljia za kifedha zinazoweza kukua, ujumuishi wa kidijitali, na ushirikiano unaozalisha matokeo chanya ya kiuchumi.

Tunapoangalia mbele kuelekea Wazo Challenge Tanzania 2026, tunataka wabunifu wajue kuwa kuna taasisi katika soko hili zinazowaamini,” aliongeza Mkuyu. “Ubunifu hustawi pale imani inapokutana na fursa, na Absa imejidhatiti kutoa vyote viwili.

Kupitia mipango ya ngazi ya nchi na ya Kundi, Absa inaendelea kujiweka kama kinara wa fikra katika uwezeshaji wa fteknolojia za kifedha, ushirikiano wa ubunifu, na ujumuishi wa kifedha, ikihakikisha kuwa mawazo yanayozaliwa Tanzania yanaweza kukua na kuwa suluhisho zinazohudumia Afrika nzima.
Share:

Wednesday, December 10, 2025

AVODA BLUE TANZANIA GRADUATES FIRST COHORT OF ENTREPRENEURS

Unleashed Africa Social Enterprises Acting Board Chairperson, Ms. Ngianasia Minja (second right), presents a certificate to Ms. Esther Kolimba, a graduand of the four-month AVODA Blue Tanzania entrepreneurship program, during a function held in Dar es Salaam. The program aims to strengthen Tanzania’s business landscape through world-class strategy, operational excellence, and faith-based leadership principles. Looking on from left are Avoda Group Founder and CEO, Mr. Jun Shiomitsu, and Avoda Uganda Country Director, Mr. Joshua Agonya.

By Peter Mgongo | Dar es Salaam, Tanzania

The AVODA Blue Tanzania Program has celebrated the graduation of its first cohort of entrepreneurs, marking a major milestone in developing globally competitive and ethically grounded business leaders in the country. The ceremony held in Dar es Salaam recently, bringing together government leaders, business executives, investors, and development partners.

Launched earlier this year, AVODA Blue Tanzania is a four-month, execution-focused entrepreneurship program adapted from the Cambridge MBA and contextualized for African markets, the program aims to strengthen Tanzania’s business landscape through world-class strategy, operational excellence, and faith-based leadership principles.

Cohort 1 brought together founders from sectors including technology, food production, logistics, fashion, education, real estate advisory, and social enterprise. Over the past four months, participants completed intensive training sessions, virtual modules, one-on-one diagnostics, and practical assignments applied directly to their businesses.

Guest of Honor, Mr. Jason Ndanguzi who was representing the ICT Commission’s Director General, Dr. Nkundwe Mwasaga, underscored the importance of entrepreneurship in advancing the country’s digital economy.

This moment aligns with Tanzania’s broader vision, as a nation, we are accelerating the Digital Economy Framework, strengthening our ICT Policy, and preparing our people and enterprises for a knowledge-based, technology-enabled future. For the ICT Commission, this program demonstrates exactly the kind of capacity-building that Tanzania needs as we transition into a digital era."

Across global innovation economies, one pattern is clear; countries rise not because they have ideas, but because they have capable founders. Founders with strategic discipline. Founders who understand technology. Founders who lead with integrity. Founders who build enterprises that last. Avoda Blue is among the few programs in Tanzania addressing this with such depth, rigor, and intentionality”, he noted.

The ICT guru added; “As the ICT Commission, we stand ready to deepen collaboration with programs that strengthen digital capability, prepare entrepreneurs for scale, integrate emerging technologies, and support the creation of sustainable businesses. Tanzania’s rise depends on entrepreneurs who are ready to build boldly, adapt quickly, and innovate continuously."

To our graduates, today marks your transition into a new identity, you are no longer simply business owners, you are architects of Tanzania’s digital and economic future. Over the last four months, you have engaged with operational frameworks, financial discipline, AI tools, product refinement, Kingdom leadership principles, and investor readiness, this kind of preparation is rare in our market, and deeply necessary”, added Mr. Ndanguzi.

Earlier the Unleashed Africa CEO, Ms. Khalila Mbowe said her social ventures reaffirms its national commitment to building world-class programs that equip Tanzania’s youth, founders, and industry leaders with the skills, networks, and mindsets needed to build high-performing, future-ready enterprises

For too long, many African entrepreneurs including many of us have operated from the back benches of business excellence, that era must be history, across our brands; from RiseUp, to JUU’s creative economy work, to The Space and its flagship Nipe Dili program, Unleashed Africa has been steadily constructing a holistic empowerment ecosystem where young people can access opportunities, develop 21st-century skills, secure business support, and deepen their leadership potential”, said Ms. Khalila.

Avoda Group Founder and CEO Jun Shiomitsu expressed deep appreciation to Unleashed Africa for being the first organization in Tanzania to believe in and partner with the AVODA mission. He noted that although expanding the program beyond Uganda was initially considered difficult, the team’s prayers and the strong Christian entrepreneurial ecosystem helped pave the way. He added that their relationship with Unleashed Africa is already bearing visible fruit, demonstrating the powerful work taking place in Tanzania.

To the graduates; first of all, you believed in us. Now, as you graduate, it is our turn to believe in you, to ensure that your businesses find the customers they need and the capital they require. It is our turn now to place our trust in you. I am confident that your businesses will achieve great things, truly great things, and I stand firmly by that confidence. Christian connections around the world have already seen and experienced our services. By graduating from Avoda, you are being planted into a massive global ecosystem, in Asia, Europe, and the Americas, among people who share your faith and who want to see you succeed,” he said.

One of the graduands, Engineer Regina Fumbuka from Multi Genius Africa, an organization working to make mathematics more appealing and easier to teach said, the Avoda program has helped her learn how to become a good leader, build effective business systems, manage a business, and maintain proper financial records. She added that the program has enabled her to progress from one level to another in her entrepreneurial journey.

Three awards were presented during the ceremony; the Exceptional Performance Award, Business Growth Excellence Award, and Servant Leadership Award. Graduates also showcased their businesses, growth milestones, and investment or partnership needs through a three-minute pitch session.
Unleashed Africa Social Enterprises Acting Board Chairperson, Ms. Ngianasia Minja (second right), presents a certificate to Mr. Alexander Rwiza, a graduand of the four-month AVODA Blue Tanzania entrepreneurship program, during a function held in Dar es Salaam recently. The program aims to strengthen Tanzania’s business landscape through world-class strategy, operational excellence, and faith-based leadership principles. Looking on from left are Avoda Group Founder and CEO, Mr. Jun Shiomitsu, and Avoda Uganda Country Director, Mr. Joshua Agonya.
Unleashed Africa Chief Executive Officer, Ms. Khalila Mbowe (right), moderates a panel discussion during the four-month AVODA Blue Tanzania entrepreneurship program graduation, adapted from the Cambridge MBA and contextualized for African markets. The program aims to strengthen Tanzania’s business landscape through world-class strategy, operational excellence, and faith-based leadership principles. The event was held in Dar es Salaam recently. On her right are Avoda Uganda Country Director, Mr. Joshua Agonya; one of the graduands, Ms. Esther Kolimba and Avoda Group Founder and CEO, Mr. Jun Shiomitsu. (Photos by Peter Mgongo)
Share:

Friday, December 5, 2025

Benki ya Absa Tanzania yang'ara tuzo za NBAA

  

Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Laurent Luswetila (kulia), akikabidhi tuzo ya mshindi wa pili wa Uwasilishaji Bora wa Taarifa za Fedha katika kitengo cha Mabenki yenye Ukubwa wa Kati kwa Mwaka 2024 zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), kwa Mkuu wa Uchambuzi wa Utendaji wa Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Stivin Augustino (wa pili kushoto) na Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa benki hiyo, Bw. Muhsin Kaye, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Wa tatu kushoto Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA. Pius Maneno.
Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Muhsin Kaye ( wa pili kushoto) akishikana mikono na Mwenyekiti wa Bodi ya NBAA, CPA Prof. Sylvia Temu, mara baada ya kupokea tuzo ya mshindi wa pili wa Uwasilishaji Bora wa Taarifa za Fedha katika kitengo cha Mabenki yenye Ukubwa wa Kati kwa Mwaka 2024 zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Laurent Luswetila, Mkurugenzi Mtendaji NBAA, CPA. Pius Maneno na Mkuu wa Uchambuzi wa Utendaji wa Biashara wa benki hiyo, Bw. Stivin Augustino.
Mkuu wa Uchambuzi wa Utendaji wa Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Stivin Augustino (kushoto) na Mdhibiti wa Masuala ya Fedha wa benki hiyo, Bw. Muhsin Kaye wakipozi mbele ya wapigapicha baada ya kukabidhiwa tuzo ya mshindi wa pili wa Uwasilishaji Bora wa Taarifa za Fedha katika kitengo cha Mabenki yenye Ukubwa wa Kati kwa Mwaka 2024, zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Uchambuzi wa Utendaji wa Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Stivin Augustino (mstari wa mbele wa tatu kushoto) akipiga picha ya pamoja na washindi mbalimbali wa tuzo za Uwasilishaji Bora wa Taarifa za Fedha katika kitengo cha Mabenki yenye Ukubwa wa Kati kwa Mwaka 2024, zinazotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), zilizofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Share:

Thursday, December 4, 2025

Absa Bank Tanzania Awards TZS 21 Million to its Customers in Latest Play Your Cards Right Raffle Draw

One of the winners of the first draw of the Absa Bank ‘Play Your Card Right’ campaign, Ms. Flora Obeto (left), receives a dummy cheque of TZS 3 million from the Absa’ Retail Banking Director, Mseka Ndabu Swere (right), during an event held alongside the second draw of the campaign in Dar es Salaam recently. During the draw, Mr. Joseph Mafuru won TZS 3 million, Ms. Xuan Lou won TZS 5 million, and Dr. Fauz Twain won TZS 10 million. Looking on is Absa Bank Tanzania Citizenship and Events Manager, Ms. Abigail Lukuvi.
One of the winners of the first draw of the Absa Bank ‘Play Your Card Right’ campaign, Ms. Flora Obeto (left), conducts the second draw of the campaign in Dar es Salaam recently. During the draw, Mr. Joseph Mafuru won TZS 3 million, Ms. Xuan Lou won TZS 5 million, and Dr. Fauz Twain won TZS 10 million. From left are Absa’s Citizenship and Events Manager, Ms. Abigail Lukuvi; Retail Banking Director, Ms. Ndabu Swere; a representative from the Gaming Board of Tanzania, Ms. Neema Tatock; and the bank’s Marketing & Communications Manager, Mr. Beda Biswalo.
Absa Tanzania’s Retail Banking Director, Ms. Ndabu Swere (centre), speaks in Dar es Salaam yesterday, during the second draw event of the Absa Bank ‘Play Your Card Right’ campaign, where the previous draw’s winner, Ms. Flora Obeto (second left), was also presented with her cash prize of TZS 3 million. During the draw, Mr. Joseph Mafuru won TZS 3 million, Ms. Xuan Lou won TZS 5 million, and Dr. Fauz Twain won TZS 10 million. From left are Absa’s Citizenship and Events Manager, Ms. Abigail Lukuvi, and a representative from the Gaming Board of Tanzania, Ms. Neema Tatock.
One of the winners of the first draw of the Absa Bank ‘Play Your Card Right’ campaign, Ms. Flora Obeto (centre), poses for a photo with some employees of Absa Bank Tanzania shortly after receiving a dummy cheque of TZS 3 million from the bank’s Director of Retail Banking, Ms. Ndabu Swere, during an event where Absa also conducted the second draw of the campaign. During the draw, Mr. Joseph Mafuru won TZS 3 million, Ms. Xuan Lou won TZS 5 million, and Dr. Fauz Twain won TZS 10 million.

Absa Bank Tanzania today hosted a vibrant press conference at Absa House, celebrating the second month winners of the ongoing Play Your Cards Right campaign. A total of TZS 18 million was awarded to three monthly winners, along with an additional TZS 3 million distributed among the Week 8 winners.

During the event, the three-monthly winners were announced and celebrated: Dr Fauz Twalib received TZS 10 million, Xuan Liu received TZS 5 million, and Joseph Constantine Mafuru received TZS 3 million. Additionally, the six weekly winners for Week 8, each awarded TZS 500,000, were officially recognized and celebrated. The weekly winners are Anita Peter Mselle, Michael Marshall Pemba, Mr. Idris Aziz Almamad Mazar, Shamma Kurban Hussein Dhirani, Christel Abdiel Ulomi, and Gheorghe Alexandru.

Reflecting on the journey of the campaign, Ms. Ndabu Swere, Director of Retail Banking, stated: “We are delighted with how Play Your Cards Right has resonated with our customers. It's encouraging to see so many embracing digital and card transactions, which are not only convenient but also enhance financial inclusion and safety. We sincerely thank our customers for their loyalty and participation.

Mr. Samuel Mkuyu, Director of Customer Experience & Digital, added: “At Absa, our purpose is to empower Africa’s tomorrow, together, one story at a time. Our brand promise is that ‘Your story matters,’ and this campaign brings that promise to life. By celebrating our customers’ stories, we reinforce that each transaction is part of a larger narrative of growth and trust.

In a heartwarming highlight, Mr. Felician Hechei, the winner of the previously announced luxury trip to the South Africa Champagne Festival, shared his experience. The trip was truly exceptional. From the business class flights to the five-star hospitality, Absa took care of everything. The Champagne Festival itself was a once-in-a-lifetime experience, and I encourage everyone to participate in future Absa campaigns.

The Play Your Cards Right campaign continues until the end of December 2025, culminating in a grand prize draw in January 2026 where one lucky customer will win TZS 30 million. “It’s going to be a fantastic start to 2026 for our winners,” Mr. Mkuyu
noted.
Share:

Wednesday, December 3, 2025

Benki ya Absa yakabidhi msaada wa mahitaji muhimu yakiwemo vyakula, sabuni, vinywaji na cherehani kwa kituo cha kulelea watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu cha Raya Islamic Orphanage Centre kilichopo Lukono, wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro

  

Meneja wa Tawi la Benki ya Absa Mkoa wa Morogoro, Bw. Godfrey Chilewa (katikati) na Ofisa wa kitengo cha fedha wa benki hiyo, Bi. Aiva Mussa, wakikabidhi kichwa cha chereheni kwa Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Raya Islamic Orphanage Centre Lugono, Bw. Ramadhani Msombeli, katika hafla ambayo benki hiyo ilikabidhi msaada wa mahitaji mengine muhimu yakiwemo vyakula, sabuni na vinywaji, kituoni hapo, mkoani Morogoro, jana.

Morogoro | Benki ya Absa imetoa msaada wa mahitaji muhimu kwa watoto yatima wanaolelewa katika kituo cha Raya Islamic Orphanage Centre kilichopo kijiji cha Lugono wilayani Mvomero, mkoani Morogoro, ikiwa ni sehemu ya mchango wa benki hiyo na wafanyakazi wake katika kuunga mkono juhudi za malezi na kuboresha ustawi wa watoto wanaoishi katika mazingira magumu.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo kwa walezi na watoto kituoni hapo jana, Meneja wa Tawi la Absa Mkoa wa Morogoro, Godfrey Chilewa, alisema hatua hiyo ni muendelezo wa benki hiyo katika kurudisha fadhila kwa jamii inayowazunguka. Alisema kituo hicho ni miongoni mwa maeneo wanayoyafikia kwa lengo la kupunguza changamoto za malezi zinazowakabili watoto yatima na wenye mazingira magumu.

Chilewa alisema benki hiyo inatambua kazi kubwa inayofanywa na vituo vya kuhudumia watoto yatima nchini, na kwamba changamoto wanazopitia zinahitaji nguvu ya pamoja kutoka kwa watu binafsi, taasisi na makampuni ili kuhakikisha watoto hao wanapata huduma bora na makuzi salama.

Watoto yatima wana uhitaji sawa wa malezi kama watoto wengine wanaokua katika familia zao, watoto hawa nao wana story za maisha yao wangependa zitimie, sisi Absa tunasema ‘Stori yako ina thamani’, Stori za maisha ya watoto hawa zina thamani kwetu na tunaamini misaada kama hii inakwenda kuchangia kukamilika kwa stori zao."

Mara nyingi watoto wanaolelewa kwenye vituo wanakosa baadhi ya mahitaji ya msingi kutokana na uwezo mdogo wa vituo hivyo. Hivyo, ni jukumu letu kama jamii kusaidia kile tunachokipata ili watoto hawa wakue kama wengine,” alisema Chilewa.

Akiendelea kueleza, alisema jamii ina wajibu wa kusaidia kujenga kizazi chenye maarifa, uwezo wa kujitegemea na dira sahihi, huku akisisitiza kuwa watoto yatima mara nyingi hukosa huduma muhimu kama chakula, mavazi, elimu na afya. Aliongeza kuwa ndoto ya Absa ni kuona changamoto hizo zinapungua kupitia ushirikiano na wadau mbalimbali akiongeza kuwa hii inaenda sambamba na lengo la benki hiyo la ‘Kuiwezesha Afrika na Tanzania ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingi’.

Saidi Hamis (27), mmoja wa vijana waliokulia kituoni hapo, alisema kituo hicho kina jumla ya watoto 113, ambapo wavulana ni 66 na wasichana 47. Alieleza kuwa kituo kilianzishwa mwaka 2013 eneo la Mindu kabla ya kuhamia Lugono, na kwa sasa wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa uzio wa kuzunguka makazi yao.

Changamoto kubwa ni kukosa uzio, jambo ambalo linatuweka katika hatari ya kuvamiwa na wanyama wakali, ikiwemo tembo wanaotoroka Hifadhi ya Taifa ya Mikumi. Tunaiomba jamii kutusaidia kufanikisha ujenzi wa uzio ili watoto wawe salama,” alisema Saidi.

Kwa upande wake, Karomelo Kizilahabi (17), mmoja wa watoto wanaolelewa kituoni, alisema msaada walioupokea utawasaidia kwa kiasi kikubwa, hasa cherehani nne walizokabidhiwa ambazo zitawawezesha kujifunza ufundi wa kushona nguo.

Cherehani hizi zitatusaidia kupata ujuzi wa kushona nguo na kutujengea uwezo wa kujitegemea baadaye. Tunawashukuru kwa kutukumbuka na tunawaombea muendelee kuwa na moyo huu,” alisema Karomelo.
Meneja wa Tawi la Benki ya Absa Mkoa wa Morogoro, Bw. Godfrey Chilewa (Katikati) na Ofisa wa kitengo cha mauzo wa benki hiyo, Bi. Grace Ndile wakikabidhi mfuko wa unga kwa Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Raya Islamic Orphanage Centre Lugono, Bw. Ramadhani Msombeli katika hafla ambayo benki hiyo ilikabidhi msaada wa mahitaji muhimu vikiwemo vyakula, sabuni, vinywaji na cherehani, kituoni hapo, mkoani Morogoro, jana.
Meneja wa Tawi la Benki ya Absa Mkoa wa Morogoro, Bw. Godfrey Chilewa (Katikati) na Meneja Masoko wa benki hiyo, Bw. Shauri Masengwa wakiwakabidhi vinywaji watoto, Karomelo Kizilahabi na Jamali Abdallah, katika hafla ambayo benki hiyo ilikabidhi msaada wa mahitaji muhimu vikiwemo vyakula, sabuni na cherehani, kwa kituo cha Raya Islamic Orphanage Centre Lugono wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, jana.
Meneja wa Tawi la Benki ya Absa Mkoa wa Morogoro, Bw. Godfrey Chilewa kushoto na baadhi wafanyakazi wenzake wa tawi hilo, wakiwa na baadhi ya watoto yatima wa Kituo cha Raya Islamic Orphanage Centre kilichopo Lugono wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, baada ya kukabidhi msaada wa mahitaji muhimu vikiwemo vyakula, sabuni, vinywaji na cherehani, kituoni hapo jana.
Meneja wa Tawi la Benki ya Absa Mkoa wa Morogoro, Bw. Godfrey Chilewa (Katikati), baadhi wafanyakazi wenzake na wasimamizi wa Kituo cha watoto yatima cha Raya Islamic Orphanage Centre kilichopo Lugono wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, wakipozi mbele ya wapiga picha, muda mfupi baada ya meneja huyo kukabidhi msaada wa mahitaji muhimu vikiwemo vyakula, sabuni, vinywaji na cherehani, vilivyotolewa na benki hiyo, kituoni hapo jana.
Share:

Monday, December 1, 2025

BENKI YA ABSA YASHINDA TUZO YA ‘BENKI INAYOPENDEKEZWA NA KUFIKIWA ZAIDI MASHARIKI NA KUSINI MWA AFRIKA’

 

Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Irene Mwilongo (katikati), pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake, wakionesha tuzo ya ‘Benki Inayopendekezwa na Kufikiwa zaidi Mashariki na Kusini mwa Afrika’ mara baada ya kukabidhiwa, katika hafla ya utoaji wa tuzo za Chaguo la Walaji Afrika 2025, jijini Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Uendeshaji wa Matawi wa Benki ya Absa Tanzania Bi. Irene Mwilongo (wa tatu kulia), akipokea tuzo ya ‘Benki Inayopendekezwa na Kufikiwa zaidi Mashariki na Kusini mwa Afrika' kutoka kwa Mwakilishi kutoka waandaaji wa tuzo hizo, Bi. Balqis Njuki, katika hafla ya kila mwaka ya utoaji wa Tuzo za Chaguo la Walaji Afrika 2025, jijini Dar es Salaam jana. Wengine ni baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo.
Mkuu wa Uchambuzi wa Utendaji wa Biashara wa Benki ya Absa Tanzani, Bw. Stivia Augustino (wa tatu kulia), akionesha tuzo ya ‘Benki Inayopendekezwa na Kufikiwa zaidi Mashariki na Kusini mwa Afrika’, katika hafla ya kila mwaka ya utoaji wa Tuzo za Chaguo la Walaji Africa 2025, jijini Dar es Salaam jana. Wengine ni baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo.
Mkuu wa Mikakati na Data wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. John Mosha (wa nne kulia), akizungumza baada ya kupokea tuzo ya ‘Benki Inayopendekezwa na Kufikiwa zaidi Mashariki na Kusini mwa Afrika’, katika hafla ya kila mwaka ya utoaji wa Tuzo za Chaguo la Walaji Africa 2025, jijini Dar es Salaam jana. Wengine ni baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive