A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Wednesday, April 15, 2026

BENKI YA ABSA TANZANIA YAONGEZA KIWANGO CHA MKOPO BINAFSI NA MUDA WA MAREJESHO KUWAWEZESHA WAFANYAKAZI WA SEKTA BINAFSI NA YA UMMA

Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benkiya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Swere (katikati), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kampeni ya “Jisogeze na Mkopo wa hadi TZS 200m”, inayolenga wafanyakazi wa sekta binafsi na umma, jijini Dar es Salaam leo. Pichani kushoto ni Bw. Aron Luhanga, Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano na kulia ni Bw. Heristraton Genesis, Mkuu wa Mikakati na Bidhaa za Wateja Binafsi.

Benki ya Absa Tanzania imetangaza maboresho katika bidhaa yake ya Mkopo Binafsi Usio na Dhamana kwa wafanyakazi wa sekta binafsi na Umma wanaopokea mishahara, hatua inayolenga kuimarisha upatikanaji wa mikopo nafuu na yenye masharti nafuu zaidi ikiwa ni sehemu ya dhamira ya benki hiyo ya kuiwezesha Africa ya Kesho, pamoja, hatua Moja baada ya nyingine.

Chini ya maboresho hayo mapya, wafanyakazi wa sekta binafsi na umma sasa wanaweza kupata mikopo hadi shilingi milioni 200 za Kitanzania, kutoka kiwango cha awali cha shilingi milioni 150. Aidha, muda wa marejesho umeongezwa hadi miezi 96 (sawa na miaka 8), huku mkopo huo ukiendelea kutolewa bila hitaji la dhamana yoyote.

Huduma hii inawahusu wateja waliopo tayari benki (ETB) pamoja na wateja wapya (NTB), kwa kuzingatia taratibu za kawaida za tathmini ya uwezo wa mkopo.

Maboresho haya yanafuatia hatua kama hiyo iliyotekelezwa awali kwa wafanyakazi wa sekta ya umma, ambapo Absa iliongeza kiwango cha mkopo hadi shilingi milioni 200, kuongeza muda wa marejesho hadi miaka 10, na kupunguza muda wa kusubiri kuongeza mkopo (top-up) kutoka miezi 6 hadi miezi 3.

Hatua hizi kwa pamoja zinaonyesha dhamira endelevu ya Absa kusaidia wateja wanaopokea mishahara katika sekta mbalimbali katika hatua muhimu za maisha yao ya kifedha.

Akizungumza wakati wa kutangaza maboresho hayo, Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Swere, alisema hatua hiyo imejengwa katika uelewa wa kina wa safari za maisha ya wateja. “Katika Absa, tunaelewa kuwa maisha ya kila mteja ni simulizi, yenye sura tofauti na nyakati muhimu. Iwe uko sekta ya umma au binafsi, jukumu letu ni kuwawezesha wateja kusonga mbele kwa kujiamini. Kwa kuboresha mikopo yetu binafsi isiyo na dhamana, tunawawezesha kusema NDIO kwa maendeleo – kwa sababu stori yao ni ya thamani sana,” alisema Bi. Ndabu.

Bi. Ndabu alisisitiza umuhimu wa unafuu na unyumbufu wa kifedha katika hatua mbalimbali za maisha. “Kuongezwa kwa muda wa marejesho na kiwango cha mkopo kunawapa wateja nafasi ya kusawazisha majukumu ya leo na malengo ya kesho. Kuanzia kuanzisha biashara, kuboresha makazi, kuwekeza katika elimu, kugharamia matibabu hadi kuunganisha madeni, bidhaa hii inawawezesha wateja kujisogeza mbele bila shinikizo lisilo la lazima la kifedha,” aliongeza.

Alibainisha pia kuwa wateja waliopo wanaokidhi vigezo wanaweza kuomba nyongeza ya mkopo au kufanya marekebisho ya mkopo (refinancing), kwa mujibu wa sera za ndani za benki na idhini ya tathmini ya mkopo.

Maboresho haya yanaungwa mkono na kampeni ya wateja ijulikanayo kama “Jisogeze na Mkopo wa hadi TZS 200m”, inayowahamasisha wateja kusonga mbele kwa ujasiri katika safari zao za kifedha.

Wateja wanaweza kuomba mkopo huo kwa kutembelea tawi lolote la Absa, kuzungumza na Afisa Mahusiano au kuwasiliana na vituo vya huduma kwa wateja vya benki hiyo.
Mkuu wa Mikakati na Bidhaa za Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Heristraton Genesis (kulia), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kampeni ya “Jisogeze na Mkopo wa hadi TZS 200m”, inayolenga wafanyakazi wa sekta binafsi na umma, jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka kushoto ni Bw. Aron Luhanga, Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano na Bi. Ndabu Swere, Mkurugenzi wa Wateja Binafsi kutoka benki hiyo
Baadhi ya wakurugenzi na wafanyakazi wa Benki ya Absa, wakifurahia uzinduzi wa kampeni ya 'Jisogeze na Mkopo wa hadi TZS 200m jijini Dar es Salaam leo.
Share:

Monday, April 13, 2026

BENKI YA ABSA TANZANIA YAKABIDHI WODI YA WAZAZI ILIYOKARABATIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA TEMEKE

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya (kushoto), na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke, Dk. Mfaume Kibwana (Katikati), wakifungua pazia kuashiria makabidhiano rasmi ya Wodi ya Wazazi, iliyofanyiwa ukarabati na Benki ya Absa. Hafla hiyo ilifanyika hospitalini hapo, Temeke, Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa benki hiyo, Bw. Aron Luhanga.

Benki ya Absa Bank Tanzania leo imekabidhi rasmi wodi iliyokarabatiwa ya Wazazi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke, ikiwa ni sehemu ya mpango wa kijamii unaoongozwa na wafanyakazi wa benki hiyo, wenye lengo la kuboresha mazingira ya huduma kwa kina mama, watoto pamoja na wahudumu wa afya.

Ukarabati huo umetekelezwa kupitia mpango wa Absa unaojulikana kama “Adopt a Ward”, ambao unaendeshwa na wafanyakazi wenyewe kwa kubaini mahitaji ya jamii, kukusanya rasilimali na kushirikiana na benki katika kuleta mabadiliko chanya yenye tija kwa jamii.

Kazi za ukarabati zilizofanyika katika wodi hiyo ni pamoja na akarabati wa paa na dari, uwekaji wa vigae kwenye kuta za vyoo, ukarabati wa madirisha, kazi za nje za mabomba maalumu ya plastiki (PVC), ukarabati wa mifumo ya umeme, kazi za mabomba ya maji, ufungaji wa milango ya alumini, ufungaji wa viti vya vyoo na sinki pamoja na uchoraji wa majengo.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya, alisema kuwa mpango huo unaonyesha imani ya muda mrefu ya benki kwamba jamii huimarika pale taasisi na watu binafsi wanapowekeza pamoja katika suluhisho za vitendo zinazoboresha maisha.

Katika Absa, tunaamini kuwa ‘Stori yako ina Thamani’, na leo tunakumbushwa kuwa hadithi za kina mama, watoto, familia na wahudumu wa afya zina umuhimu mkubwa. Ukarabati huu ni utekelezaji wa dhana yetu ya ‘Kuwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, Hatua Moja baada ya nyingine’. Pia unaonyesha utamaduni tunaoujenga Absa, ambapo watu wetu wanachukua jukumu la kubaini mahitaji ya jamii, kuhamasisha msaada na kushirikiana na benki kuleta mabadiliko endelevu.

Aliongeza kuwa mradi huo unaakisi ajenda pana ya uwajibikaji wa kijamii na uendelevu ya Absa, kwa kusaidia kuboresha mazingira ya huduma kwa heshima na ustahiki kwa wanawake na watoto, sambamba na kuimarisha mchango wa benki katika ustawi wa jamii.

Huu ni mfano halisi wa namna Absa inavyokuwa nguvu chanya katika jamii. Kwa kuboresha wodi ya Mama na Mtoto, tunawaunga mkono wahudumu wa afya wanaohudumia jamii kila siku, na pia kuboresha uzoefu wa huduma kwa kina mama na watoto. Tunaamini uwekezaji wa pamoja wa aina hii ni muhimu katika kujenga jamii imara na yenye afya.

Mpango huo uliwakutanisha wafanyakazi wa Absa kutoka idara mbalimbali, ukiakisi utamaduni wa ndani wa taasisi hiyo unaowahamasisha wafanyakazi kushiriki kikamilifu katika miradi ya maendeleo ya jamii, huku benki ikiongeza nguvu katika jitihada zao ili kuongeza athari chanya.

Mfumo huu wa utoaji unaoongozwa na wafanyakazi pamoja na msaada wa taasisi, umeendelea kuwa sehemu ya mkakati mpana wa Benki ya Absa Tanzania katika uwajibikaji kwa jamii, unaojikita katika ushirikiano, ujumuishi na uundaji wa thamani ya muda mrefu kwa jamii.

Hatua hiyo ya makabidhiano pia inaendana na lengo la Absa ya “Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, Hatua Moja baada ya nyingine” pamoja na ahadi yake ya chapa ya “Stori yako ina Thamani”, ambayo ni msingi wa namna benki hiyo inavyotoa thamani kwa wateja, jamii na wadau wake.

Kupitia uboreshaji wa mazingira katika sekta muhimu ya afya, Benkiy a Absa Tanzania inalenga kuchangia katika kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto, huku ikiimarisha umuhimu wa ushirikiano wa pamoja katika kutatua changamoto za jamii.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya (katikati), akikata utepe kuashiria makabidhiano rasmi ya Wodi ya Wazazi ya Hosptali ya Rufaa ya Mkoa Temeke, iliyofanyiwa ukarabati na Benki ya Absa. Hafla hiyo, ilifanyika hospitalini hapo, Temeke, Dar es Salaam leo. Kulia ni na Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Mfaume Kibwana na kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga.
Mkuu wa Udhibiti ya Udhibiti Ubora wa, Bw. Hosptali ya Rufaa ya Mkoa Temeke, Dk. Selemani Kivoja, akisalimiana na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Patrick Foya (kushoto), huku Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Mfaume Kibwana (kushoto), akiangalia, katika hafla ambayo beni hiyo ilikabidhi jengo la wodi ya wazazi lililokarabatiwa na benki hiyo, katika hafla hiyo ilifanyika hospitalini hapo, Temeke, Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Aron Luhanga.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Absa Tanzania wakiongozwa na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu, Bw. Patrick Foya, pamoja na watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke, wakipiga picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa hafla ya makabidhiano ya Wodi ya Wazazi iliyofanyiwa ukarabati na benki hiyo.
Share:

Sunday, March 29, 2026

BENKI YA ABSA YAENDELEA KUWAWEZESHA WANAWAKE WAJASIRIMALI KIUCHUMI

Meneja Bidhaa wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bryton Kimemeta (kushoto), akizungumza na baadhi ya wanawake wajasiriamali, wanachama wa Taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, katika semina iliyoandaliwa na taasisi hiyo kwa uwezeshaji wa benki hiyo ikihusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo hayo ni sehemu ya mikakati ya Benki ya Absa ya kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la benki hiyo la Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine, kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Meneja Msaidizi wa Uhakiki wa Biashara wa Benki ya Absa Tanzania. Bi. Miriam Ngajilo (kushoto), akizungumza na baadhi ya wanawake wajasiriamali, wanachama wa Taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, katika semina iliyoandaliwa na taasisi hiyo kwa uwezeshaji wa benki hiyo ikihusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo haya ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo ya kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la Benki ya Absa la Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine, kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, Bw. Hafizur Milon (kushoto), akizungumza kuhusu mahusiano ya kibiashara kati ya taasisi hiyo na Benki ya Absa Tanzania, wakati wa semina ya wanawake wajasiriamali wanachama wa taasisi hiyo kuhusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo haya ni sehemu ya mikakati ya Benki ya Absa katika kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la benki hiyo la 'Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine', kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Mtaalamu wa Mafunzo wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Hussein Said (kulia), akizungumza na baadhi ya wanawake wajasiriamali, wanachama wa Taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, katika semina iliyoandaliwa na taasisi hiyo kwa uwezeshaji wa benki hiyo ikihusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo haya ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo ya kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la Benki ya Absa la Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine, kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Mmoja wa wanawake wajasiariamali mwanachama wa Taasisi ya huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, Amina Makongoro akichangia hoja wakati wa semina kuhusu elimu ya kifedha na usimamizi wa biashara wenye tija, iliyoandaliwa na taasisi hiyo ikiwezeshwa na Benki ya Absa Tanzania, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo haya ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo katika kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la benki hiyo la 'Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine', kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Baadhi ya wanawake wajasiriamali wanachama wa Taasisi ya huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, wakisikiliza, wakati Meneja Bidhaa wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Bryton Kimemeta, akizungumza nao wakati wa semina kuhusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, iliyoandaliwa na Taasisi ya ASA Microfinance Tanzania kwa uwezeshaji wa benki hiyo, jijini Dar es Salaam jana. Semina hiyo ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo katika kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la benki hiyo la 'Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine', kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Share:

Friday, March 27, 2026

MRADI WA COOKFUND WALETA MAGEUZI YA MATUMIZI YA NISHATI KATIKA TAASISI ZA UMMA

Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika, akizungumza wakati wa makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama kwa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na usimamizi wa programu ukifanywa na Mfuko wa Maendeleo wa Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), inatekeleza Programu ya CookFund ili kuharakisha mpito wa matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kaya na taasisi za umma, hususan mashuleni. Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (wa pili kutoka kulia), alikuwa mgeni rasmi.

Dar es Salaam, Tanzania | Zaidi ya wanafunzi 62,000 kote Tanzania sasa wananufaika na majiko salama na safi zaidi kufuatia usakinishaji wa zaidi ya majiko ya kisasa 170 ya nishati safi ya kupikia katika shule na taasisi za umma zaidi ya 45. Hatua hii muhimu iliadhimishwa katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam, ikionesha mchango wa mpango huu katika kupunguza matumizi ya kuni na mkaa na hivyo kukabiliana na ukataji wa miti.

Mpango huu unafadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) na kutekelezwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) kupitia programu ya CookFund.

Akizungumza katika hafla hiyo, Naibu Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Salome Makamba alisema:

Mapinduzi haya kuelekea matumizi ya nishati safi ya kupikia ni kipaumbele cha kimkakati cha taifa kinachochangia kulinda mazingira, kuboresha afya ya umma na kuongeza ufanisi wa kiuchumi. Kwa kuzipatia shule na taasisi za umma teknolojia za kisasa za kupikia, tunalenga kulinda misitu yetu, kupunguza hewa chafuzi, na kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wetu. Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo kupanua upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa kuzingatia Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia (2024–2034).

Jitihada za nishati safi ya kupikia nchini zinaongozwa na Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na wizara na taasisi nyingine za Serikali, ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Maliasili na Utalii, Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, pamoja na taasisi nyingine za umma. Hadi sasa, msaada huu kwa taasisi za umma, hususan shule, unalenga taasisi zote zinazohudumia watu zaidi ya 100 kwa wakati mmoja ili kuachana na matumizi ya kuni na mkaa.

Hatua hizi zinaendana na vipaumbele vya kitaifa vya kupunguza ukataji wa miti, kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi, na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za umma. Matumizi ya kuni na mkaa huzalisha chembechembe hatarishi zinazoweza kusababisha magonjwa mbalimbali ya mfumo wa upumuaji kama pumu na saratani ya mapafu.

Kupitia programu ya CookFund, inayofadhiliwa na Umoja wa Ulaya, hatua hizi zinalenga kupunguza matumizi ya nishati za kuni na mkaa kwenda kwenye teknolojia bora na zenye ufanisi zaidi kama majiko yanayotumia mkaa mbadala, majiko ya umeme (electric pressure cookers), biyoethano, majiko banifu, pamoja na gesi. Teknolojia hizi zinatarajiwa kupunguza shinikizo kwa rasilimali za misitu, kuboresha ubora wa hewa jikoni, na kuongeza afya na usalama wa wanafunzi na watumishi. Hadi sasa, taasisi 45 zimeboresha mifumo yao ya upishi, nyingi zikiwa ni shule za msingi na sekondari.

Aidha, kupitia CookFund, UNCDF inatoa msaada wa kifedha na kiufundi kwa makampuni na wajasiriamali wanaokidhi vigezo ili kuongeza usambazaji wa nishati safi ya kupikia. Msaada huu unajumuisha uwekezaji wa mtaji na mtaji wa uendeshaji kwa ajili ya kuimarisha uwezo wa biashara zinazojihusisha na uzalishaji, uagizaji, usambazaji na uuzaji wa majiko, mafuta na bidhaa au huduma zinazohusiana na nishati safi ya kupikia.

Kwa upande wake, Mkuu wa Ushirikiano wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, Marc Stalmans, alisema:

Umoja wa Ulaya umejikita kikamilifu katika kuendeleza hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi duniani, na Tanzania siyo tofauti. Mpango huu ni sehemu ya juhudi zetu za kusaidia mpito kuelekea nishati safi. Kupitia msaada wa Umoja wa Ulaya, jamii zinazingatia mbinu endelevu zinazolinda mazingira, huku zikichochea ukuaji wa uchumi, kukuza ajira, na kuboresha upatikanaji wa nishati mashuleni, kwenye biashara pamoja na kaya.

Naye Mshauri Mkuu Maswala Kiufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika, alibainisha kuwa pamoja na msaada uliotolewa kwa taasisi 45 katika wilaya 14 za Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Dodoma na Mwanza, programu hiyo imewekeza dola milioni 10.1 katika biashara ndogo na za kati 102.

Nishati safi ya kupikia inapunguza utegemezi wa kuni na mkaa huku ikiboresha usalama, afya na ufanisi wa majiko shuleni,” alisema Bw. Malika. “CookFund inaonesha wazi kuwa teknolojia za kisasa za nishati zinaweza kuleta mageuzi makubwa katika taasisi za umma na kuboresha moja kwa moja mazingira ya kujifunzia kwa maelfu ya wanafunzi.

Kwa ujumla, programu hii imeleta matokeo chanya na yenye mageuzi makubwa, ikichangia uundaji wa ajira 27,005 (za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja), jumla ya biashara 4,933 katika mnyororo wa thamani wa nishati safi ya kupikia, kufikia kaya zaidi ya 482,089, na kupunguza zaidi ya tani 3,911,450 za uzalishaji wa hewa ukaa. Mafanikio haya yanaonesha mchango mkubwa wa programu hii katika maendeleo endelevu, ustawi wa jamii na hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi nchini Tanzania.
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, akitoa hotuba yake wakati wa makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama kwa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na usimamizi wa programu ukifanywa na Mfuko wa Maendeleo wa Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), inatekeleza Programu ya CookFund ili kuharakisha kipindi cha mpito wa matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kaya na taasisi za umma, hususan mashuleni.
Mkuu wa Ushirikiano wa Ujumbe wa EU nchini Tanzania, Bw. Marc Stalmans, akihutubia hadhira wakati wa makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama kwa Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na usimamizi wa programu ukifanywa na Mfuko wa Maendeleo wa Mitaji wa Umoja wa Mataifa (UNCDF), inatekeleza Programu ya CookFund ili kuharakisha kipindi cha mpito wa matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kaya na taasisi za umma, hususan shule. Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (wa tatu kutoka kulia), alikuwa mgeni rasmi.
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (kushoto), anapika wali akitumia jiko linalotumia nishati salama ya kupikia, wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa vya teknolojia ya upishi salama katika Shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam jana. Serikali ya Tanzania, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU) kupitia Ujumbe wake nchini, na kwa usimamizi wa programu kutoka Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuendeleza Mitaji (UNCDF), inatekeleza Mpango wa CookFund ili kuharakisha kipindi cha mpito cha matumizi ya upishi safi katika kaya na taasisi za umma, hususan mashuleni. Kutoka kulia ni Bw. Marc Stalmans, Mkuu wa Ushirikiano wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Tanzania, akiwa pamoja na Mshauri Mkuu wa Kiufundi wa UNCDF, Bw. Peter Malika.
Share:

AKIBA COMMERCIAL BANK PARTNERS WITH HANS PAUL AUTOMECH TO BOOST TANZANIA’S TOURISM SECTOR

IMG_9175Tanzania’s tourism sector remains a cornerstone of the national economy, supporting livelihoods, foreign exchange earnings, and regional development. As the industry continues to expand, empowering its key players with practical, scalable solutions is essential for sustaining long-term growth.

In a strategic move aligned with this vision, Akiba Commercial Bank Plc has partnered with Hans Paul Automech to address one of the sector’s most pressing challenges: access to reliable safari vehicles.

A Practical Solution to a Critical Industry Need

The collaboration, formalized through a Memorandum of Understanding (MoU), is designed to enable tour operators to acquire high-quality, durable, and purpose-built safari vehicles—an essential asset for delivering consistent and competitive tourism experiences.

IMG_9168

Speaking during the signing ceremony, Allen Nkya, Senior Manager for Business Banking, emphasized the bank’s strategic intent:

This partnership reflects our deliberate effort to support the tourism sector by providing tailored financial solutions that enable operators to acquire strong, durable and reliable safari vehicles. Through this arrangement, Akiba Commercial Bank will finance up to 80% of the vehicle cost, with customers contributing only 20%.”

Financing Designed Around the Tourism Cycle

A standout feature of this initiative is its flexibility. Unlike conventional financing models, this structure is tailored to the unique dynamics of the tourism industry, where revenue streams fluctuate between peak and low seasons.

By aligning repayment terms with actual cash flows, the partnership allows tour operators to invest in quality assets without placing undue pressure on their financial stability—ultimately supporting more sustainable business growth.

Addressing Longstanding Operational Challenges

With over two decades of experience in the automotive sector, Satbir, CEO of Hans Paul Automech, highlighted a persistent industry constraint:

The lack of strong and durable safari vehicles has significantly impacted many operators, as constant repairs consume both capital and profits. This partnership offers a practical and sustainable solution to this longstanding challenge.”

For years, many operators have relied on second-hand vehicles, often resulting in frequent breakdowns, rising maintenance costs, and reduced profitability. By facilitating access to reliable, high-performance safari vehicles, this partnership directly addresses that gap.

Strong Industry Backing

The initiative has been positively received across the tourism ecosystem. Sam Diah, Chairman of the Tanzania Local Tour Operators (TLTO), welcomed the collaboration as both timely and impactful, underscoring its potential to strengthen operational efficiency across the sector.

At the operational level, Gilbert Minja, Arusha Branch Manager, reaffirmed the bank’s commitment to delivering a seamless customer experience:

We are committed to ensuring a seamless process for our customers, from understanding the financing arrangements to accessing the facility within the shortest time possible.”

Driving Impact Through Collaboration

The signing event brought together key stakeholders, customers, and industry partners, all united by a shared goal: strengthening Tanzania’s tourism sector through innovation, collaboration, and practical financial solutions.

As Akiba Commercial Bank Plc continues to evolve its product offering, initiatives like this demonstrate a clear commitment to addressing real market needs. By bridging the gap between financing and operational requirements, the bank is not only supporting individual businesses but also contributing to the broader resilience and competitiveness of Tanzania’s tourism industry.

IMG_9185
Share:

Sunday, March 22, 2026

WAKULIMA KARATU KUNUFAIKA NA MAPINDUZI YA KIDIJITALI KUPITIA MIXX BY YAS

Meneja wa Mahusiano ya Biashara na Serikali wa Mixx by Yas, Suleiman Asilia (wa tatu kushoto), na Meneja wa Kibiashara Kanda ya Kaskazini wa Mixx by Yas, Eric Sosteness (kushoto kwake), pamoja na Kaimu Mkuu wa COPRA Kanda ya Kaskazini, Famia Amiri, wakimkabidhi runinga janja (Smart TV) Mwenyekiti wa ACU, Shedrack Asseri (mwenye koti jeusi), kwa ajili ya urushaji wa moja kwa moja wa minada ya mazao ya kilimo ili kuongeza uwazi na ushiriki wakati wa msimu wa mazao mbalimbali, ikiwemo ufuta.

Arusha - Wakulima wa Wilaya ya Karatu wanatarajiwa kunufaika kwa kiasi kikubwa na upatikanaji bora wa taarifa za masoko pamoja na kuongezeka kwa uwazi katika biashara ya mazao, kufuatia kuanzishwa kwa mpango wa kidijitali unaoongozwa na Mixx by Yas kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya kilimo.

Mpango huo ulizinduliwa rasmi kupitia hafla ya makabidhiano ya runinga janja (Smart TV) iliyotolewa kwa Chama Kikuu cha Ushirika Arusha (ACU) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA). Hatua hii inalenga kuboresha upatikanaji wa taarifa muhimu za masoko kwa wakulima na kuongeza ushiriki wao katika mifumo rasmi ya biashara.

Akizungumza katika hafla hiyo, Meneja wa Kibiashara Kanda ya Kaskazini wa Mixx by YasEric Sosteness, alisema kuwa suluhisho za kidijitali zinatoa fursa mpya kwa wakulima kufikia masoko kwa urahisi zaidi.

Kupitia Mixx by Yas, tumejikita kuwawezesha wakulima kwa kuwapatia suluhisho zinazowaleta karibu zaidi na masoko. Upatikanaji wa taarifa za mnada kwa wakati utawasaidia wakulima kufanya maamuzi sahihi na kuongeza kipato chao,” alisema.

Runinga hiyo janja inatarajiwa kuwa chombo muhimu katika kurusha moja kwa moja minada ya mazao ya kilimo. Kupitia teknolojia hiyo, wakulima wa Karatu na maeneo jirani wataweza kufuatilia mwenendo wa bei na shughuli za biashara bila kulazimika kuwepo katika eneo la mnada. Hatua hii inatarajiwa kuongeza uwazi, kupunguza upotoshaji wa taarifa, na kuimarisha ushindani wa haki katika soko.

Kwa upande wake, Meneja wa Mahusiano ya Biashara na Serikali wa Mixx by YasSuleiman Asilia, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya sekta binafsi na taasisi za umma katika kuleta mageuzi ya kiuchumi kwa wakulima.

Ushirikiano huu unaonesha jinsi teknolojia na ubia vinavyoweza kufungua fursa mpya kwa wakulima. Lengo letu ni kuhakikisha wakulima wanaunganishwa zaidi, wanapata taarifa sahihi na wanajumuishwa kifedha,” alieleza.

Naye Kaimu Mkuu wa COPRA Kanda ya Kaskazini, Famia Amiri, alibainisha kuwa urushaji wa moja kwa moja wa minada utaongeza uwazi na kujenga imani katika mfumo wa biashara ya mazao, hususan katika kipindi hiki ambacho nchi inaelekea msimu wa ufuta.

Mbali na mpango huo, Mixx by Yas inaendelea kutoa huduma mbalimbali zinazolenga kumwezesha mkulima, ikiwemo Mixx Kilimo inayorahisisha miamala, Afya Mkulima inayolenga ustawi wa wakulima, pamoja na Kilimo Pesa inayowezesha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa urahisi zaidi.

Kwa ujumla, mpango huu unaakisi mwelekeo wa sekta ya kilimo nchini kuelekea matumizi makubwa ya teknolojia katika kuboresha mifumo ya biashara. Kadri suluhisho hizi zinavyozidi kuenea, zinatarajiwa kuongeza tija, kuimarisha kipato cha wakulima, na kuwapa nafasi kubwa zaidi katika uchumi wa kisasa unaozidi kuwa wa kidijitali.

Share:

Thursday, March 19, 2026

TCB BANK YANZINDUA KAMPENI YA KUCHOCHEA UCHUMI NA KUWEZESHA NDOTO ZA WATANZANIA

Dar es Salaam, Tanzania – Tanzania Commercial Bank (TCB Bank) imezindua kampeni maalum inayolenga kuwawezesha Watanzania kufikia ndoto zao kupitia suluhisho bunifu za kifedha, hatua inayotarajiwa kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha ustawi wa jamii.

Kampeni hiyo inalenga kupanua upatikanaji wa huduma za kifedha kwa makundi mbalimbali ya wananchi, hususan wajasiriamali, wakulima pamoja na biashara ndogo na za kati (SMEs). Lengo kuu ni kuongeza uzalishaji, kukuza biashara na kuimarisha fursa za ajira nchini.

Kukuza Ushirikiano na Wateja

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Jema Msuya, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa TCB Bank, alisema benki hiyo imejipanga kuwa mshirika wa maendeleo kwa wateja wake kwa kutoa huduma zinazokidhi mahitaji yao halisi.

Tunataka kuwa karibu na wateja wetu na kuhakikisha kila Mtanzania anapata msaada wa kifedha unaomwezesha kufikia ndoto zake,” alisema.

 

Kwa upande wake, Alex Dwashi, Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, alieleza kuwa kampeni hiyo inalenga kujenga uhusiano wa karibu zaidi na wateja kwa kuelewa changamoto zao na kutoa suluhisho mahsusi.

Kampeni hii inalenga kugusa maisha ya Watanzania moja kwa moja kwa kuwaunga mkono katika safari ya kukuza shughuli zao za kiuchumi,” alisisitiza.

Kuwafikia Wateja Moja kwa Moja

Naye Al-Amin Lwano, Meneja Mwandamizi wa TCB Bank, alisema benki hiyo imejipanga kuwafikia wajasiriamali moja kwa moja katika maeneo yao ya biashara.

Alieleza kuwa kupitia mkakati huo, benki itatoa mikopo na huduma nyingine za kifedha zitakazosaidia kuongeza mtaji, kuboresha uzalishaji na kuimarisha ushindani wa biashara.

Tutaenda karibu na wafanyabiashara ili kuwasaidia kukuza biashara zao na kuchochea uchumi wa nchi,” alisema.

Msukumo kwa Uchumi Endelevu

Hatua hiyo inaonyesha dhamira ya Tanzania Commercial Bank (TCB Bank) katika kuchangia maendeleo ya uchumi jumuishi kwa kuwezesha wananchi kifedha. Uwezeshaji kupitia sekta ya fedha unaendelea kuwa nguzo muhimu katika kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja, kukuza ajira na kuimarisha maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Kwa ujumla, kampeni hii inaashiria mwelekeo mpya wa benki hiyo katika kujenga uchumi shirikishi unaoweka kipaumbele kwa mahitaji ya Watanzania na kusaidia kufungua fursa zaidi za kiuchumi nchini.



Share:

Wednesday, March 18, 2026

MBUNGE WA SEGEREA AWAKUMBUKA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU WAKUSIKIA BUGURUNI.

Mbunge wa Jimbo la Segerea, Agnesta Lambert (CHAUMA), ameendeleza juhudi zake za kuimarisha ustawi wa makundi maalum kwa kuwafikia watoto wenye ulemavu wa kusikia katika Shule ya Msingi ya Viziwi Buguruni, jijini Dar es Salaam ambapo amekabidhi msaada wa vyakula pamoja na mahitaji mengine muhimu, kwa lengo la kuwawezesha watoto hao kusherehekea kwa heshima na furaha sikukuu za Idd el-Fitr na Pasaka.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mbunge huyo ameeleza kuwa anahisi kuwajibika kusimamia masuala ya kijamii, hususan yanayohusu watoto wenye mahitaji maalum na kusisitiza kuwa uwekezaji katika ustawi na elimu ya watoto hao ni msingi muhimu wa kujenga jamii jumuishi na yenye usawa wa fursa.

‎Amebaini changamoto kubwa inayoikabili shule hiyo, ni upungufu wa mabweni kwa wanafunzi hao na kuahidi kufikisha suala hilo bungeni na kuongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka kipaumbele katika sekta ya elimu, na hivyo ana imani kuwa changamoto zilizopo zitapatiwa ufumbuzi.

Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule hiyo ameeleza kuwa uhaba wa mabweni unawaweka watoto hao katika hatari, ikiwemo uwezekano wa kupata ajali kutokana na mazingira yasiyo rafiki kwa hali yao.


‎Wanafunzi hao wakatoa wito kwa jamii na wadau mbalimbali kuendelea kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum, wakisisitiza umuhimu wa mshikamano wa kijamii katika kujenga mustakabali bora kwa wote.

Share:

ABSA BANK HIGHLIGHTS COMMITMENT TO WOMEN’S EMPOWERMENT

Absa Bank Tanzania Chief Information Officer, Mr. Emmanuel Mwinuka, delivered a keynote address at the Accelerate Women Executive Summit held recently in Dar es Salaam. Sponsored by Absa Bank, the summit brought together women leaders to explore how technology, leadership, and inclusion are shaping the future of the nation.
Absa Bank Tanzania Citizenship and Events Manager, Ms. Abigail Lukuvi (second from right), receives a sponsorship appreciation certificate from Acceleration Foundation Executive Director, Ms. Bernice Fernandos, during the Accelerate Women Executive Summit held recently in Dar es Salaam. Sponsored by Absa Bank, the summit brought together women leaders to explore how technology, leadership, and inclusion are shaping the nation’s future. Looking on from the left are Absa’s Project Portfolio Manager, Ms. Munira Chambuso, Chief Information Officer, Mr. Emmanuel Mwinuka, and Accounts & Merchants Authoriser, Ms. Cygrade Othman.
Absa Bank Tanzania Chief Information Officer, Mr. Emmanuel Mwinuka (centre), and Absa’s Project Portfolio Manager, Ms. Munira Chambuso (left), listen to Dar es Salaam businesswoman and MeTL Group Marketing Director, Ms. Fatema Dewji, during the Accelerate Women Executive Summit held recently in Dar es Salaam. Sponsored by Absa Bank, the summit convened women leaders to discuss how technology, leadership, and inclusion are shaping the nation’s future.
Absa Bank SME Banker, Mr. Thamrat Khamis (left), engages with a visitor during the Accelerate Women Executive Summit held recently in Dar es Salaam. Sponsored by Absa Bank, the summit brought together women leaders to examine how technology, leadership, and inclusion are driving the nation’s future.
The jubilant Absa Bank Tanzania team, led by Chief Information Officer, Mr. Emmanuel Mwinuka (second from left), poses for a commemorative photograph following the Accelerate Women Executive Summit held recently in Dar es Salaam. Sponsored by Absa Bank, the summit united women leaders to explore how technology, leadership, and inclusion are shaping the nation’s future.
Share:

Monday, March 16, 2026

ABSA BANK TANZANIA STRENGTHENS TIES WITH CLIENTS

 

Absa Bank Tanzania Managing Director, Mr. Obedi Laiser (left), Dar es Salaam Regional Sheikh, Walid Alhad Omar, and other guests serve iftar dinner during an event hosted by the bank for its clients in Dar es Salaam recently.
Dar es Salaam Regional Sheikh, Walid Alhad Omar (right), is welcomed by Absa Bank Tanzania Managing Director, Mr. Obedi Laiser, at the iftar dinner hosted by the bank for its clients in Dar es Salaam recently. Looking on (center) is Absa Bank Financial Controller, Mr. Muhsin Kaye.
Absa Bank Tanzania Retail Banking Director, Ms. Ndabu Swere (third left), together with staff members and other guests, serve iftar dinner during an event hosted by the bank for its clients in Dar es Salaam recently.
Absa Bank Tanzania Managing Director, Mr. Obedi Laiser, addresses clients and guests during the iftar dinner hosted by the bank in Dar es Salaam recently.
Dar es Salaam Regional Sheikh, Walid Alhad Omar, addresses the gathering during the iftar dinner hosted by Absa Bank Tanzania for its clients in Dar es Salaam recently.
Dar es Salaam Regional Sheikh, Walid Alhad Omar (center), Absa Bank Tanzania Managing Director, Mr. Obedi Laiser (second left), and some of the bank’s directors pose for a group photograph after the iftar dinner hosted by the bank for its clients in Dar es Salaam recently.
Absa Bank Tanzania Financial Controller, Mr. Muhsin Kashe (left), bids farewell to Dar es Salaam Regional Sheikh, Walid Alhad Omar, while the bank’s Managing Director, Mr. Obedi Laiser, looks on after the iftar dinner hosted by the bank for its clients in Dar es Salaam recently.
Share:

Sunday, March 15, 2026

JIONI YA BARAKA FAMILIA YA OYA YASHIRIKI IFTAR NA JAMII

  Taasisi ya Oya Micro-crediti imeandaa futari maalum kwa wateja wake na jamii kwa ujumla tukio lililolenga kuimarisha mshikamano wa kijamii.

Watoto kutoka kituo cha kulelea watoto mayatima kinondoni,wakitabasam kufurahia iftar iliyoandaliwa na taasisi ya  Oya Micro-Credit ikiwa nikurudisha kwa jamii hasa katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani na Kwaresma


Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni wakati wa kutafakari, kushukuru, na kushirikiana na jamii katika kujitoa kwenye mambo mablimbali. Kwetu OYA, tunaamini kuwa mafanikio ya kweli hayapimwi tu kwa ukuaji wa biashara, bali pia kwa mchango chanya tunaoutoa kwa jamii inayotuzunguka.


Oya Micro-crediti tulipata heshima ya kuandaa Iftar dinner maalum iliyowaleta pamoja watumishi wetu, baadhi ya wateja na wageni maalum katika mazingira ya mshikamano na furaha.


Moja ya sehemu iliyogusa mioyo ya wengi ilikuwa uwepo wa watoto wazuri kutoka kituo cha kulelea watoto yatima kilichopo Kinondoni watoto hao walionesha Tabasamu lao lililota furaha kubwa na kutukumbusha maana halisi ya  ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan — huruma, upendo, na kushirikiana.

Haikua tu hafla ya kufuturu pamoja, bali pia ya kuimarisha mahusiano, kujenga mshikamano wa kijamii, na kueneza matumaini matukio kama haya yanatukumbusha kuwa hata matendo madogo ya wema yanaweza kuleta furaha kubwa kwa wengine.

Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kila mmoja aliyeshiriki na kuchangia kufanya siku hii iwe ya kipekee kadri mwezi wa Ramadhan unavyoendelea, OYA itaendelea kujitahidi kushirikiana na jamii na kuendeleza maadili ya umoja, huruma, na kusaidiana.


Kwa niaba ya familia nzima ya OYA, tunawatakia wote Ramadhan yenye baraka na amani. Alisema Mkurugenzi wa OYA Bwana. Alpha Peter



Ramadan Kareem. 🌙

Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive