


.jpeg)


A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.
CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.
TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.
THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.
BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week



.jpeg)


DAR ES SALAAM: Benki ya DCB imezindua kampeni maalum ya miezi sita ijulikanayo kama "Tuma Bure, Shinda Kila Wiki", inayolenga kuhamasisha matumizi ya huduma za kidijitali na kuongeza ujumuishaji wa huduma za kifedha nchini kwa kuwapatia wateja nafasi ya kushinda zawadi mbalimbali huku wakifanya miamala bila kutozwa gharama.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Sabasaba Moshingi, amesema benki hiyo imefanya maboresho makubwa ya huduma zake za kidijitali baada ya kubaini kuwa wateja wengi wanahitaji huduma za haraka, salama, nafuu na zinazopatikana muda wote. Amesema kupitia mfumo mpya wa DCB Pesa App, wateja wanaweza kufungua akaunti popote walipo nchini na kufanya miamala mbalimbali bila makato.
Moshingi amesema kampeni hiyo pia inalenga kuunga mkono juhudi za Serikali za kuongeza ushiriki wa wananchi katika huduma rasmi za kifedha, huku akiwahimiza Watanzania kutumia huduma za benki ili kukuza biashara zao na kufikia malengo ya kiuchumi kwa urahisi zaidi.
Kwa upande wake, Mkuu wa Idara ya Masoko wa DCB, Geofrey Magugi, amesema mteja anayefungua akaunti kupitia DCB Pesa App na kufanya angalau muamala mmoja ataingia kwenye droo ya kila wiki yenye zawadi ya Shilingi 100,000 kwa washindi 10,amesema wateja watakaofanya miamala zaidi ya mitatu kwa mwezi watapata nafasi ya kushinda zawadi kubwa zaidi ikiwemo Shilingi milioni moja kila mwezi.
Naye Mkurugenzi wa Biashara wa DCB, Ramadhani Mganga, amesema kampeni hiyo itadumu hadi Desemba mwaka huu na inalenga kuwazawadia wateja wanaotumia huduma za benki kwa njia za kidijitali, amesema DCB imeendelea kuwa miongoni mwa taasisi za fedha zinazoweka kipaumbele katika ubunifu wa huduma nafuu, huku ikitoa fursa kwa Watanzania kufungua akaunti na kufanya miamala kutoka mahali popote nchini bila kulazimika kutembelea matawi ya benki.
Mganga amesema pamoja na faida ya kutuma fedha bila makato, wateja watakaoshiriki kampeni hiyo watakuwa na nafasi ya kushinda zawadi za kila wiki, kila mwezi na zawadi kubwa itakayotolewa mwishoni mwa kampeni mwezi Desemba, akiwataka Watanzania kuchangamkia fursa hiyo kwa kufungua akaunti za DCB na kutumia huduma zake za kidijitali.
Msimu wa saba wa TCB Selous Marathon umeweka rekodi mpya baada ya kuvutia zaidi ya washiriki 10,000, jambo lililoifanya kuwa mojawapo ya matukio makubwa zaidi ya michezo mkoani Morogoro.
Akizungumza kuhusu mafanikio hayo, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma, amesema tukio hilo linaunga mkono juhudi za Serikali za kuhamasisha mazoezi, kuimarisha afya za wananchi na kuleta mshikamano wa kijamii.
Amesema marathon hiyo imeendelea kukua kila mwaka na kutoa fursa kwa makundi yote ya jamii, ikiwemo watu wenye ulemavu, kushiriki katika shughuli za michezo na kujenga umoja wa Watanzania.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TCB, Adam Mihayo, amesema udhamini wa benki hiyo katika marathon hiyo unalenga kukuza afya, utalii, utunzaji wa mazingira na fursa za kiuchumi,amesema kupitia tukio hilo, TCB inalenga kutangaza Hifadhi ya Selous, kuunga mkono juhudi za upandaji miti ambapo miti 2,000 tayari imepandwa na mingine 8,000 itapandwa, sambamba na kuhamasisha matumizi ya mifumo ya malipo ya kidijitali.
Mihayo ameongeza kuwa zaidi ya washiriki 10,000 waliojitokeza wamechochea shughuli za kiuchumi mkoani Morogoro, huku sekta za hoteli, usafiri, biashara ndogo ndogo na huduma mbalimbali zikiongeza mapato kutokana na ongezeko la wageni,aidha, amesema marathon hiyo imesaidia kutangaza mradi wa reli ya kisasa ya SGR na vivutio vya utalii vya Tanzania kwa wageni kutoka ndani na nje ya nchi.
Kwa upande wao, washiriki wa marathon hiyo wameeleza kuwa mbio hizo si mashindano pekee bali ni sehemu ya kujenga afya na kuhamasisha maisha yenye mazoezi,wamesisitiza kuwa ushiriki wa wananchi katika matukio kama hayo unasaidia kupunguza magonjwa yasiyoambukiza na kuunga mkono juhudi za Serikali za kuboresha ustawi wa jamii,hukub TCB ikiahidi kuboresha zaidi maandalizi ya msimu ujao kufuatia mafanikio makubwa ya mwaka huu yaliyovuka matarajio.










President of Tanzania Pickleball Association and the East Africa Rackets Sports Club Chairman, Kartik Kapor, shakes hands with Absa Bank Tanzania Head of Large Corporates, Christopher Mgani (right), during the closing ceremony of the Tanzania Pickleball Open 2026, sponsored by the financial institution, at the Dar es Salaam Gymkhana Club.
Absa Bank Tanzania Head of Large Corporates, Christopher Mgani (left), presents awards to winners of the Tanzania Pickleball Open 2026 during the closing ceremony at the Dar es Salaam Gymkhana Club. The tournament was sponsored by Absa Bank..jpg)
Pickleball players in action during the finals of the Tanzania Pickleball Open 2026, sponsored by Absa Bank Tanzania, at the Dar es Salaam Gymkhana grounds.
A pickleball player showcases her skills during the finals of the Tanzania Pickleball Open 2026, sponsored by Absa Bank Tanzania, at the Dar es Salaam Gymkhana grounds.
Cheerful winners of the recently concluded Tanzania Pickleball Open 2026 pose during the closing ceremony at the Dar es Salaam Gymkhana Club. The tournament was sponsored by Absa Bank