Sunday, March 29, 2026
BENKI YA ABSA YAENDELEA KUWAWEZESHA WANAWAKE WAJASIRIMALI KIUCHUMI
Friday, March 27, 2026
MRADI WA COOKFUND WALETA MAGEUZI YA MATUMIZI YA NISHATI KATIKA TAASISI ZA UMMA


AKIBA COMMERCIAL BANK PARTNERS WITH HANS PAUL AUTOMECH TO BOOST TANZANIA’S TOURISM SECTOR
Tanzania’s tourism sector remains a cornerstone of the national economy, supporting livelihoods, foreign exchange earnings, and regional development. As the industry continues to expand, empowering its key players with practical, scalable solutions is essential for sustaining long-term growth.
In a strategic move aligned with this vision, Akiba Commercial Bank Plc has partnered with Hans Paul Automech to address one of the sector’s most pressing challenges: access to reliable safari vehicles.
A Practical Solution to a Critical Industry Need
The collaboration, formalized through a Memorandum of Understanding (MoU), is designed to enable tour operators to acquire high-quality, durable, and purpose-built safari vehicles—an essential asset for delivering consistent and competitive tourism experiences.
Speaking during the signing ceremony, Allen Nkya, Senior Manager for Business Banking, emphasized the bank’s strategic intent:
“This partnership reflects our deliberate effort to support the tourism sector by providing tailored financial solutions that enable operators to acquire strong, durable and reliable safari vehicles. Through this arrangement, Akiba Commercial Bank will finance up to 80% of the vehicle cost, with customers contributing only 20%.”
Financing Designed Around the Tourism Cycle
A standout feature of this initiative is its flexibility. Unlike conventional financing models, this structure is tailored to the unique dynamics of the tourism industry, where revenue streams fluctuate between peak and low seasons.
By aligning repayment terms with actual cash flows, the partnership allows tour operators to invest in quality assets without placing undue pressure on their financial stability—ultimately supporting more sustainable business growth.
Addressing Longstanding Operational Challenges
With over two decades of experience in the automotive sector, Satbir, CEO of Hans Paul Automech, highlighted a persistent industry constraint:
“The lack of strong and durable safari vehicles has significantly impacted many operators, as constant repairs consume both capital and profits. This partnership offers a practical and sustainable solution to this longstanding challenge.”
For years, many operators have relied on second-hand vehicles, often resulting in frequent breakdowns, rising maintenance costs, and reduced profitability. By facilitating access to reliable, high-performance safari vehicles, this partnership directly addresses that gap.
Strong Industry Backing
The initiative has been positively received across the tourism ecosystem. Sam Diah, Chairman of the Tanzania Local Tour Operators (TLTO), welcomed the collaboration as both timely and impactful, underscoring its potential to strengthen operational efficiency across the sector.
At the operational level, Gilbert Minja, Arusha Branch Manager, reaffirmed the bank’s commitment to delivering a seamless customer experience:
“We are committed to ensuring a seamless process for our customers, from understanding the financing arrangements to accessing the facility within the shortest time possible.”
Driving Impact Through Collaboration
The signing event brought together key stakeholders, customers, and industry partners, all united by a shared goal: strengthening Tanzania’s tourism sector through innovation, collaboration, and practical financial solutions.
As Akiba Commercial Bank Plc continues to evolve its product offering, initiatives like this demonstrate a clear commitment to addressing real market needs. By bridging the gap between financing and operational requirements, the bank is not only supporting individual businesses but also contributing to the broader resilience and competitiveness of Tanzania’s tourism industry.
Sunday, March 22, 2026
WAKULIMA KARATU KUNUFAIKA NA MAPINDUZI YA KIDIJITALI KUPITIA MIXX BY YAS
Arusha - Wakulima wa Wilaya ya Karatu wanatarajiwa kunufaika kwa kiasi kikubwa na upatikanaji bora wa taarifa za masoko pamoja na kuongezeka kwa uwazi katika biashara ya mazao, kufuatia kuanzishwa kwa mpango wa kidijitali unaoongozwa na Mixx by Yas kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya kilimo.
Mpango huo ulizinduliwa rasmi kupitia hafla ya makabidhiano ya runinga janja (Smart TV) iliyotolewa kwa Chama Kikuu cha Ushirika Arusha (ACU) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA). Hatua hii inalenga kuboresha upatikanaji wa taarifa muhimu za masoko kwa wakulima na kuongeza ushiriki wao katika mifumo rasmi ya biashara.
Akizungumza katika hafla hiyo, Meneja wa Kibiashara Kanda ya Kaskazini wa Mixx by Yas, Eric Sosteness, alisema kuwa suluhisho za kidijitali zinatoa fursa mpya kwa wakulima kufikia masoko kwa urahisi zaidi.
“Kupitia Mixx by Yas, tumejikita kuwawezesha wakulima kwa kuwapatia suluhisho zinazowaleta karibu zaidi na masoko. Upatikanaji wa taarifa za mnada kwa wakati utawasaidia wakulima kufanya maamuzi sahihi na kuongeza kipato chao,” alisema.
Runinga hiyo janja inatarajiwa kuwa chombo muhimu katika kurusha moja kwa moja minada ya mazao ya kilimo. Kupitia teknolojia hiyo, wakulima wa Karatu na maeneo jirani wataweza kufuatilia mwenendo wa bei na shughuli za biashara bila kulazimika kuwepo katika eneo la mnada. Hatua hii inatarajiwa kuongeza uwazi, kupunguza upotoshaji wa taarifa, na kuimarisha ushindani wa haki katika soko.
Kwa upande wake, Meneja wa Mahusiano ya Biashara na Serikali wa Mixx by Yas, Suleiman Asilia, alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya sekta binafsi na taasisi za umma katika kuleta mageuzi ya kiuchumi kwa wakulima.
Naye Kaimu Mkuu wa COPRA Kanda ya Kaskazini, Famia Amiri, alibainisha kuwa urushaji wa moja kwa moja wa minada utaongeza uwazi na kujenga imani katika mfumo wa biashara ya mazao, hususan katika kipindi hiki ambacho nchi inaelekea msimu wa ufuta.“Ushirikiano huu unaonesha jinsi teknolojia na ubia vinavyoweza kufungua fursa mpya kwa wakulima. Lengo letu ni kuhakikisha wakulima wanaunganishwa zaidi, wanapata taarifa sahihi na wanajumuishwa kifedha,” alieleza.
Mbali na mpango huo, Mixx by Yas inaendelea kutoa huduma mbalimbali zinazolenga kumwezesha mkulima, ikiwemo Mixx Kilimo inayorahisisha miamala, Afya Mkulima inayolenga ustawi wa wakulima, pamoja na Kilimo Pesa inayowezesha upatikanaji wa huduma za kifedha kwa urahisi zaidi.
Kwa ujumla, mpango huu unaakisi mwelekeo wa sekta ya kilimo nchini kuelekea matumizi makubwa ya teknolojia katika kuboresha mifumo ya biashara. Kadri suluhisho hizi zinavyozidi kuenea, zinatarajiwa kuongeza tija, kuimarisha kipato cha wakulima, na kuwapa nafasi kubwa zaidi katika uchumi wa kisasa unaozidi kuwa wa kidijitali.
Thursday, March 19, 2026
TCB BANK YANZINDUA KAMPENI YA KUCHOCHEA UCHUMI NA KUWEZESHA NDOTO ZA WATANZANIA
Dar es Salaam, Tanzania – Tanzania Commercial Bank (TCB Bank) imezindua kampeni maalum inayolenga kuwawezesha Watanzania kufikia ndoto zao kupitia suluhisho bunifu za kifedha, hatua inayotarajiwa kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha ustawi wa jamii.
Kampeni hiyo inalenga kupanua upatikanaji wa huduma za kifedha kwa makundi mbalimbali ya wananchi, hususan wajasiriamali, wakulima pamoja na biashara ndogo na za kati (SMEs). Lengo kuu ni kuongeza uzalishaji, kukuza biashara na kuimarisha fursa za ajira nchini.
Kukuza Ushirikiano na Wateja
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Jema Msuya, aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa TCB Bank, alisema benki hiyo imejipanga kuwa mshirika wa maendeleo kwa wateja wake kwa kutoa huduma zinazokidhi mahitaji yao halisi.
“Tunataka kuwa karibu na wateja wetu na kuhakikisha kila Mtanzania anapata msaada wa kifedha unaomwezesha kufikia ndoto zake,” alisema.
Kwa upande wake, Alex Dwashi, Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, alieleza kuwa kampeni hiyo inalenga kujenga uhusiano wa karibu zaidi na wateja kwa kuelewa changamoto zao na kutoa suluhisho mahsusi.
“Kampeni hii inalenga kugusa maisha ya Watanzania moja kwa moja kwa kuwaunga mkono katika safari ya kukuza shughuli zao za kiuchumi,” alisisitiza.
Kuwafikia Wateja Moja kwa Moja
Naye Al-Amin Lwano, Meneja Mwandamizi wa TCB Bank, alisema benki hiyo imejipanga kuwafikia wajasiriamali moja kwa moja katika maeneo yao ya biashara.
Alieleza kuwa kupitia mkakati huo, benki itatoa mikopo na huduma nyingine za kifedha zitakazosaidia kuongeza mtaji, kuboresha uzalishaji na kuimarisha ushindani wa biashara.
“Tutaenda karibu na wafanyabiashara ili kuwasaidia kukuza biashara zao na kuchochea uchumi wa nchi,” alisema.
Msukumo kwa Uchumi Endelevu
Hatua hiyo inaonyesha dhamira ya Tanzania Commercial Bank (TCB Bank) katika kuchangia maendeleo ya uchumi jumuishi kwa kuwezesha wananchi kifedha. Uwezeshaji kupitia sekta ya fedha unaendelea kuwa nguzo muhimu katika kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja, kukuza ajira na kuimarisha maendeleo ya taifa kwa ujumla.
Kwa ujumla, kampeni hii inaashiria mwelekeo mpya wa benki hiyo katika kujenga uchumi shirikishi unaoweka kipaumbele kwa mahitaji ya Watanzania na kusaidia kufungua fursa zaidi za kiuchumi nchini.
Wednesday, March 18, 2026
MBUNGE WA SEGEREA AWAKUMBUKA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU WAKUSIKIA BUGURUNI.
Mbunge wa Jimbo la Segerea, Agnesta Lambert (CHAUMA), ameendeleza juhudi zake za kuimarisha ustawi wa makundi maalum kwa kuwafikia watoto wenye ulemavu wa kusikia katika Shule ya Msingi ya Viziwi Buguruni, jijini Dar es Salaam ambapo amekabidhi msaada wa vyakula pamoja na mahitaji mengine muhimu, kwa lengo la kuwawezesha watoto hao kusherehekea kwa heshima na furaha sikukuu za Idd el-Fitr na Pasaka.
Amebaini changamoto kubwa inayoikabili shule hiyo, ni upungufu wa mabweni kwa wanafunzi hao na kuahidi kufikisha suala hilo bungeni na kuongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka kipaumbele katika sekta ya elimu, na hivyo ana imani kuwa changamoto zilizopo zitapatiwa ufumbuzi.
Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule hiyo ameeleza kuwa uhaba wa mabweni unawaweka watoto hao katika hatari, ikiwemo uwezekano wa kupata ajali kutokana na mazingira yasiyo rafiki kwa hali yao.
ABSA BANK HIGHLIGHTS COMMITMENT TO WOMEN’S EMPOWERMENT





Monday, March 16, 2026
ABSA BANK TANZANIA STRENGTHENS TIES WITH CLIENTS







Sunday, March 15, 2026
JIONI YA BARAKA FAMILIA YA OYA YASHIRIKI IFTAR NA JAMII
Taasisi ya Oya Micro-crediti imeandaa futari maalum kwa wateja wake na jamii kwa ujumla tukio lililolenga kuimarisha mshikamano wa kijamii.
Watoto kutoka kituo cha kulelea watoto mayatima kinondoni,wakitabasam kufurahia iftar iliyoandaliwa na taasisi ya Oya Micro-Credit ikiwa nikurudisha kwa jamii hasa katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani na Kwaresma
Mwezi Mtukufu wa Ramadhan ni wakati wa kutafakari, kushukuru, na kushirikiana na jamii katika kujitoa kwenye mambo mablimbali. Kwetu OYA, tunaamini kuwa mafanikio ya kweli hayapimwi tu kwa ukuaji wa biashara, bali pia kwa mchango chanya tunaoutoa kwa jamii inayotuzunguka.
Oya Micro-crediti tulipata heshima ya kuandaa Iftar dinner maalum iliyowaleta pamoja watumishi wetu, baadhi ya wateja na wageni maalum katika mazingira ya mshikamano na furaha.
Moja ya sehemu iliyogusa mioyo ya wengi ilikuwa uwepo wa watoto wazuri kutoka kituo cha kulelea watoto yatima kilichopo Kinondoni watoto hao walionesha Tabasamu lao lililota furaha kubwa na kutukumbusha maana halisi ya ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan — huruma, upendo, na kushirikiana.
Haikua tu hafla ya kufuturu pamoja, bali pia ya kuimarisha mahusiano, kujenga mshikamano wa kijamii, na kueneza matumaini matukio kama haya yanatukumbusha kuwa hata matendo madogo ya wema yanaweza kuleta furaha kubwa kwa wengine.Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kila mmoja aliyeshiriki na kuchangia kufanya siku hii iwe ya kipekee kadri mwezi wa Ramadhan unavyoendelea, OYA itaendelea kujitahidi kushirikiana na jamii na kuendeleza maadili ya umoja, huruma, na kusaidiana.
Kwa niaba ya familia nzima ya OYA, tunawatakia wote Ramadhan yenye baraka na amani. Alisema Mkurugenzi wa OYA Bwana. Alpha Peter
Ramadan Kareem. 🌙
Thursday, March 12, 2026
ABSA BANK TANZANIA TARGETS EQUIPPING 5,000 YOUNG WOMEN WITH AI SKILLS THROUGH ELEVATEHER INITIATIVE

Monday, March 9, 2026
ACI FMA Tanzania Hosts Iftar to Strengthen Financial Market Dialogue






.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)










