Saturday, July 20, 2024
MADEREVA BODABODA TANGA WASHUKURU JESHI LA POLISI KWA KUTOA ELIMU KUHUSU USALAMA BARABARANI.
Thursday, July 4, 2024
ORYX YAMPA UBALOZI SHILOLE KUHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA
Monday, July 1, 2024
Serikali ya Marekani Yashiriki Uzinduzi wa Ndondo Cup 2024, kupitia kampeni za SITETEREKI na FURAHA YANGU na CHANJO NI MAISHA
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhtfvoylyUlWkvMvq2UeFEZrFUWmXT45ottmPJwV2cd-s4_z7Grp5GIJOf9zMEPQNP5c83oopcgNKy-YDiHfAWkm825Gptf1stVguHgHiOjP8hz1I_l58-gHJ_RpV4mKk2chHunseHjbhNO0-ImlkCE1GbQ8XG84hrNu9WP_AzzQsyD4po87Vot7OwwbP6P/w640-h426/001%20(1).jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhwEpTlkpxuOfDxDZ75TGxMaXGb0PQjX1LhhIA8qvqW3DrP7g_6WvXpbCFuTtP81P9ciP2UYVQwoA0rlwdc_80v4CVCJb_Fb7R1g0tTzxv1_8Bu-iXlKBEqOwDd_L4hidjn6isWzsFklZ30LoFnC0Zq-d5L8w8pyZ3pMHCWSjsyW4ScmlEXvn4jo3eNmPqJ/w640-h396/005.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiT_Dihgvx8W9NJHvvVhZ52Ubi4BtFpU3oezcXMQds9ebTp8mEo7vcHJ8lf9ZID5Zq1FWSw5DnGXTE9VQBtMf8bEQ0QrcJeIMrMx96_mP5ebj_CH9Uo_0tXKw44qduBq0R0jh4RveOLvikRnJybMoVnQOmM1P-nIoqMvDhK-8G1vNswvNrR0PMIReAVdCzR/w640-h428/006.jpg)
Monday, June 24, 2024
ACI Financial Markets Association of Tanzania Strengthens Stakeholder Engagement and Collaboration
Sunday, June 16, 2024
WAZIRI WA AFYA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA KIDO BALOZI WA KAMPENI YA HOLELA-HOLELA ITAKUKOSTI
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgA6BkMpR3ku50E2SOzshu6T5E6sR1xrHhPqRC3HrPbXvdDq4EA-m5TEF5FUSx7bRfLp0EtDQeycjQX3Eky2rbiZz3mz_aHlUK6aSdKvKeaTXTy35QuEvY9I7tzYt0oRRbTAuphZJZ9vzatKinRzxjB2nmITZETjS5UNhBZcbcHWaHyUcVFa-1XcgH_tgAE/w640-h626/001.jpg)
Wednesday, June 12, 2024
Absa Bank Tanzania yazindua Huduma ya Mikopo ya Magari Ili Kusaidia Wateja Kununua Magari Mapya na yaliyotumika
Saturday, June 8, 2024
WABUNGE WANAWAKE NA KAMPUNI YA ORYX TANZANIA WAMPONGEZA RAIS SAMIA.
Saturday, June 1, 2024
KAMPUNI YA ORXY TANZANIA YAWAPELEKA WASAMBAZAJI WA VILAINISHI VYA KAMPUNI HIYO DUBAI
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhTpU7fmP8ooYw2A9z7p69aw7hh2pI-I0-I7hci2oDAfzW7p5WTZi9kZkec9LMD8Vea0bylkWESS_U-QjJ0TIWErapoT-6Mk-4G2oS_ptQCWIHGy0oDMm-Z1EDqX44Sapf3oW1z8EGfkBF88xUvgi50RBszo3YGjTX4hQ_0OkrI1EnpU7hxaCCzqbbj1-Gp/s16000/2023.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjiKq-OqncMj4XmBfRPzS05fsV2H4IR7YeALIu1Ca87QesVjpjfaN5FePZ0KWWH70OseTGejyHw6fP7Xjnu4DjK0fwknAFQDoQYtoPnV6y-ZpBPHtbhDMxeCa9Hv5nYzb2sahAXJ_DmeG7iH7DJq_b8txJndxgB3DlSKlZcalur7VC0gK85fw2q_UjGvul9/s600/2022.jpg)
Thursday, May 30, 2024
WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI TANGA WAFURAHIA KUJENGEWA VIVUKO VYA WAENDA KWA MIGUU.
Na Mwandishi Wetu,Tanga
KATIKA jitihada za kupunguza ajali za barabarani kwa wanafunzi jijini Tanga ,Shirika la Amend kwa kushirikiana na Ubalozi wa Uswis wamefanikiwa kuweka miundombinu salama barabarani yenye lengo la kuhakikisha wanafunzi wanavuka salama katika safari ya kwenda na kurudi shuleni.
Miundombinu hiyo salama ya barabara imefanyika katika Shule ya Msingi Makorora pamoja na Shule ya Msingi Azimio kwa kuwekewa vivuko vya Pundamilia, njia za watembea kwa miguu pamaja na alama muhimu za usalama barabarani.
Akizungumza kuhusu mradi huo wa miundombinu salama ya barabara, Mkurugenzi wa Shirika la Amend Tanzania Simon Kalolo amefafanua mradi huo umehusisha ujenzi wa njia za watembea kwa miguu, vivuko 4 vya pundamilia, matuta saba ya kupunguza mwendo kasi, alama 15 za barabarani, na michoro 16 ya usalama barabarani.
Pia wametoa elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi 1,694 na walimu wa shule za msingi Makorora na Azimio ndani ya mwezi tano, 2024 Tanga na Tanzania kwa ujumla.
Kalolo amesema mpango wa kuboresha miundombinu salama ya watembea kwa miguu ni sehemu ya mradi wa mwaka mmoja unaoitwa "Usalama wa Pikipiki kwa Vijana Tanzania".
Amesisitiza mradi huo unaungwa mkono na Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania na una bajeti ya Sh. 424,983,396 huku akifafanua tangu Septemba 2023, shughuli nyingine za mradi zimejumuisha mafunzo ya waendesha pikipiki 300 jijini Tanga, waendesha pikipiki 253 Dodoma.
Pia kampeni a uhamasishaji kuhusu masuala ya usalama wa pikipiki, na kuanzishwa kwa 'Kanuni za Maadili' kwa madereva, Waendesha pikipiki 200 zaidi watapewa mafunzo jijini Tanga ifikapo Juni 2024 na tathmini ya athari za shughuli hizo zote inafanywa hivi sasa.
“Ajali za barabarani ndiyo chanzo kikuu cha vifo vya watoto na vijana wenye umri kati ya miaka 5 na 29 duniani kote nchini Tanzania na kuna zaidi ya majeruhi 330,000 wa ajali za barabarani kwa mwaka ambayo ni ya juu kuliko wastani katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara”amesema.
Amesema mradi huo wa kuokoa maisha unaonesha ajali za barabarani zinaweza kuzuilika kazi hiyo iliyoungwa mkono na Fondation Botnar na sasa Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania, itaendelea kupunguza ajali za barabarani na kuokoa maisha.
Ameongeza kupitia Mpango Kazi wao wa Usafiri Salama na Endelevu kwa Jiji la Tanga, wanalenga kuhakikisha kila mtoto wa Tanga anakuwa na safari salama ya kwenda na kurudi shuleni.
“Hakuna sababu ya kuchelewa kuchukua hatua hili linahitaji kuwa kipaumbele cha juu kwa watunga sera wetu na Tanga ina uwezo wa kuongoza nchi na bara letu katika kukabiliana na chanzo hiki kikibwa cha vifo kwa vijana,”alisema
Kwa upande wake Katibu Tawala wa Wilaya ya Tanga Dalmia Mikaya aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Tanga James Kaji , amepongeza kutekelezwa kwa mradi huo wa miundombinu ya barabara katika Shule hiyo Makorora na Azimio na matamio yao ni kuona mradi wa usalama barabarani unakwenda katika shule zote za Tanga.
Pia amewaomba wazazi na walezi kuhakikisha wanawalinda wanafunzi dhidi ya vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia.Tunafahamu suala la usalama barabarani ni muhimu lakini tuweke nguvu kusimamia usalama dhidi ya ukatili wanaofanyiwa katika jamii zetu.”
Kwa upande wake Mwakilishi wa Ubalozi wa Uswisi Rashid Mbaramula ambaye anashughulikia Miradi amesema nchi Uswis inahistoria kubwa wa kimahusiano na Tanzania na Jiji la Tanga ni miongoni mwao huku akifafanua kuanzia mwaka 1960 Uswis imekuwa mdau mkubwa wa maendeleo na imekuwa ilishiriki kikamilifu katika kufanikisha Miradi ya maendeleo.
Amesema kupitia mradi huo madereva bodaboda zaidi ya 550 wamepatiwa mafunzo ya usalama barabarani na kufanikiwa kwa mradi huo kunatokana na ushirikiano wa wadau mbalimbali huku akiwapongeza Amend kwa kazi kubwa wanayofanya ya kutoa elimu ya usalama barabarani.
Awali Inspekta wa Jeshi la Polisi Rajab Mhumbi aliyemwakilisha Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Tanga amesema vivuko vya barabarani ambavyo vimewekwa na Amend ni vema vikalindwa na kila mmoja wetau na si jukumu la wanafunzi na walimu peke yao.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEho8VtHPVlHBYwDNnMla1Z86lLHAneKwJiWautLjVqaTglAvXxMzGjJ8BSVLLvyGNFspEoJgbLKS_3SD9hrL6alXEJFwysLzsRQ3BQlTGuRkB9fD29qdTPnEjtI_3gKtkakwrZEmOmfmLBMDgCmbtRWB6S_YlJFEQEIvRnc0uRSlqr43FiHXOORNQ/s16000/WhatsApp%20Image%202024-05-29%20at%2020.29.14.jpeg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhNwP2VhE1031OZOr_klHGeY8a26QbLNYD9uOSYV7uha2SnWDydYzc3oprWwfatd5v2ae9tYJxf1NurwFGO-beSPIAqM0Vci5tYyhcxI02r1-LRQEh-OnYMGvhmYuCht91GVgWa0g25eplfPfLfg-XGmIf79D2rIBc8BlzBWKg6A7MdaFOhzezZUg/s600/WhatsApp%20Image%202024-05-29%20at%2020.13.20.jpeg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjGWZEWS0Yefx1pKuRAwWmqYOVseSj_CRHakinSkEIvE47BGWrRMbWcPVkMQHKE7C8Zwy1C9IDTjBhHim0K9LCoscsEmDyW6QDFx_HNdjenetdpjozt5AC7ZalMXrcnphLUe7Q6aJLqrxqKNd_lOjUOseILLNDrS8AXM8mp3wsW5BI0BeFrwSeoxw/s600/WhatsApp%20Image%202024-05-29%20at%2020.13.50.jpeg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgutkK1wLbeV3neWu11O8Brl-8EfXt0hLFfrJv-jl6-syFoFw4PxI40hnG5DV5w8WXREAJiavRwsA2MqHre-VdxUmAnPQ1veEu79NnmsuY2mQv9f5eD1zQq8HsylHQjAUBr7E1AHXIaO5g2QtYlq_QT4iBQw82IoMz5IkTyrt3DLjEZIwBLIaD3AQ/s600/WhatsApp%20Image%202024-05-29%20at%2020.14.18.jpeg)
Monday, May 27, 2024
KAMPUNI YA ORYX TANZANIA YAGAWA MITUNGI 800 KWA WANANCHI WA JIOMBO LA BABU TALE MOROGORO.
MITUNGI 800 ya gesi ya Kampuni ya Oryx Gas Tanzania ikiwa na makiko yake, imetolewa bure kwa wananchi wa Jimbo Morogoro Kusini Mashariki kuunga mkono juhudi za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.
Mitungi hiyo imetolewa kwa ushirikiano wa Kampuni ya Oryx na mbunge wa kimbo hilo Hamisi Taletale (Babu Tale) katika mkutano mkuu wa CCM Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki mgeni rasmi akiwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Abdulrahman Kinana.
Akizungumza kabla ya kukabidhi mitungi hiyo Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara Abdulurahman Kinana amempongeza Mbunge Taletale kwa kushirikiana na wadau kugawa mitungi hiyo kwa wananchi hao kwani ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan
Amesisitiza Rais Samia ameanzisha kampeni ya nishati safi yenye lengo la kumtua mzigo wa kuni mwanamke na hatimaye kumpa muda mwingi katika kufanya shughuli nyingine za kimaendeleo hasa kwa kutambua mwanamke ndio nguzo ya familia.
“Kampeni hii ya nishati safi ni matokeo ya sera na ubunifu kwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. Mwaka jana alianzisha mchakato wa kuwatua akina mama mzigo wa kuni.
"Hivyo katika kufanikisha kampeni hiyo Serikali peke yake haitaweza kwasababu inahitaji fedha nyingi,hivyo nikupongeze Taletale kwa kuunga mkono jitihada za Rais katika kampeni hii,kwani tutakabidhi mitungi ya gesi kwa wananchi,lakini niwapongeze wadau wa gesi kwa kushiriki katika kufanikisha kampeni hii yenye lengo la kumtuamzigo wa kuni mwanamke,"amesema Kinana
Wakati huo huo akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Gesi ya Oryx Tanzania, Benoite Araman, Meneja wa Mifumo ya Gesi yenye Matumizi Makubwa Oryx Gas Tanzania LTD, Richard Sawere amesema hatua ya kushirikiana na Mbunge Taletale kugawa mitungi hiyo ni hatua hiyo ni kuunga mkono jitihada za Rais Dk. Samia.
Amesema Rais Dk.Samia amedhamiria ifikapo mwaka 2030 asilimia 80 ya Watanzania wawe wananatumia nishati safi ya kupikia huku akifafanua Kampuni ya Oryx pia umeamua kunusuru uharibifu wa mazingira na kulinda afya za wananchi kwa kutumia nishati safi na rafiki kwa afya za wananchi.
"Nchini Tanzania, wananchi 33,000) wanapoteza maisha kila mwaka kwa kuvuta moshi na chembe chembe zinazotokana na mkaa na kuni. Kupika na gesi ya Oryx itatatua jambo hili," amesema.
Awali akitoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya mitungi na majiko hayo, Meneja Masoko wa kampuni hiyo Peter Ndomba amesema sera ya kampuni hiyo ni kuhakikisha nchi nzima inatambua umuhimu wa kutumia gesi.
"Hii ni kampeni ya kitaifa ambayo Rais Samia Suluhu Hassan aliizindua kwa lengo la kuhakikisha kwamba miaka 10 ijayo zaidi ya asilimia 80 ya watanzania wawe wanatumia nishati safi".
Katika hatua nyingine Mbunge wa amesema kuwa Rais Samia ameelekeza kutekelezwa kwa kampeni ya nishati safi,hivyo Wana Morogoro Kusini Mashariki wameona Kuna kila sababu ya kumuunga mkono Rais Samia kwa vitendo kwa kutumia nishati safi ya kupikia inayotokana na gesi ili kuachana na kuni na mkaa.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhytnkpTpTCCY_MvvS4LmQ94EYTEdUgI8AwINv22fIgr-4fw_VjvhXtyqL4y238UKq42OG-rqPruEfrPBqZFINhJB1l4U2ddE9xRrDSXZ7a7QBRM3LiAQuCaAs4uYEnl9yEV9zdRgClaXHGIf7Ej7U103NHqtSYijYBkZYuExM5BR0E6-6Epb7WXs4gMmY/s600/WhatsApp%20Image%202024-05-27%20at%2012.47.36%20%281%29.jpeg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhLYMSeA1Euuzg8tVrc-xfEkk_Us8gLax5ATMG9uwdmsnK-M11fpktgizAts0dyw-2gscq2UgH_OhEZoaKRYBhfZYBFgT_SWQz3B84tIMyc3JH3kOySOx8igPrissYwH69YYHBPJpRG-us-wRQGvpK9nmK12U_V01pLJzhfN59VBRj5KLw3PnqdO6l2U5Y/s600/WhatsApp%20Image%202024-05-27%20at%2012.47.36.jpeg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEin4nqmrSivdlzaQgosr0P3p2S-Vxl5sKK4dTncEL1Jl-g13-5YnViBQgoSEUUtNVM2EZau2FLl242BdpaiPtRB9Q-6Q1SjikFkkCiFD8jm0HVHEce8tWAdpbH1yT7qzwX3DKiG3kVTN3ecsB4iiZiUG9ZzYVrRFCBUmxZbUcckH0ERRVmzmG20KM_qdgM/s600/WhatsApp%20Image%202024-05-27%20at%2012.47.38%20%281%29.jpeg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhtEV_mUC2s4JD8ts-HoVjVrpijZ0SjKaqyAEAosRKMtIp82uuH2Y4fZhPBY3FkLQFCU_rrybvMMsF8gxb8p2Xu4tv4haPk8QNvZkvhykLcQd6wSF6UIAqA6itr9bQWGqMSHvQEsok_di9W017uzmYGfB5weFPQGfDCUfThtoiyURfyAC7JAKuODKHl7zc/s600/WhatsApp%20Image%202024-05-27%20at%2012.47.38.jpeg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgisuHl36zQwvUIIjnYptb1yDUsem1KOXwKawKrqTqoyt4rfwod3cw_HlXmhLR0l_Pw3csTQLVZE5dxR5bXgv_5KMTMYaaszupmOAlFMOoBHVSkyx1tZFPsswPG6OMSyiBeLNEbCwfv1kqaKhaKcsYvfabWETzf5q9FhLjWk00oq4UmytWU3pJrsh3BJSM/s600/WhatsApp%20Image%202024-05-27%20at%2012.47.39%20%281%29.jpeg)