A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Monday, January 27, 2020

NBC yawataka wanawake wajasiriamali kujiunga na klabu ya biashara ya benki hiyo

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia  Uwekezaji, Angela Kairuki, (wa pili kushoto) akishikana mikono na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Rejareja Maalum wa Benki ya NBC, Ashura Waziri wakati wa semina ya kwanza ya wanawake wa Kiislam kuhusu Ujasiliamali na  Tanzania ya Viwanda iliyofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. Wengine ni baadhi ya maofisa wa NBC na waalikwa wengine.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Angela Kairuki (wa pili kushoto), akishikana mikono na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Rejareja Maalum wa Benki ya NBC, Ashura Waziri wakati wa semina ya kwanza ya wanawake wa Kiislam kuhusu Ujasiliamali na  Tanzania ya Viwanda iliyofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. Weningine kutoka kushoto ni Meneja wa Tawi la NBC Corporate, Mariam Kombo, Meneja wa Tawi la NBC samora Zubeider Haroun, pamoja na mjumbe wa kamati ya maandalizi ya semina  hiyo, Mariamu Dedes.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Rejareja Maalum wa Benki ya NBC, Ashura Waziri, akizungumza na Wanawake wajasiliamali wakati Warsha ya kwanza ya wanawake wa Kiislam kuhusu  Ujasiliamali na  Tanzania ya Viwanda iliyodhaminiwa na Benki ya NBC na kufanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. Mgeni rasmi katika semina hiyo alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Angela Kairuki akimwakilisha Makamu wa Raisi, Mama Samia suluhu Hassan.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Angela Kairuki (katikati), akipunga mkono wakati akiondoka katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es salaam juzi, baada ya kufungua semina ya kwanza ya wanawake wa Kiislam kuhusu Ujasiliamali na Tanzania ya Viwanda iliyodhaminiwa na Benki ya NBC. Kushoto ni Naibu waziri wa zamani na mmoja wa viongozi wa wanawake wa kiislamu katika Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Mama Shamin Khan pamoja na wahudhuriaji wengine.
Baadhi ya Washiriki wakiwa katika semina hiyo kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es salaam juzi. Semina hiyo ilidhaminiwa na Benki ya NBC. (Picha zote na Brian Peter)
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive