A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Tuesday, March 19, 2019

Net-Soft waja na Mwarobaini kukomesha wizi na uchakachuaji wa mafuta na bidhaa za Petroli nchini

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya SCI AMEAA Ltd, Bw. Gilad Kaham, akifafanua jambo wakati wa uzinduzi rasmi wa Mfumo wa Kidigital (FMAS), unaolenga kukomesha wizi, upotevu na uchakachuaji wa mafuta na bidhaa za petrol nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Net-Soft Consult, Bw. Richard Shirima, akiongea na wadau kuhusu faida zinazotokana na Mfumo mpya wa Kidigital (FMAS) wa kudhibiti wizi na uchakachuaji wa mafuta na bidhaa zingine za petrol katika sekta za Umma na binafsi nchini Tanzania.
 Baadhi ya wateja waliohudhuria hafla hiyo
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Net-Soft Consult, Bw. Richard Shirima (kushoto),  akimsikiliza Moja ya Mteja aliehudhulia hafla hiyo (Picha na Brian Peter).

Na Mwandishi Wetu

Kampuni ya Kimataifa SCI EMAA LTD (SCI) kwa kushirikiana na Kampuni ya Net Soft Consult-Tanzania jana wamezindua mfumo maalum wa kigitali unaolenga kukomesha wizi, upotevu na uchakachuaji wa mafuta na bidhaa zingine za petroli na gesi katika sekta binafsi na umma inchini Tanzania.

Wataalamu wa teknologia ya habari na mawasiliano wanautaja mfumo huo “Fuel Management Automation System (FMAS)” kama mwarobaini wa tatizo sugu la wizi na upotevu wa mafuta katika taasisi, mashirika na makapuni ya sekta binafsi na ile ya umma, unaosababisha hasara ya mabilioni ya shilingi.

Akiongeza katika uzinduzi wa mfumo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Net Soft Consult, Richard Shirima, amesema matumizi ya mfumo huo yapunguza kwa kiasi kikubwa gharama za uendashaji katika makampuni binafsi na taasisi za serikali, hivyo kuongeza kasa ya ukuaji wa uchumi wa Taifa.

“Mfumo huu unakwenda sambamba na sera ya Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli, inayolenga kupunguza gharama za uendeshaji na kuongeza tija katika sekta binafsi na ile ya umma--hatimae kuifanya Tanzania kutimiza ndoto zake za uchumi wa viwanda,” amesema Bw. Shirima.

“Badala ya kuajiri watu wengi kusimamia matumizi ya mafuta katika shiriki, kampuni binafsi au ya umma, kazi hii inaweza kufanywa kirahisi sana kwa kutumia mfumo huu maalum (FMAS),” ameongeza Bw. Shirima.o

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Net-Soft Consult, mfumo huu uwezesha mashirika, makampuni na taasisi binafsi na za umma, kufahamu kiwango cha mafuta yanayotumika au yanapaswa kutumika (katika shughuli zao) kwa siku, kwa wiki, mwezi na mwaka, hali itakayosaidia mashirika na makampuni husika kuweka mipanga sahihi inayohusu matumizi ya mafuta.

Bw. Shirima amesema mfumo huu unawezesha wamiliki wa makampuni ya mafuta kufahamu kiwango cha mafuta yaliogizwa, yaliyouzwa na yaliyobaki katika vituo vyake vilivyoko nchi nzima, kiwango kinachopaswa kuongezwa katika vituo husika na wakati gani.

“Kwa kutumia teknologia hii, makampuni ya kusafirisha mafuta ndani au nje ya nchi, yanaweza kufatilia magari yaliobeba mafuta na kuhakikisha yanafika mahali husika, bila kupakuliwa kinyemela njiani, hivyo kuthibiti wizi na upotevu wa mafuta,” ameongeza.

Katika sekta ya umma, Shirima amesema teknologia ya FMAS inawezesha taasisi, mashirika na kampuni ya serikali, kufatilia mafuta yanayoagizwa, kutumika katika magari na shughuli mbalimbali, kiwango kilichobaki, bila kupoteza hata “tone” moja la mafuta.

Msululu wa wafanyakazi wanaosimamia matumizi ya mafuta katika sekta mbalimbali ya umma, utapungua sana, kwa sababu kazi yote ya usimamizi na ufatiliaji itafanywa na mfumo maalamu, amesema Andrew Charles, mmoja wa watumishi wa umma uliohojiwa wakati wa uzinduzi wa mfumo huu.

“Hii itaiwezesha serikali kusevu fedha nyingi (zilizokuwa zinatumika katika kudhibiti matumizi ya mafuta) na kuzielekeza fedha hizi katika miradi mingine ya maendeleo,” ameongeza.

Mmoja wa wadau wa sekta binafsi, Salehe Mwango, amesema “Kwa kutumia mfumo huu, mashirika ya umma na binafsi yanaweza kufuatilia kwa karibu kiwango cha mafuta kinachotumika katika magari yake, kilichobaki na kinachopaswa kuongezwa, hivyo kukomesha kabisa wizi wa mafuta na bidhaa zingine za petrol.”

Mbali na kudhibiti wizi na upotevu wa mafuta, mfumo huu pia unaweza kuangalia/kufuatilia ubora wa mafuta yanayotumika katika sekta binafsi na umma, jambo litakalosaidia kuondoa tatizo sugu la uchakachuaji wa mafuta.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive