A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Friday, December 3, 2021

MIFUGO MKOMBOZI WA WANUFAIKA WA TASAF

 
ELINE MASAWE mnufaika kutoka Gezaulole akiwa na mumewe Benjamin Fanuel Masawe wakiwa nyumbani kwao kijiji cha Gezaulole mara baada ya kutembelewa na waandishi wa habari kuona miradi yao.
Benjamin Fanuel Masawe akiwalisha mbuzi wao waliowanunua mara baada ya kuingizwa na TASAF kwenye mpango wa Kaya Masikini majani.
SAYANDE SHUNA wa Kijiji cha Foo Machame Hai Kilimanjaro akimhudumia ng'ombe wake aliyemnunua kwa ruzuku ya TASAF mara baada ya kuingizwa kwenye mpango wa kaya masikini.
SAYANDE SHUNA wa Kijiji cha Foo Machame Hai Kilimanjaro akizungumza na maofisa wa TASAF kuelezea namna alivyofaidika kwa ruzuku ya TASAF mara baada ya kuingizwa kwenye mpango wa kaya masikini.
Afisa Malalamiko wa TASAF Bw. Dismas Yusuf Makwinja akimsikiliza Michael Zakaria Mumburi Mratibu TASAF Wilaya ya Hai wakati waandishi wa habari walipowatembelea wanufaika wa TASAF kijiji cha Foo Machame Kaskazini wilaya ya Hai.
Afisa Malalamiko wa TASAF Bw. Dismas Yusuf Makwinja akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu wanufaika wa TASAF katikakijiji cha Foo.
Mwenyekiti wa kijiji cha Foo Machame wilaya ya Hai Kilimanjaro Judica Munisi akiongozana na Mwandishi wa Clouds Jerome Risasi kuelekea kwa Bi SAYANDE SHUNA wa Kijiji cha Foo Machame Kaskazini Hai Kilimanjaro.
Afisa Malalamiko wa TASAF Bw. Dismas Yusuf Makwinja akifanya utambulisho kwa Bi. SAYANDE SHUNA wa Kijiji cha Foo Machame Hai mara baada ya timu ya waandishi wa habari kuwasili nyumbani kwake.
Bi. SAYANDE SHUNA wa Kijiji cha Foo Machame Hai akionesha ndama wake ambaye ametokana na ng'ombe aliowanunua kwa ruzuku ya TASAF.
Baadhi ya gombe wa Bi. SAYANDE SHUNA wa Kijiji cha Foo Machame Hai aliowanunua kwa ruzuku ya TASAF baada ya kuingizwa kwenye mpango wa Kaya Masikini.

Halmashauri ya Wilaya ya Hai ina kaya 3,523 zilizo katika Vijiji 43 zinazonufaika na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF ili kuwaondolea hali ya umaskini iliyokuwa ikiwakabili.

Kwa mwaka 2021/22 Halmashauri hiyo imetenga Shilingi Milioni 140 zitakazotumika kuziwezesha kaya hizo kuanzisha miradi ya kimaendeleo ikiwemo ujasiriamali na ufugaji ili zenyewe ziweze kujikimu kimaisha.

Hata hivyo uchunguzi umebaini kuwa shughuli za ugugaji hasa wa Ng’ombe na mbuzi ndizo zinazoleta tija kimaendeleo hivyo Tasaf inatakiwa kuwekeza katika kutoa elimu ili ufugaji huo uwe na tija.

ELINE MASAWE mnufaika kutoka Gezaulole, MARGRETH NKYA na SAYANDE SHUNA wa Kijiji cha Foo Machame Hai Kilimanjaro wamesema ili shughuli hiyo iwe na tija wanahitaji zaidi elimu ya ufugaji bora.

Nina ng’ombe wangu mmoja niliyemnunua kwa fedha za Tasaf, namfuga kwa kumkatia majani, na hata sasa ameshawahi kuzaa mara tatu hivyo huuza ndama kwa kiasi cha shilingi 250,000 na fedha ninayoipata najiendeleza kimaisha ikiwemo kujenga nyumba yangu,” alisema Margareth Nkya.

Sayande Shuna yeye mbali ya ufugaji pia ni mkulima wa mbogamboa ambapo amekuwa akitumia mbolea kutokana na mifugo kurutubisha mazao yake kama ndizi na miparachichi ili kutoa mavuno bora.

Licha ya kuuza maziwa ya ng’ombe na mbuzi, mbolea kutoka kwa ng’ombe wangu watatu na mbuzi imekuwa ikinisaidia kurutubisha mazao yangu hapa shambani,” alisema Syande.

Akizungumzia juu ya hali ya uwezeshwaji kwa kaya maskini Katibu wa Mtaa wa Gezaulole Tumaini Mkojela amesema, shughuli za ufugaji zimewawezesha wanufaika wengi kusomesha watoto wao ikilinganishwa na zamani.

Mbali na hilo Mwenyekiti wa Kijiji cha Gezaulole FADHILI NG’ANZI amesema kaya zinazowezeshwa na Tasaf zimekuwa msaada kwa wakazi jirani baada ya kujifunza stadi mbalimbali zilizowaendeleza wanufaika kimaisha.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive