A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Wednesday, December 8, 2021

FAMILIA MARATHON 2021 KUTIMUA VUMBI JUMAMOSI DISEMBA 11

Mwenyekiti wa mbio za Familia Marathon 2021, Bi. Francisca Alphonce (wa tatu Kulia), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam Disemba 11, jumamosi. Wengine ni wawakilishi wa Kampuni zinazodhamini mbio hizo.
Mkuu wa Masoko, Mawasiliano na Uhusiano wa Benki ya KCB, Christina Manyenye (wa nne kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu udhamini wao katika mbio za Familia Marathon 2021 zinazotarajiwa kutimua vumbi lake jijini Dar es Salaam jumamosi wiki hii. Usajili unaendelea kufanyika katika Tawi la KCB Mlimani City.
Ofisa Habari Familia Marathon (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam Disemba 11, jumamosi. Mbio zitaanzia Msasani Beach Club kuanzia saa 12 asubuhi zikijumuisha mbio za 21km -half marathon, 10km- Corporate Run na 5km -Social Run.
Mkurugenzi Mtendaji was Kampuni ya magari ya KP Motors, Anita Kisima (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu udhamini wao katika mbio za Familia Marathon 2021 zinazotarajiwa kutimua vumbi lake jijini Dar es Salaam jumamosi wiki hii. KP Motors itatoa zawadi ya gari aina ya Passo mpya kwa mshindi mwanamke kati ya washindi kumi atakayeshinda mbio za KM 21. Kushoto kwake ni Mkuu wa Masoko Mawasiliano na Uhusiano wa Benki ya KCB, Christina Manyenye na Ofisa Masoko wa UTT Amis, Rahim Mwanga.
Mkurugenzi Uendeshaji wa Planet Fitness, Ramadhani Mdula (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu udhamini wao katika mbio za Familia Marathon 2021 zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam jumamosi wiki hii.
Meneja wa Kampuni ya Rani Sanitary Pads, Mawi Zahor (kulia ), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu udhamini wao katika mbio za Familia Marathon 2021 zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam jumamosi wiki hii.
Waandaaji na wadhamini wa Familia Marathon 2021 wakionyesha kwa waandishi habari, Dar es Salaam leo, medani na baadhi ya zawadi watakazopewa washiriki wa mbio hizo zitakazofanyika kwa mtindo wa kutembea na kukimbia jijini humo jumamosi wiki hii. Mbio za mwaka huu zimedhaminiwa na KCB Bank, KP Motors, UTT Amis, Premier Security, Optical Centre, Rani Sanitary Pads, Planet Fitness, Knight Support na Xpress Rent.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive