A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Friday, June 11, 2021

BENKI YA NBC YASOGEA KARIBU ZAIDI KWA WAFANYABIASHARA WANAOCHIPUKIA

001Mkurugenzi wa Wateja wa Rejareja na Binafsi wa NBC, Nd Elibariki Masuke (Kulia) na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki hiyo, Bi Neemarose Singo (Kushoto), wakipeperusha bendera kuashiria uzinduzi rasmi wa kampeni ya Twende Sawa na NBC inayolenga kuwafikia wafanyabiashara wanaochipukia nchi nzima na kuwasogezea akaunti ya Kua Nasi mahususi kwa wajasiriamali isiyo na gharama za uendeshaji pamoja na kuwapa elimu ya biashara wakiwa kwenye biashara zao.

002
Mkurugenzi wa Wateja wa Rejareja na Binafsi wa NBC, Nd Elibariki Masuke akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Twende Sawa na NBC inayolenga kuwafikia wafanyabiashara wanaochipukia nchi nzima na kuwasogezea akaunti ya Kua Nasi mahususi kwa wajasiriamali isiyo na gharama za uendeshaji pamoja na kuwapa elimu ya biashara wakiwa kwenye biashara zao.
003
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo wa Benki ya NBC, Nd Raymond Urassa akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Twende Sawa na NBC inayolenga kuwafikia wafanyabiashara wanaochipukia nchi nzima na kuwasogezea akaunti ya Kua Nasi mahususi kwa wajasiriamali isiyo na gharama za uendeshaji pamoja na kuwapa elimu ya biashara wakiwa kwenye biashara zao.

 Benki ya Taifa ya Biashara leo imezindua kampeni yake ya Twende Sawa na NBC yenye lengo la kuwafuata na kuwapa elimu wafanyabiashara wanaochipukia katika maeneo yao ya kazi na biashara. Kampeni hiyo imezinduliwa leo katika hafla fupi iliyofanyika Makao Makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wadau mbali mbali wakiwemo wafanyakazi na baadhi ya wateja wa benki hiyo

Lengo kubwa la kampeni ya Twende Sawa na NBC ni kutoa elimu ya kuendesha biashara, usimamizi makini wa wapato, urasimishaji wa biashara pamoja na kuweka kumbukumbu za kifedha ili kumuwezesha mfanyabiashara anayechipukia kusimamia na kuendesha baishara yake kwa ufanisi zaidi. Pamoja na elimu itakayotolewa, kampeni ya Twende Sawa na NBC pia inatoa fursa kwa wafanyabiashara kufungua Akaunti ya Kua Nasi yenye masharti nafuu kufungua, inayotoa riba kwa amana za mteja pamoja na kutokuwa na gharama za uendeshaji za kila mwezi.

Akiongea katika hafla hiyo ya uzinduzi, Mkurugenzi wa Wateja wa Rejareja na Binafsi wa NBC, Nd Elibariki Masuke alisema kuwa lengo kubwa la Benki ya Taifa ya Biashara ni kuwa karibu zaidi na wafanyabiashara wadogo ili wawawezeshe kukuza biashara sambamba na benki hiyo. Aidha alisema kuna maboresho ambayo benki hiyo imekuwa ikifanya ili kutimiza lengo la kuwa karibu zaidi na wafanyabiashara wadogo.

“Tumeongeza wigo wa matawi ya benki yetu nchini kupitia NBC Wakala na tumeweka mfumo wa kidijitali wa kufungua akaunti, tumerahisisha ufunguaji wa akaunti ambapo mtu anahitaji kitambulisho chake cha NIDA tu hivyo tumejipanga kuwaifikia na kuwahudumia kikamilifu wafanyabisahara wa jiji la Dar es Salaam na na maeneno mengine ya nchi kote.” Alisema Nd. Masuke.

Aidha kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wadogo wa Benki ya NBC, Nd Raymond Urassa ambaye ndiyo msimamizi wa Akaunti ya Kua Nasi amasema akaunti hiyo ni mahususi na ni rafiki kwa wafanyabiashara wadogo.

“Sisi kama NBC tunatambua kwamba wafanyabiashara wadogo wanahitaji kukua kupitia benki yetu ndiyo maana tumeondoa makato ya uendeshaji ya kila mwezi, tunampa mjasiriamali faida kwa hela atakayokuwa ameweka, tunatoa vitabu vya hundi kwa gharama nafuu watakaohitaji lakini pia tumepunguza gharama za utoaji wa fedha kupitia akaunti hii ya Kua Nasi ili kumpa mjasiriamali fursa ya kukua zaidi.”

Akielezea akaunti hiyo, Nd Raymond Urassa alisema kwamba mfanyabiashara yeyote mdogo anaweza kufungua Akaunti ya Kua Nasi kupitia matawi yote ya Benki ya Taifa ya Biashara nchi nzima lakini pia kupitia mawakala wa benki hiyo ambao pia wanapatikana nchi nzima.


Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive