A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Wednesday, July 31, 2024

Benki ya Absa Tanzania Yazindua Akaunti ya Akiba ya Vijana

Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Swere (katikati), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa akaunti ya akiba ya vijana ya benki hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga na Meneja Bidhaa, Bw. George Kaindoah.
Baadhi ya waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakiwa kazini wakati wa uzinduzi wa akaunti ya akiba ya vijana ya Benki ya Absa, jijini Dar es Salaam leo.

Benki ya Absa Tanzania imezindua akaunti ya Akiba ya Vijana, bidhaa mpya ya kifedha iliyoundwa mahsusi kwa vijana wa Kitanzania wenye umri wa miaka 18 hadi 30. Hafla rasmi ya uzinduzi iliyofanyika leo, inaashiria hatua muhimu katika kujitolea kwa benki kuwawezesha vijana na kukuza utamaduni wa kuweka akiba.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi, Bi. Ndabu Swere, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, alielezea furaha yake katika kuzindua bidhaa hii mpya na kusisitiza umuhimu wake. “Leo tuko hapa kushuhudia uzinduzi wa bidhaa ya kipekee kutoka Absa Bank Tanzania - Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa. Akaunti hii inalenga vijana wenye umri wa miaka 18 hadi 30, kundi ambalo linawakilisha sehemu kubwa ya idadi ya Watanzania,” alisema Bi. Swere.

Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa imeundwa ili kuziba pengo muhimu katika soko. Wakati Benki ya Absa inatoa Akaunti za Akiba kwa Watoto wenye umri chini ya miaka 18, zinazosimamiwa na wazazi au walezi, kumekuwa na uhaba wa bidhaa maalum kwa vijana. Pengo hili mara nyingi limewalazimu vijana kutafuta huduma za kifedha mahali pengine, jambo ambalo linaifanya benki kuwa na changamoto ya kuwavuta tena mara wanapomaliza masomo na kuanza ajira au kuanzisha biashara zao.

Akaunti yetu mpya ya Akiba ya Vijana inashughulikia suala hili, ikilingana na kujitolea kwetu katika kanuni za ESG na kuwaunga mkono vijana wa Tanzania,” aliongeza Bi. Swere. “Katika Benki ya Absa Tanzania, tunaongozwa na dhamira yetu kuu ya 'Kuwawezesha Afrika kesho, pamoja, stori moja baada ya nyingine.' Leo, tunachukua hatua ya ujasiri kwa kuanzisha Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa, iliyoundwa kukuza utamaduni wa kuweka akiba miongoni mwa vijana wetu.

Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa inatoa faida nyingi, zikiwemo kuweka amana bure kupitia Absa Wakala, ATM, na matawi, kupewa kadi ya debit ya bure mteja anapofungua akaunti, huduma za benki za simu na za mtandao bure, kutokukatwa ada ya kila mwezi, ufikiaji wa akaunti saa 24/7 kupitia majukwaa ya kidijitali ya Absa, ushiriki katika programu na shughuli zinazolenga vijana, kama vile maonyesho ya kazi, matukio ya vijana, na semina, na kufaidika na mpango wa kurudishiwa pesa wa Absa Twin Rewards.

Kwa upande wake, Bw. Aron Luhanga, Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mahusiano ya Kampuni wa Absa, alisisitiza ahadi ya chapa ya benki, "Hadithi yako ina thamani," au kwa Kiingereza, “Your story matters.” “Huu kwetu ni zaidi ya msemo; ni ahadi ya kutembea pamoja na vijana, kuwasaidia katika safari ya maisha ili kuwasaidia kuandika stori bora zaidi. Tunaelewa kijana alikotoka, tunaona anakotaka kwenda, na tunaahidi kumpa msaada anaohitaji kuandika hadithi nzuri ambayo tutajivunia kuwa sehemu yake,” alisema.

Katika hitimisho lake, Bi. Swere aliwaalika vijana wote wa Kitanzania kuchukua fursa hii na kufungua Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa. Akaunti hii imeundwa kusaidia vijana kujenga tabia ya kuweka akiba na kufaidika na faida za kipekee zinazotolewa na Benki ya Absa Tanzania.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive