A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Wednesday, September 13, 2017

Benki ya NBC yazindua Klabu ya Biashara Mbeya

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, William Ntinika (kushoto), akikaribishwa na Mkurugenzi wa Biashara wa NBC, Alvis Ndunguru wakati akiwasili kwa ajili ya uzinduzi wa Klabu ya Biashara ya NBC mkoani Mbeya. Katikati ni Meneja Mahusiano wa NBC, William Kallaghe. Uzinduzi huo ulitanguliwa na semina ya siku moja juu ya kuwajengea uwezo wafanyabiasha wadogo na wa kati.  
Mwakilishi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Gabriel Mwangosi (kulia), akifundisha masuala mbalimbali kuhusu kodi katika semina ya siku moja iliyoandaliwa na NBC kwa wateja wake wadogo na wa kati mjini Mbeya. Semina hiyo ilifuatiwa na uzinduzi wa Klabu ya Biashara ya benki hiyo mkoani Mbeya hivi karibuni.
Mkurugenzi wa Biashara wa NBC,  Elvis Ndunguru akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Klabu ya Biashara ya NBC, mkoani Mbeya. Uzinduzi huo ulitanguliwa na semina ya siku moja juu ya kuwajengea uwezo wafanyabiasha wadogo na wa kati. Hafla hiyo ilihudhuriwa na wateja wa NBC, wajasiriamali na maofisa wa serikali mkoani humo.
Baadhi ya wateja wa NBC  mkoani Mbeya wakijipiga picha wenyewe ‘maaarufu kama selfie’ wakati wa hafla ya uzinduzi wa Klabu ya Biashara ya NBC mkoani humo hivi karibuni. Uzinduzi huo ulitanguliwa na semina ya siku moja juu ya kuwajengea uwezo wafanyabiasha wadogo na wa kati ilihudhuriwa na wateja wa NBC, wajasiriamali na maofisa waandamizi wa serikali mkoani humo.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive