A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Wednesday, July 31, 2024

Benki ya Absa Tanzania Yazindua Akaunti ya Akiba ya Vijana

Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Swere (katikati), akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa akaunti ya akiba ya vijana ya benki hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga na Meneja Bidhaa, Bw. George Kaindoah.
Baadhi ya waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakiwa kazini wakati wa uzinduzi wa akaunti ya akiba ya vijana ya Benki ya Absa, jijini Dar es Salaam leo.

Benki ya Absa Tanzania imezindua akaunti ya Akiba ya Vijana, bidhaa mpya ya kifedha iliyoundwa mahsusi kwa vijana wa Kitanzania wenye umri wa miaka 18 hadi 30. Hafla rasmi ya uzinduzi iliyofanyika leo, inaashiria hatua muhimu katika kujitolea kwa benki kuwawezesha vijana na kukuza utamaduni wa kuweka akiba.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi, Bi. Ndabu Swere, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, alielezea furaha yake katika kuzindua bidhaa hii mpya na kusisitiza umuhimu wake. “Leo tuko hapa kushuhudia uzinduzi wa bidhaa ya kipekee kutoka Absa Bank Tanzania - Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa. Akaunti hii inalenga vijana wenye umri wa miaka 18 hadi 30, kundi ambalo linawakilisha sehemu kubwa ya idadi ya Watanzania,” alisema Bi. Swere.

Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa imeundwa ili kuziba pengo muhimu katika soko. Wakati Benki ya Absa inatoa Akaunti za Akiba kwa Watoto wenye umri chini ya miaka 18, zinazosimamiwa na wazazi au walezi, kumekuwa na uhaba wa bidhaa maalum kwa vijana. Pengo hili mara nyingi limewalazimu vijana kutafuta huduma za kifedha mahali pengine, jambo ambalo linaifanya benki kuwa na changamoto ya kuwavuta tena mara wanapomaliza masomo na kuanza ajira au kuanzisha biashara zao.

Akaunti yetu mpya ya Akiba ya Vijana inashughulikia suala hili, ikilingana na kujitolea kwetu katika kanuni za ESG na kuwaunga mkono vijana wa Tanzania,” aliongeza Bi. Swere. “Katika Benki ya Absa Tanzania, tunaongozwa na dhamira yetu kuu ya 'Kuwawezesha Afrika kesho, pamoja, stori moja baada ya nyingine.' Leo, tunachukua hatua ya ujasiri kwa kuanzisha Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa, iliyoundwa kukuza utamaduni wa kuweka akiba miongoni mwa vijana wetu.

Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa inatoa faida nyingi, zikiwemo kuweka amana bure kupitia Absa Wakala, ATM, na matawi, kupewa kadi ya debit ya bure mteja anapofungua akaunti, huduma za benki za simu na za mtandao bure, kutokukatwa ada ya kila mwezi, ufikiaji wa akaunti saa 24/7 kupitia majukwaa ya kidijitali ya Absa, ushiriki katika programu na shughuli zinazolenga vijana, kama vile maonyesho ya kazi, matukio ya vijana, na semina, na kufaidika na mpango wa kurudishiwa pesa wa Absa Twin Rewards.

Kwa upande wake, Bw. Aron Luhanga, Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mahusiano ya Kampuni wa Absa, alisisitiza ahadi ya chapa ya benki, "Hadithi yako ina thamani," au kwa Kiingereza, “Your story matters.” “Huu kwetu ni zaidi ya msemo; ni ahadi ya kutembea pamoja na vijana, kuwasaidia katika safari ya maisha ili kuwasaidia kuandika stori bora zaidi. Tunaelewa kijana alikotoka, tunaona anakotaka kwenda, na tunaahidi kumpa msaada anaohitaji kuandika hadithi nzuri ambayo tutajivunia kuwa sehemu yake,” alisema.

Katika hitimisho lake, Bi. Swere aliwaalika vijana wote wa Kitanzania kuchukua fursa hii na kufungua Akaunti ya Akiba ya Vijana ya Absa. Akaunti hii imeundwa kusaidia vijana kujenga tabia ya kuweka akiba na kufaidika na faida za kipekee zinazotolewa na Benki ya Absa Tanzania.
Share:

Saturday, July 20, 2024

MADEREVA BODABODA TANGA WASHUKURU JESHI LA POLISI KWA KUTOA ELIMU KUHUSU USALAMA BARABARANI.

Na Mwandishi Wetu,Tanga

KAMANDA wa Polisi , Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Tanga ACP Bernard Zacharia amewataka madereva bodaboda katika Mkoa huo kuwa  mfano wa kuigwa na mabalozi wazuri wa kutii bila shuruti sheria za salama barabarani ili kuhakikisha wanakuwa salama wao na abiria zao.
Akizungumza na madereva bodaboda 204 waliohitimu mafunzo ya elimu ya usalama barabarani wilayani Tanga ,Kamanda Zacharia amesisitiza Jeshi la  Polisi linawahimiza watii sheria bila shuruti huku akiwashukuru Ubalozi wa Uswiss na Amend kwa ushirikiano wao na Jeshi la polisi kwa kuwaangalia vijana kwa ukaribu na kuwapatia mafunzo hayo.

"Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani tunafahamu kuwa bodaboda wamekua sehemu kubwa ya urahisishaji kwa abiria na mali zao,hivyo mafunzo waliyoyapata madereva bodaboda hao wa Wilaya ya Tanga na maeneo mengine ya mkoa huo yatawasaidia wao na abiria wao kuwa salama.

Amesema kwa Wilaya ya Tanga madereva bodaboda maarufu maofisa usafirishaji 204 wamehitimu mafunzo ya msasa ya usalama barabarani na kusisitiza waliopatiwa mafunzo wahakikishie wanakuwa.mabalozi kwa madereva wengine.Pia amesema anafahamu Kuna madereva bodaboda wengi waliofikiwa na mafunzo hayo katika Mkoa wa Tanga.

"Tunatarajia bodaboda Mkoa wa Tanga mtakua mfano wa kuigwa na mtakuwa mabalozi wazuri.Jeshi la Polisi linawahimiza kutii sheria bila shuruti na tunawashukuru Ubalozi wa Uswiss na Amend kwa ushirikiano huu na Jeshi la polisi kwa kuwaangalia vijana kwa ukaribu huu."

Kwa upande wake Mratibu wa Shirika la Amend Ramadhan Nyanza amesema wanaishukuru Serikali inayoongozwa na Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kushirikiana kwa karibu na mashirika yasio ya kiserikali kuzifikia jamii. 

"Katika kipindi cha mwaka mmoja kwa ufadhili wa Ubalozi wa Uswiss nchini ,- Shirika la Amend kwa kushirikiana na wadau mbalimbali tumefanikiwa kutoa mafunzo kwa vijana zaidi ya 900 kwa mkoa wa na Tanga na Dodoma."
Share:

Thursday, July 4, 2024

ORYX YAMPA UBALOZI SHILOLE KUHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

KAMPUNI ya Gesi ya Oryx  imemtangaza Mama Lishe Zuwena Mohamed maarufu Shilole (Shishifood) kuwa balozi wao katika in kuhamasisha matumizi ya nishati safi kupikia kupitia mitungi ya gesi nchini.

Lengo la Oryx kumpa Ubalozi Shilole unalenga kuunga mkono jitihata za Rais Dk.Samia Suluhu ambaye ameweka malengo kuwa ifikapo mwaka 2032 asilimia 80 ya Watanzania iwe inatuminia nishati safi ya kupikia.

Akizungumza wakati wa tukio hilo lililofanyika Julai 4 kwenye Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba yanayofanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, Meneja Mauzo na Masoko wa Oryx Gas Shaban Fundi amesema wameamua kumchagua Shilole kwasababu ni miongoni mwa wadau wanaohamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Amesema kupitia kwa Shilole wanaamini kuna wengine ambao walikuwa nyuma kwenye matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kuendelea kutumia gesi za Oryx kupikia.
"Tunafamu Shilole amekuwa mjasiriamali maarufu machi, anamiliki migahawa ya Shishifood katika miji ya Dar es Salaam na Dodoma, amekuwa mama Lishe wa kisasa na muumini  mzuri wa kutunza mazingira,hivyo Oryx tunaona fahari kumtangaza Shilole kuwa balozi wetu katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ili kwa pamoja kufikia malengo ya Rais Samia ya kuhamasisha nishati safi ya kupikia nchini."
Kwa upande wake Shilole ambaye pia ni Msanii maarufu nchini,amesema yupo tayari kushirikiana na wadau wengine kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Amesema Kampuni ya Oryx imekuwa ikiweka jitihada kubwa kuhamasisha matumizi nihati safi ya kupikia kwa Mama lishe na baba lishe nchini, hivyo ameona kuna umuhimu mkubwa wa kutoa ushirikiano.
Share:

Monday, July 1, 2024

Serikali ya Marekani Yashiriki Uzinduzi wa Ndondo Cup 2024, kupitia kampeni za SITETEREKI na FURAHA YANGU na CHANJO NI MAISHA

Mkazi wa Jiji la Dar es Salaam akipata vipimo vya afya wakati wa hafla ya uzinduzi wa michuano ya Ndondo Cup 2024. Serikali ya Marekani, kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) nchini Tanzania, imetangaza ushirikiano na mashindano ya Ndondo Cup 2024  kupitia kampeni zake mashuhuri za ‘SITETEREKI’, ‘FURAHA YANGU’ na ‘CHANJO NI MAISHA’ ili kuchochea huduma za VVU na chanjo. Mashindano haya yatafanyika katika mikoa nane nchini Tanzania, ikiwemo Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Iringa, Ruvuma, Pwani na Kagera.

Wizara ya Afya, Ofisi ya Rais – TAMISEMI na Serikali ya Marekani (USAID na PEPFAR) kupitia mradi wa Breakthrough ACTION, wameungana na kamati ya maandalizi ya Ndondo Cup, na wadhamini wengineo ikiwemo CRDB na ASAS, kusogeza huduma za afya hasa huduma za VVU na chanjo. Ushiriki huu kwenye Ndondo Cup 2024, unafanywa kupitia kampeni ya afya ya vijana iitwayo SITETEREKI, kampeni ya wanaume kupambana na VVU iitwayo FURAHA YANGU na Kampeni yab chanjo ya kitaifa iitwayo CHANJO NI MAISHA. Mashindano ya Ndondo Cup 2024 yatafanyika katika mikoa nane ya Tanzania - Dar es Salaam, Iringa, Mbeya, Ruvuma, Kagera, Dodoma, Mwanza, na Pwani.

Mashindano yalianza rasmi Juni 30, 2024, na mechi ya ufunguzi ya kusisimua kati ya Manzese Warriors na Makuburi FC kwenye Uwanja wa Kinesi, kata ya Sinza. Washiriki walipata huduma kamili za afya, ikiwa pamoja na vipimo vya VVU na matibabu na huduma za chanjo. Mgeni rasmi aliyefurahishwa na mpango huu wa ubunifu, aliipongeza kamati ya maandalizi na wadhamini kwa kujumuisha burudani na huduma za afya.

"Tumejitolea kubuni mbinu zinazotoa matokeo halisi ya kiafya," alisema Evangelina Chihoma kutoka Ofisi ya PEPFAR.

"Tunaamini kwamba michezo inaweza kuongeza nguvu kubwa katika kuleta mabadiliko ya tabia na kuboresha upatikanaji wa huduma, na tunafurahia kushirikiana na Ndondo Cup na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufanikisha mashindano haya."

Lulu Msangi, Mtaalamu wa Programu kutoka Shirika la maendeleo la Marekani (USAID) aliongezea, "Tunatumia michezo kuhamasisha Watanzania kupata chanjo na kulinda familia zao."

Mpango huu wa ubunifu utatekelezwa kwenye ngazi ya kitaifa na jamii, ukilenga kuwafikia vijana wanaoshiriki shughuli za kimichezo kupata elimu na huduma za afya hasa zinazohusu VVU na chanjo. Kwa kuingiza huduma za afya katika burudani, mpango huu unalenga upokeaji wa huduma za afya miongoni mwa wavulana na wanaume kwa kutumia umaarufu wa soka.
Mashabiki wa mpira wa miguu kutoka maeneo mbali mbali ya jiji la Dar es Salaam wakifuatilia uzinduzi wa michuano ya Ndondo Cup 2024. Serikali ya Marekani, kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) nchini Tanzania, imetangaza ushirikiano na mashindano ya Ndondo Cup 2024 kupitia kampeni zake mashuhuri za ‘SITETEREKI’, ‘FURAHA YANGU’ na ‘CHANJO NI MAISHA’ ili kuchochea huduma za VVU na chanjo. Mashindano haya yatafanyika katika mikoa nane nchini Tanzania, ikiwemo Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Iringa, Ruvuma, Pwani na Kagera.
Evangelina Chihoma ambaye ni Mtaalamu wa taarifa za mkakati kutoka PEPFAR akizungumza wakati wa uzinduzi wa michuano ya Ndondo Cup 2024. Serikali ya Marekani, kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) nchini Tanzania, imetangaza ushirikiano na mashindano ya Ndondo Cup 2024 kupitia kampeni zake mashuhuri za ‘SITETEREKI’, ‘FURAHA YANGU’ na ‘CHANJO NI MAISHA’ ili kuchochea huduma za VVU na chanjo. Mashindano haya yatafanyika katika mikoa nane nchini Tanzania, ikiwemo Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Iringa, Ruvuma, Pwani na Kagera.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive