A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Monday, December 5, 2022

Benki ya DCB yafunga mwaka ikiendelea kubeba tuzo lukuki

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu Zanzibar, Jamali Kassim Ali (katikati), akikabidhi tuzo kwa Ofisa Fedha Mkuu wa Benki ya DCB, Costantine Mtumbuka jijini Dar es Salaam hivi karibuni baada ya benki hiyo kuibuka mshindi wa kwanza wa uandaaji bora wa hesabu kwa mwaka 2021 katika kundi la benki ndogo na za kati. Hii ni mara ya saba kwa DCB kushinda tuzo hizo za kila mwaka zinatolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA). Kulia ni Meneja Fedha wa DCB, Siriaki Surumbu na wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya NBAA, CPA. Prof. Sylivia Temu. Hii ni mara ya saba kwa DCB kushinda tuzo hizo za kila mwaka zinazotolewa na NBAA.

*Yanyakua tuzo ya NBAA kwa kuwasilisha mahesabu yaliyonyooka

Ofisa Fedha Mkuu wa Benki ya DCB, Costantine Mtumbuka (kushoto), Meneja Fedha, Siriaki Surumbu (katikati) na Ofisa Masoko na Mawasiliano Wa benki hiyo, Caroline Gabriel Nnko wakionyesha tuzo ya mshindi wa kwanza wa uandaaji bora wa hesabu kwa mwaka 2021 katika kundi la benki ndogo na za kati zinatolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu Zanzibar, Jamali Kassim Ali jijini Dar es Salaam. Hii ni mara ya saba kwa DCB kushinda tuzo hizo za kila mwaka zinazotolewa na NBAA.
Maofisa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya DCB, Caroline Gabriel Nnko (kushoto), na Adelah Kaihula wakionyesha tuzo ya mshindi wa kwanza wa uandaaji bora wa hesabu kwa mwaka 2021 katika kundi la benki ndogo na za kati zinatolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu Zanzibar, Jamali Kassim Ali (hayupopichani), jijini Dar es Salaam.
Ofisa Fedha Mkuu wa Benki ya DCB, Costantine Mtumbuka (wa pili kulia waliosimama), akionyesha tuzo ya mshindi wa kwanza wa uandaaji bora wa hesabu kwa mwaka 2021 katika kundi la benki ndogo na za kati zinatolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu Zanzibar, Jamali Kassim Ali (katikati waliokaa), jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive