A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Tuesday, October 15, 2024

ZAIDI YA SH800 BILIONI KUPANUA, KUJENGA KIWANDA KIPYA CHA SARUJI MKOANI TANGA


Dar es Salaam. Serikali, kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina, na kampuni ya AMSONS, wameingia makubaliano ya kuwekeza $320 milioni (zaidi ya Sh800 bilioni) katika upanuzi wa kiwanda cha saruji Mbeya na kuanzisha kiwanda kipya cha saruji Tanga.  

 

Hayo yamesemwa leo (Oktoba 15) jijini Dar es Salaam na Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

 

Bw. Mchechu alisema kati ya fedha hizo, $190 milioni ( yapata Sh513 bilioni) zitatumika kwaajili wa ujenzi wa kiwanda kipya Tanga na $130 milioni (Sh351 bilioni) ni kwaajili ya upanuzi wa kiwanda cha Saruji Mbeya.

 

“Hivi ninavyozungumza tayari tumeshafanya maamuzi ya kimsingi. Kazi zilizobakia ni za kimenejimenti, ikiwemo kumalizia mpango wa biashara na hatua nyingine za kifedha,” alisema Bw. Mchechu.

 

 

Alisema mradi huu wa upanuzi wa kiwanda cha saruji Mbeya na ujenzi wa kiwanda kipya Tanga, unaotarajiwa kukamilika ndani ya miaka miwili hadi mitatu, utapelekea kuongezeka kwa uzalishaji wa klinka mara kumi.

 

Kwa kiwanda cha Mbeya, alifafanua, uzalishaji wa klinka, malighafi muhimu katika utengenezaji wa saruji, unatarajiwa kuongezeka kutoka tani 1,000 kwa siku hadi kufikia tani 5,000.

 

Aliendelea kufafanua kuwa kwa upande wa kiwanda kipya cha Tanga, kitakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 5,000 za klinka kwa siku, na hivyo kuleta jumla ya tani 10,000.

 

“Kuongeza kwa uzalishaji kutatufanya tuendelee kulikamata vizuri soko la nyanda za juu kusini ambalo tumekuwa tukilihudumia kwa zaidi ya asilimia 70 kwa muda mrefu,” alisema Bw. Mchechu.

 

Aliongeza: “Uwekezaji huu pia utakuwa mwanzo wa kupenye kwenye nchi jirani za Zambia, Malawi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.”

 

Bw. Mchechu alisema uwekezaji huo ni matokeo ya uboreshwaji wa mazingira rafiki ya biashara na uwekezaji yanayofanywa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Rais, Dr. Samia Suluhu Hassan.

 

“Uwekezaji huu ni sehemu ya mabadiliko ambayo Mhe. Rais amekuwa akitamani kuyaona katika mashirika ambayo Serikali ina hisa,” alisema.

 

Kwa upande wake Mkurugezi wa fedha wa AMSONS Bw. Ahmed Mhada alisema kukamilika kwa mradi wa upanuzi na ujenzi wa kiwanda kipya kutapelekea kuongezeka kwa uzalishaji wa saruji kutoka tani milioni 1.1 kwa mwaka hadi kufikia tani milioni 4.2.

 

“Inatarajiwa kuongezeka kwa uzalishaji kutapelekea kuongezeka kwa gawio mara 10 ya lile ambalo Serikali ilipata mwaka jana,” alisema Bw. Mhada

  “Inatarajiwa kuongezeka kwa uzalishaji kutapelekea kuongezeka kwa gawio kuongezeka kwa gawio mara 10 ya lile ambalo Serikali ilipata mwaka jana,” alisema Bw. Mhada.

 

Serikali, ambayo inamiliki asilimia 25 ya hisa, kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina, mwaka jana ilipata gawio la Sh3 bilioni, ikiwa ni miaka 10 ipite bila kampuni hiyo kutoa gawio.

 

Kama ongezeko la uzalishaji linatarajiwa kuongeza gawio mara 10, tafsiri yake ni kuwa serikali inatarajia kuanza kupata wastani wa Sh30 milioni kama gawio baada ya mradi kukamilika.

 

Kwa upande wa ajira, Bw. Mhada, alisema kuwa kukamilika kwa upanuzi wa kiwanda cha Saruji cha Mbeya na ujenzi wa kiwanda kipya Tanga, kutazalisha ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja 12,000.

 

Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Kiwanda cha Saruji Mbeya, Prof. Siasa Mzenzi, alimshukuru Mhe. Rais kwa kutengeneza mazingira rafiki ya biashara na uwekezaji nchini.

 

“Anachofanya Mhe. Rais, kinavutia wawekezaji kuwekeza nchini. Tuko tayari kusimamia uwekezaji huu ipasavyo kwa maslahi mapana ya Taifa letu na watu wake,” alisema Prof. Mzenzi.

 

Kadri siku zinavyozidi kwenda, idadi ya watu inazidi kuongezeka, na hatimaye mahitaji ya saruji yanazidi kupaa.


Mpaka kufikia mwezi Disemba mwaka jana, uzalishaji wa saruji Tanzania ulikuwa tani milioni 11 ikilinganishwa na mahitaji ya tani milioni 7.5.

 

Kiwanda cha Saruji cha Mbeya kinamilikiwa kwa ubia kati Kampuni ya Amsons kutoka Holcim ya Uswisi (65%), Serikali ya Tanzania kupitia kwa Msajili wa Hazina (25%) na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wenye hisa (10%).

 

Share:

Monday, October 14, 2024

Customer service: KCB Bank (T) planting trees across eight regions

.com/img/a/
KCB Bank (T) is championing sustainability as a responsible corporate citizen, advancing the Sustainable Development Goal (SDGs) no. 14 by extensive tree planting around the country.

Paschal Machango, a senior official, stood in for Cosmas Kimario, the group regional businesses director and country managing director, at an event to commemorate Customer Service Week.

.com/img/a/

He said KCB Bank has undertaken a significant environmental initiative by planting 1,500 trees across its operational regions in Tanzania, part of a strategic focus on economic, social, and environmental pillars.

The bank executive appreciated staff at the Mbagala Annex Primary School, one of the beneficiaries of the initiative, for their acceptance to host the project in the city.

This had helped to boost the bank’s participation in this crucial environmental cause, he said, asserting that the bank’s commitment extends beyond business success.

“We are dedicated to environmental conservation. Today, we are proud to have planted over 1,500 trees in schools across Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro, Zanzibar, Geita, Kahama, Mwanza, and Morogoro,” he stated.

.com/img/a/
Ruth Mussa, an assistant head teacher, expressed gratitude to KCB Bank for their engagement in the initiative, while Phina Bernard, an environmental officer with Temeke municipality, commended the bank for its impactful contribution.

Focus should also be placed on nurturing the planted trees, she stated, with the bank executive urging communities and organizations to join hands in promoting environmental stewardship and sustainability for the well-being of future generations

Share:

Sunday, October 6, 2024

Rais wa Zanzibar aipongeza Benki ya Absa Tanzania kuboresha afya ya mama na mtoto

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi (wa pili kulia), akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser kwa kutambua mchango wa benki hiyo katika kuwezesha kampeni ya ‘Uzazi ni Maisha’ iliyoanzishwa na Shirika la Amref Tanzania kwa kushirikiana na Wizara ya Afya ya Zanzibar. Ilikuwa ni katika hafla ya shukurani na uchangishaji fedha iliyofanyika katika Ikulu ya Zanzibar, jana. Wengine kutoka kushoto ni, Waziri wa Afya Zanzibar, Mhe. Nassor Mazrui, Mwenyekiti wa Bodi ya Amref, Bw. Anthony Chamungwana na Mkurugenzi Mkazi wa Amref Tanzania, Dk. Florence Temu.

Na mwandishi wetu, Zanzibar

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameipongeza Benki ya Absa Tanzania kwa mchango wake wa shs milioni 150 kuchangia kampeni ya ‘Uzazi ni Salama’ yenye lengo la kuboresha afya ya mama na mtoto wakati wa ujauzito na kujifungua.

Mheshimiwa Rais Mwinyi alitoa pongezi hizo katika hafla ya tatu ya shukurani na uchangishaji fedha wa kampeni hiyo, iliyoandaliwa na Shirika la Amref Tanzania, Wizara ya Afya Zanzibar, kwa udhamini mkuu wa Benki ya Absa Tanzania na kufanyika katika Ikulu ya Zanzibar, jana.

Leo tumekusanyika hapa kwa lengo la kuunga mkono juhudi za kuokoa maisha kupitia kampeni hii, iliyoanzishwa mwaka 2020 ikiwa na lengo la kukusanya fedha kiasi cha shs Bilioni 1."

Aidha nimefahamishwa, mwezi juni mwaka huu, Amref, wizara yetu ya afya pamoja na Benki ya Absa Tanzania wakiungwa mkono na wadau kadhaa walitoa vifaa tiba vyenye thamani ya shs milioni 262.6 kwa ajili ya vituo vya afya 28 katika mikoa mitano ya Zanzibar, niwashukuru Amref Tanzania, wadhamini wakuu Benki ya Absa Tanzania na wadau wote kwa kujitolea kuunga mkono jitihada ya serikali ya Zanzibar katika kuboresha huduma za afya”, alisema Rais Mwinyi.

Pamoja na hayo alisema ni jambo la kutia moyo kuona Zanzibar ikiwa kwenye njia sahihi ya kufikia malengo endelevu (SDG) 2030 ya kupunguza vifo vya wajawazito hadi chini ya vifo 70 kwa vizazi hai 100, vifo vya watoto wachanga hadi kufikia 12 kwa kila vizazi 1000 na vifo vya watoto chini ya miaka mitano hadi 25 kwa kila vizazi hai 1000 kufikia 2030.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Obedi Laiser alisema wametoa msaada kuunga mkono juhudi zinazofanywa za serikali za mbili za, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuwekeza katika sekta ya afya hususan katika kupunguza vifo vya akina mama na watoto.

Benki ya Absa Tanzania tunaenda sawa na lengo la taasisi yetu lisemalo ‘Kuiwezesha Afrika na Tanzania ya kesho kwa pamoja, hatua moja baada ya nyingine’ hapa tukihakikisha jamii yetu inapata huduma za afya stahiki."

Lakini pia msaada huu unaenda sambamba na ahadi yetu ya chapa tuliyoizindua hivi karibuni isemayo ‘Stori yako ina thamani’, hivyo kwa kuunga mkono juhudi hizi, tunaamini tunazisaidia serikali zetu katika kuandika stori zake zile zinazohakikisha watanzania wote wanapata huduma bora za afya”, alisema Bw. Laiser.

Awali akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkazi wa Amref Tanzania, Dk. Florence Temu alimshukuru Rais Dk. Mwinyi kwa kukubali, kujitoa na kuunga mkono kampeni ya Uzazi ni Maisha tokea ilipoanzishwa mwaka 2020.

Niwashukuru pia wadhamini wakuu, Benki ya Absa pamoja na wafadhili wetu wengine waliokuwa nasi tokea mwanzo kufanikisha malengo ya kampeni hii yenye kauli mbiu ya ‘Changia Vifaa Tiba kwa Uzazi Salama’ ambapo kati ya malengo yetu ya kukusanya kiasi cha shs Bilioni 1, hadi sasa tumeshapokea ahadi zenye thamani ya shs 989,831,145, Zaidi ya asilimia 98.9 ya malengo yetu tukipokea kiasi cha shs 740,457,422 sawa na asilimia 75”, alisema Dk. Florence.

Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na Waziri wa Afya Zanzibar, Mhe. Nassoro Mazrui, Naibu Waziri, Mhe. Hassan Khamis Hafidh, Katibu Mkuu, Dk. Mngereza Mzee Miraji, mabalozi na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa na kitaifa ya maendeleo, watendaji na watumishi wa serikali na mashirika ya umma.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi (katikati) na wengine kutoka kushoto; Mwenyekiti wa Bodi ya Amref Tanzania, Bw. Anthony Temu, Waziri wa Afya Zanzibar, Mhe. Nassor Mazrui, Mkurugenzi Mkazi wa Amref Tanzania, Dk. Florence Temu na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, wakifanya dua katika hafla ya shukurani na uchangishaji fedha wa kampeni ya ‘Uzazi ni Maisha’ iliyofanyika katika Ikulu ya Zanzibar, jana.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, akihutubia katika hafla ya shukurani na uchangishaji fedha ya kampeni ya Uzazi ni Maisha iliyofanyika katika Ikulu ya Zanzibar, jana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, akizungumza kuhusu udhamini na malengo ya benki hiyo katika kuiwezesha kampeni ya ‘Uzazi ni Maisha’ iliyoanzishwa ma Shirika la Amref Tanzania pamoja na Wizara ya Afya Zanzibar, katika hafla ya shukurani na uchangishaji fedha kwa ajili ya kampeni hiyo katika Ikulu ya Zanzibar, jana. Kampeni hiyo ina lengo la kuboresha afya ya mama na mtoto wakati wa ujauzito na kujifungua.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi (katikati),akipozi kwa picha ya kumbukubu na baadhi ya wafanyakazi wa benki ya Absa Tanzania, pamoja na viongozi wengine, mara ya baada ya hafla ya shukurani na uchangishaji fedha ya kampeni ya 'Uzazi ni Salama' iiyofanyika Ikulu ya Zanzibar, jana.
Share:

Thursday, October 3, 2024

Benki ya DCB yatenga shs bilioni 30 mikopo ya wafanyabiashara wa masokoni

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Bw. Songoro Mnyonge (wa tatu kushoto) akikata utepe kuzindua rasmi huduma ya mkopo uliopewa jina la Sokoni (Sokoni Loan), unaolenga wafanyabiashara wa masokoni katika hafla iliyofanyika katika soko la Magomeni, Kinondoni, jijini Dar es Salaam leo. Pamoja naye ni Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Bw. Sabasaba Moshingi na Meneja Mahusiano Taasisi za Kiserikali wa benki hiyo, Bi. Dalilla Issa (wa pili kulia).

Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Mstahiki Songoro Mnyonge, ameipongeza Benki ya Biashara ya DCB, kwa kutenga kiasi cha shs bilioni 30 kwa ajili ya mikopo ya wafanyabiashara ndogo ndogo, wanaoendesha biashara zao katika masoko yaliodhinishwa jijini Dar es Salaam na Dodoma.

Pongezi hizo alizitoa wakati akizindua huduma ya mkopo uliopewa jina la Sokoni (Sokoni Loan), unaowalenga wafanyabiashara wadogo wadogo wanaofanya biashara zao masokoni katika Soko la Magomeni, Kinondoni, jijini Dar es Salaam leo.

Mstahiki Meya alisema uamuzi wa DCB wa kuamua kutenga kiasi hicho unapaswa kupongezwa kwani unaunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha uchumi wa wananchi wa kipato cha chini unaimarika.

Serikali ilianzisha mikopo ya asilimia 10 kupitia Halmashauri, mikopo hii haitoshi kuwafikia wajasiriamali wadogo wote ambao ndio kundi kubwa, Halmashauri ya Kinondoni inawaunga mkono na itaendelea kushirikiana nanyi katika kuhakikisha mikopo hii inaleta tija katika masoko mbalimbali yalipo Kinondoni”, alisema Meya Songoro.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Bw. Sabasaba Moshingi alisema uzinduzi wa huduma hiyo unaendana na misingi ya kuanzishwa kwa benki hiyo, miaka 22 iliyopita ambayo ni kuwakomboa kiuchumi wananchi wenye kipato cha chini.

DCB imeendelea kusimamia vizuri misingi ya kuanzishwa kwake, tokea kuanza kwa huduma hii ya mikopo ya wafanyabiashara wa masokoni, zaidi ya wafanyabiashara 1500 wamenufaika kwa kupata mikopo ya takribani shs bilioni 3 huku tukiwa tumetenga zaidi ya shs bilioni 30 kwa mikopo hii.

Tunaamini tukishikiriana kwa pamoja, sisi kama benki, serikali, wafanyabiashara na wadau wengine tunaweza kupunguza umasikini kwa kiwango kikubwa.

DCB tutaendelea kuweka fedha zaidi kwa ajili ya mikopo ya wafanyabiashara, kuongeza nguvu kazi yetu ili tuwafikie wateja wetu mahali walipo, niwapongeze pia wale ambao tayari wamepata mikopo hii kwani mpaka muda huu hakuna mkopo kichefuchefu hata mmoja”, alisema Bw. Moshingi.

Awali akizungumza mahali hapo, Meneja wa Mikopo ya Wajasiriamali, Bi. Sheila Nicas Banzi alisema uzinduzi wa huduma hiyo umelenga kuondoa usumbufu wanaoupata wafanyabiashara hao wanapoenda kukopa katika mikopo kandamizi, maarufu kama ‘Kausha Damu’.

Akizungumza jinsi ya kupata mikopo hiyo, Bi Sheila alisema, sharti muhimu ni kuwa kuwa na kizimba cha biashara katika masoko yaliyoidhishwa na mteja kuwa mwanachama hai wa masoko hayo.

Mikopo ya DCB Sokoni inatolewa kwa dhamana ya kizimba pamoja na Umoja wa Soko husika kwa kiwango kinachoanzia shs 100,000 hadi shs 1,000,000. Zaidi ya milioni moja kutahitajika dhamana binafsi”, alisema Bi. Sheila.

Mwenyekiti wa Soko la Bw. Daudi Mohamed Dole aliishukuru DCB akisema kuingia kwa benki hiyo sokoni hapo kumewapunguzia uchungu wa tatizo la mitaji na pia muda wa kwenda katika taasisi zenye masharti yasiyo rafiki ya utoaji wa mikopo.

Wafanyabiashara wa Soko la Magomeni wanakopesheka, tunaishukuru DCB Kwa kutuletea mikopo hii, natoa ushauri kwa wafanyabiashara wa Magomeni na Masoko mengine kuchangamkia fursa hii”, alisema Bw. Dole.

Huduma ya mikopo ya DCB Sokoni imeanzia katika masoko ya Jiji la Dar es Salaam na Dodoma, inatarajiwa pia kupelekwa katika masoko mengine sehemu tofauti.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Bw. Songoro Mnyonge, akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa huduma ya mkopo uliopewa jina la Sokoni (Sokoni Loan), unaolenga wafanyabiashara wa masokoni uliofanyika katika Soko la Magomeni, Kinondoni, jijini Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Meneja wa Mikopo ya Wajasiriamali Wadogo wadogo wa Benki ya DCB, Bi. Sheila Nicas Banzi na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Sabasaba Moshingi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Sabasaba Moshingi, akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa mkopo wa Sokoni (Sokoni Loan), katika soko la Magomeni, Kinondoni, jijini Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Meneja wa Mikopo ya Wajasiriamali Wadogo wadogo wa Benki ya DCB, Bi. Sheila Nicas Banzi na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Bw. Songoro Mnyonge.
Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Ramadhani Mganga, akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa mkopo wa Sokoni (Sokoni Loan), a unaolenga wafanyabiashara wa masokoni, katika Soko la Magomeni jijini Dar es Salaam leo. Kushoto kwake ni Meneja wa Mikopo ya Wajasiriamali Wadogo wadogo wa Benki ya DCB, Bi. Sheila Nicas Banzi, Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Bw. Sabasaba Moshingi na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Bw. Songoro Mnyonge.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Bw. Songoro Mnyonge akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyabiashara mara baada ya uzinduzi rasmi wa mkopo wa Sokoni (Sokoni Loan), uliofanyika katika soko la Magomeni jijini Dar es Salaam leo.
Share:

Wednesday, October 2, 2024

Tanzania Breweries Plc (TBL) na WWF Wakabidhi Mradi wa Maji Kijiji Cha Minazi mirefu, Ruvu Stesheni

Katika hatua muhimu ya kuhakikisha upatikanaji endelevu wa maji kwa jamii za wenyeji na mazingira, Kampuni ya Tanzania Breweries Limited (TBL) na WWF Tanzania wamekabidhi rasmi miundombinu ya mfumo wa maji unaotumia nishati ya jua, ikijumuisha kisima, sehemu ya kunyweshea mifugo, na kituo cha maji kwa matumizi ya nyumbani katika Wilaya ya Kibaha.
Katika tukio hilo hilo, washirika hao wawili pia walizindua mradi wa majaribio wa miradi ya urejeshaji wa mazingira chini ya mpango wa "Bankable Nature Solutions" (BNbS) ili kuimarisha usalama wa maji wa muda mrefu na ulinzi wa mazingira.

Hafla ya makabidhiano iliyofanyika Kijiji cha Minazimikinda, Wilaya ya Kibaha, ilihudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Mheshimiwa Nickson Simon John, ambaye alisifu ushirikiano kati ya TBL na WWF. Alisisitiza umuhimu wa ushirikiano katika kukabiliana na changamoto za maji nchini, hususan katika maeneo yanayokua kwa kasi kama Pwani na Dar es Salaam.

"Maji ni rasilimali muhimu kwa ukuaji wa jamii zetu na uchumi. Ushirikiano huu unaonesha nguvu ya kufanya kazi kwa pamoja katika kutatua uhaba wa maji. Juhudi za TBL na WWF Tanzania za kuboresha usalama wa maji, hasa katika Dar es Salaam na maeneo jirani, ni za kupongezwa na ni hatua muhimu kuelekea kuhakikisha upatikanaji endelevu wa maji safi kwa wote," alisema Mkuu wa Wilaya, Mheshimiwa Nickson Simon John.

Mfumo mpya wa maji unaotumia nishati ya jua utatoa maji safi na ya kuaminika kwa jamii zinazozunguka, ukiwasaidia kaya na mifugo katika eneo hilo. Miundombinu hii inashughulikia changamoto za uhaba wa maji kwa sasa na kutumia teknolojia rafiki wa mazingira ili kuhakikisha matumizi endelevu kwa muda mrefu.
Mradi huu ni sehemu ya dhamira kubwa ya TBL kwa uendelevu, inayooana na mkakati wake wa kuleta athari chanya kwa jamii inazozihudumia huku ikiunga mkono uhifadhi wa rasilimali za asili za Tanzania. Ushirikiano na WWF Tanzania chini ya mpango wa BNbS unalenga kuhakikisha kuwa mifumo ya asili inabaki salama wakati changamoto za maji zinashughulikiwa.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa TBL Michelle Kilpin, alisisitiza umuhimu wa mradi huo: "Kwa TBL, uendelevu ni msingi wa shughuli zetu. Mfumo huu wa maji unaotumia nishati ya jua, pamoja na uzinduzi wa mradi wa majaribio wa Bankable Nature Solutions, ni hatua muhimu kuelekea kuhakikisha kwamba watu na mazingira wote wananufaika na juhudi zetu. Kwa kushirikiana kwa karibu na WWF Tanzania, tunahakikisha upatikanaji wa maji kwa jamii hii na kulinda mifumo muhimu ya ikolojia ambayo ni muhimu kwa mustakabali wetu."
Mbinu ya Bankable Nature Solutions (BNbS) inatumia rasilimali za asili kwa njia endelevu, ikigeuza juhudi za uhifadhi wa mazingira kuwa miradi inayoweza kujiendesha kifedha na kuleta manufaa kwa uchumi na jamii. Kupitia mpango huu, TBL na WWF Tanzania wanalenga kuunda mfano wa kurudiwa unaoweza kutekelezwa nchi nzima ili kukabiliana na uhaba wa maji na kuimarisha uhifadhi wa mazingira.

Mkurugenzi wa Nchi wa WWF Tanzania, Dkt. Amani Ngusaru, alielezea umuhimu wa kulinda vyanzo vya maji. “Ulinzi wa vyanzo muhimu vya maji ni muhimu kwa kudumisha maisha ya binadamu na usawa wa mazingira. Kupitia mbinu za ubunifu kama Bankable Nature Solutions, tunaweza kuunda suluhisho la muda mrefu kwa ajili ya watu na mazingira.”

"Ushirikiano wetu na TBL unaonesha jinsi biashara na mashirika ya uhifadhi wa mazingira yanavyoweza kushirikiana kufanikisha matokeo ya kudumu. Kwa uzinduzi wa mradi wa majaribio wa BNbS hapa Kibaha, tunaweka msingi wa suluhisho za muda mrefu na endelevu ambazo zinalinda rasilimali zetu za asili huku zikihakikisha jamii zinapata huduma muhimu kama maji." alisema Dkt. Ngusaru

Tukio hilo lilihudhuriwa na viongozi wa eneo hilo, wanajamii, na wadau muhimu ambao walipongeza mpango huo kwa kuwa na mtazamo wa mbali na manufaa ya muda mrefu kwa jamii. Kisima cha maji cha nishati ya jua, sehemu ya kunyweshea mifugo, na kituo cha maji kwa matumizi ya nyumbani vinatarajiwa kunufaisha moja kwa moja mamia ya kaya na mifugo yao.

Ushirikiano kati ya TBL na WWF Tanzania haukabiliani tu na upungufu wa maji, bali pia unaimarisha ulinzi wa vyanzo vya maji, muhimu kwa kuhifadhi bioanuwai na kudumisha huduma za mazingira kwa vizazi vijavyo.
Share:

Monday, September 30, 2024

Light Upon Light Summit in Zanzibar Set to Inspire and Unite Global Muslim Community12th & 13th October 2024.

  

Zanzibar, Tanzania – The much-anticipated Light Upon Light Summit is set to take place on the beautiful island of Zanzibar on 12th and 13th October 2024. Organized by Light Upon Light (London) in collaboration with The Grand Mufti's Office of Zanzibar, this prestigious event will bring together leading Islamic scholars, thought leaders, and over 15,000 attendees for two transformative days of learning, reflection, and spiritual growth. The summit’s featured guest will be the renowned Islamic scholar, Sheikh Ismail ibn Musa Menk (Mufti Menk), Grand Mufti of Zimbabwe.


The Light Upon Light Summit will address crucial societal topics such as Unity, Peace and Respect. Additionally, the summit in Collaboration with The Zanzibar Commission for Tourism will promote the growth of Halaal Tourism in Zanzibar, a sector currently valued globally at USD 250 billion. Attendees from Tanzania, East Africa, the United Kingdom, and GCC nations will converge for this unique opportunity to engage in knowledge exchange, foster social unity, and explore investment opportunities.


• Day 1 (12th October 2024):


The summit will take place at Amani Stadium, Zanzibar, where participants will engage with Islamic scholars through inspirational sermons, Quran recitations, and captivating Nasheed performances.


• Day 2 (13th October 2024):


A more exclusive Gala Dinner and Motivational Evening will be held at Hotel Verde, limited to 400 attendees. This exclusive gathering will allow participants to connect with scholars and explore the potential for Muslim-Friendly Tourism investments in Zanzibar.



Get Your Tickets Now!


Tickets are available online at www.nilipe.co.tz or at the following physical locations:


Dar-es-Salaam:


• Karak House - Masaki


• Taste Me - Coco Beach


• Kanzu Point - City Mall


Zanzibar:


• Poaz Grill - Mlandege


• Taste Me - Mazizini


This is an opportunity not to be missed! Engage with world-renowned scholars, contribute to essential social discussions, and help shape the future of Zanzibar’s tourism and social unity. Purchase your tickets today and be part of this extraordinary event.



Thank You to Our Sponsors:


We would like to extend our heartfelt gratitude to the following sponsors for their generous support in making this event possible:


• Silent Ocean


• KCB Bank


• CRDB Bank


• Ashton Media


• Mjini FM


• Clouds Media


• Vista Print


• Infinity Development


• Azam


Your contributions are helping to make this event a truly remarkable and impactful gathering.


Share:

Saturday, September 14, 2024

Benki ya Biashara DCB kuendelea kuboresha Maisha ya Watanzania

Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro (wa nne kulia) akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Sabasaba Moshingi baada ya kumaliza Mkutano Mkuu wa 22 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam leo.

*Yajivunia kutoa Mikopo ya zaidi ya Shs Bilioni 740 Tokea Ilipoanzishwa

BENKI YA BIASHARA YA DCB imesema itaendelea kusimamia misingi ya kuanzishwa kwake ambayo ni kusaidia miradi endelevu ya kupunguza umasikini, kuendeleza jamii na kutoa huduma bora zinazokidhi mahitaji halisi ya kila siku ya wateja wao.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki ya Biashara DCB, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Sabasaba Moshingi alisema, tokea kuanzishwa kwa DCB, takriban miaka 22 iliyopita benki hiyo imeendelea kukua mwaka hadi mwaka ikiendelea kutoa masuluhisho tofauti kwa wateja wake wa kada zote na hivyo kudhihirisha ukweli kuwa DCB ni ‘Mkombozi wa Kweli’ wa maisha ya watanzania.

Ikiwa ni Mkutano wake Mkuu wa kwanza tokea ajiunge na DCB, Bw. Moshingi akileta uzoefu wake wa miongo kadhaa katika tasnia za kibenki anasema benki inaendelea kujivunia kuwa kiongozi katika kuleta ufumbuzi wa tatizo la mitaji ya kibiashara kwa wajasiriamali wadogo wadogo kwa kuingiza sokoni bidhaa zenye ubunifu na kwa kutumia teknolojia za kisasa zinazoendana na mageuzi ya sayansi na teknolojia yanayoendelea duniani kote.

Benki ya Biashara DCB imekuwa mstari wa mbele katika kutoa mikopo kwa wajasiriamali wadogo wanaopata changamoto za kupata huduma hizo katika baadhi ya taasisi za kifedha kutokana na kutokidhi masharti waliyoweka, lakini pia tumeendelea kufanya vizuri katika mikopo ya watu binafsi na vikundi vya wajasiriamali huku tukiendelea kuboresha mikopo hiyo ili iendane na mahitaji yao, kwa kipindi cha miaka 22 tokea DCB imeanzishwa, tunajivunia kutoa mikopo yenye thamani ya zaidi ya shs bilioni 741 iliyowanufaisha zaidi ya watanzania 420,000”, alisema Bwana Moshingi.

Katika kipindi hiki cha mwaka mmoja tokea mkurugenzi mtendaji huyu mpya aingie madarakani, Benki ya biashara DCB imepiga hatua kadhaa za maendeleo ikiwa ni pamoja uimarishaji wa huduma za kibenki kwa njia za kidigitali pamoja na kuanzisha mikopo yenye lengo la kuinua maisha ya makundi maalumu hususan wanawake wajasiriamali.

Tumeanzisha huduma maalumu iitwayo ‘Tausi’ ikiwalenga wanawake yenye lengo la kuinua vipato vya wanawake wajasiriamali wadogo, tukianzia na mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Dodoma kwa kutoa mikopo ya kuendeleza biashara zao, kuwapa elimu ya kifedha pamoja na mbinu za uendeshaji wa biashara".

Sifa za kuwa mwanachama lazima uwe mkazi wa eneo husika, uwe na biashara, tukitumia mfumo wa kikundi kinachoanzia watu 15 hadi 30 wenye umri kuanzia miaka 18 mpaka 65, huku mikopo ikianzia 300,000 hadi milioni 1 kutegemea na aina ya biashara ya mteja na marejesho ni kati ya miezi mitano hadi 10”.

Bwana Moshingi anaongeza kuwa mbali na mikopo ya wanawake, DCB pia imeendelea kufanya vizuri katika mikopo mingine ya vikundi, mikopo ya nyumba, mikopo ya wafanyakazi hususan walimu, mikopo ya guta, pikipiki na bajaji na mingineyo.

Kwa upande wa huduma za jamii, benki yetu imekuwa mstari wa mbele pia katika kuisaidia serikali yetu katika kuwaletea watu wake maendelea hususan katika nyanja za elimu na afya kupitia miradi yetu mbalimbali inayoendelea, bila kusahau akaunti maalumu ya elimu ya DCB Skonga yenye lengo la kuboresha elimu ya watoto wetu".

Mwaka jana tulikabidhi madawati katika shule tano za Manispaa zote za jiji la Dar es Salaam na kauli mbiu isemayo ‘Elimu Mpango Mzima na Mama Samia’ tukikusudia kukabidhi madawati 1000 katika shule mbalimbali nchini kati ya mwaka 2023 na 2025, mradi huu unaendelea vizuri na wiki ijayo tutakabidhi baadhi ya madawati haya katika Shule ya Msingi ya Msisiri B, Kinondoni, jijini Dar es Salaam”, alisema.

Aidha anaongeza, “Ukiacha hayo benki yetu imeendelea kuwa mstari wa mbele katika kuuunga mkono serikali yetu katika miradi yake ya kimkakati kama tulivyofanya hivi karibuni tulipodhamini walimu 1000 kutoka Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwenda kufanya utalii katika mbuga za mikumi kwa kutumia treni ya SGR, kwa kufanya hivyo tunasaidia kuitangaza treni hii pamoja na utalii wa nchi yetu ndani na nje ya Tanzania”.

Pamoja na hayo mkurugenzi huyo anasema DCB imeendelea pia kufanya vizuri katika huduma na akaunti nyingine zikiwemo; Wahi Akaunti, akaunti ya mshahara, mikopo ya nusu mshahara, akaunti za wastaafu, huduma za malipo ya serikali (GePG) pamoja na malipo mengine kwa watoa huduma mbalimbali yanayofanyika katika matawi ya benkina kwa njia za mtandao.

Kaimu Mkurugenzi wa Fedha DCB, Bwana Siriaki Surumbu alisema benki imeendelea kukuza mapato ikijikita katika shughuli za utoaji mikopo yenye ubora hasa kwa vikundi maalum vya wanawake na wajasiliamali mbalimbali. Maboresho katika vitengo mbalimbali vya huduma hususan huduma za kidigitali ambazo zitaongeza ufanisi katika utoaji huduma na kuongeza mapato ya benki.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro alisema benki imekuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan katika ajenda yake ya kuona huduma za kibenki zinawafikia watanzania wote wakifanya huduma zao za kibenki kwa njia za kidigitali kuwa bora zaidi na zenye gharama nafuu.

Bi Nanyaro alisema kwa sasa mkakati wa kuhahakisha huduma zake zinapatikana nchi nzima unaendelea vizuri ukiwezeshwa na uimarishaji wa huduma hizo, kusambaa kwa mtandao wa mawakala zaidi ya 1000 nchini kote pamoja na vituo vidogo 1500 vya kutolea huduma katika maeneo ya kimkakati.

Nipende kutoa shukurani kwa serikali yetu chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira yanayosaidia sekta ya fedha kufanya biashara katika mazingira bora na wezeshi, lakini pia kwa kuona umuhimu wa kushirikisha sekta binafasi katika miradi ya kimkakati inayoendelea kwa mafanikio katika sehemu mbalimbali nchini".

Nipende pia kuwahakikishia wanahisa wetu, wateja wetu na wadau wetu kuwa benki yenu ipo katika mikono salama na inaendelea vizuri chini ya uongozi wa Bwana Moshingi, menejimenti, wafanyakazi wote pamoja na Bodi ya wakurugenzi".

Tunachohitaji tu ni ushirikiano kutoka kwenu wanahisa wote, wadau pamoja na wateja wetu ili benki yetu izidi kufanya vizuri sokoni na kutekeleza mikakati yote ya maendeleo tuliyojiwekea".

Natoa wito kwa watanzania wote kujiunga na benki yetu na kufaidika na fursa mbalimbali za huduma bora za kibenki tunazozitoa, DCB ni Mkombozi wa Kweli kwa watanzania wote, Wajasiriamali wadogo na wa kati, wanawake na vijana, DCB ni Mkombozi wa Kweli kwa wafanyabiashara wa kada zote”, anamaliza Bi Nanyaro.
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro, akizungumza na wanahisa wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika kwa jijini Dar es Salaam leo. Bi Zawadia alisema DCB Itaendelea kusimamia misingi ya kuanzishwa kwake ambayo ni kusaidia miradi endelevu ya kupunguza umasikini, kuendeleza jamii na kutoa huduma bora zinazokidhi mahitaji halisi ya kila siku ya wateja wao.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Sabasaba Moshingi , akizungumza na wanahisa wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. Bwana Moshingi aliwaambia wanahisa kuwa DCB chini ya uongozi wake, kwa kushirikiana na Bodi pamoja na wafanyakazi wote wamejizatiti kuandika upya historia ya benki hiyo na hii ikianza kuonekana baada ya DCB kufanya vizuri katika robo ya kwanza na ya pili mwaka huu.
Mwanasheria Mshauri wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Alex Mgongolwa, akizungumza na wanahisa wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bodi ya Ukaguzi na Usimamizi wa Benki ya Biashara ya DCB, Prof. Tadeo Satta, akizungumza na wanahisa wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Sabasaba Moshingi (kulia) akizungumza na baadhi ya wawakilishi wa wanahisa wa benki hiyo wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Bw. Selemani Kateti, Mwakilishi kutoka UTT AMIS, Bw. Medson Enock na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni, Bw. Rajab Gondomo.

Kuhusu DCB

Benki ya Biashara ya DCB ilianzishwa mwaka 2002 na mwaka unaofuata kupewa leseni ya kujiendesha kama benki ya kijamii, ikijulikana kama Benki ya Watu wa Dar es Salaam ‘Dar es Salaam Community Bank’ ambayo wanahisa wake waanzilishi wakiwa ni Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam pamoja na Manispaa zake za Ilala, Kinondoni na Temeke. Wanahisa wengine ni Mifuko ya NHIF na UTT AMIS pamoja na wananchi wa kawaida.

Kuanzishwa kwa DCB kulitokana na maono ya Rais mstaafu wa awamu za tatu, Hayati Benjamin William Mkapa kutoka na kilio cha wananchi wenye kipato cha chini na cha kati kukosa mikopo ya mitaji katika benki za kibiashara kutokana na kutokidhi vigezo vilivyowekwa.

Katika miaka hii 22 tokea kuanzishwa kwa DCB, benki imepitia hatua mbalimbali; ilikuwa benki ya kwanza kuorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es salaam (DSE) mnamo mwaka 2008, ambapo Februari 2012 ilifanikiwa kuhuisha leseni yake kutoka benki ya kijamii na kuwa benki kamili ya kibiashara na kubadilisha jina kutoka Benki ya Watu wa Dar es Salaam na kuwa Benki ya Biashara ya DCB.

Benki ya DCB ina mtandao wa matawi 9 ya kibenki ndani na nje ya Dar es Salaam ikiwa na mtandao wa mawakala 1000 na vituo vya kutolea huduma 1500 sehemu mbalimbali nchini. Ina zaidi ya mashine 280 za ATM zilizounganishwa na Umoja Switch, lakini pia inatumia Kadi za Visa zinazoweza kutumika katika mashine zinazosapoti kadi hizo ndani na nje ya nchi.
Share:

Wednesday, September 11, 2024

TUME YA SAYANSI YA TEKNOLOJIA YAANZISHA MFUMO KUWASAIDIA WASICHANA NA WANAWAKE KIDIJITALI

KATIKA kuwasaidia Wasichana na Wanawake kumudu maisha na kuisaidia jamii Tume ya Sayansi na Teknolojia ( Costech), imezindua Program mbili kwa ajili ya kuwajengea uwezo kidijitali.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 10, 2025 jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Costech, Dkt. Amos Nungu amesema kuwa Program hizo ni kwa ajili ya wasichana ambao hawakumaliza masomo yao na Wanawake wenye mawazo au biashara zinazohusiana na Teknolojia.


Lengo ni kuwapa ujuzi na taaluma ya kiteknolojia ili waweze kuja na biashara ambazo zinaweza zikasaidia waweze kumudu maisha yao, na wasaidie jamii.


Dkt. Nungu amesema Program ya kwanza inajulikana kama 'Future Femtech' inayowasaidia wanawake wenye kampuni changa au mawazo machanga ya kiteknolojia.


Amesema Program ya pili ijulikanayo kama 'Kuzatech' inaangalia mabinti ambao walikuwa shule lakini kwa namna moja au nyingine wakashindwa kuendelea na masomo hivyo wamewapa fursa ya kupata mafunzo kidijitali.


"Sasa hizi Program mbili tunazifanya kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo,"amesema.


Nungu amesema Kuzatech wataunganika na Future Femtech ambao baadhi yao ni wahitimu wa vyuo vikuu wenye mawazo ya biashara ambapo wadogo wanapata fursa ya kuungana na hawa wakubwa ili waweze kupata mafunzo yatakayowasaidia kuwa nankitu cha kufanya.


Kwa upande wake Meneja Usimamizi na Uhaulishaji Teknolojia Costech, Dkt. Erasto Mlyuka amesema Program hiyo ya Future Femtech inawalenga wasichana ambao wamekuwa ni waanzilishi wa kampuni changa.


Amesema hupewa msaada wa kitaalam kwa maana ya mafunzo elekezi ya kujengewa uwezo pia kupewa fedha za kuwawezesha kufanya biashara zao.


Amesema program hizo zitatengeneza ajira kwa wanawake ili na wenyewe wapate nafasi ya kuchangia kwenye pato la nchi kwa kuwa na kipato halali.


Mbunifu kutoka Arusha, ambaye ni mnufaika wa Future Femtech, Pamela Chogo amesema mafunzo aliyoyapata ni chachu kubwa kwenye ubunifu wa biashara.


Amesema Program hizo ni muhimu kwa sababu zinasaidia kupata elimu ya ujasiriamali.
Share:

Monday, September 2, 2024

BENKI YA KCB YAUNGAMKONO KUWEZESHA IBADA YA SHUKRANI SHULE YA MARIAN BAGAMOYO YATOA MILIONI 30.

BENKI Ya KCB imewezesha kwakutoa Shilingi milioni 30 katika sherehe ya shukrani ya Marian Schools, iliyojumuisha mbio za miguu, matembezi, na misa ya shukrani.
Mkurugenzi wa Biashara wa Benki hiyo Cosmas Kimario na Mgeni rasmi wa sherehe hizo ,aliipongeza Taasisi za Marian kwa mafanikio makubwa waliyoyafikia kielimu, kijamii, na kiuchumi.

Kimario alisisitiza kuwa tangu kuanzishwa mwaka 1997, Taasisi za Marian zimeonyesha dhamira thabiti ya kutoa elimu bora na kuzalisha wahitimu wenye mchango mkubwa katika jamii na tija kazini.

Aliendelea kwa kueleza jinsi Marian ilivyopanua shughuli zake kutoka shule moja, Marian Girls Secondary School, hadi kuwa na shule tatu za sekondari, zahanati, hoteli, na chuo kikuu (Marian University), kilichoanzishwa mwaka 2014.

Mafanikio haya yameleta mabadiliko chanya katika elimu, jamii, na uchumi wa taifa. Wahitimu wa Marian Schools wameiva kielimu na kinidhamu, wakitoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya taifa.

Kwa upande wake Meneja wa Shule za Marian Valentine Bayo alitoa historia fupi ya Taasisi za Marian, akisema: "Mnamo mwaka 1991 nilitumwa hapa na wakubwa wangu wa Shirika la Roho Mtakatifu (Holy Ghost Fathers) kama padre kijana kwa kazi ya uinjilishaji.

Kutokana na hali ya uduni wa eneo hili ambalo lilikuwa limesahaulika, tulianzisha juhudi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuanzisha shule za chekechea na ufundi. Hatimaye, juhudi hizi zilipelekea kujengwa shule ya sekondari ya wasichana ya Marian mnamo mwaka 1997.

Aidha katika ushirikiano kati ya Benki ya KCB na Taasisi za Marian kati ya mwaka 2021 na 2024, KCB Bank imewekeza katika miradi mbalimbali ya Taasisi za Marian, ikiwa ni pamoja na ukarabati wa shule za Marian Girls na Marian Primary, ujenzi wa majengo ya ghorofa sita kwa ajili ya madarasa na hosteli za Marian Boys School, na kuchangia baadhi ya gharama za uendeshaji wa taasisi hizi.

Sherehe hizi pia zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Askofu Mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu Zanzibar, Agustine Shao; Mkuu wa Shirika la Holy Ghost, Mhe. Shauri Selenda; Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo; Meneja na Mwanzilishi wa huuShirika la Roho Mtakatifu; wenyeviti wa bodi za Taasisi za Marian; pamoja na wazazi, wanafunzi, na wafanyakazi wa taasisi hizo.

Share:

KAMPUNI YA ORYX GAS TANZANIA YAMKOSHA WAZIRI WA NISHATI YAKABIDHI MITUNGI NA MAJIKO 1000 KWA MAMA NA BABA LISHE.

KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania yamkosha Naibu Waziri wa Nishati yakabidhi mitungi na majiko yake 1000 kwa washiriki wa mashindano ya kupika kwa gesi ya Oryx mkoani Mbeya ili kuwawezesha kurahisisha shughuli zao za mapishi.

Akizungumza wakati akihitimisha mashindano ya kupika kutumia Nishati ya ORYX kwa Mama na Baba Lishe wa Mkoa wa mbeya, Naibu Waziri Judith Kapinga aliyekuwa mgeni rasmi amesema Serikali imekuwa kinara wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini na lengo ni kufika asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia nishati mbadala kwaajili ya kupikia.
"Maombi ya wananchi kwa wadau wa gesi ni kupunguzwa kwa bei ya nishati hiyo ambayo kwa sasa ni ipo juu kulingana na kipato Cha wananchi ambao ndio watumiaji wakubwa wa Nishati hiyo. Tunashauri wadau katika sekta hii kutengenezwe mfumo ambao utakuwa rafiki kwa Mwananchi kununua gesi kidogo kidogo pindi anapokuwa na uhitaji."

Amesisitiza kukiwa na uwezo wa gesi kununuliwa kidogo kidogo anaamini wananchi wengi watatumia gesi na hivyo kusaidia kupunguza Kasi ya uharibu wa mazingira lakini pia kulinda afya za wananchi.

Naibu Waziri Kapinga amesema katika mwaka wa fedha uliopita wamegawa mitungi kwa wananchi na mwaka huu wa fedha wametenga fedha kwa ajili ya kuendelea kugawa nishati mbadala ya kupikia kwa wananchi huku akisisitiza kuwa Rais DK.Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuona asilimia kubwa ya Watanzania wanatumia nishati hiyo.
Kuhusu mashindano hayo ya mapishi, Naibu Waziri Kapinga amempongeza Spika wa Bunge Dk.Tulia Ackson kuandaa mashindano hayo makubwa na kushirikisha Mama na Baba Lishe 1000 kushindana kupika kwa gesi kwani yamekuwa ya mfano na yametumika kutoa elimu ya nishati na utunzaji mazingira.

Naibu Waziri pia amewashukuru Oryx gas kwa kuendelea kuishika mkono Serikali katika kusaidia kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, wanafanya kazi nzuri na wamekuwa wakifika kila mahali wakigawa mitungi na majiko yake kwa jamii.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Gas Tanzania Benoit Araman amesema lengo kuu la mashindano ya mapishi ni kuhamasika matumizi ya nishati safi kwa lengo la kulinda mazingira ambayo yamekuwa yakiharibiwa kwasababu ya kukata kuni na mkaa.
"Kwa miaka zaidi ya 15 iliyopita upatikanaji wa nishati ya kupikia umekuwa ukipangwa na kujadiliwa lakini hivi sasa Serikali inayoongozwa na Rais DK.Samia Suluhu Hassan amekuwa na hamasa kubwa ya kuhimiza wananchi kutumia nishati safi ya kupikia."

"Oryx Gasi tunaamini kupika kwa gesi kunakwenda kusaidia kulinda mazingira sambamba na kupunguza muda mwingi kwa wanawake kuwa porini kutafuta kuni na mkaa kwa ajili ya kuanda chakula.Pia kupika kwa gesi kutasaidia kuwalinda wanawake dhidi ya wanyama wakali walioko misitu lakini kuwalinda dhidi ya vitendo vya ukatilii ambavyo wanakutana navyo wakiwa porini."Amesema Benoit.

Ameongeza "pamoja na kusaidia makundi mbalimbali kuyawawezesha kupata mitungi ya gesi ya Oryx lakini wanajivunia kuwafikia Mama na Baba Lishe zaidi ya 12000 ambao wamepata elimu ya matumizi salama ya kupika kwa gesi sambamba na kuwapa mitungi midogo na mikubwa kwa lengo la kuwawezesha kufanya shughuli za mapishi kwa urahisi na kuwa salama kiafya," amesema.

Kwa upande wao baadhi ya Mama na Baba Lishe walioshiriki mashindano ya kupika kwa gesi wamesema kupitia mashindano hayo wamenufaika na mafunzo waliyoyapata sambamba na kuelezwa umuhimu wa kutunza mazingira na wanatoa shukrani kwa waandaaji wakiongozwa na Spika wa Bunge na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini Dk.Tulia Ackson.
Share:

Tuesday, August 27, 2024

ORYX GAS TANZANIA YAMTUA MZIGO WA KUNI NA MKAA MAMA NA BABA LISHE MKOANI MBEYA


MAMA na BABA LISHE MKOANI mbeya wameingia Kwenye kinyang'anyiro cha kutafuta mpushi bora anaeweza  kutumia gesi ya Kampuni ya Oryx Gas huku  lengo la mashindano hayo ni kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia  kama ambavyo Rais Dk.Samia amedhamiria kuhakikisha asilimia 80 ya watanzania iwe inatumia nishati hiyo.
Akizungumza na wana habari mkoani hapa leo Agosti 27,2024 jijini Mbeya , Meneja Miradi ya Nishati Safi kutoka Kampuni ya Oryx Gas Tanzania Peter Ndomba amesema mashindano hayo yanatija kubwa kwa Mama Lishe na Baba Lishe kwani wanatambua kundi hilo ndilo linaloathirika kiafya kutokana na kutumia kuni na mkaa kwa muda mrefu.

"Mama baba Lishe anakaa muda mrefu anapokua anapopika kwa kutumia  mkaa kwani  tunaambiwa wananchi wengi wa Tanzania wanapoteza maisha kila mwaka kutokana na matatizo ya kupumua au matatizo ambayo yanatokana na madhara ya kuni na mkaa.

"Sasa katika kundi hilo tunaweza kusema Mama na Baba Lishe ndio waathirika wakubwa , hivyo ni jamii ambayo sasa hivi sisi Oryx tunamkakati wa kuhamasisha iachane na matumizi ya Kuni na mkaa. na kuni  na mkaa kwasababu wao ndio wanakaa jikoni muda mrefu katika kupika kila siku ndani ya siku 365,"amesema Ndomba.

Amesisitiza kwa hiyo Mama Lishe na Baba Lishe waanze kubadilika na kuanza kutumia nishati safi hivyo kutawasaidia kukabiliana na changamoto za kiafya na kuokoa maisha yao, mashindano ya kupika kwa gesi ya Oryx kunalenga kuliepusha kundi hilo dhidi ya madhara yanayotokana na matumizi  ya kuni na mkaa.
"Lengo la mashindano haya ni katika muendelezo  ambao Oryx tumeuanza muda mrefu wa kuhamasisha na kusaidia kuhakikisha  matumizi ya nishati safi ya kupikia katika mapishi.


Kwa hiyo ujumbe wetu kwa watu watumie gesi katika kupika mapishi.Tunaamini nishati safi ya kupikia ni suluhisho la changamoto nyingi hasa za kiafya,kimazingira na kiuchumi,"amefafanua.
Share:

Thursday, August 15, 2024

TCB YAKUTANA NA SPIKA WA BUNGE LA TANZANIA KUJADILI NAMNA BORA YA KUKUZA SEKTA YA FEDHA.

Katika jitihada za kuimarisha ushirikiano baina ya taasisi za kifedha na mihimili ya Serikali, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara Tanzania (TCB), Bw. Adam Mihayo, amemtembelea na kuzungumza na Spika wa Bunge la Tanzania, Mheshimiwa Tulia Ackson.  

Bw. Mihayo ameambatana na Mkurugenzi wa Biashara za Wateja Wadogo na wa Kati wa benki hiyo Bi. Lilian Mtali, katika ziara hiyo ambayo inafungua ukurasa mpya wa ushirikiano baina ya Benki ya TCB na Bunge la Tanzania katika kuwainua wajasiriamali wadogo na wa kati nchini.  

Mazungumzo na kiongozi huyo wa Bunge linaloundwa na wabunge 393 kutoka majimbo 239 yamejikita katika masuala nyeti yanayohusu majimbo mbalimbali katika jitihada za kuendelea kuwainua wajasiriamali wadogo na wa kati. 

Wakitambua mchango mkubwa wa kundi hili katika ukuaji uchumi na uzalishaji wa ajira mpya, mazungumzo yao yamejikita katika mpango wa utoaji wa mikopo yenye riba nafuu kwa wajasiriamali. Miradi hii itasaidia kukuza na kuchochea mazingira ya biashara kwa wajasiriamali pamoja na biashara zao. 

“Lengo letu sio kutoa jibu moja kwa nchi nzima. Huwezi kuwa na suluhisho moja kwa watu wote, ndiyo maana ni muhimu kuwasikiliza wadau wengi iwezekanavyo. Njia hii itatusaidia kutoa majibu yatakayokidhi mahitaji ya wajasiriamali kulingana maeneo wanayoishi hata wale walioko vijijini,” amesema Bw. Mihayo. 

Kwa upande wake, Mheshimiwa Tulia Ackson amebainisha umuhimu wa ushirikiano huo na kusisitiza wajibu wa Bunge katika kutunga sera zinazowezesha maendeleo ya wajasiriamali na kuhakikisha kwamba biashara zao zinapata rasilimali zinazohitajika ili kukua. “Maendeleo ya wajasiriamali ni muhimu kwa ukuaji uchumi wa taifa letu, kupitia ushirikiano huu na Benki ya TCB, tunaweza kutengeneza mazingira yatakayowezesha ukuaji wa biashara,“ amesema. 

Kikao hicho kimehitimishwa kwa azimio la ushirikiano wa pamoja na kuendelea kubuni nyanja mbalimbali za ushirikiano lengo likiwa kuinua sekta ya wajasiriamali.




Share:

ZAIDI YA WANAHISA 5000 WA MWANGA HAKIKA BANK WASHIRIKI MKUTANO MKUU WA NNE WA WANAHISA.

Mwenyekiti  wa Bodi ya  Wakurugenzi ya Mwanga Hakika Benki, Mhandisi Rithuan Mringo (watatu kushoto), akizungumza na wanahisa wa benki hiyo wakati wa Hafla ya Mkutano Mkuu wa nne wa wanahisa wa Benki hiyo uliyofanyika Wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro wengine pichani kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Jagjit Singh, Makamo Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa Mwanga Hakika benki  Mhandisi Raymond Thadeus , Pamoja na viongozi wengine wa bodi hiyo.
Makamo Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa Mwanga Hakika benki  Mhandisi Raymond Thadeus (wapili kushoto), akizungumza na wanahisa wa benki hiyo wakati wa Hafla ya Mkutano Mkuu wa nne wa wanahisa wa Benki hiyo uliyofanyika Wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro wengine pichani ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Jagjit Singh, Mwenyekiti  wa Bodi ya  Wakurugenzi ya Mwanga Hakika Benki, Mhandisi Rithuan Mringo Pamoja na viongozi wengine wa bodi hiyo.
Wanahisa wa Mwanga Hakika Bank wakiwa katika usahili kwaajili ya kushiriki Mkutano huo.
Wanahisa wa Mwanga Hakika Bank wakifuatilia Mkutano huo.


Benki ya Mwanga Hakika Imefanya mkutano mkuu wa nne na wanahisa wa benki hiyo yaani AGM (Annual General Meeting) wilayani Mwanga, mkoani Kilimanjaro.
Mkutano huu una lengo la kutimiza matakwa ya serikali inavyoagiza kila kampuni kufanya mkutano mkuu na wanahisa wao kila mwaka.


Akizungumza wakati ,mkutano huo  Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi  wa Mwanga Hakika Benki Mhandisi Ruthuan Mringo ameeleza kuwa mkutano huo ulikuwa na lengo la kuendelea kuimarisha mahusiano mazuri  yaliyopo baina ya wanahisa na benki yao, ili kuwataarifu wanahisa  kuhusu benki ilipoanza ilipo sasa na mwendelezo wake ili kuweza kupata taarifa kamili na Ili wanahisa hao waweze kutathmini maendeleo ya benki hiyo na kubaini kama Kuna changamoto ziweze kutatuliwa. 

 Pia wanahisa  wanayo nafasi kubwa ya kutoa ushauri juu ya maswala ya kimaendeleo yatakayo ikuza benki hiyo ili iendelee kuwa imaara siku hadi siku.


Mkutano huu ni mkutano wa nne na wanahisa wa benki ya Mwanga Hakika, ambapo mkutano wa kwanza ulifanyika mwaka  (2021) na kuhudhuriwa na wanahisa mbalimbali, kwa lengo la kuimarisha uhusiano wao na wanahisa wa benki hiyo. Amesema Mringo.


Mbali na hayo, benki ya Mwanga Hakika imekuwa ni desturi yetu kufanya mkutano huo wilayani Mwanga, mkoani Kilimanjaro kwasababu benki hiyo ch

Benki hiyo imeendelea kuimarika siku hadi siku na kwamba tangu kuanzishwa kwake mwaka 2020 kumekuwepo ongezeko la amana za wateja kutoka Sh80.06 bilioni kwa mwaka 2022 hadi kufikia Sh142.19 bilioni sawa na ongezeko la asilimia 78.

Aidha amesema ukuaji wa mikopo kwa wateja umeongezeka kutoka Sh80.69 bilioni hadi kufikia Sh131.44 bilioni.

"Ukuaji huu unaonyesha uwezo wetu wa kusaidia wateja wetu kufikia malengo yao ya kifedhabkwa kuwapatia mikopo yenye masharti nafuu,"amesema Mringo 

Amesema jumla ya mali za benki hiyo zimeongezeka na kufikia Sh208.93 bilioni, ikilinganishwa na Sh116.95 bilioni mwaka 2022 ambapo ni sawa na ongezeko la asilimia 79.

"Mapato yetu ya Benki yamefikia Sh20.06 bilioni kutoka Sh 13 .41 bilioni mwaka 2022, ongezeko la asilimia 50 , ukuaji huu unatokana na juhudi zetu za kuboresha huduma na kuongeza Wigo kwa wateja wetu,"amesema Mringo
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive