A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Friday, October 24, 2025

Benki ya Absa Tanzania na ASA Microfinance Yaadhimisha Miaka Minne ya Mafanikio katika Kuwawezesha Wanawake na Kubadilisha Jamii

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (Katikati), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, wakati akitangaza mafanikio ya ushirikiano wa kibiashara kati ya benki hiyo na taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance kwa kipindi cha miaka minne. Kupitia ushirikiano huo, Benki ya Absa imeikopesha ASA kiasi cha shs billioni 40 zilizoiwezesha taasisi hiyo kutoa mikopo kwa wanawake wajasiriamali zaidi ya 50,000 kutoka sehemu mbalimbali nchini Tanzania. Wengine kutoka kushoto ni, Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa, Bi. Abigail Lukuvi, Mkurugenzi wa wateja wa Makampuni wa Absa, Nellyana Mmanyi, Ofisa Mtendaji Mkuu wa ASA Microfinance Tanzania, Bw. Muhammad Shah Newaj na Meneja Mahusiano ya Jamii na Utawala wa ASA, Bi. Veneranda Francis.

Benki ya Absa Tanzania, kwa ushirikiano na taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance, inajivunia kuadhimisha mwaka wa nne wa ushirikiano wa kipekee ambao umewezesha zaidi ya wanawake wajasiriamali 50,000 nchini Tanzania kupata mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 40 za Kitanzania.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2022, ushirikiano huu wa muda mrefu umeenda zaidi ya kutoa mikopo pekee, kila mwanamke mjasiriamali aliyewezeshwa si tu anabadilisha maisha yake binafsi, bali pia anagusa maisha ya familia yake, wafanyakazi, wasambazaji, na jamii pana inayomzunguka. Utafiti wa maendeleo unaonyesha kwamba kumwezesha mjasiriamali mmoja mwanamke nchini Tanzania kunaweza kuinua maisha ya watu 15 hadi 20 walioko karibu naye, hii inamaanisha kwamba ushirikiano kati ya Benki ya Absa na ASA Microfinance umegusa maisha ya karibu watanzania milioni moja, ukiimarisha familia na kuchochea ukuaji jumuishi wa kiuchumi.

Akizungumza kuhusu mafanikio haya jijini Dar es Salaam leo katika mkutano na waandishi wa habari, Obedi Laiser, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, alisema: “Taasisi nyingi huzingatia uwezeshaji wa wanawake kama mradi wa muda mfupi, kwa Absa, hili ni jukumu lenye kusukumwa na dhamira ya kweli. Kwa kuwawezesha zaidi ya wanawake 50,000 kupata mitaji na kukuza biashara zao, tunaona athari chanya zinazopanuka, zinazobadilisha familia, kuelimisha watoto, kuunda ajira, na kujenga ustahimilivu katika jamii. Hivi ndivyo tunavyoishi kauli mbiu yetu ya Kuiwezesha Afrika ya kesho, pamoja… hatua moja baada ya nyingine, kwa sababu kwetu Absa, Stori yako ina thamani.

Kwa upande wake, Muhammad Shah Newaj, Ofisa Mtendaji kuu wa ASA Microfinance Tanzania, aliongeza:

Ushirikiano wetu na Benki ya Absa Tanzania umeleta mageuzi makubwa. Kupitia msaada wa Absa, ASA imeweza kupanua huduma za mikopo midogo kwa maelfu ya wanawake wajasiriamali ambao wangeachwa nje ya mfumo rasmi wa kifedha. Pamoja, hatufadhili biashara pekee , tunafadhili heshima, matumaini, na fursa zinazoinua vizazi.

Katika kipindi cha miaka minne iliyopita, ushirikiano huu umeunganisha utoaji wa mitaji na mafunzo ya elimu ya kifedha, kuhakikisha kwamba wanawake wajasiriamali hawapati mikopo tu bali pia maarifa ya kuiendesha kwa uendelevu. Mapema mwezi huu, wanawake 50 kutoka Dar es Salaam walishiriki katika programu ya elimu ya kifedha iliyojumuisha mada za upangaji bajetiakibauwekezaji, na utunzaji wa kumbukumbu, hatua muhimu katika kubadilisha mikopo kuwa uwezeshaji endelevu wa kiuchumi.

Mpango huu unaonyesha mkakati wa Uwajibikaji wa Kijamii wa Absa, unaolenga ujumuishaji wa kifedha, ujasiriamali, na maendeleo endelevu. Pia unaendana na ajenda ya kitaifa ya ujumuishaji wa kifedha nchini Tanzania kwa kupanua huduma za mikopo na elimu kwa makundi yasiyohudumiwa ipasavyo, hivyo kuleta mabadiliko ya kudumu ya ustahimilivu wa kiuchumi.

Kupitia ushirikiano huu endelevu, Benki ya Absa Tanzania na ASA Microfinance zinaendelea kuandika simulizi za mabadiliko , simulizi ambazo mwanamke mmoja aliyewezeshwa hubadilisha si maisha yake tu, bali pia maisha ya wengi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (wa tatu kushoto), akikabidhi tuzo kwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, Bw. Muhammad Shah Newaj, kwa kutambua mchango wa taasisi hiyo, katika kuwawezesha wanawake wajasiriamali nchini, kwa kupitia masuluhisho mbalimbali ya kifedha. Ilikuwa ni katika hafla ambayo Absa ilitangaza mafanikio ya ushirikiano wa kibiashara kati ya benki na taasisi hiyo kwa kipindi cha miaka minne. Kupitia ushirikiano huo, Benki ya Absa imeikopesha ASA kiasi cha shs billioni 40 zilizoiwezesha taasisi hiyo kutoa mikopo kwa wanawake wajasiriamali zaidi ya 50,000 kutoka sehemu mbalimbali nchini Tanzania. Wengine kutoka kushoto ni, Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa, Bi. Abigail Lukuvi, Mkurugenzi wa wateja wa Makampuni wa Absa, Bi. Nellyana Mmanyi, na Meneja Mahusiano ya Jamii na Utawala wa ASA Microfinance, Bi. Veneranda Francis.
Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigal Lukuvi (kushoto), akizungumza katika hafla ambayo, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Obedi Laiser (wa tatu kushoto), akitangaza mafanikio ya ushirikiano wa kibiashara kati ya benki hiyo na taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance kwa kipindi cha miaka minne. Kupitia ushirikiano huo, Benki ya Absa imeikopesha ASA kiasi cha shs billioni 40 zilizoiwezesha taasisi hiyo kutoa mikopo kwa wanawake wajasiriamali zaidi ya 50,000 kutoka sehemu mbalimbali nchini Tanzania. Wengine kutoka kushoto kwake ni, Mkurugenzi wa wateja wa Makampuni, Bi. Nellyana Mmanyi, Ofisa Mtendaji Mkuu wa ASA Microfinance Tanzania, Bw. Muhammad Shah na Meneja Mahusiano ya Jamii na Utawala wa ASA, Bi. Veneranda Francis.
Share:

Saturday, October 18, 2025

BENKI YA ABSA TANZANIA YAZINDUA KLABU YA MATEMBEZI NA MBIO FUPI IKIHAMASISHA UMUHIMU WA MAZOEZI KWA AFYA YA MWILI NA AKILI

Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Melvin Saprapasen (katikati) na Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha wa Absa Tanzania, Bi.Irene Rwegalulira (kushoto) wakizindua rasmi Klabu ya matembezi na mbio fupi ya benki hiyo itakayoshirikisha wafanyakazi wa kitengo hicho na wateja wao. Hafla hii ilifanyika jijini Dar es Salaam leo. Klabu hiyo itaendesha matembezi hayo mara mbili kwa mwezi ikiwa na malengo ya kuimarisha mahusiano kati ya benki na wateja na pia kuhamasisha umuhimu wa mazoezi ya mwili kwa ustawi wa afya ya mwili na akili.
Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (kulia) akiwatangulia baadhi ya wafanyakazi na wateja wa kitengo cha biashar, wakati wa uzinduzi rasmi wa Klabu ya matembezi na mbio fupi ya benki hiyo itakayoshirikisha wafanyakazi wa kitengo hicho na wateja. Hafla hii ilifanyika jijini Dar es Salaam leo. Klabu hiyo itaendesha matembezi hayo mara mbili kwa mwezi ikiwa na malengo ya kuimarisha mahusiano kati ya benki na wateja na pia kuhamasisha umuhimu wa mazoezi ya mwili kwa ustawi wa afya ya mwili na akili.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Absa Tanzania kitengo cha biashara pamoja na wateja wao, wakishiriki matembezi na mbio fupi jijini Dar es Salaam leo katika hafla ya uzinduzi rasmi wa Klabu ya matembezi na mbio fupi ya benki hiyo itakayoshirikisha wafanyakazi wa kitengo hicho na wateja. Klabu hiyo itaendesha matembezi hayo mara mbili kwa mwezi ikiwa na malengo ya kuimarisha mahusiano kati ya benki na wateja na pia kuhamasisha umuhimu wa mazoezi ya mwili kwa ustawi wa afya ya mwili na akili.
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Absa Tanzania kitengo cha biashara pamoja na wateja, wakipiga picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi rasmi wa Klabu ya matembezi na mbio fupi ya benki hiyo itakayoshirikisha wafanyakazi wa kitengo hicho na wateja. Klabu hiyo itaendesha matembezi hayo mara mbili kwa mwezi ikiwa na malengo ya kuimarisha mahusiano kati ya benki na wateja na pia kuhamasisha umuhimu wa mazoezi ya mwili kwa ustawi wa afya ya mwili na akili.
Share:

Tuesday, October 14, 2025

Absa Tanzania Celebrates Innovation and Inclusion at GirlCode Hackathon 2025

Absa Bank Tanzania Director of Technology, Mr. Emanuel Mwinuka (fourth from left), speaks with participants of the program titled “Absa GirlCode Hackathon 2025,” in which female university students were required to develop digital codes that provide solutions to support the banking sector and other industries. The event took place in Dar es Salaam over the weekend.

Absa Bank Tanzania has reaffirmed its commitment to empowering women in technology with the successful conclusion of the GirlCode Hackathon 2025, a high-energy, 36-hour innovation challenge that brought together young women coders, developers, and entrepreneurs from across the country.

The event, held in partnership with the Women in Tech Centre and Girl Code Africa, provided a platform for participants to develop digital solutions addressing real-world challenges in Fintech, Artificial Intelligence, and Cybersecurity.

In her closing address in Dar es Salaam over the weekend, the Director of Human Resources at Absa Bank Tanzania, Mr Patrick Foya commended the participants for their creativity, determination, and problem-solving spirit.

Your solutions stood out not only for their technical excellence but also for their potential to make a real difference, you’ve tackled complex challenges with boldness and brilliance, you’ve proven that innovation knows no gender, and that the future of technology is brighter because of you”, he said.

The HR Director also emphasized that the hackathon was more than a competition-it was a platform for learning, growth, and transformation where participants collaborated to design solutions ranging from ecosystem banking platforms to AI-powered optimization engines, demonstrating that young Tanzanian women are ready to lead the next wave of technological innovation.

When women are given the opportunity, they don’t just participate, they lead,” he added. “The next generation of tech leaders is already here.

Highlighting Absa’s role in nurturing female talent, the Director reiterated the bank’s commitment to creating inclusive pathways for women in technology in line with Absa’s purpose of Empowering Africa’s Tomorrow, Together, One Story at a Time, under the brand message “Your Story Matters.”.

Events like this are not just about coding, they’re about creating pipelines,” he said. “We are identifying talent, nurturing potential, and opening doors, Absa Bank Tanzania is committed to ensuring that young women who participated here today have access to opportunities such as internships, mentorships, and future employment.

Addressing those who did not win awards, the HR Director offered a message of encouragement; “Every great technologist has faced setbacks,” he reminded them. “What matters is how you respond, take what you’ve learned here and keep building, keep dreaming, and keep pushing boundaries.

One of the participants in the challenge, Mariam Saidi Mohammed, a computer software developer, expressed her gratitude to Absa Bank together with the GirlCode Hackathon for organizing the event, saying that it had helped her build confidence in finding solutions to various challenges through technology.

I would like to encourage all women with ideas not to be afraid, come forward, you can solve many problems through technology,” said Ms. Mariam.

Speaking at the event, the Bank’s Director of Technology, Mr. Emanuel Mwinuka, said that the Absa GirlCode Hackathon will help address the gender imbalance among computer systems professionals in the country, which has been a major challenge in many workplaces.

This challenge is not only in banks but also in other industries. That is why we at Absa decided to encourage young women from universities and workplaces to take advantage of opportunities in the world of technology and also provide solutions through technology."

Today’s event has been very successful, we have had three winners, since this event is also taking place in other countries, the first-place winner will have the opportunity to compete with winners from other nations through their solutions, and the best solution will receive another award,” said Mr. Mwinuka.

The Girl Code Hackathon 2025 was concluded with award presentations, networking sessions, and a shared commitment to sustaining the momentum of empowering women in the tech ecosystem.
The Director of Human Resources at Absa Bank Tanzania, Mr. Patrick Foya (second from right), presents a certificate to the first-place winners, the Tokiva Sisters team, during the “Absa GirlCode Hackathon 2025” program, where female university students were required to create digital codes offering solutions beneficial to the banking sector and other industries. The event was held in Dar es Salaam over the weekend. From right: Absa Bank’s Director of Operations, Mr. Oscar Mwamfwagasi, and Director of Technology, Mr. Emanuel Mwinuka.
The Director of Operations at Absa Bank Tanzania, Mr. Oscar Mwamfwagasi (right), presents a certificate to the third-place winners, the Tech Divas team, during the “Absa GirlCode Hackathon 2025” program, where female university students were required to design digital codes offering solutions to support the banking sector and other industries. The event was held in Dar es Salaam over the weekend.
Absa Bank Tanzania Citizenship and Events Manager, Abigail Lukuvi (centre), speaks with some of the participants of the “Absa GirlCode Hackathon 2025” program, where female university students were required to create digital codes that provide solutions to benefit the banking sector and the broader community. The event took place in Dar es Salaam over the weekend.
Share:

Monday, October 13, 2025

TANZANIA KUSHINDANA VIPENGELE 20 TUZO ZA UTALII DUNIANI

Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru (katikati), akizungumza na waandishi wa habari jijini  Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kampeni ya upigaji kura wa tuzo  za kimataifa zinazotambua na kuthamini ubora, ubunifu na huduma bora katika sekta ya utalii na usafiri duniani. Wengine pichani kutoka (kushoto), ni Meneja Mawasiliano wa Bodi hiyo Paulina Mkama pamoja na Meneja Masoko wa Vivian Temi,


‎Meneja Mawasiliano wa Bodi yaUtaliiTanzania(TTB), hiyo Paulina Mkama (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini  Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kampeni ya upigaji kura wa tuzo  za kimataifa zinazotambua na kuthamini ubora, ubunifu na huduma bora katika sekta ya utalii na usafiri duniani. (Katikati), ni Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru pamoja na Meneja Masoko wa wa bodi hiyo  Vivian Temi

.com/img/a/

Na Mwandishi Wetu 

Tanzania imeingia kwenye kinyang’anyiro cha  Tuzo za Dunia za Utalii ( World Travel Award 2025) baada ya kuteuliwa kushiriki katika vipengele 20  vyenye  wagombea 24 vikiwemo taasisi na wadau mbalimbali wa sekta ya utalii.


Akizungumza Oktoba 13, 2025 jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kampeni ya upigaji kura, Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amesema  hatua hiyo ni ya kihistoria kwani inaonyesha jinsi Tanzania inavyozidi kutambulika kimataifa.


“Kwa kawaida Tanzania imekuwa ikishinda katika tuzo za ngazi ya Afrika , lakini mwaka huu tumeingia katika mashindano ya dunia, mwaka  jana tulichaguliwa kama nchi bora kwa safari za utalii, jambo ambalo limeendelea kuitangaza nchi yetu zaidi,” amesema  Mafuru.


Ameeleza kuwa  World Travel Award( WTA) ni tuzo za kimataifa zinazotambua na kuthamini ubora, ubunifu na huduma bora katika sekta ya utalii na usafiri duniani.


“Tuzo hizi zilianzishwa mwaka 1993, na kwa sasa zinajulikana kama, Oscars za sekta za Utalii , kutokana na heshima na ushawishi wake katika kuonyesha viwango vya juu vya ubora duniani,” amefafanua  Mafuru.


Mafuru amesema  lengo la tuzo hizo ni kutambua na kuhamasisha ubora katika nyanja zote za utalii, ikiwemo mashirika ya ndege, hifadhi za taifa, hoteli, miji ya kitalii, kampuni za usafiri na taasisi za utalii za kitaifa kama TTB.


Amewahamasisha watanzania wote kujitokeza kupiga kura kupitia simu zao na mitandao ya kijamii katika kampeni iliyoanza  oktoba 6 hadi  oktoba 16,2025 , ili Tanzania iweze kushinda katika vipengele mbalimbali ikiwemo Nchi bora ya Utalii, Bodi Bora ya Utalii, Hifadhi Bora, Kivutio Bora na Uwanja bora wa ndege.


“Ushindi katika tuzo hizi utaongeza hadhi ya Tanzania katika sekta ya utalii duniani, kuongeza idadi ya watalii na kuimarisha juhudi za kulinda rasilimali na urithi wa taifa,” amesema .


Aidha, Mafuru amesisitiza  kuwa mafanikio yanayoonekana sasa ni matokeo ya uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii, chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ambaye amekuwa kinara katika kutangaza vivutio vya utalii kupitia ziara na filamu ya Royal Tour pamoja na hotuba zake

Share:

Sunday, October 5, 2025

BENKI YA ABSA TANZANIA KUENDELEA KUWAWEZESHA WAJASIRIAMALI WENGI ZAIDI NCHINI

Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (kulia), akizungumza na baadhi ya wanawake wajasiriamali, wanachama wa taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, katika semina iliyoandaliwa na taasisi hiyo kwa uwezeshaji wa benki hiyo ikihusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo haya ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo ya kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la Benki ya Absa la Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine, kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, Mr. Muhammed Shah Newaj (kulia), akizungumza kuhusu mahusiano ya kibiashara kati ya taasisi hiyo na Benki ya Absa Tanzania, wakati wa semina ya wanawake wajasiriamali wanachama wa taasisi hiyo kuhusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo haya ni sehemu ya mikakati ya Benki ya Absa katika kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la benki hiyo la 'Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine', kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Mkufunzi wa masuala ya kifedha, Bw. Edmund Munyagi (kulia), akifundisha kuhusu 'Usimamizi Binafsi wa Fedha' wakati wa semina iliyoandaliwa na Taasisi ya huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania na kuwezeshwa na Benki ya Absa Tanzania, ikishirikisha wanawake wajasiriamali wanachama wa taasisi hiyo jijini Dar es Salaam jana. Semina hiyo iliyohusu elimu ya kifedha na usimamizi wa biashara wenye tija ni sehemu ya mikakati ya Benki ya Absa nchini ya kuwawezesha wajasiriamali sambamba na Lengo la benki hiyo la Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine, kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Mmoja wa wanawake wajasiariamali mwanachama wa Taasisi ya huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, akichangia hoja wakati wa semina kuhusu elimu ya kifedha na usimamizi wa biashara wenye tija, iliyoandaliwa na taasisi hiyo ikiwezeshwa na Benki ya Absa Tanzania, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo haya ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo katika kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la benki hiyo la 'Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine', kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Baadhi ya wanawake wajasiriamali wanachama wa Taasisi ya huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania, wakishagilia wakati Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi akizungumza nao wakati wa semina kuhusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, iliyoandaliwa na Taasisi ya ASA Microfinance Tanzania kwa uwezeshaji wa benki hiyo, jijini Dar es Salaam jana. Semina hiyo ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo katika kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la benki hiyo la 'Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine', kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.
Meneja Huduma za Jamii na Matukio wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Abigail Lukuvi (katikati), baadhi ya wafanyakazi wa Taasisi inayotoa huduma za kifedha ya ASA Microfinance Tanzania na wanachama wao, wakionesha alama ya ushindi mara baada ya semina iliyoandaliwa na taasisi hiyo kwa uwezeshaji wa benki hiyo ikihusu elimu ya kifedha na jinsi ya kusimamia biashara kwa ufanisi, jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo hayo ni sehemu ya mikakati ya benki hiyo ya kuwawezesha wajasiriamali nchini sambamba na Lengo la Benki ya Absa la Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja, hatua moja baada ya nyingine, kupitia chapa ya benki hiyo inayosema 'Stori yako ni ya thamani'.

Share:

Monday, September 29, 2025

Airtel Africa Foundation unveils plan for improving 10 million lives in Africa by 2030

Airtel Africa Foundation, the philanthropic arm of Airtel Africa plc, today unveiled its plans to directly improve the lives of 10 million people across the continent by 2030. The strategy will be delivered through targeted initiatives under four core pillars namely Financial Empowerment, Education, Environmental Protection and Digital Inclusion (FEED).

Outlining the ambitious target, Dr. Segun Ogunsanya, Chairman of the Airtel Africa Foundation, stated, “Our 2030 vision is a transformed Africa where over 10 million lives are directly improved through our interventions. We are not just donating resources, we are building a pipeline of talent and fostering innovation to ensure the global digital revolution leaves no African behind. This is a strategic, measurable commitment to unlocking the continent's demographic dividend.

The Foundation’s mission will be executed by creating a cycle of empowerment through targeted programmes. These include ‘Connecting Schools’, which provides free connectivity and devices, and the ‘Airtel Africa Fellowship’, offering full undergraduate scholarships in tech and STEM fields, complemented by mentorship and internships.

A key early success underscoring the Foundation's impact is its ongoing partnership with UNICEF. This collaboration has already connected more than 1,800 schools, benefitted over one million students, and trained more than 17,000 teachers in digital education across the Foundation’s 14 markets of operation.

In addition, the Foundation will leverage its dedicated Employee Volunteer Programme, channelling the skills and passion of its people directly into community initiatives. For the 2025/26 financial year, the Foundation has set specific expansion targets, with programmes now active across all its operating countries, from Nigeria to Zambia, Malawi, Rwanda, and the Democratic Republic of the Congo.

Commenting on the company's support for the Foundation, Airtel Africa’s Chief Executive Officer, Sunil Taldar, said, “We cannot thrive in a place that is not thriving. This understanding is the very reason the Airtel Africa Foundation was born. It is our vehicle to catalyse transformation, by systematically investing in the pillars that underpin a resilient and dynamic society. We have remained dedicated to transforming lives both as a business imperative as well as our overarching philosophy. For us, helping to connect the unconnected, banking the unbanked and enabling businesses and economies to thrive are the three most significant objectives of our business.
Share:

Thursday, September 25, 2025

LG Electronics yafungua duka jipya la kisasa jijini Dar es Salaam

 

Kutoka Kushoto ni Meneja Mkaazi wa kampuni ya LG Tanzania, Aashim Wadhw, Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania (MeTL) Indrabhuwan Singh, na Mkurugenzi wa F&S, Frank Rwamlima, pamoja na Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya (MeTL) Fatma Dewji, wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi Duka jipya la LG Electronics Mlimani City, Dar es Salaam.”

Dar es Salaam, Septemba 24, 2025 – Kampuni ya LG Electronics Kanda ya Afrika Mashariki imezindua duka jipya la bidhaa zake (brandshop) katika Kituo cha Ununuzi cha Mlimani City jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha uwepo wake kwenye soko la Afrika Mashariki.

Duka hilo jipya limefunguliwa kwa ushirikiano na kampuni ya F&S pamoja na msambazaji rasmi wa bidhaa za LG nchini, METL. Hatua hiyo inalenga kuongeza urahisi wa upatikanaji wa bidhaa za LG huku wateja wakipewa huduma za kisasa zenye viwango vya kimataifa.

Akizungumza wakati wa uzinduzi, Meneja wa LG Electronics Tanzania, Aashim Wadhwa alisema“Duka hili jipya ni uthibitisho wa dhamira ya LG kuendelea kuwapatia wateja wa Tanzania teknolojia za kisasa na huduma bora zaidi. Dar es Salaam ni jiji lenye kasi kubwa ya ukuaji, na tunaona fursa kubwa ya kushirikiana na ukuaji huo kwa kuwakaribia zaidi wateja wetu na kuhakikisha wanapata msaada wa baada ya mauzo kwa kiwango cha juu.”

Katika duka hili, wateja wataweza kushuhudia na kutumia moja kwa moja ubunifu wa hivi karibuni wa LG, ikiwemo vifaa vya nyumbani (home appliances), vifaa vya burudani majumbani (home entertainment systems) na suluhisho za hali ya hewa (HVAC). Pia kutakuwa na huduma ya haraka, usaidizi wa baada ya mauzo na uhakika wa kupata bidhaa halisi.

Mwakilishi wa F&S alisema Frank Mwamlima-F&S Tunafurahia kushirikiana na LG na METL kuwaletea Watanzania uzoefu wa ununuzi wa kisasa.

 Duka hili litawawezesha wateja kuona na kutumia bidhaa za LG moja kwa moja, na hivyo kuwasaidia kufanya maamuzi sahihi ya ununuzi katika mazingira ya kiwango cha kimataifa.

”kwa upande wake, mwakilishi wa METL aliongeza kuwa“Uzinduzi huu ni ishara ya uhusiano unaozidi kukua kati ya METL na LG East Africa. LG ni chapa inayotambulika duniani kwa ubora na uimara wake, na duka hili linaonesha dhamira yetu ya pamoja ya kuwaletea Watanzania bidhaa zenye viwango vya juu, imara na za kuaminika.”

Kwa mujibu wa tafiti, soko la vifaa vya nyumbani Afrika Mashariki linatarajiwa kukua kwa wastani wa asilimia 6.55 kila mwaka, huku familia nyingi zikielekeza kipaumbele katika teknolojia endelevu na zenye kuokoa gharama.


Duka jipya la LG jijini Dar es Salaam ni sehemu ya mkakati mpana wa upanuzi wa kampuni hiyo katika ukanda wa Afrika Mashariki, ambapo tayari imejitanua katika nchi mbalimbali zikiwemo Kenya, Sudan, Ethiopia, Tanzania, Somalia, Uganda, Zambia, Sudan Kusini na Rwanda. Kupitia uwekezaji huu, LG inalenga kuongeza upatikanaji wa bidhaa zake, kuboresha huduma kwa wateja na kuimarisha uzoefu wa matumizi ya teknolojia za kisasa.

Share:

Sunday, September 21, 2025

Airtel Tanzania yaifikisha SmartWASOMI kwa walimu wa IT visiwani Zanzibar

Ofisa Vifaa vya Intaneti wa Mradi wa Airtel SmartWASOMI, Bw. Harrison Isdory (kushoto), akitoa maelekezo kuhusu matumizi ya baadhi ya vifaa vya intaneti katika warsha iliyoandaliwa kwa walimu wa IT, mjini Zanzibar hivi karibuni, iliyoandaliwa na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data.

Airtel Tanzania, kupitia Airtel Africa Foundation na kwa kushirikiana na UNICEF pamoja na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imeendesha warsha ya mafunzo kwa walimu wa Zanzibar mwishoni mwa wiki, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wa Airtel SmartWASOMI. Mpango huu wa elimu ya kidijitali unalenga kuongeza upatikanaji wa elimu bora kupitia teknolojia kote nchini Tanzania.

Warsha hiyo iliwaunganisha walimu 36 kutoka shule mbalimbali za sekondari ambazo tayari zimeunganishwa na jukwaa la Airtel SmartWASOMI. Tangu uzinduzi wake mwezi Mei 2024 na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, mpango wa Airtel SmartWASOMI umefikia zaidi ya shule 400 na umeleta athari chanya kwa maelfu ya walimu na wanafunzi nchini. Jukwaa hili linatoa huduma ya bure ya mtandao kwa rasilimali muhimu za kielimu, ikiwa ni pamoja na maudhui yaliyoidhinishwa na Taasisi ya Elimu Tanzania (TIE) na Shule Direct, hivyo kuwawezesha walimu na wanafunzi kujifunza bila wasiwasi wa gharama za data.

Mgeni rasmi katika tukio hilo, Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari Zanzibar, Bi. Asia Iddy Issa, alisifu mpango huo na kusisitiza kwamba unakwenda sambamba na malengo ya kitaifa.

Mpango huu unasaidia ndoto yetu ya kuunda kizazi chenye uelewa wa kidijitali na unatatua changamoto zilizokwamisha upatikanaji wa nyenzo bora za kujifunzia, hasa katika maeneo yenye uhitaji mkubwa kwa kuwajengea uwezo walimu na kuondoa kikwazo cha gharama za data, tunapunguza pengo kati ya mbinu za kiasili za ufundishaji na ufundishaji wa kisasa,” alisema Asia.

Akaendeleo kusema, “Tunakaribisha kwa moyo mmoja suluhisho kama hili bunifu, kwani linakamilisha juhudi zetu za kuimarisha mfumo wa elimu kwa njia ya kidijitali, tunatarajia kuona shule nyingi zaidi Zanzibar zikifaidi kupitia Airtel SmartWASOMI, na tumejizatiti kushirikiana na wadau wote kuhakikisha kuna matokeo ya kudumu.

Akizungumza kwa niaba ya Wizara ya Elimu, Mkuu wa Idara ya Elimu ya Sekondari Zanzibar, Mfaume Jaffary Mfaume ambaye pia alifungua warsha hiyo, alisisitiza umuhimu wa kuwaunga mkono walimu katika mabadiliko ya kidijitali.

Warsha hii inawawezesha walimu kutumia kwa ufanisi zana za kidijitali ili kuboresha utoaji wa somo, kurahisisha upangaji wa masomo, na kuleta matokeo bora ya kujifunza, Airtel SmartWASOMI ni njia rahisi, thabiti na jumuishi ya kuwaunganisha walimu na wanafunzi na rasilimali bora za kujifunzia bila gharama za data,” alisema.

Katika warsha hiyo, walimu walipata mafunzo ya vitendo kuhusu namna ya kuvinjari maudhui ya mitaala, kuunganisha rasilimali za kidijitali katika masomo yao, na kufuatilia ushiriki wa wanafunzi kwa ufanisi zaidi. Pia walihimizwa kujifunza kwa kushirikiana, kushirikiana mawazo, na kujenga mtandao wa walimu waliowezeshwa kwa njia ya kidijitali.

Walimu waliohudhuria walielezea shukrani zao kwa Airtel Africa Foundation, UNICEF na serikali kwa kuanzisha mpango unaosaidia mbinu za kisasa, zinazopatikana kwa urahisi na zenye ufanisi katika shule.

Kwa upande wake, Yussuf Mwadini Haji, mwalimu wa Shule ya Sekondari Hamamni, alisema, “Kabla ya warsha hii, wengi wetu hatukujua uwezo mkubwa wa zana za kidijitali. Sasa najisikia kuwa na ujasiri na hamasa ya kufanya masomo yangu yawe ya kuvutia zaidi kwa wanafunzi.

Mwalimu mwingine, Amina Hamza Shaabani kutoka Shule ya Sekondari Forodhani, aliongeza, “Airtel SMARTWASOMI imefungua fursa mpya. Sasa tunapata maudhui ya kisasa bila gharama za data, jambo ambalo limepunguza mzigo mkubwa.

Mafunzo haya ni sehemu ya dhamira pana ya Airtel Tanzania ya kuunganisha zaidi ya shule 1,000 ifikapo mwisho wa mwaka 2025. Kampuni hiI ya mawasiliano inaendelea kuwekeza katika miundombinu ya kidijitali, ushirikiano na jamii, pamoja na kushirikiana kwa karibu na wadau ili kupanua wigo na manufaa ya mpango wa Airtel SmartWASOMI. Mpango huu unachangia moja kwa moja malengo ya taifa ya kuboresha uelewa wa kidijitali, kupunguza pengo la elimu, na kuhakikisha walimu na wanafunzi katika maeneo yote wanapata elimu bora ya kidijitali.
Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari visiwani Zanzibar, Bi. Asia Iddy Issa, akizungumza katika katika warsha iliyoandaliwa kwa walimu wa IT, mjini Zanzibar hivi karibuni, iliyoandaliwa na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data.
Ofisa Vifaa vya Intaneti wa Mradi wa Airtel SmartWASOMI, Bw. Harrison Isdory (kushoto), na Mratibu wa Elimu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TIE), Bw. Charles Manyama (kulia), wakiangalia wakati Mwalimu wa Shule ya Sekondari Hammamni ya mjini Zanzibar, Bw. Yussuf Mwadini Haji, akifanya usajili katika mfumo wa TIE, wakati wa warsha iliyoandaliwa kwa walimu hao, visiwani humo, jana, iliyoandaliwa na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data.
Ofisa Vifaa vya Intaneti wa Mradi wa Airtel SmartWASOMI, Bw. Harrison Isdory (kulia), akizungumza na baadhi ya walimu wa IT mjini Zanzibar, katika warsha iliyoandaliwa kwa walimu hao, na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data.
Baadhi ya walimu wa IT mjini Zanzibar hivi karibuni, wakiwa katika warsha iliyoandaliwa kwa walimu hao na Airtel Tanzania kupitia Airtel Africa Foundation, kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Wizara ya Elimu, chini ya mpango wa Airtel SmartWASOMI, unaolenga kuboresha elimu ya kidigitali kwa kuwawezesha walimu na wanafunzi kupata maudhui ya kielimu kupitia maktaba mtandao ya Taasisi ya Elimu Tanzania na Shule Direct bila gharama ya vifurushi vya data.
Share:

Sunday, August 31, 2025

DK.MWINYI:CCM ITAFANYA KAMPENI ZA KISTAARABU KWA SERA ZENYE TIJA KWA WANANCHI

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ambaye pia ni Mgombea Mteule wa Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo katika Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na kuahidi kuwa CCM itafanya kampeni za kistaarabu zitakazozingatia Utamaduni, Silka na Desturi za Wazanzibari.

Dkt. Mwinyi amechukua fomu hiyo katika Afisi za Tume ya Uchaguzi leo, tarehe 30 Agosti 2025, asubuhi, na hatimaye msafara wake ukaelekea Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui kupitia Barabara ya Miembeni, Kariakoo, Rahaleo na Michenzani, akisindikizwa na mamia ya wanachama wa chama hicho waliokuwa wamejipanga pembezoni mwa barabara.

Aidha, Dkt. Mwinyi amezuru Kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Hayati Abeid Amani Karume, na kisha kuzungumza na Wazee wa Chama Cha Mapinduzi afisini hapo.

Akizungumza na mamia ya wanachama wa CCM katika Uwanja wa Mao Tse Tung, Mgombea Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesisitiza kuwa CCM itafanya kampeni zitakazoepuka chuki, mifarakano na ubaguzi miongoni mwa wananchi, na badala yake kufanya kampeni zitakazowaunganisha Wazanzibari kwa kuzingatia maslahi yao ya kijamii na kiuchumi.

Ameeleza kuwa katika kampeni hizo, CCM itaonesha mafanikio yaliyopatikana katika awamu ya kwanza ya Uongozi wa Awamu ya Nane pamoja na utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2025–2030, ambayo itawasilishwa kwa wananchi wakati wa kampeni.

Aidha, ametoa wito kwa wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla kuungana na kuwapigia kura wagombea wote walioteuliwa na chama hicho katika nafasi zote kuanzia Urais, Ubunge, Uwakilishi na Udiwani ili kuhakikisha CCM inaendelea kushika dola.

Halikadhalika, Dkt. Mwinyi amewahakikishia wananchi kuwa CCM itaendelea kudumisha hali ya utulivu na amani iliyopo nchini wakati wa kampeni, uchaguzi na baada ya uchaguzi.
Share:

Thursday, August 28, 2025

Absa Bank Tanzania champions CEO collaboration and investment at The 200 CEOs Business Forum as Diamond Sponsor

Deputy Permanent Secretary in the Ministry of Industry and Trade, Honorable Dr. Suleiman Hassan Serera (left), presents a certificate of appreciation to Absa Bank Tanzania Managing Director, Mr. Obedi Laiser, in recognition of Absa’s ‘Diamond’ sponsorship during the 3rd edition of the 200 CEOs Business Forum, held in Dar es Salaam yesterday.

Dar es Salaam, Absa Bank Tanzania reaffirmed its commitment to powering growth in Tanzania’s real economy as the Diamond Sponsor of The 200 CEOs Business Forum, an exclusive convening of the nation’s top corporate leaders.

The high-level forum was graced by Deputy Permanent Secretary, Ministry of Industry and Trade, Honorable Dr. Suleiman Hassan Serera, as the Guest of Honor, alongside senior government dignitaries including the Minister of Finance, Minister of Construction, Minister of Investment and Plan, the Commissioner, Tanzania Revenue Authority, the Permanent Secretary, Ministry of Finance, and the Governor, Bank of Tanzania, among others.

The Forum advanced a clear public–private agenda. Opening perspectives from the Tanzania Investment Centre (TIC), Tanzania National Business Council (TNBC), Zanzibar Investment Promotion Authority (ZIPA) and the Tanzania Association of Management Consultants (TAOMAC) framed a pro-investment outlook. Senior government principals set near-term priorities to boost competitiveness, and the Guest of Honour’s keynote called for coordinated action to scale jobs and exports. A macro update from the Bank of Tanzania guided boardroom planning, while Absa’s sponsor briefing linked tailored financing and risk solutions to execution on the ground. Three focused dialogues then addressed leadership and governance, health and workforce resilience, and the financing pathways to unlock growth - culminating in PPP insights from the national centre and a celebratory gala recognising excellence across industries.

Absa’s Diamond Sponsorship underscores the bank’s long-term partnership with Tanzania’s public and private sectors to accelerate inclusive growth. By convening policy-makers and industry leaders in one room, the forum enables practical alignment on regulations, bankable projects and risk-sharing structures that catalyse investment at scale—turning ambition into action.

Speaking at the event, Mr. Obedi S. Laiser, Managing Director, Absa Bank Tanzania, said: “This forum is more than a meeting of minds; it is a platform for decisions that move capital, create jobs, formalise value chains, and unlock export potential. As Absa, we are proud to stand with Tanzania’s business leaders at this pivotal moment. Our purpose -‘Empowering Africa’s tomorrow, together… one story at a time’ - comes alive when we back the ambitions of CEOs and entrepreneurs with practical, well-priced, and timely financial solutions.

Your Story Matters is not just a promise - it is how we show up. We listened closely to the priorities and needs of CEOs and in response, deliver solutions designed for business momentum, including the Absa Infinite Card, Absa Business Credit Card, Vehicle Asset Finance (VAF), comprehensive Cash Management and Payments capabilities, Trade & Working Capital solutions, Treasury & Risk Management, and our digital corporate banking platforms that help finance teams operate with speed and control.” Mr. Laiser added.

Throughout the day, CEOs engaged with Absa’s representatives at the Absa solutions booth. Executives explored seamless travel and spend control with the Absa Infinite Card, streamlined expenses via the Absa Business Credit Card, and fleet and equipment renewal through Vehicle Asset Finance/Commercial Asset Finance. Risk protection and liquidity planning were front and centre with Bancassurance and the Flexi Fixed Deposit, while relationship-led banking under our Prestige and Premier offering, and cross-border convenience through Diaspora Banking met the needs of affluent and international clients. Public-sector attendees also experienced the speed and convenience of e-Loans for Government Employees—all reinforcing Absa’s promise that Your Story Matters.
Absa Bank Tanzania Managing Director, Mr. Obedi Laiser (left), makes a contribution on the topic “Finance as a Catalyst for Business Growth in Tanzania: Strategy & Opportunities” during a panel discussion at the Absa-sponsored 3rd edition of the 200 CEOs Business Forum, held in Dar es Salaam yesterday. Seated beside him are his fellow panelists.
Absa Bank Tanzania Managing Director, Mr. Obedi Laiser (centre), displays a certificate of appreciation shortly after it was presented to him by the Deputy Permanent Secretary in the Ministry of Industry and Trade, Honorable Dr. Suleiman Hassan Serera (second left), during the 3rd edition of the 200 CEOs Business Forum, which was primarily sponsored by the financial institution, in Dar es Salaam yesterday. Looking on are some of the bank’s senior officials.
Share:

STANBIC BANK URGES LOCAL CAPITAL MOBILISATION TO BOOST SOE TRANSFORMATION

Tanzania’s Deputy Prime Minister, Hon. Dr. Doto Biteko (fourth right), presents a Certificate of Appreciation to Stanbic Bank Tanzania CEO, Manzi Rwegasira, for sponsoring the Chairpersons and CEOs Forum for Public Institutions, shortly after the conference concluded in Arusha.

Arusha, Tanzania’s state-owned enterprises (SOEs) must prioritise mobilisation of local capital and stronger financial pathways to succeed in the global economy, Stanbic Bank executives urged at the Chairpersons and CEOs Forum 2025.

Building Bridges Between Public and Private Sectors
Ester Manase Lobore, Executive Director and Head of Corporate & Investment Banking at Stanbic Bank Tanzania, described the Forum as a critical bridge connecting public and private sectors.

We see this as an opportunity to build a new bridge of cooperation – one that links the public and private sectors for the benefit of our nation,” she said.

Over the past five years, Stanbic has channelled over USD 1 billion in affordable financing into strategic projects, reinforcing the role of financial institutions in aligning investment with national priorities.

Leveraging Strengths for Transformation

Manzi Rwegasira, Chief Executive of Stanbic Bank Tanzania, emphasised that real transformation happens when SOEs provide foundational services and infrastructure, while the private sector brings capital, innovation, and expertise. He highlighted three key areas for future competitiveness:
  1. Financing transformative projects
  2. Digitising systems for efficiency and transparency
  3. Building institutional capacity through technical expertise
Government Engagement and Performance Tracking

Guest of Honour, Deputy Prime Minister Hon. Dr. Doto Biteko, highlighted the success of the six resolutions evaluated by the Treasury Registrar last year, with 90% already implemented.

Treasury Registrar Nehemia Mchechu launched the Performance Monitoring Dashboard for Public Institutions, a digital tool that tracks SOE performance in real-time, enabling better decision-making and accountability.

A Platform for Sustainable Synergies

Now in its third edition, the Chairpersons and CEOs Forum has become a leading platform for dialogue on SOE reform and global competitiveness. Discussions emphasised that sustainable synergies require government reforms and active private sector engagement.

For Stanbic Bank Tanzania, participating as a Resilience Sponsor, the Forum highlighted the bank’s role in supporting national priorities—not just through financing, but by sharing insights on how SOEs and private institutions can collaborate to secure Tanzania’s global economic standing.

ABOUT STANBIC BANK TANZANIA

Stanbic Bank Tanzania is a leading financial services provider, offering a wide range of banking solutions to individuals, businesses, and institutions. Committed to sustainable investment and strategic partnerships, Stanbic Bank plays a key role in Tanzania’s economic development and regional integration. The bank is part of the Standard Bank Group, Africa’s largest bank by assets, with a presence in 20 countries across the continent.

For more information, contact:
Dickson Senzi – Senior Manager, External Affairs, Communication and Reputation
Share:

Absa Bank Tanzania yasisitiza dhamira yake kuendeleza ukuaji wa uchumi halisi nchini Tanzania

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dk. Suleiman Hassan Serera (kushoto), akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser, kwa kutambua mchango wa benki hiyo kama mdhamini mkuu wa Kongamano la Biashara la tatu la Maofisa Watendaji Wakuu (200 CEO Business Forum), lililofanyika jijini Dar es Salaam jana.

Benki ya Absa Tanzania imeendelea kusisitiza dhamira yake ya kuendeleza ukuaji wa uchumi halisi wa nchini Tanzania, ikidhamini jukwaa mahsusi linalowakutanisha watendaji wakuu wa makampuni nchini, likijulikana kwa jina la ‘The 200 CEOs Business Forum’.

Jukwaa hilo la ngazi ya juu lilihudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda na Biashara, Dkt Suleiman Hassan Serera, sambamba na viongozi wengine waandamizi wa Serikali akiwemo Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), na wengineo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mgeni rasmi Dkt. Serera alisitiza umuhimu wa hatua za pamoja ili kupanua ajira na mauzo ya nje huku Benki Kuu ya Tanzania ikitoa mrejesho wa mwelekeo wa uchumi unaosaidia kupanga maamuzi ya bodi, na uwasilisho wa udhamini wa Absa ukugusia suluhisho za kifedha ambazo benki ya Absa inatoa kuwawezesha kampuni kuendesha na kusimamia biashara kwa urahisi ambapo katika mijadala mitatu iliyofanyika ikijikita katika uongozi na utawala bora, afya na uimara wa rasilimali watu, pamoja na njia za ufadhili zinazofungua ukuaji na kuhitimishwa na dira ya PPP.

Akizungumza katika hafla hiyo, Bw. Obedi Laiser, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania alisema Jukwaa hili si mkutano wa mawazo pekee bali ni chombo cha maamuzi yanayosukuma mitaji, kuunda ajira, kurasimisha minyororo ya thamani na kufungua fursa za mauzo ya nje akisema kama Absa, wanajivunia kusimama pamoja na viongozi wa biashara wa Tanzania katika wakati huu nyeti hususani kupitia dhamira yao ya “Kuiwezesha Afrika ya Kesho, Pamoja… hatua moja baada ya nyingine”.

Stori yako ina thamani” si ahadi tu, ndivyo tunavyojitokeza, tumesikiliza kwa makini vipaumbele na mahitaji ya wakurugenzi wakuu, na kwa kujibu tunawasilisha suluhisho zinazochochea kasi ya biashara, zikiwemo Absa Infinite Card, Absa Business Credit Card, Vehicle Asset Finance (VAF), uwezo mpana wa Cash Management & Payments, Trade & Working Capital, Treasury & Risk Management, pamoja na majukwaa yetu ya kidijitali ya benki kwa makampuni yanayosaidia idara za fedha kufanya kazi kwa kasi na udhibiti.

Tunawezesha malengo ya Watendaji wakuu (CEOs) na wajasiriamali kupitia suluhisho bora za kifedha, zenye bei shindani na zinazotolewa kwa wakati na umahiri.” Bw. Laiser aliongeza.

Udhamini huu mkubwa wa Absa unaonesha ushirikiano wa muda mrefu wa benki na Serikali na sekta binafsi wa kuharakisha ukuaji jumuishi. Kuwakutanisha watunga sera na viongozi wa viwanda katika ukumbi mmoja kunawawezesha kuoanisha kanuni, kuandaa miradi inayoweza kufadhiliwa na kuweka mifumo inayochochea uwekezaji kwa kiwango kikubwa - kigeuza dhamira kuwa utekelezaji.

Aidha watendaji hao walipata nafasi za kuzungumza na wafanyakazi wa Absa wakioneshwa suluhisho mbalimbali za kifedha zinazorahisisha maisha yao. Miongono mwa hizo ni huduma ya kifahari inayorahisisha safari za kimataifa kupitia Absa Infinite Card, udhibiti wa matumizi ya kampuni kwa Absa Business Credit Card, udhamini wa manunuzi ya magari binafsi na ya kibiashara kupitia Vehicle & Commercial Asset Finance. Ulinzi wa hatari na mipango ya ukwasi kupitia Bancassurance na Flexi Fixed Deposit, huduma za Prestige na Premier kwa wateja wa hadhi ya juu, Diaspora Banking ikirahisisha miamala ya kuvuka mipaka, na kwa upande wa sekta ya umma, e-Loans, yote yakithibitisha ahadi ya Absa kwamba Stori yako ina thamani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Absa Tanzania, Bw. Obedi Laiser (kushoto), akichangia mada isemayo “Fedha kama chachu ya ukuaji wa biashara Tanzania; Mikakati na Fursa”, wakati wa Kongamano la Biashara la tatu la Maofisa Watendaji Wakuu (200 CEO Business Forum), lililofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Share:

Airtel Money Yazindua “Airtel Money Ni Buree” na Ni Nafuu” kuongeza uhuru wa kufanya miamala Airtel Money

Balozi wa Airtel Money, Lukas Mhavile, akizunumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana wakati wa uzinduzi wa Kampeni za Airtel Money Ni Buree na Ni Nafuu, kulia ni Mkuruenzi wa Airtel Money, Andrew Rugamba, na kussoto ni Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Airtel, Jackson Mmbando. “Kampeni Airtel Money ni Bure na Ni Nafuu inaleta unafuu zaidi na kuwapa uhuru wa kufanya mambo mengi zaidi. Airtel Money Ni Bure, mteja ataweza kufanya miamala yake ya kutuma pesa Airtel Kwenda Airtel BURE kupitia my Airtel APP kiwango cha hadi milioni 5, Airtel Money Ni Nafuuu, mteja ataweza kutoa pesa chini ya kiwango cha shilingi 10,000 BURE Bila TOZO ya serikali. Hii inamaana ya kwamba Airtel tutalipa TOZO hiyo ili mteja wetu aweze kufanya muamala wake BURE kabisa.

Airtel Money Tanzania leo imetangaza uzinduzi wa kampeni mbili kabambe maalum kwa wateja wake wa Airtel Money itakayojulikana kama Airtel Money Ni Buree na Ni Nafuu, ikiwa na lengo la kuendelea kutoa uhuru zaidi kwa wateja wote wanaotumia Airtel Money.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika Makao Makuu ya Airtel Tanzania jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Airtel Money, Andrew Rugamba, alisisitiza manufaa ya kampeni ya Airtel Money ni Bure na Ni Nafuu:

Kampeni Airtel Money ni Bure na Ni Nafuu inaleta unafuu zaidi katika kutuma na kutoa pesa, ikiwasaidia wateja wetu kuokoa zaidi na kuwapa uhuru wa kufanya mambo mengi zaidi kwa fedha zao."

Airtel Money Ni Bure, mteja ataweza kufanya miamala yake ya kutuma pesa Airtel Kwenda Airtel BURE kupitia my Airtel APP kiwango cha hadi milioni 5,

Airtel Money Ni Nafuuu, mteja wetu ataweza kutoa pesa chini ya kiwango cha shilingi 10,000 BURE Bila TOZO ya serikali. Hii inamaana ya kwamba Airtel tutalipa TOZO hiyo ili mteja wetu aweze kufanya muamala wake BURE kabisa.

Uzinduzi huu unathibitisha dhamira ya Airtel kuunga mkono juhudi za Serikali za kukuza ujumuishi wa kifedha kupitia mifumo ya kidijitali na kuharakisha safari ya kuelekea kwenye uchumi usiotegemea pesa taslimu.

Airtel Money tunaamini huduma za kifedha zinapaswa kuwa nafuu, jumuishi na kupatikana kwa kila mmoja. Airtel Money kwa kuamua kubeba gharama za huduma za kutoa pesa chini ya shilingi elfu kumi, au kuwezesha Wateja wetu kutuma pesa Kiwango chochote BURE kupitia App yetu, tunajibu moja kwa moja mahitaji ya huduma bora na nafuu ambapo-hii itasaidia wateja wetu kuokoa pesa na kuzitumia kufanya mambo mengine iwe ni kununua umeme, muda wa maongezi au huduma nyingine. Hivi ndivyo tunavyosukuma mbele ujumuishi wa kifedha na kufanya miamala ya kidijitali kuwa nafuu kwa kila Mtanzania.

Rugamba aliongeza kuwa kampeni za Airtel Money Ni Buree na Ni Nafuu zimetengenezwa ili kuimarisha mfumo wa kifedha wa kidijitali nchini na kuongeza manufaa kwa wateja katika kila muamala wanaofanya.

Kwa upande wake, Meneja Uhusiano wa Airtel jackson Mmbando alisema: “Wateja wetu wametuambia wanataka huduma nafuu zaidi na rahisi zaidi. Airtel Money Ni Nafuu inaleta yote mawili. Airtel Money Ni Bureee na Nafuuu inathibitisha dhamira ya Airtel katika kutoa huduma za kifedha zilizo nafuu, bunifu na jumuishi ambazo zinaendana na dira ya kitaifa ya Tanzania ya kuwa na uchumi imara wa kidijitali.
Mkuruenzi wa Airtel Money, Andrew Rugamba, katikati akizunumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana wakati wa uzinduzi wa Kampeni za Ni Buree na ni Nafuu wakati wa kutoa pesa kutoka Airtel kwenda airtel kulia ni Balozi wa Airtel Maoney, Lukas Mhavile, na kusoto ni Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Airtel, Jackson M,bando. “Kampeni Airtel Money ni Bure na Ni Nafuu inaleta unafuu zaidi na kuwapa uhuru wa kufanya mambo mengi zaidi. Airtel Money Ni Bure, mteja ataweza kufanya miamala yake ya kutuma pesa Airtel Kwenda Airtel BURE kupitia my Airtel APP kiwango chochote yaani hadi milioni 5, Airtel Money Ni Nafuuu, mteja ataweza kutoa pesa chini ya kiwango cha shilingi 10,000 BURE Bila TOZO ya serikali. Hii inamaana ya kwamba Airtel tutalipa TOZO hiyo ili mteja wetu aweze kufanya muamala wake BURE kabisa.
Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Airtel, Jackson Mmbando, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana wakati wa uzinduzi wa Kampeni za Ni Buree na ni Nafuu ambapo sasa wateja wa Airtel Money wataweza kutoa pesa chini ya kiasi cha 10000 bila makato ya TOZO na pia Airtel Ni BURE wataweza kutuma pesa kiwango chohote BURE kupitia Airtel App (wakwanza kushoto) ni Mkurugenzi wa Airtel Money, Andrew Rugamba, katikati Balozi wa Airtel Money, Lukas Mhavile.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive