A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Saturday, September 14, 2024

Benki ya Biashara DCB kuendelea kuboresha Maisha ya Watanzania

Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro (wa nne kulia) akishikana mikono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Sabasaba Moshingi baada ya kumaliza Mkutano Mkuu wa 22 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika kwa njia ya mtandao jijini Dar es Salaam leo.

*Yajivunia kutoa Mikopo ya zaidi ya Shs Bilioni 740 Tokea Ilipoanzishwa

BENKI YA BIASHARA YA DCB imesema itaendelea kusimamia misingi ya kuanzishwa kwake ambayo ni kusaidia miradi endelevu ya kupunguza umasikini, kuendeleza jamii na kutoa huduma bora zinazokidhi mahitaji halisi ya kila siku ya wateja wao.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa Mwaka wa Wanahisa wa benki ya Biashara DCB, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Sabasaba Moshingi alisema, tokea kuanzishwa kwa DCB, takriban miaka 22 iliyopita benki hiyo imeendelea kukua mwaka hadi mwaka ikiendelea kutoa masuluhisho tofauti kwa wateja wake wa kada zote na hivyo kudhihirisha ukweli kuwa DCB ni ‘Mkombozi wa Kweli’ wa maisha ya watanzania.

Ikiwa ni Mkutano wake Mkuu wa kwanza tokea ajiunge na DCB, Bw. Moshingi akileta uzoefu wake wa miongo kadhaa katika tasnia za kibenki anasema benki inaendelea kujivunia kuwa kiongozi katika kuleta ufumbuzi wa tatizo la mitaji ya kibiashara kwa wajasiriamali wadogo wadogo kwa kuingiza sokoni bidhaa zenye ubunifu na kwa kutumia teknolojia za kisasa zinazoendana na mageuzi ya sayansi na teknolojia yanayoendelea duniani kote.

Benki ya Biashara DCB imekuwa mstari wa mbele katika kutoa mikopo kwa wajasiriamali wadogo wanaopata changamoto za kupata huduma hizo katika baadhi ya taasisi za kifedha kutokana na kutokidhi masharti waliyoweka, lakini pia tumeendelea kufanya vizuri katika mikopo ya watu binafsi na vikundi vya wajasiriamali huku tukiendelea kuboresha mikopo hiyo ili iendane na mahitaji yao, kwa kipindi cha miaka 22 tokea DCB imeanzishwa, tunajivunia kutoa mikopo yenye thamani ya zaidi ya shs bilioni 741 iliyowanufaisha zaidi ya watanzania 420,000”, alisema Bwana Moshingi.

Katika kipindi hiki cha mwaka mmoja tokea mkurugenzi mtendaji huyu mpya aingie madarakani, Benki ya biashara DCB imepiga hatua kadhaa za maendeleo ikiwa ni pamoja uimarishaji wa huduma za kibenki kwa njia za kidigitali pamoja na kuanzisha mikopo yenye lengo la kuinua maisha ya makundi maalumu hususan wanawake wajasiriamali.

Tumeanzisha huduma maalumu iitwayo ‘Tausi’ ikiwalenga wanawake yenye lengo la kuinua vipato vya wanawake wajasiriamali wadogo, tukianzia na mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Dodoma kwa kutoa mikopo ya kuendeleza biashara zao, kuwapa elimu ya kifedha pamoja na mbinu za uendeshaji wa biashara".

Sifa za kuwa mwanachama lazima uwe mkazi wa eneo husika, uwe na biashara, tukitumia mfumo wa kikundi kinachoanzia watu 15 hadi 30 wenye umri kuanzia miaka 18 mpaka 65, huku mikopo ikianzia 300,000 hadi milioni 1 kutegemea na aina ya biashara ya mteja na marejesho ni kati ya miezi mitano hadi 10”.

Bwana Moshingi anaongeza kuwa mbali na mikopo ya wanawake, DCB pia imeendelea kufanya vizuri katika mikopo mingine ya vikundi, mikopo ya nyumba, mikopo ya wafanyakazi hususan walimu, mikopo ya guta, pikipiki na bajaji na mingineyo.

Kwa upande wa huduma za jamii, benki yetu imekuwa mstari wa mbele pia katika kuisaidia serikali yetu katika kuwaletea watu wake maendelea hususan katika nyanja za elimu na afya kupitia miradi yetu mbalimbali inayoendelea, bila kusahau akaunti maalumu ya elimu ya DCB Skonga yenye lengo la kuboresha elimu ya watoto wetu".

Mwaka jana tulikabidhi madawati katika shule tano za Manispaa zote za jiji la Dar es Salaam na kauli mbiu isemayo ‘Elimu Mpango Mzima na Mama Samia’ tukikusudia kukabidhi madawati 1000 katika shule mbalimbali nchini kati ya mwaka 2023 na 2025, mradi huu unaendelea vizuri na wiki ijayo tutakabidhi baadhi ya madawati haya katika Shule ya Msingi ya Msisiri B, Kinondoni, jijini Dar es Salaam”, alisema.

Aidha anaongeza, “Ukiacha hayo benki yetu imeendelea kuwa mstari wa mbele katika kuuunga mkono serikali yetu katika miradi yake ya kimkakati kama tulivyofanya hivi karibuni tulipodhamini walimu 1000 kutoka Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwenda kufanya utalii katika mbuga za mikumi kwa kutumia treni ya SGR, kwa kufanya hivyo tunasaidia kuitangaza treni hii pamoja na utalii wa nchi yetu ndani na nje ya Tanzania”.

Pamoja na hayo mkurugenzi huyo anasema DCB imeendelea pia kufanya vizuri katika huduma na akaunti nyingine zikiwemo; Wahi Akaunti, akaunti ya mshahara, mikopo ya nusu mshahara, akaunti za wastaafu, huduma za malipo ya serikali (GePG) pamoja na malipo mengine kwa watoa huduma mbalimbali yanayofanyika katika matawi ya benkina kwa njia za mtandao.

Kaimu Mkurugenzi wa Fedha DCB, Bwana Siriaki Surumbu alisema benki imeendelea kukuza mapato ikijikita katika shughuli za utoaji mikopo yenye ubora hasa kwa vikundi maalum vya wanawake na wajasiliamali mbalimbali. Maboresho katika vitengo mbalimbali vya huduma hususan huduma za kidigitali ambazo zitaongeza ufanisi katika utoaji huduma na kuongeza mapato ya benki.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro alisema benki imekuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan katika ajenda yake ya kuona huduma za kibenki zinawafikia watanzania wote wakifanya huduma zao za kibenki kwa njia za kidigitali kuwa bora zaidi na zenye gharama nafuu.

Bi Nanyaro alisema kwa sasa mkakati wa kuhahakisha huduma zake zinapatikana nchi nzima unaendelea vizuri ukiwezeshwa na uimarishaji wa huduma hizo, kusambaa kwa mtandao wa mawakala zaidi ya 1000 nchini kote pamoja na vituo vidogo 1500 vya kutolea huduma katika maeneo ya kimkakati.

Nipende kutoa shukurani kwa serikali yetu chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira yanayosaidia sekta ya fedha kufanya biashara katika mazingira bora na wezeshi, lakini pia kwa kuona umuhimu wa kushirikisha sekta binafasi katika miradi ya kimkakati inayoendelea kwa mafanikio katika sehemu mbalimbali nchini".

Nipende pia kuwahakikishia wanahisa wetu, wateja wetu na wadau wetu kuwa benki yenu ipo katika mikono salama na inaendelea vizuri chini ya uongozi wa Bwana Moshingi, menejimenti, wafanyakazi wote pamoja na Bodi ya wakurugenzi".

Tunachohitaji tu ni ushirikiano kutoka kwenu wanahisa wote, wadau pamoja na wateja wetu ili benki yetu izidi kufanya vizuri sokoni na kutekeleza mikakati yote ya maendeleo tuliyojiwekea".

Natoa wito kwa watanzania wote kujiunga na benki yetu na kufaidika na fursa mbalimbali za huduma bora za kibenki tunazozitoa, DCB ni Mkombozi wa Kweli kwa watanzania wote, Wajasiriamali wadogo na wa kati, wanawake na vijana, DCB ni Mkombozi wa Kweli kwa wafanyabiashara wa kada zote”, anamaliza Bi Nanyaro.
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Biashara ya DCB, Bi. Zawadia Nanyaro, akizungumza na wanahisa wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika kwa jijini Dar es Salaam leo. Bi Zawadia alisema DCB Itaendelea kusimamia misingi ya kuanzishwa kwake ambayo ni kusaidia miradi endelevu ya kupunguza umasikini, kuendeleza jamii na kutoa huduma bora zinazokidhi mahitaji halisi ya kila siku ya wateja wao.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Sabasaba Moshingi , akizungumza na wanahisa wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. Bwana Moshingi aliwaambia wanahisa kuwa DCB chini ya uongozi wake, kwa kushirikiana na Bodi pamoja na wafanyakazi wote wamejizatiti kuandika upya historia ya benki hiyo na hii ikianza kuonekana baada ya DCB kufanya vizuri katika robo ya kwanza na ya pili mwaka huu.
Mwanasheria Mshauri wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Alex Mgongolwa, akizungumza na wanahisa wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bodi ya Ukaguzi na Usimamizi wa Benki ya Biashara ya DCB, Prof. Tadeo Satta, akizungumza na wanahisa wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Bw. Sabasaba Moshingi (kulia) akizungumza na baadhi ya wawakilishi wa wanahisa wa benki hiyo wakati wa Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka wa Wanahisa wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Bw. Selemani Kateti, Mwakilishi kutoka UTT AMIS, Bw. Medson Enock na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni, Bw. Rajab Gondomo.

Kuhusu DCB

Benki ya Biashara ya DCB ilianzishwa mwaka 2002 na mwaka unaofuata kupewa leseni ya kujiendesha kama benki ya kijamii, ikijulikana kama Benki ya Watu wa Dar es Salaam ‘Dar es Salaam Community Bank’ ambayo wanahisa wake waanzilishi wakiwa ni Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam pamoja na Manispaa zake za Ilala, Kinondoni na Temeke. Wanahisa wengine ni Mifuko ya NHIF na UTT AMIS pamoja na wananchi wa kawaida.

Kuanzishwa kwa DCB kulitokana na maono ya Rais mstaafu wa awamu za tatu, Hayati Benjamin William Mkapa kutoka na kilio cha wananchi wenye kipato cha chini na cha kati kukosa mikopo ya mitaji katika benki za kibiashara kutokana na kutokidhi vigezo vilivyowekwa.

Katika miaka hii 22 tokea kuanzishwa kwa DCB, benki imepitia hatua mbalimbali; ilikuwa benki ya kwanza kuorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es salaam (DSE) mnamo mwaka 2008, ambapo Februari 2012 ilifanikiwa kuhuisha leseni yake kutoka benki ya kijamii na kuwa benki kamili ya kibiashara na kubadilisha jina kutoka Benki ya Watu wa Dar es Salaam na kuwa Benki ya Biashara ya DCB.

Benki ya DCB ina mtandao wa matawi 9 ya kibenki ndani na nje ya Dar es Salaam ikiwa na mtandao wa mawakala 1000 na vituo vya kutolea huduma 1500 sehemu mbalimbali nchini. Ina zaidi ya mashine 280 za ATM zilizounganishwa na Umoja Switch, lakini pia inatumia Kadi za Visa zinazoweza kutumika katika mashine zinazosapoti kadi hizo ndani na nje ya nchi.
Share:

Wednesday, September 11, 2024

TUME YA SAYANSI YA TEKNOLOJIA YAANZISHA MFUMO KUWASAIDIA WASICHANA NA WANAWAKE KIDIJITALI

KATIKA kuwasaidia Wasichana na Wanawake kumudu maisha na kuisaidia jamii Tume ya Sayansi na Teknolojia ( Costech), imezindua Program mbili kwa ajili ya kuwajengea uwezo kidijitali.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 10, 2025 jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Costech, Dkt. Amos Nungu amesema kuwa Program hizo ni kwa ajili ya wasichana ambao hawakumaliza masomo yao na Wanawake wenye mawazo au biashara zinazohusiana na Teknolojia.


Lengo ni kuwapa ujuzi na taaluma ya kiteknolojia ili waweze kuja na biashara ambazo zinaweza zikasaidia waweze kumudu maisha yao, na wasaidie jamii.


Dkt. Nungu amesema Program ya kwanza inajulikana kama 'Future Femtech' inayowasaidia wanawake wenye kampuni changa au mawazo machanga ya kiteknolojia.


Amesema Program ya pili ijulikanayo kama 'Kuzatech' inaangalia mabinti ambao walikuwa shule lakini kwa namna moja au nyingine wakashindwa kuendelea na masomo hivyo wamewapa fursa ya kupata mafunzo kidijitali.


"Sasa hizi Program mbili tunazifanya kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo,"amesema.


Nungu amesema Kuzatech wataunganika na Future Femtech ambao baadhi yao ni wahitimu wa vyuo vikuu wenye mawazo ya biashara ambapo wadogo wanapata fursa ya kuungana na hawa wakubwa ili waweze kupata mafunzo yatakayowasaidia kuwa nankitu cha kufanya.


Kwa upande wake Meneja Usimamizi na Uhaulishaji Teknolojia Costech, Dkt. Erasto Mlyuka amesema Program hiyo ya Future Femtech inawalenga wasichana ambao wamekuwa ni waanzilishi wa kampuni changa.


Amesema hupewa msaada wa kitaalam kwa maana ya mafunzo elekezi ya kujengewa uwezo pia kupewa fedha za kuwawezesha kufanya biashara zao.


Amesema program hizo zitatengeneza ajira kwa wanawake ili na wenyewe wapate nafasi ya kuchangia kwenye pato la nchi kwa kuwa na kipato halali.


Mbunifu kutoka Arusha, ambaye ni mnufaika wa Future Femtech, Pamela Chogo amesema mafunzo aliyoyapata ni chachu kubwa kwenye ubunifu wa biashara.


Amesema Program hizo ni muhimu kwa sababu zinasaidia kupata elimu ya ujasiriamali.
Share:

Monday, September 2, 2024

BENKI YA KCB YAUNGAMKONO KUWEZESHA IBADA YA SHUKRANI SHULE YA MARIAN BAGAMOYO YATOA MILIONI 30.

BENKI Ya KCB imewezesha kwakutoa Shilingi milioni 30 katika sherehe ya shukrani ya Marian Schools, iliyojumuisha mbio za miguu, matembezi, na misa ya shukrani.
Mkurugenzi wa Biashara wa Benki hiyo Cosmas Kimario na Mgeni rasmi wa sherehe hizo ,aliipongeza Taasisi za Marian kwa mafanikio makubwa waliyoyafikia kielimu, kijamii, na kiuchumi.

Kimario alisisitiza kuwa tangu kuanzishwa mwaka 1997, Taasisi za Marian zimeonyesha dhamira thabiti ya kutoa elimu bora na kuzalisha wahitimu wenye mchango mkubwa katika jamii na tija kazini.

Aliendelea kwa kueleza jinsi Marian ilivyopanua shughuli zake kutoka shule moja, Marian Girls Secondary School, hadi kuwa na shule tatu za sekondari, zahanati, hoteli, na chuo kikuu (Marian University), kilichoanzishwa mwaka 2014.

Mafanikio haya yameleta mabadiliko chanya katika elimu, jamii, na uchumi wa taifa. Wahitimu wa Marian Schools wameiva kielimu na kinidhamu, wakitoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya taifa.

Kwa upande wake Meneja wa Shule za Marian Valentine Bayo alitoa historia fupi ya Taasisi za Marian, akisema: "Mnamo mwaka 1991 nilitumwa hapa na wakubwa wangu wa Shirika la Roho Mtakatifu (Holy Ghost Fathers) kama padre kijana kwa kazi ya uinjilishaji.

Kutokana na hali ya uduni wa eneo hili ambalo lilikuwa limesahaulika, tulianzisha juhudi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuanzisha shule za chekechea na ufundi. Hatimaye, juhudi hizi zilipelekea kujengwa shule ya sekondari ya wasichana ya Marian mnamo mwaka 1997.

Aidha katika ushirikiano kati ya Benki ya KCB na Taasisi za Marian kati ya mwaka 2021 na 2024, KCB Bank imewekeza katika miradi mbalimbali ya Taasisi za Marian, ikiwa ni pamoja na ukarabati wa shule za Marian Girls na Marian Primary, ujenzi wa majengo ya ghorofa sita kwa ajili ya madarasa na hosteli za Marian Boys School, na kuchangia baadhi ya gharama za uendeshaji wa taasisi hizi.

Sherehe hizi pia zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Askofu Mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu Zanzibar, Agustine Shao; Mkuu wa Shirika la Holy Ghost, Mhe. Shauri Selenda; Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo; Meneja na Mwanzilishi wa huuShirika la Roho Mtakatifu; wenyeviti wa bodi za Taasisi za Marian; pamoja na wazazi, wanafunzi, na wafanyakazi wa taasisi hizo.

Share:

KAMPUNI YA ORYX GAS TANZANIA YAMKOSHA WAZIRI WA NISHATI YAKABIDHI MITUNGI NA MAJIKO 1000 KWA MAMA NA BABA LISHE.

KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania yamkosha Naibu Waziri wa Nishati yakabidhi mitungi na majiko yake 1000 kwa washiriki wa mashindano ya kupika kwa gesi ya Oryx mkoani Mbeya ili kuwawezesha kurahisisha shughuli zao za mapishi.

Akizungumza wakati akihitimisha mashindano ya kupika kutumia Nishati ya ORYX kwa Mama na Baba Lishe wa Mkoa wa mbeya, Naibu Waziri Judith Kapinga aliyekuwa mgeni rasmi amesema Serikali imekuwa kinara wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini na lengo ni kufika asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia nishati mbadala kwaajili ya kupikia.
"Maombi ya wananchi kwa wadau wa gesi ni kupunguzwa kwa bei ya nishati hiyo ambayo kwa sasa ni ipo juu kulingana na kipato Cha wananchi ambao ndio watumiaji wakubwa wa Nishati hiyo. Tunashauri wadau katika sekta hii kutengenezwe mfumo ambao utakuwa rafiki kwa Mwananchi kununua gesi kidogo kidogo pindi anapokuwa na uhitaji."

Amesisitiza kukiwa na uwezo wa gesi kununuliwa kidogo kidogo anaamini wananchi wengi watatumia gesi na hivyo kusaidia kupunguza Kasi ya uharibu wa mazingira lakini pia kulinda afya za wananchi.

Naibu Waziri Kapinga amesema katika mwaka wa fedha uliopita wamegawa mitungi kwa wananchi na mwaka huu wa fedha wametenga fedha kwa ajili ya kuendelea kugawa nishati mbadala ya kupikia kwa wananchi huku akisisitiza kuwa Rais DK.Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuona asilimia kubwa ya Watanzania wanatumia nishati hiyo.
Kuhusu mashindano hayo ya mapishi, Naibu Waziri Kapinga amempongeza Spika wa Bunge Dk.Tulia Ackson kuandaa mashindano hayo makubwa na kushirikisha Mama na Baba Lishe 1000 kushindana kupika kwa gesi kwani yamekuwa ya mfano na yametumika kutoa elimu ya nishati na utunzaji mazingira.

Naibu Waziri pia amewashukuru Oryx gas kwa kuendelea kuishika mkono Serikali katika kusaidia kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, wanafanya kazi nzuri na wamekuwa wakifika kila mahali wakigawa mitungi na majiko yake kwa jamii.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Gas Tanzania Benoit Araman amesema lengo kuu la mashindano ya mapishi ni kuhamasika matumizi ya nishati safi kwa lengo la kulinda mazingira ambayo yamekuwa yakiharibiwa kwasababu ya kukata kuni na mkaa.
"Kwa miaka zaidi ya 15 iliyopita upatikanaji wa nishati ya kupikia umekuwa ukipangwa na kujadiliwa lakini hivi sasa Serikali inayoongozwa na Rais DK.Samia Suluhu Hassan amekuwa na hamasa kubwa ya kuhimiza wananchi kutumia nishati safi ya kupikia."

"Oryx Gasi tunaamini kupika kwa gesi kunakwenda kusaidia kulinda mazingira sambamba na kupunguza muda mwingi kwa wanawake kuwa porini kutafuta kuni na mkaa kwa ajili ya kuanda chakula.Pia kupika kwa gesi kutasaidia kuwalinda wanawake dhidi ya wanyama wakali walioko misitu lakini kuwalinda dhidi ya vitendo vya ukatilii ambavyo wanakutana navyo wakiwa porini."Amesema Benoit.

Ameongeza "pamoja na kusaidia makundi mbalimbali kuyawawezesha kupata mitungi ya gesi ya Oryx lakini wanajivunia kuwafikia Mama na Baba Lishe zaidi ya 12000 ambao wamepata elimu ya matumizi salama ya kupika kwa gesi sambamba na kuwapa mitungi midogo na mikubwa kwa lengo la kuwawezesha kufanya shughuli za mapishi kwa urahisi na kuwa salama kiafya," amesema.

Kwa upande wao baadhi ya Mama na Baba Lishe walioshiriki mashindano ya kupika kwa gesi wamesema kupitia mashindano hayo wamenufaika na mafunzo waliyoyapata sambamba na kuelezwa umuhimu wa kutunza mazingira na wanatoa shukrani kwa waandaaji wakiongozwa na Spika wa Bunge na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini Dk.Tulia Ackson.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive