A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Monday, April 19, 2021

Benki ya Absa yatoa msaada wa wheelchairs 20 kwa wanafunzi wenye ulemavu

  
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Bakari Msulwa (wa tatu kushoto), akikabidhi moja ya viti mwendo 20 (wheelchairs) kwa mtoto mwenye ulemavu, Briton Andrew vilivyotolewa msaada na Benki ya Absa Tanzania katika hafla iliyofanyika mkoani Morogoro leo. Kushoto kwake ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Absa, Aron Luhanga na wengine kutoka kushoto ni Mshauri kutoka Taasisi ya Ikupa Trust Fund, Peter Charles; mama wa mtoto, Stella Philipo na Meneja wa Tawi la Absa Morogoro, Godfrey Chilewa. Viti hivyo vina thamani ya shs milioni 10 vitakabidhiwa kwa shule za msingi tano zenye wanafunzi wenye ulemavu katika mikoa ya, Morogoro (5), Dodoma (5), Iringa (2), Mbeya (3), na Zanzibar (5).
Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania Aron Luhanga (wa tatu kushoto), akikabidhi moja ya viti mwendo 20 (wheelchairs) Agnes Yohana, mama wa mwanafunzi mwenye ulemavu, Santieli Mduma (aliyekaa), vilivyotolewa msaada na Benki ya Absa Tanzania katika hafla iliyofanyika mkoani Morogoro leo. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Bakari Msulwa na Meneja wa Tawi la Absa Morogoro, Godfrey Chilewa. Viti hivyo vina thamani ya shs milioni 10 vitakabidhiwa kwa shule za msingi tano zenye wanafunzi wenye ulemavu katika mikoa ya, Morogoro (5), Dodoma (5), Iringa (2), Mbeya (3), na Zanzibar (5).
Meneja wa Tawi la Absa Morogoro, Godfrey Chilewa (katikati), akikabidhi moja ya viti mwendo 20 (wheelchairs) Steven Francis, baba wa mwanafunzi mwenye ulemavu, Flora Steven (aliyekaa), vilivyotolewa msaada na Benki ya Absa Tanzania katika hafla iliyofanyika mkoani Morogoro leo. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Bakari Msulwa na Ofisa Elimu Maalum Manispaa ya Morogoro, Daniel Maganga. Viti hivyo vina thamani ya shs milioni 10 vitakabidhiwa kwa shule za msingi tano zenye wanafunzi wenye ulemavu katika mikoa ya, Morogoro (5), Dodoma (5), Iringa (2), Mbeya (3), na Zanzibar (5).
Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Bakari Msulwa, Bakari Msulwa (wa pili kushoto), akiwa na, kutoka kushoto; Meneja wa Tawi la Absa Morogoro, Godfrey Chilewa, Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania Aron Luhanga, Ofisa Elimu Maalum Manispaa ya Morogoro, Daniel Maganga na Mshauri kutoka Taasisi ya Ikupa Trust Fund, Peter Charles, wakipiga picha na wanafunzi watano wenye ulemavu baada ya kukabidhiwa msaada wa viti mwendo vilivyotolewa na Benki ya Absa mkoani Morogoro leo. Viti hivyo vina thamani ya shs milioni 10 vitakabidhiwa kwa shule za msingi tano zenye wanafunzi wenye ulemavu katika mikoa ya, Morogoro (5), Dodoma (5), Iringa (2), Mbeya (3), na Zanzibar (5).
Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania Aron Luhanga (kulia) na Meneja wa Tawi la Absa Morogoro, Godfrey Chilewa wakikabidhi moja ya viti mwendo 20 (wheelchairs) kwa mwanafunzi mwenye ulemavu, Hassan Moyo (aliyekaa), vilivyotolewa msaada na benki hiyo katika hafla iliyofanyika mkoani Morogoro leo. Viti hivyo vina thamani ya shs milioni 10 vitakabidhiwa kwa shule za msingi tano zenye wanafunzi wenye ulemavu katika mikoa ya, Morogoro (5), Dodoma (5), Iringa (2), Mbeya (3), na Zanzibar (5).
Mshauri wa masuala ya walemavu kutoka Taasisi ya Ikupa Trust Fund, Peter Charles (wa pili kulia) akikabidhi moja ya viti mwendo 20 (wheelchairs) Halima Liana, mama wa mwanafunzi mwenye ulemavu, Hassan Moyo (aliyekaa), vilivyotolewa msaada na Benki ya Absa Tanzania katika hafla iliyofanyika mkoani Morogoro leo. Kushoto kwake ni Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga, Ofisa Elimu Maalum Manispaa ya Morogoro, Daniel Maganga na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Bakari Msulwa (kushoto kabisa). Viti hivyo vina thamani ya shs milioni 10 vitakabidhiwa kwa shule za msingi tano zenye wanafunzi wenye ulemavu katika mikoa ya, Morogoro (5), Dodoma (5), Iringa (2), Mbeya (3), na Zanzibar (5).

Benki ya Absa Tanzania imekabidhi vifaa vya usafiri 20 (wheelchairs) kwa wanafunzi walemavu waliopo shule za msingi katika mikoa ya Morogoro, Dodoma, Iringa, Mbeya na Zanzibar.

Vifaa hivi vina thamani ya Tsh milioni 10 na vitagawiwa kwa wanafunzi hao kuanzia mkoa wa Morogoro (5), Dodoma (5), Iringa (2), Mbeya (3) na Zanzibar (5).

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya vifaa hivyo mjini Morogoro jana, Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mahusiano, Bw. Aron Luhanga amesema “benki yetu inatambua umuhimu wa kuisaidia jamii katika kila nyanja na inasimama kidete kuhakikisha vijana wanafikia malengo yao kwa wakati na kwa kupata huduma stahili. Ndio maana leo tunashirikiana na shirika la Ikupa Trust Fund kwa kuwapatia wanafunzi hawa vifaa vya usafiri hivi ili waweze kufika shuleni kwa wakati na kuendelea na ratiba zao za masomo bila kukwamishwa”.

Bw. Aron alisisitiza kwamba Benki ya Absa ina lengo kuu la kuhakikisha vijana na watu katika jamii wananufaika zaidi kwa kufikia malengo yao ikiwa ndiyo moja ya nguzi kuu katika kuimarisha mchango wetu kwa jamii. Kwa kujali kwao ila pia kuzingatia vitu muhimu vya kuwasaidia vijana katika jamii kufikia malengo yao kwa upesi na kwa njia sahihi.

Akipokea vifaa hivyo Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Bakari Msulwa alitoa wito kwa wazazi nchini kuwapekeka shuleni watoto wao wenye ulemavu ili kuweza kutambua vipaji vyao na kuviendeleaa.

Alisema kuzaliwa ama kupata ulemavu sio mwisho wa ndoto katika maisha kwani kuna walemavu wanaofanya vizuri katika njanja mbalimbali zikiwemo nafasi za uongozi serikalini, wanasiasa, wanamichezo na wataalamu mbalimbali.

"nachukua nafasi hii kuipongeza Benki ya Absa kwa kushirikiana na taasisi ya Ikupa Trust Fund na ni imani yangu tukio hili litaleta hamasa kwa taasisi na makampuni mengine kuiga Mfano wa Absa", alisema.

Kwa upande wake Meneja wa tawi la Absa mkoani Morogoro, Bw. Godfrey Chilewa pia amesema “kama benki tunazidi kuekeza nguvu katika jamii zinazotuzunguka huku tukishirikiana na wadau kama Ikupa Trust Fund na kwa kushikana mkono zaidi na uongozi mzima wa serikali yetu ili kuhakikisha tunaipa jamii huduma stahili na kufanikisha malengo ya watu pia”.

Mmoja wa wazazi wa wanafunzi waliokabidhiwa viti mwendo hivyo aliishukuru Benki ya Absa akisema kifaa hicho kitamrahisishia mtoto wake kwenda shuleni ukizingatia kuwa shule nyingi za msingi wilayani hapo ni za kutwa licha ya kuwa na vitengo maalumu vya wenye ulemavu.

"Naishukuru Absa, serikali na Ikupa, naona kama Absa imechukua jukumu la kuwa baba wa mtoto wangu kwani baba yake alishafariki, najua mtoto wangu anapoenda shule na ulemavu wake unapungua", alisema mama huyo.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive