A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Thursday, February 28, 2019

WAZIRI JAFO AIPONGEZA DCB KWA KUJIENDESHA KWA FAIDA

Waziri wa  Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo (wa pili kulia), akizungumza na waandishi wa habari wakati alipotembelea tawi la Benki ya Biashara ya DCB jijini Dodoma leo. Wengine kutoka kushoto ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano, Rahma Ngassa,  Mkurugenzi Mtendaji, Godfrey Ndalahwa na Meneja wa DCB Dodoma, Joseph Njile.  
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa (katikati),akizungumza na waandishi wa habari wakati Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemeni Jafo (wa pili kilia), akitembelea tawi la benki hiyo mjini Dodoma leo. Wengine kutoka kushoto ni Mkuu wa Masoko na Mawasiliano, Rahma Ngassa na Meneja wa DCB Dodoma, Joseph Njile.

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Patrobas Katambi (katikati), akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa (kushoto), wakati akitembelea tawi la benki hiyo mjini Dodoma leo. Kulia ni Mhasibu wa tawi hilo, Daniel Makyao.
Waziri wa  Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo (katikati waliokaa), akipiga picha na uongozi wa DCB pamoja na baadhi ya wateja waliokuwepo tawini hapo wakati wa ziara yake mjini Dodoma leo.
Share:

Wednesday, February 27, 2019

NBC KUIMARISHA UHUSIANO WAKE NA JESHI LA MAGEREZA

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki  ya NBC, Theobald Sabi, (kushoto),
akiagana na Mkuu wa jeshi la Magereza nchini, Phaustine Kasike, alipotembelea ofisini kwake Makao Makuu ya jeshi hilo jijini Dar es Salaam hivi karibuni
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi,  (wa pili kulia), akizungumza na Mkuu wa jeshi la Magereza nchini, Phaustine Kasike, (katikati) wakati alipotembelea ofisini kwake kwamazungumzo juu ya kuangalia njia bora za kudumisha uhusiano baina yaNBC na Jeshi hilo. Kushoto kwa Theobald Sabi ni Mkurugenzi wa Idaraya Wateja wa Makampuni, Linley Kapya, pamoja na maofisa kutoka jeshila Magereza.
Mkurugenzi wa Idara ya Wateja wa Makampuni, Linley Kapya (wa pili kulia), akizungumza na Mkuu wa jeshi la Magereza nchini, Phaustine Kasike, (katikati) wakati uongozi wa Benki hiyo walipotembelea ofisini kwake kwa mazungumzo juu ya kuangalia njia bora za kudumishaMahusiano  baina ya NBC na jeshi hilo. Wa tatu kulia ni MkurugenziMtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi, pamoja na Meneja Mahusiano wa
NBC, William Kallaghe pamoja na maofisa wa jeshi hilo.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Phaustine Kasikeakizungumza katika kikao na uongozi wa Benki ya NBC, uliomtembeleaofinisi kwake, Makao Makuu ya Magereza jijini Dar es Salaam.  Wanaomsikiliza kushoto kwake ni  Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi, pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Wateja wa Makampuni, Linley Kapya na kulia kwake ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Uwesu Ngarama, pamoja na Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Mhandisi Tusekile Mwaisabila. Hafla hiyo ilifanyika  jijini Dar es Salaam.

Kamishna wa Huduma za Urekebishaji Mhandisi Tusekile Mwaisabila,   akizungumza na Uongozi wa Benki ya NBC pamoja naMkuu wa jeshi la Magereza nchini, Phaustine Kasike katika hafla hiyo.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Phaustine Kasikepamoja na Mkurugenzi ya NBC, Theobald Sabi, (watatu kushoto)  akipigapicha ya pamoja na uongozi wa Benki ya NBC pamoja na maofisa wa jeshi
hilo.
Share:

VIJANA WA KITANZANIA KUPATA FURSA YA KIPEKEE

Vijana wa Kitanzania kupata fursa ya kipekee!

Shindano la ujasiriamali la Tujenge TZ Innovation Challenge linapokea  michanganuo kutoka kwa wajasiriamali vijana hadi tarehe 13 mwezi wa tatu mwaka huu. 

Vijana kupewa fursa ya kupata mafunzo, wawekezaji na mengine mengi kwa ajili ya kukuza biashara zao.
Share:

Monday, February 18, 2019

Uber yazindua bima ya Ulinzi dhidi ya Majeraha kwa madereva na abiria nchini Tanzania bila gharama yoyote ya ziada


Madereva na abiria wa Uber nchini Tanzania watakuwa na amani zaidi wakitumia Uber, kwa kuwa Uber imetangaza kuzindua bima ya Ulinzi dhidi ya Majeraha, inayotolewa na UAP Old Mutual. Tangazo hili ni sehemu ya ahadi kuu ya Uber katika eneo la Mashariki ya Kati na Afrika (MEA) na ni suluhisho la kipekee, la kwanza kwa madereva na abiria linalotumia programu za teknolojia nchini Tanzania.

Madereva wote wa Uber, pamoja na madereva wa uberPOA watafaidika na bima hii bunifu bila gharama yoyote ya ziada; kuanzia wakati unapokubali safari, wakati unaendesha gari kumchukua abiria, na hadi wakati safari inapokamilika. Bima ya abiria itawashughulikia kuanzia wakati safari zao zinapoanza, hadi mwisho wa safari.

Katika tukio la bahati mbaya la ajali au tukio linalohusiana na uhalifu na kusababisha majeraha wakati wa safari, abiria na madereva wataweza kupata faida zifuatazo:

  • Bima ya matibabu: Ikiwa ajali itatokea Wakati wa Safari, bima hii itawafidia madereva na abiria kwa gharama husika za matibabu hadi TZS 1 250 000. Kwa kuongezea, bima hii hufidia gharama za huduma ya ambulensi.
  • Malipo ya kifo na mazishi: Katika tukio la bahati mbaya ambapo dereva au abiria anaaga dunia kama matokeo ya ajali Wakati wa Safari, watu wanaomtegemea au warithi watafaidika na malipo ya pesa taslimu ya TZS 5 000 000. Watapata pia kiasi cha TZS 500 000 cha gharama za mazishi.
  • Malipo ya kulemazwa kabisa: Katika tukio la bahati mbaya ambapo dereva au abiria amelemazwa kabisa kama matokeo ya ajali Wakati wa Safari, watafaidika na malipo ya pesa taslimu ya TZS 5 000 000. Kiasi kinategemea na hali ya ulemavu, kama iliyobainishwa na UAP Old Mutual.
  • Faida ya malipo ya kila siku kwa madereva (majeraha): Ikiwa dereva amelazwa kwa zaidi ya saa 48 kama matokeo ya ajali ambayo ilifanyika Wakati wa Safari hivyo basi hawezi kuendelea kuendesha gari kwa sababu ya majeraha hayo, atapokea malipo ya kila siku ya TZS 10 000 hadi siku 30 ikiwa amethibitishwa na daktari kuwa hafai kufanya kazi.

Akitoa maoni yake kuhusu ushirikiano huu, Alfred Msemo, Mkuu wa Uber nchini Tanzania alielezea, “Tunaamini ushirikiano huu na UAP Old Mutual utahusika pakubwa katika kufanikisha lengo letu la chaguo thabiti, la bei nafuu, na salama la usafiri kwa Watanzania wote. Tutaendelea kuchukua maoni kutoka kwa watumiaji wetu wote ili kuhakikisha tunaboresha zaidi uzoefu wao ili waweze kutumia Uber kwa ujasiri zaidi”.  

Damas Filied, UAP Old Mutual Life Assurance, “Kama biashara kuu ya Afrika tunagundua kwamba tunajukumu kubwa, tukishirikiana na washikadau wengine kuwaunga mkono wateja wetu kwa kulinda kile ambacho ni muhimu kwao. Toleo hili la bidhaa bunifu, ni mfano mwema wa hilo, na tunatazamia ushirikiano wa muda mrefu unaofaidi pande zote.”

Sera ya Ulinzi dhidi ya Majeraha, ambayo itaanza kutumika tarehe 21 Desemba 2018, imetengenezwa hasa kwa madereva wale walio barabarani na kwa abiria wanaohitaji chaguo salama, thabiti na la bei nafuu la kuzunguka katika mji wao. Uber inaendelea kuimarisha usalama unaopatikana kupitia programu ya Uber na kuhakikisha safari salama wakati wa kila safari iliyopatikana kupitia programu ya Uber. Hivi karibuni Uber ilizindua Zana ya Usalama yenye vipengele vipya kama vile Kituo cha Usalama na Watu Unaowaamini kwa abiria na taarifa inayoweza kugeuzwa kukufaa ya kasi na kitufe cha dharura cha dereva ambacho huwaunganisha madereva moja kwa moja kwa makampuni binafsi ya usalama yakihitajika kupitia mtoa huduma mwingine.
Share:

Friday, February 15, 2019

BENKI YA NBC YACHANGIA UJENZI WA KITUO CHA POLISI RUANGWA MKOANI LINDI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (wa pili kushoto), akipokea mfano wa hundi ya shs 11,270,000 kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi, kwa ajili ya kununulia mifuko 1000 ya saruji kama  mchango wa NBC kuchangia ujenzi wa kituo cha polisi cha Wilaya ya Ruangwa, Mkoani Lindi. Hafla ya makabidhiano  iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. 

BENKI ya NBC imetoa msaada wa mifuko 1000 ya saruji kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa kuchangia ujenzi wa kituo cha polisi cha Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi.

Msaada huo umekabidhiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu  Kassim Majaliwa katika ofisi zake Ikulu jijini Dar es Salaam leo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi anasema  NBC ni Benki ya Wazalendo na tunajiona fahari kuweka juhudi zetu katika kuhakikisha kila mwananchi na mzalendo waTaifa letu anaishi kwa usalama na utulivu.

“Kama taasisi ya fedha ni imani yetu kuwa Jeshi la Polisi likiwezeshwa kwa miundo mbinu mbalimbali ikiwemo majengo ya vituo pamoja na makazi ya askari litaweza kutekeleza majukumu yake ya kila siku kwa ufanisi ambayo ni kulinda usalama wa raia na mali zao.

Benki ya NBC inajua pia eneo litakalojengwa kituo hiki wapo wateja wetu na wale wateja watarajiwa hivyo ujenzi wa kituo hiki utasaidia sana kuimarisha hali ya ulinzi na usalama katika wilaya hiyo hivyo kuwafanya wakazi wake kuzalisha mali katika hali ya utulivu hiyvo kukuza uchumi wao na wa Taifa.




“Benki ya NBC inapenda kutoa pongezi kwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais John  Pombe Joseph Magufuli kwa jitihada zake katika kujenga mazingira wezeshi kwa sekta binafsi ili kwa pamoja kutimiza azma ya kuelekea Tanzania ya viwanda.
Share:

Wednesday, February 6, 2019

At last, the boys secured their inheritance rights

Perepetua Buzima (left) discussing (about boundaries of the plot) with a woman who bought a house which was at the centre of inheritance conflict which involved two boys and their step-father. Finally, the case was peacefully resolved by Mbogwe district paralegals and all interesting parties got their rights.  
For years, thousands of female-children and widows denied their inheritance rights after the death of a father in many families across Tanzania. Although many cases go unreported, there are countless incidents of widows and girls being pushed out of family houses and denied their rights in the course of the distribution of inheritance wealth left by a deceased father.
However, over time, the trend is changing as male-children are also subjected to problems and denied their inheritance rights after the death of their parents in a family.
Young boys—Samson Kuhali (20) and MashakaKuhali (17) —residents of Masumbwe, Mbogwe district (Geita)—stands out as real examples of male-children who experienced untold harassment and chased out of their matrimonial house after the death of their mother.
Before the death, the boys were living peacefully with their mother and step-father in the same house (jointly built by the couple) located at Masumbwe village, Mbogwe district. The family lived in harmony and unity.
But the situation changed drastically after the death of their mother. Step-father began mistreating the boys by denying them basic rights including meeting their daily needs. He later chased the two boys out of the house on the grounds that they had no right to inherit the property.
Led by Ms. Perepetua Ruben Buzima a sister to the deceased, the relatives fought hard to claim back the house and ensure the boys’ access to their inheritance right. They  use quick a lot of financial resources and time to follow up on the case in various channels, their struggle ended in vain, as step-father refused to give the boys their rights
Relatives of the deceased went to Mbogwe District Social Welfare Office, where they were advised to lodge a case with Masumbwe primary court. Step-father was summoned but rejected to appear before the court. Deceased relatives were allowed by the court to select a person who would oversee distribution of the disputed inheritance house. Family members convened a meeting and appointed Raphael Ruben (50) overseer of the distribution process. However, step-father refused to cooperate. He took the matter back to primary court magistrate who failed to resolve the conflict. The deceased family consulted a lawyer who agreed to assist at a higher cost which they could not afford.
Some villagers advised the family to seek paralegals assistance. They met Mbogwe district paralegal, who assisted them—re-organizing necessary documents and filed an appeal at Mbogwe District Land and Housing Tribunal. The court summoned the step-father, heard arguments of both sides and ordered the house to be sold at a market price and proceeds divided equally to both conflicting parties (the two boys and their step-father).
The house was finally sold out at Shs 2.5 million and proceeds divided as per court order. The boys have since relocated to another village where they are now doing small businesses to support their families.
“Before paralegals’ intervention, we (family) spent a lot of money, energy and time in this case--preparing court documents and related costs, it became easier after paralegal step in to assist…within no time, the case has been concluded, and the boys secured their rights,” says Perepetua Buzima, deceased’s young sister.
“We are grateful that justice prevailed. The boys got their shares and invested in small businesses, I now understand the importance of preparing a will to protect our families, particularly wife and children from inheritance problems,” says Julie Mozao, a family friend.
Share:

Monday, February 4, 2019

Wafanyakazi wa Benki ya Biashara ya DCB washerehekea kumaliza salama zoezi la uuzaji hisa

01
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya  DCB, Godfrey Ndalahwa (wa tatu kulia), akigonisha glasi na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo kushereheka kumaliza salama msimu wa uuzaji wa hisa za benki hiyo uliyoanza Novemba 12 mwaka jana na kuhitimishwa Januari 31 mwaka huu. Hisa moja iliuzwa kwa bei pungufu ya shs 265. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi.
02
Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya Biashara ya DCB, Isidory Msaki (kushoto), akifungua ‘champaigne’ huku baadhi ya maofisa wa benki hiyo wakishangilia katika hafla ya wafanyakazi hao kusherehekea kumaliza salama msimu wa uuzaji wa hisa za benki hiyo uliyoanza Novemba 12 mwaka jana na kuhitimishwa Januari 31 mwaka huu. Hisa moja iliuzwa kwa bei pungufu ya shs 265. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi. Kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji, Godfrey Ndalahwa, Mkurugenzi wa Fedha, Zacharia Kapama na wafanyakazi wengine.
03
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya  DCB, Godfrey Ndalahwa ( kulia), akigonisha glasi na Meneja wa Tawi la Magomeni, Haika Machaku (kushoto),  kushereheka kumaliza salama msimu wa uuzaji wa hisa za benki hiyo uliyoanza Novemba 12 mwaka jana na kuhitimishwa Januari 31 mwaka huu. Hisa moja iliuzwa kwa bei pungufu ya shs 265. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi.
04
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa (katikati), akishangilia wakati baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo wakifungua chupa za ‘champagne’ katika hafla ya wafanyakazi hao kusherehekea kumaliza salama msimu wa uuzaji wa hisa za benki hiyo uliyoanza Novemba 12 mwaka jana hadi Januari 31 mwaka huu. Hisa moja iliuzwa kwa bei pungufu ya shs 265. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam juzi.
05
Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya DCB, wakiwa na nyuso zenye furaha na matumaini  katika hafla hiyo. Benki ya DCB ilizindua zoezi la uuzaji wa hisa zake Novemba 12 mwaka jana na kuhitimisha zoezi hilo Januari 31 mwaka huu ikiuza hiza hizo kwa bei pungufu ya shs 265 kwa hisa.
06
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Godfrey Ndalahwa (kulia), akigonganisha glasi pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa DCB katika hafla hiyo.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive