A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Monday, January 31, 2022

Dr. Ngozi Okonjo-Iweala, Director General of the World Trade Organization, Joins the Group of Thirty


WASHINGTON—January 31, 2022 | The Group of Thirty (G30) announced today that Dr. Ngozi Okonjo-Iweala has joined the Group’s membership. She brings an exceptional and unique record of leadership, in Africa, at the World Bank and numerous international fora, and in her current role as Director-General of the World Trade Organization.

The Group of Thirty, founded in 1978, is an independent global body comprised of economic and financial leaders from the public and private sectors and academia. It aims to deepen understanding of economic and financial issues, and of the international repercussions of decisions taken in the public and private sectors. Members participate in the Group in their personal capacities, not on behalf of any organization, public or private, to which they may be affiliated.

Dr. Jacob A. Frenkel, Chairman of the Board of Trustees, said: “We are delighted to welcome Ngozi Okonjo-Iweala as a member of the Group of Thirty. Her exemplary contributions to the international system, at both a national and global level, assure she will be a vital voice in our deliberations on the contours of globalization in the years ahead.

Tharman Shanmugaratnam, Chairman of the G30, said: “We look forward to Ngozi’s engagement in the Group’s discussions and work on key issues facing the international economy. Ngozi has been and remains a preeminent leader of our times.

Dr. Okonjo-Iweala said: “I thank the Group of Thirty for this opportunity, and am honored to join its distinguished membership. I look forward to supporting the Group’s mission and working with G30 members on some of the most important issues of the day.

A full G30 membership list is available at http://group30.org/members.
Share:

Sunday, January 30, 2022

Benki ya DCB kupitia mfuko wake wa kuisaidia jamii wa DCB FOUNDATION wasaidia kampeni ya usafi wa mazingira Temeke.

   
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo (wa tatu kushoto) akifanya usafi pamoja na wafanyakazi wa Benki ya Biashara ya DCB katika siku ya usafi ya mwisho wa mwezi iliyofanyika kiwilaya katika kata ya Keko jijini Dar es Salaam jana. DCB imeshiriki kampeni hiyo kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii wa DCB Foundation kwa kufanya usafi na kukabidhi msaada wa vifaa vya kufanyia usafi.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo (katikati), Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Brino Londo (kulia) na Ofisa Masoko wa benki hiyo, Agness Ntabaye wakifanya usafi katika siku ya usafi ya mwisho wa mwezi iliyofanyika kiwilaya katika kata ya Keko jijini Dar es Salaam jana. DCB imeshiriki kampeni hiyo kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii wa DCB Foundation kwa kufanya usafi na kukabidhi msaada wa vifaa vya kufanyia usafi.
Meya wa Manispaa ya Temeke, Abdallah Mtinika (kulia) akipokea sehemu ya vifaa vya kufanyia usafi kutoka kwa Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Brino Londo katika siku ya usafi ya mwisho wa mwezi iliyofanyika kiwilaya katika kata ya Keko jijini Dar es Salaam jana. DCB imeshiriki kampeni hiyo kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii wa DCB Foundation kwa kufanya usafi na kukabidhi msaada wa vifaa vya kufanyia usafi.
Meya wa Manispaa ya Temeke, Abdallah Mtinika (kulia) akipokea sehemu ya vifaa vya kufanyia usafi kutoka kwa Meneja wa Benki ya Biashara ya DCB Tawi la Temeke, Loyce Lwiza katika tukio la siku ya usafi ya mwisho wa mwezi lililofanyika kiwilaya katika kata ya Keko jijini Dar es Salaam jana. Benki ya DCB chini ya mfuko wake wa kusaidia jamii wa DCB Foundation wasaidia usafi wa mazingira ya Wilaya ya Temeke.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo (katikati) akishikana mikono na Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Brino Londo baada ya kukabidhiwa vifaa vya kufanyia usafi katika siku ya usafi ya mwisho wa mwezi iliyofanyika kiwilaya katika kata ya Keko jijini Dar es Salaam jana. DCB imeshiriki kampeni hiyo kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii wa DCB Foundation kwa kufanya usafi na kukabidhi msaada wa vifaa vya kufanyia usafi.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo (wa tatu kushoto), Ofisa Masoko wa benki hiyo, Agness Ntabaye (wa pili kushoto) na Meneja Mahusiano wa Benki ya Biashara ya DCB, Brino Londo wakiwa pamoja wakati wa zoezi la siku ya usafi ya mwisho wa mwezi ambapo kiwilaya ilifanyika katika Kata ya Keko jijini Dar es Salaam. DCB imeshiriki kampeni hiyo kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii wa DCB Foundation kwa kufanya usafi na kukabidhi msaada wa vifaa vya kufanyia usafi.
Share:

DCB KUWAWEZESHA WANAWAKE KIUCHUMI

  
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Pamela Nchimbi (kushoto) akizungumza katika kongamano la wanawake lililoandaliwa na Kampuni ya ushauri wa masuala ya fedha ya Bridge Consult kwa udhamini mkuu wa Benki ya DCB jijini Dar es Salaam jana. Lengo la jukwaa hilo ni kubadilishana mawazo na kupeana ujuzi wa masuala ya kifedha, uwekezaji pamoja na maendeleo endelevu.
Mkuu wa Wateja Binafsi wa Benki ya Biashara ya DCB, Fortunata Benedict akitoa elimu ya maswala ya fedha katika kongamano la wanawake lililoandaliwa na Kampuni ya ushauri wa masuala ya Kifedha ya Bridge Consult kwa udhamini mkuu wa Benki ya DCB jijini Dar es Salaam jana. Lengo la jukwaa hilo ni kubadilishana mawazo na kupeana ujuzi wa masuala ya kifedha, uwekezaji pamoja na maendeleo endelevu.
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Dk. Anna Abdul akizungumza katika kongamano la wanawake lililoandaliwa na Kampuni ya ushauri wa masuala ya kifedha ya Bridge Consult kwa udhamini mkuu wa Benki ya DCB jijini Dar es Salaam jana. Lengo la jukwaa hilo ni kubadilishana mawazo na kupeana ujuzi wa masuala ya kifedha, uwekezaji pamoja na maendeleo endelevu.
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Pamela Nchimbi (wa pili kulia) akitoa elimu ya masuala ya maendeleo endelevu katika kongamano la wanawake lililoandaliwa na Kampuni ya ushauri wa masuala ya kifedha ya Bridge Consult kwa udhamini mkuu wa Benki ya DCB jijini Dar es Salaam jana. Lengo la jukwaa hilo ni kubadilishana mawazo na kupeana ujuzi wa masuala ya kifedha, uwekezaji pamoja na maendeleo endelevu. Kutoka kulia ni Mtaalamu wa masuala ya Kimaisha, Mihaela Marcu, Mshauri wa masuala ya afya kwa jamii, Naomi Serbantez na Mkurugenzi wa Mgahawa wa Terrace, Sarah Raqey.
Baadhi ya washiriki wakichangia mada katika kongamano la wanawake lililoandaliwa na Kampuni ya ushauri wa masuala ya kifedha ya Bridge Consult kwa udhamini mkuu wa Benki ya DCB jijini Dar es Salaam jana. Lengo la jukwaa hilo ni kubadilishana mawazo na kupeana ujuzi wa masuala ya kifedha, uwekezaji pamoja na maendeleo endelevu.
Share:

Monday, January 24, 2022

WANANCHI WA KATAVI WAIPOKEA KWA SHANGWE TANZANIA COMMERCIAL BANK

 .com/img/a/

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mh. Mwamvua Mrindoko (kushoto),  akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Tawi jipya la Tanzania Commercial Bank (TCB) katika Manispaa ya Mpanda  mjini mkoani Katavi,  kulia ni  Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Onesmo Buswelu  Meneja wa Tawi la Mpanda Julius Mlang'a  pamoja na maofisa wa kamati ya ulinzi ya mkoa..com/img/a/Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mh. Mwamvua Mrindoko wa  (kushoto),  akipokea kadi ya ATM kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Commercial Bank TCB,  Sabasaba Moshingi, alipofungua akaunti alipoalikwa kuwa mgeni rasmi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Tawi jipya la Tanzania Commercial Bank  lililofunguliwa katika Manispaa ya Mpanda  mjini mkoani Katavi jana  wengine pichani ni Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Onesmo Buswelu  Meneja wa Tawi la Mpanda Julius Mlang'a  pamoja na maofisa wa wengite kutoka TCB

.com/img/a/

Tanzania Commercial Bank (TCB)  imezindua tawi jipya Mkoa wa Katavi Wilaya ya Mpanda ikiwa ni jitihada za kusogeza huduma za kibenki kwa wateja na Wananchi kwa ujumla.

Tawi hilo la kwanza kwa taasisi za fedha kuzinduliwa Mkoa Katavi Wilaya ya Mpanda, limezinduliwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Mwanamvua Mrindoko .

 

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Commercial Bank (TCB) Sabasaba Moshingi alisema huo ni mwendelezo wa Tanzania Commercial Bank katika kusogeza huduma kwa wateja wake.

 

Alisema tawi hilo jipya la Mpanda litarahisisha utoaji huduma za kibenki kwa wateja wake hali ambayo itapunguza mzunguko wa wananchi kuzifuata huduma za kibenki maeneo mengine ya mbali

Aliongeza kuwa Tanzania Commercial Bank (TCB) imezingatia shughuli za kiuchumi zinazoendeshwa Wilayani humo kwa  wafanyabiashar  wafugaji na wakulima wa na kufungua tawi hilo hivyo wateja hawatalazimika kwenda mjini kupata huduma za kibenki kama hapo awali

 

AlisemaTanzania Commercial Bank sio kwamba tu ni benki kubwa nchini, bali inatoa mchango mkubwa katika shughuli za kijamii  hasa kuinua elimu pamoja na Afya.

Kwa kuona umuhimu wa kusongeza huduma kwa wateja hasa maeneo ya vijijini Tanzania Commercial Bank (TCB) inaendelea kuwawezesha mawakala watakaosaidia kutoa huduma hizo jambo ambalo litasaidia kusogeza huduma kwa wateja wetu nchi mzima.

 

Aliongeza, kwa sasa Benki hiyo ina matawi  82 Mawakala tunao zaidi 3,800  mashine zakutolea pesa ATM zetu tunazojitegemea Kama TanzaniaCommercial Bank ni 84 lakini zile ATM ambazo tupo chini ya Umoja Switch ni zaidi ya 250.

 

Akizungumza na wadau mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa Tawi jipya la Tanzania Commercial Bank  Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mhe. Mwanamvua Mrindoko  ameupongeza uongozi wa Tanzania CVommercial Banki  kwa kuja kuwekeza katika  Mkoa huu na anaamini kwa wingi wa watu waliojitikeza katika tukio hili watakwenda kufungua akaunti.

 

Mrindoko pia ameipongeza  Tanzania Commercial  Banki (TCB)  kwa kufika Mkoani Katavi na kuwakaribisha kwani fursa zipo nyingi katika mkoa huo zikiwemo za uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara pamoja na mazao mengine  ya kimkakati.

 

Mkuu wa Mkoa wa Katavi aliuhakikishia uongozi wa Tanzania Commercial  Banki (TCB)  kwamba Katavi ni mkoa unaokua kwa kasi sana kutokana na shughuli za uzalishaji na za kimaendeleo hivyo huduma ya  Tanzania Commercial Bank kwakfungua tawi hilo limekuja wakati muafaka

 

“Kuzinduliwa kwa Tawi la Tanzania Commercial Bank (TCB)  hapa Katavi maana yake ni kwamba huduma za kibenki zitapatikana kwa urahisi zaidi hivyo wafanyakazi, wakulima na wafanyabiashara wa Katavi jitokezeni kwa wingi wenu kuchangamkieni  fursa hii na kuja kufungua akaunti na kufanya miamala mengine kama kulipa kodi alisisitiza Mrindoko

Share:

Wednesday, January 19, 2022

Tanzania Commercial Bank yakabidhi majengo ya kisasa shule ya msingi kitunga, wilaya ya muleba mkoani kagera

.com/img/a/Katibu Tawala Mkoa wa Kagera Prof: Faustin Kamuzora (wa pili kulia), akikata utepe wakati akikabidhiwa msaada wa jengo la madarasa, Vyoo, pamoja na Madawati mapya 50 lililokarabatiwa na Tanzania Commercial Bank (TCB) Hafla ya makabidhiano hayo yalifanyika katika Shule ya Msingi Kitunga iliyopo wilaya ya Muleba mkoani Kagera kushoto ni Mkurugenzi wa BiasharaWateja Wakubwa wa Tanzania Commercial Bank Adolfina William, Mkurugenzi wa Mipango na Mikakati wa Benki hiyo Muondakweli Kaniki pamoja na Mkuu wa Shule hiyo Hashim Kibaiza, Tanzania Commercial Bank kupitia mpango wake wa kusaidia jamii (CSR) imetumia zaidi kiasi cha shs milioni 36 kukamilisha ujenzi wa Madawati pamoja na choo   Madawati pamoja na choo cha walimu chenye matundu mawili 

.com/img/a/


Mkurugenzi wa Biashara Wateja Wakubwa wa Tanzania Commercial Bank Adolfina William,akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa jengo la madarasa, Vyoo, pamoja na Madawati mapya 50 lililokarabatiwa na Tanzania Commercial Bank (TCB) Hafla ya makabidhiano hayo yalifanyika katika Shule ya Msingi Kitunga iliyopo wilaya ya Muleba mkoani Kagera kupitia mpango wake wa kusaidia jamii (CSR) imetumia zaidi kiasi cha shs milioni 36 kukamilisha ujenzi wa madarasa Madawati pamoja na choo.

.com/img/a/

Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Prof Faustin Kamuzora amewataka wazazi na wakazi wa Mkoa wa Kagera kusaidiana na serikali katika kutatua changamoto za walimu.

Hayo ameyasema wakati wa kukabidhiwa ukarabati wa madarasa, madawati na Choo cha matundu mawili kilichojengwa na Tanzania Commercial Bank (TCB) kitakachosaidia kuboresha mazingira rafiki ya walimu kufundisha.

Prof Kamuzora amesema, wazazi na walezi wengi wa watoto wamesoma katika shule hiyo ila walimu wamekuwa na changamoto ya mazingira ambayo si rafiki na inaweza kupelekea walimu hao kuondoka na kwenda sehemu zingine.

“Walimu hawa wakiondoka tutakosa wa kuwafundisha watoto wetu, nyie wazazi wengi mmesoma hapa na mtu aliyesoma miaka ya nyuma akija hapa atapashangaa ila tusiwaachie serikali peke yake ila tushirikiane pamoja na wadau wa elimu pia,” amesema Prof Kamuzora.

Amesema, Benki ya TCB wamekuja na kujenga choo ila hii isiwe mwisho katika kutoa msaada bali walimu pia wanahitaji elimu ya fedha sababu wengi wamekuwa wanaingia katika mikopo inayowadidimiza kimaslahi.

Aidha, Prof Kamuzora ameitaka elimu ya fedha kuanza kutolewa mashuleni ili wanafunzi waanze kuwa na uelewa mkubwa na itawasaidia baadae.

“Na kwa upande wa walimu, haimaanishi ndio unajua kila kitu nao ni muhimu kuwa uelewa juu ya elimu ya fedha,”Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa Tanzania Commercial Bank Adolphina William amesema wananchi wa Kijiji cha Msole wameweza kufurahia mradi wa kukarabati madarasa, kukabidhi madawati na walimu kupata choo cha kisasa.



Amesema, mradi huo uliofanyika katika Shule ya Kituga umeweza kugharimu kiasi cha Milioni 36.3 hadi kukamilika kwake.



“Tanzania Commercial Bank imekuwa inatenga fedha kila mwaka kwa ajili ya kusaidia jamii na mwaka huu tumetenga takribani Milioni 500 na kujikita zaidi katika sekta ya elimu na afya,” amesema Adolphina.


Kwa upande wa Mkuu wa shule Hashim kibaiza ameishukuru Tanzania Commercial Bank kwa kufanikisha mradi huo ambao utaenda kuboresha mazingira bora ya walimu katika kuinua taaluma.

Ameomba wadau mbalimbali kuiga mfano kwa Tanzania Commercial Banki ili kuendelea kujikita katika kusaidia jamii ikiwemo shule yao ya Kitunga.



Tanzania Commercial Bank imekabidhi ukarabati wa madarasa mawili, ujenzi wa choo cha walimu pamoja na kuchangia madawati 50 katika shule ya Msingi Kitunga iliyopo Muleba, mkoani Kagera mradi umegharimu Milioni 36,274,500 pesa za kitanzania.
Share:

Monday, January 17, 2022

NAIBU KATIMU MKUU WIZARA YA NISHATI ATEMBELEA SOKO LA KARUME

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Kheri Mahimbali, ametembelea soko la Karume lililoteketea kwa moto usiku wa kuamkia Januari 16 jijini Dar es Salaam.

Akiwa katika soko hilo, alikagua na kushuhudia athari mbalimbali zilizotokana na moto huo ambao umeathiri miundombinu mbalimbali ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na kusababisha baadhi ya sehemu kukosa umeme.

Akizungumza mara baada ya kutembelea soko hilo Naibu Katibu Mkuu Mahimbali amesema kuwa kazi ya kuhakikisha huduma ya umeme inarejea katika Mikoa ya Ilala na Temeke inaendelea ambapo mafundi tayari wapo katika maeneo hayo.

 

Moto huo ulianza majira ya saa 9 usiku ambapo jitihada za kuuzima moto huo zilifanyika ili kudhibiti moto usienee katika makazi ya wananchi lakini kutokana na miundombinu ya soko hilo kazi ya kuzima ilikuwa ngumu na kusababisha na kuteketea kwa soko lote.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Kheri Mahimbali (katikati) akimsiliza Meneja wa Tanesco Kanda ya Mashariki Dar es Saalam na Pwani, Keneth Boimanda (kulia) wakati alipotembelea soko la Karume na kukagua miundombinu ya TANESCO iliyoathirika na moto huo, Januari 16, 2022. 


Share:

Tuesday, January 4, 2022

Rais Samia Ateua watatu, Dk Baghayo Saqware ndani arejeshwa TIRA

Rais Samia Suluhu Hassan.


Na Mwandishi Wetu


RAIS Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi katika taasisi tatu tofauti nchini.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu, ilisema Rais amemteua Dk Baghayo Saqware kuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).             

Dk. Saqware ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo cha Uhasibu Tanzania (TIA), aliwahi  kuongoza taasisi hiyo kwa mafanikio lakini aliondolewa na Rais wa Serikali ya awamu ya tano, Dk. John Pombe Magufuli.

Baadhi ya mafanikio aliyoyapata ni  kuongezeka kwa mapato ya Serikali kupitia tozo za kibima kutoka sh. Bilioni 10.1  mwaka 2015 hadi sh bilioni 12.1 mwaka 2018, sawa na ongezeko la asilimia 11;

Mafanikio mengine ni kuzuia ubadhirifu kwa kuimarisha mfumo wa kieletroniki wa TIRA MIS wenye kuzuia na kuhakiki bima zote za magari nchini. Hatua hii imesaidia kupunguza ubadhirifu na kuwalinda watumiaji wa huduma za bima ya magari na vyombo vingine vya moto.

Mafanikio mengine ni kupanua wigo wa utoaji huduma za bima kwa kuanzisha na kutekelezwa kwa kanuni za kusimamia huduma za bima kupitia mabenki (Bancassurance Regulations 2019) ambazo zilipitishwa na Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Philipo Mpango wakati huo Machi 2019.

Kanuni hizi zimelenga kuongeza upatikaji wa huduma za bima nchini kwa urahisi na ufanisi kupitia mtandao wa matawi ya benki Tanzania. Utekelezaji huu ulileta uhasama baina ya Kamishna wa Bima na madalali wa bima (Insurance Brokers) ambao waliamini uanzishwaji wa kanuni hizi zinalengo la kuua biashara ya udalali, jambo ambalo si sahihi.

Kuondoa kero kwa wateja na wafanyabiashara ya bima ni moja ya mafanikio wakati ule baada ya kutekeleza kwa vitendo mabadiliko ya sheria namba 10 ya mwaka 2009 kifungu namba 72 kinachoelekeza ada za bima kulipwa moja kwa moja kwa kampuni ya bima bila kupitia kwa mtu wa kati (insurance intermediaries).

Mafanikio mengine ni kuthibiti utoroshwaji wa tozo za bima kwa kuanzisha utaratibu wa ithibati (“accreditation”) kwa makampuni na madalali wa nje ya nchi wanaofanya biashara ya bima mtawanyo na kampuni zilizosajiliwa nchini.

Mengine ni kuongeza uwezo wa kubakiza tozo nchini (Retention Level) kulinda wateja wa bima kwa mfumo bora wa malipo ya fidia, kulinda ajira za Watanzania, kuweka utaratibu wa kuratibu wataalamu bima nchini.

Mbali na Dk Saqware, Rais Samia pia  amemteua Charles Itembe kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Eneo Maalumu la Mauzo ya Nje (EPZA). Itembe ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Azania.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya Ikulu, Rais Samia pia amemteua Ernest Mchanga kuwa Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha (JFC).

Mchanga ni Katibu Msaidizi, Fedha na Utawala, Tume ya Pamoja ya Fedha (JFC) kutoka Wizara ya Fedha na Mipango.  Uteuzi huo ulianza Januari mosi mwaka huu

Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive