A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Thursday, August 16, 2018

KAMPUNI YA KIMATAIFA YA VISA ON MOBILE WASHIRIKIANA NA MAXMALIPO

Kampuni ya kimataifa ya teknolojia ya malipo, imetangaza rasmi ushirikiano wa kimkakati kati yao na Maxcom Afrika ambayo itawawezesha wauzaji zaidi ya 30,000 kupokea malipo ya Visa kwa kutumia simu ya mkononi pamoja na mawakala 20,000 ambao watawezeshwa kupokea amana na kutoa malipo na kuunganisha watanzania na mfumo wa kimatiaifa wa malipo 

Kampuni ya Visa imejitolea kuleta njia rahisi zaidi, za kuaminika na salama za kufanya malipo duniani kote. Sasa, pamoja na malipo kwa kadi za plastiki, wateja wanaweza kutumia simu zao kufanya malipo kwa Visa. 
Visa kwenye simu itawezesha wateja kufanya malipo mbalimbali au kutuma pesa kwa familia na marafiki, bila kukatwa malipo. 


Huduma hii ambayo inatolewa kupita akaunti ya benki huunganisha akaunti ya mteja ya benki na hudumza za benki za simu bila na kuwezesha mteja kufanya malipo ya ndani nan nje ya nchi kwa kutumia huduma ya Visa kwa simu. 
Pia itawezesha huduma za kuweka na kutoa pesa kwa kutoka kwa mawakala wa benki maalumu. 


Ushirikiano wetu na Maxcom Afrika utahakikisha kuwa Watanzania wanaweza kulipa kwa kutumia Visa kwenye simu zao kwa wauzaji wapya zaidi ya 30,000. 


Ushirikiano huu unasisitiza jinsi Visa wamejitolea kuhakikisha na kupanua wigo wa malipo kwa malipo ya simu duniani kote, "alisema Meneja Mkuu wa Visa wa Afrika Mashariki, Sunny Walia.


Maxcom Afrika inatoa njia rahisi, salama na ya kuaminika ya kufanya malip kwa watu binafsi na biashara nchini Tanzania. 
Maxcom Afrika inawezesha malipo kwenye mtandao na moja kwa moja kwenye simu ya mkononi.


Wamejenga vipengele vya usalama kulinda wanunuzi na wauzaji wote kwa kuhakikisha taarifa za shughuli zinafichwa kwa kutumia viwango vya benki huku wakikutuma taarifa ya malipo kwa  akaunti za benki. Maxcom Afrika inatoa malipo ya hapopapo, huduma za mtandao na huduma kwa njia ya simu iliyounganishwa na terminal ya usindikaji kadi.


"Lengo letu la msingi ni kusaidia wateja wao kupata chaguo mbalimbali za kulipia kufanya kazi kwa usahihi na salama kwenye vifaa vyao vya mkononi. Kuunganisha kwa huduma ya Visa kwenye Simu ya Mkono itatuwezesha kutoa huduma bora zaidi wakati wateja wetu wanapokutana mtandaoni, katika biashara zao au mawakala wa benki.


Ushirikiano huu ni muafaka kwa kuwa unatimiza haja ya mifumo salama ya malipo kwa wateja wetu na wafanyabiashara, "alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Maxcom Africa, Juma Rajabu.


Maxcom sasa hutoa huduma za malipo huduma mbalimbali, sekta ya usafiri, afya na bima, huduma za kifedha na huduma za malipo ya biashara. 


Visa imeidhinisha Maxcom Afrika kama mshirika wa ubunifu na huduma zao zitatimiza malengo ya ajenda ya kuingizwa wote katika huduma za fedha nchini Tanzania.


Hudum ya Visa kwenye simu huwawezesha wateja kupata fedha zao moja kwa moja kutoka kwa akaunti zao za benki kupitia programu zao za benki za simu za kulipa wafanyabiashara au kutuma fedha kwa watu binafsi bila ada ya malipo, pamoja na kuhifadhi au kuondoa fedha kwa wakala wowote wa Visa. Wafanyabiashara waliojisajili na huduma hii watapata msimbo wa kipekee wa QR na Nambari ya sehemu ya mauzo ambayo wateja wao kusoma kwa kutumia smartphone ili kufanya malipo. 


Fedha zinahamia moja kwa moja kutoka kwa akaunti ya benki ya mteja  kwenye akaunti ya mfanyabiashara na hutoa taarifa ya muda halisi kwa pande zote mbili. 
Wakala wa benki waliojisajili pia watapokea msimbo wa QR na Nambari ya sehemu ya mauzo ambazo wateja wanaweza kusoma kwa kutumia smartphone ili kuweka au kutoa fedha ndani au kutoka kwenye akaunti za benki zilizowezeshwa.
Share:

Monday, August 6, 2018

COCONUT FOUNDATION KUASHISHA MASHINDANO YA ELIMU SHULE ZA MSINGI

Mkurugenzi Mipango na Uendeshaji  wa Taasisi  ya Coconut Foundation Baraka Koukara, akizungumza na waandishi wa habari watika wa ufunguzi wa mashindano ya tahajia katika Shule za Msingi Tanzania (kushoto) ni Mkurugenzi  wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano wa Taasisi ya hiyo Zena Msonde (kulia) ni MenejaMradi wa Coconut Foundation Anna Mwalongo pamoja na Mkurugenzi Rasilimali watu na Utawala Saluna Ally haflaya uzinduzi huo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi  wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano wa Taasisi ya Coconut Foundation, Zena Msonde ( kushoto), akizungumza na waandishi wa habari watika wa ufunguzi wa mashindano ya tahajia katika Shule za Msingi Tanzania (katikati) ni Mkurugenzi Mipango na Uendeshaji  wa Taasisi hiyo Baraka Koukara pamoja na Mkurugenzi Rasilimali watu na Utawala Saluna Ally haflaya uzinduzi huo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi  Rasilimali watu na Utawala wa Taasisi ya Coconut Foundation, Saluna Ally (katikati)akizungumza na waandishi wa habari watika wa ufunguzi wa mashindano ya tahajia katika Shule za Msingi Tanzania (kushoto) ni Mkurugenzi Mipango na Uendeshaji  wa Taasisi hiyo Baraka Koukara pamoja na Meneja Mradi  Anna Mwalongo haflaya uzinduzi huo imefanyika leo jijini Dar es Salaam.

UFUNGUZI WA MASHINDANO YA TAHAJIA KWA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI TANZANIA. (TANZANIA NATIONAL SPELLING BEE COMPETITIONS 2018)
Taasisi isiyo ya kiserikali ya Coconut Foundation kwa kushirikiana na wizara ya elimu na TAMISEMI, imeanzisha mashindano ya kutamka herufi za maneno magumu ya lugha ya kiingereza, yenye lengo la kukuza elimu bora, uwezo wa kujieleza na stadi muhimu za maisha kwa wanafunzi wa shule za msingi Tanzania katika kuwaanda wawe nguvukazi sahihi ya uchumi wa viwanda.
Kwa mwaka 2018, zaidi ya shule 100 kutoka mikoa ya Dar es salaam na Lindi zitashiriki kuanzia ngazi ya shule mpaka kitaifa kuanzia mwezi huu Agosti mpaka kilele chake mwezi Novemba, na washindi 10 bora wakitarajia mialiko ya kimataifa. Shindano hili linahusisha shule zote za umma na binafsi, wadau mbalimbali wa elimu na umma kwa ujumla.
Kwa mwaka 2018, Mashindano haya yanaanzia ngazi ya shule ambapo washindi 21 hupatikana kufuzu ngazi ya kimkoa. Kutokana na uwingi wa shule, mkoa wa Dar es salaam manispaa zake 5 yaani Ubungo, Temeke, Ilala, Kigamboni na Kinondoni zitafanya mashindano ya kimkoa hivyo kufanya mikoa 6 pamoja na Lindi. Washindi 50 kutoka kila mkoa watafuzu mashindano ya kitaifa ili kupata washindi 10 bora kutoka makundi mawili kulingana na ngazi za madarasa. Mwaka jana 2017 washindi wa juu walipata nafasi ya kwenda kushiriki mashindano ya Afrika Mashariki nchini Uganda na mashindano ya Afrika nzima nchini Afrika Kusini. Mipango zaidi kuhusu mwaka huu itatangazwa pindi itakapokamilika. Aidha, zawadi mbalimbali hutolewa kwa washindi.
Mashindano haya yenye kuifikia mikoa yote hapo mapema baadae, yatahusisha lugha za kiswahili na kiingereza lakini kwa mwaka 2018 ni kiingereza peke yake; yana lengo la kumuwezesha mwanafunzi kutawala kutawala mawasiliano katika kujieleza binafsi, kujiamini, kujua misamiati mingi ya lugha, kuzungumza katika halaiki za watu wengi, kukuza usikivu yakinifu, kusoma, kuandika, kumudu muda na kufanya mambo kwa wakati, kuishi katika timu na kupata utajiri wa maarifa na stadi mbalimbali ambazo hutunzwa katika fasihi mbalimbali na wataalamu.
Taasisi ya COCONUT FOUNDATION imesema kuwa Mashindano haya yamefanyiwa utafiti na kubaini kiini cha vijana wengi kutoibuka washindi katika soko shindani la ajira baada ya kuhitimu masomo, siyo elimu mbovu bali kukosa uwezo wa ndani kuzikabili changamoto bila woga, na uwezo wa kuitafsiri elimu waliyoipata kutoka nadharia kwenda kwenye matokeo ya kivitendo katika kuzitatua changamoto hizo. Tangu mwaka 2011 kutoka kwenye mwanzo mgumu mpaka kufikia mwaka jana 2017 ambapo shindano la kwanza la majaribio lilifanyika kwa mkoa wa Dar es salaam pekee, taasisi imesema uzoefu ulioonekana ni kuwa madhara ya kisaikolojia ya utotoni na mafunzo au malezi ya awali na msingi, humuathiri mwanadamu maisha yake yote ikiwa hakuna jitihada za utambuzi.
Kuwajengea wanafunzi haiba ya ushindi na kujitawala kuanzia ngazi za utotoni wawe vinara hapo baadae katika ulimwengu wa ajira, biashara na maendeleo mapana ya taifa na dunia kwa ujumla, ndilo lengo kuu la mashindano haya na kwa upekee kabisa taasisi hiyo imejikita kuleta chachu inayohitajika lakini haipo katika mtaala wa kawaida.
Taasisi inazikaribisha shule mbalimbali kujisajili, wadau mbalimbali wa maendeleoya elimu kuunga mkono jitihada hizi na vijana waliohitimu elimu hasa katika fani za lugha kuomba nafasi ya kujitolea ili kukuza ueledi wao na nafasi za ajira.
Aidha, taasisi inaomba ushirikiano kwa vyombo mbalimbali vya habari ili kukuza ufanisi wa shindano hili lenye kuendana na sera ya viwanda, katika kumjenga kijana mtanzania tangu hatua za awali.
Taasisi ya Coconut (Coconut Foundation) ni asasi isiyo ya kiserikali iliyosajiliwa mwaka mwaka 2015 chini ya wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, jinsia, ,wazee na watoto; yenye lengo wa ukuzaji kiwango cha elimu ya kimatokeo kwa kuchagiza stadi muhimu zisizo katika mtaala wa kawaida bila kuuharibu mtaala uliopo bali kushirikiana na wizara husika; kwa kuwafanya wanafunzi wapende kujifunza na kujitegemea zaidi. Taasisi ina makao yake Kijitonyama, Dar es salaam.
Tunawatakia wote utendaji mwema wa maendeleo ya elimu Tanzania na ujenzi wa uchumi wa viwanda.
.........................
.........................
Coconut Foundation
DATE EVENT VENUE 9th July -21st September
2018
Training/Instructions on Spelling
guideline to students
At a respective participating school
21st July 2018 Teachers/facilitators envisioning
(T.O.T)
Coconut Foundation offices
4th August 2018 On-stage facilitators training
(judges/callers/Child carers etc)
Coconut Foundation offices
18th August 2018 Endorsement event(stakeholders
forum)
At one of the schools (to be advised soon
22nd-29th September 2018 School competitions At a respective participating school
1st October 2018
Strictly deadline at 1600
hours
End of submitting names of school
winners for regional BEE competitions
Submission at info@coconutfoundation.or.
6th October 2018 Temeke Regional competition National Museum Theatre, Posta-Dar es sala 13th October 2018 Kigamboni Regional Competition National Museum TheatrePosta-Dar es salaa 20th October 2018 Ubungo Regional Competition National Museum Theatre, Posta-Dar es sala 27th October 2018 Lindi Regional Competition Hall- Lindi 3rd November 2018 Ilala Regional Competition National Museum Theatre, Posta-Dar es sala 10th November 2018 Kinondoni Regional Competition National Museum Theatre, Posta-Dar es sala 15th November 2018 Lindi regional winners travel to Dar
es salaam for national competition
Dar es salaam-Mtwara road
16th November 2018 Orientation for all national
contestants
JNICC Hall (Julius Nyerere International Convention Centre) ,Posta-Dar es sal 17TH November 2018 Grand Finale Tanzania National Spelling Bee Competition
JNICC Hall (Julius Nyerere Internation Convention Centre) ,Posta-Dar e salaam 18th November 2018 Lindi regional winners traveling
back to Lindi
Dar es salaam-Mtwara road.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive