A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Saturday, August 31, 2019

Bibi kizee arudishiwa ardhi iliyochukuliwa na mwenye pesa Korogwe Tanga

DSC_0912
Bibi kizee na Mkazi wa Korogwe, Bi. Amina Kirua, akilima katika shamba lake alilonyang’wa na jirani yake Tajiri, lakini baadae alirudishiwa baada ya kusaidiwa na wasaidizi wa kisheria Wilayani Korogwe. Msaada huo ni sehemu ya mradi mkubwa na nchi nzima wa kuwawezesha watanzania maskini na wahitaji, unaofadhiliwa na shirika la Legal Services Facility (LSF). (Picha na Mpiga Picha Wetu).

Tanzania inakumbana na changamoto nyingi zinazohusiana na umilikaji wa ardhi, hasa sehemu za vijijini. Changamoto hizi ni pamoja na migogoro kati ya wakulima na wafugaji, migogoro ihusuyo muda wa umiliki wa ardhi, uporaji wa ardhi na wakulima kunyang’anywa ardhi. Waathirika wakubwa wa migogoro ya aina hii ya ardhi ni wanawake na wazee waishio vijijini,” anasema mtaalamu wa masuala ya ardhi Charity Mugabi katika utafiti wa hivi karibuni na kuongeza: “Sera ya Ardhi tuliyo nayo kwa sasa na utekelezaji wake havijaweza kutatua migogoro ya ardhi nchini.”
Bibi Amina Kirua alikuwa akimiliki ekari 6 katika Wilaya ya Korogwe Vijijini Mkoa wa Tanga. Alinunua ekari hizo sita takriban miaka 25 iliyopita kutoka kwa jirani yake, ambaye ameshafariki dunia. Bibi huyu anaishi peke yake, lakini ana watoto wawili wa baba tofauti.
Ni bibi maskini anayetegemea shamba lake linalomsaidia kupata kipato cha kuendeshea maisha yake na watoto wake Hassan Bembe na Musoli Jumbe, ambaye huyu wa pili ana matatizo ya akili. Kwa miaka mingi, Bibi Amina amekuwa akilima kwa kujikimu na wanakijiji wengi katika Wilaya ya Korogwe Vijini.
Wakati fulani mtoto wake mwenye matatizo ya akili alihitaji uangalizi wa karibu kwa sababu ya matatizo ya kiafya. Hali hiyo ilimfanya Bibi Amina atumie muda wake mwingi kumtunza mtoto wake. Hivyo, aliacha kulima kama alivyokuwa akifanya kwa zaidi ya miezi miwili ili amtunze mtoto wake.
Baada ya mtoto wake kupata nafuu, alienda shambani kwa lengo la kuendelea na shughuli zake za kilimo. Lakini hakuamini alipokuta jirani yake ambaye ana uwezo wa kifedha akilima shamba hilo kwa madai kwamba yeye ndie mumiliki halali wa shamba hilo. Hivyo, mgogoro wa ardhi ulianza kati ya majirani hao, huku yule mwenye uwezo wa pesa akitumia uwezo wake wa pesa kuwahonga watendaji ili kumnyang’anya Bibi Amina ardhi, ambaye ni mumiliki halali, na kupewa yeye na hivyo kumfanya Bibi Amina kupoteza haki yake ya kumiliki ardhi.
Wanakijiji wenzake walimshauri Bibi Amina kupeleka malalamiko yake kwenye Baraza la Kata Korogwe Vijijini. Kutokana na nguvu ya pesa, Baraza la Kata liliamua kuwa ardhi ni mali ya yule mwenye pesa na hivyo Bibi Amina akapoteza haki yake.
“Kutokana na uamuzi wa Baraza la Kata, nilipoteza umiliki wa ardhi, lakini sikukata tamaa kwa sababu nilijua kwamba ardhi hiyo ni mali yangu, kwani niliinunua kwa pesa yangu mwenyewe,” alisema Bibi Amina. Kwa kweli, alikuwa ndiye mumiliki halali wa ardhi hiyo, lakini hakuwa na jinsi kutokana na uamuzi huo wa Baraza la Kata.
Watendaji walewale waliopokea pesa kutoka kwa jirani yake Bibi Amina na kumpokonya ardhi Bibi Amina walienda kwake kwa siri kumshauri aende kumwona msaidizi wa kisheria wa Wilaya ya Korogwe Vijijini Maimuna Hosean kwa msaada zaidi.
Wasaidizi wa kisheria walimsaidia Bibi Amina kuandaa hati, ushahidi na kukata rufaa kwenda Baraza  la  Ardhi  na  Nyumba  la  Wilaya Korogwe Mjini. Baada ya kusikiliza shauri lake, Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya lilitoa uamuzi kwamba yeye ndiye mumiliki halali wa ardhi hiyo.
“Kuanzia hapo, yule jirani yake aliyetumia nguvu ya pesa kumnayang’anya ardhi alishindwa kesi na hadi leo hajambugudhi tena Bibi Amina kuhusu umiliki wake wa ardhi,” alisema Yahaya Seif, ambaye ni msaidizi wa kisheria aliyeongoza wasaidizi wa kisheria wenzake kumtetea Bibi Amina kupata haki yake ya kumiliki ardhi kwenye Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya.
“Huduma za msaada wa kisheria hazina budi kuwafikia wanaume na wanawake wazee wanaokabiliwa na migogoro ya ardhi kutokana na uzee, umaskini na kutojua kusoma na kuandika sehemu mbalimbali za Tanzania vijijini,” alisema kiongozi mmoja, ambaye ni jirani wa Bibi Amina.
“Migogoro ya ardhi kama huu siyo mipya sehemu mbalimbali za Bara la Afrika… watu wachache wenye uwezo wa pesa na uchu wa kujilimbikizia mali hawaridhiki na walichonacho. Wanataka wachukue hata sehemu ndogo ya ardhi ambayo inamilikiwa na maskini. Hatua za kisheria lazima zichukuliwe kuanzia ngazi ya kijiji hadi taifa kuwalinda wanaume na wanawake maskini dhidi ya unyanganyaji wa ardhi,” alisema mwanaharakati mmoja wa haki za binadamu, Bw Ramadhan Mweli.
Share:

Tuesday, August 27, 2019

Facebook Celebrates 'Icons of Change' from across Sub-Saharan Africa with a Youth Gathering in Accra, Ghana

Facebook’s Communications Manager Francophone Africa, Olivia Nloga moderates a panel discussion at the Facebook Icons of Change Youth Event held in Accra Ghana. The panel featured four youths from across Africa who shared testimonies of how they are driving impact in their communities 
Left to Right, Facebook’s Head of Public Policy, Africa Kojo Boayke and Hon. Vincent Sowah Odotei (MP) Deputy Minister of Communications, Ghana at the Facebook Icons of Change Youth Event in Accra, Ghana.
Youths at a workshop at the Facebook Icons of Change Youth Event held in Accra Ghana last week. The event aimed to celebrate Africa's next generation of leaders and innovators, whilst providing opportunities to learn, network, connect and create positive dialogue.
Youths at a workshop at the Facebook Icons of Change Youth Event held in Accra Ghana last week. The event aimed to celebrate Africa's next generation of leaders and innovators, whilst providing opportunities to learn, network, connect and create positive dialogue.
Youths at a workshop at the Facebook Icons of Change Youth Event held in Accra Ghana last week. The event aimed to celebrate Africa's next generation of leaders and innovators, whilst providing opportunities to learn, network, connect and create positive dialogue.
Facebook Africa Team at the Facebook Icons of Change Event held in Accra Ghana. From Top Left to right: Olivia Nloga Communications Manager Francophone Africa, Kezia Anim Addo Communications Manager Sub Saharan Africa, Carolina Annand EMEA Communications Manager, Community Initiatives, Kiran Yoliswa Strategic Partner Manager, Communities, and Phil Oduor Policy Programs Manager for Economic Impact and Digital LiteracyFrom Bottom Left to Right: Kojo Boayke, Head of Public Policy, Africa, Janet Kemboi Communications Manager East Africa and Chimdi Aneke Program Manager Product Partnerships Sub-Saharan Africa  

Youths from across Africa at the Facebook Icons of Change Youth Event held in Accra Ghana last week. The event aimed to to celebrate Africa's next generation of leaders and innovators, whilst providing opportunities to learn, network, connect and create positive dialogue.

Facebook is bringing together 40 young leaders, developers, entrepreneurs and change makers from across Sub-Saharan Africa, to a two day event in Accra, Ghana, titled “Celebrating Icons of Change”. Taking place on 23 & 24th August, the event aims to celebrate Africa's next generation of leaders and innovators, whilst providing opportunities to network, connect and create positive dialogue. To celebrate Facebook also created a short film featuring five of the participants in their home country - titled 'Icons of Change' (available to view here - https://www.facebook.com/watch/?v=495921581209081)

With attendees hailing from 15 countries from across Sub-Saharan African, participants will be made up of Facebook Community Leaders, Developer Circle Leads, entrepreneurs, SMBs, as well as future change makers from the Africa Leadership University (ALU). Spending two days networking, attending leadership and digital skills workshops, and hearing from other young inspirational leaders from across the Continent, attendees will also be given the opportunity to give back to local communities in Accra by hosting workshops such as Coding for kids, and mentorship sessions for other young, up-and-coming SMBs and entrepreneurs.

Kezia Anim-Addo, Facebook Communictaions Manager, Sub-Saharan Africa, commented: “I'm so proud that we're bringing the first event of its kind for Facebook to the Continent and to Ghana. At Facebook, we see our role as supporting and investing in various communities here on the continent, in particular the youth. This event is about celebrating those people, the amazing talent, innovation and businesses we’re seeing emerge, and the young people who are accelerating this growth, and building an incredible future for the Continent. It's a privilege for us to be able to bring together 40 icons of change, and we look forward to what the two days will hold.”

Attendees represent countries from the region, including Ghana, Madagascar, Burkina Faso, Kenya, Senegal, Nigeria, Ethiopia, Botswana, DRC, South Africa, Cameroon and Zambia, and include:

Facebook Community Leaders who have started Facebook Groups dedicated to a topic or collective experience, and are having a positive impact in their community. Martin Beck Nworah, for example, oversees a community of more than 100,000 members on the Tale of Nigerians page, while Gameli Adzaho from Ghana, who runs GLabGhana - a community group who bring together students, teachers, researchers, scientists and science enthusiasts to network, learn and share scientific knowledge, for the good of humanity.

Facebook Developer Circle leads, a community-driven initiative for developers, that members join for free - allowing them to connect, share ideas, learn, and collaborate.

SMBs & Entrepreneurs, these are young people who have started businesses which are making an impact in their communities and beyond. For example, Kahitouo from Burkina Faso, founder of FasoPro which specialises in packaging and selling African insects as alternative sources of protein, and now has 360 sales outlets across 25 cities in Burkina Faso.
Share:

Monday, August 26, 2019

Tanga Cement yazidi kujimarisha Sekta ya Viwanda vya Saruji Tanzania


Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Tanga Cement, Lau Masha (wa nne lushoto), alizungumza wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa wanahisa wa kampuni hiyo jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki. Kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Reinhardt Swart na baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Tanga Cement.

Kampuni ya Tanga Cement (TCPLC) imetangaza kupata faida ya uendeshaji ya shilingi za Kitanzania Bilioni 14.9 kwa kipindi cha mwaka kinachoishia Disemba 31, 2018 kutoka hasara iliyotokana na uendeshaji ya shilingi Bilioni 10.99 kwa Mwaka 2017.

Akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu wa mwaka wa wanahisa wa Kampuni hiyo Jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Tanga Cement, Lau Masha alisema pia kuwa utendaji wa mwaka 2018 umesaidia kupunguza hasara baada ya kodi ya shilingi billion 11.3 kutoka shilingi bilioni 26.3 kwa mwaka 2017.

“mauzo ya kundi letu yalipanda kwa 25% na kufika shilingi bilioni 214.9 kutoka shilini bilioni  171.8 zilizopatikana kwa mwaka uliopita wakati faida ghafi kwa mwaka iliongezeka kwa 91% na kuwa shilingi bilioni 56.2 kutoka shilingi bilioni 29.4 zilizopatikana mwaka uliopita,” alisema.

Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa ukuaji wa biashara ulijikita katika ukuuaji wa simenti na secta ya ujenzi nchini Tanzania. Matumaini miundombinu chini ya mipango ya dira ya maendeleo ya serikali ya mwaka 2025.

Pamoja na hayo mwenyekiti huyo alisema kutokana na Tanzania kuwa soko la pili kwa ukubwa kwa masuala ya ujenzi Afrika Mashariki, uzalishaji wa simenti unatarajiwa kuongezeka hivyo Kampuni yao imejipanga kuhakikisha inanufaika na ukuaji huo katika soko la Kanda.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Reinhardt Swart alisema, kampuni iliongeza uzalishaji kwa kipindi chote hiki cha mwaka na kuweza kuzalisha mapato ya ziada kutokana na mauzo ya klika ya ziada iliyozalishwa.

Mkurugenazi huyo aliongeza kuwa mkataba wao na Kampuni ya reli Tanzania (TRC) umewawezesha kupata mabehewa zaidi ambayo yapo kwa ajili ya usafirishaji katika maeneo yao ya kimikakati ya usambazaji. Unafuu huo unapunguza gharama za kuhifadhi na usafirishaji huku ukuupa nguvu usafiri wa reli na usambazaji nchini Tanzania

“Ingawa kushuka kwa thamani ya fedha na riba tunayolipa kutokana na mkopo tuliochukua kwa ajili ya mtaji wa uwekezaji mpya wa kinu namba mbili (TK2) vimeendelea kubakia kuwa matumizi ya gharama kubwa, hasara baada ya kodi kwa mwaka 2018 ilipungua,” aliongeza Mkurugenzi huyo.

Pamoja na mafanikio hayo kampuni haikutangaza gawio la mpito kwa wanahisa wake kwa mwaka 2018 kutokana sababu zilizoelezwa mahali hapo kuwa ni hali iliyotokana na utendaji wake wa kifedha kwa mwaka 2017 hivyo bodi kuamua kutumia busara kutotangaza gawio la mwisho ili fedha iliyopo kutumika katika shughuli za utendaji na kulipia madeni.
Share:

Wednesday, August 21, 2019

Wateja wa kampuni ya nishati ya jua ya Mobisol wazidi kuongezeka

Meneja Mauzo wa Mobisol Kanda ya Pwani,  Wesley Muyenze (kulia), akizungumza na waandishi wa habari juu ya mafaniko na mikakati ya kampuni hiyo jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Maafisa wa Kampuni ya Mobisol (kulia), wakitoa huduma kwa wateja wao  walipokwenda kufanya manunuzi ya bidhaa za Mobisol.

KAMPUNI ya usambazaji wa huduma  za vifaa vinavyotumia umeme unaotokana na nishati ya jua (Mobisol), imesema kuwa kwa sasa watanzania wengi wanauelewa juu ya matumizi ya umeme wa sola hali iliyochangia  kampuni hiyo kupata wateja zaidi 100,000 na kuwahudumia watu  500,000.

Hayo yamebainishwa jijini Dar es Salaam jana na Meneja Mauzo wa Mobisol Kanda ya Pwani,  Wesley Muyenze wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya mafaniko na mikakati ya kampuni hiyo.

Alisema umeme wa jua ni chanzo kinachofaa cha nishati mbadala majumbani na nchi nyingi tayari zimegundua ukweli na zimeachana na vyanzo vya kuzalisha nishati ya
umeme vilivyozoeleka kama  makaa ya mawe.

Muyenze alisema anawashukuru watanzania ambao baadhi yao wameachana na nishati ya umeme inayotokana na vyanzo vilivyozoeleka na kutumia nishati ya jua inayouzwa na kampuni ya Mobisol.

"Hata hivyo kutokana na kuongezeka kwa wateja katika kampuni yetu,  tumeamua kutoa zawadi ambapo mteja akinunua mtambo wa W 40 anapata betri na paneli bure kabisa, kwahiyo niwaombe watanzania na wateja wetu wafike madukani kwetu ili waweze kununua bidhaa zetu na kujipatia zawadi hizo, " alisema.

Aidha alisema anatambua kuwa  kuwahudumia wateja zaidi ya 500,000 si kazi ndogo na kuongeza kuwa hali hiyo imetokana na kukua kwa uelewa wa wananchi juu ya matumizi hayo  ya nishati ya umeme unatokana na jua.

Hata hivyo alisema nchi haiwezi kufikia uchumi wa viwanda bila kuwa na umeme wa uhakika katika maeneo mengi ya nchi hivyo kama kampuni watahakikisha wanawafikia wananchi hasa waliopo vijijini.

Naye mteja wa mitambo ya umeme  inayouzwa katika kampuni hiyo kutoka Tarime,  Sophia Simon alisema mitambo inayouzwa na kampuni hiyo ni imara na tangu ainunue haijawahi kuzima hata kama mvua inyeshe wiki nzima.
Share:

Wednesday, August 14, 2019

Facebook, together with Africa Check, expands its local language coverage as part of its Third-Party Fact-Checking Programme



Facebook, today with Africa Check announced that it has added new local language support for several African languages as part of its Third-Party Fact-Checking programme - which helps to assess the accuracy of news on Facebook, and aims to reduce the spread of misinformation.

Launched in 2018 across five countries in Sub-Saharan Africa, including South Africa, Kenya, Nigeria, Senegal and Cameroon, Facebook has partnered with Africa Check, Africa's first independent fact-checking organization, to expand its local language coverage across:

·  Nigeria, in Yoruba and Igbo, adding to Hausa which was already supported
·  Swahili in Kenya
·  Wolof in Senegal
·  AfrikaansZuluSetswanaSothoNorthern Sotho and Southern Ndebele in South Africa

Kojo Boakye, Facebook Head of Public Policy, Africa, said: “We continue to make significant investments in our efforts to fight the spread of false news on our platform, whilst building supportive, safe, informed and inclusive communities. Our third-party fact-checking programme is just one of many ways we are doing this, and with the expansion of local language coverage, this will help in further improving the quality of information people see on Facebook. We know there is still more to do, and we’re committed to this.

Commenting, Noko Makgato, executive director of Africa Check, said "We're thrilled to be expanding the arsenal of the languages we cover in our work on Facebook's third-party fact-checking programme. In countries as linguistically diverse as Nigeria, South Africa, Kenya and Senegal, fact-checking in local languages is vital. Not only does it let us fact-check more content on Facebook, it also means we'll be reaching more people across Africa with verified, credible information."

About Third-Party Fact-Checking
Facebook's fact-checking programme relies on feedback from the Facebook community, as one of many signals Facebook uses to raise potentially false stories to fact-checkers for review. Local articles will be fact-checked alongside the verification of photos and videos. If one of Facebook’s fact-checking partners identifies a story as false, Facebook will show it lower in News Feed, significantly reducing its distribution.

Share:

Absa Group Reports 3% Increase in Earnings, Bolstered by Improved SA Retail and Business Banking Unit Performance



Absa Group Limited, one of Africa’s largest financial services providers and parent company of Barclays Tanzania reported a 3% increase in earnings for the first half of 2019 as its retail unit in South Africa gained market share, mitigating the negative effects of a difficult economy.

Absa Group, which has a presence in 12 countries in Africa and an office in London, said normalised headline earnings increased to R8.3 billion during the first six months of the year from R8.04 billion during the same period in 2018. Income and costs both grew at 6%. Normalised earnings are considered the best measure of underlying group performance as it strips out the distorting effect of items related to the separation from Barclays PLC.

“Despite the tough operating environment, we have been able to maintain revenue momentum in our key target areas, with total revenue growth improving to 6%,” said Jason Quinn, Absa Group Financial Director.

Absa Group’s largest business unit, Retail and Business Banking South Africa (RBB SA), is showing faster than market growth in key product areas, in line with the group’s commitment to regain its leading position. RBB SA increased its share of home loans new business, with home loan registrations growing 16% - more than double the growth in total home loan registrations in South Africa during the first half. Retail deposits grew 12% while the market increased 9%. New personal loans increased 20%. RBB SA reported a 4% increase in earnings.

Corporate and Investment Banking (CIB) earnings decreased 5% on a pan-African basis, following a difficult trading period in South Africa. However, the client franchise continued to perform well with notable client acquisitions across the countries in which Absa has a presence. The corporate franchise extended its track record of double-digit revenue growth.

Absa’s subsidiaries outside of South Africa, collectively known as Absa Regional Operations (ARO), continued to increase their contribution to group earnings. ARO’s earnings rose 8% during the period, to account for more than a fifth of total Absa Group earnings.

Business Review

“We’ve made significant progress with Absa’s reorganisation following the implementation of our new strategy in March 2018, and we are beginning to see the benefits,” said René van Wyk, Absa Group CEO. “There is still, however, significant work to be done before we can reach our growth, returns and cost targets - a difficult task in a challenging environment,” he said.

RBB SA, which accounts for more than 60% of Absa group income, has largely completed its reorganisation and expects to reap further benefits from its integration with Absa’s wealth and investment management and insurance business. The integration, which is underway, will result in a seamless offer for customers between banking and non-banking services.

At CIB, significant work has been undertaken to form an integrated pan-African franchise with a single growth strategy that covers all of the countries where Absa has a presence.

ARO is implementing its new operating model, aligned to the group strategy which devolves accountability and decision-making closer to the customer interface.

“ARO remains a key contributor to the Group’s performance and with our strong focus on entrenching our brand across the African continent, we have built a strong base to drive growth and to attain our pan-African aspirations. Our results reflect a financial institution that has paid attention to market demand and the need to focus on regionally sourced earnings and growth,” said Peter Matlare, Deputy Chief Executive Officer, Absa Group and ARO CEO.

Matlare added: “Our investments in digitalisation and new ways of banking allow us to challenge existing models and positions Absa for growth. Our investment focus is to ensure that our brand delivers sustainable returns in complex markets, which require a deep understanding of local requirements and the need to always put the client at the heart of the business.”

Parallel to the reorganisation work across business units, Absa continues to make good progress in separating its operations from Barclays PLC, and in enhancing its digital capability.

After launching ChatBanking on WhatsApp, Samsung Pay, Timiza and Jumo, earlier, Absa significantly enhanced its Absa app in the first half of the year, resulting in a 20% increase in the number of app users.

Outlook

South Africa’s economic growth outlook appears muted, with gross domestic product (GDP) expected to grow 0.5% in 2019. The prospects for stronger growth are constrained by the slowing global economy, plus weak business sentiment and decelerating household income growth in South Africa. In the group’s ARO markets, GDP is expected to grow 5.5%.

“While Absa’s return on equity (RoE) is likely to be marginally lower in 2019, the group remains committed to its RoE target of 18% to 20% in 2021,” Quinn said.

Absa Group headline earnings (South African Rand million)


Note: Normalised financial results, which strip out the distorting effect of separation-related items, are presented to better reflect the Group’s underlying performance.
Share:

Tuesday, August 13, 2019

NBC yazidi kuboresha mtandao wa mawakala wake

Na Mwandishi Wetu,
BENKI ya NBC imewahakikishia wateja na wananchi kwa ujumla kuwa mtandao wa mawakala wake unazidi kuongezeka sehemu mbalimbali nchini kote huku wakizidi kuboresha huduma za NBC Wakala ili kuhakikisha wateja wanapata huduma bora na zinazokidhi mahitaji yao.

Akizungumza wakati wa semina iliyoandaliwa na benki hiyo kwa Mawakala wake zaidi ya 600 jijini Dar es Salaam hivi karibuni Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi alisema pamoja na kuboresha mtandao wa mawakala benki imeendelea pia kuboresha mtandao wake wa kidigitali, ATM na matawi yao yaliyotapakaa sehemu mbalimbali nchini.

Akizungumzia kuhusu semina mawakala Bwana Sabi alisema, semina hiyo pamoja na kwamba ni matakwa ya ya kisheria ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), bali pia wanapata fursa ya kukutana na wafanyabiashara na kuzungumza jinsi biashara inavyokwenda, maeneo ya kuboresha, changamoto zinazowakabili na kuona jinsi benki inavyoweza kuzitatua.

“Tumezungumza mengi, lakini zaidi ni fursa kwa walaji wa mwisho za huduma za kibenki, tumeweza kuwaeleza mawakala juu ya huduma za benki na jinsi mtandao huu wa mawakala unaokuwa kwa kasi unavyoimarika, na pia ambavyo tunaendelea kuboresha huduma zetu.

“Utaratibu huu utaendelea japo mara mbili kila mwaka ili kuhakikisha tunakuwa karibu sana na wenzetu hawa mawakala  ambao ni muhimu sana kwetu katika kuhakikisha  walaji wa mwisho wa huduma zetu wanapata huduma zilizo bora na zinazokidhi mahitaji yao,” aliongeza mkurugenzi huyo.  

Naye Mkuu wa Huduma za Benki Kidigitali wa NBC, Deogratius Mosha alisema NBC Wakala iliyoanza Mwezi June, 2018 na kufikisha mawakala zaidi ya 1800 ni moja ya mkakati wa benk hiyo katika kuunga mkono azma ya serikali katika kuhakikisha wananchi walio wengi wanafikiwa na huduma za kibenki.

“Tumekutana hapa ili kufahamu kutoka kwao yale yanayojiri katika maeneo wanayofanyia biashara na pia kuwajengea uwezo na elimu ya utoaji wa huduma za kibenki sambamba na kanuni za sheria ya utoaji wa huduma za kibenki inavyotaka tufanye,” alisema.    

Pamoja na hayo alisema NBC ipo mbioni katika kuhakikisha kuwa huduma zao nyingi zinapatikana kupitia mawakala kama kufungua akaunti za papo hapo (fasta akaunti), vituo vya kukusanya taarifa za miamala, huduma za mikopo, bima, taarifa za ubadilishaji wa fedha za kigeni, na pia wateja kuwasilisha malalamiko na maoni kuhusu huduma za NBC tofauti na ilivyo sasa ambapo huduma hizo hupatikana katika matawi pekee.

“NBC inayo malengo kuwa ifikapo Mwaka 2020 sehemu kubwa ya huduma zinazopatikana kwenye matawi ziweze kupatikana kupitia mawakala wao na hiyo itawasaidia pia katika kuwaongezea kipato,” aliongeza Bwana Mosha.

Mmoja wa Mawakala waliohudhuria semina hiyo, Mama Tumaini Bureta wa Mikocheni, Dar es Salaam alitoa pongezi kwa NBC akisema amejifunza mengi hapo ikiwa ni mara yake ya kwanza kushiriki hivyo ana matumaini mrejesho waliotoa kwa NBC ukitekelezwa unaweza kuboresha huduma wazitoazo na wao kufaidika kwa sehemu kubwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi, akizungumza na baadhi ya mawakala wa benki hiyo wakati wa Semina ya siku moja kuhusu elimu ya utoaji wa huduma za kifedha kwa mawakala iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mkuu wa huduma za benki kidigitali wa Benki ya NBC, Deogratius Mosha, akizungumza na baadhi ya mawakala wa benki hiyo wakati wa Semina ya siku moja kuhusu elimu ya utoaji wa huduma za kifedha kwa mawakala iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Meneja Ukuzaji wa Biashara wa Kitengo cha biashara ndogondogo na za kati wa Benki ya Taifa ya Biashara, Jonathan Bitababaje, akizungumza na baadhi ya mawakala wa benki hiyo wakati wa Semina ya siku moja kuhusu elimu ya utoaji wa huduma za kifedha kwa mawakala iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Theobald Sabi, akizungumza na baadhi ya mawakala wa benki hiyo wakati wa Semina ya siku moja kuhusu elimu ya utoaji wa huduma za kifedha kwa mawakala iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Pamoja naye ni baadhi ya maofisa wa ngazi za juu wa benki hiyo.
Mkuu wa huduma za benki kidigitali wa Benki ya NBC, Deogratius Mosha (kushoto), akikabidhi cheti kwa mmoja wa mawakala wao Monica Kikoti baada ya kuhudhuria semina kuhusu elimu ya utoaji wa huduma za kifedha kwa mawakala iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Baadhi ya Mawakala wa Benki ya NBC wakihudhuria semina iliyoandaliwa na benki hiyo juu ya utoaji wa huduma za kifedha kupitia NBC Wakala, jijini hivi karibuni.
Mnadhimu Mkuu Ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya NBC, Joyce Mbago (kushoto), akikabidhi cheti cha wakala wa benki hiyo Dianarose Buddybruno katika semina kuhusu elimu ya utoaji wa huduma za kifedha kwa mawakala hao iliyoandaliwa na NBC jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Share:

FAINALI ZA PROPHET SUGUYE CUP ZAFANA

Na Mwandishi Wetu,
Mashindano ya mpira wa miguu yaliyopewa jina la Prophet Suguye Cup ambayo yalikuwa yanatimua vumbi katika viwanja vya Shule ya Msingi Misitu iliyopo Kivule, Ukonga, Dar es Salaam na kudhaminiwa na Muasisi wa Mashindano hayo Nabii Nicolaus Suguye wa Kanisa la WRM lenye Makao yake Makuu Kivule matembele ya Pili, Ukonga, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi kwa mshindi wa mashindano hayo, muasisi wa mashindano hayo Nabii Nicolaus Suguye amesema lengo la Mashindano hayo ni kuwaweka pamoja na kuwahamasisha vijana kufanya kazi ili kuwasaidia kukwepa maovu yatokanayo na kukaa vijiweni bila shughuli maalumu.

Mashindano hayo yalianza kutimua vumbi tarehe 25 Mei 2019 na kufikia tamati hapo jumamosi ya tarehe 10 Agosti 2019 kwa timu ya FAIRPLAY kuibuka wafalme wa kwanza wa mashindano hayo yaliyoshirikisha timu 24 kutoka maeneo yanayounganisha jimbo la Ukonga wilayani Ilala, Dar es Salaam.

Timu ya FAIRPLAY ya KIVULE jijini DAR ES SALAAM imeibuka kidedea na kuchukua ubingwa wa mashindano hayo baada ya kuichabanga timu ya KIVULE FOREST kwa jumla ya bao mbili kwa moja, katika fainali ya ligi ya mpira wa miguu ya PROPHET SUGUYE CUP.


Wachezaji wa Fairplay FC wakifurahia baada yakukabidhiwa kombe na Nabii Nicolaus Suguye wa Kanisa la WRM na Muanzilishi wa ligi hiyo, wakati wa mchezo wa fainali katika mchezo wa Ligi ya Prophet  Suguye Cup iliyokuwa ikiendelea katika Viwanja vya Shule ya Msingi Misitu Kivule, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam ambapo Fair Play iliibuka kidedea kwa mabao 2-1. Nakufanikiwa kushika nafasi ya kwanza katika Mchezo huo nakukabidhiwa kombe na Mwanzilishi wa ligi hiyo Nabii Nicolaus Suguye.
Mshambuliaji wa timu ya Fair Play FC, akijaribu kuwatoka mabeki wa  Kivule Forest FC, wakati wa mchezo wa Fainali Ligi ya Prophet  Suguye Cup iliyokuwa ikiendelea katika Viwanja vya Shule ya Msingi Misitu Kivule nje kidogo ya Jiji la DaresSalaam ambapo Fair Play iliibuka kidedea kwa mabao 2-1, nakufanikiwa kushika nafasi ya kwanza katika mchezo huo nakukabidhiwa kombe na Mwanzilishi wa ligi hiyo Nabii Nicolaus Suguye wa kanisa la WRM.
Nahodha wa Fair Play akipokea kombe kutoka kwa Mwanzilishi wa ligi hiyo Nabii Nicolaus Suguye wa kanisa la WRM baada ya kuibuka na ushindi wakati wa mchezo wa Fainali katika mchezo wa Ligi ya Prophet Suguye Cup iliyokuwa ikiendelea katika Viwanja vya Shule ya Msingi Misitu Kivule, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam ambapo ambapo Fair Play iliibuka kidedea kwa mabao 2-1. Nakufanikiwa kushika nafasi ya kwanza katika   Mchezo huo nakukabidhiwa kombe na Mwanzilishi wa ligi hiyo Nabii Nichoraus Suguye wa kanisa la WRM lililopo Kivule Matembele ya pili, Mchezo huo umepigwa leo viwanjani hapo.
Nahodha wa Kivule Forest FC, Jolvin Balotel akipokea kombe kutoka kwa Nabii wa Kanisa la UKOMBOZI MINISTRIES FOR ALL NATIONS-BG.MALISA baada ya kushika nafasi ya pili wakati wa mchezo wa Fainali Ligi ya Prophet Suguye Cup iliyokuwa ikiendelea katika Viwanja vya Shule ya Msingi Misitu Kivule, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam ambapo Fair Play iliibuka kidedea kwa mabao 2-1. Nakufanikiwa kushika nafasi ya kwanza katika Mchezo huo.
Nahodha wa Kivule FC akionesha kombe baada yakukabidhiwa.
Wachezaji wa timu hizo wakiwania mpira wakati wa mchezo wa fainali.
Share:

Monday, August 12, 2019

RAIS WA AFRIKA KUSINI KUTUA NCHINI JUMATANO NA KUPOKELEWA NA RAIS DKT. JOHN MAGUFULI


Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa anatarajiwa kuwasili Nchini Jumatano ya August 14 kwa Mwaliko wa Ziara ya kitaifa (State Visit) ya siku mbili ambapo atapokelewa na Mwenyeji wake Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amesema Rais Ramaphosia atawasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere majira ya Saa Tano usiku na baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili ataendelea kubaki Nchini kwaajili ya kushiriki Mkutano Mkubwa wa Viongozi wakuu Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini Mwa Afrika SADC.

Aidha RC Makonda amesema Maraisi wa Mataifa mengine wataendelea kuingia Nchini kuanzia August 16 ambapo amewataka wananchi kuwa wakarimu kwa wageni na kutumia vizuri fursa ya ujio wa Viongozi hao.
Share:

Thursday, August 8, 2019

DCB KUSHIRIKIANA NA MANISPAA KUTEKELEZA MIRADI YA KIMKAKATI

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (kushoto), akikabidhi cheti kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya  DCB, Godfrey Ndalahwa kwa kutambua mchango wa benki hiyo katika kufanikisha Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Shirikisho la Serikali za Mitaa (ALAT), uliofanyika mjini Mwanza hivi karibuni. Katikati ni Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo.  (Picha na DCB).

Wziri Mkuu Kassim Majaliwa (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Biashara ya DCB, Rahma Ngassa baada ya kukabidhi cheti kwa Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa (hayupo pichani), kwa kutambua mchango wa benki hiyo katika kufanikisha Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Shirikisho la Serikali


Na Mwandishi Wetu

 BENKI ya Baisahara ya DCB imesema itaendelea kushirikiana kwa karibu zaidi na manispaa mbalimbali nchini na kwa sasa ikija na mpango maalumu kupitia huduma maalumu (municipal bonds), ili kuziwezesha manispaa hizo kupata pesa kwa ajili ya kutekeleza miradi ya kimkakati.

Akizungumza Jijini Mwanza hivi karibuni Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa alisema mpango huo utakaosaidia upatikaji wa fedha kuendesha miradi ya kimkakati una masharti wezeshi kwa mkopaji na tayari wameshaanza mazungumzo na manispaa na wadau wengine muhimu katika mchakato huo.c

"Mchakato wa uanzishwaji wa huduma hii unaendelea tutakachofanya ni kuongeza manispaa na halmashauri nyingine ambazo pia zina miradi ya kimkakati kuweza kujumuishwa kwenye mpango huu.

 “Ombi langu ni kwamba najua vyanzo viko vingi lakini hii yenyewe inaweza ikawa chanzo kizuri cha kutafuta pesa, na vilevile ni chanzo kizuri kwa ajili ya kusaidia umma wa wawekezaji wakubwa na wadogo kupata fursa ya kuwekeza kwenye miradi yetu”, aliongeza.

Mkurugenzi Mtendaji huyo wa DCB alizungumzia pia udhamini na ushiriki wao katika mikutano mbalimbali na shughuli za kijamii ikiwemo Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Shirikisho la Serikali za Mitaa (ALAT) uliofanyika mjini Mwanza hivi karibuni akisema hiyo imetokana na azma ya kuanzishwa kwa benki hiyo ikiwa na kuwahudumia wananchi na wajasiriamali wadogowadogo hasa wanawake na vijana na kufanikiwa kwa azma hiyo kumechangiwa kwa kiasi kikubwa na ushirikiano kutoka katika manispaa na halmashari za Jiji la Dar es Salaam ilikoanzishwa.

"Tumekuwa tukishirikiana kwa karibu sana na manispaa na halmashauri zote za Jiji la Dar es Salaam katika kutoa mikopo ya wanawake na vijana na mafanikio ni makubwa mpaka sasa hivi ukiaangalia hiyo pesa iliyotoka  na wanufaika wamenufaika mara tatu na hii ni kwa sababu ya weledi na uzoefu tulionao”, alisema.

Akizungumza mafanikio ya zoezi la uuzaji hisa lililofanyika hivi karibuni Bwana Ndalahwa alisema zoezi hilo lilifanikiwa kwa asilimia 108  na hiyo imechangiwa sana na   historia yao na mahusiano yao ya karibu na manispaa na halmashauri kwa maana ya kwamba wao ndiyo waanzilishi.

Kuhusu maendeleo ya DCB na mikakati ya kuzidi kujipanua, Mkurugenzi wa DCB alisema wigo wa kufanya biashara umeongezeka kutoka Dar es Salaam pekee na sasa wameruhusiwa kuendesha biashara nchini nzima wakiwa na matawi manane likiwemo la Dodoma pamoja na  mawakala 1000 nchi nzima huku wakipatikana kwenye mtandao hivyo huduma zao kupatikana nchi nzima.

Pamoja na hayo mkurugenzi hiyo alizungumzia huduma yao mpya ya DCB Lamba kwanza inayomwezesha mteja kupata riba ya hadi asilimia 14 siku mteja anapoamua kuwekeza huku akitoa wito kwa watanzania kujiunga na huduma ya DCB Digital kwa njia ya simu za mkononi kwa kubonyeza alama ya nyota 150 nyota 85 reli ili kujiunga na kupata huduma mbalimbali za benki hiyo kwa lugha rahisi wakiita ‘DCB kwanza simu  yako Tawi letu’.


Benki ya DCB ilianzishwa mwaka 2002, ikianzishwa na Maspaa za Dar es Salaam na kujulikana kama Benki ya Wananchi wa Dar es Salaam. Lengo kuu ilikuwa ni kusaidia wajasiriamali wadogowadogo. Baada ya kuanzishwa iliweza kutekeleza lengo hilo na na kuendelea kukua. Mwaka 2008 ilikuwa benki ya kwanza kuorodheshwa kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), na iliendelea kukua hivyo hivyo na baadae kubadilisha jina kutoka Dar es Salaam Community Bank na  kuwa DCB Commercial Bank kwa sasa.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive