A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Friday, January 31, 2020

DCB YATENGENEZA FAIDA YA SHILINGI BILIONI 2.3 MWAKA 2019

Mkurugenzi wa Fedha wa Benki ya Biashara ya DCB, Zacharia Kapama (wa pili kushoto), akisoma hotuba yake katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kutangaza  taarifa za fedha ambapo alisema DCB imepata faida ya shs bilioni 2.3 kwa mwaka 2019 ikiwa ni ongezeko la asilimia 43 kutoka faida ya mwaka 2018 ambayo ilikuwa shs bilioni 1.6. Wengine kutoka kushoto ni; Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano, Rahma Ngassa, Mkurugenzi wa Biashara, James Ngaluko na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Fortunata Benedict, wote kutoka DCB.  

Benki ya biashara ya DCB (DCB Commercial Bank Plc) imetangaza kupata faida ya shilingi bilioni 2.3 katika mwaka 2019, ikiwakilisha ongezeko la asilimia 43 kutoka faida ya mwaka 2018 ambayo ilikuwa shilingi bilioni 1.6

Katika taarifa iliyotolewa kwa vyombo mbalimbali vya habari leo tarehe 31 Januari 2020 na iliyochapishwa katika magazeti kwa mujibu wa sharia za benki kuu, utendaji wa benki umeendelea kuimarika ikilinganishwa na mwaka uliotangulia huku ufanisi katika nyanja zote muhimu ukiongezeka kwa kiwango cha kuridhisha.

Akiwakilisha taarifa za fedha za robo ya nne ya mwaka 2019, mkurugenzi wa Fedha wa benki ya DCB Ndugu Zacharia Kapama, ameeleza kuwa mafanikio haya yametokana na ukuaji wa mizania ya benki, ambao umechagizwa na ukuaji wa amana za wateja kwa asilimia 14 (Shilingi bilioni 10.1), ikilinganishwa na mwaka uliotangulia.

Ukuaji wa amana umeisaidia benki pia kuongeza ukuaji wa mikopo ambapo benki imefanikiwa kuongeza kiwango ghafi cha mikopo kwa asilimia 11 (shilingi bilioni 8.0), ambacho ni kiasi kikubwa ukilinganisha na ongezeko la mikopo katika miaka miwili iliyotangulia. Mikopo ghafi ya benki imekua kutoka shilingi bilioni 90.5 mwaka 2018 kufikia shilingi bilioni 93.3 mwaka 2019.

Ili kufikia kiwango hiki, benki imefanikiwa kutoa mikopo mipya kwa wateja wake kinachofikia shilingi bilioni 60, huku shilingi bilioni 18 zikiwakilisha mikopo kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati (SMEs), na Shilingi Billioni 10 ikiwakilisha mikopo ya wanawake na vijana. Benki pia imeendelea kutoa mikopo kwa sekta mbalimbali zikiwemo sekta binafsi za biashara, elimu afya na ujenzi.

Akielezea upatikanaji wa faida, Ndugu Kapama ameainisha kuwa ukuaji wa faida, ukiachilia mbali kuchangiwa na ukuaji wa mizania, pia umechagizwa na ongezeko la mapato yasiyotokana na riba baada ya benki kufanikiwa kukuza idadi ya wateja wake kutoka 175,000 mwaka 2018 kufikia wateja 194,000 mwaka 2020. Ongezeko hili limeongeza idadi ya akaunti za amana na miamala ya kibenki, huku wateja wakifurahia huduma za kidijitali bila kwenda matawini.

Kwa kuongezea, ufanisi wa benki umeongezeka hasa katika usimamizi wa matumizi ya riba na yasiyo ya riba. Benki imefanikiwa kudhibiti ukuaji wa matumizi yasiyo ya riba, huku ikihakikisha huduma kwa wateja zinaboreshwa. Benki pia imefanikiwa kudhibiti ongezeko la riba kwa wateja na kuhakikisha wateja wanapata thamani bora ya huduma zake bila kuathiri ukuaji wake.

Katika taarifa hiyo, Ndugu Kapama pia ameainisha upunguaji wa mikopo chechefu ya wateja kutoka asilimia 19 mwaka 2018 kufikia asilimia 13 mwaka 2019. Hii imetokana na juhudi za benki kuhakikisha kuna ufanisi na usimamizi madhubuti katika utoaji mikopo na ukusanyaji madeni. Benki itaendelea na juhudi za kuhakikisha mikopo chechefu inafikia kiwango kinachokubalika na wadau wa sekta ya fedha mnamo mwaka huu wa 2020.

Katika miaka yake takriban 17 ya uendeshaji, benki ya DCB imeweza kukuza idadi ya matawi kutoka tawi moja na kufikia manane (8) hadi mwaka huu wa 2019. Pia imekuza idadi ya wateja kufikia 194,000. Ukuaji huu umechangia benki kupata faida mfululizo tangu mwaka 2004 hadi mwaka 2015, na imekuwa ikitoa gawio kwa wanahisa wake katika kipindi chote cha miaka 12.

Hapo mbeleni, benki ya DCB, inatazamia kukuza mizania yake kwa kutumia fursa za ukuzaji biashara na ina azimia kutumia ipasavyo fursa na njia mbadala za utoaji huduma kwa wateja kupitia mitandao, wakala wa kibenki, na upanuzi wa mitandao ya matawi na vituo vidogo vya huduma ambapo itasaidia kwa kiasi kikubwa utengenezaji wa mapato kupitia njia ya mapato yasiyo ya riba.

Benki ya DCB ndio benki ya kwanza kuorodheshwa katika soko la hisa la Dar es Salaam huku ikiwa ndio benki pekee iliyokua kutoka benki ya wananchi/jamii (community bank) na kufanikiwa kuwa benki ya biashara (commercial bank).

Benki ya DCB imefanikiwa kukuza mtandao wa matawi yake kufikia manane huku ikifungua tawi Dodoma na inaendelea na mchakato wa kufungua matawi na vituo vya huduma (service centers) katika mikoa mingine na imefungua mtandao wa mawakala na huduma za kijiditali hadi kufikia mawakala zaidi ya 700 nchini nzima.

Benki imefanikiwa kuongeza mtaji wake kupitia soko la hisa kwa miaka yote 18 huku ikipata faida mfululizo na kujiimarisha kibiashara. Hivi sasa benki inao uwezo wa kutoa mikopo mikubwa zaidi na ya muda mrefu kwa wateja.

Benki imefanikiwa kuzindua mfumo wa akaunti za kidijitali ambapo umeiwezesha kuhudumia wateja wengi zaidi na kuwafikia hadi wale wa vijijini. Hii imeongeza ukuaji wa mapato na ongezeko la idadi ya wateja na ufanisi katika utoaji huduma.

Akielezea maboresho zaidi ya huduma za kibenki yaliyofanyika, Mkurugenzi wa biashara Mr James Ngaluko  alieleza:

Benki imefanikiwa kuzindua huduma na bidhaa mpya kwa wateja wake ambazo ni Lamba kwanza (Fixed deposit), Akaunti ya Skonga, DCB sokoni, pamoja na garantii za wakandarasi zisizo na dhamana wakati wa kuomba tenda.

Tumeboresha huduma ya mikopo ya nyumba ujenzi wa nyumba kwa kuongeza ushirikiano na Tanzania Mortgage Refinancing Company.

Tumeongeza ufanisi wa huduma ya mikopo kwa ushirikiano na  taasisi ya ushauri FSDT, hivyo kufanya huduma ya utoaji mikopo kwa wateja kuwa ya haraka Zaidi.

Benki imeboresha gharama zake kwa kuondoa gharama katika akaunti za community kama vikoba, akaunti za miradi ya serikali, na akaunti za wastaafu. Hii imepelekea kuongeza idadi kubwa ya wateja ambao wengi ni wa kipato cha cha chini na cha kati.

Benki ya Biashara ya DCB ilianzishwa mwaka 2002 (Ikijulikana kama Dar es Salaam Community Bank)  kutokana na kilio cha wakazi wengi wa jiji la Dar es Salaam kutokuwa na namna ya kupata mitaji midogo ya biashara jambo ambalo lilikuwa changamoto kubwa kwa wajasiriamali wadogo wadogo katika jitihada za kuboresha biashara zao sambamba na masharti magumu kutoka kwa benki nyingi za kibiashara. Kwa kipindi chote cha miaka 17 ya uendeshaji, jukumu mama la benki hii limeendelea kuwa ni kutoa huduma bora za kifedha huku ikijikita zaidi katika kutengeneza miradi endelevu ya kupunguza umaskini na kuendeleza jamii.
Share:

Thursday, January 30, 2020

KAMPENI YA USAFI YA OMO NG’ARISHA YAZINDULIWA

Umati wa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waliofurika katika Uwanja wa Mbagala Zakhem, Dar es Salaam jana, kushuhudia uzinduzi rasmi wa Kampeni usafi ya OMO Ng'arisha Festival wakifuatilia matukio ya uzinduzi huo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Unilever Tanzania, David Minja (wa nne kushoto), akikata utepe kuzindua kampeni ya kitaifa ya usafi wa iliyopewa jina la Omo Ng'arisha Festival katika Uwanja wa Mbagala Zakhem, jijini Dar es Salaam jana.
Wasichana wa promosheni wa Kampeni ya OMO Ng'arisha festival, wakishika mifuko yenye sabuni za Omo kunogesha uzinduzI rasmi wa kampeni ya miezi sita ya usafi iliyopewa jina la OMO Ng'arisha Festival katika Uwanja wa Mbagala Zakhem, jijini Dar es Salaam jana.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Unilever Tanzania, David Minja, akizungumza na umati wa watu uliojitokesa katika Uwanja wa Mbagala Zakhem, Dar es Salaam jana kushuhudia uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya usafi iliyopewa jina la OMO Ng'arisha familia katika Uwanja wa Mbagala Zakhem, jijini Dar es Salaam.
Wakazi wa Jiji la Dar e Salaam wakichangamkia kununua sabuni za OMO wakati wa uzinduzi wa kampeni ya OMO Ng'arisha Festival jijini humo jana.
Mkazi wa Jiji la Dar es Salaam akisikiliza maelezo kuhusu ubora wa sabuni ya OMO kutoka kwa wasichana wa mauzo wa bidhaa hiyo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya OMO Ng'arisha Festival jijini Dar es Salaam jana.
Hapa wakionyesha jinsi ya ufuaji bora wa nguo kwa kutuma sabuni ya OMO ili kupata matokeo bora. Hapo ni katika Uwanja wa Mbagala Zakhem, Dar es Salaam kwenye wa Kampeni ya OMO Ng'arisha Festival.
Balozi wa Kampeni ya OMO Ng'arisha Festival, msanii nguli wa muziki wa taarabu nchini Tanzania, Bi. Isha Mashauzi akifanya vitu vyake wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo jijini Dar es Salaam jana.
Msani mahiri wa muziki wa singeli, Seif Mwinjuma 'Sholo Mwamba' akikonga nyoyo za maelfu ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waliofurika katika Uwanja wa Mbagala Zakhem, Dar es Salaam jana kushuhudia uzinduzi rasmi wa Kampeni ya OMO Ng'arisha Festival.


UNILEVER TANZANIA Kampuni inayotengeneza bidhaa mbalimbali leo inazindua kampeni maalumu ya usafi kwa kipindi cha miezi sita iitwayo ‘OmoNg’arisha Festival’ itakayofanyika Tanzania nzima ikiwa na lengo la kuhamasisha faida, ubora na matumizi sahihi ya sabuni bora ya Omo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo katika Uwanja wa Mbagala Zakhem, Jijini Dar es Salaam leo, Meneja Masoko wa bidhaa ya Omo, Bi. Upendo Mkusa alisema ni matumaini yao kwa kupitia kampeni hiyo jamii itatambua matumizi sahihi ili kupata matokeo yanayotarajiwa.

“Ni matumaini yetu watanzania watatumia sabuni ya Omo kwa usahihi kutokana na ukweli kuwa Omo Fast Action na Omo Extra Fresh ni bora katika kupambana na uchafu kwani ina nguvu zaidi ya mara 10 kuliko sabuni za kawaida na ni ukweli kuwa ukitumia Omo kufulia nguo za familia yako wewe na nguo za familia yako mtang’aa, nguo zako ziking’aa wewe na familia yako mtang’aa, pia tunataka kuona watanzania waking’aa,” alitanabaisha Bi. Upendo.

Akizungumza zaidi kuhusu kampeni hiyo, Bi.Upendo meneja masoko wa Omo alisema mara baada ya uzinduzi huo, kampeni hiyo itaendelea katika mikoa ya Dodoma, Dar, Mwanza, Arusha, Moshi na Mbeya. Kuifanya kampeni hii kuwa yenye bashasha na mvuto, Unilever Tanzania inamtangaza Msanii maarufu nchini Tanzania, Bi. Isha Mashauzi kuwa  Balozi wa Kampeni hii ya Omo Ng’arisha, ambaye atakayeshiriki katika matukio mbalimbali katika kampeni hii ikiwemo michezo ya kufurahisha na burudani ya muziki kutoka kwa wasanii mbalimbali.

Kampeni itashirikisha timu ya promosheni ya Omo kwa kupita mlango kwa mlango majumbani, kwenye maeneo ya wazi na katika sehemu za biashara kuijulisha jamii juu ya ubora, faida na matumizi sahihi ya OMO, ambayo ni moja ya bidhaa kubwa zaidi ya Unilever.

Bi. Upendo meneja huyo alisema pia, wameandaa zoezi maalumu la kuwatambua Wanawake Wajasiriamali 10 katika kila mkoa watakapofanya kampeni hiyo na kuwapa zawadi itakayowasaidia kuboresha biashara zao hivyo kuwafanya kung’aa.“Ni imani yetu wanawake hawa miongoni mwao kuna wenye biashara ndogondogo, tutawatambua na kuwapa zawadi. Ni matarajio yetu utambuzi huu utaleta tija na kuwa kichocheo katika utendaji wao na kukuza biashara zao’’, alimalizia Bi Upendo Mkusa. 

Akizungumza kwenye uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Unilever Tanzania, Bw. David Minja, alisema “Unilever inatambua na kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kuendeleza uchumi wa viwanda na katika kuwaletea watu wake maendeleo na kwa kuonyesha uungaji wetu mkono, timu yetu ya kampeni katika mikoa hiyo tuliyoitaja itatembelea katika mahospitali ambako tutaonyesha moyo wa kujali kwa kutoa msaada wa sabuni za Omo kwenye hospitali ya mikoa hiyo tukiongozwa na balozi wetu wa Omo Bi. IshaMashauzi.

“Katika kuendelea kuunga mkono kwa vitendo juhudi za serikali ya awamu ya tano, tutakuwa mstari wa mbele kuhimiza jamii na wananchi kufanya usafi wa mazingira yao, na nina furaha kwamba kupitia kampeni ya Omo Ng’arisha katika kila mkoa tutakaopitia, timu yetu ya Omo Ng’arisha itashiriki katika shughuli za usafi kwa kushirikiana na viongozi wa mkoa huo,” aliongeza Bw.Minja.

Aidha Mkurugenzi Mkuu huyo alisema Unilever inatoa shukrani kubwa kwa ushirikiano inaoupata kutoka mamlaka mbalimbali za kibiashara na kiserikali hapa nchini. “Tunaipongeza Serikali ya awamu ya tano kwa kuweka mazingira wezeshi na juhudi yake katika kuzifanyia kazi changamoto mbalimbali zinazoikabili jumuiya ya wafanyabiashara. Kwa upande wetu tunaahidi kuongeza ubora wa bidhaa zetu kuhakikisha zinakidhi mahitaji ya wateja wetu, tukifanya biashara kwa kuzingatia kanuni na taratibu zote zilizopo huku tukiangalia namna bora zaidi ya kuinufaisha jamii ya watanzania,” alisema.    

Licha ya bidhaa ya Omo ikiwa na aina mbili za Omo Fast Action na Omo Extra Fresh yenye nguvu mara kumi zaidi, Unilever inazo bidhaa nyingine kama; Sunlight-sabuni ya unga, inayotakatisha vizuri, yenye manukato na kulainisha ngozi, mafuta ya mgando na losheni ya Vaseline yenye uwezo wa kutunza ngozi,Vim-sabuni ya kusafishia ambayo ni kiboko ya uchafu wa nyumbani,  AXE-sprei ya mwili kwa wanaume inayokuacha na harufu nzuri kwa zaidi ya masaa 48 na Royco mchuzi mix, kiungo cha chakula chenye viungo asilia 16 kwa kuongeza ladha murua ya chakula.
Share:

Monday, January 27, 2020

NBC yawataka wanawake wajasiriamali kujiunga na klabu ya biashara ya benki hiyo

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia  Uwekezaji, Angela Kairuki, (wa pili kushoto) akishikana mikono na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Rejareja Maalum wa Benki ya NBC, Ashura Waziri wakati wa semina ya kwanza ya wanawake wa Kiislam kuhusu Ujasiliamali na  Tanzania ya Viwanda iliyofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. Wengine ni baadhi ya maofisa wa NBC na waalikwa wengine.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Angela Kairuki (wa pili kushoto), akishikana mikono na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Rejareja Maalum wa Benki ya NBC, Ashura Waziri wakati wa semina ya kwanza ya wanawake wa Kiislam kuhusu Ujasiliamali na  Tanzania ya Viwanda iliyofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. Weningine kutoka kushoto ni Meneja wa Tawi la NBC Corporate, Mariam Kombo, Meneja wa Tawi la NBC samora Zubeider Haroun, pamoja na mjumbe wa kamati ya maandalizi ya semina  hiyo, Mariamu Dedes.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Rejareja Maalum wa Benki ya NBC, Ashura Waziri, akizungumza na Wanawake wajasiliamali wakati Warsha ya kwanza ya wanawake wa Kiislam kuhusu  Ujasiliamali na  Tanzania ya Viwanda iliyodhaminiwa na Benki ya NBC na kufanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita. Mgeni rasmi katika semina hiyo alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Angela Kairuki akimwakilisha Makamu wa Raisi, Mama Samia suluhu Hassan.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Angela Kairuki (katikati), akipunga mkono wakati akiondoka katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es salaam juzi, baada ya kufungua semina ya kwanza ya wanawake wa Kiislam kuhusu Ujasiliamali na Tanzania ya Viwanda iliyodhaminiwa na Benki ya NBC. Kushoto ni Naibu waziri wa zamani na mmoja wa viongozi wa wanawake wa kiislamu katika Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Mama Shamin Khan pamoja na wahudhuriaji wengine.
Baadhi ya Washiriki wakiwa katika semina hiyo kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es salaam juzi. Semina hiyo ilidhaminiwa na Benki ya NBC. (Picha zote na Brian Peter)
Share:

Tuesday, January 21, 2020

BILLION PAINTS YATOA NDOO 500 ZA RANGI KATIKA KUBORESHA ELIMU DAR

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akizungumza na wanahabari wakati alipokwenda kutembelea kiwanda cha utengenezaji wa rangi cha Billion Paints
Meneja Masoko wa  kampuni ya utengenezaji wa Rangi cha Billion Paints Ruth Muruve, 
akizungumza na wanahabari wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda alipokwenda kutembelea kiwanda hicho.
 
Januari 21 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amepokea ndoo mia tano kutoka katika kampuni ya utengenezaji wa rangi cha Billion Paints ambazo zimeelekezwa katika shule jijini humo ikiwa ni sehemu ya ushiriki wao katika kuboresha sekta ya elimu nchini.

Akizungumza mara baada ya kutembelea kiwanda hicho na kukabidhiwa rangi hizo Makonda amesema kuwa kiwanda hicho ambacho kilianzishwa mwaka 2017 na kijana mtanzania aliyeitikia wito wa Rais Magufuli katika suala la ujenzi wa viwanda matunda yameanza kuonekana na wamekuwa sehemu ya ushiriki wa shughuli za kijamii ikiwemo elimu.

Makonda amesema kuwa rangi hizo zitasaidia katika ujenzi wa vyumba vya madarasa 380 kwa uwiano wa wanafunzi 50 kwa darasa moja unaendelea katika Wilaya ya Temeke ambako wanafunzi 5970 wameshindwa kuanza masomo yao kutokana na ufinyu wa madarasa.

"Wanafunzi 5970 waliofaulu walikosa vyumba vya madarasa na kupitia waraka uliotolewa na Wizara ya elimu tunategemea kufikia Machi Mosi wanafunzi  wote watakuwa darasani wakiendelea na masomo, na tunawashukuru Billion Paints kwa mchango huu na kwa kutambua hili tutachora 'Billion' ili kutambua mchango huu" ameeleza.

Aidha Makonda amesema kuwa hadi kufikia sasa shule mpya nne zimeanzishwa, ujenzi wa madarasa na matundu ya choo unaendelea na hiyo ni pamoja na ukarabati wa miundombinu na madawati.

"Ninawaomba wadau na washiriki kama Billion wajitokeze na tushirikiane katika kuimarisha sekta hii adhimu na wazazi hawatachangishwa chochote elimu itatolewa bure kama Rais Dkt. John Joseph Magufuli alivyoelekeza" amesema Makonda.

Vilevile amewashauri vijana kutumia fursa mbalimbali zinazojitokeza ili kuweza kujikwamua kiuchumi na kujenga taifa imara kama mwanzilishi wa kiwanda hicho alivyothubutu na kuajiri vijana wengine arobaini.

Kwa upande wake Meneja masoko wa kiwanda hicho Ruth Muruve amesema kuwa wataendelea kushirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam katika kuboresha sekta ya elimu nchini na wametoa rangi hizo ili kutengeneza mazingira bora ya ujifunzaji kwa wanafunzi.

Amesema kuwa kampuni hiyo ya wazawa inazalisha aina saba za rangi na inapatikana kwa gharama nafuu.


Share:

Liquid Telecom to launch first 5G wholesale roaming network service in South Africa

lqt0632_gd
Liquid Telecom to launch first 5G wholesale roaming network service in South Africa
Access to ultra-fast roaming network will enable network operators to create innovative, reliable and scalable digital services for their customers

Johannesburg, January 20, 2020 – Leading pan-African telecoms group Liquid Telecom is to launch the first 5G wholesale roaming service in South Africa. Available from early 2020 in all major South African cities, this latest fifth generation of mobile internet connectivity will enable wholesale operators to create innovative, ultra-fast and scalable digital services for their customers.

The 5G wholesale network will also help accelerate the evolution of the Fourth Industrial Revolution (4IR) in South Africa. Reliable connectivity up to 10 times faster than 4G will allow businesses to harness trends such as the Internet of Things (IoT), robotics and artificial intelligence (AI) to innovate transformative new services, increase productivity and deliver more connected customer experiences.

 “This breakthrough 5G wholesale service will create innovation in every aspect of South African society and industry,” says Strive Masiyiwa, Chairman, Liquid Telecom. “For the first time, mobile network operators and ISPs will have open access to Liquid Telecom’s new 5G mobile network. The launch of the service also underscores Liquid Telecom’s vision to bring high-speed connectivity to everyone.”

Liquid Telecom will use its 3.5GHz spectrum asset to build the 5G network and provide nationwide 5G wholesale services to the market early in 2020.

One of the most profound implications of the new service will be its impact on South Africa’s 4IR ambitions, where connected devices communicate with each other, automating the factory floor without the need for human intervention. The fusion of 5G, IoT and other technologies like AI and robotics will touch and transform every facet of business, creating entirely new ways of serving existing needs.

“This is a milestone moment for Liquid Telecom South Africa,” said Nic Rudnick, Group CEO. “Our wholesale operating partners can exploit our new ultra-fast 5G roaming network to build the next generation of communications and make innovation possible, anytime, anywhere. 5G will facilitate real-time remote collaboration, improved business efficiency and lower costs – ultimately driving growth in the South African economy.”

The launch of the 5G wholesale roaming service is another step towards Liquid Telecom ‘Building Africa’s digital future’. The organisation has been investing heavily across the continent where it operates Africa’s largest independent fibre network, spanning almost 70,000km length.

About Liquid Telecom

Liquid Telecom is a leading communications solutions provider across 13 countries primarily in Eastern, Southern and South Africa that serves mobile operators, carriers, enterprise, media and content companies and retail customers with high-speed, reliable connectivity, hosting and co-location and digital services.

 It has built Africa’s largest independent fibre network, approaching 70,000km, and operates state-of-the-art data centres in Johannesburg, Cape Town and Nairobi, with a combined potential 19,000 square metres of rack space and 78 MW of power.

This is in addition to offering leading cloud-based services, such as Microsoft Office365 and Microsoft Azure across our fibre footprint. Through this combined offering Liquid Telecom is enhancing customers’ experience on their digital journey. In October 2019, Liquid Telecom was recognised as ‘The Best African Wholesale Carrier’ for the 8th consecutive year at the Global Carrier Awards. www.liquidtelecom.com
Share:

Wednesday, January 15, 2020

SAYONA DRINKS LIMITED LAUNCHES ‘TWIST AVATAR’ INTO THE MARKET


15th January 2020, Dar es salaam. Sayona drinks customers will now have more choices after the Dar es Salaam-based fast-growing beverage company - Sayona Drinks Limited re-launches its soft drink brand by the name of TWIST. Sayona Drinks seeks to provide its consumers with as many options as possible that fit within their various tastes.

Unveiling the re-branded product at the launch event, Pawan Patel, Sayona Drinks Limited Managing Director said, “Twist is refreshing, has great taste and provides real value for money. Twist comes in 7 distinctive flavours of Passion, Orange, Lemon, Mango, Pineapple, Ginger and Cola flavours. He also mentioned that the brand will soon introduce more exciting flavours in the near future.

He added that at Sayona, we aim to meet the ever-changing tastes of our consumers and this is the reason why we strive to be innovative by introducing new products in the market every year.

“We believe in Twist, we have a strong product that is different from anything currently available in the market to give our consumers a complete refreshing experience.” He said.
For his part, Nitin Menon Sayona Drinks Limited Group General Manager spoke about the consumer journey and pricing of the new product.

Mr. Menon said, the move for re-launching Twist comes as a result of working to reshape the company’s growth strategy in line with changing consumer tastes and buying habits.

“Our new exciting Twist drink comes in a distinctive 300ml & 400ml PET bottles. The product will retail at the price of 500/= and will be available across Tanzania,” he added.

He also used the opportunity to officially announce to the Public about the partnership with Tanzania’s bongo flava star Rajabu Abdul Kahali a.k.a Harmonize as Sayona Drinks official brand ambassador who was present during the launch.

“We are delighted to have Harmonize on board as our brand ambassador. He is an iconic cool (Jipoze) figure, a fresh face to young Tanzanians, hardworking, supports locals and aspires to take the Tanzanian music industry to greater heights. This is something that completely suits our mission and vision of becoming a giant soft drink company in Africa,” Mr. Menon said.

“We are confident that this collaboration will help to position Sayona drinks among the top brands in the industry. Harmonize will help us to engage our target audience in Tanzania and working with him as a brand ambassador is just one of the many exciting upcoming projects that our company will have with him.

For his part, Harmonize remarked that he was honoured to work with Sayona Drinks Limited and that it was the beginning of a fantastic collaboration with the group.

Speaking about the newly re-launched drink, Harmonize said “Twist is a cool drink with great flavours. I have consumed it several times and been a part of re-designing the brand, I’m confident that Tanzanians will love it and the drink will become popular beyond our borders. I’m also very glad to be associated with the Sayona Group who take pride in the quality of their products.”
Share:

Thursday, January 9, 2020

Wateja watano wa NBC washinda Yamaha, Ibuka Kidedea na NBC Malengo

Meneja wa Kampeni ya Ibuka Kidedea na NBC Malengo, Mtenya Cheya (kushoto), akizungumza na mmoja washindi aliyeshinda zawadi ya bodaboda katika droo ya tatu ya kampeni hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kushoto kwake ni Meneja wa Bidhaa za Kuwekeza wa NBC, Dorothea Mabonye, Meneja Chapa na Mawasiliano wa benki hiyo, David Raymond na Wakaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Elibariki Sengasenga na Abdallah Hemedi.
Meneja Chapa na Mawasiliano wa Benki ya NBC, David Raymond (wa tatu kushoto), akizungumza waandishi wa habari katika droo ya tatu ya kampeni ya Ibuka Kidedea na NBC Malengo jijini Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni; Meneja wa kampeni hiyo, Mtenya Cheya, Meneja wa Bidhaa za Kuwekeza wa NBC, Dorothea Mabonye, na mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Elibariki Sengasenga.
Maofisa wa NBC na kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, wakichezesha droo ya tatu ya kqampeni ya Ibuka Kidedea na NBC Malengo ambapo wateja watano walijishindia pikipiki mpya aina ya Yamaha.
Meneja wa Kampeni ya Ibuka Kidedea na NBC Malengo, Mtenya Cheya  (kushoto), akizungumza na mmoja washindi aliyeshinda zawadi ya bodaboda, huku Meneja Bidhaa za Kuwekeza, Dorothea Mabonye (kushoto kwake) akishangilia katika droo ya tatu ya kampeni hiyo jijini Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto kwa Dorothea ni; Meneja Chapa na Mawasiliano wa benki hiyo, David Raymond, Wakaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Elibariki Sengasenga na Abdallah Hemedi pamoja na waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imewahamasisha watanzania kutumia akaunti ya malengo ya benki hiyo kama suluhisho ya changamoto mbalimbali za kifedha hivyo kuwawezesha kutimiza malengo ya ndoto zao.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo kwenye droo ya tatu ya kampeni ya Ibuka kidedea na NBC Malengo, Meneja Chapa na Mawasiliano wa benki hiyo, David Raymond alisema kwamba wateja wa benki hiyo waendelee kutumia benki hiyo ili kutatua changamoto zao za kila siku.

“Huu ni mwanzo wa mwaka na watanzania wengi wanakabiliwa na majukumu kadhaa kama vile ada za shule, kodi za nyumba na bima za gari na nyumba, ni muhimu kwao kuendelea kuwa karibu na benki hii na kwa wale ambao bado hawajafungua akaunti ya malengo ni vyema wakufungua ili waweze kunufaika na zawadi,” alisema Raymond.

Meneja huyo wa Chapa na Mawasiliano alisema kwamba droo hiyo ni ya tatu ambayo ilianza mwezi wa Oktoba mwaka jana na washindi kadhaa wa bodaboda na safari za kutalii mbuga za wanyama Serengeti na Visiwani shelisheli walikwenda na kurudi salama kwa usimamizi na ufadhili wa benki hiyo kupitia kampeni ya malengo akaunti.

Kwenye droo hiyo ya jana washindi watano waliibuka kidedea kwa kujishindia pikipiki aina ya Yamaha, washindi hao ni; Luka Haule Baraka wa Dodoma, Juma Halfani kutoka Songea, Rebeka Ndosh anayeishi Mwanza, Rosemary Kibodya wa Dar es Salaam na Restituta Mbuya wa Morogoro.



Kampeni ya Ibuka Kidedea na NBC Malengo itashuhudia washindi watatu wakiibuka kidedea na kujishindia zawadi ya pikipiki ya miguu mitatu aina ya Toyo katika droo kubwa inayotarajiwa kufanyika Mwezi Machi mwaka huu.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive