A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Thursday, February 4, 2021

MAENDELEO BENKI YAZINDUA KAMPENI YA UPENDO WOTE KWAKO

  
Meneja wa Huduma kwa wataja wa Maendeleo Benki, Syvia Chaula (katikati), akizungumza na wanahabari wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kampeni ya UPENDO WOTE KWAKO itakayoanza siku ya leo tarehe 04/02/2021 hadi tarehe 13/02/2021 ikihamasisha wateja wote wa Maendeleo Bank kutumia huduma ya MB Mobile (*150*50#) pamoja na huduma za mitandao ya simu kuweka fedha katika akaunti zao za Maendeleo Bank. Kutoka kushoto ni Mratibu wa Kampeni ya Upendo wote kwako wa Maendeleo Benki Eliupendo Mziray pamoja na Mkuu wa Idara ya Uendeshaji wa Teknohama wa Benki hiyo George Wandwalo.
Meneja wa Huduma kwa wataja wa Maendeleo Benki, Syvia Chaula (katikati), akionesha maandishi kuashiria uzinduzi rasmi i wa Kampeni ya UPENDO WOTE KWAKO itakayoanza siku ya leo tarehe 04/02/2021 hadi tarehe 13/02/2021 ikihamasisha wateja wote wa Maendeleo Bank kutumia huduma ya MB Mobile (*150*50#) pamoja na huduma za mitandao ya simu kuweka fedha katika akaunti zao za Maendeleo Bank. Kutoka kushoto ni Mratibu wa Kampeni ya Upendo wote kwako wa Maendeleo Benki Eliupendo Mziray pamoja na Mkuu wa Idara ya Uendeshaji wa Teknohama wa Benki hiyo George Wandwalo.
Mkuu wa Idara ya Uendeshaji wa Teknohama wa Maendeleo Benki George Wandwalo (katikati), akizungumza na wanahabari wakati wa hafla ya uzinduzi wa Kampeni ya UPENDO WOTE KWAKO itakayoanza siku ya leo tarehe 04/02/2021 hadi tarehe 13/02/2021 ikihamasisha wateja wote wa Maendeleo Bank kutumia huduma ya MB Mobile (*150*50#) pamoja na huduma za mitandao ya simu kuweka fedha katika akaunti zao za Maendeleo Bank. Kutoka kushoto ni Mratibu wa Kampeni ya Upendo wote kwako wa Maendeleo Benki Eliupendo Mziray pamoja Meneja wa Huduma kwa wataja wa Maendeleo Benki, Syvia Chaula.

Na Mwandishi Wetu | Dar es Salaam | Leo tarehe 04/02/2021 katika ukumbi wa Mikutano wa Maendeleo Bank iliyopo Posta jijini Dar es Salaam, Meneja wa huduma kwa Wateja wa Maendeleo Bank Sylvia Chaula, amezindua rasmi kampeni ya UPENDO WOTE KWAKO itakayoanza siku ya leo tarehe 04/02/2021 hadi tarehe 13/02/2021 ikihamasisha wateja wote wa Maendeleo Bank kutumia huduma ya MB Mobile (*150*50#) pamoja na huduma za mitandao ya simu kuweka fedha katika akaunti zao za Maendeleo Bank.

Sylvia Chaula ameeleza kuwa kilele cha kampeni ya UPENDO WOTE KWAKO kitakuwa ni siku ya wapendanao (Valentine’s day) yaani tarehe 14/02/2021 ambapo washindi watatu watakaoshinda watapata zawadi mbalimbali kama vile Laptop, Simu Janja, Saa pamoja na kupata chakula cha usiku na Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Bank Dr Ibrahim Mwangalaba pamoja na jopo la wafanyakazi wa Maendeleo Bank katika Hotel ya Holiday Inn iliyopo Posta.

Washindi wote watatu wapata nafasi adhimu ya kuwaalika wapendwa wao katika chakula cha usiku, yaani kila mshindi atakuja na +plus one wake katika siku hiyo ambapo pamoja na chakula cha usiku pia kutakuwa na tukio la washindi kupokea zawadi zao kutoka Maendeleo Bank.” Aliongeza Sylvia Chaula.

Unajua maneno matupu hayanogeshi shughuli, siku hiyo ya wapendanao sisi kama Maendeleo Bank tunapenda kutumia muda wetu kuwaonyesha wateja wetu kuwa tunawapenda, tunawajali na kuwathamii ndio mana tumechagua siku hiyo kuwaonyesha wateja wetu upendo tulio nao kwao kwa vitendo na sio maneno.” Aliongeza Mkuu wa Kitengo cha Uendeshaji wa Bank na Tehama Ndg. George Wandwalo.

Maendeleo Bank imeendelea kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha inatoa huduma na kuja na majawabu mbalimbali yanayoweza kuwakwamua watu kiuchumi na hivyo kutoka kwenye hali moja ya maisha na kwenda kwenye hatua nyingine.

Maendeleo Bank imekuwa ikifanya hivi kwa kuja na huduma mbalimbali kama vile Huduma za Mikopo kwa Wajasiriamali wadogo wadogo, Wafanyakazi, Taasisi, Vikundi, na huduma nyingine nyingi za kibenki.

Kwa mawasiliano zaidi;
Eliupendo Mziray,
Mratibu wa Kampeni ya Upendo Wote Kwako
Maendeleo Bank
0758698022
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive