A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Tuesday, April 26, 2022

ZAIDI YA WATOTO 62,155 KUNUFAIKA NA CHANJO YA POLIO IKUNGI

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Singida Jerry Muro akiongoza kikao cha kuratibu zoezi la Kitaifa la chanjo ya polio kilichofanyika mkoani Singida jana. Kushoto ni Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Winfrida Funto na kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ally Mwanga. 
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo akizungumza kwenye kikao hicho.
Katibu Tawala wa wilaya hiyo Winfrida Funto akizungumza kwenye kikao hicho.
Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Oliva Njoka akitoa taarifa kuhusu maandalizi ya chanjo hiyo.
Mwenyekiti wa Halmashauri yaWilaya hiyo Ally Mwanga akizungumza kwenye kikao hicho.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo Mika Likapakapa akichangia jambo kwenye kikao  hicho.
Mratibu wa Elimu ya Afya na Uhamasishaji Wilaya ya Ikungi Braison Shoo akizungumzia ugonjwa huo.
Kikao kikiendelea.
Wajumbe wakiwa kwenye kikao hicho.
Baadhi ya madiwani wa Halmashauri hiyo wakiwa kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea.


Na Dotto Mwaibale, Ikungi.


MKUU wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Jerry Muro ametoa onyo kwa mtu yeyote wilayani hapa kutokwamisha mchakato wa utoaji wa chanjo ya polio kitaifa utakaoanza Aprili 28 mwaka huu unaotarajiwa kuwafikia watoto 62,155 na atakayebainika akifanya hivyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.

Muro alitoa onyo hilo wakati akizungumza na maafisa mbalimbali, viongozi wa dini, wadau wa maendeleo na timu ya wataalamu watakaoratibu zoezi hilo wilayani hapa ambapo alihamasisha wananchi wote kujitokeza bila kukosa wakati zoezi hilo litakapoanza.

"Sisi hapa Ikungi tupo tayari mpaka sasa  tumepokea jumla ya chanjo 71,400 na tumesambaza dozi 70,000 katika vituo vya kutolea afya na kuwa watalifanya kwenye vijiji vyote 101 na zaidi ya vitongoji 500" alisema Muro.

Alisema tayari wamewapanga wataalamu kwenye vituo 140 na watafika kwenye maeneo yote na kila mtoto aliopo kwenye wilaya hiyo watahakikisha anapata chanjo hiyo.

Muro alisema kwamba miundombinu yote pamoja na timu ya wataalamu kwa ajili ya kuwezesha ufanikishaji wa zoezi hilo yamekamilika kwa asilimia 100.

Aidha Muro alitoa mwito kwa wazazi wilayani humo kuacha tabia ya kuwapeleka watoto wao kwa waganga wa kienyeji kwani hawana uwezo wa kutoa chanjo ya polio badala yake wawapeleke kwenye vituo vya afya wakiwapeleka huko wanaweza kupigwa na ugonjwa  huo na hata kupata kifo.

Muro aliwaomba wazazi hao kuanzia Aprili 28 hadi Mei Mosi kuwa ni kipindi cha mzazi kumpeleka mtoto wake kituo cha afya na yale maeneo yaliopo  pembezoni kabisa mwa wilaya hiyo watayafikia kupitia kampeni ya nyumba kwa nyumba.
Muro alitumia nafasi hiyo kupiga marufuku tabia ya wazazi ambao kila wakipewa elimu na kuambiwa umuhimu wa kuwapeleka watoto wao vituo vya afya kwa ajili ya kupewa chanjo wamekuwa mstari wa mbele kukahidi kwa sababu ya imani na mila potofu hivyo kuanzia jana mzazi yeyote watakaye mbaini anakendwa kinyume na maagizo ya kitaifa ya zoezi hilo  atakamatwa na kuchuliwa hatua kali za kisheria na kuwa mfano kwa wengine wote katika wilaya hiyo.
"Tumepata taarifa kuwa kuna watu wamejipanga kukwamisha zoezi ili sasa mimi nawaambia kuwa kabla ya kuanza kukwama sisi watakwama wao na waomba watu wote wenye imani potofu dhidi ya chanjo hii watuache kwanza tufanye kazi nipo hapa kwa ajili ya kuwatoa mashaka wananchi wote wa wilaya ya Ikungi kuwa chanjo hizi ni salama zimedhibitishwa na wataalamu wa afya wa kimataifa na hapa nchini" alisema Muro.
Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ikungi,  Oliva Njoka alisema wamepokea maagizo kutoka wizarani kuwa kunakampeni ya kitaifa ya chanjo hiyo kwa nchi nzima ambapo watachanjwa watoto walio na umri chini ya miaka mitano na kuwa tayari wamekwisha anza maandalizi kwa kupata mafunzo ngazi ya halmashauri kwa timu ya uendeshaji na pia watatoa mafunzo kwa wale wahudumu watakao kuwa wakichanja.
Mratibu wa Elimu ya Afya na Uhamasishaji Wilaya ya Ikungi Braison Shoo alisema hivi sasa wapo kwenye kampeni ambayo wanatarajia kuianza Aprili 28 hadi Mei Mosi ya chanjo ya matone kwa watoto waliochini ya miaka mitano ambapo aliwaomba wananchi wote wa wilaya hiyo kujitokeza kwa wingi kupeleka watoto wao kupata chanjo.
Alisema lengo la chanjo hiyo ni kuongeza kinga katika jamii baada ya kutokea mlipuko wa ugonjwa huo nchi jirani ya Malawi hivyo aliendelea kuwasihi wananchi kujitokeza kwa wingi wakati wa zoezi la  chanjo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Ally Mwanga na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo,  Mika Likapakapa walisema watakwenda kuwahimiza madiwani na viongozi wa chama na serikali ngazi za vijiji na kata kwa ajili ya kuhamasisha zoezi hilo ili kuwafikia wananchi wengi zaidi.


Share:

Sunday, April 24, 2022

TANZANIA COMMERCIAL BANK SPONSORS FOR FREE HEALTH TESTING DAR ES SALAM


Tanzania Commercial Bank Bank Manager Edward Mwoleka (center), undergoing a blood test by Alliance Insurance Specialist Ravi Kumar, while Tanzania Commercial Bank teamed up with Alliance insurance to provide free diagnostic tests to the residents of Mbagala and its suburbs for free. Head of Alliance Insurance Group, KVA Krishnan. The ceremony took place today at the Tanzania Commercial Bank branch in Mbagala.

 


Tanzania Commercial Bank Bank Manager Edward Mwoleka and Alliance Insurance Group CEO KVA Krishnan watching one of Dar es Salaam's residents, Joseph John, receive a blood pressure test from Alliance Insurance Group Specialist Ravi Kumar, while Tanzania Commercial Bank teamed up with Alliance insurance to provide free diagnostic tests to the residents of Mbagala and its suburbs free of charge.

 


Some of the citizens who showed up at the TCB Mbagala branch in the provision of various diagnostic tests conducted by Alliance Insurance incorporation to various residents of Mbagala.

 


Tanzania Commercial Bank Bank Manager Edward Mwoleka, CEO of Alliance Insurance Group, KVA Krishnan and (name not found) greet each other at a special screening ceremony conducted by Alliance Insurance incorporation for various residents of Mbagala.

 


.Mbagala resident receiving a blood pressure check from Alliance Insurance Group Specialist Ravi Kumar, while Tanzania Commercial Bank teamed up with Alliance insurance to provide free diagnostic tests to residents of Mbagala and its suburbs free of charge.

 


Tanzania Commercial Bank Mbagala Branch Manager Edward Mwoleka witnessing one of the Dar es Salaam residents receiving a sugar test from Laboratory Laboratory Specialist Husna Hassan as Tanzania Commercial Bank teamed up with Alliance insurance to provide diagnostic tests for Mbagala residents and its free suburbs



Hundreds of people today have come forward to test their health for free at Tanzania Commercial Bank Mbagala branch located in Temeke Municipal Council as part of Tanzania Commercial Bank as well as Alliance Insurance Corporation to care for their customers and the general public.


Speaking at the event, Tanzania Commercial Bank Mbagala Branch Manager Edward Mwoleka said: "Every Tanzanian would like to know his health so Tanzania Commercial Bank has decided to support the efforts of the sixth phase Government under President Mama Samia Suluhu Hassan especially in the health by providing free testing services at no cost to the people of mbagala.and its environs ”.


"Tanzania Commercial Bank has every reason to care for Tanzanians and give them what they want which is why today we have joined our Alliance Insurance Corporation colleagues in providing free diagnostic services for various diseases".


Mwoleka has urged Tanzanians and residents of Mbagala to join TCB Bank as it has been providing quality and friendly services to every Tanzanian as well as caring for the community.


"We have loans ranging from small, medium and large business so I urge our customers to come forward and get services at our beloved bank."


"We also have retirement loans so he urged retirees to come forward and join these opportunities. The Bank also offers a wide range of soft and friendly loans ”.


For his part, Alliance Insurance spokesman Justin Erick thanked Tanzania Commercial Bank for trusting them and working together to ensure they provide better services to the people.


He added that all insurance services are available in all branches of Tanzania Commercial Bank so he urged the people of Mbagala to be proud of the existence of Alliance Insurance as it is the first company with quality in Tanzania in the provision of services.

  

Share:

Saturday, April 23, 2022

Absa Bank pledges to maintain quality services for sustainable growth

Absa Bank Tanzania Head of Retail Banking, Ndabu Lilian Swere speaking to the media about the iftar meal hosted by Absa to its Zanzibar customers and stakeholders in the Isle yesterday.
Absa Bank Tanzania Head of Business Banking, Melvin Saprapasen (right), serves an Iftar meal to one of the bank’s Zanzibar customers at an occasion of breaking the fast hosted by Absa to its customers and stakeholders in the Isles yesterday.
Absa Bank Tanzania Zanzibar Branch Manager, Rabia Abood (left), serves an Iftar meal to one of the bank’s customers, Nuru Mohamed Ali at an occasion of breaking the fast hosted by Absa to its customers and stakeholders in the Isles yesterday.
Absa Bank Tanzania Citizenship Manager, Hellen Siria (left), serves an iftar meal to one of the bank’s Zanzibar customers, at the fast-breaking event hosted by Absa to its customers and stakeholders in the Isles yesterday.
Absa Bank Tanzania Zanzibar Branch Manager, Rabia Abood, receives some of the invited guests to the Iftar meal hosted by the bank to its customers and stakeholders in the Isles yesterday.
Sheikh Khalid Ali Mfaume (second), represented Zanzibar Chief Mufti at the Iftar meal hosted by Absa Bank, chats with the Absa Tanzania Head of Business Banking, Melvin Saprapasen (right), after the function in the Isles yesterday. Looking on from left are Sheikh Salum Maridhia from Zanzibar Chief Mufti Office and Absa Tanzania Director for Corporate and Investment Banking, Hugo Chilufya.

By Our Reporter

Absa Bank Tanzania has pledged to maintain the quality of services to its customers to ensure it sustainable growth, it has been revealed in Zanzibar at the weekend.

Speaking during the Iftar dinner hosted for the banks customers to break the fast during the ongoing holy month of Ramadhan, Absa's Head of Business Banking, Melvin Saprapasen said: “we are confident about the future as we continue to innovate and come up with new products and solutions that are more digitalised that make it easier for our clients to access and enjoy our services.

He pointed out the year 2021 had been a very good one from the financial performance perspective as the Bank was able to recover from a reported loss position of TZS 532 million in 2020 to register a Tsh 9.4 billion profit after tax (PAT) in 2021.

During the year the bank also launched an SME lending product and improved its SME digital transactional banking channel as part of product and customer segments expansion and digital offering improvements,” noted Saprapasen.

Public sector support participation improved significantly in 2021 as the Bank role to contribute more positively to the socio-economic development of Tanzania continues to gather more pace, 

The bank’s Head of Retail Banking, Ndabu Lilian Swere, commenting on the upward trend indicators, said: “during the year 2021, the bank launched a number of innovative product diversifications, including launching a retail mobile lending product in partnership with Tigo Tanzania that has reached thousands of customers and assisted them to access financial services more conveniently and improve their lives and wellbeing.

Ms Ndabu noted that the bank has a well-established tradition of hosting Iftar dinners each year as part of its policy to shove back to reciprocate customer loyalty, adding that the bank focused on providing services to small, medium and large customers, including working with government and local and international agencies.

Sheikh Khalid Ali Mfaume, representing the chief Mufti of Zanzibar in the event, commended Absa for the gesture, alluding to one of the tales of Prophet Mohammad that "he who feeds a fasting believer is repaid the equivalent of all the blessings of those hosted.

The bank continues to have a strong capital position and operates well above regulatory and internal capital requirements. The bank’s digital capabilities continued to evolve and improve, attracting more customers and increasing usage from existing customers.

In 2021, Absa Bank Tanzania won several international and local Excellence Awards, including the Best Banking Cards Tanzania Award (by Global Brands Magazine), The Most Innovative Retail Bank, Tanzania Award (by Global Business Outlook) and Best Financial Institution in using ICT 2021 by Tanzania Commission of ICT.
Share:

Friday, April 22, 2022

WANANCHI IKUNGI WAHIMIZWA KUTUNZA CHAKULA ILI KUJIKIGA NA BAA LA NJAA

 Mwenyekiti  wa  Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ikungi Mika Likapakapa akiwahutubia Wananchi wa Kijiji cha Mwisi Kata ya Lighwa katika mkutano wa hadhara wa kuzungumzia maendeleo na kupokea kero za wananchi ili zifanyiwe kazi ulioandaliwa na Diwani wa Kata hiyo Gabriel Mukhandi na kuhudhuriwa na umati wa watu uliofanyika jana mkoani Singida.
Katibu wa CCM Wilaya ya Ikungi, Stamili Dendego akizungumza kwenye mkutano huo.
Diwani wa Kata ya Lighwa Gabriel Mukhandi akijibu maswali ya wananchi katika mkutano huo.
Katibu Mwenezi wa CCM  Wilaya ya IKungi, Pius Sanka akizungumzia Wana CCM wa kijijiji hicho wenye sifa kujitokeza kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.
Share:

Thursday, April 21, 2022

AKIBA COMMERCIAL BANK YAFUTURISHA WATEJA WAKE DAR ES SALAM

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Akiba Commercial Bank  Plc Silvest Arumas akizungumza wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo ikiwa ni sehemu ya jitihada za benki hiyo katika kuwajali wateja wake 

Baadhi ya wageni waalikwa wakifuturu katika hafla iliyoandaliwa na Akiba Commercial Bank ikiwa ni sehemu ya jitihada za benki hiyo katika kuwajali na kuwa karibu  na wateja wao.


Wateja na wageni waalikwa wa Akiba Commercial Bank wakichukua mlo wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na benki hiyo ikiwa ni sehemu ya jitihada za benki hiyo katika kuwajali wateja wake

Akiba Commercial Bank tunatambua nakuheshimu imani za wateja na wadau wetu
 Akizungumza katika halfla ya futari iliyoandaliwa na ACB Mkurugenzi Mtendaji wa Akiba Commercial Bank  Plc Bw. Silvest Arumas  alisema benki hiyo imeweka mipango mikakati kwaajili ya wateja wake hasa katika kipindi hiki cha Ramadhan

Tunaupa umuhimu wa kipekee sana mwezi mtukufu wa Ramadhan sio tu kwa wateja na wadau bali ni kwa waislamu wote kwani kama benki tunadhamini nakujali kila dini hivyo hivyo tumejikita kikamilifu katika mwezi huu wa Ramadhan kwaajili ya kuwashika mkono ndugu zetu waislam.

Akiba Commercial Bank, umekuwa ni utaratibu wetu kama benki yenye kujali na kutambua umuhimu wa mwezi huu mtukufu wa Ramadhan tumekuwa tukiwaruhusu wafanyakazi kutoka kazini mapema kwaajili ya ibada na matayarisho ya futari.

Pia Akiba Commercial Bank, umekuwa pia ni utaratibu wetu kufanya hafla yakuandaa futari kwa wateja wetu kila mwaka kwaajili ya kuwaunga mkono ndugu zetu waislamu katika funga yao pia kudumisha mahusiano kati ya wateja na benki yao pendwa.
Share:

Wednesday, April 20, 2022

BENKI YA ABC YATOA VIFAA VYENYE THAMANI YA ZAIDI YA MILIONI 2 KUSAIDIA UJENZI WA CHOO CHA WAALIMU SHULE YA MSINGI MTAWALA MANISPAA YA MOROGORO.

 


Meneja BANC ABC-Kanda ya Morogoro , Raphael Kalinga,(katikati), akikabidhi vifaa vya ujenzi wa Choo kwa Afisa Elimu Msingi Manispaa ya Morogoro, Chausiku masegenya (wapili kutoka kulia), kulia Diwani wa Viti Maalum Mhe. Hadija Kibati.

Meneja BANC ABC-Kanda ya Morogoro , Raphael Kalinga, akimkabidhi taarifa ya manunuzi ya vifaa vya ujenzi , Afisa Elimu Msingi Manispaa ya Morogoro, Chausiku masegenya.

Afisa Elimu Msingi Manispaa ya Morogoro, Chausiku masegenya.akizungumza katika hafla hiyo.

Meneja BANC ABC-Kanda ya Morogoro , Raphael Kalinga akizungumza katika hafla hiyo.

Diwani wa Viti Maalum Mhe. Hadija Kibati akisalimiana na waalimu waliojitokeza katika hafla hiyo.

Waalimu wa shule ya Msingi Mtawala. 

BENKI ya ABC Kanda ya  Morogoro, imekabidhi vitu vyenye thamani ya  zaidi ya milioni 2 katika kusaidia ujenzi wa Choo cha Waalimu katika Shule ya Msingi Mtawalaa Manispaa ya Morogoro ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali kusaidia kuondoa changamoto zilizopo kwenye sekta ya elimu hususani katika upande wa vyoo.

Hafla hiyo fupi ya kukabidhi vifaa hivyo, imefanyika leo Aprili 20/2022 katika shule hiyo huku tukishuhudia Afisa Elimu Msingi Manispaa ya Morogoro , Chausiku masegenya ,akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi mara baada ya kupokea vifaa hivyo, Masegenya, ameishukuru Benki ya ABC  huku akibainisha kuwa msaada huo utagusa maisha ya Waalimu  wengi kwa miaka mingi ijayo.

“Wadau wetu muhimu na washirika kama Benki ya ABC ndio nguzo muhimu kwa mafanikio yetu. Tunashukuru kwa msaada huu ambao utasaidia katika kuweka mazingira rafiki kwa waalimu ya kupata huduma ya choo , lakini pia kuwaondolea adha ya kutoka nje kwa ajili ya kufuata huduma ya choo" Amesema Masegenya.

Mwisho, Masegenya, ametoa wito kwa taasisi zingine za kifedha na wadau wanaopenda kuunga mkono juhudi za serikali za kuboresha mazingira ya vyoo pamoja na mazingira ya kujifunzia katika shule za umma zilizopo Manispaa ya Morogoro  kujitokeza kwa wingi katika jitihada hizo.

Naye Diwani wa Viti Maalum anayetokana na Kata ya Mwembesongo, Mhe. Hadija Kibati, ameishukuru Benki ya ABC Kwa kuwaunga mkono kwenye sekta ya elimu kwa kuwapa vifaa hivyo  ambayo yatasaidia kuondosha changamoto ya choo cha walimu shuleni hapo.

Kwa upande wa Meneja BANC ABC-Kanda ya Morogoro , Raphael Kalinga, akizungumza wakati wa halfa ya makabidhiano hayo, amesema kwamba  utoaji wa misaada kwa jamii  ni sehemu ya dhamira endelevu ya benki hiyo katika kusaidia sekta za elimu na kuona benki hiyo inachukulia kwa uzito sana suala la uwekezaji kwenye sekta ya elimu.

Kalinga, amesema wametoa msaada huo ili kuunga mkono Serikali na  juhudi za wananchi na kurudisha kwao ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa na hamasa ya kutenegeneza miundombinu ya elimu kwa manufaa ya sasa na kizazi cha baadae.

“Benki yetu inajivunia kuona Taifa linapiga hatua kubwa kwenye sekta ya elimu ambapo kupitia sera ya serikali elimu bure imeongeza idadi ya wanafunzi lakini pia ufaulu ambao maendeleo yake yanaakiisi hadi kiwango chetu cha uchumi ambapo mwaka jana nchi iliingia kwenye uchumi wa kati” Amesema Kalinga.

“Tumejitolea kuhudumia watu, biashara na jamii kwa ujumla. Benki yetu ya ABC, tumeguswa na changamoto ambayo iliwasilishwa kwetu , dhamira yetu kwa jamii ni kuona ni kuona tunaunga mkono na  kusaidia juhudi za kielimu na ustawi wa wanafunzi wetu na shule kote nchini na sio kwa Manispaa hii ya Morogoro pekee,  hivyo ni muhimu zaidi tukiweka jitihada katika kuboresha mazingira ya vyoo shuleni ili sasa Waalimu waweze kuwa na mahala rafiki kwa kutumia na kuacha kutoka eneo lao kwenda mbali  na shule zao,  ABC tutaendelea kushirikiana na Serikali kwa kadri tunavyoweza kuguswa na changamoto katika jamii ” Ameongeza Kalinga.

Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Mtawala, Mwl. Godfrey Binagwa , ameishukuru Benki ya ABC kwa msaada huo ambao wameutoa ambao utasaidia kuondoa changamoto walizokuwa wakikabiliana nazo za uhaba wa choo cha walimu.

Vifaa hivyo vya ujenzi ambayo walikabidhi benki hiyo ni Mifuko 50 ya saruji, mchanga Lori 1, Kokoto Lori 1, Mawe Lori 1, Milango 2 ya mbao, Fremu 2 za milango, Tofali za block 400 pamoja na Mabati 70.

Share:

Wednesday, April 13, 2022

TANZANIA COMMERCIAL BANK YASHIRIKIANA NA TRC KUZINDUA UJENZI WA RELI TABORA

Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Commercial Bank, Nd Sabasaba Moshingi  akiweka udongo kwenye jiwe la msingi wakati wa hafla ya uzinduzi wa ujenzi wa reli ya kisasa kipande cha nne (SGR) kinachotoka Tabora hadi Makutupora, Mkoani Dodoma iliyofanyika Cheyo B, Mkoani Tabora leo ambapo katika uzinduzi huo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Makame Mbalawa akimuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzanian Mh Samia Suluhu.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Makame Mbalawa  akimsikiliza Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Commercial Bank, Nd Sabasaba Moshingi  alipotembelea banda laBenkihiyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa ujenzi wa reli ya kisasa kipande cha nne (SGR) kinachotoka Tabora hadi Makutupora, Mkoani Dodoma iliyofanyika Cheyo B, Mkoani Tabora.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Makame Mbalawa  akisalimiana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Commercial Bank, Nd Sabasaba Moshingi (kulia), wakati wa hafla ya uzinduzi wa ujenzi wa reli ya kisasa kipande cha nne (SGR) kinachotoka Tabora hadi Makutupora, Mkoani Dodoma iliyofanyika Cheyo B, Mkoani Tabora
Afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Commercial Bank, Nd Sabasaba Moshingi akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa ujenzi wa reli ya kisasa kipande cha nne (SGR) kinachotoka Tabora hadi Makutupora, Mkoani Dodoma iliyofanyika Cheyo B, Mkoani Tabora.

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Makame Mbalawa akiwa katikapicha ya pamojana wakuu wa idara kutoka taasisi mbalimbali


Tanzania Commercial Bank TCB) imesema itaendelea kuwa mdau mkubwa wa maendeleo  ili kuboresha uchumi wa Tanzania.


TCB imeshirikia kikamilifu katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi kuashiria uzinduzi wa ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kipande cha kutoka Tabora mpaka Makutupora Mkoani Dodoma.

Hayo yamesemwa na Afisa  Mtendaji Mkuu wa Tanzania Commercial Bank Sabasaba Moshingi  wakati wa uzinduzi wa mradi wa uwekaji wa jiwe la msingi wa ujenzi wa reli ya Kisasa (SGR) awamu ya tatu leo Mkoani Tabora

 Moshingi amesema, Tanzania Commercial Bank  ni benki kubwa nchini  na  wamejitoa na wameshiriki kwa hatua kubwa katika kuhakikisha shirika la Reli Tanzania (TRC) linafanikisha mradi wa SGR Lot 4 kwa mafanikio makubwa.

“Tanzania commercial Bank ni wadau wakubwa wa maendeleo hapa nchini na kuchangia ujenzi wa Taifa, TRC ni wenzetu hivyo mradi huu wa SGR utaleta mafanikio kwa mkoa wa Tabora,”amesema

“Kufanikiwa kwa mradi huu kutarahisha usafiri wa kutoka Tabora hadi Dar es Salaam kwa masaa sita, na treni ya mizigo kwa masaa kumi pia kutafungua fursa za kiuchumi kwa mikoa ya Tabora, Dodoma, Singida , Shinyanga hadi Mwanza,”amesema

Moshingi amesema, wananchi wa Tabora kwa sasa wataanza kukua kiuchumi, kwa kusafirisha mazao yao kwenda Dar es Salaam ambapo ndio soko kuu la biashara na usafiri utakuwani ni wa uhakika zaidi.

Amewahimiza wakazi wa Tabora kujipatia huduma Bora zinazopatika Tanzania Commercial Bank ili waweze kwenda na kazi ya Uchumi kupitia mradi huo "amesema

Moshingi ameeleza kuwa kwa Sasa Tanzania Commercial Bank ina matawi kila pembe ya Tanzania hivyo imejipanga vema kutoa huduma kwa watanzania pamoja na wageni kutoka nje
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive