A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Tuesday, February 25, 2020

NBC yadhamini Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezeji katika Sekta ya Madini

Wakala wa Mauzo katika Kitengo cha Hazina na Masoko ya Fedha za Kigeni wa Benki ya NBC, Emmanuel Charles Gasirabo akihojiwa na vyombo vya habari wakati wa mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini uliomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. NBC ilidhamini mkutano huo.
Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa (kushoto), akitembelea mabanda ya maonyesho ya wadau wa sekta ya madini wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini uliomalizika juzi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. NBC ilidhamini mkutano huo. Anayemuongoza katikati ni Waziri wa Madini, Doto Biteko.
Kamishna wa Tume ya Madini, Prof. Abdulkarim Mruma, akishikana mikono na Meneja Mahusiano wa Taasisi za Umma wa Benki ya NBC, Azza Mnzava (wa pili kushoto), mara baada ya kamishna huyo kutembelea banda la NBC wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini uliomalizika juzi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. NBC ilidhamini mkutano huo. Wengine kushoto ni Wakala wa Mauzo katika Kitengo cha Hazina na Masoko ya Fedha za Kigeni, Emmanuel Gasirabo (kushoto), na Meneja Mahusiano Kitengo cha Wateja Rejerejea Maalumu, Daniel Kaila.
Meneja Masoko wa NBC, Alina Maria Kimaryo, akisalimiana Makamu wa Rais wa Kampuni ya Geita Gold Mine, Simon Shayo baada ya kutembelea banda la NBC wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini uliomalizika juzi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. NBC ilidhamini mkutano huo. Kulia ni Ofisa Mahusiano wa NBC kitengo cha Wateja Maalumu, Daniel Kaila.
Meneja Masoko wa Benki ya NBC, Alina Maria Kimaryo (kulia), akizungumza na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Geita Gold Mine, Simon Shayo baada ya kutembelea banda la NBC wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini uliomalizika juzi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. NBC ilidhamini mkutano. Wanaoangalia kutoka kushoto ni Meneja Mahusiano wa Taasisi za Umma wa NBC, Azza Mnzava na Wakala wa Mauzo katika Kitengo cha Hazina na Masoko ya Fedha za Kigeni, Emannuel Gasirabo.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive