A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Wednesday, February 21, 2018

Tanga Cement yaboresha sekta ya afya na elimu Singida

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Tanga Cement (TCPLC), Reinhardt Swart (kulia), akikabidhi msaada wa  mifuko 3500 ya Saruji yenye thamani ya shs 46,462,500 kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba  kusaidia uboreshaji wa sekta ya afya na elimu katika halmashauri ya Iramba mkoani Singida. Hafla hiyo ilifanyika eneo la kiwanda,  Pongwe, Tanga jana. Wengine ni maofisa wa kampuni hiyo pamoja na viongozi wa halmashauri.

Meneja Mahusiano na Mawasiliano ya Nje wa Kampuni ya Tanga Cement (TCPLC), Bi. Mtanga Noor (kushoto) akizungumza katika hafla ambayo Mkurugenzi Mtendaji wa TCPLC, Reinhardt Swart (kulia), alikabidhi msaada wa  mifuko 3500 ya saruji yenye thamani ya shs milioni 46,462,500 kwa Waziri wa Ndani, Mwigulu Nchemba (wa pili kulia), kusaidia ujenzi wa hosteli ya wasichana katika Shule 22 za kata  ya halmashauri ya Iramba mkoani singida. Makabidhiano yalifanyika eneo la kiwanda, Pongwe, Tanga jana. Wengine ni maofisa wa kampuni hiyo pamoja na viongozi wa halmashauri.

Meneja Rasilimali Watu wa Kampuni ya Tanga Cement (TCPLC), Diana Malambugi (kulia), akikabidhi msaada wa  mifuko 3500 ya Saruji yenye thamani ya shs 46,462,500 kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwiguru Nchemba  kusaidia uboreshaji wa sekta ya afya na elimu katika halmashauri ya Iramba mkoani Singida. Hafla hiyo ilifanyika enel la kiwanda, Pongwe, Tanga jana. Wengine kutoka kushoto ni Meneja Mahusiano na Mawasiliano ya Nje wa kampuni hiyo,  Bi. Mtanga Noor, Meneja Kiwanda Mhandisi Ben Leman a Mkurugenzi Mtendaji, Reinhardt Swart.
Meneja Kiwanda wa Kampuni ya Tanga Cement (TCPLC), Mhandisi  Ben Lema (kushoto), akifafanua jambo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba (katikati), alipokwenda kupokea msaada wa  mifuko 3500 ya saruji yenye thamani ya shs milioni 46,462,500 iliyokabidhiwa kwake na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Reinhardt Swart (kushoto kwa waziri), kusaidia ujenzi wa hosteli ya wasichana katika shule 22 za kata  ya  halmashauri ya Iramba mkoani singida.
Waziri wa Mambo ya Nchi, Mwigulu Nchemba (wa pili kulia), akizungumza baada ya kupokea msaada wa mifuko 3500 ya saruji yenta thamani ya shs 46,462,500  kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya  Tanga Cement (TCPLC) , Reinhardt Swart (kulia), iliyotolewa na kampuni hiyo kusaidia ujenzi wa hosteli ya wasichana katika shule 22 za kata  ya Halmashauri ya Iramba mkoani singida. Wengine ni maofisa wa kampuni hiyo pamoja na viongozi wa halmashauri.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive