A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Wednesday, August 2, 2017

ATE yaanza kundi la pili la Programu ya Mwanamke wa Wakati Ujao (Female Future)

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya TPB Plc, Sabasaba Moshingi (katikati) akisalimiana na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Sanjay Rughani wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya miezi tisa ya program ya Mwanamke wa Wakati Ujao ya kundi la pili yanayoendeshwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE)  kwa kushirikiana na Shirikisho la Vyama vya Waajiri Nchini Norway (NHO) jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo yana lengo la kuwaandaa wafanyakazi wanawake kushika nafasi za juu za uongozi katika makampuni na bodi za wakurugenzi.
Mwenyekiti wa Bodi ya ATE, Bi. Jayne Nyimbo (wa pili kushoto), Mkuu wa Idara ya Sheria ya ATE, Suzan Ndomba (kushoto) ma Mkurugenzi Mtendaji wa ATE, Dk. Aggrey Mlimuka (katikati), wakifurahi na Mkuu wa Kitengo cha mafunzo na maendeleo wa Acacia Mining, Janeth Lekashingo katika hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Bodi ya ATE, Bi. Jayne Nyimbo (kushoto), akisalimiana na Mkurugenzu wa Kampuni ya Statoil Tz,  Gunnar Mentzsen    huku Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Sanjay Rughani akiangalia  wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya  program ya Mwanamke wa Wakati Ujao yanayoendeshwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE)  kwa kushirikiana na Shirikisho la Vyama vya Waajiri Nchini Norway (NHO) jijini Dar es Salaam.
Mhadhiri wa Taasisi ya  Uongozi ya Afrika Mashariki na Kusini (ESAMI), Prof. Apollonia Kerenge (kulia), akizungumza na washiriki wa kundi la pili wa mafunzo ya miezi tisa ya program ya Mwanamke wa Wakati Ujao yanayoendeshwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE)  kwa kushirikiana na Shireikisho la Vyama vya Waajiri Nchini Norway (NHO) jijini Dar es Salaam jana. Mafunzo yana lengo la kuwaandaa wafanyakazi wanawake kushika nafasi za juu za uongozi katika makampuni na bodi za wakurugenzi.   
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TIB Corporate, Frank Mugeta (kulia), akizungumza na washiriki  wa mafunzo ya miezi tisa ya program ya Mwanamke wa Wakati Ujao yanayoendeshwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE)  kwa kushirikiana na Shireikisho la Vyama vya Waajiri Nchini Norway (NHO) jijini Dar es Salaam juzi. Mafunzo yana lengo la kuwaandaa wafanyakazi wanawake  kushika nafasi za juu za uongozi katika makampuni na bodi za wakurugenzi.   
Mratibu wa Program ya Mwanamke wa Wakati Ujao ya Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Lilian Machera akizungumza na washiriki hao kuhusu utaratibu wa mafunzo hayo yenye malengo ya kuwaandaa wafanyakazi wanawake kushika nafasi za juu za uongozi katika makampuni na bodi za wakurugenzi.   
Mmoja wa washiriki wa mafunzo ya program ya Wanawake wa Wakati Ujao, Bi. Anna Nyimbo akijitambulisha kabla ya kuanza kwa mafunzo hayo yatakayochukua kipindi cha miezi tisa.  

Washiriki wa kundi la pili la mafunzo ya program ya Mwanamke wa Wakati Ujao wakipiga picha ya kumbukumbu pamoja na baadhi ya viongozi wa ATE pamoja na wakurugenzi wa makampuni 16 yanayofadhili mafunzo hayo. Makampuni hayo ni; Acacia Mining, Alistair Equipment Services (T) Ltd, AngloGold Ashanti, Geita Gold Mine, Cartrack Tanzania Limited, EFC Microfinance Bank, Ubalozi wa Denmark, Global Health Program-Tanzania, HJFMRI, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),  Benki ya NMB Plc, Mfuko wa PPF , Songas Limited, Benki ya Standard Chartered, Statoil Tanzania AS, Benki ya TIB Corporate, Benki ya TPB Bank Plc na Under The Same Sun.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive