A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


  • CRDB Bank Share up 16PC in three weeks

    CRDB bank share price has made an abrupt U-turn after appreciating by 16 per cent in the last three weeks.

  • TIB slashes losses, bad loans up!

    TIB Development Bank has considerably reduced its net loss 17 times to 582m/- in this year quarter two (Q2) after cutting expenses.

  • MALINZI blesses TFF elections

    THE ousted Tanzania Football Federation (TFF) President Jamal Malinzi has expressed gratitude to the government, sponsors and football stakeholders in the country for their massive support.

  • Barrick, government talks next week

    BARRICK Gold will begin discussions with the government on the concentrate export ban and other issues next week

Thursday, April 4, 2024

KAMPUNI ya Gesi ya Oryx Tanzania imeahidi kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kulinda afya za watanzania.

Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani Meja Edward Gowele(wa tatu kushoto) akimkabadhi mtungi wa gesi ya Oryx Furaha Mawikia wakati wa hafla ya kukabidhi mitungi ya gesi na majiko yake 400 kwa wanawake wa vijiji vya Mwalusembe ,Kinene,Kitomondo na Kisele wilayani Mkuranga. Wengine pichani ni Balozi wa Heshima Shelisheli nchini Tanzania Maryvyonne Pool(watatu  kulia) Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Oryx Janeth Mutashobya (wa kwanza kulia), Katibu Tawala Wilaya ya Mkuranga Omary Mwanga.
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Meja Edward Gowele(kulia) pamoja na  Balozi wa Heshima wa Shelisheli nchini Tanzania Maryvyonne wakiangalia vyakula vya asili ya kitanzania ugali,wali na mboga ambazo vimepikwa kwa kutumia jiko la gesi ya Oryx wakati wa hafla ya kukabidhi mitungi ya gesi 400 yakiwa na
majiko yake kwa wanawake wa Kata ya Mwalusembe wilayani humo.
Baadhi ya wanawake wa Kata ya Mwalusembe wilayani Mkuranga mkoani Pwani wakiendelea kupika chakula kwa kutumia jiko la Oryx wakati wa hafla ya kukabidhi mitungi ya gesi ya Oryx kwa wanawake wa vijiji vya kata ya Mwalusembe wilayani Mkuranga.

Na Mwandishi Wetu, Mkuranga

Hayo yameelezwa na Meneja Usalama Afya na Mazingira wa Oryx Energies Tanzania, Janet Mutashobya, alipomwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo Benoite Araman wakati wa hafla ya kugawa mitungi 400 ya gesi na majiko yake kwa akinamama wa Kata ya Mwalusembe wilayani Mkuranga mkoani Pwani.

Ugawaji wa mitungi hiyo umefanyika kwa ushirikiano wa Balozi wa Heshima wa Shelisheli nchini Tanzania Maryvyonne Pool ambaye pia ni Mwanzilishi wa taasisi ya African Reflections Foundation ambayo imekuwa ikijihusisha na kusaidia jamii katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo

"Kupika kwa gesi ya Oryx ni kulinda mazingira kwa kuacha kukata miti. Pia ni kulinda afya ya wanawake kwa kuwaepusha kuvuta moshi na mvuke unaoathiri mapafu na afya yao unaotokana na kuni na mkaa," amesema.

Ameongeza kupika kwa kutumia nishati safi kunafungua fursa kwa wanawake kutumia muda mwingi kujishughulisha na shughuli za uzalishaji wa kiuchumi.

"Kwa kuanawake wanatumia muda mchache kupika hivyo wanapata nafasi kufanya shughuli nyingine za maendeleo na kuepuka kugombana na wenza wao kwa kuchelewesha chakula. Kwa kutumia gesi ya Oryx, Watoto wanakua na muda mwingi zaidi kusoma na sio kwenda kutafuta kuni,"amesema Mutashobya.

Aidha amesema kwa  miaka mingi Oryx Gas imekuwa kampuni kiongozi katika kukuza matumizi ya Gesi nchini Tanzania na Kuanzia Julai  mwaka 2021 wamekuwa mstari wa mbele kutekeleza maelekezo ya Serikali waliyopokea toka kwa Rais Dk.Samia Suluhu Hassan ifikapo mwaka 2023 asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia.

Amesema kupitia mipango hiyo Oryx Gas inataka kutokomeza matumizi ya nishati chafu ya kuni na mkaa ambayo si tu mbaya kwa afya zetu bali pia ni hatari kwa mazingira yao  na pia Oryx Gas inatekeleza juhudi za kueneza matumizi ya nishati safi kwa Watanzania wengi ipasavyo ambayo ni ndoto kubwa ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake Balozi Pool amesema  uamuzi wa kushirikiana na Oryx kutoa mitungi hiyo kwa wanawake wa vijiji vya kata vya Mwalusembe, unatokana na kutambua na kuunga mkono jitihada za Rais Samia za kuhamasisha nishati safi ya kupikia.

“Hii kwangu si mara ya kwanza kwani mwaka 2022 nilinunua mitungi ya gesi na kugawa kwa wanawake wa Mkuranga kwa sababu mimi ni balozi wa heshima hapa Mkuranga. Ndio maana nimekuwa nikishiriki katika miradi ya maendeleo ukiwemo wa kilimo cha kisasa cha umwagiliaji,” amefafanua.

Ameeleza taasisi yake imekuwa ikiwasidia wanawake na vijana kulima, huku akibainisha kuwa hatua hiyo ya kusaidia wanawake hao kupata nishati safi ya kupikia imetokana na kutambua mchango wa Rais Dk. Samia baada ya kuwa champion wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi.

"Kulifanyika mkutano wa mazingira wa kimataifa Dubai ambapo Rais Samia alichaguliwa kuwa champion wa kuhamasisha nishati safi ya kupikia , hivyo ni vema kumuunga mkono Rais Samia katika ajenda hiyo.

“Katika ule mkutano nilikaa meza moja na Rais (Dk.Samia) pamoja na Bilionea wa Marekani Bill Gate ambapo Rais Samia alichaguliwa kuwa champion wa Afrika katika kuhamasisha nishati safi, hivyo anastahili pongezi na nimeahidi kuunga mkono na kumsaidia kadri nitakavyoweza,”amesema Balozi Pool.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Rufiji ambaye pia anakaimu nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga, Meja Edward Giwele, amesema umefika wakati wa kumuunga mkono kwa vitendo Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Amesema kufanya hivyo kutasaidia kuokoa mazingira na kutanua fursa za kiuchumi hususan kwa wanawake wa wilaya hiyo nan a maeneo mengine nchini.

"Tumegawa mitungi ya gesi 400 kwa wanawake wa kijiji cha Kinene katika kata ya Mwalusembe ndani ya wilaya Mkuranga ikiwa sehemu ya mwendelezo wa jitihada za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha tunatumia nishati safi au nishati mbadala na kuachana na matumizi ya kuni na mkaa."

Amewapongeza Oryx na Balozi Pool Afrika Reflections Foundation kwa kushirikiana na kuhakikisha wanagwa mitungi hiyo kwa akinamama tena wa hali ya chini kabisa katika kijiji hiki cha Kinene.

Awali KatibuTawala Wilaya ya Mkuranga Omar Mwanga, amesema Wilaya  hiyo ni miongoni mwa wahanga wa uharibifu wa mazingira kwani misitu mingi ya asili imekatwa mkaa kwa matumizi mbalimbali ikiwemo kuwivisha chakula.

"Miti inakatwa kwa ajili ya kuchoma mkaa katika maeneo yetu, misitu ya vijiji ambayo imehifadhiwa na mingine ya asili imekuwa ikiathirika na wananchi kufanya shughuli za kijamii hasa zaidi ya hizi shughuli za ukataji mkaa, kwa hiyo na sisi tunaendelea kuhamasisha kama wanavyofanya Kampuni ya Gesi ya Oryx Tanzania.
Share:

MKANDALASI MKUU WA UJENZI WA RELI YA UMEME KAMPUNI YA YAPI MERKEZI YAWAKUMBUKA WATOTO MWEZI HUU WA RAMADHANI





Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
KAMPUNI ya Yapi Merkezi, ambayo ni Mkandarasi Mkuu wa Reli ya umeme (SGR), imetoa msaada kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha Mama Mwana kilichopo Vingunguti jijini Dar es Salaam ikiwa ni sehemu yao ya kujitolea kwa Jamii. Mchango huo umelenga kutoa mahitaji muhimu kwa watoto wanaoishi katika kituo hicho kwa wakati wa sikukuu zijazo za Eid El fitir.

Kampuni hio imetoa msaada wa bidhaa mbalimbali ikiwemo chakula, vifaa vya usafi, mafriji , nguo za Eid ikiwa ni sehemu moja ya kuwapa faraja watoto hao katika kipindi hiki cha sikukuu.

Bi Amisa Juma, Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano Yapi Merkezi, alitoa shukrani zake za dhati kwa kupata fursa ya kusaidia Kituo cha Watoto Yatima cha Mama Mwana. Alisema, "Yapi Merkezi ina nia ya dhati ya kuleta matokeo chanya katika jamii tunazofanyia kazi. Tunapokaribia msimu wa sikukuu ya Eid, ni jukumu na Furaha kwetu kutoa msaada kwa Kituo cha watoto yatima cha Mama Mwana na kuleta tabasamu kwenye nyuso za hawa watoto wanaostahili."

Bi Juma aliongeza zaidi, "Mchango wetu unaakisi tunu kuu za Yapi Merkezi nazo ni ukarimu, na uwajibikaji wa kijamii.

Tunatumai kupitia mchango huu, tunaweza kuwapa faraja na furaha watoto wa kituo cha Mama Mwana, huku tukiendelea kuwakumbusha kuwa wana haki ya kuthaminiwa na kutunzwa, pamoja na kuhimiza zaidi Makampuni mengine ya kiserikali na kibinafsi kuendelea kufariji Jamii hizi.

Hafla ya kukabidhi msaada huo, iliyoambatana na furaha na shukrani, ilihudhuriwa na wawakilishi kutoka Menejimenti na wafanyakazi wa kampuni ya Yapi Merkezi wakiongozwa na Bw. Levent Doruck, kama Afisa Mkuu wa Fedha wa kampuni iyo, ambaye aliwasilisha dhamira ya dhati ya kampuni hiyo ya kuendelea kusaidia juhudi zinazoendelea za kuboresha mazingira ya watoto yatima au wanaoishi katika hali ngumu.

Mlezi mkuu wa kituo cha Mama Mwana Bi Saada Omar, alitoa shukran zake za dhati na kupongeza kampuni ya Yapi Merkezi kwa moyo na ukarimu wao , huku akiendelea kusisitiza faida na umuhimu wa michango hiyo kwa ustawi wa Watoto hao.

Yapi Merkezi imeahidi kuendelea kukuza ushirikiano na kituo cha Watoto Yatima cha Mama Mwana, ikisisitiza dhamira yake ya uwajibikaji wa kampuni kwa jamii na mipango ya maendeleo ya jamii
Share:

Benki ya Absa kuendelea kuwezesha hadithi za watoto kielimu

Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Lilian Swere akizungumza katika hafla ambayo benki hiyo pia ilikabidhi msaada wa vifaa vya shule kwa watoto yatima wanaolelewa wa vituo vya Tuyata Orphanage Centre na Watoto Wetu Tanzania vilivyopo chini ya Taasisi ya Adonai El Roi Foundation jijini Dar es Salaam jana.

Na mwandishi wetu, Dar es Salaam.

Benki ya Absa Tanzania imesema itaendelea kuweka kipaumbele katika kufanikisha ndoto za kielimu za watoto wa kitanzania katika kuboresha huduma za kibenki zinazohusu watoto, hususan akaunti yake maalumu ya watoto ya Absa Child Savings Account.

Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla waliyowaandalia watoto wenye uhitaji kutoka katika vituo vya watoto yatima vilivyo chini ya Taasisi ya Adonai El Roi, Mkurugenzi wa Wateja Binafsi wa Benki ya Absa, Bi. Ndabu Lilian Swere alisema hayo yanaenda kupitia lengo kuu la Benki Absa ambalo ni kuiwezesha Afrika na Tanzania ya Kesho Pamoja hatua Moja baadae ya nyingine kiuchumi sambamba na ahadi mpya ya Chapa yake isemayo ‘Story Yako ni ya Thamani’.

Watoto wana ndoto nyingi katika maisha yao, wapo wanaotamani kuwa madaktari, wanasheria, viongozi wa makampuni, viongozi wa kisiasa, tunathamini Story za watoto wetu, Absa tupo hapa kuwasapoti ili waweze kikamilisha ndoto za story zao.

Absa inatoa Huduma za kibenki kwa makundi mbalimbali, ni kwa kutumia huduma hizi pia tunawezesha hadithi za wazazi ama walezi wa watoto hawa nao pia kuweza kikamilisha hadithi zao mbalimbali za kiuchumi.

Hii si mara ya kwanza kwa Absa kufanya shughuli za kujitolea kusaidia jamii, hivi karibuni tulisaidia watoto wanaozaliwa kabla ya siku zao, hawa pia tutaangalia ni namna gani nyingine bora zaidi ya kuwasaidia”, aliongeza Bi Ndabu.

Akizungumza kuhusu akaunti ya watoto ya benki hiyo, Mkuu wa Mkakati na Bidhaa za Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bwana Heristraton Genesis alisema akaunti hiyo haina makato ya mwezi na anaweza kupokea riba hata mara mbili endapo hatatoa pesa zaidi ya mara moja katika kipindi cha miezi mitatu.

katika kuonyesha Benki ya Absa imejipanga vizuri katika kuziwezesha ndoto za watoto, tunatoa riba mara mbili katika kile kiasi kilichokaa ndani ya miezi mitatu Ili kuwarejeshea watoto waweze kukamilisha story za ndoto zao za kielimu.

Ni rahisi kufungua akaunti hii, mahitaji ni kitambulisho cha taifa cha mzazi ama mlezi, cheti cha kuzaliwa cha mtoto ama utambulisho wowote kutoka shule anakosoma mtoto, na akaunti inaweza kuendeshwa kwa kutumia huduma zetu za kidigitali bila kuhitajika kufika katika matawi ya benki”, alisema Bwana Genesis.

Naye Mwanzilishi wa asasi ya Adonai El Roi inayolea vituo mbalimbali vya watoto nchini, Bi. Ngole Melaisho alisema lengo lao kubwa la shirika lao lisilo la kiserikali pamoja na mambo mengine ni kutokomeza umasikini katika vituo hivi.

Taasisi yetu Ina malengo ya kuwafuatilia watoto hawa kwa umakini waweze kuendeleza ndoto zao kwa kupitia kukuza vipaji vilivyo ndani yao.

Nipende kuhamasisha watanzania waendelee kusaidia vituo hivi na pia kuongeza upendo kwa watoto hawa waweze kukamilisha malengo yao”, aliongeza Bi. Ngole.
Mkuu wa Mikakati na Bidhaa za Wateja Binafsi wa Benki ya Absa, Bwana Heristraton Genesis akizungumza katika hafla ambayo benki hiyo pia ilikabidhi msaada wa vifaa vya shule kwa watoto yatima wanaolelewa wa vituo vya Tuyata Orphanage Centre na Watoto Wetu Tanzania vilivyopo chini ya Taasisi ya Adonai El Roi Foundation jijini Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi wa Benki ya Absa Tanzania, Bi. Ndabu Lilian Swere (wa pili kulia) akikabidhi begi lenye vifaa vya shule kwa mmoja wa watoto wanaolelewa katika Kituo cha Watoto Wetu Tanzania, Johnson Helman katika hafla iliyoandaliwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Mikakati na Bidhaa za Wateja Binafsi, Bwana Heristraton Genesis (kulia) na Meneja Kitengo cha Kadi wa benki hiyo, Elfrida Mruma wakishirikiana kutengeneza keki na watoto yatima wa vituo vya Tuyata Orphanage Centre na Watoto Wetu Tanzania vilivyopo chini ya Taasisi ya Adonai El Roi Foundation katika hafla ambayo benki hiyo pia ilikabidhi msaada wa vifaa vya shule kwa watoto hao jijini Dar es Salaam jana
Meneja Msaidizi wa Hoteli ya Johari Rotana, Ahmed Said (kulia) akikabidhi begi lenye vifaa vya shule kwa mmoja wa watoto wanaolelewa katika Kituo cha Watoto Wetu Tanzania, Abigael Maliki katika hafla iliyoandaliwa na Benki ya Absa kwa kushirikiana na hoteli hiyo kwa watoto wa vituo vya Watoto Wetu na Tuyata vilivyo chini ya Taasisi ya Adonai El ROI, jijini Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Kitengo cha Bima wa Benki ya Absa Tanzania, Sandeep Chavda (kushoto), Mkuu wa Mikakati na Bidhaa za Wateja Binafsi, Bwana Heristraton Genesis, Mkuu wa Kitengo cha Wateja Maalum, Thereza Majinge na Meneja Kitengo cha Kadi wa benki hiyo, Elfrida Mruma wakipiga picha ya pamoja na watoto wa watoto yatima wa vituo vya Tuyata Orphanage Centre na Watoto Wetu Tanzania vilivyopo chini ya Taasisi ya Adonai El Roi Foundation baada ya kukabidhi msaada wa vifaa vya shule katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
Share:

Friday, March 29, 2024

KAMPUNI YA MAFUTA YA PUMA TANZANIA WAYAKUMBUKA WATEJA WAKE

KAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha watanzania na wadau mbalimbali katika futari iliyoandaliwa na Kampuni hiyo huku ikitumia nafasi hiyo kuwaomba Watanzania kuendelea kutumia bidhaa zinazotoka Kampuni hiyo 
Hafla ya futari iliyoandaliwa na Kampuni hiyo ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wake Fatma Abdallah imefanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa wadau mbalimbali wakiwemo wakuu wa taasisi za umma na binafsi pamoja na wateja wa kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Mgeni rasmi katika Iftar hiyo alikuwa Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Walid aliyewakilishwa na Sheikh wa Wilaya ya Temeke ...

Akizungumza wakati wa Iftar hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni hiyo Dk Selemani Majige ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa ni vema kila Mtanzania kwa nafasi yake kuendelea kuliombea Taifa sambamba na kumuunga mkono Rais Dk.Samia Suluhu Hassan.
"Tunafahamu kwa sasa tunaendelea na Mfungo wa Ramadhan pamoja na Kwaresima hivyo wakati tukiendelea na Mfungo ni vema tukaliombea Taifa letu lakini wakati huo huo kudumisha Umoja,amani na mshikamano,"amesema Dk Majige.

Amesisitiza kuendelea kudumisha amani katika nchini Kunafanya uchumi Wetu kuendelea kuimarika  na biashara zetu ziendelee vizuri."Kulinda amani ni jambo kubwa kwani kama hakuna amani basi hata biashara haziwezi kufanyika vizuri.

"Hivyo kupitia mwezi mtukufu wa Ramadhan ni vema kuendelea kumuomba Mungu na kuendelea kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ili aendelee kutuongoza na kudumisha amani katika taifa letu."
Pia amewaomba Watanzania kuendelea kutumia mafuta  ya Puma Energy Tanzania pamoja na bidhaa zake zote huku akifafanua mafuta ya Kampuni hiyo yana ubora na viwango vya hali ya juu.

"Tunawaomba muendelee kutumia mafuta ya Puma  ili tuongeze faida na tukiongeza faida Serikali inapata gawio na inapotoa gawio zinapatikana fedha ambazo zinakwenda kuhudumia jamii katika maeneo mbalimbali,"
Kwa upande wake Sheikh wa Wilaya ya Temeke Sheikh Zailai Hassan Mkoyogole aliyemwakilishwa  Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Omar  aliyekuwa mgeni rasmi, amesema kipindi hiki cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan jambo kubwa ni kuzidisha wema kwa maana wanadamu ni wakosaji mbele za Mwenyezi Mungu.

"Binadamu anamkosea Mwenyezi Mungu kwa vitu vingi hivyo sasa ameleta Mwezi mtukufu wa Ramadhan ili kutubu kwa yale yote ambayo ameyafanya.Hivyo kinachotakiwa katika mwezi huu ni kufanya yale yaliyomema na kurejea  kwake,"
Pia amesema Mwenyezi Mungu anapenda kuombwa ,hivyo ametoa wito kwa watu wote kurejea kwa Muumba  na kuomba msamaha.

Awali Mkurugenzi Mkuu wa Puma Energy Tanzania Fatma Abdallah  amewashukuru wadau  kwakuitikia wito  katika futari hiyo huku akitumia nafasi hiyo kuwaomba Watanzania kuwaunga mkono kwa kununua bidhaa za mafuta ya Kampuni hiyo.

Aidha amesema  kama Puma Energy Tanzania wataendelea kuunga mkono juhudi za Serikali hasa katika utekelezaji matumizi ya  nishati safi ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa lengo la  kuendelea kutunza mazingira .

"Puma  Energy Tanzania tunatambua mwelekeo wa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na hasa kwenye suala la nishati safi hivyo tutaendelea kua mstari wa mbele kutoa elimu kwa lengo la kuhakikisha   mazingira yanalindwa na matumizi ya nishati  safi kwa watanzania yanakuwa kipaumbele."

Wakati huo huo Mkurugenzi Mkuu UDA- RT  Waziri Kindamba aliyeshiriki futari hiyo amewapongeza kwa kuandaa futari hiyo ni kuwaalika wateja wao ambao wanatumia bidhaa zao ikiwemo vilainishi na mafuta.
Share:

BancABC Tanzania yatoa msaada pamoja na kufuturisha kituo cha watoto yatima cha New Faraja

Mkuu wa Kitengo cha Idara ya Udhibiti BancABC Tanzania Saleh Geva (wapiliKushoto), akiwahudumia futari watoto wanaolelewa kwenye Kituo cha Watoto yatima cha New Faraja kilichopo Mburahati Jijini Dar es Salaam. BancABC Tanzania ambayo ni kampuni tanzu ya Atlas Mara ilitoa msaada wa vyakula mbalimbali pamoja na kuandaa futari kwa watoto waliopo kwenye kituo hicho kama ishara ya kuonyesha upendo kwenye kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadan.

Baadhi ya watoto wanaolelewa kwenye kituo cha watoto yatima cha New Faraja kilichopo Mburahati Jijini Dar es Salaam wakifuatilia hotuba pamoja na nasaha kutoka kwa viongozi wa BancABC Tanzania mara baada ya benki hiyo kutoa msaada wa vyakula mbali mbali pamoja na kuwaandalia futari watoto hao ikiwa ni ishara ya kuonyesha upendo kwenye kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadan.

Mkuu wa kitengo cha Udhibiti wa BancABC Tanzania (kushoto), akimkabidhi msaada wa vyakula mbali mbali Mkurugenzi wa Kituo cha Watoto yatima cha New Faraja kilichopo Mburahati Jijini Dar es Salaam.


Dar es Salaam Ijumaa 29 Marchi 2024 BancABC Tanzania, ambayo ni kampuni tanzu ya Atlas Mara imetoa msaada wa vyakula mbali mbali pamoja na kuandaa futari kwa watoto wanaolelewa kwenye kituo cha watoto yatima cha New Faraja kilicho Mburahati Jijini Dar es Salaam ikiwa ni ishara ya kuonyesha upendo kwenye kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadan.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam mara ya kukabidhi msaada huo, Mkuu wa Idara ya Udhibiti BancABC Tanzania Saleh Geva alisema benki hiyo imetoa msaada pamoja na kufuturisha kituo cha Watoto yatima cha New Faraja kama ishara ya kuonyesha upendo pamoja na kuwapa tabasamu na hasa kwenye kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadan. ‘Watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu wanahitaji kuonyesha upendo. Sisi BancABC Tanzania na hasa wafanyakazi tumefarajika sana kujumuika nao   pamoja na kupata wasaa wa kufuturu na watoto wanaolelewa kwenye kituo hiki. Kilikuwa ni kipindi faraja sana kwao lakini furaha kwetu kuona watoto hawa wakitabasamu. Lengo letu ilikuwa ni kufanikiwa kuona watoto hawa wajisikia kama sehemu ya Jamii ya Watanzania’, alisema Geva.

Geva aliongeza ‘Kuwafanya watoto hawa watabasamu na kufurai kunawapa matumaini yao ya maisha ya baadae. Kuja kwetu kufuturu na watoto hawa kumetuonyesha kwa nini BancABC Tanzania imekuwa ikijikita sana kwenye kusaidia Jamii ambayo inayotuzunguka. Tutaendelea na utamanduni huu wa kusaidia Jamii ambayo inaishi kwenye mazingira mangumu kwa sababu tunaamini ni moja Kati ya nguzo ya sisi kuendelea kukua kibiashara’,

‘Furaha yetu sisi BancABC Tanzania ni kuona tukibadilisha maisha ya Watanzania. Tunaamini kwenye Jamii yenye usawa na ndio sababu mwaka huu tuliamua kuja kufuturu na watoto hawa ambao wanaishi kwenye mazingira magumu ’, alisema Geva.

 ‘BancABC Tanzania, ikiwa ni taasisi ya kutoa huduma za kifedha imekuwa ikifanya kazi kubwa sana kuwafikia Watanzania na hasa wale ambao bado hawafikiwa na huduma za kibenki. Kwa sasa, BancABC Tanzania tunao mawakala zaidi ya 700 nchini kote’, alisema Geva huku akiongeza kuwa benki hiyo inayo akaunti maalum kwa ajili ya wajasiriamali wadogo na wa kati kwa ajili ya kutoa mikopo ya kuimarisha biashara zao’.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa kituo cha New Faraja Zamda Idrisa alisema kuwa wamefarijika kwa kuona taasisi binafsi kama BancABC Tanzania ikiunga mkono Jamii ambayo inaishi kwenye mazingira mangumu.

Aliongeza ‘Msaada wenu umekuja kwenye muda muafaka kwani watoto hawa wanahitaji kuonyesha upendo kama watoto wengine. Tunawashukuru kwa msaada wenu na tunawaombea kwa Mwenyezi Mungu azidi kuwafungulia riziki kwenye maisha yenu ya kila siku’.

‘Tunatoa rai kwa taasisi zingine pamoja na watu binafsi wazidi kutusaidia kwani watoto hawa wanahitaji kuvaa, kusoma, chakula pamoja na matibabu na kituo chetu hakina wadhamini bali tunatengemea misaada kutoka kwa wadau mbali mbali kama BancABC Tanzania walivyokuja hapa kutusaidia kwa siku ya leo.

Share:

Wednesday, March 27, 2024

BODABODA TANGA WAPATA MAFUNZO MAALUM YA UTOAJI WA HUDUMA YA KWANZA


Na Mwandishi Wetu,Tanga


MADEREVA bodaboda katika Jiji la Tanga wamepatiwa mafunzo ya huduma ya kwanza kwa lengo la kuwawezesha madereva hao kutoa msaada wa huduma ya kwanza inapotokea ajali

Mafunzo hayo ya huduma ya kwanza kwa madereva wa bodaboda inakwenda sambamba na elimu ya Usalama barabarani inayotolewa na Taasisi ya AMEND kwa kushirikiana na Ubalozi wa Uswisi ambao ndio wanaofadhili mradi wa utolewaji wa mafunzo hayo kwa madereva bodaboda.

Baadhi ya wadau ambao wanashirikishwa katika kutekeleza mradi huo wameeleza kwa kina kuhusu umuhimu wa mafunzo hayo kwa sababu yanakwenda kupunguza changamoto ya ajali za barabarani ambazo zimekuwa zikisababisha vifo na ulemavu kwa madereva wengi wa bodaboda na watumiaji wengine wa usafiri huo.


Akieleza zaidi kuhusu mafunzo hayo CPL Hamisi anayetoka Kitengo cha Elimu Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Tanga amesema wanaushukuru AMEND na Ubalozi wa Uswisi kwa kuona haja ya kutekeleza mradi huo kwani unakwenda kuongeza uelewa kwa madereva bodaboda kujiepusha na ajali pamoja na kutoa huduma ya kwanza inapotokea ajali.

Amesema ni muhimu kutolewa kwa huduma ya kwanza pale ajali inapotokea huku akisisitiza anapaswa kutoa hiyo ni mtu aliyepata elimu ya mafunzo ya jinsi ya kutoa huduma ya kwanza kwa mtu aliyepata ajali

"Mafunzo haya yatasaidia kuokoa maisha kwa mtu aliyepata ajali ya bodaboda,"amesema na kutoa mwito kwa baadhi ya bodaboda kuacha kujihusisha na vitendo vya uhalifu zinapotokea ajali na badala yake watumie elimu waliyoipata kuokoa maisha ya waliopatwa na ajali barabarani.

Kwa upande wake Ofisa Miradi kutoka AMEND Scolastica Mbilinyi ameeleza kwamba lengo la kutoa elimu ya huduma ya kwanza kwa bodaboda ni kusaidia kuokoa maisha ya watu pindi ajali zinapotokea.


Ameongeza wamekuwa na mradi huo wa kutoa mafunzo ya usalama barabarani kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo Jeshi la Polisi na  Msalaba Mwekundu pamoja na wadau wote muhimu.

Aidha amesema AMEND miongoni mwa mambo wanayofanya ni pamoja na kutoa elimu ya usalama barabarani, ujenzi wa miundombinu ya barabara kwenye shule zilizopo maeneo hatarishi na kwa wakati huu huo wanatoa mafunzo ya huduma ya kwanza kwa madereva.

Pamoja na hayo amesema mpaka sasa  AMEND kwa ufadhili wa ubalozi wa Uswiswi wameshatoa elimu ya usalama barabarani katika mikoa ya Tanga na Dodoma na lengo ni kuwafikia madereva wa bodaboda 750.

Wakati huo huo Diana Kashmiry kutoka Kikosi kazi cha huduma ya kwanza- Shirika la Msalaba Mwekundu amesema elimu wanayoitoa inamuwezesha dereva bodaboda kufahamu changamoto aliyoipata mtu ajalini na jinsi ya kumsaidia kwa kumpa huduma ya kwanza

Aidha ametoa angalizo kutokana na mazingira hatarishi yanayokuwepo katika ajali, ni vema kwa mtu asiye na vifaa vya kutoa huduma ya kwanza asiye huduma hiyo ili kumuepusha na madhara yanayoweza kujitokeza yakiwemo ya magonjwa ya kuambukiza.
Share:

Tuesday, March 26, 2024

BENKI YA DCB YAZINDUA PROGRAMU YA VICOBA KUBORESHA MAISHA YA WATANZANIA

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara DCB, Bwana Sabasaba Moshingi (wa pili kulia), akizungumza wakati wa uzinduzi programu ya DCB Vicoba pamoja na uzinduzi wa mradi wa kumiliki Coaster 5 wa Umoja wa Vikundi vya Ujasiriamali Kivule (UVUKI) uliopo chini ya Shirikisho la Vikundi vya Ujasiriamali Tanzania (SHIVUTA), uliofanyika Kitunda, Ilala, nje kidogo kutoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam leo.

KATIKA kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita katika kuhakikisha huduma za Kifedha zinawafikia watu wengi, kirahisi na gharama nafuu, Benki ya Biashara ya DCB imezindua programu ya VICOBA ikiwalenga wateja wa Vicoba na makundi mengine ya kijamii.
Uzinduzi wa DCB VicobaApp umefanyika Kitunda, Ilala nje kidogo ya jijini Dar es Salaam leo sambamba na hafla ya uzinduzi wa mradi wa kumiliki Coaster tano ulioandaliwa na Umoja wa Vikundi vya Ujasiriamali Kivule (UVUKI), chini ya Shirikisho la Vikundi vya Ujasiriamali Tanzania (SHIVUTA).

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB, Bwana Sabasaba Moshingi alisema programu hiyo itawawezesha wanachama wa vicoba kufanya miamala yao kwa urahisi na usalama zaidi, hivyo kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika jamii.

Tunatambua umuhimu wa teknolojia katika kuboresha maisha ya watu, na ndio maana tumeamua kuja na DCB VicobaApp ili kusaidia wanachama wa vikoba na makundi mengine ya kijamii kupata huduma za kifedha kwa urahisi zaidi kupitia simu zao za mkononi.

Ikianzishwa takribani miaka 22 iliyopita kupitia wito wa Rais Mstaafu Hayati Benjamin William Mkapa, kipaumbele chetu kikubwa kimekuwa ni kuinua maisha ya watanzania wenye kipato cha wastani kiuchumi, hususan wajasiriamali wadogo na wa kati lakini tukiangaza zaidi kwa watanzania ambao mara kadhaa wamekuwa wakikosa vigezo vya kupata mikopo na urahisi wa kuwekeza katika benki za kibiashara,” alisema Bwana Moshingi.

Ni katika muktadha huo Bwana Moshingi alisema, DCB imekuwa mwanzilishi na kuwa kinara katika kuanzisha huduma za mikopo kwa wajasiriamali wadogo wadogo, wateja binafsi na kwa vikundi vya Vikoba hivyo kwa kupitia ushirikiano huu wateja wa benki yetu wataweza kuzifikia akaunti kirahisi mahali walipo na kwa wakati wowote na kupata huduma.

Alisema kwa kupitia DCB VicobaApp, wateja wa vicoba wataweza kupata huduma mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuweka pesa bila makato yoyote, kukopa mikopo na kufanya marejesho, kuchagua viongozi wa wa vikundi vyao, kupata ujumbe mfupi kwa kila mjumbe pale mjumbe mmoja anapoweka pesa kwenye kikoba, yote yakifanyika kupitia simu za mkononi.

Naye Mkurugenzi wa Biashara wa DCB, Bi. Lilian Mtali alisema benki yao inajivunia kuwa moja ya benki waanzilishi kwa kutoa mikopo ya wajasiriamali ikiwemo mikopo midogomidogo ya kuanzia hata kiasi cha shs elfu 30 hadi milioni 5 kwa wateja wadogo.

"DCB pia tunajivunia kutoa mikopo ya kiasi cha shs trilioni 1 kwa wajasiriamali na wafanyakazi ambapo sasa benki inao uwezo wa kutoa mkopo wa hadi kiasi cha shs bilioni 5 kwa mtu mmoja.

Katika kuhakikisha lengo letu la kuboresha maisha ya watanzania na kuwapunguzia umasikini linatimia, DCB kila mara imekuwa ikianzisha akaunti na huduma zenye ubunifu, mfano akaunti ya elimu ya DCB Skonga, Wahi Akaunti kwa wenye mahitaji ya kutimiza malengo kwa njia ya kuwekeza kidogo kidogo, akaunti za Mshahara & Mikopo ya nusu mshahara, akaunti ya Wastaafu, Mikopo ya Nyumba, Akaunti maalum (FDR) na nyinginezo nyingi,” aliongeza Bi Lilian.

Ikiwekeza zaidi katika huduma za kibenki kwa njia za kidigitali, DCB ina mtandao wa mawakala zaidi ya 1500 na vituo vidogo vya kutokea huduma zaidi ya 700 katika maeneo ya kimkakati sehemu mbalimbali nchini huku ikiwa na mtandao wa Matawi 9 ya kibenki jijini Dar es Salaam na mikoani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara DCB, Bwana Sabasaba Moshingi (katikati), Mkurugenzi wa Biashara wa benki hiyo, Bi. Lilian Mtali (kulia) na Mkurugenzi wa Shirikisho la Vikundi vya Ujasiriamali Tanzania (SHIVUTA), Andrew Paul wakiwasili tayari kwa uzinduzi programu ya DCB Vicoba pamoja na uzinduzi wa mradi wa kumiliki Coaster 5 wa Umoja wa Vikundi vya Ujasiriamali Kivule (UVUKI) uliopo chini ya Shirikisho la Vikundi vya Ujasiriamali Tanzania (SHIVUTA) uliofanyika Kitunda, Ilala, jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya Wana vikoba waliohudhuria uzinduzi wa DCB VikobaApp wakiwa katika hafla hiyo, Kitunda, Ilala, Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara DCB, Bwana Sabasaba Moshingi (katikati) akiagana na Mkurugenzi wa Shirikisho la Vikundi vya Ujasiriamali Tanzania (SHIVUTA), Bwana Andrew Paul mara baada ya uzinduzi programu ya DCB Vicoba pamoja na mradi wa kumiliki Coaster 5 wa Umoja wa Vikundi vya Ujasiriamali Kivule (UVUKI) uliopo chini ya Shirikisho la Vikundi vya Ujasiriamali Tanzania (SHIVUTA) uliofanyika Kitunda, Ilala jijini Dar es Salaam leo. Wengine ni Viongozi wa Umoja wa Vikundi vya Ujasiriamali Kivule (UVUKI).
Share:

Monday, March 25, 2024

BENKI YA EQUITY TANZANIA YAFUTURISHA WATEJA WAKE ZANZIBAR

Zanzibar, 23 Machi 2024. Benki ya Equity katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani imefuturisha wateja wake katika mji mkongwe wa Zanzibar ikiwa ni ishara ya shukurani kwa wateja na wadau wake wa karibu kwa kuendelea kuichagua benki hiyo kama benki yao pendwa.

Akiongea kwenye hafla hiyo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Bw. Rojas Mdoe amesema kwamba Benki ya Equity Tanzania inathamini mchango wa wateja wakekatika ukuwaji wa amana za benki na kwa kutumia huduma za benki. Akaendelea kusema, dhumuni kubwa la kuandaa Futari hii ni kuwashukuru wateja wake kwa kuwa bega kwa bega kuhakikisha tunabadilisha maisha ya kila Mtanzania.

Aliendelea na kusema kuwa benki yetu inaendelea kuboresha huduma zake na kuhakikisha kuwa inatanua wigo wake wa upatikanaji nchini ili kuweza kuwafikia wateja wote Tanzania na kuhakikisha kuwa inatimiza dhamira yake ya kubadilisha maisha ya kila Mtanzania.

Akizungumza katika hafla hiyo, Waziri Afisi ya Raisi Kazi, Uchumi na Uwekezaji Mh. Sharif A. Sharif alisema, nawapongeza sana benki ya Equity kwa kuunga mkono juhudi za serikali kwa kukuza uchumi wa taifa letu kwa kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anatumia mifumo rasmi ya kifedha (financial inclusion). Vilevile kwa ubunifumkubwa wa kutoa huduma bora za kibenki za kidijitali.

Kuhusu Benki ya Equity

Equity Bank (T) ni Benki yenye matawi 16 nchini, mawakala zaidi ya 2,000 ikiwa na zaidi ya wafanyakazi zaidi ya 400 ikiwa ni moja ya uwekezaji mkubwa zaidi ulioanzia nchini Kenya na baadaye kusambaa katika nchi nyingine 5 za Afrika Mashariki, ikiwemo Tanzania, Uganda, Congo-DRC, Rwanda na Sudan ya Kusini.
Share:

Saturday, March 23, 2024

KAMPUNI YA ORYX TANZANIA YAWAKOMBOA WAKAANGA SAMAKI FERI YAKABIDHI MITUNGI 700 YA GAS BURE


KAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imeahidi kufunga mtambo mkubwa wa nshati safi ya kupikia katika Soko la Samaki la Kimataifa Feri jijini Dar es Salaam ambapo wajasiriamali wa soko hilo watakuwa na urahisi wa kuipata nishati hiyo na kwa gharama nafuu kwa ajili ya kukaanga samaki.

Hatua hiyo imekuja baada ya wajasiriamali wa soko hilo kutoa ombi kwa Kampuni ya Oryx Gas pamoja na Mbunge wa Jimbo la Ilala ambaye pia ni Naibu Spika wa Bunge Muss Zungu baada ya kupokea ombi kutoka kwa wajasiriamali wa soko hilo walioomba kufungiwa mtungi mkubwa wa gesi wakiamini utawasaidia katika shughuli zao.

Ahadi ya kufungwa kwa mtungi mkubwa wa gesi imetolewa wakati wa hafla ya kukabidhi mitungi 700 ya gesi ya Oryx kwa Baba na Mama Lishe wa soko la Samaki la Kimataifa Feri jijini Dar es Salaam leo Machi 22,2024.

Wakati anazungumza mbele ya wajasiriamali hao,Zungu amewahakikishia Mama Lishi na Baba lishe katika Soko la Samaki la Kimataifa Feri kuwa watafungiwa mtambo wa nishati safi ya kupikia ili kuwaepusha kutumia fedha nyingi kununua gesi kupitia mitungi midogo.

Amesema hatua hiyo ni utekelezaji wa mkakati wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa lengo la kulinda mazingira kuwaweka wanawake katika nafasi nzuri ya kujiendeleza kiuchumi.

Zungu kabla ya kueleza hayo alipokea maombi ya wafanyabiashara hao kupitia kwa kiongozi Zone Namba 7 katika soko hilo, Said Mpinji aliyelalamika kuwa wanalazimika kutumia sh. 110,000 kila siku kujaza gesi ya kuendeshea shughuli za baba na mama lishe.

Hivyo Zungu amesema tayari amezungumza na kampuni ya Gesi ya Oryx Tanzania kupitia kwa Mkurugenzi Mkuu wake, Benoit Araman na amekubali kufunga mifumo ya gesi ya kisasa kasha kusambaza huduma hiyo kwa wafanyabiashara hao kwa gharama nafuu.

“Mkombozi wetu ni Rais Dk.Samia Suluhu Hassan ambaye ameanzisha kampeni ya nishati safi ya kupikia, kuhakikisha Watanzania wanaishi maisha mazuri.

“Oryx wamekubali kuweka mtungi mmoja mkubwa na mifumo ya usambazaji, kasha watasambaza huduma kwa mama na baba lishe waliopo hapa na kuwafungia mita halafu watakuwa wakilipia huduma kama wanavyofanya katika umeme,” amefafanua.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Oryx  Benoit Araman amesema Oryx wamewafikia wajasiriamali hao kwa lengo la kutekeleza mkakati wa Rais Dk. Samia wa matumizi ya nishati safi ya kupikia kulinda mazingira na afya za wananchi.

"Tangu Julai mwaka 2021, tulianza mkakati huu baada ya Rais Dk Samia kutangaza kuwa Serikali yake inataka kuona hadi mwaka 2030 asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia nishati safi ya kupikia."

Wakati huo huo Mwenykiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam Abbasi Mtemvu aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, ameeleza kuwa ugawaji wa mitungi kwa baba na Mama Lishe hao ni utekelezaji wa Ilani huku akitumia nafasi hiyo kumpongeza Zungu kwa namna anavyowatetea wananchi wa jimbo lake.

 Aidha ameipongeza Serikali kwa kuendelea kupeleka maendeleo kwa wananchi.Pia amewataka mama na baba lishe wa sokoni hapo kujiandaa kupokea mitaji kutoka serikali ili kunua biashara zao. 

 Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilala Jijini Dar es Salaam, Mussa Zungu (katikati) akiwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu ( wa pili kulia),Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo ( wa kwanza kulia), Diwani wa Kata ya Kivukoni Sharik Choughle ( wa kwanza kushoto), Mkurugenzi wa Kampuni ya Gasi ya Orxy, Benoite Araman ( wa pili kushoto) wakimkabidhi mtungi wa gesi mama lishe na mfanyabiashara katika soko la Samaki la Kimataifa Feri, Happy Kiondo wakati wa makabidhiano ya mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa mama lishe na baba lishe wa soko hilo leo Machi 22, 2024.


Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilala Jijini Dar es Salaam, Mussa Zungu (katikati) akiwa na Diwani wa Kata ya Kivukoni Sharik Choughle ( wa kwanza kushoto), Meneja Mauzo wa Kampuni ya Gasi ya Orxy , Shaban Fundi (wa pili kushoto) wakimkabidhi mtungi wa gesi ya kupikia ya Oryx Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Zone no.7 wa Soko la Samaki la Kimataifa Feri Jijini Dar es Salaam, Saidi Mpinji wakati wa makabidhiano ya mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa mama lishe na baba lishe wa soko hilo leo Machi 22, 2024. Anayeshuhudia makabidhiano hayo ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo (kulia).


Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilala Jijini Dar es Salaam, Mussa Zungu (katikati) akiwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu ( wa pili kulia),Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo ( wa kwanza kulia), Diwani wa Kata ya Kivukoni Sharik Choughle ( wa kwanza kushoto), Mkurugenzi wa Kampuni ya Gasi ya Orxy, Benoite Araman ( wa pili kushoto) wakimkabidhi mtungi wa gesi mama lishe na mfanyabiashara katika soko la Samaki la Kimataifa Feri, Happy Kiondo wakati wa makabidhiano ya mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa mama lishe na baba lishe wa soko hilo leo Machi 22, 2024.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilala Jijini Dar es Salaam, Mussa Zungu (katikati) akiwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu ( wa pili kulia),Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo ( wa kwanza kulia), Diwani wa Kata ya Kivukoni Sharik Choughle ( wa kwanza kushoto), Mkurugenzi wa Kampuni ya Gasi ya Orxy, Benoite Araman ( wa pili kushoto) wakimkabidhi mtungi wa gesi mmoja wa mama lishe na mfanyabiashara katika soko la Samaki la Kimataifa Feri wakati wa makabidhiano ya mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa mama lishe na baba lishe wa soko hilo leo Machi 22, 2024.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilala Jijini Dar es Salaam, Mussa Zungu (katikati) akiwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu ( wa pili kulia),Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo ( wa kwanza kulia), Diwani wa Kata ya Kivukoni Sharik Choughle ( wa kwanza kushoto), Mkurugenzi wa Kampuni ya Gasi ya Orxy, Benoite Araman ( wa pili kushoto) wakimkabidhi mtungi wa gesi mama lishe na mfanyabiashara katika soko la Samaki la Kimataifa Feri, Salma Mohammed wakati wa makabidhiano ya mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa mama lishe na baba lishe wa soko hilo leo Machi 22, 2024.



Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilala Jijini Dar es Salaam, Mussa Zungu akiwa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Gesi ya Orxy, Benoite Araman wakiwasikiliza wafanyabiashara wa samaki katika soko la Samaki la Kimataifa Feri, Jijini Dar es Salaam leo Machi 22, 2024.


Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilala Jijini Dar es Salaam, Mussa Zungu ( kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Kampuni ya Gesi ya Orxy, Benoite Araman katika hafla ya kukabidhi mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa wajasiriamali wa soko la Samaki la Kimataifa Feri, Jijini Dar es Salaam leo Machi 22, 2024


Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilala Jijini Dar es Salaam, Mussa Zungu akizungumza katika hafla ya kukabidhi mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa wajasiriamali wa soko la Samaki la Kimataifa Feri, Jijini Dar es Salaam leo Machi 22, 2024.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilala Jijini Dar es Salaam, Mussa Zungu akizungumza katika hafla ya kukabidhi mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa wajasiriamali wa soko la Samaki la Kimataifa Feri, Jijini Dar es Salaam leo Machi 22, 2024.



Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu akizungumza katika hafla ya kukabidhi mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa wajasiriamali wa soko la Samaki la Kimataifa Feri, Jijini Dar es Salaam leo Machi 22, 2024.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo akizungumza katika hafla ya kukabidhi mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa wajasiriamali wa soko la Samaki la Kimataifa Feri, Jijini Dar es Salaam leo Machi 22, 2024.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Gasi ya Orxy, Benoite Araman akizungumza katika hafla ya kukabidhi mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa wajasiriamali wa soko la Samaki la Kimataifa Feri, Jijini Dar es Salaam leo Machi 22, 2024.Diwani wa Kata ya Kivukoni Sharik Choughle akizungumza katika hafla ya kukabidhi mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa wajasiriamali wa soko la Samaki la Kimataifa Feri, Jijini Dar es Salaam leo Machi 22, 2024.Baadhi ya wajasiriamali wa soko la Samaki la Kimataifa Feri wakiwa kwenye hafla ya makabidhiano ya mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa wajasiriamali hao, Jijini Dar es Salaam leo Machi 22, 2024.Meneja Masoko wa Kampuni ya Gesi ya Orxy Peter Ndomba akitoa elimu ya matumizi sahihi ya mtungi wa kupikia wa gesi ya Orxy katika hafla ya makabidhiano ya mitungi ya kupikia ya gesi ya Orxy 700 kwa wajasiriamali wa soko la Samaki la Kimataifa Feri, Jijini Dar es Salaam leo Machi 22, 2024.
Share:

Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive