Mbunge wa Jimbo la Segerea, Agnesta Lambert (CHAUMA), ameendeleza juhudi zake za kuimarisha ustawi wa makundi maalum kwa kuwafikia watoto wenye ulemavu wa kusikia katika Shule ya Msingi ya Viziwi Buguruni, jijini Dar es Salaam ambapo amekabidhi msaada wa vyakula pamoja na mahitaji mengine muhimu, kwa lengo la kuwawezesha watoto hao kusherehekea kwa heshima na furaha sikukuu za Idd el-Fitr na Pasaka.
Amebaini changamoto kubwa inayoikabili shule hiyo, ni upungufu wa mabweni kwa wanafunzi hao na kuahidi kufikisha suala hilo bungeni na kuongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka kipaumbele katika sekta ya elimu, na hivyo ana imani kuwa changamoto zilizopo zitapatiwa ufumbuzi.
Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule hiyo ameeleza kuwa uhaba wa mabweni unawaweka watoto hao katika hatari, ikiwemo uwezekano wa kupata ajali kutokana na mazingira yasiyo rafiki kwa hali yao.







0 comments:
Post a Comment