A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Friday, August 14, 2020

ABSA TANZANIA KUENDELEA KUWA MSTARI WA MBELE KUSAIDIA JAMII

Meneja Huduma za Jamii wa Benki ya Absa Tanzania, Hellen Siria (kushoto) na Meneja Miradi wa Makampuni kutoka Shirika linalojihusisha na kuboresha maisha ya watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu hasa wale walioathirika na ugonjwa wa ukimwi (Pact), Beatrice Kamugisha, wakikabidhi vifaa vya saluni kwa mmoja wa wanafunzi  aliyehitimu mafunzo katika Chuo cha Ufundi cha Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi Tanzania (Veta), Neema Bakari, chini ya udhamini wa Benki ya Absa kupitia Mpango wa Kizazi Kipya unaoratibiwa na Pact pamoja na Shirika la Walio katika Mapambano na Aids (WAMATA). Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za WAMATA, Dar es Salaam leo.
Meneja Huduma za Jamii wa Benki ya Absa Tanzania, Hellen Siria (kulia) akikabidhi cherehani kwa mmoja wa wanafunzi aliyehitimu mafunzo katika Chuo cha Ufundi cha Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi Tanzania (Veta), Happy Kalinga, chini ya udhamini wa Benki ya Absa kupitia Mpango wa Kizazi Kipya unaoratibiwa na Shirika linalojihusisha na kuboresha maisha ya watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu hasa wale walioathirika na ugonjwa wa ukimwi (Pact) pamoja na Shirika la Walio katika Mapambano na Aids (WAMATA). Katikati ni Meneja Miradi wa Makampuni kutoka Pact, Beatrice Kamugisha. Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za WAMATA, Dar es Salaam leo.
Meneja Huduma za Jamii wa Benki ya Absa Tanzania, Hellen Siria (kushoto) vifaa vya saluni kwa mmoja wa wanafunzi aliyehitimu mafunzo katika Chuo cha Ufundi cha Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi Tanzania (Veta), Rehema Shabani, chini ya udhamini wa Benki ya Absa kupitia Mpango wa Kizazi Kipya unaoratibiwa na Shirika linalojihusisha na kuboresha maisha ya watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu hasa wale walioathirika na ugonjwa wa ukimwi (Pact), pamoja na Shirika la Walio katika Mapambano na Aids (WAMATA). Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za WAMATA, Dar es Salaam leo. Kulia ni Meneja Miradi wa Makampuni kutoka Pact, Beatrice Kamugisha na Meneja Mradi wa Kizazi Kipya kutoka WAMATA, Omari Chambo.
Meneja Huduma za Jamii wa Benki ya Absa Tanzania, Hellen Siria (wa pili kulia) akikabidhi vitendea kazi vya upambaji kwa mmoja wa wanafunzi aliyehitimu mafunzo katika Chuo cha Ufundi cha Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi Tanzania (Veta), Maisha Ally, chini ya udhamini wa Benki ya Absa kupitia Mpango wa Kizazi Kipya unaoratibiwa na Shirika linalojihusisha na kuboresha maisha ya watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu hasa wale walioathirika na ugonjwa wa ukimwi (Pact), pamoja na Shirika la Walio katika Mapambano na Aids (WAMATA). Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za WAMATA, Dar es Salaam leo. Kushoto ni Meneja Miradi wa Makampuni kutoka Pact, Beatrice Kamugisha na Meneja Mradi wa Kizazi Kipya kutoka WAMATA, Omari Chambo.
Meneja Mradi wa Kizazi Kipya kutoka Shirika la Walio katika Mapambano na Aids (WAMATA), Omari Chambo (kushoto) akikabidhi vitendea kazi vya upambaji kwa mmoja wa wanafunzi aliyehitimu mafunzo katika Chuo cha Ufundi cha Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi Tanzania (Veta), Maisha Ally, chini ya udhamini wa Benki ya Absa kupitia Mpango wa Kizazi Kipya unaoratibiwa na Shirika linalojihusisha na kuboresha maisha ya watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu hasa wale walioathirika na ugonjwa wa ukimwi (Pact), pamoja na Shirika la WAMATA. Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za WAMATA, Dar es Salaam leo. Wa tatu kushoto ni Meneja Huduma za Jamii wa Benki ya Absa Tanzania, Hellen Siria na Meneja Miradi wa Makampuni kutoka Pact, Beatrice Kamugisha.
Meneja Huduma za Jamii wa Benki ya Absa Tanzania, Hellen Siria (kulia) akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi vitenbdea kazi kwa wanafunzi waliohitimu mafunzo katika Chuo cha Ufundi cha Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi Tanzania (Veta), chini ya udhamini wa Benki ya Absa kupitia Mpango wa Kizazi Kipya unaoratibiwa na Shirika linalojihusisha na kuboresha maisha ya watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu hasa wale walioathirika na ugonjwa wa ukimwi (Pact), pamoja na Shirika la WAMATA. Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za WAMATA, Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Ofisa Elimu wa WAMATA Wilaya ya Ilala, Doreen Phillemon, Meneja Mradi wa Kizazi Kipya WAMATA, Omari Chambo na Meneja Miradi wa Makampuni kutoka Pact, Beatrice Kamugisha.
Mmoja wa wahitimu wa waliohitimu mafunzo katika Chuo cha Ufundi cha Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi Tanzania (Veta), Happy Kalinga akitoa shukrani katika hafla hiyo.
Meneja Miradi wa Makampuni kutoka Shirika linalojihusisha na kuboresha maisha ya watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu hasa wale walioathirika na ugonjwa wa ukimwi (Pact), Beatrice Kamugisha (katikati) akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi vitendea kazi kwa wanafunzi waliohitimu mafunzo katika Chuo cha Ufundi cha Mamlaka ya Mafunzo ya Ufundi Stadi Tanzania (Veta), chini ya udhamini wa Benki ya Absa kupitia Mpango wa Kizazi Kipya unaoratibiwa na Shirika la Pact, pamoja na Shirika la WAMATA. Hafla hiyo ilifanyika katika ofisi za WAMATA, Dar es Salaam leo. kushoto ni Ofisa Elimu wa WAMATA Wilaya ya Ilala, Doreen Phillemon na Meneja Huduma za Jamii wa Benki ya Absa Tanzania, Hellen Siria.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive