A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Wednesday, January 10, 2018

Stanbic Bank yaanza mwaka 2018 na akaunti ya HATUA,

Dar es Salaam, Sunday 07th January 2018. Stanbic Bank Tanzania imezindua akaunti mpya ijulikanayo kama HATUA, ambayo ni kwa ajili ya watoto yenye lengo la kuwasaidia wazazi kuwawekea akiba watoto wao huku wakiwajengea utamaduni wa kujiwekea akiba.
Kwa kuanzishwa kwa aina hii mpya ya akaunti, Stanbic bank inaendelea kuwapatia wateja wake huduma mpya na bora za kibenki kila siku kuendana na mahitaji ya wateja an hali halisi ya soko.
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa akaunti hiyo uliofanyika katika makao makuu ya benki hiyo Kinondoni jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, mkuu wa mauzo wa benki hiyo Shangwe Kisanji amesema kuwa benki hiyo imekuwa mstari wa mbele katika kuwapatia wateja wake huduma mpya kila mara na nyakati zote huduma hizo huendana na mahitaji ya wateja na mahitaji ya jumla ya soko la huduma za kibenki hapa nchini.
“Wakati wote tumekuwa tukiangalia njia mbalimbali za kuwahudumia vyema wateja wetu katika kutunza fedha zao ikiwemo kuwawekea watoto akiba kwa manufaa yao ya baadae na pia kuwajengea utamaduni wa kujiwekea akiba wawapo wakubwa, utamaduni ambao ni muhimu sana kwa uchumi na maisha yao”
Ameeleza kuwa akaunti hiyo ya HATUA ni muendelezo mzuri wa kuwatoa watoto kwenye utamaduni wa kujiwekea akiba kwenye vibubu na badala yake kuanza utamaduni wa kujiwekea akiba kwa njia rasmi zaidi.
Amesema akaunti hiyo haina makato ya huduma na kiwango cha chini cha amana ni shilingi 20,000 tu. Amebainisha kuwa akaunti hiyo haina masharti magumu ya kuiendesha  na inaruhusu kutolewa kwa fedha mara moja kwa robo ya mwaka ili kusaidia katika majukumu yanayowahusu watoto kama vile ada za shule, sare na kadhalika. Amesema pia akaunti hiyo hujipatia riba kulingana na amana iliyopo.
Note to Editors
Stanbic Bank Tanzania is part of the Standard Bank Group, Africa’s largest bank by assets. Stanbic Bank Tanzania provides the full spectrum of financial services. It’s Corporate and Investment Banking division serves a wide range of requirements for banking, finance, trading, investment, risk management and advisory services. Corporate and Investment Banking delivers this comprehensive range of products and services relating to: investment banking; global markets; and global transactional products and services.

Stanbic Bank’s corporate and investment banking expertise is focused on industry sectors that are most relevant to emerging markets. It has strong offerings in mining and metals; oil, gas and renewables; power and infrastructure; agribusiness; telecommunications and media; and financial institutions.

Stanbic Bank Tanzania’s personal and business banking unit offers banking and other financial services to individuals and small-to-medium enterprises. This unit serves the increasing need among Tanzania’s small business and individual customers for banking products that can meet their shifting expectations and growing wealth.

Picha  za matukio mbalimbali ya hafla ya uzinduzi wa akaunti mpya ya HATUA ya benki ya Stanbik jijini Dar es salaam. Akaunti hiyo mpya ni kwa ajili ya watoto na ina lengo la kuwasaidia wazazi na walezi katika mahitaji ya watoto kama vile ada za shule na pia kuwajengea watoto utamaduni mzuri wa kujiwekea akiba
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive