A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Sunday, March 1, 2020

Benki ya Absa Tanzania yadhamini Kili Marathon 2020 kwa mafanikio

Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga (katikati), pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo wakishiriki mbio za Kilomita 21 za Kilimanjaro marathon pamoja na wakimbiaji wengine. Absa ilikuwa mmoja wa wadhamini ikigharamia kituo cha kutoa maji ya kunywa na viburudisho kwa wakimbiaji. Mashindano hayo yalifanyika mjini Moshi, Kilimanjaro leo.  
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga (kushoto), akimpongeza mmoja wa wakimbiaji wao aliyeshiriki mbio za kilomita 42 wakati wa mashindano ya Kilimanjaro marathon 2020 pamoja na wakimbiaji wengine mjini Moshi, Kilimanjaro leo. Absa ilikuwa mmoja wa wadhamini ikigharamia kituo cha kutoa maji ya kunywa na viburudisho kwa wakimbiaji. Mashindano hayo yalifanyika Moshi, Kilimanjaro leo.
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga (kushoto), pamoja na wakimbiaji wengine wakionyesha medali zao walizopewa baada ya kushiriki mshindamo ya Kilimanjaro Marathon 2020 katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika Moshi, mkoani Kilimanjaro leo. Absa ilikuwa mmoja wa wadhamini ikigharamia kituo cha kutoa maji ya kunywa na viburudisho kwa wakimbiaji pamoja na kupeleka wafanyakazi wake kushiriki mbio hizo.
Baadhi ya wakimbiaji wa Benki ya Absa Tanzania pamoja na wakimbiaji wengine, wakitimua mbio wakati wa mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2020 mjini Moshi Kilimanjaro leo. Absa ilidhamini mashindano hayo kwa kutoa kituo cha maji na viburudisho kwa wakimbiaji pamoja na kupeleka wafanyakazi wake kushiriki mbio hizo.
Mkimbiaji akipewa maji ili kupoza kiu katika kituo cha maji kilichowekwa kwa ufadhili wa Benki ya Absa Tanzania wakati wa mashindano ya mwaka huu ya Kilimanjaro Marathon mjini Moshi, Kilimanjaro leo.  
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Anna Mghirwa (kulia), akikabidhi cheti cha shukurani kwa Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Absa Tanzania, Aron Luhanga kwa kutambua mchango wa benki hiyo katika kufanikisha mashindano ya mwaka huu ya Kilimanjaro Marathon yaliyofanyika leo katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika Moshi Mkoani Kilimanjaro. Anayeshuhudia ni Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe.
Wakimbiaji wa Benki ya Absa Tanzania, wakipiga picha ya kumbukumbu mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya Kilimanjaro Marathon 2020 katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika, Mjini Moshi, Kimanjaro juzi. Absa ilidhamini mashindano hayo kwa kutoa kituo cha maji na viburudisho kwa wakimbiaji pamoja na kupeleka wafanyakazi wake kushiriki mbio hizo.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive