A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Monday, May 18, 2020

WAKAZI WA VINGUNGUTI SASA WATAKIWA KUKAA MKAO WA KIBIASHARA

IMG-20200517-WA0045
IMG-20200517-WA0047%2B%25281%2529Ujenzi wa Machinjio ya kisasa yanayojengwa Vingunguti Jijini Dar es Salaam, yamefikia hatua za mwisho  wenye thamani ya shilingi  Billion 12.4, ambapo jengo Hilo lina vyumba 2 vya kufanyia ibada kwa Wakristo Pamoja na Waislam.

Akizungumza  mara Baada ya kufanya ziara katika Machinjio hayo, Meya wa Ilala ambae pia ni Diwani wa Vingunguti,  Omary Kumbilamoto,  amesema vyumba hivyo vimejengwa kutokana na agizo la Rais John Magufuli ambapo limetekelezwa na wafanyakazi katika machinjio hayo watasali kulingana na dini zao.

Aidha amesema jengo hilo litafungwa mafriji makubwa yenye uwezo wa kuhifadhi ng'ombe zilizochinjwa(Nyama) 1000 Pamoja na mbuzi 1000, na kuongeza kuwa uchinjaji utafanyika kwa saa 24, kutokana na kufungwa kamera za kusaidia usalama, Pamoja na mashine za kuchinjia za kisasa zitawekwa katika Machinjio hayo.

Ameongeza kuwa  machinjio yatakuwa ya kisasa na kuwavutia watu wengi hata watalii pia, kwani kutajengwa mabwawa ya maji taka ambayo yatachakatwa na kupata maji Safi kwa ajili ya umwagiliaji wa bustani zinazozunguka eneo Hilo.

Pia amewataka wafanyabiashara wa Vingunguti kutumia fursa kwani miguu, maini, ngozi, mikia ya ng'ombe ni tija hivyo waitumie vizuri kwani machinjio hayo yatakuwa Ni bora Tanzania nzima na ya kimataifa.

Mbali na hayo amewataka wafanyabiashara wa hoteli zinazozunguka machinjio hayo kuboresha zaidi Pamoja na wahudumu kuwa wakarimu Pindi wageni watakapofika ili kuwavutia zaidi.Ujenzi wa Machinjio ya kisasa yanayojengwa Vingunguti Jijini Dar es Salaam, yamefikia hatua za mwisho  wenye thamani ya shilingi  Billion 12.4, ambapo jengo Hilo lina vyumba 2 vya kufanyia ibada kwa Wakristo Pamoja na Waislam.

Akizungumza  mara Baada ya kufanya ziara katika Machinjio hayo, Meya wa Ilala ambae pia ni Diwani wa Vingunguti,  Omary Kumbilamoto,  amesema vyumba hivyo vimejengwa kutokana na agizo la Rais John Magufuli ambapo limetekelezwa na wafanyakazi katika machinjio hayo watasali kulingana na dini zao.

Aidha amesema jengo hilo litafungwa mafriji makubwa yenye uwezo wa kuhifadhi ng'ombe zilizochinjwa(Nyama) 1000 Pamoja na mbuzi 1000, na kuongeza kuwa uchinjaji utafanyika kwa saa 24, kutokana na kufungwa kamera za kusaidia usalama, Pamoja na mashine za kuchinjia za kisasa zitawekwa katika Machinjio hayo.

Ameongeza kuwa  machinjio yatakuwa ya kisasa na kuwavutia watu wengi hata watalii pia, kwani kutajengwa mabwawa ya maji taka ambayo yatachakatwa na kupata maji Safi kwa ajili ya umwagiliaji wa bustani zinazozunguka eneo Hilo.

Pia amewataka wafanyabiashara wa Vingunguti kutumia fursa kwani miguu, maini, ngozi, mikia ya ng'ombe ni tija hivyo waitumie vizuri kwani machinjio hayo yatakuwa Ni bora Tanzania nzima na ya kimataifa.

Mbali na hayo amewataka wafanyabiashara wa hoteli zinazozunguka machinjio hayo kuboresha zaidi Pamoja na wahudumu kuwa wakarimu Pindi wageni watakapofika ili kuwavutia zaidi.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive