A blog that gives out financial institutions news on time with accurate informations.


Tuesday, May 5, 2020

Absa Tanzania yaunga mkono juhudi za serikali mapambano dhidi ya Covid-19

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, (katikati), akimshukuru Mkurugenzi Rasilimali Watu na Utumishi wa Benki ya Absa Tanzania, Patrick Foya (kushoto), baada ya kupokea msaada wa vifaa tiba kwa ajili ya kuisaidia serikali katika kupambana na ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayotokana na virusi vya Corona (Covid-19) kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Prof. Mabula Daudi Mchembe. Vifaa hivyo vikiwemo barakoa, vitakasa mikono na gloves vyenye thamani ya shs milioni 20 vimekabidhiwa katika ofisi za wizara hiyo jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi Rasilimali watu na Utumishi wa Benki ya Absa Tanzania Patrick Foya (kushoto), akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada wa vifaa tiba kusaidia juhudi za serikali katika kupambana na ugonjwa wa corona (Covid-19), kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya. Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (katikati) kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Prof. Mabula Daudi Mchembe. Vifaa hivyo vikiwemo barakoa, vitakasa mikono na gloves vyenye thamani ya shs milioni 20 vimekabidhiwa katika ofisi za wizara hiyo jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya. Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, akizungumza wakati akipokea vifaa tiba kutoka kwa Mkurugenzi wa Rasiliamali Watu na Utumishi wa Benki ya Absa Tanzania, Patrick Foya (kushoto) ikiwa ni mchango wa benki hiyo katika kusaidia juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virusi vya Corona (Covid-19). Vifaa hivyo vikiwemo barakoa, vitakasa mikono na gloves vyenye thamani ya shs milioni 20 vimekabidhiwa katika ofisi za wizara, Dar es Salaam leo.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Propellerads

Search Brazuka Kibenki

FOLLOW US ON FACEBOOK

  • ()
  • ()
Show more

Labels

Blog Archive